Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TIST International Limited, Georgy Kytika kulia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutambulisha tamasha la kistaarabu lenye mahadhi ya kiafrika litakalofanyika katika ukumbi wa Next Door Arena Osterbay jijini Dar es Salaam Agosti 30 mwaka huu. Kushoto ni mzalishaji wa kampuni ya TIST, Neema Mbuya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TIST International Limited, Georgy Kytika katikati, Kushoto ni mzalishaji wa kampuni ya TIST, Neema Mbuya na Meneja masoko wa kampuni ya TIST, Annie mosses wakisikiliza swali kwa mwandishi wa haari hayupo pichani.

KAMPUNI inayojishughulisha na Burudani nchini ya TIST inatarajia kufanya tamasha la kistaarabu la mziki wa Rhumba linalotarajia kufanyika katika ukumbi wa Next Door arena Osterbay jijini Dar es Salaam Agosti 30 mwaka huu.

Akizungumza wakati wa kutambulisha tamasha la Rhumba Festival jijini Dar es salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TIST International Limited, Georgy Kytika amesema kuwa siku hiyo watu wastaarabu waende wakajionee mziki wa kistaarabu wenye mahadhi ya Afrika jinsi utakavyotumbuizwa na wasanii mbalimbali wa hapa nchini wakiongozwa na SAUTI SOL kutoka nchini Kenya.

Amesema kuwa "Onesho la tamasha hilo ambalo litakuwa la kihistoria hapa nchini pia kutakuwa na utambulisho aina nyingine ya burudani ambapo mtanzania usiwaze kukosa katika tamasha hilo la Rhumba".

Amesema kuwa mziki utakuwa wakistaarabu watu waende wamependeza na suti zao kwani Burudani itakuwa ya kistaarabu na yenye kufurahisha kwa watakaohudhuria.

Kiingilio katika tamasha hilo Kyatika amesema kuwa itakuwa VIP shilingi 50,000/= na VVIP ni shilingi 100,000/=.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...