Na Victor Masangu, Pwani

Katibu wa siasa,uenezi na Mafunzi wa chama cha mapinduzi (CCM) Dkt. David Mramba amewaasa wananchi hususan vijana kuwa wazalendo na nchi yao na kuachana kabisa na vitendo vya kutumika kwa maslahi ya makundi ya watu wengine na badala yake kuhakikisha wanaweka misingi ya kuwa walinzi na kudumisha amani.

Dkt. Mramba ameyabainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake kuhusiana na masuala ya wananchi kuwa na jukumu la kulinda amani katika maeneo yao na kuwahimiza wanapaswa kuzingatia katiba na sheria na kutojiingiza katika vitendo ambayo vinaweza kkuhatarisha usalama wa maisha yao

."Suala la amani ni jambo la muhimu sana katika yetu hivyo niwasihi wananchi wote wa Mkoa wa Pwani msikubali hata kidogo kuwashawishi kufanya vitendo vyovyote ambavyo vinaweza kuhatarisha usalma wa maisha , ikiwemo mali pamoja na uchumi wetu kwani amani ni msingi mkubwa wa maendeleo,"amebainisha Dkt. Mramba .

Aidha Katibu huyo amewahimzia wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda watoto wao na kwamba kila kijana anapaswa kufikiria mustakabali wake ikiwa pamoja na kuweza kulinda amani na kuitunza katika maeneo yao wanayoishi.

Pia Katibu huyo amebainisha kwamba Mkoa wa Pwani umebarikiwa kuwa na lango muhimu la uchumi wa Taifa wakiwemo wakulima,wafugaji ,wavuvi, na wafanyabiashara na wawekezaji kwa hiyo kunahitajika kuwa na mazingira mazuri yenye amani na utulivu.

Mramba pia amewaomba wananchi wote wa Mkoa wa Pwani kuendelea kuwa walinzi wa amani na kwamba wanatakiwa kushirikiana bega kwa bega na vyombo vya dola katika kulinda usalama na tuendelee kujenga Tanzania yenye umoja na mshikamano na maendeleo.

Aidha Katiba amebainisha kwamba chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kinampomgeza na kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa mstari wa mbela katika kudumisha hali ya amani na utulivu katika Taifa la Tanzania.


Na. Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Makatibu Wakuu ya Maandalizi ya Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2027), Dkt. Jim Yonazi, amesema michuano ya AFCON ni fursa adhimu ya kuitangaza Tanzania Kimataifa kupitia sekta mbalimbali ikiwemo ya utalii na uwekezaji hivyo ni jukumu la kila sekta kuhakikisha inachangamkia na kushiriki kikamilifu katika kufanikisha michuano hiyo.

Ameyasema hayo hii leo 01 Julai 2026 wakati wa ziara ya Kamati hiyo inayojumuisha Makatibu Wakuu wa kisekta na baadhi ya wakuu wa Taasisi walipotembelea na kukagua maendeleo ya maandalizi kuelekea michuano hiyo ikiwemo kuangalia miundombinu na vituo vya michezo vitakavyotumika katika michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2027) ili kufanikisha mashindano hayo makubwa ya soka barani Afrika.

Katika ziara hiyo, Kamati imekagua maendeleo ya maboresho katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Uwanja wa Mazoezi wa Shule ya Sheria (Law School Grounds), Uwanja wa Mazoezi wa Leaders Club, Uwanja wa Mazoezi wa Gymkhana (Gymkhana Club), Uwanja wa Mazoezi wa Farasi pamoja na Uwanja wa Taifa wa Benjamin Mkapa ili kujionea utayari wa miundombinu itakayotumika wakati wa mashindano hayo.

