Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo amefungua semina ya kimkakati inayolenga kulifanya jiji la Dar es salaam kuwa katika mpangilio wa kisasa na kuhakikisha mitaa yote inawekwa katika mfumo wa anwani za makazi na Postikodi Kama ilivyo kwa majiji makubwa ulimwenguni.

RC Makonda amesema Mfumo huo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi kwakuwa utarahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo kuwezesha kila mwananchi kuwa na anwani, kuwasaidia wageni kujua maeneo, kudhibiti wezi na matapeli, ulinzi na usalama, kusaidia kampeni ya usafi pamoja na kusaidia Jeshi la zimamoto na uokoaji kufika haraka kwenye eneo lenye dharura Kama ajali ya Moto au nyinginezo na kuokoa maisha.

Aidha RC Makonda amewapongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA kwa kuzifikia Kata 45 Kati ya 102 za mkoa huo na kueleza kuwa atawapatia ushirikiano wa kutosha kuhakikisha Mfumo wa anwani za makazi na Postikodi unafikia jiji Zima.Pamoja na hayo RC Makonda amewaomba TCRA kupeleka elimu hiyo kwa Madiwani na wenyeviti wa mitaa ili kuwajengea uelewa.

Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi unalenga kuhakikika kila Eneo, Kata na Mtaa vinapewa majina na kila nyumba inakuwa na namba ya utambuzi.
CHO2

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...