Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abulla amewataka Mabalozi walioteuliwa karibuni kuendana na kasi ya viongozi wakuu wa Serikali wakati wakiwakilisha Tanzania katika nchi zao walizopangiwa.

Mhe.Hemed alieleza hayo alipofanya mazungumzo na mabalozi hao walipofika Ofisini kwake Vuga Jijini Zanzibar kwa lengo la kuagana nae.

Alisema Imani ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyonayo kwa Mabalozi hao ni ishara kuwa na wana uwezo na vigezo vizuri vya kuiwakilisha Tanzania katika maneo yao ya kazi waliopangiwa.

Makamu wa Pili wa Rais Aliwataka balozi hao kutumia fursa hiyo kwa kujenga ushawishi na kuvutia wawekezaji tofauti na ili waje kuekeza nchini Tanzania kutokana na vivutio mbali mbali vilivyopo.

Aliwaasa kuzingatia miongozo waliyopewa na viongozi wakuu hasa maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akiwaapisha.

Akizungumza kwa niaba ya Mabalozi wenzake, Balozi Grace Afraid Olotu Balozi wa Tanzania nchini Sweden alisema miongoni mwa maeneo watakayokwenda kuyasisimia ni kukuza hadhi ya bidhaa zinazozalishwa nchini Tanzania ili ziweze kukubalika katika soko la kimataifa hasa nchi za Umoja wa Ulaya.

Balozi Grace alieleza kuwa watatua dhamana zao walizokabidhiwa katika kuhakikisha wanajenga Diplomasia ya Uchumi kwa lengo la kukuza uchumi wa Tanzani.

Mabalozi waliofika Kumuaga Makamu wa Pili wa Rais ni pamoja na Balozi wa anaewakilisha Tanzania nchini Sweden, Balozi wa anaewakilisha Tanzania nchini Marekani, Balozi wa anaewakilisha Tanzania nchini Italia, Balozi wa anaewakilisha Tanzania nchini Geneva pamoja na Balozi wa anaewakilisha Tanzania nchini Rwanda.




Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akiwaelekeza Mabalozi walioteuliwa Karibuni kuiwakilisha Tanzania katika mataifa tofauti kuzingatia maelekezao ya Mhe. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kukuza Diplomasia ya Uchumi.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...