Na Grace Michael, Katavi
SERIKALI imepongeza jitihada za kusogeza huduma za matibabu zinazofanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kupitia mpango wake wa kupeleka Madaktari Bingwa katika mikoa mbalimbali nchini hususan yenye upungufu wa wataalam.
Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bw. Amos Makala wakati akizindua huduma za Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo.
“Wazo la kuanzisha na kuendeleza mpango huu ni la manufaa makubwa kwa wananchi wetu kwani sio wananchi wote wanaweza kuzifikia huduma hizi za kitaalam huko zilipo hivyo kuleta huduma hizi hasa katika Mkoa huu jambo zuri na la kupongezwa sana,” alisema Bw. Makala.
Alisema kuwa kitendo cha NHIF kupeleka Madaktari hao kinapunguza gharama kwa wananchi na upotevu wa muda wa kufuata huduma hizo katika Hospitali kubwa lakini pia inasaidia kwa kiwango kikubwa kuimarisha huduma za matibabu katika hospitali wanazopeleka mpango huo.
Kutokana na umuhimu huo, alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi wote wenye uhitaji kujitokeza ili wanufaike na huduma hizo lakini pia kuhakikisha kila mwananchi anakuwa mlinzi wa huduma za Mfuko ili uweze kuimarika na kuendelea kuwahudumia Watanzania.
“Mbali na kuleta wataalam hawa lakini pia wameleta na dawa na vitendanishi mbalimbali kwa ajili ya kuhakikisha wananchi hawakosi huduma walizofuata, tunawashukuru sana NHIF,” alisema Bw. Makala.
Mkuu
wa Mkoa wa Katavi. Bw. Amos Makala akihutubia wananchi wakati wa
uzinduzi wa mpango wa Madaktari Bingwa unaotekelezwa na Mfuko wa Taifa
wa Bima ya Afya Mkoani humo.
Mkurugenzi
wa Huduma za Matibabu na Ushauri wa Kiufundi, Dkt. Aifena Mramba akitoa
maelezo ya awali katika hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Madaktari Bingwa
Mkoani Katavi.
Mkuu
wa Mkoa wa Katavi. Bw. Amos Makala akipokea dawa na vitendanishi
ambavyo vitatumika katika zoezi la kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa
Katavi kupitia Mpango wa Madaktari Bingwa.
Madaktari Bingwa wakifuatilia tukio la uzinduzi wa kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi. Bw. Amos Makala akimwangalia mtoto aliyeletwa hospitalini hapo kwa ajili ya huduma za Madaktari Bingwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...