Dkt. Yonazi amesema ili kufanikisha AFCON 2027 kila sekta inapaswa kuweka nguvu ya pamoja katika kuelekea kwenye michuano hiyo kwa kuzingatia faida zake ikiwemo ya kukuza uchumi wa jamii na Nchi kwa ujumla

"AFCON 2027 ni zaidi ya mashindano ya soka; ni jukwaa la kuitangaza Tanzania Duniani hivyo kila taasisi inapaswa kutekeleza wajibu wake ili kuhakikisha nchi inanufaika ipasavyo na fursa hii," amesema Dkt. Yonazi.

Aidha, ameielekeza Bodi ya Utaliii Tanzania (TTB) kuandaa mkakati mahsusi wa kuitangaza Tanzania kupitia mashindano hayo kwa kuonesha vivutio vya utalii, utamaduni na fursa za uwekezaji kwa wageni watakaofika nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Maendeelo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Boniface Tamba, amesema maboresho ya miundombinu yanaendelea vizuri na kwamba ujenzi wa barabara zinazoingia na kutoka katika vituo pamoja na viwanja vya michezo umefikia hatua za mwisho za ukamilishaji.

"Maandalizi yanaendelea kwa kasi na miundombinu muhimu ipo katika hatua za mwisho ili kuhakikisha Tanzania inakuwa tayari kuandaa AFCON 2027 kwa viwango vinavyotakiwa," amesema Bw. Tamba.

Kamati ya Makatibu Wakuu inaendelea na ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya AFCON 2027, ambapo baada ya kukamilisha ukaguzi katika Mkoa wa Dar es Salaam itatembelea Zanzibar kabla ya kuhitimisha ziara hiyo itatembelea katika viwanja vilivyopo Jijini Arusha.














Na Mwandishi Wetu.
SERIKALI imeimarisha kwa kiwango kikubwa ufuatiliaji katika mipaka, vituo vya kuingilia nchini na mfumo mzima wa huduma za afya ili kuzuia ugonjwa wa Ebola kuingia nchini kutoka mataifa jirani.

Akizungumza katika semina ya wanahabari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji wa Afya kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Rahma Hingora, alisema kuwa licha ya Tanzania kutokuwa na kisa chochote cha Ebola, ufuatiliaji umeimarishwa katika vituo vyote vya mipakani, viwanja vya ndege, bandari na vituo vikuu vya usafiri.

"Ingawa Tanzania haina mlipuko wa Ebola kwa sasa, hatuchukulii jambo hili kwa uzembe," alisema Dkt. Hingora.

"Tunaendelea kuimarisha maandalizi ya dharura, kuongeza uwezo wa wahudumu wa afya na kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa ili kulinda taifa."
Dkt. Hingora alisisitiza kuwa utoaji wa taarifa sahihi na kwa wakati ni muhimu sawa na maandalizi ya kitabibu, akionya kuwa uvumi na taarifa potofu husababisha hofu, hupunguza imani ya wananchi kwa mamlaka za afya na kudhoofisha juhudi za kukabiliana na milipuko.

Aliwataka wanahabari kuripoti kwa uwajibikaji kwa kutumia taarifa zilizothibitishwa kutoka vyanzo rasmi, akieleza kuwa vyombo vya habari ni washirika muhimu katika kulinda afya ya umma.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Mkuu wa Kitengo cha Mabadiliko ya Kijamii na Tabia wa UNICEF Tanzania, Dkt. Awete Araya, ambaye alikumbusha mafunzo yaliyopatikana kutokana na milipuko ya Ebola iliyowahi kutokea Afrika Magharibi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

"Silaha yenye nguvu zaidi katika maandalizi dhidi ya Ebola ni taarifa zinazoaminika," alisema Dkt. Araya mbele ya wanahabari na washawishi wa mitandao ya kijamii.

"Jamii huchukua hatua kulingana na kile wanachosikia, wanachoamini na wanachokiona kwenye mitandao ya kijamii. Ninyi si watazamaji tu, bali ni wahusika wa mstari wa mbele katika kukabiliana na dharura za afya."

Alionya kuwa taarifa za uongo zinaweza kuzifanya familia kuficha wagonjwa na kupoteza imani kwa mamlaka za afya, jambo linaloweza kuchelewesha hatua muhimu za kuokoa maisha.

