Afisa Habari Mkuu,kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Joyce Mgaya,akizungumza na watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam mara baada ya kuwasili jijini Dodoma kwa ajili ya ziara ya mafunzo pamoja na kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
.....
WATOTO Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wametembelea Mji wa Serikali Mtumba Dodoam huku wakiushukuru Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ( BRELA) kwa kudhamini ziara ya mafunzo kwa kutumia reli ya kisasa (SGR).

Akizungumza leo Aprili 29,2025 kwa niaba ya BRELA, Afisa Habari Mkuu, BRELA Bi. Joyce Mgaya amesema ziara hiyo in kuonesha dhamira ya BRELA katika kusaidia makundi yenye uhitaji maalum.

“Mtendaji Mkuu wetu aliona ni jambo jema kuwapa watoto hawa fursa ya kutembelea makao makuu ya nchi na kujionea miradi ya maendeleo inayotekelezwa,” amesema Bi Mgaya.

Hata hivyo ameongeza kuwa kwa wengi wao,ni mara ya kwanza kupanda treni ya SGR na kufika Dodoma, na kwamba ziara hiyo ni sehemu ya mikakati ya BRELA kusaidia jamii kupitia programu mbalimbali za kuwafikia wananchi.

Aidha Bi.Mgaya ametoa wito kwa Taasisi zingine ziendelee kuwakimbilia watu wenye mahitaji Kwa kuhakikisha wanawasaidia mahitaji mbalimbali.
Kwa upande wake Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo cha TUYATA, Bi Fauzia Jabir amesema kuwa wanaishukuru BRELA kwa safari hiyo kwani watoto wengi wamefurahi na katika maisha yao hawajawahi kupanda treni.

“Watoto wamefurahi mno, jambo hili halijawahi kutokea. BRELA imefanya jambo kubwa kwa kusimama na watoto hawa wahitaji. Wamehamasika kusoma zaidi baada ya kuona uzuri na fursa zilizopo nchini,” amesema Bi Jabir.

Hata hivyo, ameeleza kuwa licha ya mafanikio ya kielimu waliyonayo, kituo hicho kinakabiliwa na changamoto kubwa ya makazi kwa watoto yatima, na hivyo kuomba msaada wa ujenzi wa nyumba za makazi kwa watoto na wajane.

Mmoja wa walionufaika na kituo hicho, Bi Ayman Jaffar Abubakar ambaye pia ni msemaji wa TUYATA, amesema kulea watoto kutoka mazingira mbalimbali si kazi rahisi lakini kwa neema ya Mungu, wanajitahidi kutoa malezi bora na kuwaelekeza katika njia sahihi.

“Watoto wengi wanaishi kwa walezi, hivyo ni changamoto kuwafuatilia kikamilifu. Tunaishukuru BRELA kwa kutuunga mkono na tunaomba waendelee kuwa nasi hadi tufikie malengo yetu,” amesema
WATOTO Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wakiwa ndani ya reli ya kisasa (SGR) kuja jijini Dodoma kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
WATOTO Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wakishuka ndani ya reli ya kisasa (SGR) mara baada ya kuwasili jijini Dodoma kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Afisa Habari Mkuu,kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Joyce Mgaya,akizungumza na watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam mara baada ya kuwasili jijini Dodoma kwa ajili ya ziara ya mafunzo pamoja na kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam wakifurahia Mji wa Serikali Mtumba baada ya kutembelea ziara ya mafunzo iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Afisa Habari Mkuu,kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Joyce Mgaya,akizungumza na waandishi ya habari jijini Dodoma mara baada ya kudhamini ziara ya mafunzo ya Watoto Yatima na wenye Ulemavu 100 kutoka Kituo cha Kulelea Yatima cha Tulee Yatima Tanzania (TUYATA) kutoka Dar es Salaam mara baada ya kutembelea Mji wa Serikali Mtumba ziara iliyodhaminiwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo cha TUYATA, Bi Fauzia Jabir,akiishukuru BRELA kwa safari hiyo kwani watoto wengi wamefurahi na katika maisha yao hawajawahi kupanda treni.
Mmoja wa walionufaika na kituo cha TUYATA na msemaji wa TUYATA Bi Ayman Jaffar Abubakar,akielezea historia yake kwa waandishi wa habari.

