Baada ya mazungumzo yao, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) alimkabidhi Mhe. António Guterres zawadi ya kitabu kuhusu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutambua kuvutiwa kwa muda mrefu kwa Katibu Mkuu huyo na maono, uongozi na mchango wa Mwalimu Nyerere katika kuhimiza amani, maendeleo na ushirikiano wa kimataifa.
Baada ya mazungumzo yao, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) alimkabidhi Mhe. António Guterres zawadi ya kitabu kuhusu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutambua kuvutiwa kwa muda mrefu kwa Katibu Mkuu huyo na maono, uongozi na mchango wa Mwalimu Nyerere katika kuhimiza amani, maendeleo na ushirikiano wa kimataifa.
Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Uzinduzi na utambulisho rasmi wa mfuko huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau wa sekta ya fedha, masoko ya mitaji, wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi, pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari.
Hafla hiyo iliongozwa na Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba, huku Afisa Mtendaji Mkuu wa CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, akiwaongoza viongozi wengine wa kampuni hiyo kuelezea manufaa na fursa zinazotokana na mfuko huo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Mwangalaba aliipongeza CORE Securities Limited kwa kuanzisha mfuko huo, akieleza kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na kupanua wigo wa huduma za uwekezaji kwa wananchi wengi zaidi.
Alisema kwa muda mrefu mipango ya kustaafu nchini imekuwa ikihusishwa zaidi na watu wenye ajira rasmi ambao ni takribani asilimia chache zaidi ya wananchi wote, hali iliyosababisha sehemu kubwa ya wananchi, hususan walio katika sekta isiyo rasmi, kukosa fursa za maandalizi ya maisha ya baadaye.
“Kupitia FPRF, taifa linapata jukwaa jumuishi linalomwezesha kila Mtanzania — awe ameajiriwa rasmi, amejiajiri, mfanyabiashara au anayejishughulisha na shughuli za sekta isiyo rasmi — kuwekeza na kujiandaa kwa maisha ya baadaye kwa uhuru, unyumbufu na heshima,” alisema Dkt. Mwangalaba.
Aidha, aliwahimiza wananchi kujenga utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza kwa malengo ya muda mrefu, huku akisisitiza umuhimu wa kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kufanya maamuzi ya uwekezaji.
“Mipango ya kustaafu haipaswi kuonekana kama fursa ya watu wachache wenye ajira rasmi pekee. Kila Mtanzania anastahili kuwa na usalama na heshima ya kifedha baada ya miaka yake ya uzalishaji, na mfuko huu ni sehemu ya suluhisho la kufanikisha lengo hilo...nawapongeza sana CORE Securities kwa mpango huu” alisisitiza.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, alisema FPRF imeundwa kuziba mapengo yaliyopo katika mifumo ya kawaida ya pensheni kwa kutoa chaguzi zenye unyumbufu zaidi katika uwekezaji na upatikanaji wa mafao.
“Ingawa mifuko ya hifadhi ya jamii kama NSSF na PSSSF inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika ustawi wa wananchi, FPRF imeundwa kuikamilisha mifumo hiyo kwa kutoa fursa za ziada za uwekezaji kwa watu ambao awali hawakuwa na nafasi ya kushiriki,” alisema.
Alifafanua kuwa CMSA iliidhinisha mfuko huo tarehe 28 Aprili 2026 kwa mujibu wa Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana pamoja na Kanuni za Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja za mwaka 1997, huku NMB Bank PLC ikiidhinishwa kuwa Mdhamini na Mlezi wa mfuko huo.
Kwa mujibu wa CPA Fumbuka, mfuko huo umeidhinishwa kukusanya hadi shilingi bilioni 10 kupitia uuzaji wa vipande vya uwekezaji milioni 100, kila kimoja kikiwa na thamani ya shilingi 100.
Alisema muundo wa FPRF umeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji tofauti ya kifedha na viwango vya uvumilivu wa hatari za uwekezaji kwa makundi mbalimbali ya umri.
“Mahitaji ya kifedha ya kijana aliyeanza kazi ni tofauti na ya mtu anayekaribia kustaafu. Ndiyo maana tumeandaa mipango tofauti inayowawezesha wawekezaji kuchagua mkakati unaoendana na umri, kipato na matarajio yao ya muda mrefu,” alieleza.
Mfuko huo utakuwa na mipango mitatu ya uwekezaji ambayo ni Youngsters’ Plan kwa wawekezaji wenye umri chini ya miaka 35, Middle-Agers’ Plan kwa wenye umri kati ya miaka 35 na 50, na Seniors’ Plan kwa wawekezaji wenye umri zaidi ya miaka 50, ambao uwekezaji wake utazingatia zaidi dhamana za Serikali.
CPA Fumbuka alibainisha kuwa tofauti na mifuko mingi ya pensheni inayohitaji michango ya muda mrefu kabla ya mafao kupatikana, FPRF ina kipindi cha miaka mitano pekee ambapo baada ya hapo, mwekezaji ataweza kupata fedha zake kwa mkupuo, kwa malipo ya pensheni ya kawaida au kwa mchanganyiko wa njia hizo.
“Mahitaji ya kifedha ya watu hubadilika kadri muda unavyokwenda. Wapo wanaohitaji mapato ya kila mwezi baada ya kustaafu, na wapo wanaoweza kuhitaji sehemu ya akiba zao kwa ajili ya matibabu, familia au biashara. Mfuko huu unawapa uhuru wa kufanya maamuzi hayo kulingana na mahitaji yao,” alisema.
Aliongeza kuwa mwananchi anaweza kuanza uwekezaji kwa kiasi cha shilingi 10,000 tu, sawa na vipande 100 vya uwekezaji, na kuongeza uwekezaji wake taratibu kulingana na uwezo wake wa kifedha.
Mbali na hilo, mfuko huo unatoa faida ya ukwasi (liquidity), ambapo baada ya kipindi cha miaka mitano, wawekezaji wataweza kuuza vipande vyao kwa thamani halisi ya mali za mfuko (NAV), huku malipo yakifanyika ndani ya siku mbili za biashara.
