Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani imekamata bidhaa mbalimbali za magendo katika Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo viroba 50 vya mchele, madumu 10 ya mafuta ya kula na sabuni box 25 aina ya Malaika.

Kwa mujibu wa Meneja Msaidizi wa Forodha mkoa wa Pwani Bi. Melinda Matinyi bidhaa hizo za magendo zimekamatwa Machi 19.2026 kufuatia operesheni ya udhibiti wa bidhaa zinazoingizwa nchini au kusafirishwa bila kufuata taratibu za kisheria za forodha.

Amesema idhaa zilizokamatwa zimehifadhiwa katika yadi ya TRA Bagamoyo kwa ajili ya kuendelea na taratibu za kiforodha na hatua nyingine za kisheria.

Mamlaka ya Mapato Tanzania imeendelea kutoa wito kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kufuata sheria na taratibu za kodi na forodha ili kuepuka hasara na adhabu zinazoweza kujitokeza pindi wanapojihusisha na vitendohivyo.


 

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

TUME ya Ushindani (FCC) kanda ya Nyanda za Juu Kusini  imetoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa mpana ili waweze kufanya maamuzi sahihi wanaponunua na kutumia bidhaa mbalimbali  ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Akitoa elimu hiyo Mkoani Njombe, Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) Nyanda za Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga, amesisitiza umuhimu wa kila mlaji kufahamu haki zake za msingi.alieza kuwa haki hizo ni pamoja na kupata bidhaa bora, kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa, pamoja na haki ya kulalamika pale mlaji anapodhulumiwa.

Aidha, Bw. Mbanga ameeleza madhara makubwa yatokanayo na matumizi ya bidhaa bandia, akibainisha kuwa bidhaa hizo zinaweza kusababisha athari za kiafya, kupoteza fedha, na kudhoofisha uchumi wa nchi. Amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii zao ili kupunguza matumizi ya bidhaa hizo hatarishi.

“FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi.”amesema Bw. Mbanga

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameacha alama chanya kwa wanafunzi wa FDC Njombe, ambapo wengi wao wameeleza kuwa elimu hiyo imewafungua macho na kuwapa nguvu ya kusimamia haki zao kama walaji, huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia nchini.

Kupitia mafunzo hayo, walikumbushwa kuwa mlaji ana nafasi kubwa katika kulinda afya yake na uchumi wa taifa kwa kuchagua bidhaa zilizo salama na zenye ubora unaokubalika.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) Mkoani Njombe wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia yaliyotolewa  na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.


Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Ndugu Bakari Machumu akiwa kwenye picha na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Ndugu Gerson Msigwa katika Ofisi ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Machi, 2026.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Ndugu Bakari Machumu akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Ndugu Gerson Msigwa katika Ofisi ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Machi, 2026.
▫️Hatua kubwa kwa maendeleo ya Ngumi Kimataifa

20-03-2026 - Dar es Salaam.
SHIRIKISHO la Ngumi Tanzania (BFT) linapenda kuutaarifu umma na wadau wa mchezo wa ngumi kuwa Tanzania imekuwa rasmi mwanachama wa World Boxing, Shirikisho la Kimataifa la Ngumi linalotambuliwa na Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC).

Uamuzi wa kuipokea Tanzania ulifikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya World Boxing kilichofanyika tarehe 15-03-2026, ambapo Tanzania iliungana na mataifa mengine nane yaliyopitishwa kuwa wanachama wapya.

Mataifa hayo ni Zambia, Msumbiji, Urusi, Tonga, Cyprus, Belarus, Niue na Papua New Guinea.

Kwa uamuzi huo, World Boxing sasa ina jumla ya wanachama 168 duniani, hatua inayoendelea kuimarisha ukuaji na usimamizi wa mchezo wa ngumi kimataifa.

World Boxing imepewa dhamana na Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC) kusimamia na kuratibu mashindano ya ngumi katika matukio makubwa ya kimataifa, ikiwemo Michezo ya Olimpiki, Michezo ya Jumuiya ya Madola, pamoja na Michezo ya Kimabara kama African Games.

