Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewapa Siku tano kuanzia leo October 22 Wakandarasi ambao miradi yao imekuwa ikisuasua kuhakikisha wanaanza kazi mara moja na kubainisha kuwa wakandarasi watakaokaidi agizo hilo Watakamatwa na Vyombo vya dola na Mikataba yao kuvunjwa.

RC Makonda amesema wapo wakandarasi ambao Walidanganya kwenye nyaraka za kuomba tenda kuwa wana Vifaa vya Kutosha, Wataalamu na Fedha za kutosha ili waatiwe kazi lakini baada ya kupata kazi wamekuwa wakikwama kufanya kazi kutokana na uhaba wa Vifaa jambo linalopelekea miradi kutokamilika kwa wakati na kuleta Usumbufu kwa wananchi.

Aidha RC Makonda amezionya Bodi za Manunuzi zitakazobainika kutoa tenda kwa wakandarasi kwa rushwa bila kuangalia uwezo wa Kampuni kuwa watachukuliwa hatua.

Miongoni mwa Miradi ambayo RC Makonda amesema imekuwa ikisuasua ni Ujenzi wa Mto Ng'ombe, Mfereji wa Buguruni Kisiwani, Tabata Roman Catholic,  Barabara ya Kivule na Barabara ya Kawe




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...