Uwekezaji katika mfuko huo utafanyika kwa njia ya kielektroniki kupitia mfumo wa CORE Securities Limited, matawi maalumu ya NMB Bank PLC pamoja na mawakala walioidhinishwa na kuunganishwa na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa wa chama hicho, Bw. Nelson Mabula, alisema CWT imejiridhisha kuhusu usalama, uwazi na manufaa ya mfuko huo kwa wanachama wake.
“Kiwango cha chini cha kuanzia uwekezaji cha shilingi 10,000 kinawapa fursa wanachama wetu wengi kushiriki. Tunaamini huu ni uwekezaji wenye manufaa kwa walimu na wafanyakazi wengine, na kama taasisi tutahamasisha wanachama wetu kushiriki ili wawe sehemu ya fursa hii ya kujenga ustawi wao wa kifedha wa muda mrefu,” alisema.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (kushoto) akimkabidhi Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Bw. Nelson Mabula (kulia) mfuko wenye nyaraka muhimu kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Anaeshuhudia katikati ni Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (kushoto) akimkabidhi Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba (kulia) mfuko wenye nyaraka muhimu kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (kulia) akimkabidhi Mwakilishi kutoka benki ya NMB Bw Avith Massawe (kushoto) mfuko wenye nyaraka muhimu kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi huku benki ya NMB ikiwa Mdhamini na Mlezi wa mfuko huo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (wa pili kushoto) sambamba na Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba (wa pili kuli), Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Bw. Nelson Mabula (kulia) na Mwakilishi kutoka benki ya NMB Bw Avith Massawe (kushoto) wakionesha nyaraka ya muongozo kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi huku benki ya NMB ikiwa Mdhamini na Mlezi wa mfuko huo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Mwangalaba (pichani) aliipongeza CORE Securities Limited kwa kuanzisha mfuko huo, akieleza kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na kupanua wigo wa huduma za uwekezaji kwa wananchi wengi zaidi.
Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka (pichani) alisema FPRF imeundwa kuziba mapengo yaliyopo katika mifumo ya kawaida ya pensheni kwa kutoa chaguzi zenye unyumbufu zaidi katika uwekezaji na upatikanaji wa mafao.
Msimamizi wa Mfumo wa Teknolojia wa Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), Bw Ibrahim Isack (pichani) akifafanua kuhusu uendeshwaji wa mfumo wa teknolojia wa mfuko huo wakati wa hafla hiyo.
Uzinduzi na utambulisho rasmi wa mfuko huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau wa sekta ya fedha, masoko ya mitaji, wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi, pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari.
Na Janeth Raphael MichuziTv
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema serikali imechukua hatua madhubuti kumaliza changamoto za kukatika kwa umeme zilizokuwa zikiathiri baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, hali iliyokuwa ikisababisha wilaya nzima kukosa umeme pindi hitilafu zinapotokea kwenye baadhi ya sehemu za mtandao.
Ndejembi amebainisha hayo leo wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Usambazaji Umeme (Switching Station) pamoja na transfoma mpya zilizojengwa kwa lengo la kuimarisha na kudhibiti mfumo wa usambazaji umeme katika wilaya hiyo.
Amesema uwepo wa miundombinu hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya mgao wa umeme wa ghafla, ambao hapo awali ulikuwa ukisababisha maeneo mengi ya Kongwa na wilaya jirani kuathirika pindi hitilafu inapotokea sehemu moja ya mfumo.
“Kwa muda mrefu, changamoto ya voltage ndogo na kukatika kwa umeme mara kwa mara ilikuwa kikwazo kikubwa kwa wananchi na wajasiriamali wadogo, hususan waliokuwa wakishindwa kuendesha shughuli za uzalishaji kama kusaga nafaka na kukamua mafuta kutokana na uhaba wa umeme wa uhakika,” amesema Ndejembi.
Ameongeza kuwa serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuliweka sekta ya nishati katika kipaumbele cha juu, hali iliyowezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuboresha maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.
Amesema zaidi ya shilingi bilioni 10 zimewekezwa katika eneo la Mbande kwa ajili ya ujenzi wa Switching Station hiyo, hatua ambayo itanufaisha wakazi wa wilaya za Kongwa, Kiteto, Gairo, Chamwino na Mpwapwa kwa kupata umeme wa uhakika na wa kutosha.
“Lengo letu siyo tu kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa kuwasha taa, bali ni umeme wa kuendesha viwanda na shughuli za uzalishaji. Hii itasaidia kukuza uchumi wa maeneo haya na kuongeza fursa za ajira,” ameongeza.
Uzinduzi wa mradi huo unatajwa kuwa sehemu ya jitihada za serikali kuboresha miundombinu ya nishati nchini na kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika unafika kwa wananchi wengi zaidi, hususan maeneo ya vijijini na pembezoni.
Aidha limewataka ndugu wote wenye ualbino nchini Tanzania na duniani kote, wasikate tamaa na kuwakumbusha waendelee kuamini katika uwezo wao,kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutimiza ndoto zao na kwamba Dunia inahitaji mchango, vipaji na uwezo wenu.
Hayo yamesemwa na Boniventura Mwalongo ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO)
na Mjumbe wa Kamati Maalumu ya Pamoja ya Kushughulikia Changamoto za Watu Wenye Ualbino nchini alipokuwa akitoa salamu katika Maadhimisho ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika Juni 13,2026.
“TRAMEPRO inapenda kuwahakikishia watu wote wenye ualbino kwamba itaendelea kuwa sauti yao na mshirika wao katika kutetea haki, usawa, heshima na maendeleo yao. Ahadi yetu ni kwamba kamwe hatutawasaliti katika kusimamia haki zenu na haki za binadamu kwa ujumla.
“Tutaendelea kushirikiana na Serikali, Bunge, taasisi mbalimbali, wadau wa maendeleo na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha kuwa watu wenye ualbino wanapata ulinzi, heshima, fursa na haki zote wanazostahili kama raia wengine,”amesema na kuongeza "Utu, usawa, upendo na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye amani kwa wote."
Akieleza zaidi kuhusu maadhimisho hayo amesema TRAMEPRO inaamini siku hiyo ni fursa muhimu ya kuendelea kuelimisha jamii kuhusu haki, usawa, usalama, afya na ustawi wa watu wenye ualbino, pamoja na kupinga ubaguzi, unyanyapaa na vitendo vyote vya ukatili vinavyokiuka haki zao za msingi.
