Afisa Tarafa Mihambwe
Gavana Emmanuel Shilatu ametembelea na kujionea ujenzi wa vyumba viwili
vya Madarasa na chumba kimoja cha ofisi kwenye shule ya msingi Namunda
iliyopo Kijiji cha Namunda kata ya Kitama ukiendelea kwa kasi tangu
usimame Agosti, 2018.
Gavana Shilatu
alijionea hayo kwenye ziara yake ya ufuatiliaji wa mradi huo wa ujenzi
alioagiza ujengwe mara moja siku alipotembelea mradi huo Mei 16, 2019
kutokana na kutelekezwa tangu mwaka jana kwenye usawa wa ngazi ya
msingi.
Gavana Shilatu
aliwasisitizia uongozi wa Kijiji na kamati ya ujenzi kuacha malumbano ya
wenyewe kwa wenyewe na wawe wazalendo kwa kuhakikisha wanathamini pesa
ya umma na ujenzi uwe wenye ubora na viwango vinavyolingana na thamani
ya pesa.
Katika ziara hiyo ya
ufuatiliaji Gavana Shilatu aliambatana na uongozi wa Serikali ya Kijiji
cha Namunda pamoja na kamati ya ujenzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...