Jengo la NSSF Njombe.

Majengo ya kisasa yameanza kushamiri katika Mkoa  mpya wa Njombe ambao ulianzishwa rasmi mwaka 2012. zimeanza kujengwa majengo ya kisasa ya serikali, hoteli na ya watu binafsi. Pia imejengwa stendi mpya ya kisasa, soko la kisasa.
 Kanisa la Katoliki la ST Joseph la Njombe Mjini
 Baadhi ya majengo yanayochepuka Njombe Mjini
 Mtaa wa Mlowezi katikati ya Mji wa Njombe
 Benki ya NMB Njombe
 Jengo la CCM Mkoa wa Njombe lililopo Mjimwema

 Soko Kuu la kisasa la ghorofa  Mjini Njombe likiwa katika hatua za ujenzi

Moja ya vituo vipya  vya mafuta vilivyopo  Njombe. (PICHA ZOTE KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)

Mkoa wa Njombe ni mmojawapo kati ya mikoa mipya nchini Tanzania wenye postikodi namba 59000 [1], ukiwa umeanzishwa rasmi mwaka 2012[2]. Umepakana na mikoa ya MorogoroRuvumaMbeya na Iringa.
Kutokana na hadhi mpya, wilaya ya Njombe imegawanyika kati ya ile ya mjini na ile ya vijijini. Pia, mwezi wa Machi 2012, imeanzishwa wilaya ya Wanging'ombe.
Mwaka 2012 katika eneo hilo kulikuwa na wakazi 702,097 Census 2012. Jalada kutoka ya awali juu ya March 5, 2016. Iliwekwa mnamo 14 February 2016. katika wilaya sita zifuatazo: Njombe Mjini (wakazi 130,233), Njombe Vijijini (wakazi 85,747), Makambako (wakazi 93,827), Makete (wakazi 97,266), Ludewa (wakazi 133,218), Wanging'ombe (wakazi 161,816).
Makabila makubwa ya wenyeji mkoani Njombe ni WabenaWakinga na Wapangwa, na uwiano wao ni 37:11:3.
Kabila la Wabena liko wilaya ya Njombe na eneo la Malangali likiwa linapakana na wilaya ya Ulanga na wilaya ya Kilombero (Mkoa wa Morogoro), Wakinga wako wilaya ya Makete na Wapangwa wako katika wilaya ya Ludewa.
Yapo pia makabila madogo kama vile WawanjiWakisiWamandaWamagoma n.k. ambao kwa ujumla wao wanachukua asilimia 6 iliyosalia ya watu Mkoani Njombe.
Karibu wakazi wote wa mkoa ni Wakristo, hasa Walutheri na Wakatoliki.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...