Bodi ya Utalii Tanzania imeshiki kutoa taarifa za utalii wa Tanzania kwa watalii takribani 570 waliowasili kwa meli ya kitalii ya kampuni ya Nautical Majuro katika Bandari ya Dar es Salaam .

Ujio wa Meli hii ya kitalii ni mwendelezo wa juhudi zinazofanywa kwa kushirikiana na wadau wa Utalii wa Tanzania kwa dhamira ya kuwajulisha watalii kutoka katika nchi mbalimbali duniani kuwa wanaweza kuja kuvitembelea vivutio vya utalii vya Tanzania kwa kutumia njia mbali mbali za usafiri (meli, ndege na njia ya barabara).

Watalii hawa wameweza kutembelea Pori la Akiba la Selous, eneo la Mlima Kilimanjaro, Mji wa Kihistoria wa Bagamoyo na jiji la Dar es Salaam.

Meli hii imeanza safari zake katika bara la ulaya imewasili Tanzania tarehe 2/01/2018 saa 2 asubuhi na kuondoka saa moja usiku.
Baadhi ya Watalii wakishuka kutoka kwenye meli ya kitalii ya kampuni ya Nautica Majuro katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mtalii wakipiga picha “Selfie” punde baada ya kuwalisili katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mtalii akicheza ngoma baada kunogewa na mrindimo wa ngoma ya utamaduni wa Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...