Na.Khadija seif,Globu ya jamii

KAMPUNI ya Hawaii kupitia bidhaa ya maziwa ya cowbell wamsainisha mkataba msanii wa bongo movie monalisa.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kusaini mkataba huo meneja masoko amesema wanategemea ubalozi huo utakua wa ufanisi zaidi na kukuza kipato katika kampuni hiyo.

"Wapo wasanii wengi lakini tumeweza kumpa ubalozi huo monalisa kutokana na sababu nyingi ikiwemo jamii inamchukuliaje pamoja na swala la heshima na nidhamu,"

Mpanda ameweka wazi kuwa hofu kubwa kwa makampuni kujitokeza kutoa ubalozi kwa wasanii wengine ni kutokana na kuhusishwa kwenye skendo chafu na kupelekea wateja kutokua na imani na bidhaa husika.

Kwa upande wake Yvonne cherry a.k.a Monalisa amewapongeza kampuni hiyo kwa kuona juhudi zake na kumteua kua balozi wa muda wa kipindi cha mwaka mmoja.

"Nategemea kuwa na matunda mazuri kwenye kazi zangu na ufanisi mkubwa kwenye kampuni ili kuwafikia wateja wote,"

Hata hivyo amewataka wasanii wengine kujenga misingi mizuri ya nidhamu ili kupewa mikataba mbalimbali kunufaika wao wenyewe na kuongeza pato la taifa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...