KAMPUNI ya kuzalisha bidhaa za umeme wa jua Zola
imeahidi kuwazawadia mitambo ya Zola wanafunzi wa kidato cha nne
watakaofaulu vizuri mwaka huu ili iwe chachu kwao ya kujisomea zaidi.
Ahadi
hiyo ilitolewa jana Jijini Arushawakati wa uzinduzi wa ofisi ya Zola
mkoani Arusha,Mkurugenzi wa Kampuni ya Zola Afrika Mashariki Yusuph
Nassor alisema serikali ya sasa imejilota mumsaidia mtoto kielimu kwa
kutoa elimu bure, hivyo na wao wanaunga mkono jitihada hizo.
Licha ya kusaidia sekta ya elimu pia watajielekeza kutoa sehemu ya faida yao kwa kusaidia sekta ya afya na nyingine.
Naye
Mkuu wa Wilaya Longido Frack Mwaisumbe akizungumza kwaniaba ya Mkuu wa
Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alippngeza kampuni hiyi kwa kuamua kusaidia
serikali katika sekta ya elimu.
"Kwa kutoa zawadi hizi kutachangia kuinua elimu na watoto watasoma kwa uahindani na kuinua mkoa wetu kielimu,"alisema.Mwaisumbe
alisema baada ya zawadi hizo kutolewa mkoa utafanya vizuri kitaifa
zaidi ya mwaka jana 2019 iliposhika nafasi ya tatu katika matokeo ya
kidato cha nne.
Pia aliipongeza kwa kuajiri vijana wakitanzania wengi na kuwa kampuni ya kwanza yakizalendo.Balozi
wa Kampuni ya Zola, Idris Sultan aliahidi kuitangaza zaidi kampuni hiyo
ili watanzania hasa wa pembezoni wasio na fursa ya kutumia umeme wa
Shirika la Tanesco watumie wa Zola unaotegemea jua.
"Wengi
hawajuwi umeme huu wa jua lakini nitatangaza kote niendako ili watu
wauelewe na vijana pia nitawahamasisha wanapojenga wawe na miundombinu
ya Zola, kwani hata ukiwekewa wa Tanesco haizuii kutumia huu inakuwa
faida kwako ukikatika wa Tanesco unawasha wa Zola, "alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...