Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Mhe Godfrey Mheluka (kushoto) akimweleza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja changamoto ambazo wananchi wake wanapata kutokana na Tembo kuvamia mazao yao eneo la Ranchi ya Kitengule Wilaya ya Karagwe na Kerwa mkoani kagera.
KAGERA
Wizara ya Maliasilii na Utalii
imewataka wananchi wa Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera kutoa taarifa kwa
uongozi wa Wilaya mara tu wanapokumbana na changamoto ya kuvamiwa na
Tembo katik
a maeneo yao .
Wito huo unatolewa na Wizara hiyo baada ya wanyama hao kuvamia Eneo la Ranchi ya kitengule Wilaya ya karagwe na kerwa wilayani humo na kusababisha uharibifu katika maeneo ya mashamba pamoja na mifugo hali ambayo imesababisha hofu kubwa kwa wananchi wilayani humo
Akizungumza Mkoani humo kwajili ya kutatua mgogoro huo Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Mary Masanja ametoa maelekezo kwa mkuu wa kanda hiyo kuwa wanyama hao watatolewa si chini ya miezi miwili na kupelekwa kwenye hifadhi ya burigi chato ambako ndipo walipokuwa.
‘’ kwahiyo niwatoe wasiwasi na ziara yangu hii ilikuwa ni moja ya kutatua changamoto ambazo tumezisikia, tunasikia kuwa hadi watu wanakufa kwa changamoto za wanyama wakali wakiwemo tembo ,kwahiyo wizara tumelichukua na tunakwenda kulifanyia kazi kwa haraka zaidi kuhakikisha kwamba hali inatulia na wananchi waendelee kuishi kwa amani’’ alisema Mhe. Mary
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya
hiyo Godfrey Mheluka ameshukuru kwa kitendo cha Naibu Waziri kuwasaidia
changamoto hiyo huku akisema tembo hao wasipo hamishwa wanaweza kuhama
na kwenda sehemu nyingine.
‘’tunashukuru sana kwa kutuahidi kutolewa kwa hawa tembo ,kubwa
zaidi kagera sugar wameshanza kilimo cha miwa kwahiyo ina maana
wasipoondoka wataendelea kula ile miwa lakini jambo jingine la pili
tunapakana na mto na Uganda ,kwahiyo tusipowahamisha ipo siku wataenda
Uganda, kwahiyo sisi tunashukuru sana kwa ujio wako wa kuja hapa kwani
tumepata faraja kubwa, hata hivyo tunawashukuru sana TANAPA tumekuwa
tukishirikiana nao sana, hivi ninavyoongea wameshaweka tayari kituo
pale’’
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...