 


Wasanii wa filamu na maigizo nchini wametakiwa kutumia Lugha ya kiswahili kama fursa ya kibiashara kimataifa ili kuongeza tija itokanayo na filamu hizo katika kujiongezea kipato chao


Rai hiyo imetolewa na Dkt Godwin Maimu ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa tamasha la kimataifa la filamu za kiswahili (ISFF) wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam ambapo amesema lengo la kuanzisha tamasha hilo ni kubidhaisha lugha ya kiswahili kimataifa kupitia filamu za kiswahili zitakazoonyeshwa katika mataifa mbalimbali.


Kwa upande wake mchunguzi lugha mkuu kutoka baraza la kiswahili Tanzania (BAKITA) amewasisi wasanii nchini Kutumia lugha ya kiswahili kwa ufasaha ili kulinda hadhi ya lugha hiyo huku wakiendelea kuutangaza utamaduni wa kitanzania kimataifa 


Naye Dusabimana Apollos msanii kutoka nchini Rwanda amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kwa wasanii wa afrika mashariki katika kukuza matumizi ya lugha ya kiswahili hususan katika masoko ya kimataifa








 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhwan Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ORICA  baada ya kutembelea banda lao katika maadhimisho  ya Wiki ya  Usalama na Afya  Mahala Pa Kazi yanayendelea kufanyika mkoani Singida.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhwan Kikwetev akitembela banda la Orica Tanzania na kujifunza kuhusu shughuli zao za ulipuaji migodi wakati akifanya ukaguzi katika maadhimisho ya Wiki ya kimataifa ya Usalama mahali pa kazi inayofanyika kitaifa mkoani Singida


WAKATI  Dunia ikiadhimisha Siku ya Usalama Kazini Aprili 28, 2025 chini ya kaulimbiu ‘Nafasi ya Akili Mnemba na Teknolojia za Kidijitali katika Kuimarisha Usalama na Afya Mahala Pa Kazi, Orica Tanzania inayojishughulisha na utengenezaji Pamoja na uuzaji wa baruti kwa ajili ya ulipuaji migodini imetoa wito wa kuhakikisha usalama unazingatiwa wakati wa kazi ili kuepusha madhara yatokanayo na ajali za baruti.

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi Duniani yanayoendelea Kitaifa mkoani Singida, Mhandisi wa Baruti kutoka Orica Bw. Boaz Samwel amesema kuwa baruti ni kihatarishi kikubwa migodini na huweza kuleta madhara makubwa endapo hakitatumiwa kwa kuzingatia kanuni za matumizi sahihi.

“Kupitia maonesho haya, tumekuja na teknolojia ya kisasa inayotumia Akili Mnemba kwa ajili ya ulipuaji bila madhara yoyote na kupitia teknolojia hii, kazi ya ulipuaji inaweza kufanyika kwa ufanisi na usalama zaidi pasipo kuwepo mtu yeyote ndani ya eneo la karibu na mlipuko.” amesema Bw.Samwel.

“Tofauti na miaka ya nyuma, Teknolojia imebadili kwa kiasi kikubwa sana mfumo mzima wa ulipuaji na kuifanya kazi hii kuwa rahisi na salama zaidi, kipaumbele kikubwa kikiwa ni kulinda uhai wa watu, mazingira na ufanisi katika uzalishaji.

Amesema ili kupunguza na kuondoa madhara yanayoweza kutokea maeneo ya migodini, licha ya Orica kuwa watengenezaji na wauzaji wa baruti , wao pia wamekuwa wakitoa ushauri kwa matumizi sahihi ya teknolojia salama katika kazi hiyo kwa kuzingatia sheria na taratibu zote za Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA).

Bw.Boaz amezitaja baadhi ya teknolojia zinazotumia akili Mnemba kuwa ni pamoja Blast IQ, ORBS, 4D, RHINO, OREpro 3D, ENVIROTrack, FRAGTrack na GroundProbe inayoweza kuhisi na kutambua mabadiliko yoyote katika mwamba na kutoa taarifa wakati huo huo na kuzuia ajali inayoweza kusababishwa na kuanguka kwa mwamba.

