Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba ameipongeza Idara ya Afya kwa kushika nafasi ya Kwanza katika Halmashauri tisa za Mkoa wa Mtwara katika Kampeni ya Chanjo ya Kitaifa
Ameyasema hayo wakati akipokea taarifa ya tathimini ya Kampeni ya Chanjo ya Kitaifa Wilayani humo.
"Kazi mliyoifanya idara ya Afya ni ya kubwa kuwa washindi wa kwanza katika Halmashauri tisa si kazi ndogo,hongereni Sana,"alisema Waryuba
Naye Mganga Mkuu wa Wilaya, Antipas Swai alisema kuwa halmashauri imepata asilimia 117 kwa Surua Rubella na asulimia 115 kwa polio ya sindano
Kampeni ya Chanjo ya Kitaifa katika Wilaya ya Tandahimba ilianza Oktoba 17 Hadi Oktoba 21 mwaka huu ambapo wananchi walijitokeza kwa wingi kuleta watoto kupatiwa huduma hiyo
Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba akitoa pongezi kwa idara ya Afya
Mganga Mfawidhi wa hospital ya Wilaya Antipas Swai
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...