Dkt. Araya alisema UNICEF itaendelea kuisaidia Tanzania katika mawasiliano ya hatari, ushirikishwaji wa jamii, udhibiti wa maambukizi pamoja na kuboresha huduma za maji, usafi na mazingira, huku watoto walio katika mazingira hatarishi wakiendelea kuwa kipaumbele katika mwitikio wa dharura.

Kwa upande wa utekelezaji, hatua za ulinzi tayari zimeanza kutekelezwa.
Ofisa Mkuu wa Afya wa Bandari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dkt. Mustapha Mpagama, alisema mamlaka zimeweka vifaa vya kisasa vya kupima joto la mwili katika maeneo ya kuingilia nchini na kutoa mafunzo maalumu kwa wahudumu wa afya wanaofanya kazi mipakani.

Aidha, alisema ongezeko la watu wanaovuka mipaka limeifanya Serikali kuimarisha zaidi hatua za kujikinga dhidi ya kuenea kwa ugonjwa huo.

Alieleza kuwa usafiri wa anga, barabara, usafirishaji wa mizigo na biashara za mipakani ni miongoni mwa njia zinazoweza kuchangia kusambaa kwa magonjwa ya mlipuko ikiwa tahadhari hazitachukuliwa.

Washiriki wa semina walikubaliana kuoanisha njia za mawasiliano ili kuhakikisha kuwa tishio lolote la kiafya katika ukanda huu linakabiliwa kwa kutoa elimu ya haraka, sahihi na inayozingatia ukweli.

Kwa sasa Tanzania inaendelea kubaki huru dhidi ya Ebola bila kuwa na kisa chochote kilichothibitishwa nchini.

Hata hivyo, kutokana na milipuko inayoendelea katika nchi jirani kama Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Wizara ya Afya imeendelea kuimarisha ufuatiliaji, uchunguzi wa wasafiri mipakani pamoja na hatua nyingine za kinga katika vituo vyote vya kuingilia nchini.





Antonia Nsimbi akionesha Shati alilotengeneza kwa kutuma Maganda ya Parachichi.
Antonia Nsimbi akionesha Shati alilotengeneza kwa kutuma Maganda ya Vitunguu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MHITIMU wa Chuo Kikuu cha Saint Augustine cha Mwanza, Antonia Nsimbi, amefanikiwa kujiajiri baada ya kupata mafunzo ya ufundi stadi katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA), ambapo sasa anatengeneza mavazi ya ubunifu kwa kutumia maganda ya parachichi, vitunguu na madafu kama malighafi.

Akizungumza katika banda la VETA kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam, Antonia alisema baada ya kuhitimu elimu ya chuo kikuu alikaa kwa muda akisaka ajira bila mafanikio, jambo lililomsukuma kutafuta ujuzi wa kujiajiri kupitia VETA.

Alisema mafunzo aliyoyapata yalimwezesha kubuni teknolojia ya kuchakata maganda ya parachichi, vitunguu na madafu na kuyatumia kutengeneza mavazi ya kipekee ambayo kwa sasa yanapata soko kutokana na ubunifu wake na matumizi ya malighafi rafiki kwa mazingira.

"Nilipoanza haikuwa rahisi, lakini kwa sasa naona matunda ya ubunifu huu. Wateja wanapenda bidhaa hizi kwa sababu ni tofauti na zinatengenezwa kwa kutumia malighafi ambazo wengi hawakudhani zinaweza kutumika kutengeneza mavazi," alisema Antonia

Antonia aliwahimiza vijana kuacha kusubiri ajira za kuajiriwa pekee na badala yake kutumia fursa zinazotolewa na VETA kupata ujuzi unaowawezesha kujiajiri na kuanzisha biashara zinazokidhi mahitaji ya soko.

