Na. Catherine Sungura-Dodoma
Serikali
kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
imeahidi kuipatia kiasi cha shilingi bilioni mbili hospitali ya rufaa ya
kanda KCMC ili kuweza kutoa huduma za tiba za mionzi hospitalini hapo.
Hayo
yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Ummy Mwalimu wakati akijibu maswali kwa kamati ya kudumu ya Bunge
ya huduma na maendeleo ya jamii jijini hapo.
“Tumekubaliana
na Katibu Mkuu kuitafuta hiyo bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa
jengo la mionzi (bunker) kwa hospitali hii tutawapatia".
Aidha,
Waziri Ummy amesema kuwa wizara yake inayo muelekeo kwa hospitali zote
za rufaa za kanda kutoa huduma za mionzi hivyo hakutakuwa na haja ya
wagonjwa wa kanda ya kaskazini kusafiri hadi Ocean road kupata huduma za
mionzi.
"Wizara tumeanza kutoa huduma za
mionzi,mwaka jana tulizindua hospitali ya Bugando,lengo letu ni kuweka
huduma hizi kwenye hospitali zote za rufaa za kanda kama Mbeya na
tunafikiria kuweka na hapa kwenye hosputali ya Benjamin
Mkapa".Alisisitiza Waziri Ummy
Hata hivyo
Waziri Ummy amesema wizara imeweza kuwapatia hospitali ya KCMC fedha
kwa ajili ya watumishi pamoja na dawa kiasi cha shilingi bilioni 5
katika kipindi cha miezi sita."Kama serikali itaendelea kuthamini suala
la ubia katika utoaji wa huduma za afya na mashirika ya dini na watu
binafsi".
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa KCMC Dkt.
Gilliard Masenga amesema kuwa asilimia sitini ya wagonjwa wa saratani
wanahitaji huduma ya mionzi na hospitali hiyo imeweza kuona jumla ya
wagonjwa 4323 kwa kipindi cha mwaka jana na kufanya uchunguzi wa
magonjwa ya saratani ambapo kati yao watoto 239 na watu wazima ni
4084,aidha wamefanya kampeni maalum ya upimaji na ushauri katika wilaya
ya Arumeru na watu 307 walipatiwa huduma ya uchunguzi wa awali wa
saratani.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akijibu maswali kwenye kamati hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali ya rufaa ya kanda KCMC Dkt. Gilliard
Masenga akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya hospitali ya
KCMC kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 kwenye kamati ya kudumu ya
Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii.
Wabunge wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii wakati wa kuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya hospitali ya KCMC na hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii wakifuatilia taarifa kutoka hospitali hizo mbili .
Wabunge wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii wakati wa kuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya hospitali ya KCMC na hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii wakifuatilia taarifa kutoka hospitali hizo mbili .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...