Waziri wa Madini, Doto Biteko tarehe 16 Januari, 2019 amekutana na kampuni  inayojishughulisha na uyeyushaji wa madini ya bati katika wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ya Tanzaplus katika Ofisi za Wizara ya Madini zilizopo jijini Dodoma.  Kikao chake  pia kilishirikisha Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Madini, Augustine Ollal, Mhandisi Migodi Mkuu kutoka Tume ya Madini, Conrad Mtui pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Madini. 

Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kampuni ya Tanzaplus Minerals kwa kushirikiana na kampuni nyingine ya AIMGROUP kutambulisha teknolojia ya mfumo wa usimamizi wa uzalishaji, usafirishaji na uuzaji wa madini. Waziri Biteko aliitaka kampuni ya Tanzaplus kuendelea kufanya utafiti zaidi juu ya mfumo husika kwa kushirikisha wadau mbalimbali  kabla ya kuwasilisha pendekezo lake Serikalini.
 Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akizungumza na watendaji wa kampuni inayojishughulisha na uyeyushaji wa madini ya bati katika wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ya Tanzaplus. Waliokaa kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Madini, Augustine Ollal, na Upendo Fatukubonye na Hamis Mhando ambao ni watendaji kutoka kampuni ya Tanzaplus.
 Mkurugenzi kutoka kampuni ya Tanzaplus, Hamis Mhando (kulia) akielezea  jinsi teknolojia ya mfumo wa usimamizi wa uzalishaji, usafirishaji na uuzaji wa madini inavyofanya kazi.
Wataalam kutoka Wizara ya Madini wakinukuu maelekezo mbalimbali yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Madini, Doto Biteko (hayupo pichani) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...