Amesema uwekezaji huu ni maendeleo makubwa katika sekta ya madini ikiendelea kubadilika kwa njia ya kidijitali na uvumbuzi.

Akitoa mtazamo mpana kuhusu dhamira ya Orica Tanzania, Daniel Paul, Mtaalamu wa Rasilimali Watu kwa Kanda ya Kusini mwa Afrika ya Orica — akizungumza kwa niaba ya Mhandisi Asha Mambo, Meneja wa Eneo la Orica Tanzania — alisema:

"Katika Orica Tanzania, tunaamini kuwa usalama, afya, na ustawi wa wafanyakazi ni nguzo kuu za mafanikio ya biashara yetu. Kama sehemu ya Orica Limited, kampuni inayoongoza duniani katika vilipuzi vya kibiashara, mifumo ya ulipuaji na huduma za madini inayofanya kazi katika zaidi ya nchi 100, tumejikita katika kuweka viwango vya juu zaidi vya usalama — katika shughuli zetu pamoja na katika sera na taratibu.

Alisisitiza zaidi kuwa usalama si jukumu la wachache, bali ni wajibu wa pamoja kwa wadau wote — imani ambayo inaendelea kuimarisha mafanikio na uimara wa Orica Tanzania.

Orica inafanya kazi katika zaidi ya nchi 100, ikiwa na zaidi ya miaka 150 ya uzoefu. Mashirika na makampuni mbalimbali yameshiriki katika maonesho hayo yaliyodumu kwa wiki nzima.

Akiongea wakati wa ufungaji, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete amewataka washiriki kuimarisha juhudi za usalama wa wafanyakazi na kuwa kipaumbele katika shughuli zao.

Na Diana Byera – Missenyi

Kampeini ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia wilayani Missenyi Mkoani Kagera, imefanikiwa kwa asilimia 95.3 ndani ya siku 15 tangu ilipozinduliwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, Aprili 14 mwaka huu katika viwanja vya Mayunga, Manispaa ya Bukoba.

Mratibu wa kampeini hiyo wilayani Missenyi Maxmillan Fransis, alisema kuwa ndani ya siku hizo 15, kuanzia Aprili 15 hadi Aprili 28, kata zote 15 zilizopangwa kufikiwa zimefikiwa, na vijiji 43 vilivyopangwa kufikiwa, 41 vilifikwa.

"Kampeini imekuwa na mafanikio makubwa na mwitikio mkubwa sana. Mwanzoni ilipangwa iwe ya siku 10, lakini serikali iliongeza siku 5 kulingana na uhitaji wa wananchi, Tumefikia vijiji 41, na vijiji viwili ambavyo kampeini haikufanikiwa, tulifika lakini viongozi walisema wana misiba mikubwa. Vingine vyote vimenufaika na kampeini hiyo," alisema.

Aliongeza kuwa kupitia kampeni hiyo, makundi mbalimbali yalipata elimu, yakiwemo ya bodaboda, wanafunzi, wakulima, wazee, watu wenye ulemavu, taasisi binafsi, waajiriwa serikalini, huku elimu kuhusu umiliki wa ardhi, matumizi sahihi ya ardhi, wosia, mirathi, ukatili na matunzo ya watoto ikitolewa katika mikutano ya hadhara ili kunufaisha umma na kuwafundisha kufuata sheria.

Alisema kuwa migogoro iliyojitokeza kwa wingi ni ya ardhi, mirathi na ukatili, ambapo mingi imetatuliwa kwa njia ya usuluhishi. Migogoro ambayo haijatatuliwa imekabidhiwa kwa vitengo husika ili kupata utatuzi wa kudumu.

Aidha, migogoro ya kisheria kwa wananchi ambao hawana mawakili, tayari mashauri yao yamekabidhiwa kwa mawakili ili kuwasaidia kuendelea na hatua za mahakama.

