Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
USAFIRI
wa pikipiki umekuwa maarufu zaidi barani Afrika hasa katika ukanda wa
Afrika Mashariki hasa kwa nchi za Tanzania, Kenya na Uganda ambako
nchini Tanzania hufahamika zaidi kwa jina la bodaboda huku Kenya wakiita
pikipikis, Rwanda wakiita Moto na Nigeria wakiita Okada.
Pikipiki
ni jina lililotokana na mlio/sauti ya kifaa chenyewe 'Pikipiki'
wengine huita 'Tukutuku' na umekuwa usafiri wa dharura kwa watu wengi
pindi wanapochelewa mahali au wanapotaka kukwepa foleni katika miji
yenye misongamano.
Ripoti
zinaonesha kuwa nchi za Afrika Kusini, Nigeria, Tanzania, Kenya,
Uganda, Misri, Morocco, Angola, Algeria na Ethiopia zina uwingi wa
pikipiki zinazotumika kusafirisha abiria na bidhaa na hiyo ni kutokana
na kupitika kwa urahisi katika barabara za nchi hizo huku madereva wa
vyombo hivyo wakihusishwa na matukio ya kusababisha ajali, wizi na
kuvunja sheria za barabara.
Kutokana
na urahisi na masafa marefu ya kuvuka mipaka ambayo pikipiki inaweza
kukatiza ndipo ulipoanzia msamiati wa bodaboda kwa maana ya "border to
border" nchini uganda pikipiki zilianza kuvuka mpaka kuelekea Kenya
kupitia mji wa Busia katika miaka ya 1990 hapo ndio msamiati wa bodaboda
ukashamiri zaidi.
Nchini
Uganda kwa mujibu wa Shirika la utangazaji la BBC imeelezwa kuwa mwaka
2000 kulikuwa pikipiki nyingi kuliko matatu (daladala) ambazo zilizokuwa
zikiendesha shughuli za usafirishaji wa watu na mizigo nchini humo.
Vijana
wengi nchini Uganda wamejitengenezea ajira kupitia uendeshaji wa
bodaboda pamoja na kuwa kivutio kwa watalii wanaokuja nchini humo.
Nchini
Kenya imeelezwa kuwa zaidi ya pikipiki 16,000 husajiliwa kwa mwezi na
inaelezwa kuwa hadi sasa kuna zaidi ya pikipiki milioni moja zinazofanya
kazi.
Nchini
Tanzania ripoti zinaonesha kuwa kwa mwaka 2010 kulikuwa na ongezeko la
pikipiki hadi kufikia 1,047,659 na nyingi humilikiwa na vijana ikiwa ni
sehemu ya kujitafutia ridhiki zao.
Katika
maeneo mengi ya Miji usafiri wa bodaboda umekuwa maarufu na wenye
ulazima katika kuharakisha safari, na hali ya kusimamia usalama wa
madereva na abiria umewekewa mkazo hasa katika kuzingatia matumizi ya
kofia ngumu (helmet,) kutobeba abiria zaidi ya mmoja na kutotumia pombe
wakati wa kuendesha vyombo hivyo.
Licha
ya kurahishisha usafiri bado bodaboda nchini Tanzania zinakupambana na
changamoto mbalimbali ikiwemo vifo (3,468 kwa mwaka 2015) huku asilimia
60 ya wagonjwa wanaotibiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili asilimia
60 ni majeruhi wa ajali za pikipiki.
Kutokana
na maendeleo ya sayansi na teknolojia usafiri wa bodaboda umepanda
hadhi, watumiaji wamekuwa wakitumia simu zao kupata usafiri wa bodaboda
kupitia Uber au Taxify mahali popote.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...