Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
IMEELEZWA kuwa Marekani imeongeza nchi saba zaidi zinatarajiwa kuongezwa katika orodha ya nchi ambazo zimezuiliwa kuingia nchini humo na kuelezwa kuwa nchi hizo zitazuiwa kupata baadhi ya Visa pamoja na kutolewa katika ushiriki wa bahati nasibu ya green card, vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti.

Imeelezwa kuwa Rais wa Marekani Donald Trump akiwa David nchini Uswizi kupitia gazeti la Wall Street Journal amethibitisha mpango wake kuongeza idadi ya nchi katika orodha ya nchi zilizozuiwa kuingia nchini humo.

Imeelezwa kuwa nchi ambazo zinaweza kuwa kwenye orodha hiyo ni pamoja na Myanmar, Nigeria, Sudan, Tanzania, Eritrea, Belarus na Kygyzstan.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2017 Trump akisaini zuio la namna hiyo kwa nchi zenye waislamu wengi zaidi ikiwemo Iran, Iraq, Syria, Yemen, Libya, Somalia, Venezuela, Korea kaskazini na Chad ambayo iliondolewa mwaka 2018.

 Orodha ya nchi hizo zinategemewa kuchapishwa mapema Januari 27 huku shirika la habari la Kimataifa la Reuters limeripoti kuwa mmoja wa Mwandamizi wa Serikali ya Rais Trump amedokeza kuwa orodha hiyo inakuja baada nchi hizo kushindwa kufuata masharti ya kiusalama ikiwemo taarifa za alama za vidole pamoja na taarifa za mapambano ya kigaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...