
Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma
Wakati Tanzania ikiendelea kukabiliwa na changamoto ya ongezeko la taka ngumu mijini na vijijini, Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha mapato yatokanayo na shughuli za usafi na udhibiti wa taka yanatumika moja kwa moja kuboresha huduma hizo pamoja na kuimarisha mazingira.
Hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi wa ukusanyaji na usimamizi wa taka huku Serikali ikihimiza jamii kuanza kuzitazama taka kama rasilimali yenye thamani ya kiuchumi badala ya mzigo wa mazingira.
Akizungumza leo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe amesema halmashauri zote zinapaswa kutenga na kurejesha asilimia 10 ya mapato yanayotokana na shughuli za udhibiti wa taka ili kuviwezesha vitengo vya usafi wa mazingira kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Mkutano huo umebeba kaulimbiu isemayo “Taka Ngumu ni Mali; Tumia, Rejeleza na Weka Miji Safi.”
Profesa Shemdoe amesema bado hali ya usimamizi wa taka nchini si ya kuridhisha kutokana na baadhi ya halmashauri kushindwa kuwa na maeneo rasmi ya kutupia taka.
Amesema kati ya halmashauri 184 zilizopo nchini, ni halmashauri 43 pekee zenye madampo rasmi, jambo ambalo linaathiri juhudi za usafi wa mazingira na kuongeza hatari ya uchafuzi wa mazingira pamoja na magonjwa ya mlipuko.
“Ni muhimu kuhakikisha taka zinakusanywa na kuhifadhiwa katika maeneo maalum ili kulinda afya za wananchi na kuweka mazingira safi katika miji na makazi yetu,” amesema.
Aidha, ameonya kuhusu tabia ya utupaji holela wa taka kwenye mitaro ya maji, akisema hali hiyo imekuwa chanzo kikubwa cha mafuriko wakati wa mvua kutokana na kuziba kwa mifumo ya maji.
Kwa mujibu wa Profesa Shemdoe, viongozi wa mikoa, wilaya pamoja na serikali za mitaa wanapaswa kuhakikisha suala la usafi wa mazingira linakuwa agenda ya kudumu katika vikao vya maamuzi ili kuongeza uwajibikaji katika jamii.
Katika hatua nyingine, Serikali imehimiza wananchi kuanza kutenganisha taka kuanzia zinakozalishwa ili kurahisisha shughuli za urejelezaji wa plastiki, vyuma, karatasi na taka nyingine zinazoweza kutumika tena.
Amesema mfumo huo utasaidia kuongeza thamani ya taka na kufungua fursa mpya za ajira na biashara kwa wananchi, hususan vijana na wanawake.
“Tunapaswa kubadili mtazamo kuhusu taka. Zinaweza kuwa chanzo kikubwa cha kipato kupitia shughuli za ukusanyaji, uchakataji na urejelezaji,” amesema.
Profesa Shemdoe pia amewataka vijana na wanawake kutumia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kuanzisha miradi ya ukusanyaji na uchakataji wa taka ngumu ili kujiongezea kipato huku wakichangia uhifadhi wa mazingira.
Amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo Japan kutafuta teknolojia za kisasa za uteketezaji na urejelezaji wa taka kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu la usimamizi wa taka nchini.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema Mkoa wa Dodoma umeongeza bajeti ya usafi wa mazingira kutoka Shilingi milioni 750 hadi Shilingi bilioni 3 kwa mwaka wa fedha 2026/27.
Amesema fedha hizo zitatumika kununua vifaa vya usafi, kuboresha ukusanyaji wa taka pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utunzaji wa mazingira.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Mabadiliko ya Tabianchi na Tathmini kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Kanizio Manyika amesema Tanzania huzalisha zaidi ya tani milioni 17 za taka ngumu kila mwaka huku asilimia 60 hadi 75 ya taka hizo zikibaki kwenye mazingira kutokana na kutokusanywa ipasavyo.
Ameonya kuwa hali hiyo ni tishio kwa afya za wananchi na mazingira na kusisitiza umuhimu wa kuwa na mifumo endelevu ya usimamizi wa taka.
Kwa upande wake, mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Joseph Birango amesema takwimu zinaonyesha magonjwa sita kati ya 10 yanayoisumbua jamii yanachangiwa na uchafuzi wa mazingira pamoja na mifumo duni ya usimamizi wa taka.
Awali, Mwenyekiti wa Wakuu wa Vitengo vya Udhibiti wa Taka na Usafi wa Mazingira Tanzania Bara, William Mpangala aliitaka Serikali kutoa maelekezo madhubuti zaidi kwa halmashauri ili kuhakikisha fedha zinazotokana na shughuli za udhibiti wa taka zinarejeshwa kikamilifu katika kuboresha huduma za usafi wa mazingira.



