Meneja Mradi wa Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa (TANCDA) Happy Nchimbi akizungumza leo jijini Dar es Salaam kwenye mkutano Mkuu wa Asasi ya kuelimisha jamii kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza
 Waandishi wa habari wa Asasi ya kuelimisha jamii kuhusu magonjwa yasiyoambukiza wakifuatilia kwa makini

 Mwenyekiti wa Asasi hiyo Leon Bahati akifafanua jambo wakati wa mkutano huo ambapo amettumia nafasi hiyo kuhamasisha waandishi wa habari kuandika habari zinazoelimisha kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
 Mwanzilishi wa Taasisi ya kutoa elimu ya kisukari kwa jamii(DICOCO)Lucy Johnbosco akizungumza wakati wa mkutano huo ambapo amesisitiza umuhimuwa jamii kutambua umuhimu wa kupima afya zao kila wakati.Lucy amekuwa akiishi na ugonjwa wa kisukari kwa mwaka 19 sasa.
 Makamu Mwenyekiti wa Asasi hiyo Exuper Kachenje (aliyesimama) akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya washiriki wa mkutano mkuu wa asasi ya kuelimisha jamii kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza wakifanya mazoezi ya kunyoosha viungo kabla ya kumalizika kwa mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 
 
Na Said Mwishehe,Michuzi Globu ya jamii

ASASI ya Kuelimisha jamii kuhusu magonjwa yasiyoambukiza inayohusisha waandishi wa habari nchini(TOANCD), imefanya mkutano Mkuu wa mwaka na kuazimia mambo mbalimbali yakiwemo ya kuendelea kuandika habari zinazoelimisha kuhusu magonjwa hayo ambayo yamekuwa tishio na kusababisha vifo vya Watanzania walio wengi.

Pamoja na mambo mengine asasi hiyo imewahamasisha waandishi wengine nchini kujiunga nao kwa lengo la kuufikisha elimu na habari zinazohusu magonjwa hayo kwa wananchi walio wengi ili kuyatokomeza ambayo mengi yanatokana na staili ya maisha ambayo imekuwa chanzo kikubwa cha magonywa yasiyo ya kuambukiza.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano huo mkuu wa mwaka, Mwenyekiti wa Asasi hiyo Leon Bahati amesema ni jukumu la waandishi wenye utashi wa kuandika kuhusu habari zinazohusu magonjwa hayo kutumia fursa waliyonayo kutoa elimu kwa jamii kwa kuandika habari kwa wingi na hatimaye kuokoa jamii ya watanzania.

Amefafanua magonjwa yasiyoambukiza ni magonjwa yasiyo na vimelea vinavyoweza kusambazwa na kutoa mfano wa magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, saratani, magonjwa sugu ya njia ya hewa, kisukari, magonjwa ya akili na mengine ya kurithi kama vile selimundu.

"Magonjwa haya yanaongezeka kwa kasi na kuathiri hata watu wenye umri mdogo wakiwemo watoto.Kutokana na uwepo wa magonjwa haya kumeibuka utapeli mwingi, hivyo ni jukumu letu waandishi kupitia asasi hii kuhakikisha tunahabarisha umma jinsi ya kujiepusha na magonjwa haya na kwa wale ambayo tayari wanayo ni jinsi gani wanaweza kuwa na mfumo ambao utawawezesha kuishi,"amesema Bahati.

Ameongeza waandishi ni kundi ambalo linaweza kuwafikia watu wengi kwa urahisi zaidi kwa umoja wao wanaweza kuandaa vipindi vya redio na vya tevisheni pamoja na kuandika makala mbalimbali ambazo zitasaidia watu kubadilika. 

Bahati amesema kwa mwaka 2016 watu milioni 42 sawa ya asilimia 71 ya vifo vyote walifariki dunia kutokana na magonjwa yasiyoambukizwa huku asilimia 75 ya vifo vyote vinavyohusu watu kwenye umri wa miaka 30 hadi 70 husababisha magonjwa hayo.

Kwa upande wake Meneja Mradi wa Shirikisho la Vyama vya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa (TANCDA) Happy Nchimbi amewakumbusha waandishi wa habari nchini na hasa walioko kwenye chama hicho kuendelea kutoa elimu na vipindi mbalimbali kwa jamii kuhusu magonjwa yasiyoambukizwa kwani yamekuwa tishio  kutokana na mtindo wa maisha.

Amesema tayari kuna juhudi zinazoendelea kufanyika na matokeo yanaonekana kwa jamii kwani watu wengi hivi sasa wamekuwa wakipima afya zao, kufanya mazoezi pamoja na kubadilisha mitindo ya maisha kutokana na mradi walionao wa uelimishaji kwa jamii.

Nchimbi amesema shirikisho hilo tayari kwa mwaka jana limefanikiwa kuwafikia watu zaidi ya 1000 wakiwemo wanafunzi wa kike 40 ambao wanao uwezo wa kusimama na kutoa elimu kwa wanafunzi wenzao huku katika jamii takribani wakinamama 16 nao wamepewa elimu  ya masuala ya  kujikinga na magonjwa yasiyoambukizwa.

Amesema mradi huo umewafikia pia wanafunzi wa Dar es Salaam na Arusha na wanaendelea na utoaji wa elimu kuhusu magonjwa hayo , hivyo amesisitiza waandishi wa habari kutumia kalamu zao kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...