Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kueleza uamuzi wa Serikali kuongeza muda wa Sensa ya Viwanda Tanzania Bara hadi Agosti 31,2015 na hatua zitakazochukuliwa kwa viwanda vitakavyoshindwa kutoa takwimu za uzalishaji kwenye Madodoso ya Sensa.
Kaimu Meneja wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Mkoa wa Dar es salaam Bw.
Albert Kapala akitoa ufafanuzi wa lengo la Sensa ya Viwanda na Idadi ya viwanda
vilivyotoa taarifa za Sensa hiyo jijini Dar es salaam.
NA: Veronica Kazimoto
SERIKALI imeongeza muda wa mwisho wa kukamilisha zoezi la ukusanyaji wa takwimu za Sensa
ya viwanda kote nchini hadi Agosti 31 , 2015 kufuatia viwanda vipatavyo 366
vilivyoko jijini Dar es salaam kushindwa kuwasilisha taarifa muhimu za
uzalishaji kwenye madodoso ya Sensa hiyo.
Akitoa
taarifa ya kuongezwa kwa muda wa Sensa hiyo hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam Saidi Meck Sadiki amesema kuwa Viwanda 366 ambayo ni sawa
na asilimia 20 katika jijini Dar es salaam vimeshindwa kukamilisha na kurudisha
madodoso ya taarifa muhimu za viwanda hivyo.
Amesema
Sensa hiyo ilianza Machi 9 mwaka huu na ilitarajiwa kukamilika Juni 8, 2015
lengo likiwa kukusanya takwimu sahihi zinazohusu Sekta ya Viwanda na mchango
wake katika uchumi wa Tanzania.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...