Muonekano wa barabara ya Kikweni- Usangi Km 12.5 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Mbunge wa Mwanga Profesa Jumanne Maghembe akisisitiza jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), mhe. Elius John Kwandikwa alipokagua barabara ya Kikweni- Usangi Km 12.5 na Kikweni-Ugweno km 17 ambazo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea wilayani Mwanga (kulia), ni meneja wa TANROADS mkoa wa Kilimanjaro Eng. Nkolante Ntije.
Mbunge wa Mwanga Profesa Jumanne Maghembe akisisitiza jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), mhe. Elius John Kwandikwa alipokagua barabara ya Kikweni- Usangi Km 12.5 na Kikweni-Ugweno km 17 ambazo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), mhe. Elius John Kwandikwa akisisitiza uendeshaji makini na mahiri wa pikipiki za bodaboda kwa vijana wa Kata ya Kifula-Ugweno wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro kufuatia kuanza kukamilika kwa barabara za lami katika baadhi ya maeneo yenye milima na kona kali ili kuepuka ajali.
Muonekano wa jengo la wodi ya mama na mtoto katika hospitali ya rufaa ya Mawenzi mjini Moshi linalojengwa na Wakala wa Majengo nchini TBA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...