Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
INAYAT Kassam ambae ni Mkurugenzi wa kampuni ya Scorpio Africa Ltd amejizolea umaarufu tena baada ya kuwa mmoja wa Watu waliojitolea kuokoa manusura wa shambulizi la Kigaidi la Westgate mwaka 2013 na kuendelea kupata sifa baada ya kujitokeza kwa mara nyingine  kuokoa Watu waliokuwepo eneo Riverside Nairobi, Kenya lililoshambuliwa na Magaidi wa Alshabaab jana.
Septemba 21 miaka 6 iliyopita wakati magaidi walipovamia Westgate na kuua watu 62 Inayat alijitokeza na kushirikiana na vyombo vya dola na kuwanusuru mamia ya watu.
Akiwa mkufunzi wa usalama na mjuzi wa kutumia silaha za moto alijitokeza tena jana eneo la Riverside na kushirikiana na vyombo vya dola kuwaokoa manusura.

Watu wengi wamemshukuru na kumwita shujaa wa Kenya kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...