Watu wawili wa familia moja, wanashikiliwa na Polisi Mkoani Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya mfanyabiashara wa ufuta Oswald Malambo na kupora kiasi cha shilingi milioni 55.

Watuhumiwa hao ambao ni wakazi wa Kata ya Ifumbo Wilayani Chunya, inasemekana waliweka kitu kinachodhaniwa ni sumu kwenye kinywaji alichotumia mfanyabiashara huo, wakati wakiwa kwenye hotel baada ya kufanikiwa kuuza ufuta.

Kamada wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ulrich Matei, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.

Kamanda, amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Raphael Walolile na Goliat Walolile.Amesema tukio hilo lilitokea Juni 2 mwaka huu na kwamba marehemu ndiye aliyetoa taarifa za kwamba alinyweshwa sumu na watuhumiwa lakini bado haijathibitishwa.

“Kwa sasa bado tunasubiri taarifa za daktari na kama itabainika ni sumu sheria zitachukuliwa dhidi yao ikiwa na kufunguliwa shitaka la mauaji,”

Aidha, akizungumzia hilo, Msemaji wa familia hiyo, Mhandisi Selemani Malambo, alisema ndugu yao alienda kuuza ufuta eneo la Mbalizi Halmashauri ya Mbeya, akiwa mzima lakini baada ya kuuza ufuta wakati akijiandaa kurudi aliombwa na watuhumiwa wakafanye mazungumzo.

Mhandisi Malambo amesema watuhumiwa walimtaka ndugu yao huyo wakazungumze naye kwenye moja ya bar zilizopo katika eneo la Kabwe Jijini Mbeya na alipofika katika eneo hilo, watuhumiwa hao, walimtaka awaache wadogo zake nje jambo lililofanyika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Urlch Matei

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...