Pia maadhimisho hayo yanakumbusha wajibu wa pamoja wa kujenga jamii inayoheshimu utu, usawa na haki za kila mwanadamu bila kujali tofauti zake za kimaumbile.
“TRAMEPRO inatoa pongezi kwa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Albinism Sports Club, Serikali, Bunge, wataalamu wa tiba asili, wadau wa afya, elimu, michezo na mazingira pamoja na wanachama wote wa TRAMEPRO kwa mchango wao katika kuimarisha ustawi, usalama na maendeleo ya watu wenye ualbino nchini.”
Wakati huo huo Mwalongo ametumia maadhimisho hayo kueleza wanatambua na kupongeza mechi ya kirafiki iliyochezwa Juni 6,2026 kati ya Bunge Sports Club na Albinism Sports Club, ambayo imeendelea kuwa mfano bora wa matumizi ya michezo katika kuhamasisha ushirikishwaji, mshikamano, uelewa na mapambano dhidi ya ubaguzi kwa watu wenye ualbino.
Tukio hilo limeonesha michezo ni nyenzo muhimu ya kuunganisha jamii na kuimarisha mshikamano wa kitaifa.Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa Bunge Sports Club, Waheshimiwa Wabunge na wadau wote walioshiriki kufanikisha tukio hilo muhimu.
Aidha, wanaguswa na moyo wa upendo, utu na kujali uliooneshwa na Salma Kikwete, ambaye baada ya kuguswa na hali halisi ya baadhi ya wachezaji wa Albinism Sports Club alionesha moyo wa kuwafariji na kuwasaidia. Kitendo hicho ni mfano wa kuigwa katika kujenga jamii yenye huruma, mshikamano na usawa.
“Pia tunatoa shukrani kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)kwa kuwezesha upatikanaji wa miche iliyotumika katika zoezi hilo. Mchango huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za Serikali, mashirika ya kiraia na wananchi katika kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”
Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma, ameishauri Serikali kupitia upya masharti mapya yanayowataka madereva walioko kazini kufanyiwa mafunzo na mitihani upya ili kuhuisha leseni zao, akisema utaratibu huo unaweza kuhatarisha ajira na maisha ya maelfu ya wananchi wanaotegemea udereva kama chanzo cha kipato.
Akichangia mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali bungeni, Musukuma amesema kuna madereva wengi nchini ambao wamefanya kazi kwa zaidi ya miaka 30 bila kusababisha ajali kubwa, hivyo hawapaswi kulazimishwa kurudi darasani na kufanya mitihani inayoweza kuwaondoa kazini.
Amesema utekelezaji wa masharti hayo mapya unaweza kuwaongezea mzigo mkubwa madereva wenye kipato cha chini, ambao tayari wanakabiliwa na changamoto za kifamilia na maisha ya kila siku yanayotegemea mshahara wao wa kila mwezi.
Mbunge huyo pia ametumia nafasi hiyo kuikosoa Serikali kuhusu baadhi ya miradi ya maendeleo, hususan ujenzi wa masoko na stendi za kisasa, akidai kuwa baadhi ya miradi hiyo haitimizi mahitaji halisi ya wananchi katika maeneo husika.
Katika hoja nyingine, Musukuma amepinga matumizi makubwa ya fedha za umma katika maonesho, mikutano na warsha za watumishi wa umma, akisema shughuli hizo zinagharimu Serikali fedha nyingi kupitia safari, malazi na posho, fedha ambazo angependa zielekezwe zaidi kwenye huduma za maendeleo.
Badala yake, ameshauri Serikali kuimarisha matumizi ya teknolojia za mawasiliano, ikiwemo mikutano ya mtandaoni, ili kupunguza gharama zisizo za lazima na kuongeza ufanisi katika utendaji wa shughuli za serikali.
📍Dodoma
Tume ya Madini imeanza kutoa elimu kwa wananchi kuhusu sekta ya madini katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu rasilimali madini na fursa zinazotokana na sekta hiyo.
Maonesho hayo yaliyoanza leo Juni 16, 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026, yakikutanisha taasisi mbalimbali za umma kwa lengo la kuonesha huduma wanazotoa kwa wananchi chini ya kaulimbiu isemayo, “Kuchochea Uwajibikaji kwa Huduma Endelevu.”
Kupitia banda lake, Tume ya Madini inatoa elimu kuhusu aina mbalimbali za madini yanayopatikana nchini, mchango wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa taifa, pamoja na fursa za uwekezaji, ajira na ushiriki wa wananchi katika shughuli za uchimbaji na biashara ya madini.
Aidha, wananchi wanaotembelea banda la Tume wanapata fursa ya kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi kwa wadau wa sekta ya madini, sambamba na kupata ufafanuzi kuhusu taratibu na miongozo inayosimamia shughuli za madini nchini.
Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho Juni 17, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.
Wananchi wamehimizwa kutembelea mabanda mbalimbali ili kujionea huduma zinazotolewa na taasisi za umma na kupata elimu itakayowawezesha kunufaika na fursa zilizopo katika sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo sekta ya madini.
TANZANIA imeonyesha mafanikio makubwa katika kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia, ambapo kiwango cha kitaifa cha upatikanaji kimeongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 28.6 mwaka 2025.
Ongezeko hilo la mara nne zaidi, linadhihirisha athari za jitihada mahsusi za serikali, dhamira ya kisiasa na ushirikiano na wadau wa maendeleo pamoja na sekta binafsi.
Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Innocent Luoga, ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa Maadhimisho ya Miaka 13 ya Mpango wa Energising Development (EnDev) nchini.
Amesema mafanikio hayo yanaonyesha dhamira ya Tanzania kuhakikisha wananchi wanapata nishati safi, salama na nafuu ya kupikia na kwamba chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kupikia safi kumepewa kipaumbele cha kitaifa na kuingizwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050.