Akizungumzia mafanikio hayo, Rais wa Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT), Ndg. Lukelo Willilo, amesema:

“Kupatikana kwa uanachama wa World Boxing ni hatua muhimu na ya kihistoria kwa maendeleo ya ngumi nchini Tanzania. Fursa hii itawawezesha mabondia wetu kushiriki kikamilifu katika mashindano ya kimataifa na kuongeza ushindani pamoja na viwango vyao. Tunaendelea kujipanga kuhakikisha Tanzania inanufaika ipasavyo na uanachama huu.”

Kupatikana kwa uanachama huu ni hatua muhimu kwa maendeleo ya mchezo wa ngumi nchini Tanzania, kwani utafungua fursa zaidi kwa mabondia kushiriki mashindano ya kimataifa na kukuza viwango vya ushindani.

 Na MWANDISHI WETU


NAIBU Kadhi Mkuu Sheikh Khamis Ngeruko, amevitaka vituo vya kulea yatima nchini kuto kufuga watoto hao badala yake wawalee na kuwakuza katika maadili mema.

Ameyasema hayo Dar es Salaam katika futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Yono Auction Mart katika Kituo cha Kulea Yatima cha Mwana, kilichopo Vingunguti, juzi.

Akizungumza kwa niaba ya Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dk. Aboubakar Zubeir, Naibu Kadhi Sheikh Ngeruko, ameeleza vipo vituo vinavyo ishi na yatima kwa mfumo wa kuwafuga hali ambayo haiwakuzi katika njia inayo paswa.

“Yatima anatakiwa kulelewa siyo kufugwa. Alelewe kama mtata anaye lelewa akiwa nyumbani. Apewe mahitaji yote muhimu hususan elimu dunia na elimu ahera kulingana na imani ya mtoto,”alieleza Sheikh Ngeruko.

“Nataka tuandae semina itakayo washirikisha watu wanaoendesha vituo hivi vya kulea watoto. Tuwape elimu hii ya kuto kuwa fuga badala yake wawalee ili baada ya kukua wajitegemee kimaisha na kuwa na maadili mema,”alisema.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Yono Auction Mart, Stanley Kevela, alisema wataendeleza utamaduni wa kusaidia makundi yenye mahitaji maalumu hususan kutoa sadaka kwa yatima kwani hata vitabu vitakatifu vimeelekeza hilo.

Makamu Mkurugenzi Mkuu wa Yono Auction Mart, Dk.Scolastica Kevela, alikemea vikali wanawake wanao tupa watoto baada ya kujifungua na kuitaka jamii kulaani vitendo hivyo.

Dk. Scolastica ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Njombe, alimpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kitendo cha kishujaa cha kumwasili mtoto mchanga hivi karibuni.

“Tunamshukuru Rais Dk. Samia kwa kitendo hicho kinacho thibitisha, upendo na kujali malezi ya watoto. Nikiwa mmoja wa wanawake wanao kemea ukatili na toa wito kwa jamii kusimamia malezi ya watoto wetu,”alisema.

Alieleza,kampuni yake itaendelea na utamaduni wa kutoa gawio kwa jamii hususan wenye mahitaji maalumu, kushiriki shughuli za maendeleo kuunga mkono jitihada za Rais Dk. Samia.

“Wito wangu kwa jamii. Kama umeajaaliwa kipato toa kiasi kwa jamii hasa watoto hawa wenye mahitaji maalumu. Mungu atakubariki kwani mali na fedha vyote tutaviacha hapa duniani,”alisema Dk. Kevela.

Uongozi wa Kituo cha Mwana ulishukuru wadau hao kuwakumbuka watoto katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuomba jamii kuendelea kusaidia kituo hicho chenye watoto 55 wa jinsia na rika mbalimbali.






Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Jimbo la Mbarali, Bahati Ndingo, amesema ataongoza jimbo hilo kwa kusikiliza wananchi na kuwasemea katika vyombo vya maamuzi ili kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili.

Akizungumza katika mahojiano na mwandishi, Ndingo alisema katika kipindi chake cha ubunge atakuwa daraja kati ya wananchi na Serikali kwa kuhakikisha maoni, ushauri na mapendekezo yao yanapelekwa kwenye hatua za utekelezaji.

Alisema dhamira yake ni kufuatilia kwa karibu masuala muhimu ya maendeleo ya jimbo hilo, hususan kwa kuibua hoja na kuzifikisha bungeni ili zipatiwe ufumbuzi kwa manufaa ya wananchi wa Mbarali.

“Ubunge wangu huu nitakuwa daraja la wananchi wangu, kuwasikiliza kwa yale wanayonishauri na kuyapeleka katika hatua za utekelezaji huku nikifuatilia zaidi,” alisema Ndingo.

Mbunge huyo alisema Mbarali ni miongoni mwa maeneo yanayotegemea zaidi uchumi wa kilimo, hasa zao la mpunga, hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kuboresha miundombinu ya barabara ili kurahisisha usafirishaji na shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi.

Alieleza kuwa kipindi cha masika kimesababisha baadhi ya barabara kuharibika, jambo ambalo limeathiri mawasiliano kati ya maeneo mbalimbali ya jimbo hilo. Hata hivyo, alisema matarajio ni kwamba Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) utaanza kazi ya kurekebisha miundombinu hiyo mara baada ya mvua kupungua.

Ndingo pia alisema amejiwekea dhamira ya kutumia nafasi yake katika Bunge lijalo kutoa mchango mkubwa zaidi kwa maendeleo ya wananchi wa Mbarali, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Aidha, alisema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ina nia ya dhati ya kuwahudumia wananchi, na kwamba yeye kama mbunge anao wajibu wa kuunga mkono jitihada hizo kwa kutoa ushauri na mchango unaolenga kuharakisha maendeleo ya jimbo hilo.

Kwa upande mwingine, aliwataka wananchi wa Mbarali kuwa na umoja na kuzungumza lugha moja yenye lengo la kujenga jimbo lao kwa pamoja, akisisitiza kuwa maendeleo ya kweli yanahitaji mshikamano na ushirikiano kutoka kwa kila mmoja.

Alisema kwa ushirikiano huo, Mbarali inaweza kufikia maendeleo yanayoonekana na kuwanufaisha wananchi wake katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, ametembelea Bandari ya Durban iliyopo nchini Afrika Kusini, kwaajili ya kujionea utendaji na uwekezaji mkubwa katika bandari hiyo inayohesabika miongoni mwa bandari kuu za kontena barani Afrika.

Bandari ya Durban ina jumla ya gati 58 zinazohudumia aina mbalimbali za mizigo ikiwemo makasha (containers), magari, mizigo ya kawaida (break bulk), mizigo mikavu (dry bulk), pamoja na abiria. Kwa mwaka, bandari hiyo hushughulikia makasha milioni 2.6, tani milioni 13 za mizigo mikavu, tani milioni 4.6 za break bulk, magari 560,000 na takribani kilolita milioni 22 za mizigo ya vimiminika (liquid bulk).

Akizungumza baada ya ziara hiyo iliyofanyika Machi 20, 2026, Waziri Kihenzile amesema ameridhishwa na kiwango kikubwa cha uwekezaji katika miundombinu ya bandari na reli, pamoja na namna ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi unavyoongeza ufanisi wa huduma bandarini.

Ametolea mfano mkataba wa miaka 25 kati ya bandari hiyo na kampuni ya ICTSI ulioanza Januari 2026 kwa ajili ya kuendesha Pier 2, unaolenga kuongeza uwezo wa kuhudumia makasha (TEUs) na kuongeza kasi ya utendaji kazi bandarini kwa zaidi ya mara mbili.

