Kuelekea Tamasha la Kihistoria la Pasaka kwa mwaka 2019, Kampuni ya Msama Promotions imetoa msaada katika vituo Sita vya Watoto wasiojiweza  ili kujikimu kimaisha.

Msama Promotions imetoa msaada huo kwenye vituo vya Sifa (Bunju), Zaidia (Sinza), Maunga (Mkwajuni), Honoratha (Temeke), Watoto Wetu Tanzania na Mwandaliwa (Boko).

Akizungumza na Waandishi wa Habari baaada ya kutoa msaada huo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Alex Msama amesema Tamasha hilo linafanya kazi yake pamoja na kuisaidia jamii isiyojiweza.

"Kama kawaida yetu Kampuni ya Msama Promotions kujali Watoto Yatima, kuwasaidia kwa kiwasomesha kuwapa mambo mbalimbali ikiwemo Chakula na Malazi", amesema Msama.

Pia, Msama ametoa wito kwa Kampuni nyingine kuwasaidia Watoto hao wasiojiweza ili kujikimu kimaisha kama ilivyo kwa Watoto wengine waliokuwa na wazazi wao.

Tamasha hilo la Kihistoria linatarajiwa kufanyika April 21, 2019 katika jiji la Dar es Salaam ambapo linatarajiwa kuzunguka mikoa 10, likiwa na lengo la kuombea Taifa pamoja na Viongozi wake akiwemo Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akijiandaa kugawa msaada wa vyakula katika vituo sita ambavyo ni Sifa (Bunju), Zaidia (Sinza), Maunga (Mkwajuni), Honoratha (Temeke), Watoto Wetu Tanzania pamoja na Mwandaliwa (Boko).
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akikabidhi msaada wa vyakula kwa baadhi ya vituo vya watoto wasiojiweza,Msama ametoa msaada huo kwa vituo sita ambavyo ni Sifa (Bunju), Zaidia (Sinza), Maunga (Mkwajuni), Honoratha (Temeke), Watoto Wetu Tanzania pamoja na Mwandaliwa (Boko).
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari mara baada ya kutoa msaada kwa vituo sita vya jijini Dar,ikiwa ni sehemu ya fedha zilizokuwa zikipatikana katika tamasha la pasaka,ambalo hufanyika kila mwaka,likianzia jijini Dar na kuendelea katika mikoa zaidi ya 10
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akifurahia jambo na mmoja wa watoto mara baada ya  kutoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo vyakula  kwa vituo sita vya jijini Dar,ikiwa ni sehemu ya fedha zilizokuwa zikipatikana katika tamasha la pasaka,ambalo hufanyika kila mwaka,likianzia jijini Dar na kuendelea katika mikoa zaidi ya 10
Mara baada ya kutoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali,Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama pia alipata wasaa wa kula chakula cha pamoja na baadhi ya watoto hao waishio katika mazingira magumu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...