Mhandisi Luoga ameeleza kuwa, Mkakati wa Kitaifa wa Kupikia Safi 2024–2034 unalenga kufikia asilimia 80 ya upatikanaji wa kupikia safi ifikapo mwaka 2034, huku National Energy Compact 2025–2030 ikilenga asilimia 75 ifikapo mwaka 2030.
Ameongeza ingawa kumekuwa na mafanikio, zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania bado wanategemea kuni na mkaa, hali inayochangia uchafuzi wa hewa majumbani, uharibifu wa mazingira na mzigo wa muda kwa wanawake na watoto.
Kupitia mpango wa EnDev, changamoto hizo zimepunguzwa kwa kusambaza teknolojia nafuu na bora za kupikia, hususan Jiko Matawi linalozalishwa nchini.
Majiko hayo hupunguza matumizi ya kuni kwa hadi asilimia 40, kuboresha ustawi wa kaya na kusaidia uhifadhi wa misitu pamoja na juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Tangu mwaka 2013 hadi 2026, EnDev imefanikisha upatikanaji wa suluhisho za taa za sola kwa takribani watu 300,000 na suluhisho za kupikia safi kwa watu milioni 2 kupitia majiko bora na teknolojia za kupikia kwa umeme.
Mpango huo umewezesha zaidi ya wazalishaji 120 wa Jiko Matawi kufanya kazi katika mikoa 20, na hivyo kuunda ajira na kuimarisha ujasiriamali wa ndani.
Aidha, Mhandisi Luoga amesifu kuanzishwa kwa Chama cha Kitaifa cha Wazalishaji wa Jiko Matawi, akisisitiza kuwa serikali itaendelea kuunda mazingira wezeshi kupitia mageuzi ya sera, uendelezaji wa masoko na upatikanaji wa fedha. Amesema mafanikio ya EnDev yanatoa msingi thabiti wa kupanua suluhisho za nishati safi na kuboresha maisha ya mamilioni ya kaya nchini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa SNV Tanzania, Mary Rauscher, amesema kwa zaidi ya muongo mmoja, EnDev imepanua upatikanaji wa nishati safi, nafuu na endelevu kwa karibu watu milioni 2, hususan vijijini na maeneo yaliyokuwa hayajahudumiwa.
Ameongeza kuwa kupitia mbinu za soko, mpango huu umechochea ukuaji wa sekta binafsi, kuwawezesha wajasiriamali wa ndani na kuimarisha mnyororo mzima wa thamani kuanzia kupikia safi hadi suluhisho za solar off-grid.
Rauscher amesisitiza kuwa maendeleo endelevu yanahitaji mageuzi ya mifumo katika sekta za nishati, kilimo na maji.SNV inalenga kuimarisha taasisi, kuwezesha masoko jumuishi na kushughulikia mizizi ya ukosefu wa usawa.
Amesisitiza kuwa usawa wa kijinsia na ujumuishaji wa kijamii ni kiini cha kazi zao, kuhakikisha wanawake, vijana na makundi yaliyotengwa si wadau pekee bali pia ni wahamasishaji wakuu wa mabadiliko.
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


BENKI ya NMB imezindua rasmi NMB Mkononi Super App ikiwa ni jukwaa jipya la kidijitali linalolenga kubadili namna Watanzania wanavyosimamia maisha yao ya kifedha kwa kuweka huduma mbalimbali za benki, uwekezaji, akiba, mikopo na bima katika mfumo mmoja wa kisasa.
Akizungumza leo Juni 16,2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna amesema uzinduzi wa Super App hiyo unaashiria mwanzo wa enzi mpya ya huduma za kifedha nchini zinazokidhi mahitaji ya kizazi cha sasa na cha baadaye.
"Kuzingatia mahitaji ya leo na ya kesho, tunapoizindua Super App tunazindua namna mpya ya Watanzania kusimamia maisha yao ya kifedha, namna mpya ya kulinda maisha yao kupitia bima, namna mpya ya kuwekeza na kuweka akiba," amesema.
Amesema dunia imebadilika kwa kasi ambapo huduma nyingi sasa zinapatikana kupitia simu za mkononi, hivyo ni muhimu sekta ya fedha nayo kwenda sambamba na mabadiliko hayo.
"Leo watu wanasoma kupitia simu, wanasafiri kupitia simu, wanawasiliana kupitia simu na hata maisha yao ya kila siku yako kwenye simu. Sasa tumekusanya huduma zote muhimu za kifedha sehemu moja kwa urahisi, usalama na kasi inayoendana na mahitaji ya mteja wa sasa," amesema.
Zaipuna amesema NMB imeboresha mfumo huo baada ya kusikiliza maoni ya wateja wake waliotaka huduma nyingi zaidi zipatikane kupitia programu moja.
Miongoni mwa maboresho hayo ni uwezo wa mteja kuona akaunti zake zote katika sehemu moja bila kulazimika kutumia mifumo tofauti, pamoja na uwezo wa kuziunganisha mwenyewe ndani ya programu.
Aidha, amesema wateja sasa wanaweza kuweka standing orders kupitia simu zao, jambo litakalowarahisishia kufanya uhamisho wa fedha au kuweka akiba kwa wakati bila kukumbushwa kila mwezi.
Kwa mujibu wa Zaipuna, Super App hiyo pia imeongeza uwezo wa kufungua akaunti mpya kidijitali bila kufika tawi lolote la benki.
"Mteja hatahitaji kufika benki wala tawi lolote. Ataweza kufungua akaunti yake mwenyewe kupitia simu yake popote alipo," alisema.
Aliongeza kuwa mfumo huo unamwezesha mteja kupata taarifa mbalimbali za kifedha, kufuatilia mwenendo wa matumizi na kufanya maamuzi bora ya kifedha kupitia taarifa zinazopatikana ndani ya programu.
Zaipuna alisema hata watu ambao si wateja wa NMB sasa wanaweza kupakua programu hiyo na kuanza safari ya kujiunga na huduma za benki kwa urahisi.
Kuhusu huduma za mikopo, alisema kupitia Super App mteja binafsi anaweza kuomba mkopo wa hadi shilingi milioni mbili moja kwa moja kupitia simu yake, huku wafanyabiashara wadogo na wa kati wakipata fursa ya kuomba mikopo ya hadi shilingi milioni tano.
