NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA.
MKUU wa wilaya ya
Kibaha ,mkoani Pwani ,mhandisi Martin Ntemo amewataka wadau wa elimu na
maendeleo wilayani humo, kuunga mkono juhudi za Serikali za kutatua
changamoto za sekta ya elimu ikiwemo kuondoa upungufu wa madawati na
majengo ya madarasa ,ili hali kuweka mazingira bora kwa wanafunzi.
Aidha amewaasa walimu, kufanyia ukarabati madawati yanayoharibika kwenye shule zao ili kukabiliana na upungufu wa madawati.Akizungumza na walimu
na wanafunzi wa shule za msingi Maendeleo na Maili Moja wakati wa
kukabidhi madawati 250 yaliyotolewa na Halmashauri ya Mji wa Kibaha kwa
shule hizo ,Ntemo alisema huu sio wakati wa kuiachia serikali pekee
kutatua changamoto za elimu.
Ntemo alisema
,serikali inaendelea na mpango wa kukabiliana na changamoto za elimu ili
kuhakikisha wanafunzi wanasoma kwenye mazingira magumu.“Tunaishukuru
halmashauri kwa kutoa madawati hayo ambayo yatasaidia kukabili
changamoto ya baadhi ya wanafunzi kukaa chini lakini pia hakikisheni
mnafanya ukarabati pale madawati yanapoharibika ili kupunguza changamoto
hii,” alisema Ntemo.
Naye mkurugenzi wa
Halmashauri ya Mji wa Kibaha Jenifa Omolo alieleza, halmashauri ina
upungufu wa madawati 2,000 kwa shule za msingi ambapo kwenye karakana ya
Iramba Furniture wametengeneza madawati 500 na karakana ya mtaji wa
maskini ni nguvu zake mwenyewe wanatengeneza madawati 200.
Omolo alisema kuwa madawati yaliyosalia watayatengeneza kabla ya mwaka wa fedha kwisha Julai mwaka huu.Kwa upande wake
mwalimu mkuu wa shule ya msingi Maendeleo Mariam Mkama aliishukuru
Halmashauri kwa kuwapatia madawati hayo kwani itasaidia kupunguza
upungufu wa madawati hayo.Wanafunzi wa shule hizo walishukuru msaada huo kwani madawati hayo yatasaidia kusoma vizuri na kuwa na mwandiko mzuri
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...