Akitaja mafanikio yaliyopatikana, alisema kuwa elimu ya masuala ya kisheria imetolewa na kufikia wananchi 14,020, ambapo wanaume ni 6,905 na wanawake ni 7,115.

Aidha, watendaji wa vijiji, kata, wenyeviti wa vijiji na vitongoji pamoja na madiwani wamejengewa uwezo juu ya masuala ya kisheria kutokana na kushughulikia kero za wananchi kila siku, ambazo zinahitaji utaalamu wa masuala ya kisheria.

Changamoto zilizojitokeza ni pamoja na uwepo wa malalamiko ya muda mrefu kuhusu matumizi ya ardhi baina ya wananchi na serikali za vijiji, jambo ambalo limechochea uvunjifu wa amani na baadhi ya wananchi kugoma kuchangia maendeleo ya vijiji kwa sababu ya migogoro ya ardhi.








Na Mwandishi Wetu – Singida

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesisitiza umuhimu wa wananchi kujiunga na kuchangia Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili kunufaika na mafao mbalimbali yakiwemo Mafao ya Matibabu kwa Wananchi waliojiajiri. Kwa upande wa wafanyakazi wa NSSF, Mhe.Waziri amewataka kuendelea kuhudumia wanachama kwa weledi.

Mhe. Ridhiwani amesisitiza hayo alipotembelea banda la NSSF kwenye Maonesho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani, yanayofanyika Kitaifa katika viwanja vya Mandewe, mkoani Singida.

Amesema NSSF ina jukumu kubwa la kutoa huduma za hifadhi ya jamii kwa wanachama wa sekta binafsi na kuwafikia wananchi waliojiajiri kupitia Mfumo wake wa Hifadhi Skimu, ili kuhakikisha hata wale waliojiajiri wenyewe wanapata mafao ya muda mfupi na mrefu.

“NSSF ina wajibu mkubwa wa kuimarisha maisha ya wanachama wake, hasa pale wanapokumbwa na majanga yanayoathiri kipato chao. Hivyo amesisitiza kuendelea kutoa elimu ya mafao na huduma zinazotolewa na Mfuko huo kwa wananchi.

Aidha, Mhe. Ridhiwani alionesha kuridhishwa na jinsi NSSF ilivyotekeleza dhana ya usalama na afya mahala pa kazi.

Kwa upande wake, Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida, Bw. Oscar Kalimilwa, amesema NSSF imeshiriki maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu hifadhi ya jamii, kusajili wanachama wapya kutoka sekta binafsi pamoja na wale waliojiajiri wenyewe.

Bw. Kalimilwa alisisitiza kuwa maonesho hayo yamewapa nafasi ya kuwakumbusha waajiri wa sekta binafsi juu ya wajibu wao wa kuwasajili na kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.

“Ninatoa rai kwa waajiri kuhakikisha michango ya wafanyakazi wao inawasilishwa NSSF kwa wakati kwani hilo ni takwa la kisheria. Kufanya hivyo kutawahakikishia wanachama kulipwa mafao yao kwa wakati na kuondoa usumbufu usio wa lazima," alisema.

Vilevile, aliwahamasisha wananchi waliojiajiri, wakiwemo bodaboda, mama lishe, wavuvi, wakulima, wachimbaji wadogo, wasusi, vinyozi, wasanii na wajasiriamali wengine, kujiunga na kuchangia katika NSSF kupitia Hifadhi Skimu.

Alibainisha kuwa mwanachama aliyejiajiri anapaswa kuchangia si chini ya shilingi 30,000/- kwa mwezi ili kupata mafao mbalimbali yakiwemo ya matibabu, na shilingi 52,200/- mwanachama atapata Mafao ya matibabu yeye na familia yake wakiwemo watoto wanne. Ameongeza kuwa michango hiyo inaweza kufanyika kidijitali kupitia simu za kiganjani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa uharaka.










Na Belinda Joseph-Songea DC.

