MWANZA

Wadau wa Sekta ya Milki mkoani Mwanza wamesisitizwa kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia sheria, taratibu na misingi ya taaluma ya milki ili kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kutoa huduma bora na zenye kuaminika kwa wananchi.

Msisitizo huo umetolewa leo Machi 17, 2026 mkoani Mwanza na Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa huo, Bw. Wilson Luge, wakati akifunga kikao kazi cha wadau wa Sekta ya Milki kilichoandaliwa na Kitengo cha Milki kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Amesema mafunzo na semina zinazotolewa kwa wadau wa Sekta ya Milki yana mchango mkubwa katika kuongeza uelewa wa kitaalamu pamoja na kuimarisha utendaji kazi katika kutoa huduma bora kwa wananchi, hususan katika masuala yanayohusu tathmini ya mali na usimamizi wa milki.

“Tunapenda kuishukuru Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Kitengo cha Milki kwa kutoa semina na mafunzo kwa wadau wetu wa Sekta ya Milki. Mafunzo haya yatawasaidia kuongeza ujuzi na kuimarisha weledi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku,” amesema Luge.

Aidha, amewasisitiza wadau hao wa sekta ya milki kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao na kujiepusha na vitendo vinavyokiuka sheria ikiwemo kujihusisha na masuala ya utakatishaji fedha, huku akielezea umuhimu wa kufuata taratibu zote za kisheria na kitaaluma katika kutoaji huduma za tathmini ya mali.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Kitengo cha Milki (Real Estate) inaendesha mijadala ya pamoja na wadau kwa lengo la kupata maoni kuhusu utambuzi na usajili wa Wadau wa Sekta ya Milki ili kuboresha na kukuza sekta ya milki nchini.

Mijadala hiyo inalenga kutoa elimu, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazoikabili sekta ya milki nchini ambapo tayari kitengo hicho kimefanya vikao vya mijadala katika mkoa wa Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Tanga, Mwanza na Morogoro.

Menejimenti ya Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) imebuni mfuko wa kushirikisha wadau (stakeholders) kuwezesha kusaidia matibabu ya Upandikizaji wa Viungo kwa kuanza na Upandikizaji Uloto kwa watoto wenye Selimundu(Sickle cell) na Upandikizaji Figo kwa Wananchi wenye Uhitaji. Akiwasilisha mpango huo kwenye mkutano wa Wenyeviti wa Bodi na Wakurugenzi wa Mashirika ambayo Serikali ina hisa ndogo (Miinority Interest Forum ) ulioandaliwa na ofisi ya Msajili wa Hazina, mjini Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa BMH ,Prof Abel Makubi ameeleza kuwa mfuko huo unajengwa kwa Dhana ya Wadau wenye Moyo wa Huruma wa kusaidia huduma za matibabu zenye gharama kubwa kwa Wananchi wenye uhitaji katika kuunga mkono juhudi za Serikali. Prof. Abel Makubi ameeleza kuwa mfuko huo unachangiwa na wadau kutoka mashirika ya umma chini ya uratibu ya Msajili wa Hazina, Mashirika Binafisi na mtu mmoja mmoja , na unategemewa kukusanya TZ shilingi billion 7 ndani ya miaka miwili ili kusaidia huduma hizo katika Matibabu, vifaa, kupanua miundombinu mbinu na kuendelea kujengea uwezo watalamu wa taaluma hizo.  

Mfuko huo unategemewa kuzinduliwa rasmi tarehe 8 Mei 2026 katika kilele cha Maadhimisho ya Miaka 10 ya BMH , na Wadau takribani 200 wameshirikishwa katika mpango huu .

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. John Jingu, amesema kuanzishwa kwa Mfuko wa Pamoja wa Ruzuku kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs Basket Fund - NBF) kutarahisisha upatikanaji wa rasilimali fedha na uendelevu kwa Mashirika hayo nchini.

Akizungumza Machi 18, 2026, wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha kwanza cha Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu Mchakato wa Uanzishwaji wa Mfuko huo, kilichofanyika katika ukumbi wa Four Points by Sheraton Jijini Dar es Salaam, Dkt. Jingu amesema Mfuko huo utakuwa chombo muhimu cha kuimarisha sekta ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Dkt. Jingu ameeleza kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto za utegemezi wa ufadhili kutoka nje ya nchi, ambao wakati mwingine huambatana na masharti magumu yasiyoendana na maadili na utamaduni wa Kitanzania.