Amesema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa wa teknolojia uliofanywa na benki hiyo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ili kuhakikisha huduma zake zinakidhi viwango vya kimataifa.
Katika kuelezea umuhimu wa programu hiyo kwa vijana, Zaipuna alisema kizazi cha sasa kinahitaji huduma zinazopatikana muda wote na zinazokwenda sambamba na kasi ya maisha ya kidijitali.
"Vijana wa leo wanataka kusimamia fedha zao kupitia simu. Simu imekuwa biashara, benki na sehemu ya maisha yao ya kila siku. Hii Super App imejengwa kwa ajili yao na kwa ajili ya Watanzania wote," amesema.
Amewahimiza pia wabunifu wa teknolojia na wajasiriamali wa kidijitali kutumia fursa iliyopo ndani ya mfumo huo kuendeleza ubunifu wao kwa kushirikiana na NMB.
Kwa mujibu wake, benki hiyo inayohudumia zaidi ya wateja milioni 10 inalenga kuifanya Super App kuwa jukwaa la huduma mbalimbali za kifedha na biashara.
Zaipuna amesema moja ya huduma muhimu zilizoboreshwa ni usimamizi wa vikundi vya kijamii na kiuchumi kupitia mfumo huo.
Amesema vikundi vitaweza kufungua akaunti, kuwaalika wanachama, kuweka kanuni zao za uendeshaji, kusimamia michango, mikopo ya ndani na kutoa taarifa za kifedha kwa uwazi zaidi bila kulazimika kukutana ana kwa ana.
"Vikundi vimekuwa shule ya kwanza ya elimu ya fedha kwa Watanzania wengi. Kupitia mfumo huu vitapata uwazi, usalama na ufanisi zaidi katika usimamizi wa fedha zao," amesema.
Ameeleza kuwa wanachama wataweza kuona michango yao, taarifa za kifedha na kushiriki maamuzi muhimu popote walipo kupitia simu zao.
Katika hatua nyingine, amesema Super App hiyo imeanza pia kutoa huduma za ununuzi wa bima kidijitali, ikiwemo bima za magari, pikipiki na mali dhidi ya moto.
Kwa mujibu wake, mteja anaweza kujinunulia bima au kumnunulia mtu mwingine kwa kutumia taarifa za msingi kama namba ya usajili wa gari au taarifa nyingine zinazohitajika, hatua inayorahisisha upatikanaji wa huduma za bima nchini.
Amesisitiza uzinduzi wa NMB Mkononi Super App ni sehemu ya mkakati wa benki hiyo kuendelea kuongoza mapinduzi ya huduma za kifedha kidijitali nchini kwa kuwapatia Watanzania huduma salama, rahisi na zenye kasi zinazowawezesha kufikia malengo yao ya kifedha.
Katika jamii ya Kimaasai, maisha ya mwanaume hupitia hatua mbalimbali za kimila zinazoonyesha ukuaji, Miongoni mwa hatua hizo muhimu ni kufanyiwa sherehe inayojulikana kwa jina la Orkiteng le Sirit ikimaanisha ni mwisho wa ujana na kuingia uzeeni.
Katika hatua hii ambapo mtu anatawazwa kuingia rika la uzee, wazee wa jamii hiyo huchagua Dume la rika ambalo lina afya njema na lililohasiwa tangu utoto wake, dume hili siku ya shughuli ndio hutolewa mwanzo kwenye boma lenye Ng’ombe wengi na kumwagiwa maziwa kisha hunyongwa hadi kufa.
Sherehe ya Orkiteng le Sirit , si sherehe ya kawaida bali ni tukio la heshima kubwa linalofanyika kwa kufuata mila na desturi za kale zilizorithishwa kutoka kizazi hadi kizazi. Kwa jamii ya Kimaasai, ni hatua ya ukamilifu wa mwanaume na uthibitisho kwamba ametimiza majukumu yake ya kifamilia na kijamii, kufanyiwa sherehe hii hakuangalii umri ila inazingatia jinsia kwa kuwa anayefanyiwa sherehe hii ni mwanaume pekee, vigezo vinavyoangaliwa ili mwanaume afanyiwe sherehe hii, ni lazima awe ameoa, awe na watoto wa kike na kiume na awe mtu mwema na maadili katika jamii.
Akizungumza wakati wa sherehe hiyo, Alaigwanani wa kabila la kimasai Maningo Rinjo amesema viongozi wa mila wa ukoo kama (Laizer, Mollel, Laitayo, Ngidong’i) ndio wenye jukumu la kumchagua dume atakayechinjwa baada ya kujiridhisha kuwa ana sifa zote zinazotakiwa kwa mujibu wa mila na desturi za Kimaasai ili kutekeleza jukumu hilo la kijamii ambalo linahudhuriwa na ndugu wote wa familia na jamii yote ya wamasai inayozunguka Kijiji hicho.
“Si kila dume anaruhusiwa kutumika katika sherehe hii, sisi viongozi wa mila hukagua na kuthibitisha sifa zake kabla ya kutoa ruhusa ya kuchinjwa, dume wa kutekeleza sherehe hii lazima awe amehasiwa tangu utotoni, hajawahi kumpanda dume jike, pembe zake ziwe zimenyooka bila kupinda mithili ya pembe za mbogo, asiwe mgonjwa na sifa zingine za ndani ambazo viongozi wa kimila ndio huzichunguza kwa undani,” alisema Alaigwanani Maningo Rinjo.
Alaigwanani Olonyori Lemoyan kutoka Ukoo wa Laizer Kata ya Nainokanoka Ngorongoro alisisitiza kuwa si kila mwanaume anastahili kufanya sherehe ya Orkiteng le Sirit, moja wa masharti muhimu ili mwanaume afanyiwe tukio hilo kuwa
na familia yenye watoto wa kike na kiume, awe na mali na uelekeo wa maisha, mtu anayejali watu na awe ni rafiki wa ukoo wake na jamii inayomzunguka pamoja na kupata ridhaa ya ukoo wake kufanya sherehe hiyo.
