Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipohutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Maonesho wa Mandewa, wilayani Ikungi, mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.
Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtuma kuwahakikishia wananchi wa Mkoa wa Singida kuwa miradi yote ya maendeleo iliyoahidiwa itaendelea kutekelezwa hatua kwa hatua kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali.
"Mheshimiwa Rais amenituma niwahakikishie kwamba mambo ambayo wabunge wenu wamekuwa wakiyasema na ambayo aliwaahidi wananchi wa Singida yatakwenda kutekelezwa," amesema.
Amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya barabara ikiwemo Sabasaba–Sepuka–Ndago–Kizaga, Njia Panda–Makiungu–Mungaa–Misughaa–Ndago, Mkiwa–Itigi–Rungwa–Makongorosi, Iguguno–Nduguti–Sibiti, pamoja na Singida–Ilongero–Haydom, hatua zitakazorahisisha usafirishaji, biashara na kufungua fursa zaidi za kiuchumi katika Mkoa wa Singida na maeneo jirani.
Aidha, amesema Serikali itaendelea na utekelezaji wa reli ya kisasa (SGR) itakayofika Singida pamoja na ujenzi wa uwanja wa ndege wa kisasa utakaohudumia ndege za ukubwa mbalimbali na kuongeza fursa za uwekezaji na biashara.
Waziri Mkuu amesema kuchelewa kwa baadhi ya miradi kulitokana na uamuzi wa Serikali kuelekeza rasilimali katika kukamilisha miradi ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere, Reli ya Kisasa (SGR) na Daraja la Kigongo–Busisi, ambayo sasa imeanza kutoa manufaa makubwa kwa Taifa.
"Tulifanya uamuzi wa kufunga mkanda ili tukamilishe miradi ya kimkakati. Leo Tanzania ina ziada ya umeme na miradi hiyo imeendelea kutoa manufaa makubwa kwa wananchi na uchumi wa Taifa," amesema.
Amesema Serikali itaendelea kuboresha huduma za maji, afya, elimu na miundombinu mingine ya kijamii sambamba na utekelezaji wa miradi hiyo ili kuongeza ustawi wa wananchi wa Mkoa wa Singida na Taifa kwa ujumla.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM - Bara) Ndg Stephen Wasira, amewataka Watanzania kuhifadhi na kuishi kulingana na urithi wa Mwalimu Julius Nyerere.
Akizungumza katika mahojiano maalumu, na ujumbe kutoka Serikali ya Angola, leo Juni 27, 2026. Wasira amemuelezea Mwalimu Nyerere kuwa kiongozi wa kipekee ambaye aliwaunganisha wananchi, alitawala kwa uadilifu mkubwa, na kuondoka madarakani bila kujilimbikizia mali.
Wasira alisema mojawapo ya sifa kuu za Mwalimu Nyerere ni uwezo wake wa kuwahamasisha Watanzania kushiriki kikamilifu katika masuala muhimu ya kitaifa badala ya kuwa watazamaji ukiwemo ulinzi wa taifa lao.
“Aliwashirikisha watu wote. Akieleza sababu ya vita, akawaambia ‘vita hii ni yetu sote.’ kila Mtu alipoona kiongozi wake anamweleza wazi hivi ndivyo ilivyotokea, hivi ndivyo tulivyoamua…basi mtu alishiriki moja kwa moja,”alisema Wasira akirejea Vita ya Kagera.
Kuhusu urithi halisi wa Nyerere, Wasira alitaja mambo mawili makuu ambayo yanapaswa kulindwa kwa umakini.
“Jambo moja tunalolikumbuka na tunalojaribu kulihifadhi kati ya aliyotuachia ni Uhuru. Pili ni Umoja. Kwa sababu Umoja hapa ni kitu tunachojivunia sana, nchi isiyo na ukabila, ambapo watu wa makabila na dini tofauti wanaishi pamoja kwa amani.” Amesema.
Alisema sehemu iliyogusa zaidi katika mazungumzo hayo yalikuwa maelezo ya Wasira kuhusu maisha ya Mwalimu Nyerere baada ya kung’atuka madarakani.
