Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim
Wangabo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mkwamba, kilichopo wilaya
ya Nkasi katika ziara yake ya kuelemisha na kuwakataza wananchi kuacha
tabia ya kuharibu vyanzo vya maji kwa kufanya shughui za kibinaadamu
katika milima ya safu za Lyamba Lyamfipa Mkoani Rukwa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh.
Joachim Wangabo akiwasalimia baadhi ya watoto waliohudhuria kwenye
mkutano wake wa hadhara alioufanya katika Kijiji cha Swahila, Wilayani
Nkasi kuhamasisha utunzaji wa mazingira.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim
Wangabo (kushoto) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Tambarukwa,
kilichopo wilaya ya Nkasi katika ziara yake ya kuelemisha na kuwakataza
wananchi kuacha tabia ya kuharibu vyanzo vya maji kwa kufanya shughui za
kibinaadamu katika milima ya safu za Lyamba Lyamfipa Mkoani Rukwa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim
Wangabo (aiyevaa rain boot) akizungumza na wananchi wa kijiji cha
Swahila, kilichopo wilaya ya Nkasi katika ziara yake ya kuelemisha na
kuwakataza wananchi kuacha tabia ya kuharibu vyanzo vya maji kwa kufanya
shughui za kibinaadamu katika milima ya safu za Lyamba Lyamfipa Mkoani
Rukwa.
……………….
Mkuu wa Mkoa wa
Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaonya wananchi wanaokaa karibu na milima
ya Lyamba Lyamfipa kuacha maramoja kufanya shughuli za kibinaadamu
katika milima hiyo baada ya shughuli hizo kuharibu mazingira na vyanzo
vya maji vilivyomo na matokeo yake kuwasababishia maisha magumu wananchi
wanaoishi katika bonde la ziwa Rukwa lililozungukwa na milima hiyo.
Amesema kuwa kuwa
na maji ni jambo zuri lakini kuendelea kubaki nayo kwa miongo kadhaa
ijayo ni jambo kubwa zaidi na kuongeza kuwa milima hiyo ndio chanzo cha
maji cha Ziwa Rukwa, ziwa lililobeba jina la mkoa na hivyo kutokuwepo
kwa ziwa hilo ni kuondoa asili ya mkoa jambo ambalo hataruhusu litokee.
“Milima hii yote
ndio chanzo cha maji cha watu wanaoishi bonde la Ziwa Rukwa pamoja na
Ziwa Rukwa lenyewe, mkiharibu hiyo milima hiyo ni sawa na kufanya mauaji
kwa watu wanaoishi katika bonde la Ziwa Rukwa, kwasababu watakosa maji
wale wananchi lakini hata mifugo itakosa maji huko lakini tatu hata ziwa
rukwa lenyewe litakauka litajaa tope kwa hivyo vitendo vya kibinaadamu
vya kukata miti na maji yaliyopo yatakwisha litafutika,” Alisisitiza
Mh. Wangabo
ameyasema hayo alipofanya ziara katika vijiji vilivyo karibu na milima
ya Safu za Lyamba Lyamfipa katika Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga na
kuendelea kutoa elimu kwa wananchi hao juu ya utunzaji wa vyanzo vya
maji na milima hiyo ili kupunguza athari za mvua zinazowatokea watu
wanaoishi katika bonde la Ziwa Rukwa.
Amesema kuwa
kutotunza vyanzo vya maji na vyanzo vya mvua kutasababisha kilimo chetu
kutokuwa na tija na kueleza kuwa milima hiyo ndio tegemezo kwa mkoa wa
Rukwa pamoja na mikoa ya jirani na hivyo utunzaji wake ni umuhimu kwa
nchi.
Ameongeza kuwa
mahala ambapo pamefyekwa na kulimwa si sawa na mahali ambapo hapajalimwa
na penye miti kwani mvua ikija itachimba mahali ambapo pameshaharibika
na kuacha maeneo ambayo yana miti na nyasi.
Katika hatua
nyingine amewataka wananchi hao kuwa watulivu na kutoshawishiwa na
wanasiasa wasiopenda utulivu uliopo hasa katika kipindi hiki cha
kuelekea uchaguzi mkuu wa Madiwani, Wabunge na Rais.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...