Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Mhe. Paul Makonda leo amefungua semina ya kimkakati inayolenga kulifanya
jiji la Dar es salaam kuwa katika mpangilio wa kisasa na kuhakikisha
mitaa yote inawekwa katika mfumo wa anwani za makazi na Postikodi Kama
ilivyo kwa majiji makubwa ulimwenguni.
RC Makonda amesema Mfumo huo ni
ukombozi mkubwa kwa wananchi kwakuwa utarahisisha huduma kwa wananchi
ikiwemo kuwezesha kila mwananchi kuwa na anwani, kuwasaidia wageni kujua
maeneo, kudhibiti wezi na matapeli, ulinzi na usalama, kusaidia kampeni
ya usafi pamoja na kusaidia Jeshi la zimamoto na uokoaji kufika haraka
kwenye eneo lenye dharura Kama ajali ya Moto au nyinginezo na kuokoa
maisha.
Aidha
RC Makonda amewapongeza
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA kwa kuzifikia Kata 45 Kati ya 102
za mkoa huo na kueleza kuwa atawapatia ushirikiano wa kutosha
kuhakikisha Mfumo wa anwani za makazi na Postikodi unafikia jiji
Zima.Pamoja na hayo RC Makonda amewaomba TCRA kupeleka elimu hiyo kwa
Madiwani na wenyeviti wa mitaa ili kuwajengea uelewa.
Mfumo wa Anwani za Makazi na
Postikodi unalenga kuhakikika kila Eneo, Kata na Mtaa vinapewa majina na
kila nyumba inakuwa na namba ya utambuzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...