Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imewahukumu wakulima wawili na mfanyabiashara mmoja kutumikia kifungo cha miaka 20 gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na vipande vitano vya meno ya tembo na kuongoza uhalifu.

Washtakiwa waliohukumiwa ni Amiri Fransis (44), mkulima Mkazi wa Tanga, Jairab Rashid (33), mkulima na Ibrahim Mkande (30) ambaye ni mfanyabiashara.

Hukumu hiyo imesomwa leo Novemba 19 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya kuridhika na ushahidi wa mashahidi sita wa upande wa Jamhuri uliowasilishwa mahamani hapo pamoja na vielelezo vinne ikiwemo hati ya tathimini ya nyara za Serikali.

Hakimu alisema washtakiwa walikuwa wanatuhumiwa na makosa mawili ya kuongoza mtandao wa kiarifu na kukutwa na nyara za Serikali, Mahakama imewakuta na hatia, ambapo watatumikia kifungo cha miaka 20 jela.

Akisoma hukumu hiyo, hakimu Shaidi amesema, makosa haya ni makubwa sana, yanapelekea kuharibu utalii wa Taifa zima."Nyie ni wabinafsi sana m nataka kujinufaisha kibinafsi kwa Mali ambazo zinasaidia Taifa zima" amesema Hakimu Shaidi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...