“Orkiteng le Sirit ni heshima kubwa katika jamii ya Kimaasai. Mwanaume lazima awe ametimiza wajibu wake wa kifamilia kwa kupata watoto wa kike na wa kiume. Bila kutimiza sharti hilo, hawezi kufikia hatua hii muhimu ya maisha,” alisema Alaigwanani Olonyori Lemoyan.
Wakati wa sherehe hizo baada ya dume kunyongwa na kutolewa nyama zake, mwanaume anayehitimu (anayepandishwa rika) pamoja na mke wake na mama yake mzazi wanatakiwa hukalia utumbo wa dume hilo kama ishara ya kuaga rasmi ujana na kuingia katika hatua ya uzee. Kitendo hicho hubeba maana kubwa ya kiutamaduni na kuashiria mwanzo wa jukumu jipya ndani ya jamii na kuachana na usharobaro na mambo yote ya ujana.
Baada ya taratibu hizo kukamilika, rika la Korianga huungana na mwenzao aliyeingia hatua ya uzee timilifu huimba nyimbo za furaha na heshima huku wakielekea bomani, wakimpongeza mwenzao kwa kufikia hatua hiyo adhimu. Nyimbo hizo huashiria kukubalika kwake rasmi katika kundi la wazee na kupewa nafasi ya kushiriki kikamilifu katika mila, desturi na maamuzi yanayohusu ustawi wa jamii.
Orkiteng le Sirit si tu sherehe ya kuchinja dume laa hasha, ni alama ya mafanikio ya maisha, uwajibikaji wa kifamilia na heshima ya kuwa mzee katika jamii ya Kimaasai. Hatua hii ni urithi wa kipekee unaoendelea kuunganisha vizazi na kuhifadhi utamaduni wenye thamani kubwa kwa jamii hiyo.

Na GULATONE MASIGA
Katika zama za teknolojia na mawasiliano ya kidijitali, mitandao ya kijamii imekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Kupitia majukwaa mbalimbali, wananchi wanapata habari, wanabadilishana mawazo, wanafanya biashara, wanajifunza na hata kushiriki katika mijadala ya masuala ya kitaifa na kimataifa.
Hata hivyo, pamoja na manufaa hayo makubwa, mitandao ya kijamii imegeuka kuwa chombo kinachoweza kutumika vibaya kueneza chuki, taarifa za uongo, uchochezi na hamasa zinazoweza kuhatarisha amani na utulivu wa jamii.
Kwa siku za karibuni, Tanzania imeshuhudia kampeni na hamasa kubwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii zinazohamasisha vurugu, ghasia na uvunjifu wa sheria kwa madai ya kudai haki au kuonyesha kutoridhika na hali fulani za kisiasa na kijamii.
Wakati haki ya kutoa maoni ni msingi muhimu wa demokrasia, ni lazima kutofautisha kati ya maoni yenye kujenga na uchochezi unaoweza kusababisha madhara kwa taifa zima.
Somo Kutoka Kumbukumbu za Oktoba 2025
Watanzania wengi bado wanakumbuka yaliyotokea mwezi Oktoba 2025. Kilichoanza kama kampeni na hamasa katika mitandao ya kijamii kiligeuka kuwa hali iliyosababisha taharuki, hofu na maumivu kwa sehemu mbalimbali za nchi.
Kulishuhudiwa matukio ya vifo na majeruhi. Miundombinu ya umma iliharibiwa na kuchomwa moto. Baadhi ya biashara na mali binafsi ziliporwa au kuharibiwa. Usafiri ulitatizika katika maeneo mbalimbali, huku wananchi wa kawaida wakibeba mzigo mkubwa wa madhara yaliyotokana na yaliyoitwa maandamano ya amani.
Athari zake hazikuishia kwa waliohusika moja kwa moja pekee. Wafanyabiashara walipoteza mitaji yao. Wanafunzi walikosa utulivu wa kujifunza. Wawekezaji walipata wasiwasi kuhusu mazingira ya biashara. Familia nyingi ziliishi katika hofu na sintofahamu.
Haya ni maumivu ambayo hayapaswi kusahaulika kwa urahisi.
Ukweli Mchungu wa Mitandao ya Kijamii
Moja ya mambo yanayopaswa kutafakariwa kwa kina ni kwamba sehemu kubwa ya wanaohamasisha vurugu na machafuko hawapo maeneo ambayo matukio hayo yanatokea. Wengine wako maelfu ya kilomita mbali katika nchi za Ulaya, Marekani au maeneo mengine duniani.
Wao hawatakutana na moshi wa matairi yanayowaka. Hawatapoteza biashara zao. Hawatakuwa kwenye foleni za dharura hospitalini. Hawatapoteza ajira wala kuhangaika na usafiri au kutafuta chakula kwa sababu shughuli za kiuchumi zimesimama.
Mara nyingi, anayepata madhara ni mwananchi wa kawaida. Ni mama lishe anayekosa wateja. Ni dereva anayekosa safari. Ni mfanyabiashara anayepoteza mtaji wake. Ni mwanafunzi anayekosa masomo. Ni taifa lote linalopoteza muda na rasilimali ambazo zingeelekezwa katika maendeleo mengine zinatumika kujenga upya miundombinu iliyoharibiwa na kuhudumia waathirika.
Ndiyo maana ni muhimu kila Mtanzania kutambua kuwa si kila ujumbe unaosambaa mtandaoni unapaswa kufuatwa bila kuhoji. Elimu ya kidijitali inahitaji uwezo wa kuchambua taarifa, kutambua propaganda, na kupima matokeo ya kile kinachohamasishwa.
Amani ni Mtaji wa Maendeleo
Tanzania imejijengea sifa ya kuwa taifa la amani, umoja na mshikamano kwa miongo mingi. Hii si bahati mbaya. Ni matokeo ya juhudi za viongozi, taasisi na wananchi waliotanguliza maslahi ya taifa mbele ya tofauti zao.
Amani ndiyo imewezesha uwekezaji katika sekta mbalimbali. Ndiyo imewezesha ujenzi wa shule, hospitali, barabara, miradi ya maji na umeme. Ndiyo imewezesha biashara kukua na vijana kupata fursa za ajira.
