Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

IRAN imekiri kuidungua kimakosa ndege ya abiria ya Ukraine (Boeing 737) na kuua abiria wote 176 waliokuwamo na kueleza kuwa makosa ya kibinadamu yalitokea baada ya ndege hiyo kukatisha katika eneo linalomilikiwa na kikosi cha Mapinduzi cha nchi hiyo na kueleza kuwa maafisa waliofanya kosa hilo watachukuliwa hatua.

Televisheni ya taifa ya Iran imetoa taarifa hiyo leo ambapo awali Iran ilikanusha kutohusika na udunguaji wa ndege hiyo katika Mji kuu Terhan siku ya Jumatano. 

Pia taarifa hiyo imefuatiwa na radhi iliyoombwa na Rais wa Iran Hassan Rouhani ambaye ameeleza kuwa Serikali inajutia kitendo hicho kilicholeta madhara makubwa na kuelekeza maombi na sala zake kwa wafiwa na familia zilizoathirika.

Pia Waziri wa mambo ya kigeni wa nchi hiyo Javad Zarif ameomba radhi kwa familia, wafiwa na mataifa yaliyoathirika na tukio hilo na kusema kuwa ndege hiyo ilidunguliwa kwa bahati mbaya baada ya kupitia sehemu nyeti ya jeshi.

Hii inakuja siku chache baada ya Iran kukana madai ya wachunguzi kutoka nje ambao waliinyooshea kidole nchi hiyo kwa kuhusika
na tukio hilo ambalo mara baada ya kutokea Rais wa Marekani Donald Trump alieleza akuwa Iran inahusika na shambulio hilo huku Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau akisema kuwa vyombo vya usalama vya Canada vina ushahidi kuwa Iran imeitungua Boeing 737.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...