Alisema changamoto ya ajira inaweza kupunguzwa endapo vijana wataamua kuwekeza katika ubunifu na ujuzi wa vitendo, akibainisha kuwa vyuo vya VETA vina mchango mkubwa katika kuwawezesha wahitimu kujenga maisha yao kupitia shughuli za uzalishaji.

Aidha, alieleza kuwa kusubiri ajira serikalini au sekta binafsi kunaweza kuchukua muda mrefu kutokana na idadi kubwa ya wahitaji wa ajira ikilinganishwa na nafasi zinazopatikana, hivyo akasisitiza umuhimu wa kujiajiri kwa kutumia ujuzi unaopatikana kupitia mafunzo ya ufundi stadi.
Na Mwandishi Wetu

UTEKELEZWAJI wa Sera ya Taifa ya Uchumi wa Buluu umetajwa kuwa lango kuu la uchumi kutokana na fursa mbalimbali zinazopatikana katika sekta hiyo. Sekta ya uchumi wa buluu inahusisha mambo sita ambayo ni uvuvi, usafirishaji, utalii, gesi, petrol na umwagiliaji.

Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Uchumi wa Buluu na Uratibu Ofisi ya Makamu wa Rais, Magdalena Ngotolainyo, amesema hayo Juni 30, 2026 wakati akizungumzia uchumi wa buluu.

Alisema Tanzania ni nchi iliyobarikiwa si kwa ardhi yenye rutuba pekee, wala si kwa madini, wanyamapori na vivutio vya utalii pekee, bali pia kwa utajiri mkubwa uliomo ndani ya maji yake. Bahari, maziwa, mito, mabwawa, maeneo oevu, maji chini ya ardhi na ukanda mpana wa pwani ni hazina ya kipekee ambayo, ikitumika kwa maarifa na uendelevu, inaweza kuwa injini mpya ya mageuzi ya kiuchumi na ustawi wa wananchi. Hii ndiyo nguvu ya Uchumi wa Buluu.

Alisema uchumi wa buluu unahusisha matumizi endelevu ya rasilimali zinazopatikana katika bahari, maziwa, mito, mabonde ya maji, maeneo oevu na maji yaliyo chini ya ardhi kwa ajili ya kukuza uchumi, kuboresha maisha ya jamii na kulinda mazingira. Kwa Tanzania, dhana hii si nadharia ya mbali.

"Ni uhalisia unaoonekana katika kila pembe ya nchi: kuanzia Bahari ya Hindi hadi Ziwa Victoria, kutoka Ziwa Tanganyika hadi Ziwa Nyasa, na kutoka mito mikubwa hadi ukanda wa pwani wenye fursa zisizohesabika," alisema.

Aidha, alisema kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Uchumi wa Buluu ya mwaka 2024, Tanzania ina rasilimali kubwa za maji zinazoweza kuwa msingi imara wa maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kimazingira. 

Tanzania ina takribani kilomita za mraba 61,500 za maeneo ya maji baridi yanayofaa kwa matumizi mbalimbali, yanayokadiriwa kuwa na mita za ujazo bilioni 126 kwa mwaka. Aidha, Tanzania ina kilomita za mraba 64,000 za maji ya kitaifa katika bahari na kilomita za mraba 223,000 za Ukanda Maalumu wa Uchumi wa Bahari.

"Haya si maeneo ya kijiografia tu; ni maeneo ya fursa, ajira, uwekezaji na maendeleo," alisema.

Aidha, alisema ukanda wa pwani wa Tanzania wenye urefu wa kilomita 1,424 ni lango muhimu la uchumi wa taifa. Pwani hii inawezesha shughuli za uvuvi, usafirishaji wa baharini, utalii wa fukwe, ukuzaji wa viumbe maji, uhifadhi wa mazingira na biashara ya kimataifa. Alisema bandari rasmi 86 na zisizo rasmi 885 zilizopo nchini zinaonesha namna Tanzania ilivyo na nafasi kubwa ya kuwa kitovu cha usafirishaji na biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na nchi jirani zisizo na bahari.
Magdalena Ngotolainyo , Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Uchumi wa Buluu Katoka Ofisi ya Makamu wa Rais







Na Oscar Assenga, Tanga

WAZIRI wa Nishati, Dkt. Deogratius Ndejembi, amesema ujenzi wa Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) umefikia asilimia 86, huku mafuta ya kwanza yakitarajiwa kupokelewa katika Kituo cha Chongoleani, Tanga, na kusafirishwa Januari mwaka 2027.