“Jukumu la Mfuko huu litakuwa ni kutafuta rasilimali fedha, kuratibu utoaji wa ruzuku na kuhakikisha Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanakuwa na uwezo wa kutoa huduma bora na kuchangia ustawi wa jamii na Taifa kwa ujumla,” amesema Dkt Jingu.

Aidha, amebainisha kuwa kutokana na mabadiliko ya sera za ufadhili kimataifa, ni muhimu kwa Mashirika hayo kubadilika na kujiimarisha kwa kutumia mikakati mbadala itakayohakikisha uendelevu wa shughuli zao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dkt. Abdulmajid Nsekela, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB amesema mafanikio ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati yanategemea uwajibikaji wa kila mmoja kwa nafasi yake huku akisisitiza kuwa ni muhimu Wajumbe wa Kamati kufanya kazi kwa weledi, kwa kuzingatia misingi ya uwazi na uwajibikaji ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NacoNGO), Jasper Makala, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, amesema Mashirika mengi kwa sasa yanafanya kazi bila uhakika wa uendelevu wa miradi yao hivyo uwepo wa Kamati hiyo itasaidia kuongeza uhakika wa rasilimali fedha na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu wa Mashirika hayo.

“Mfuko huu utakuwa suluhisho muhimu kwa changamoto ya uhaba wa rasilimali fedha na utasaidia Mashirika kupanga na kutekeleza shughuli zao kwa ufanisi zaidi,” amesisitiza Makala.

Naye Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kutoka Wizara hiyo, ambaye pia ni Katibu wa Kamati hiyo, Vikness Mayao, amesema Mfuko huo utakuwa chachu ya maendeleo kwa Mashirika hayo, kwa kuwa utaongeza tija katika utekelezaji wa miradi ya kijamii.

Ameongeza kuwa kupitia Mfuko huo, Mashirika yatapata fursa ya kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuchangia kwa kiwango kikubwa katika maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.








Farida Mangube Morogoro

Lori la mizigo lenye namba za usajili T729 BBT pamoja na tela namba T677 BTY limeteketea kwa moto katika eneo la Lugono, karibu na Nyama Choma  Barabara Kuu ya Iringa–Morogoro.

Tukio hilo la Lori kuwaka moto limetokea usiku wa kuamkia March 19  katika mazingira ambayo bado hayajafahamika wazi ambapo limeathiri vibaya sehemu ya mbele ya gari hiyo.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilifika  katika eneo la tukio na kufanikiwa kuudhibiti moto huo kabla haujasambaa zaidi, licha ya uharibifu mkubwa uliokwisha kutokea 

Mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, akiwemo mwandishi wa Michuzi Blog, walishuhudia lori hilo likiwa limeteketea huku juhudi za uokoaji zikiendelea.

Kwa mujibu wa taarifa za awali, mtu mmoja anasadikika kupoteza maisha kufuatia tukio hilo. Inadaiwa kuwa mwili wa mtu huyo uliungua vibaya kiasi cha kufanya utambuzi kuwa mgumu, huku mabaki yanayoaminika kuwa ya binadamu yakionekana katika eneo la tukio, ingawa utambuzi rasmi bado unasubiri uthibitisho wa mamlaka husika.

Wakati huo huo, jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro zinaendelea ili kutoa taarifa rasmi kuhusu chanzo cha ajali hiyo, kuthibitisha idadi ya waathirika pamoja na kueleza hatua zinazochukuliwa.

Aendelea kutufuatilia Michuzi Blog na Michuzi Tv ili kupata taarifa zaidi

 

Katika kuendeleza dhamira ya uwajibikaji kwa jamii, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limetembelea Kituo cha Watoto Yatima cha Umra Orphanage jijini Dar es Salaam, na kutoa msaada wa mahitaji muhimu sambamba na kuwapa faraja watoto wanaolelewa kituoni hapo, kuelekea sikukuu ya Idd.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Meneja wa Masoko na Mahusiano ya Umma wa STAMICO, Deus Alex , amesema lengo la watumishi wa shirika hilo ni kushiriki na jamii kwa vitendo, hususan kwa makundi yenye uhitaji maalum.