“Vizazi vijavyo vitamkumbuka Mwalimu Nyerere kama mtu aliyepigania uhuru wa nchi yake. Aliongoza nchi yake kwa miaka 24 kama Rais, na akaondoka madarakani akaenda kijijini. Akarudi kuwa mkulima mdogo. Hakuwa na pesa. Hakuwa na akaunti benki nje wala ndani ya nchi. Ni mtu wa kipekee sana,” alisema.
Aidha, alisema Mwalimu Nyerere aliamini kwamba uhuru wa Tanganyika hauwezi kuwa matunda zaidi pasipo nchi zingine za bara hilo kuwa huru.
"Mwalimu Nyerere aliamini kwamba uhuru wa Tanganyika bila uhuru wa Afrika kwamba usingekamilika mpaka nchi zote za Afrika ziwe huru.
“Alitoa mchango mkubwa wa ukombozi hasa kwa nchi za Kusini mwa Afrika, na mwisho aliamini katika umoja wa Afrika jambo ambalo hadi anaondoka duniani hakuweza kulikamilisha,” alieleza.
Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro imeanza utekelezaji wa mpango maalum wa kuboresha eneo la Endoro ili litumike kama sehemu ya utalii tiba kwa watalii pamoja na shughuli nyingine zinazohitaji utulivu.
Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Abdul-Razaq Badru akiwa na Wakurugenzi wa Bodi katika eneo hilo lenye Maporomoko ya Maji (Water Falls), Mapango ya Tembo, Msitu, Wanyama wakubwa na maarufu kwa utalii wa kutembea (Walking Safaris)
Ameeleza kuwa kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Utalii (TDL) eneo la Endoro linaboreshwa kwa ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya Utalii ili yatumike kama sehemu za utalii tiba, utafiti, utalii wa kutembea, mapumziko binafsi na kuondoa msongo wa mawazo.
“Endoro ni eneo lenye utulivu, lina kivutio cha Mapango ya Tembo na maporomoko ya maji yenye urefu wa mita 40, mamlaka imeamua kuboresha miundombinu yake ili mgeni akifika hapa na hasira aweze kupata utulivu na kurudi katika hali yake ya kawaida”,alisema kamishna Badru.
Makamu Mwenyekiti wa bodi hiyo Dkt. Harieth Mtae amepongeza jitihada hizo na kusema zitatoa fursa ya kuongezeka kwa idadi ya watalii wanaotembelea kivutio hicho kilichopo hifadhi ya Ngorongoro.
Wakurugenzi wa bodi hiyo pia wamekagua geti la kisasa la kuingilia ndani ya hifadhi linalofanya kazi katika mfumo wa kisasa pamoja na minara ya mawasiliano ndani ya hifadhi inayolenga kuboresha huduma kwa watalii.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 27, 2026) alipoweka jiwe la msingi la Jengo la Taaluma la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani Singida.
Waziri Mkuu amesema ujenzi wa jengo hilo unaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuboresha mazingira ya elimu ya juu na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi.
"Leo hii jengo hili la chuo chetu liko Singida. Hii ni hatua kubwa sana. Hongereni bodi, hongereni chuo, hongereni wanafunzi. Tunawatakia kila la heri," amesema.
Aidha, amewapongeza wahandisi, washauri na wakandarasi wazawa wanaotekeleza mradi huo akisema ushiriki wao unaonesha uwezo wa Watanzania katika kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo.
"Nimefurahishwa kwamba wahandisi wanaojenga ni wazawa, kwa sababu pia Mheshimiwa Rais alielekeza kwamba lazima tujenge uchumi unaomilikiwa na Watanzania na kujenga sekta binafsi ya ndani sambamba na uwekezaji kutoka nje," amesema.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha, Mhandisi Mshamu Ali Munde, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu kwa kuwekeza katika vyuo vya elimu ya juu ili kuongeza upatikanaji wa elimu bora, kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, kuimarisha tafiti, ubunifu na matumizi ya teknolojia pamoja na kuzalisha wataalamu wenye ujuzi unaohitajika katika utekelezaji wa dira ya maendeleo ya Taifa.
