Mkurugenzi
Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Hisham Hendi (kulia) akipunga mkono kwa
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi
Seif Ali Iddi (haonekani pichani) wakati akikabidhi kiasi cha shilingi
milioni 300 kwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar zilizotolewa na kampuni
ya Vodacom leo ili kupambana na kudhibiti ongezeko la virusi vya Corona
visiwani humo, ambapo walifanya makabidhiano kwa njia ya mtandao.
Pembeni ni Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation, Rosalynn Mworia.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali
Iddi na Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Shaaban Seif
Mohammed wanaonekana kwenye Skrini wakiongea na Mkurugenzi Mkuu wa
Vodacom Tanzania PLC, Hisham Hendi na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania
Foundation, Rosalynn Mworia wakati Taasisi ya Vodacom Tanzania
Foundation walipokabidhi kiasi cha shilingi milioni 300 kwa serikali ya
Mapinduzi Zanzibar leo ili kupambana na kudhibiti ongezeko la virusi vya
Corona visiwani humo. Makabidhiano hayo yalifanyika kwa njia ya mtandao
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...