Amesema msaada huo haujalenga tu kukidhi mahitaji ya msingi, bali pia kuwajengea watoto hao imani, matumaini na ujasiri wa kuamini katika ndoto zao licha ya changamoto wanazokutana nazo.

“Tumekuja hapa si kwa ajili ya kutoa mahitaji pekee, bali pia kuwa karibu na watoto hawa, kuwapa moyo na kuwahakikishia kuwa wana uwezo wa kufikia mafanikio makubwa katika maisha yao,” amesema Mtukamazina.

Ameongeza kuwa, STAMICO itaendelea kutambua na kushirikiana na jamii inayowazunguka, kama sehemu ya mchango wake katika kujenga taifa lenye mshikamano na ustawi wa pamoja.

Kwa upande wake, Katibu wa Umra Orphanage Center, Hamza Ahmed Kanyange, amepongeza hatua hiyo akisema msaada uliotolewa umefika kwa wakati muafaka na umeleta faraja kubwa kwa watoto pamoja na walezi wao.

Amesema ujio wa STAMICO umeongeza furaha na kuwapa watoto motisha mpya, huku akibainisha kuwa vituo vya aina hiyo bado vinakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji ushirikiano wa wadau.

Aidha, ametoa wito kwa taasisi, makampuni na watu binafsi kuendelea kujitokeza kusaidia makundi yenye mahitaji maalum, ili kuhakikisha wanapata huduma bora na maisha yenye matumaini.



















NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) itaendelea kutoa fursa za mafunzo endelevu ya viongozi wa elimu wa ngazi mbalimbali na wadau wengine wa elimu ili waweze kuimarisha uongozi, usimamizi na uendeshaji wa shule kwa ajili ya utoaji wa elimu bora nchini.

Ameyasema hayo Mkurugenzi wa Elimu msingi, Abdul Maulid wakati akimwakilisha Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir katika ufungaji mafunzo ya uongozi, usimamizi na utawala bora wa elimu kwa Maafisa Elimu Kata Tanzania Bara yaliyofanyika katika Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), katika Halmashauri ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

Amesema mafunzo hayo yamekusudiwa kuwajengea uwezo viongozi na wasimamizi wa taasisi za elimu ili waweze kusimamia ipasavyo rasilimali na michakato ya utoaji wa elimu, huku wakizingatia misingi ya uongozi bora, uwazi na uwajibikaji.

"Ni matumaini yetu kuwa, ADEM mtaendelea kutoa mafunzo yanayoelenga kuimarisha uongozi, usimamizi na uendeshaji wa elimu kwa njia endelevu na yenye mafanikio pamoja na kufanya tafiti mbalimbali zakielimu na kutoa ushauri wa kitaalam katika masuala ya uongozi. Ninawasihi muendelee kufanya kazi kwa weledi ili kutimiza malengo ya kuanzishwa kwa ADEM". Amesema

Ameongeza kuwa ushirikishwaji wa jamii, matumizi sahihi ya takwimu za elimu na utoaji wa fursa za mafunzo endelevu kwa walimu ni mambo muhimu katika kuimarisha ubora wa elimu.

Ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo kutumia maarifa waliyoyapata kuboresha utendaji wao, akisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa weledi, ubunifu, kujituma na uzalendo ili kufanikisha malengo ya sekta ya elimu nchini.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid amesema kuwa mafunzo hayo yametekelezwa kama sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya kuimarisha mifumo ya usimamizi wa elimu kwa kuzingatia misingi ya uongozi bora, uwajibikaji na ufanisi katika utoaji wa huduma za elimu.

"Mpango huu ulianza kwa kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo Walimu Wakuu wa shule za msingi kuhusu Uongozi, Usimamizi na Utawala Bora wa Elimu, yaliyowahusisha Walimu Wakuu 17,817 kutoka Mikoa yote 26 ya Tanzania Bara". Amesema

Amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwaimarisha Walimu Wakuu katika kusimamia shule kwa kutumia mbinu stahiki za uongozi pamoja na kuzingatia sera, miongozo na viwango vya kitaifa ili kuhakikisha kuwa shughuli za ufundishaji na ujifunzaji zinafanyika kwa ubora, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa.

Pamoja na hayo Dkt. Maulid amesema kuwa tathmini inaonyesha kiwango kikubwa cha mabadiliko ya kiutendaji kwa walimu wakuu katika kuongoza na kusimamia shule zao baada ya kupatiwa mafunzo hayo.

`













Top News