*Rais Magufuli asifiwa kwa utendaji kazi, aungwa mkono, SADC kuleta mabadiliko chanya kwa wenye viwanda

*Kiwanda cha Keda Ceremics Limited kulipa kodi ya zaidi ya dola milioni 12 kwa Serikali

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

WIKI ya nne ya viwanda imehitimishwa kwa washiriki wa maonesho hayo kutoa nchi mbalimbali ndani ya jumuiya ya SADC kutembelea viwanda mbalimbali Tanzania bara na visiwani na kujionea namna viwanda hivyo vinavyofanya kazi pamoja na kutengeneza fursa mbalimbali hasa za masoko kwa wanajumuiya hao.

Ziara iliyofanywa katika kiwanda cha usindikaji wa matunda cha Elven agri kilichopo Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani walishiriki walijionea namna matunda yanavyochakatwa na kukaushwa na baadaye kusafirishwa katika nchi mbalimbali ndani ya jumuiya ikiwemo Botswana na Zambia pamoja na nchi za nje ikiwemo Marekani, kiwanda hicho chenye takribani ya heka 900 kinatoa ajira kwa wanawake na vijana pamoja na kushiriki shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo kujenga shule pamoja na miundombinu ya maji.

Msimamizi wa kiwanda hicho Martin Matembo amesema kuwa bidhaa za matunda yakiwemo maembe, nanasi, papai, na ndizi zinazosindikwa kiwandani hapo zinauzwa nchini pamoja na kupelekwa nje ya nchi na kupitia SADC wamepata fursa kubwa kupitia wiki ya viwanda kwani wamejenga mahusiano bora na makubaliano ya kibiashara na washiriki wa mkutano huo kutoka nchi za Afrika Kusini, Zambia na Botswana.

Amesema kuwa mkutano mkuu wa 39 wa wakuu wa nchi na serikali utaleta mabadiliko chanya nchini hasa kwa wenye viwanda katika jumuiya hiyo, na amesisitiza ushirikiano ndani ya jumuiya hiyo ili kuleta ushindani katika soko la dunia.

Kiwanda cha pili kilichotembelewa ni cha Motisun Group kilichopo Chalinze Mkoani Pwani ambacho kina viwanda vinavyozalisha bidhaa za plastiki, vinywaji, mabati pamoja na rangi za nyumba (kiboko paints).

Kiwanda hicho kinachozaliwa sharubati (juisi) ni matokeo ya jitihada za Rais Dkt. John Magufuli katika kujenga nchi ya viwanda na kupitia kiwanda hicho wakulima wamekuwa wanafaidika kwa kuwa kiwanda hununua matunda kutoka kwa mkulima yeyote huku uhitaji wa matunda kwa kiwanda hicho ukifika tani 300 kwa siku.

Abubakar Mlawa mkuu wa kitengo Cha Mawasiliano wa kiwanda hicho ameeleza kuwa kupitia maonesho hayo ya viwanda lazima wananchi wajifunze kupenda na kuthamini bidhaa za ndani;

"Mahitaji ya juisi ni makubwa sana hasa katika nchi za Zambia, Kongo na Malawi ila tuna changamoto ya maji, tunahitaji maji zaidi ya lita milioni mbili kwa siku kwa ajili ya uendeshaji lakini tunapata maji lita laki tano hivyo tunaomba Serikali itusaidie tuweze kupata maji kutoka mto Ruvu" ameeleza Mlawa.

Kiwanda hicho ambacho hulipa kodi kwa serikali takribani zaidi ya shilingi milioni 700 kimetoa ajira kwa wazawa kwa asilimia 95, huku bidhaa zikiuzwa ndani kwa asilimia 70 na ziuzwazo nje ni asilimia 30 pekee.

Aidha kiwanda hicho kinashiriki kwa kutoa bure huduma za kijamii zikiwemo afya, gari la wagonjwa na huduma ya zima moto bure.

Kiwanda cha tatu kilichotembelewa ni cha Keda Ceremics Limited kilichopo Chalinze Mikoani Pwani ambacho kinazalisha Tiles ambazo huuza na kusafirishwa katika nchi za Kenya, Ghana na Senegal.

Akitoa taarifa ya kiwanda hicho Kaimu Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bruce Ni amesema kuwa kiwanda hicho chenye uwekezaji wa dola milioni 56 ni matokeo ya jitihada zilioneshwa na Rais Magufuli na asilimia 30 za malighafi zinazotumika katika uzalishaji hupatikana Tanzania.

Ni amesema kuwa mkutano huu umetengeneza fursa kwao na kujenga mahusiano bora na nchi za Kenya, Rwanda, na Burundi na mipango yao hadi kufikia mwaka 2026 watakuwa wamelipa kodi kwa serikali zaidi ya dola milioni 12.
Meneja Masoko na Mauzo Tanzania wa kiwanda cha kusindika matunda cha Elven Agri company,Brit Bahyare akisoma hotuba yake fupi mbele ya Wajumbe wa mkutano wa 39 wa SADC walioshiriki wiki ya nne ya viwanda,ambao wametembelea kiwanda hicho jana kwa ajili ya kuangalia ubora wa bidhaa na mazingira ya uzalishaji kwa Tanzania. 
Afisa Msimamizi wa kiwanda cha matunda cha Elven Agri ,Martin Leonard Matemba (kulia) akitoa ufafanuzi mbele ya wajumbe wa SADC waliopata fursa ya kutembelea kiwanda hicho cha kusindika matunda Elven Agri company kilichpo wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.
Msemaji wa Makampuni ya Motisun Group wamiliki wa Sayona,Aboubakary Mlawa akiwaonesha wajumbe wa mkutano wa 39 wa SADC box la Juice ikiwa tayari kusafirishwa maeneo mbalimbali katika kiwanda cha kusindika matunda cha Sayona kilichopo Mboga - Msoga Chalinze mkoa wa Pwani.
Wajumbe wa mkutano wa 39 wa SADC walioshiriki wiki ya nne ya viwanda wakiangalia namna Juice inavyo sindikwa katiak kiwanda cha Sayona kilichopo Mboga - Msoga Chalinze mkoa wa Pwani.
Wajumbe wa mkutano wa 39 wa SADC walioshiriki wiki ya nne ya viwanda wakikagua kiwanda cha Keda kinachotengeneza marumaru aina ya Twyford kilichopo Chalinze mkoani Pwani
Wajumbe wa mkutano wa 39 wa SADC walioshiriki wiki ya nne ya viwanda wakiendelea kukagua kiwanda cha Keda kinachotengeneza marumaru aina ya Twyford kilichopo Chalinze mkoani Pwani.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)
(Picha zote na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...