Dkt. Ndejembi alisema hayo leo baada ya kutembelea eneo la mradi Chongoleani, mkoani Tanga, kujionea maendeleo ya utekelezaji wake, ambapo alieleza kuwa matarajio ni kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwisho wa Agosti mwaka huu.

Alisema kazi nyingi muhimu zimekamilika na kilichobaki ni hatua za mwisho ikiwemo kukamilisha miundombinu ya umeme ili kuwezesha mitambo ya kusukuma mafuta kufanya kazi.

"Nimefurahishwa na maendeleo ya mradi. Kazi kubwa imefanyika na tunaamini ifikapo mwisho wa Agosti ujenzi utakuwa umekamilika. Ratiba inaonyesha kuwa meli ya kwanza itachukua mafuta ghafi kutoka Chongoleani mwezi Januari, 2027," alisema.

Hata hivyo, alisema changamoto iliyobaki ni kukamilika kwa njia ya umeme kutoka Majani Mapana kuelekea eneo la mradi, huku akiutaka mkandarasi anayetekeleza kazi hiyo chini ya Tanesco kuhakikisha anakamilisha mradi huo kwa wakati.

Alionya kuwa mkandarasi atakayeshindwa kutekeleza kazi hiyo ndani ya muda uliopangwa atachukuliwa hatua, ikiwemo kuondolewa katika orodha ya wakandarasi wanaofanya kazi na Tanesco.

Dkt. Ndejembi alisema EACOP ni mradi wa kimkakati kwa Tanzania, Uganda na ukanda mzima wa Afrika Mashariki, akibainisha kuwa bomba hilo lenye urefu wa zaidi ya kilomita 1,400 ni la kwanza duniani lenye mfumo wa kupashwa joto katika urefu wake wote.

Alisema Serikali ya Tanzania imewekeza zaidi ya Sh bilioni 973 kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), ambalo linamiliki asilimia 15 ya hisa za mradi huo kwa kushirikiana na kampuni za UNOC, TotalEnergies na CNOOC.

Aidha, aliwataka Watanzania kuendelea kutumia fursa zinazotokana na mradi huo, akieleza kuwa zaidi ya Watanzania 3,000 wamepata ajira za moja kwa moja, huku vijana wengine zaidi ya 100 wakipelekwa Madimba kwa mafunzo ya kuongeza ujuzi kabla ya kuajiriwa.

Aliongeza kuwa zaidi ya vijana 400 kutoka Chongoleani wamepatiwa mafunzo na kuajiriwa katika maeneo mbalimbali ya mradi huo, huku fursa nyingine nyingi zikiendelea kujitokeza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, alisema mradi huo umeendelea kuleta manufaa makubwa kwa mkoa huo kupitia ongezeko la shughuli za Bandari ya Tanga, mapato ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na fursa za ajira kwa wananchi.

Alisema vifaa vingi vya mradi vimepitia Bandari ya Tanga kabla ya kusafirishwa katika maeneo mbalimbali ya utekelezaji wa bomba hilo, jambo lililochochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi.

Balozi Burian alisema pia mradi huo umezingatia viwango vya kimataifa vya utunzaji wa mazingira, akieleza kuwa shughuli za uvuvi zinaendelea kama kawaida na hakuna viumbe hai walioathirika kutokana na ujenzi wa gati na miundombinu mingine.

Aliongeza kuwa kupitia mradi huo, Halmashauri na jamii zinazozunguka eneo la mradi zimenufaika na miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa uwanja wa mpira unaotumiwa na klabu ya Coastal Union.