Akizungumza
Mei 12, 2026 katika Kongamano la Kwanza la Kisayansi la Wauguzi
lililoambatana na Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika
katika Hotel Verde Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi alisema Serikali
itaendelea kuwekeza zaidi katika kuboresha huduma za afya ili
kuhakikisha wananchi wanapata matibabu bora na ya kisasa.
Alieleza
kuwa Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya afya
ikiwemo ujenzi wa Hospitali Mpya ya Mnazi Mmoja pamoja na Hospitali ya
Saratani Binguni, sambamba na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa na
kuimarisha mafunzo kwa watumishi wa sekta hiyo.Na Mwandishi Wetu, BRUSSELS
KAMPUNI ya ndege ya Brussels Airlines ya nchini Ubelgiji imeandika historia mpya kwa kutangaza kuanza kwa safari za moja kwa moja kati ya Brussels nchini Belgium na Kilimanjaro International Airport kuanzia Juni 3, 2026.
Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, safari hizo zitafanyika mara mbili kwa wiki, kila Jumatano na Jumamosi, hatua inayotajwa kuwa chachu mpya kwa sekta ya usafiri wa anga, biashara na utalii nchini Tanzania.
Uzinduzi wa safari hizi unaonekana kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Ubelgiji huku ukirahisisha usafiri kwa watalii, wafanyabiashara na wananchi wa pande zote mbili.
Kuanzishwa kwa safari hizi za moja kwa moja kunatarajiwa kuongeza ushindani wa huduma za usafiri wa anga kwa kupunguza muda wa safari na kutoa chaguo zaidi kwa abiria wanaosafiri kati ya Afrika Mashariki na Ulaya.
Aidha, hatua hiyo inatajwa kuwa muhimu katika kukuza biashara ya kimataifa, hasa kwa bidhaa zinazohitaji usafirishaji wa haraka kama matunda, mboga mboga, maua, minofu ya samaki pamoja na bidhaa nyingine zinazouzwa katika masoko ya Ubelgiji na nchi jirani za Ulaya.
Ubelgiji imeendelea kuwa miongoni mwa washirika muhimu wa Tanzania katika biashara ya bidhaa za kilimo na madini, huku ikiwa moja ya nchi chache za Ulaya ambapo thamani ya bidhaa zinazotoka Tanzania kwenda nchini humo ni kubwa kuliko bidhaa zinazoagizwa kutoka huko.
Katika sekta ya utalii, safari hizi mpya zinatarajiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka Ubelgiji na mataifa jirani ya Ulaya wanaotembelea vivutio maarufu vya Tanzania kama Serengeti National Park, Ngorongoro Conservation Area na Mount Kilimanjaro.
Takwimu zinaonesha kuwa idadi ya watalii kutoka Ubelgiji imeongezeka kwa kasi kutoka takribani watalii 9,000 mwaka 2018 hadi zaidi ya 18,000 mwaka 2024, jambo linalodhihirisha kuimarika kwa mahusiano ya watu wa nchi hizo mbili pamoja na kuongezeka kwa hamasa ya kutembelea Tanzania.
Mafanikio haya yanaelezwa kuwa matokeo ya mahusiano ya muda mrefu na ya kirafiki kati ya Tanzania na Ubelgiji yaliyoendelea kuimarishwa chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia diplomasia ya uchumi, maboresho ya sera, uwekezaji katika miundombinu pamoja na mazingira ya amani na utulivu nchini.
Serikali imewataka wafanyabiashara na wadau wa sekta ya utalii kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na safari hizi mpya ili kuongeza na kukuza biashara, uwekezaji na mapato yatokanayo na utalii pamoja na kuimarisha zaidi uhusiano wa Tanzania na mataifa ya Ulaya.

Dar es Salaam, Tanzania — Women leaders, professionals and changemakers
have been urged to embrace continuous learning and digital skills
development in order to remain competitive in today’s rapidly evolving
workplace shaped by artificial intelligence (AI) and digital
transformation.
Speakers at the event
emphasized that the rise of AI and digital technologies is transforming
industries globally, creating both opportunities and challenges for
women. They noted that many working mothers risk being left behind if
they fail to upgrade their skills and embrace innovation-driven careers.

Meanwhile, Founder and CEO of Unleashed Africa Social Enterprises, Khalila Mbowe, highlighted concerns over bias in artificial intelligence systems used in recruitment and promotions. She warned that unless ethical safeguards are introduced, AI could reinforce workplace inequalities instead of eliminating them.
The discussions explored critical issues affecting women in the digital era, including bridging the digital gender gap in AI adoption, ethical leadership, responsible use of technology, and addressing bias in AI-driven recruitment and promotions. Participants also highlighted the importance of adaptability, lifelong learning, networking and mentorship in helping women remain relevant in highly competitive environments.
Founder of HASH Tanzania, Vivian Temi, said the initiative aims to create a supportive community where women can openly discuss challenges facing mothers and caregivers in workplaces increasingly influenced by automation and digital systems.

“We want women to understand that caregiving should never limit their dreams, ambitions or leadership potential. Women deserve opportunities to grow, reskill and thrive while still taking care of their families,” she said.
A fireside discussion featuring Veronica Muumba, Head of Talent Management at CRDB Bank Plc, and moderated by Maureen Njeri, Head of Brand and Marketing at Settlo Technologies Limited, highlighted how institutions can create supportive environments for employees balancing caregiving and career advancement.
The discussion showcased how progressive workplace policies such as flexible working arrangements, mentorship programs, wellness initiatives and digital upskilling opportunities are helping women thrive professionally while maintaining family responsibilities.
Participants also took part in an interactive panel discussion moderated by Lucy Tomeka, featuring Shumbana Walwa of Equity Bank Tanzania, emotional intelligence counselor Ngianasia Marealle Minja and Kai Mollel of Stanbic Bank Tanzania. The panelists shared practical experiences on overcoming workplace barriers, adapting to technological shifts and building sustainable careers while caregiving.
Many attendees called for stronger workplace policies that support women through flexible work arrangements, access to digital training, affordable childcare services and inclusive leadership programs that promote gender equality in decision-making spaces.
The event concluded with a renewed call for governments, private sector institutions and development partners to invest more in women’s digital empowerment and skills development to ensure they fully participate in shaping the future economy.
Participants agreed that empowering women with technology, financial literacy and leadership skills is not only critical for gender equality, but also essential for sustainable social and economic development across Africa in the digital age.



.jpeg)
.jpeg)










.jpeg)


.jpeg)



























