Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba amewataka viongozi wa vyama vya msingi (Amcos) kuacha vitendo vya ubadhilifu na utoaji wa vyeti hewa katika msimu huu wa Korosho

Akizungumza na Viongozi wa vyama vya msingi amesema wao  wamekuwa ni chanzo Cha vyeti hewa.

"Sitaki kusikia  vyeti hewa  anayeleta  mzigo wake  ndiye  anayepaswa kulipwa  na si vinginevyo,hatutawavumilia hatua kali tutawachukulia,wakulima wapewe haki zao,"amesema Waryuba

Amesema viongozi ili waweze kuitenda kazi hii kwa weledi  ni lazima wapate makarani waaminifu ambao wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi

Hakikisheni  makarani wenu wawe na mkataba  na wadhaminiwe  na watu wenye dhamana hatutaki makarani wababaishaji,"amesema Waryuba

Aidha aliwataka wakulima kukausha korosho zao ili waweze kupata kilo sahihi wanapopeleka ghalani 

"Wakulima kausheni vizuri korosho ili zinapokwenda ghalani ziwe na kilo sahihi,mnapopeleka korosho hazijakauka vizuri zinapokaa zinakauka hivyo zinapokuja kupimwa Tena zinaonekana zimepungua utata unaanzia Hapo,"anasema Waryuba.
 Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba  akifafanua Jambo kwa viongozi wa Amcos 
Afisa Ushirika wa Wilaya Sudi Rajabu.
Baadhi ya Wananchi wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...