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Huduma za Mradi wa EACOP, Jofrey Mponda, ambaye pia alizungumza kwa niaba ya uongozi wa EACOP Tanzania, alisema mradi umefikia hatua za mwisho za utekelezaji, huku zaidi ya asilimia 90 ya kazi ikiwa imekamilika.

Alisema mradi huo unaounganisha mikoa 18 ya Tanzania na wilaya 27 umeingia katika hatua ya ukaguzi na makabidhiano ya mifumo mbalimbali, ikiwemo vituo vya kusukuma mafuta, matenki ya kuhifadhi mafuta na miundombinu mingine muhimu.

Mponda alisema pampu sita za kusukuma mafuta zimejengwa, mbili zikiwa nchini Uganda na nne nchini Tanzania, huku pampu mbili za kupunguza shinikizo la mafuta zikiwa Chongoleani.

Alibainisha kuwa matenki manne ya kupokelea mafuta tayari yamekamilika, huku kazi iliyobaki ikiwa ni kuunganisha mfumo wa umeme ili kuwezesha mitambo yote kuanza kufanya kazi kwa wakati.

Alisema EACOP inaendelea kushirikiana kwa karibu na Tanesco kuhakikisha miundombinu ya umeme inakamilika ifikapo Septemba mwaka huu, hatua itakayowezesha maandalizi ya kupokea mafuta ya kwanza mwezi Januari, 2027.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Christine Grau, Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, katika Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yamefanyika Juni 30,2026, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kumuaga Balozi Grau anayehitimisha kipindi chake cha uwakilishi nchini Tanzania. Viongozi hao walitathmini ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya na kujadili namna ya kuuendeleza kwa manufaa ya pande zote mbili.

Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu umuhimu wa kuimarisha misingi ya utawala bora, amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa kama nguzo ya maendeleo endelevu ya Taifa. Katika muktadha huo, CCM ilisisitiza dhamira yake ya kuendelea kujenga Taifa linaloongozwa kwa misingi ya haki, uwajibikaji na utulivu wa kisiasa.

Pia, ilitambua changamoto zilizojitokeza nchini katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu uliopita na umuhimu wa hatua ambazo Serikali inaendelea kuzichukua katika kuimarisha imani ya wananchi, ikiwemo kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi, Tume ya Upelelezi wa Jinai na hatua nyingine za kisheria zinazolenga kuhakikisha ukweli, uwajibikaji na haki vinaendelea kutawala katika kulinda amani na mshikamano wa Taifa.

Aidha, ilielezwa kuwa ajenda ya kuendelea kuimarisha demokrasia nchini, ikiwemo mchakato wa Katiba Mpya ambao umeainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, inabaki kuwa sehemu muhimu ya maono ya muda mrefu ya kuimarisha utawala bora na mshikamano wa Taifa.

Viongozi hao pia walitambua nafasi ya vijana katika mustakabali wa maendeleo ya Tanzania na umuhimu wa kuhakikisha kizazi hicho kinaendelea kuwa sehemu ya safari ya Taifa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na ujenzi wa uchumi wenye ushindani na maendeleo jumuishi.

CCM inathamini ushirikiano wake na Umoja wa Ulaya na inaamini kuwa ushirikiano huo utaendelea kuimarika kwa kuzingatia misingi ya kuheshimiana, maslahi ya pamoja na dhamira ya pamoja ya kuendeleza maendeleo endelevu ya Tanzania.







 
Perhaps no decision is as critical for a trader as choosing a reliable broker. A good broker will provide you with the necessary conditions for your success, while a dishonest one may steal all your money.


With the popularity of Forex trading in Africa, the number of dishonest brokers has also increased, and this decision has never been so critical. Here are 10 factors that will help you make an informed decision and find a reliable platform.


1. Regulation and Licensing

In Africa, local regulators include the FSCA (South Africa) and CMA (Kenya). However, many well-known brokers are also licensed by international regulators, such as CySEC (Cyprus) and the FCA (UK), or other reputable regulators. 

