Na Woinde Shizza Michuzi Blog ,Arusha

Wadau mbalimbali jijini Arusha wamejitokeza kusaidia mashindano ya shirikisho la michezo kwa shule za sekondari Afrika Mashariki (FEASSA) kwa kujitolea mahitaji muhimu ikiwemo maji,vyakula na usafiri ili kufanikisha michuano hiyo ya kimataifa.

Mwenyekiti wa Umoja wa Shule zisizomilikiwa na serikali (Tamongsco) mkoa wa Arusha Isabella Mwampamba akizungumza wakati akikabidhi sehemu ya vitu walivyovitoa, amesema kuwa lengo lao ni kuunga mkono serikali katika michuano hiyo ili iweze kufanya kazi vizuri na kuliletea taifa heshima

Afisa Elimu mkoa wa Arusha Halfani Masukira ameushukuru umoja wa shule binafsi kwa kujitoa kufanikisha mashindano hayo muhimu ambayo yanatarajia kuanza Agosti 15 mwaka huu na kuwakutanisha watu zaidi ya 3000

Mjumbe kamati ya michezo hiyo Halifa Kiembe amesema kuwa michezo hiyo ni muhimu katika kukuza na kuibua vipaji muhimu ambavyo vitaiwezesha Tanzania na Afrika Mashariki kung`ara kimataifa

Feassa ya tikisa Arusha Tz ni mashindano ya Esti africa yanayo jumuisha Nchi 7 yatakayo shirikisha shule za sekondari na msingi kuanza mwaka huu mashindano hayo yamenza kutimua vumbi Leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...