Historia inaonesha kuwa pale ambapo amani inapotoweka, maendeleo husimama. Wawekezaji huondoka. Uchumi hudorora. Huduma za kijamii huathirika. Mwisho wa siku, gharama hulipwa na wananchi wenyewe.
Kwa sababu hiyo, amani si jambo la kuchukuliwa kawaida. Ni rasilimali ya taifa inayohitaji kulindwa kila siku.
Matumizi Chanya ya Mitandao ya Kijamii
Badala ya kutumia mitandao ya kijamii kueneza chuki, vurugu au taharuki, kuna fursa kubwa zaidi za kuitumia kwa manufaa ya jamii.
Vijana wanaweza kuitumia kujifunza ujuzi mpya, kutangaza biashara zao, kutafuta masoko, kuhamasisha shughuli za maendeleo na kujenga mitandao ya kitaaluma.
Wananchi wanaweza kuitumia kutoa maoni kwa staha, kuibua changamoto za jamii na kushiriki katika mijadala yenye kujenga suluhisho.
Mitandao ya kijamii inaweza kuwa daraja la maendeleo au chanzo cha migogoro. Mwelekeo wake unategemea namna tunavyoichagua kuitumia.
Wajibu wa Kila Mtanzania
Katika kipindi hiki ambacho taarifa husambaa kwa kasi kubwa, kila Mtanzania ana wajibu wa kuwa mlinzi wa amani.
Tusisambaze taarifa ambazo hatujazithibitisha. Tusikubali kutumiwa kama vyombo vya kueneza chuki au uchochezi. Tujiulize kila mara: Je, ujumbe ninaoshiriki kuusambaza unajenga au unabomoa? Unaleta suluhisho au unachochea mgogoro?
Tofauti za maoni ni sehemu ya jamii yoyote ya kidemokrasia. Lakini tofauti hizo zinapaswa kushughulikiwa kwa njia za kistaarabu, za kisheria na zinazolinda maisha na mali za wananchi.
Hitimisho
Watanzania walipata somo kubwa kutokana na matukio ya Oktoba 2025. Somo hilo linapaswa kutukumbusha kuwa amani ikivurugika, hakuna anayebaki salama. Madhara yake huwagusa wote bila kujali itikadi, dini, kabila au hali ya kiuchumi.
Tusikubali tena kuingia katika mkumbo wa hamasa zinazoweza kusababisha machafuko, vurugu na uharibifu. Badala yake, tuutumie uwezo wa teknolojia na mitandao ya kijamii kujenga uchumi, kuimarisha umoja wa kitaifa, kuitangaza Nchi yetu kwa uzuri wake na kuharakisha maendeleo ya nchi yetu.
Amani ya Tanzania ni wajibu wa kila Mtanzania. Tukiilinda leo, tutakuwa tumelinda ustawi wa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Kwa Maoni Na Ushauri
0768497974
Ushirikiano huu unadhihirisha dhamira ya dhati ya Benki ya Exim Tanzania ya kutoa zaidi ya huduma za kibenki kwa wananchi na kutoa suluhisho bunifu kwa wateja ili kukidhi mahitaji yao yanayobadilika kila siku na hatimaye kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Kupitia huduma hii ya ufadhili wa magari, wateja wapya na waliopo wa Benki ya Exim Tanzania watapata mikopo ya kununua magari mapya na yaliyotumika ya aina mbalimbali, ikiwemo chapa zinazozidi kupata umaarufu kutokana na ubunifu na ubora wake kama Jetour, Eicher, Sany na JAC Motors.
Wateja watanufaika na malipo ya kila mwezi yenye unafuu kwa kipindi cha hadi miezi 72, jambo linalofanya ndoto ya kumiliki gari la kuaminika na lenye ubora wa hali ya juu kufikiwa kwa urahisi zaidi kuliko wakati mwingine wowote
Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini makubaliano hayo, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim Tanzania Shani Kinswaga alisema ushirikiano huo umebuniwa mahsusi kwa ajili ya kuwahudumia makundi mbalimbali ya wateja, ikiwemo waajiriwa, wamiliki wa biashara, wajasiriamali, watu wenye kipato kikubwa, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi za kibiashara zinazohitaji suluhisho bora za usafiri bila kuathiri mtaji wao wa uendeshaji.
"Benki ya Exim Tanzania tunaendelea kujizatiti kwa kutumia ubunifu wa hali ya juu kuwawezesha wateja wetu na kuwasaidia kufikia malengo yao. Ushirikiano wetu na Africarriers unatuwezesha kutoa huduma rahisi na zinazobadilika za ufadhili wa magari ambazo zitawawezesha watu binafsi na wamiliki wa biashara kupata usafiri wa kuaminika huku wakihifadhi rasilimali zao za kifedha kwa mahitaji mengine muhimu," alisema Shani.
Mpango wa Ufadhili wa Umiliki wa Magari kupitia Benki ya Exim unawapa fursa wateja wetu ya kupata magari mapya au yaliyotumika kwa urahisi zaidi. Wateja watahitajika kuchangia asilimia 20 hadi 30 tu ya gharama ya gari kama malipo ya awali, huku malipo kwa wauzaji wa magari yakifanywa moja kwa moja ili kuhakikisha mchakato wa ununuzi unakuwa rahisi na wa haraka zaidi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Fedha wa Kundi la Africarriers, Mustafa Rashid, alisema kuwa kwa kuunganisha mpango mpana wa upatikanaji wa magari unaotolewa na Africarriers na uwezo wa Exim Bank katika utoaji wa huduma za mikopo na ufadhili, taasisi hizo mbili zimeleta suluhisho rahisi na yenye tija ya kuwawezesha watu binafsi na wafanyabiashara kumiliki magari.
"Ushirikiano huu ni udhihirisho wa dhati wa dhamira yetu ya kutoa suluhisho za usafiri zinazofikika na kuaminika kwa Watanzania. Kwa kushirikiana na Benki ya Exim Tanzania, tunawapa wateja chaguo bora na rahisi la kumiliki magari huku likichochea ukuaji wa biashara na maendeleo ya uchumi wa nchi," alisema Mustafa.
