Baadhi ya
watuhumiwa wa kosa la utupaji taka ovyo, wakiingia katika gari la
Mahakama Inayotembea leo, wakati gari hilo likiwa ngazi ya Mahakama ya
Hakimu Mkazi Sokoine maafrufu ‘Mahakama ya Jiji’ kwa ajili ya
kusikiliza mashauri yao kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es
Salaam.
Mkuu wa
Wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema (wa pili kushoto) akiwa katika gari
la Mahakama Inayotembea leo kwa ajili ya kusikiliza mashauri ya
watuhumiwa wa utupaji wa taka ngumu ovyo baada ya kuvunja Sheria ya
Mazingira namba mbili ya Mwaka 2004, pamoja na sheria ndogondogo za
jiji , wakati gari hilo likiwa ngazi ya Mahakama ya Hakimu Mkazi
Sokoine maarufu ‘Mahakama ya Jiji’ kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar
es Salaam.
Mkuu wa
Wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema (kushoto) akizungumza jambo leo na
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Mhe. Martha Mpaze
,wakati gari la Mahakama Inayotembea, likiwa ngazi ya Mahakama ya
Hakimu Mkazi Sokoine maarufu ‘Mahakama ya Jiji’.
Mkuu wa
Wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema (kushoto) akizungumza jambo leo na
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Bw. Omary Kumbilamoto wakati gari la
Mahakama Inayotembea, likiwa ngazi ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine
maarufu ‘Mahakama ya Jiji’.
(Picha na Magreth Kinabo- Mahakama)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...