 

If a broker is not regulated or does not display its license clearly, it is a bad sign. 


2. Transparency of Company Information

A reliable broker will always be transparent about its activities, business, and background. You should be able to find all the necessary information regarding the company, including where they are registered, where they are based, legal documents such as Terms and Conditions, Risk Disclosure, etc.

 

Be careful of brokers that do not provide clear, transparent, and consistent information.


3. Segregation of Client Funds

A trustworthy broker will always keep your funds separate from the company's funds. This means that it will not be able to use your funds for its own expenses, and your funds will not be compromised even if the company is facing financial problems.


4. Trading Conditions and Costs

Ensure that your broker clearly states that they keep client funds in separate accounts.

Beware of promises that sound too good to be true. If a broker promises you guaranteed profits, "zero risk" trading, or extremely high returns, it is most likely a scam.

 

Instead, look for reasonable and competitive trading conditions such as low spreads, transparent commissions, fast execution, and no hidden fees. A reliable broker should clearly explain their trading fees.

5. Deposit and Withdrawal Process

One of the best ways to detect a bad broker is to test their withdrawal process. A reputable provider should offer several ways to deposit and withdraw money, such as bank transfer, country-specific payment systems, and e-wallets. This should be possible without any “hidden conditions.”

 

If it is difficult or slow to withdraw money, this is a red flag.


6. Reliability of the Trading Platform

The trading platform should be stable, fast, and user-friendly. Most brokers offer such platforms as MetaTrader 4 (MT4) or MetaTrader 5 (MT5).

 

Beware of a platform that crashes or freezes frequently. Also, check the execution speed and accuracy of the price feeds. Bad tools can cost you money, regardless of how skilled a trader you are. 

7. Support You Can Count On

When things go wrong with your trade, you need someone to answer. Brokers that are available 24/5 or 24/7, answer quickly, and provide accurate information instead of copy-paste answers are a good choice. 

 

It also matters that support is available in your local language. JustMarkets, for example, offers support in 23 languages. 

 

Before depositing money, test the support first. If it's bad before you deposit, it'll only get worse after.


8. Local Presence and Payment Options

Local support is important to traders from Africa. Brokers with knowledge of the region can provide region-specific deposit and withdrawal methods, as well as education. This makes trading more convenient for users and saves them money on fees.


9. Educational Resources

Brokers that offer webinars, analysis, tutorials, and guides are, at the very least, the ones that care about you not blowing your account on day one. Services that focus solely on promotions and bonuses should be taken with a grain of salt.


10. Traders' Reviews

Testimonials on the broker's site are always glowing and positive, with no guarantee that the company did not write them themselves. Therefore, check reviews from real traders on trustworthy websites such as Trustpilot.

 

While no broker is perfect, if you start to see a pattern with negative reviews, then you should probably stay away.


Before You Start Trading

First off, check their site for regulatory compliance, transparency, reliable withdrawal methods, and customer support. Also, stay away from brokers who guarantee you profits or try to conceal information from you. A good broker will never promise you the world but will instead provide you with a safe platform for you to trade on.

 

JustMarkets checks all 10 of the boxes mentioned above

It holds regulatory licenses from FSA (Seychelles), FSC (Mauritius), FSCA (South Africa), FSC (BVI), and CySEC (Cyprus), keeps client funds in segregated accounts, runs an educational library on its website, offers support in 23 languages, and strives to provide the best possible trading conditions. 

 

Risk Warning: Trading financial instruments involves significant risk and may not be suitable for all investors. Market conditions can change rapidly, and losses may exceed deposits. Ensure you understand the risks involved and trade responsibly.

 



Maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba aliyoyatoa wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani Ikungi na katika Manispaa ya Singida Juni 27, 2026 ya kusikiliza na kusuluhisha migogoro ya ardhi iliyopo mkoani humo yameanza kutekelezwa leo Juni 30, 2026.