Halmashauri ya Wilaya ya Songea imejipanga kwa mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, unaotarajiwa kuingia Mei 10 kupitia Kata ya Mpandangindo na kufanya mkesha katika Kata ya Magagura, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea mafanikio ya maendeleo katika maeneo yote ya Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika Mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani wa robo ya tatu kwa mwaka wa fedha 2024/2025, uliofanyika Aprili 29, 2025 katika Ukumbi wa Halmashauri Lundusi, Mkurugenzi Mtendaji Bi. Elizabeth Mathias Gumbo amewataka viongozi na wananchi kushiriki kwa wingi kwenye shughuli hiyo muhimu ya kitaifa.

"Tunatarajia kupokea Mwenge wa Uhuru na tunawaomba viongozi wote, wananchi na wadau wa maendeleo kushiriki kikamilifu, Tukio hili si la kawaida ni nafasi ya kuonesha na kusherehekea mafanikio yetu kama Halmashauri," alisema Bi. Gumbo.

Katika mkutano huo, Baraza la Madiwani likiongozwa na Makamu Mwenyekiti Simon Kapinga, limeipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa kila kata ndani ya Halmashauri hiyo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Viongozi pia walimpongeza Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Peramiho kwa mchango wake mkubwa, hususan kwa kuhakikisha upatikanaji wa madaktari bingwa waliowahudumia wananchi wa Songea.

Mkutano huo umejadili ajenda 10 muhimu na uliambatana na uwasilishaji wa taarifa kutoka kwenye kamati mbalimbali za Halmashauri, ikiwemo Kamati ya Maadili, Elimu Afya na Maji, Uchumi Ujenzi na Mazingira, Kudhibiti UKIMWI, pamoja na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango.



 Na Belinda Joseph-Songea DC.


Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Peramiho kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Elizabeth Gumbo, leo tarehe 29 Aprili 2025, amefungua rasmi mafunzo ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Mafunzo hayo ya siku moja yamefanyika katika Ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo katika Shule ya Sekondari ya Maposeni.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Bi. Gumbo amesema: “Ni matumaini yangu kuwa, kupitia semina hii, kila mshiriki atapata uelewa wa kutosha utakaomwezesha kutekeleza majukumu yake ipasavyo ili kufanikisha zoezi hili muhimu.”

Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo washiriki kuhusu mbinu bora za kujaza fomu, matumizi ya Mfumo wa Uandikishaji Wapiga Kura (Voters Registration System), pamoja na matumizi sahihi ya vifaa vya kuandikisha wapiga kura.





WAFANYABIASHARA 50 waliyokuwa wamepanga kwenye fremu za jengo lililoporomoka Kariakoo Novemba 16, 2024 wamefungua kesi katika Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi wakidai fidia ya Sh. Bilioni 40 kwa wamiliki wa jengo.

Walalamikaji wanadai kiasi hicho cha pesa kama fidia ya hasara ya uwekezaji na biashara waliyowasababishia kutokana na uzembe wa wadaiwa kufanya ujenzi wa chini kwa chini kinyume na makubaliano ya mkataba wa upangaji kati yao uliosababisha kuporomoka kwa jengo hilo.

Katika hati ya madai iliyowasilishwa mahakamani hapo na wakili Peter Madelekaa, wadai hao wanadai kuwa, fidia hiyo inatokana na uzembe wa ujenzi wa chini kwa chini uliosababisha kuporomoka kwa jengo hilo na kuharibu fremu zao za rejareja na biashara za jumla.

Aidha, wameiomba Mahakama itamke wadaiwa Zenabu Ismail kama mwakilishi wa kisheria wa marehemu Abdallah Salim, Ashour Ashour,

kama mwakilishi wa marehemu Awadhi Ashur Abeid na Leondela Mdete kwamba walikiuka mikataba ya upangaji kati yao kwa kufanya ujenzi wa kizembe.

Hati hiyo ya madai inaelekeza kwamba kesi hiyo imefunguliwa na Kanali Naftal Swai na wenzake 49 ambao walikuwa wamepanga katika jengo lililopo Kiwanja namba 12, kitaru 7, eneo la Kariakoo, Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam.

Inadaiwa kati ya Januari 2023 hadi Desemba 31, 2024, wadai na wadaiwa waliingia katika mikataba ya upangaji kwa njia ya mdomo na kwa maandishi kuhusu jengo hilo.