Ushirikiano huu unaakisi dhamira ya pamoja ya taasisi hizi mbili katika kupanua upatikanaji magari na kuwawezesha Watanzania wengi zaidi kutimiza ndoto zao za kumiliki magari, ikiwemo magari mapya kabisa. Kupitia huduma hii, watu binafsi na familia wataweza kubadilisha ndoto zao kuwa uhalisia huku wakifurahia urahisi, uhuru na fursa mbalimbali zinazotokana na umiliki wa gari.
Exim Bank inawahimiza wateja wake kutembelea tawi lolote la benki hiyo au yadi za magari za Africarriers zilizopo kote nchini ili kupata taarifa zaidi kuhusu huduma hii na aina mbalimbali za magari yanayopatikana, na kisha kuchukua hatua kuelekea kumiliki magari bora ya ndoto zao.
Mkuu wa masoko wa Africarriers Ltd Mohamed Ladha (kushoto) akielezea zaidi ubora wa magari kwa Menejimenti, Wafanyakazi na Wateja wa Benki ya Exim Tanzania baada ya utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Africarriers na Benki ya Exim Tanzania yenye lengo kufadhili na kurahisisha ununuzi wa magari kwa watu binafsi, wajasiriamali, biashara ndogo na za kati (SMEs), pamoja na taasisi mbalimbali nchini kupitia mikopo yenye masharti nafuu ya ulipaji. Tukio hilo lilishuhudiwa na Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim Tanzania, Shani Kinswaga (wa nne kulia), Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu (wa tano kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Africarriers Ltd Bw Fidahussein Rashid (wa tatu kushoto) jijini Dar es Salaam juni 16 2026.

.jpeg)
Wabunge wameipongeza Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kuendelea kupanua wigo wa huduma za hifadhi ya jamii kupitia Skimu ya Hifadhi kwa Wananchi Waliojiajiri, wakisema mpango huo unatoa fursa kwa mamilioni ya Watanzania kunufaika na huduma za hifadhi ya jamii.
Aidha, wamepongeza uwekezaji uliofanywa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) katika Kiwanda cha Kimataifa cha Bidhaa za Ngozi cha Kilimanjaro (KLICL), wakisema mradi huo una mchango mkubwa katika kukuza viwanda, kuongeza thamani ya mazao ya mifugo na kutengeneza ajira.
Pongezi hizo zilitolewa Juni 15, 2026 jijini Dodoma wakati wa semina ya wabunge kuhusu Skimu ya Hifadhi kwa Wananchi Waliojiajiri na Mradi wa Kiwanda cha Kimataifa cha Bidhaa za Ngozi cha Kilimanjaro.
Akizungumza kwa niaba ya Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu, Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, aliipongeza NSSF pamoja na PSSSF kwa kuendelea kutoa elimu kwa wabunge kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na mifuko hiyo.
Mhe. Sillo alisema elimu hiyo ni muhimu kwa wabunge kwani itawawezesha kuwa mabalozi wa kuhamasisha wananchi katika majimbo yao kujiunga na mifumo ya hifadhi ya jamii na kufahamu uwekezaji unaofanywa na mifuko hiyo.
Baadhi ya wabunge walioshiriki semina hiyo, akiwemo Mhe. Said Salimu na Mhe. Rashid Shangazi, waliipongeza NSSF kwa juhudi zake za kuwafikia wananchi waliojiajiri na kuimarisha huduma za hifadhi ya jamii nchini.
Walisema skimu hiyo itasaidia kujenga utamaduni wa kuweka akiba, kuongeza usalama wa kipato na kuwapa wananchi waliojiajiri fursa ya kunufaika na huduma za hifadhi ya jamii.
Kwa upande wa uwekezaji wa PSSSF, wabunge Jackson Kiswaga na Rashid Shangazi waliipongeza PSSSF kwa uwekezaji kwenye kiwanda hicho, huku wakiishauri sekta binafsi ikaribushwe katika uendeshaji wa kiwanda ili kuongeza nguvu katika masoko na uzalishaji.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, alisema Serikali inaendelea kuimarisha huduma za hifadhi ya jamii kwa kuwajumuisha wananchi waliojiajiri, ambao kwa muda mrefu walikuwa nje ya mifumo rasmi ya hifadhi ya jamii licha ya mchango wao mkubwa katika uchumi wa taifa.
Kuhusu PSSSF, Mhe. Sangu alisema mradi wa kiwanda hicho unamilikiwa kwa ubia kati ya Mfuko huo na Jeshi la Magereza kupitia kampuni yake ya Prisons Corporation Sole (PCS) na kuwa umekuwa na manufaa makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema mfuko huo unalenga kuandikisha wananchi waliojiajiri milioni 3.7 ifikapo Juni 2031 kupitia Skimu ya Hifadhi ya Jamii. Alisema takribani asilimia 85 ya nguvu kazi nchini, sawa na wananchi milioni 20.98 wenye uwezo wa kufanya kazi, wamejiajiri, jambo linaloifanya skimu hiyo kuwa nyenzo muhimu ya kuwafikia makundi mbalimbali ya wananchi.
Bw. Mshomba alisema wanachama wa skimu hiyo watanufaika na mafao mbalimbali yakiwemo pensheni ya uzee, mafao ya urithi, ulemavu, uzazi na matibabu. Alisema wananchi sasa wanaweza kujiunga, kuchangia na kufuatilia taarifa zao kwa njia za kidijitali kupitia simu za mkononi, huku kiwango cha chini cha mchango kikiwa shilingi 30,000 kwa mwezi.
Naye, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Fortunatus Magambo, amesema kiwanda hicho kinazalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na kimekuwa na mchango mkubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla.
Alisema kiwanda hicho kimeongeza ajira kwa wananchi, kimeboresha kipato cha wananchi hususan wafugaji kupitia upatikanaji wa soko la uhakika la ngozi, na kuchochea mnyororo wa thamani wa sekta ya mifugo nchini.
“Kiwanda chetu kinazalisha bidhaa zenye ubora mkubwa, kimeongeza ajira kwa wananchi na kimefungua soko la uhakika la ngozi kwa wafugaji wetu, jambo linalonufaisha jamii na taifa kwa ujumla,” alisema Bw. Magambo.





































.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)