WATANZANIA wameshauriwa kuchangamkia fursa katika vyuo vya elimu ya juu nje ya nchi ili kupata ujuzi unaoendana na mabadiliko ya haraka ya teknolojia.
Ushauri huo umetolewa jijini Dar es Salaam na Mwambata wa Mwenza wa Taasisi ya Elimu ya Juu ya Edugate ya Uingereza Aliyuthuman Sadhique alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa programu maalumu ya kusaidia wanafunzi katika nchi zenye uchumi wa kati inayofahamika kama LICAP.
Amesema program hiyo inalenga kuwafikia wanafunzi na wahitimu mbalimbali kutimiza malengo katika vyuo maalumu vilivyopo Uingereza na Sri Lanka.“Edugate kwa kushirikiana na Taasisi ya British Colledge of Upplies Studies ya Sri Lanka tumedhamilia kuwekeza katika elimu hapa nchini hususan kuwawezesha watanzania kwenda kusoma nje ya nchi ikiwemo kuwasaidia kimasomo,”amesema.
Ameongeza kuwa "Leo tutazindua program hiyo ambapo uzinduzi utaaendana na kongamano maalumu litakalo toa fursa kwa watanzania kuzitambua fursa hizo za elimu,"Sadhique amesema kongamano halitakuwa na malipo yoyote na mtu yoyote anaweza kuhudhuria hususan wenye nia ya dhati ya kwenda kujiendeleza nje ya nchi.
Amewataka wale wote wenye nia ya kusoma nje ya nchi kuhudhuria kongamano hilo na kwamba litakuwa na faida kubwa husan kwa wahitimu wa Teknolojia ya habari na Mawasiliano (IT), Usimamizi wa fedha, uhandisi na taaluma zingine .
Ushauri huo umetolewa jijini Dar es Salaam na Mwambata wa Mwenza wa Taasisi ya Elimu ya Juu ya Edugate ya Uingereza Aliyuthuman Sadhique alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa programu maalumu ya kusaidia wanafunzi katika nchi zenye uchumi wa kati inayofahamika kama LICAP.
Amesema program hiyo inalenga kuwafikia wanafunzi na wahitimu mbalimbali kutimiza malengo katika vyuo maalumu vilivyopo Uingereza na Sri Lanka.“Edugate kwa kushirikiana na Taasisi ya British Colledge of Upplies Studies ya Sri Lanka tumedhamilia kuwekeza katika elimu hapa nchini hususan kuwawezesha watanzania kwenda kusoma nje ya nchi ikiwemo kuwasaidia kimasomo,”amesema.
Ameongeza kuwa "Leo tutazindua program hiyo ambapo uzinduzi utaaendana na kongamano maalumu litakalo toa fursa kwa watanzania kuzitambua fursa hizo za elimu,"Sadhique amesema kongamano halitakuwa na malipo yoyote na mtu yoyote anaweza kuhudhuria hususan wenye nia ya dhati ya kwenda kujiendeleza nje ya nchi.
Amewataka wale wote wenye nia ya kusoma nje ya nchi kuhudhuria kongamano hilo na kwamba litakuwa na faida kubwa husan kwa wahitimu wa Teknolojia ya habari na Mawasiliano (IT), Usimamizi wa fedha, uhandisi na taaluma zingine .
Amesema kwamba kwa wale ambao ufaulu wao utaonekana kuwa ni wajuu watasaidiwa kupata udhamini kupitia program hiyo ya LICAP.
Mmoja wa waratibu wa kongamano hilo David Munanka, amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka ambapo serikali ya awamu ya tano inatekeleza dira yake ya kuelekea uchumi wa viwanda na kuongeza mwenye sifa na nia ya kusoma shahada au astahashada nje ya nchi anaweza kuhudhuria kongamano hilo bure.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...