Amesema Wizara ya Fedha itaendelea kuhakikisha rasilimali za Serikali zinaelekezwa katika miradi yenye tija kwa wananchi, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA).
Awali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo, amesema jengo hilo la taaluma lina ukubwa wa mita za mraba 9,250 na litakuwa na kumbi za mafunzo, madarasa, kumbi za mihadhara, ukumbi wa mikutano pamoja na ofisi za watumishi.
Amesema mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 13.5 umefikia asilimia 63 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba, 2026. Aidha, ameiomba Serikali kuendelea kuwekeza katika ujenzi wa mabweni ili kukidhi ongezeko la wanafunzi litakalotokana na kukamilika kwa mradi huo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TIA, Prof. Jehovaness Aikaeli, amesema bodi itaendelea kusimamia utekelezaji wa mradi huo kwa kuzingatia thamani ya fedha na kukamilika kwa wakati, huku akieleza kuwa mradi huo utachangia kuzalisha rasilimali watu yenye ujuzi kwa maendeleo ya Mkoa wa Singida na Taifa kwa ujumla.
Naye, Mhandisi Mkazi Mshauri wa Mradi, Henry Chundu, amesema jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi wapatao 3,500 kwa wakati mmoja na limejengwa kwa kuzingatia viwango vya kisasa, ikiwemo mifumo ya usalama dhidi ya moto, matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira na miundombinu ya kuvuna maji ya mvua.
Benki ya Equity Bank Tanzania imeungana na wadau mbalimbali katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Biashara Ndogo, Ndogo na za Kati (SME Day) yaliyofanyika katika Ukumbi wa NSSF Mafao House, Ilala, Dar es Salaam, ambapo ilishiriki kama mshirika na mfadhili wa hafla hiyo iliyoandaliwa na SIDO.
Katika hafla hiyo, Equity Bank Tanzania na SIDO zilisaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya kimkakati yenye lengo la kuwawezesha zaidi ya wajasiriamali 8,000 nchini Tanzania kupitia huduma za kifedha, mafunzo ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uunganishaji wa masoko, ili kuimarisha ukuaji wa wa biashara ndogo na kati zinazochangia uchumi na ajira nchini
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Bi. Theresia Aloyce Mayanie, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo, wa Kati, na Binafsi kutoka Equity Bank Tanzania, alisema benki hiyo itaendelea kuwa mshirika mkuu wa maendeleo ya wajasiriamali nchini kupitia suluhisho mbalimbali za kifedha. Bi. Theresia alisema: "Equity Bank tunaamini kuwa wajasiriamali ndio injini ya ukuaji wa uchumi.
Kupitia ushirikiano wetu na SIDO, tunalenga kuwawezesha maelfu ya wafanyabiashara kupata mitaji, maarifa na fursa zitakazowasaidia kukuza biashara zao na kuboresha maisha yao.
Kwa ujumla, benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na taasisi za serikali na sekta binafsi ili kuimarisha mazingira ya biashara na kusaidia ukuaji endelevu wa wajasiriamali nchini Tanzania. @equitybanktz

▪️Ni Mkutano mkubwa wa Madini na Uwekezaji
▪️Washiriki 2000 kutoka mataifa 50 Duniani kushiriki
▪️Kauli Mbiu ya Mkutano inalenga kuongeza thamani madini kwa maendelezo ya Viwanda
▪️Serikali na Sekta Binafsi kushirikiana kuandaa mkutano huo
▪️Waziri Mavunde azindua rasmi maandalizi ya mkutano huo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia S. Hassan anatarajiwa kufungua rasmi Mkutano wa Saba wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIC 2026) utakaofanyika Novemba 19 hadi 21, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.
Akizungumza leo Juni 27, 2026 wakati wa uzinduzi wa TMIC 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imeamua kujenga uchumi wa viwanda unaotokana na madini kwa kuwekeza katika uchakataji na uyeyushaji wa madini badala ya kuendelea kuuza malighafi.
