Kaimu Mkuu Afisa Mkuu wa biashara, David Umoh akizindua kampeni mpya iitwayo Ujanja Ni, wateja kuwa na Uwezo wa kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama nafuu kupitia huduma zilizoboreshwa zaidi.pembeni yake ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko, William Mpinga. 
Kaimu Mkuu Afisa Mkuu wa biashara, David Umoh akizindua kampeni mpya iitwayo Ujanja Ni, wateja kuwa na Uwezo wa kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama nafuu kupitia huduma zilizoboreshwa zaidi.pembeni yake ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko, William Mpinga.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko, William Mpinga akifafanua Jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa kampeni mpya iitwayo Ujanja Ni, wateja kuwa na Uwezo wa kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama nafuu kupitia huduma zilizoboreshwa zaidi. Pembeni yeke ni Kaimu Mkuu Afisa Mkuu wa biashara, David Umoh



 Kwa mara ya kwanza Tanzania, Tigo imezindua kampeni ijulikanayo kama ‘Ujanja Ni’ ikiwa na lengo la kuwapa wateja thamani ya pesa zao kila wanapotumia bidhaa za Tigo. 

Kampeni hii itawapa wateja uwezo wa kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama nafuu kupitia huduma zilizoboreshwa zaidi. Vifurushi vyote vya sauti vinampa mteja uhuru wa kupiga simu mitandao yote kwa bei ile ile.

Huduma hii ni ya kwanza katika soko la simu na ni suluhisho kwa wateja wa Tigo kwasababu itaweza kubadili namna ambavyo watu wanatumia huduma za mawasiliano hapa nchini.

“Huduma hizi zinampa mteja uhuru wa kupiga simu kwenda mtandao wowote kwa gharama ileile na wateja wanaweza kununua kifurushi chochote cha dakika, intaneti au vifurushi mchanganyiko na kufurahia faida zote muhimu kwa gharama nafuu zaidi,” alisema Kaimu Ofisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, David Umoh wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.

Aidha, vifurushi vyote vimeboreshwa kwa kuongezewa muda wa maongezi, SMS pamoja na intaneti.Pia, huduma hizi zinakuja pamoja na vifurushi vya wiki na mwezi ili kumpa mteja uwezo wa kuwasiliana zaidi, kuperuzi na kupata thamani ya pesa yake katika kila matumizi anayoyafanya.

Uzinduzi wa kampeni hii unaendana na jitihada za Serikali za kuhakikisha huduma za kupiga simu kwenda mitandao yote zinakuwa nafuu na huduma hii inampa mteja uwezo wa kufurahia mtandao mkubwa zaidi wa 4G+ hapa nchini.

“Kama kampuni ya kidigitali tunaamini kuwa huduma hii itasaidia kuongeza uhuru wa mawasiliano na kuwaunganisha wateja wetu na wapendwa wao bila mipaka kutoka Tigo kwenda mitandao mingine.Tunaanzisha huduma hii chini ya kampeni iitwayo ‘Ujanja ni’ ikiwa na maana kwamba ujanja ni kutumia fursa hii ya kupiga simu kwenda mitandao yote ukiwa na Tigo,” alisema Umoh

Pia huduma hii inawapa wateja uhuru zaidi kupitia vifurushi vya wiki pamoja na mwezi vya sauti na intaneti ambavyo vina thamani zaidi sokoni.Vifurushi hivi vinadumu kwa muda mrefu huku vikimpa mteja nafasi ya kuokoa pesa kwani vinapatikana kwa bei nafuu.

“Kwa mara ya kwanza, zaidi ya wateja 12 milioni hawatakuwa na wasiwasi tena pale wanapotaka kuwasiliana na watu waliopo kwenye mitandao mingine hapa nchini. Hii inadhihirisha jitihada zetu za kuwa mtandao ambao unampa mteja thamani zaidi kupitia huduma za kibunifu,” alisema Umoh.

Ili kupata huduma hii mteja wa Tigo anaweza kupiga *147*00# na kuchagua vifurushi vya wiki na vya mwezi kupitia menyu iliyorahisishwa.Huduma hii inapatikana pia kupitiaTigo Pesa App kwa kupiga *150*01# , au kwa kupitia tovuti ya Tigo au kwa kupiga namba ya huduma kwa wateja 100.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...