Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
LICHA ya kutajwa na jarida la Forbe kwa kuwa mwanamke tajiri zaidi barani Afrika anayemiliki dola za kimarekani bilioni 2.2 (46) amekumbana na kashfa za ubadhilifu wa fedha kupitia mikataba kutoka sekta ya ardhi, gesi, mafuta na madini wakati wa utawala wa baba yake Jose Eduardo Did Santos aliyetawala kwa miaka 38.

Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa hati zilizovuja zinaonesha utajiri huo umetokana na unyonyaji na ufisadi kutoka kwa nchi hiyo ambayo ni tajiri zaidi katika maliasili.

Hati hizo zinaonesha kuwa Isabela na mumewe waliruhusiwa kununua mali za Serikali kupitia mikataba mibovu iliyopitishwa wakati wa uongozi wa baba yake.

Isabela anayeishi London, Uingereza na kumiliki mali nyingi huko yeye na mume wake ambaye ni mfanyabiashara maarufu kutoka nchini Kongo na mama wa watoto wa tatu amekana madai hayo na kueleza kuwa hizo ni vita vya kisiasa kwa Serikali iliyopo dhidi yake.

Isabela ambaye alitangaza kuwania kugombea urais nchini humo kwa kueleza kuwa uongozi ni kuhudumu na atafanya awezavyo katika maisha yake katika kuhudumu katika nafasi hiyo.

Hadi sasa tajiri huyo yupo chini ya uangalizi wa Mamlaka ya kupambana na rushwa huku mali zake zilizopo ndani ya nchi zikiwa zimeshikiliwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...