Amesema kaulimbiu ya mkutano huo, "Madini Yaliyoongezwa Thamani: Chachu ya Ukuaji wa Viwanda na Uchumi," inaakisi dira ya serikali ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchakataji wa madini barani Afrika.
Kwa mujibu wa Mhe. Mavunde, amesema Tanzania tayari ina viwanda vinane vya kusafisha dhahabu, huku Mkoa wa Dodoma ukiwa na viwanda tisa vinavyojengwa na vinavyoendelea na uzalishaji pamoja na kiwanda kikubwa cha kuyeyusha madini ya nikeli na shaba.
"Zaidi ya Sh bilioni 600 zinawekezwa katika ujenzi wa kiwanda cha chuma kitakachotumia asilimia 100 ya malighafi za ndani, huku uwekezaji mwingine ukiendelea Kigamboni na Tanga kwa ajili ya uchakataji wa madini ya 'Heavy Mineral Sands' na mradi wa madini ya niobium wa Panda Hill, Mbeya," amesema Mhe. Mavunde
Amesema, katika kuongeza ushiriki wa Watanzania kwenye sekta hiyo, thamani ya manunuzi kupitia mpango wa 'Local Content' imefikia Sh trilioni 5.1, huku bidhaa 20 zikitakiwa kuzalishwa na wazawa kwa ajili ya kuhudumia migodi mikubwa.
Amesisitiza wafanyabiashara kuzingatia uaminifu na viwango vya kimataifa ili kunufaika zaidi na fursa hizo.
Amesema sekta ya madini imeendelea kuimarisha mchango wake katika uchumi kwa kuingiza Sh trilioni 1.374 katika Mfuko Mkuu wa Serikali, kiwango kilichovuka lengo la Sh trilioni 1.2 kwa mwaka huu wa fedha.
Mhe. Mavunde, amesema Serikali imeidhinisha asilimia 10 ya mapato yote ya sekta ya madini kuelekezwa kwenye utafiti wa kina wa jiofizikia ili kuongeza maeneo yanayofahamika kuwa na madini kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.
Aidha, amesema Serikali inaandaa mfuko maalumu wa mikopo kwa wachimbaji wadogo, ambao licha ya changamoto za mitaji na teknolojia, wanachangia takribani asilimia 40 ya mapato ya sekta ya madini.
Katika hatua nyingine, amesema Serikali inaanza operesheni ya kufuta kidijitali leseni zote za madini zisizotumika. Wamiliki watakaoshindwa kuwasilisha taarifa ndani ya muda uliowekwa watapewa notisi ya siku 30 kabla ya leseni hizo kujifuta moja kwa moja.
Nae, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha utajiri wa madini unakuwa chachu ya kukuza viwanda vya ndani, kuongeza ajira na kuimarisha uchumi kupitia uongezaji thamani badala ya kuishia kwenye uchimbaji pekee.
Amesema TMIC 2026 utawakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za fedha, kampuni za madini, wataalamu wa teknolojia, watafiti na wadau wengine kutoka duniani kote kujadili fursa za uwekezaji na maendeleo ya sekta hiyo.
"Huu ni wakati wa kuingia katika awamu mpya ya uwekezaji, ubunifu na ukuaji wa sekta ya madini nchini," amesema.
Kwa upande wa Katibu Mtendaji wa Chemba ya Migodi Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka, amesema mkutano huo unatarajiwa kuwakutanisha washiriki zaidi ya 2,000 na watoa mada zaidi ya 100 kutoka mataifa zaidi ya 50, huku zaidi ya mada 20 zikijadiliwa zikiwemo sera, kodi, uwekezaji, teknolojia, nishati safi, madini ya kimkakati, uongezaji thamani na masuala ya mazingira, jamii na utawala bora (ESG).
Mchwampaka amesema TMIC 2026 pia utaweka mkazo katika maendeleo ya wachimbaji wadogo pamoja na ushirikishwaji wa wanawake na watu wenye ulemavu katika mnyororo mzima wa uongezaji thamani wa madini. Mkutano huo unatarajiwa kufungwa rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi.



.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)












.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)