Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba amewaomba wananchi wajitokeze ili waweze kupata huduma ya kisheria katika wiki hii ya Sheria.

Waryuba alisema kuwa wananchi wanaonekana elimu ya wiki ya Sheria hawana ya kutosha  ndiyo maana hawajitokezi kwa wingi kupata huduma hii

Akizungumza katika uzinduzi wa wiki ya sheria katika viwanja vya mahakama ya Wilaya, Waryuba alieleza kuwa kauli mbiu ya mwaka huu uwekezaji na biashara ni  wajibu wa mahakama  na wadau kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji inaendana na maendeleo ya sekta ya viwanda nchini.

"Wananchi wanahitaji elimu kuhusu wiki hii ya Sheria ili waweze kupata huduma za kisheria bure ,lakini inaoneha wengi wao bado uelewa ni mdogo kuhusu wiki hii,alisema Waryuba.

Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi Joseph Waruku alieleza kuwa moja ya maboresho ya nguzo ya mahakama ni kubadilisha mtazamo wa wananchi kuhusu taswira ya mahakama ili kuongeza Imani ya wananchi na wadau kwa ujumla

Waruku alieleza kuwa lengo la wiki ya  Sheria ni kutoa elimu kwa wananchi 

"Mahakama ni chombo ambacho kinatoa haki kwa kufuata kanuni ,"alisema Waruku.
  Baadhi ya wanafunzi ambao walijitokeza kuunga mkono maandamano  ya wiki ya sheria.
DC Waryuba akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa wiki ya Sheria
 Hakimu Mkazi Mfawidhi    wa Mahakama ya Wilaya ya Tandahimba Joseph Waruku akieleza umuhimu wa wiki ya sheria
Maadhimisho ya wiki ya sheria Wilayani Tandahimba yaliambatana na maandamano  ambao yalipokewa na Dc Waryuba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...