Meneja wa Chapa ya Valeur Superior Brandy,
Bi. Warda Kimaro akizungumza katika uzinduzi wa shindano lijulikanalo kama ‘Valeur Comedy Nights’ leo katika viwanja vya TCC Club Chang’ombe, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja
Mkuu wa kampuni ya Vuvuzela Bw. Evans
Bukuku
Meneja
Mkuu wa kampuni ya Vuvuzela, Bw. Evans
Bukuku akizungumza jinsi shindano hilo litakavyofanyika katika manispaa 3 za Dar es Salaam uzinduzi huo uliofanyika wa shindano lijulikanalo kama ‘Valeur Comedy Nights’ leo katika viwanja vya TCC Club Chang’ombe, jijini Dar es Salaam. Na kulia ni Meneja wa Chapa ya Valeur Superior Brandy,
Bi. Warda Kimaro
Wawakilishi
kutoka Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) wakiongezea kuhusiana na Valeur Comedy Nights’ wakiwa na
Mkuu wa kampuni ya Vuvuzela Bw. Evans
Bukuku. Picha na Avila Kakingo Globu ya Jamii.
TANZANIA Distilleries Limited (TDL) kupitia chapa yake ya ‘Valeur Superior Brandy’, kwa kushirikiana na kampuni ya Vuvuzela Company Ltd leo hii imezindua rasmi shindano lijulikanalo kama ‘Valeur Comedy Nights’. Hili ni shindano la kusaka, kuinua na kuendeleza vipaji vya Sanaa ya ucheshi litakaloanza wiki hii jijini Dar Es Salaam.
Vuvuzela ni kampuni inayojihusisha na Sanaa ya ucheshi, ikimiliki pia onyesho kubwa la Sanaa ya ucheshi jijini Dar Es Salaam lijulikanalo kama ‘Evans Comedy Night’.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Meneja wa Chapa ya Valeur Superior Brandy, Bi. Warda Kimaro alisema. “Kauli mbiu ya chapa yetu ya Valeur Superior Brandy ni ‘Kwa story zinazonoga’.
Watumiaji wapenzi wa Valeur hupenda sana story nzuri wakiwa katika mapumziko yao, tunaamini kwamba story nzuri na sanaa ya ucheshi vitaweza kufanya mapumziko ya wapenzi wa Valeur kuwa bora zaidi.
Tumeungana na Vuvuzela Entertainment na tuko hapa leo kuzindua ‘Valeur Comedy Nights’. Lengo letu ni kusaka na kukuza vipaji vya Sanaa ya ucheshi hapa Tanzania, kuwafanya wasanii hawa kugundua fursa waliyo nayo kupitia sanaa hii ya ucheshi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...