Na
Bashir Yakub.
Wako wasimamizi
wa mirathi wa
aina mbili. Kwanza ni yule
ambaye marehemu mwenyewe
amemteua kabla ya
kufa kwake na akaandika/kusema kwenye
wosia kuwa fulani
ndiye atasimamia mirathi
yangu baada ya
kuondoka.
Pili, ni yule
ambaye hakuteuliwa na
marehemu mwenyewe bali
ameteuliwa na wanafamilia
kwenye kikao cha
familia. Kwa walio wengi
huyu ndiye tunamjua
kuwa ni lazima
jina lake lipelekwe
mahakamani kwa ajili
ya kuthibitishwa ili
aweze kuwa msimamizi kamili.
Makala yatapitia Sheria
ya Usimamizi wa Mirathi, Sura ya 352 na kanuni zake.
1. HAKI
NA WAJIBU WA
WASIMAMIZI WA MIRATHI.
Haki na wajibu
wa msimamia mirathi
aliyeteuliwa na marehemu kabla ya kifo na ambaye
hakuteuliwa na marehemu ni sawa.
Awe aliteuliwa na
marehemu mwenyewe au
aliteuliwa na wanafamilia
bado haki na wajibu
alionao ni uleule.
Wajibu mkuu wa
msimamia mirathi ni
kuwa mwadilifu, na kuenenda
kwa mujibu wa
sheria katika kila
hatua anayopiga katika kusimamia
kwake mirathi.
2. SIO
LAZIMA MSIMAMIZI WA MIRATHI
AWE NDUGU/MWANAFAMILIA.
Hili ni muhimu zaidi
kulieleza. Sio kweli
kuwa msimamizi wa
mirathi lazima awe mtoto
wa marehemu, shangazi, baba mdogo/mkubwa,
mjomba kaka,dada nk. Bali msimamizi
wa mirathi anaweza
kuwa yeyote. Suala la
msingi ni atimize
sifa za kuwa
msimamizi wa mirathi. Na katika sifa hamna udugu.
Hakuna haja ya
kuwa na ugomvi
kuwa msimamizi wa
mirathi lazima atoke
katika familia. Hakuna ulazima
huo ikiwa mmeshindwa
kuaminiana kwenye familia. Mnaweza kumteua
hata kiongozi wa
dini au mtu mwingine
yeyote muadilifu ambaye
mnadhani ataweza kutenda
haki katika usimamizi.
Jambo jingine msimamizi
wa mirathi sio
lazima awe mmoja. Ikiwa
kuna pande mbili zinazozana
basi sheria inaruhusu
kila upande kutoa
msimamizi wa mirathi
ili alinde maslahi
ya upande wake.
Kwahiyo wasimamizi watakuwa
wawili na sheria
haikatazi.
Nyongeza ya hapo ni
kuwa hata kampuni au taasisi inaweza kuteuliwa kusimamia mirathi.
KUSOMA ZAIDI
sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...