Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) katika mpango wake wa kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini leo tarehe 18/5/2021 imefanikiwa kutoa mafunzo Kwa wachimbaji 409 katika Mkoa wa Mara kwa kipindi cha siku tatu.
Mafunzo hayo yaliyofunguliwa tarehe 16/5/2021 na mheshimiwa Waziri wa Madini Doto Biteko yamefanyika kwa nadhari na vitendo katika sehemu mbalimbali za Mkoa wa Mara ambapo jumla ya wachimbaji wadogo wa Madini 270 walipata mafunzo Kwa vitendo ambapo eneo la Buhemba wachimbaji wadogo 37 , Gedeli wachimbaji 126,Nyamongo wachimbaji 67, Ikungu wachimbaji 40 , Kwa upande wa nadharia jumla ya wachimbaji 139 walifundishwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...