Kaimu Katibu tawala wa mkoa wa Arusha David Lyamongi wakati akifungua warsha ya siku moja ya wadau wa vyombo vya habari nchini
Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Arusha Cloud Gwandu akizungumza katika warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kufanyika katika ukumbi uliopo ofisi ya mkuu wa mkoa Arusha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) Joseph Butiku aliwataka waandishi wa habari nchini kujiuliza na kujitazama juu ya tahamani ya Taifa
Mwandishi wa Habari kutoka kituo cha ITV akiwa katika warsha hiyo. 
Waandishi waliojitokeza kwaajili ya warsha ya siku moja wakiwa katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa moa Arusha 
Baadhi ya waandishi wa habari waliohidhuria warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ikiwa na lengo la yenye lengo la kulinda na kudumisha amani kipindi cha uchaguzi mkuu
Baadhi ya waandishi wa habari waliohidhuria warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ikiwa na lengo la yenye lengo la kulinda na kudumisha amani kipindi cha uchaguzi mkuu 
Baadhi ya waandishi wa habari waliohidhuria warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ikiwa na lengo la yenye lengo la kulinda na kudumisha amani kipindi cha uchaguzi mkuu 

Na.Vero Ignatus,Arusha

Wadau wa habari nchini wameaswa kutumia kalamu zao kwa weledi uzalendo na utaifa kama nyenzo za uandishi wa habari kwa lengo la kuhakikisha suala zima la Amani ya nchi linapewa kipaumbele wakati wote wa kabla na baada ya uchaguzi mkuu ili kulinda Amani na Umoja wa Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu tawala wa mkoa wa Arusha David Lyamongi wakati akifungua warsha ya siku moja ya wadau wa vyombo vya habari nchini yenye lengo la kulinda na kudumisha amani kipindi cha uchaguzi mkuu iliyoandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF)

Alisema kuwa bila vyombo vya habari hakuna jambo lolote litakalofanikiwa kwani ni muhimili wan ne baada ya mihimili mitatu ya kikatiba hivyo busara inahitaji ikiendana na maadili ya uandishi wenye weledi na uzalendo kwa taifa lao.

Akaeleza kuwa sehemu yoyote duniani vyombo vya habari ni muhimu katika kuhabarisha umma kwenye suala zima la maendeleo hivyo kama hawatakuwa na weledi na utaifa wanaweza kuipelekea na kutumia vibaya tasnia hiyo hivyo nchi kujikuta ikiingia katika mchafuko.

’’Niwaombe waandishi wa habari nchini kuweka mbele utaifa weledi uzalendo katika kutekeleza majulumu yenu wakati wote tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu kwa kutumia kalamu zenu vizuri katika kujenga na kudumisha amani ,umoja ,maendeleo na mshikamano wakati wote kabla na baada ya uchaguzi mkuu’’

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) Joseph Butiku aliwataka waandishi wa habari nchini kujiuliza na kujitazama juu ya thamani ya Taifa lao katika kuhakikisha umoja ,maadili na mshikamano vinaendelea kudumishwa wakati wote wa uchaguzi mkuu pamoja na maisha ya kila siku ili kuleta maendeleo

Akawasihi kuhakikisha wanaimarisha mshikamano uliyopo nchini kwa kutumia taaluma yao katika kuhakikisha Taifa linaendelea kudumisha Amani ,mshikamano uzalendo na Utaifa kwa kujenga weledi wa taarifa zao wanazoziandika katika kukuza maendeleo ya Taifa.

‘’Kazi kubwa ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) ni kuhakikusha kuwa kukuza na kuimarisha uwezo wa viongozi na wananchi kwenye maswala ya uchaguzi,amani,umoja na maendeleo,huku tukijua kwamba uchaguzi ni shughuli muhimu inayofanywa katika kupiga kura na kupigiwa kura hivyo suala la amani wakati wote wa uchaguzi ni muhimu kwa ustawi wa taifa ‘’

Awali mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Arusha( APC)Cloud Gwandu ameishukuru Taasisi ya Mwalimu Nyerere(MNF) kwa kutoa warsha hiyo ya mafunzo kwa waandishi wa habari itakayowasaidia kuwajengea uwezo wa kuripoti kipindi chote cha uchaguzi mkuu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...