Viongozi na watendaji wa mkoa wa Singida na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakishirikiana na Timu ya Watalaamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu walikusanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kusuluhisha migogoro ya ardhi ya mamia ya mwananchi waliojitokeza wakiwa na vielelezo mbalimbali.

Akizungumza Mkuu wa wilaya ya Singida alimshukuru Kamishina wa Ardhi, Nathaniel Mathew Nhonge kwa kujitoa kwa moyo kutatua migogoro ya ardhi mkoa wa Singida kama ilivyoelekezwa na Waziri Mkuu.

Zoezi hilo limekadiriwa kuendeshwa kwa siku nne ili kuhakikisha kwamba kila mwananchi aliyejitokeza anasikilizwa na suala lake linafanyiwa kazi.

Mkuuwa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, Kamishina wa Ardhi, Nathaniel Mathew Nhonge na Mkuu wa wilaya ya Singida Godwin Gondwe ni miongoni mwa viongozi walioongoza usuluhishi huo.






Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya biashara, uwekezaji na viwanda kwa kufanya mageuzi ya sera, sheria, kanuni na mifumo ya utoaji huduma ili kuiwezesha sekta binafsi kuwa mhimili wa ukuaji wa uchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Amesema hayo leo, Jumanne Juni 30, 2026, alipokuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Mwaka 2026 lililoandaliwa na Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) katika Hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema Serikali imejipanga kuhama kutoka katika mfumo wa kudhibiti biashara kwenda katika mfumo wa kuwezesha biashara kwa kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji, kupunguza urasimu, kuimarisha matumizi ya teknolojia na kuongeza ufanisi wa taasisi zinazotoa huduma kwa wafanyabiashara na wawekezaji.

"Ajenda ya sekta binafsi ni ajenda ya Taifa. Hatuwezi kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 bila sekta binafsi yenye nguvu, inayowezeshwa na inayoshirikiana kwa karibu na Serikali," amesema.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kupokea na kufanyia kazi mapendekezo ya sekta binafsi yanayolenga kuboresha mazingira ya biashara, kuondoa vikwazo vinavyokwamisha uwekezaji na kuongeza ushindani wa bidhaa na huduma za Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Waziri Mkuu amesema amani, utulivu na mshikamano wa Taifa ni msingi muhimu wa maendeleo ya uchumi, hivyo kila Mtanzania ana wajibu wa kuendelea kuvilinda ili kuwezesha biashara, uwekezaji na uzalishaji kustawi.

Awali, Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga alisema Serikali inaendelea kujenga mazingira rafiki ya biashara kwa kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, kukuza matumizi ya teknolojia na kuhakikisha taasisi za umma zinafanya kazi kwa mtazamo wa kuwezesha biashara badala ya kuzikwamisha.

Kwa upande wake, Rais wa Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC), Bw. Vincent Minja alisema chemba hiyo imeendelea kufanya mageuzi ya kiutawala na kidijitali yanayolenga kuboresha huduma kwa wanachama, kuimarisha uwakilishi wa sekta binafsi na kuongeza ushindani wa biashara za Tanzania.

Katika kongamano hilo, Waziri Mkuu alizindua rasmi Mfumo wa Kidijitali wa Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania, utakaorahisisha utoaji wa huduma mbalimbali za chemba hiyo, ikiwemo usajili wa wanachama, utoaji wa vyeti vya asili ya bidhaa na huduma nyingine za biashara kwa njia ya mtandao.

Aidha, alishuhudia utiaji saini wa hati mbalimbali za makubaliano ya ushirikiano kati ya Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania na taasisi za umma pamoja na sekta binafsi, hatua inayolenga kuimarisha biashara, uwekezaji, utafiti, ubunifu na maendeleo ya sekta binafsi nchini.

Kongamano hilo lilihudhuriwa na viongozi wa Serikali, taasisi za umma, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, mabalozi, wawekezaji na wafanyabiashara kutoka ndani na nje ya nchi.






Top News