Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe
Innocent Bashungwa azindua kliniki ya Biashara Zanzibar. Tukio hili
lilishuhudiwa na Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe Balozi Amina Salum
Ali. Huduma ya Kliniki ya Biashara inalenga kutatua changamoto za
biashara kwa wafanyabiashara kwa kuwahudumia ana kwa ana. Huduma hii
hujumuisha taasisi zote za kimkakati katika kusaidia mnyororo wa
biashara. Huduma ya Kliniki ya Biashara ilianzishwa na inasimamiwa na
TanTrade
Watendaji kutoka taasisi
mbalimbali za serikali ambazo ni wezeshi katika mnyororo mzima wa
thamani ya biashara wakitoa huduma ya kusikiliza changamoto za
wafanyabaishara Zanzibar kupitia huduma ya kliniki ya biashara
inayoratibiwa na TanTrade
Katibu wa kampuni ya ZASCI Bw
Rajah Lee akimuonesha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TanTrade Dkt
Ng’wanza Kamata zao la Mwani uliothirika na ukungu katika eneo la
Glacilaria-Zanzibar. Kampuni ya ZASCI ni miongoni mwa makampuni
yanayozalisha na kuuza bidhaa ya zao la mwani-Zanzibar na TanTrade
imekuwa na jukumu la kutoa mafunzo kwa wazalishaji wa zao hilo katika
kuongeza thamani zao hilo na kulitafutia masoko ya nje.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa TanTrade akiangalia zao la mwani na kusaidia kuvuna mwani aina ya
Cottonue pamoja na wakulima wa Mwani katika eneo la Bweleo Magharibi ya
Unguja. Lengo la kufanya ziara katika eneo la uzalishaji wa Zao la Mwani
ni kufahamu maendeleo ya uzalishaji wa zao la mwani.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade
Bi Latifa Khamis akimpa maelezo Mhe Innocent Bashungwa Waziri wa Viwanda
na Biashara namna Huduma ya Kliniki ya Biashara itakavyofanya kazi
Zanzibar ili kutatua changamoto mbalimbali za wafanyabiashara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...