Inadaiwa kuwa wadai waliwekeza na kuendesha biashara mbalimbali zikiwemo maduka ya rejareja, thamani ya jumla ya uwekezaji na biashara za zilizokuwa zikiendeshwa katika jengo ni Sh bilioni 40.

Pia, wadai wanadai kwamba wadaiwa walikiuka masharti na vigezo vya mkataba wa upangaji kati yao kwa walifanya ujenzi wa chini kwa chini kwa uzembe na bila idhini, ulisababisha kuporomoka kwa jengo hilo.

Hivyo, walalamikaji wanaomba Mahakama itoe hukumu na amri dhidi ya wadaiwa na pia wameomba mahakama itamke kwamba gharama za kesi zilipwe na wadaiwa.

Kesi hiyo ambayo imepangwa kusikilizwa mbele ya Jaji Mohamed Gwae, imetajwa leo Aprili 29,20255 mbele ya Naibu Msajili Rose Kangwa.




Na Mwandishi wetu
KAMPUNI ya Envaita nchini yaja na suluhisho la Kidigitali la kutumia njia mpya zakualika watu katika matukio mbalimbali badala ili kusaidia kuokoa muda ,kutunza mazingira na kupunguza usumbufu kwa waalikwaji.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuona hali ya ukuaji wa teknolojia duniani kuanza kukua kwa kasi na kuondokana na mifumo ya kinailojia na kuelekea katika mifumo ya Kidigitali.

Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam,Meneja Mawasiliano wa Kampuni hiyo,PrayGod Mushi wakati akiongea na waandishi wa habari akitambulisha mfumo huo mpya wa utoaji wa kadi kwa njia ya kidigitali katika Mikutano mbalimbali iwe Harusi na Mikutano mikubwa inayofanywa na makampuni mbalimbali nchini.

Amesema mialiko ya kidigitali inasaidia kwa kiasi kikubwa kupanga bajeti kwakuwa unakuwa na idadi kamili ya watu wanaohudhulia tukio lako.

"Kampuni yetu imeanza rasmi mwaka 2022 tukiwa na wafanyakazi wachache lakini kwa sasa tunawafanyakazi zaidi ya 30 ambapo tunafanya kazi nchi nzima kuhakikisha huduma ya kualika katika matukio mbalimbali kidigitali.

"Njia ya kidigitali ni nzuri lakini changamoto iliyopo watu bado hawaelewi wanadhani ni utapeli au wakati mwingine wanaona kama wanadharaulika kwa kutumiwa kadi za mialiko kwa simu lakini ndo teknoloji inavyotupeleka huko kwa sasa na kuondokana na mitazamo wa zamani,"amesema

Amesema kwa kutumia njia hiyo ya kidigitali wanahakikisha taarifa za ualikaji zote zinatakiwa kukaa katika mfumo huo na kujua ni walengwa gani wanapelekewa mialiko hiyo ambapo wao kazi yao nzima ni kuwasimamia kadi kufika kwa wakati kwa njia hiyo ya kidigitali na kufanya ufatiliaji wa kuwakumbusha kabda ya tukio.

"Mteja anapokuja kutupa kazi yake tunahakikisha tunaanza nae mwanzo wa utoaji wa kadi kwa njia hiyo ya kidigitali,kisha kuwatumia walengwa wake wote na sisi wenyewe tutaanza kuwakumbusha siku kabla ya tukio muhimu na siku ya tukio tunakuja wenyewe kusimamia watu wanapoingia kwa kuzihakiki (scan) kadi hizo ili kuzuia watu kuvamia,"amesema.

Amesema bado uelewa ni mdogo kwa watanzania wengi lakini kwa sasa taratibu wanaanza kuzoea kwa sababu kadi hizi zinawaondolea usumbufu wa ucheleweshaji wa utumaji wa kadi katika matukio yao.

Mfumo wetu ulivyo kadi haiwezi kutumika mara mbili katika tukio wala hakuna atayeweza kuingia kwenye sherehe bila kualikwa hivyo mfumo unasoma maelezo ya mtu husika moja kwa moja pindi wanaposcan,"amesema


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2025.

Top News