Waziri huyo amesema uzoefu huo unaonesha umuhimu wa sekta binafsi katika kuboresha ufanisi wa bandari, ambapo amebainisha kuwa Tanzania tayari inanufaika na ushiriki wa sekta binafsi kupitia kampuni kama DP World na Adani Ports (kupitia TEAGTL/TICTS) katika uendeshaji wa sehemu ya bandari.

Aidha, ameeleza kuwa juhudi hizo zinaenda sambamba na uwekezaji wa Serikali katika miundombinu ya reli, ikiwemo Standard Gauge Railway (SGR), Meter Gauge Railway (MGR) na TAZARA, ili kuharakisha upakiaji, upakuaji na usafirishaji wa mizigo.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Bandari ya Dar es Salaam inaendelea kuimarika kila siku na kuwa lango lenye ushindani mkubwa kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, huku ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi ukiendelea kuleta matokeo chanya katika sekta ya uchukuzi.










Tanzania yafanya maandalizi ya kuendesha mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala ili kuongeza idadi ya wanawake waliothibitishwa kwenye ngazi ya maamuzi na ushiriki kwenye utatuzi wa migogoro ndani na nje ya nchi.

Hayo yameelezwa leo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (Tanzania International Arbitration Centre – TIAC), ndugu Godson Nyange wakakti akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbu wa Wakili House, Dar es Salaam ili kuhabarisha umma kuhusu matukio hayo ambayo yamepangwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 jijini Dar es Salaam

Ndugu Nyange amesema kuwa kongamano hilo litafanyika tarehe 27 Machi, 2026 na litaongozwa na kauli mbiu isemayo, “Kutoka Majadiliano hadi Hatua: Kuendeleza Ushirikishwaji wa Wanawake katika Utatuzi wa Migogoro kwa Njia Mbadala (“From Dialogue to Action: Advancing Women’s Inclusion in Alternative Dispute Resolution (ADR).”) Kongamano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Wakili House jijini Dar es Salaam na litawaleta pamoja wataalamu wa sheria, watunga sera, wanataaluma, viongozi wa biashara, wataalamu wa ADR pamoja na wataalamu kutoka kada mbalimbali ili kuzitathimini kwa kina hatua za kuongeza ushiriki wa wanawake katika utatuzi wa migogoro.

Pia, ameongeza kuwa kongamano hilo litatanguliwa na mafunzo yatakayofanyika tarehe 24 hadi 26 Machi, 2026 na yatafanyika kwenye ukumbi wa Wakili House jijini Dar es Saalam ambapo mafunzo hayo yataongozwa na mada isemayo, “Kujenga Uwezo na Kujiamini kwa Wanawake katika Utatuzi Mbadala wa Migogoro (ADR).”

“Kihistoria, Sekta ya Utatuzi wa Migogoro kwa Njia Mbadala (ADR) imekuwa ikitawaliwa zaidi na wanaume, huku wanawake wakiwa wachache katika nafasi za usuluhishi (arbitration), upatanishi (mediation) na majukumu mengine ya ADR hasa katika nafasi za juu za kufanya maamuzi. Hali hii imeonekana duniani kote na barani Afrika ambapo tafiti zinaonyesha kuwa takribani asilimia 72 ya wasuluhishi katika kesi zinazohusiana na Afrika ni wanaume, wakati asilimia 28 tu ni wanawake. Vilevile, wanawake wanawakilisha takribani asilimia 29 hadi 34 ya uteuzi wa wasuluhishi katika taasisi kubwa za kimataifa za usuluhishi,” amefafanua ndugu Nyange.

Akizungumza kwa niaba ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (OWMS), Bi. Mercy Kyamba, Mkurugenzi Msaidizi – Sehemu ya Udhibiti Ubora wa Ofisi hiyo amesema kuwa OWMS inashirikiana na TIAC kuendesha mafunzo na kufanya kongamano hilo kwa kuwa OWMS pamoja na majukumu mengine, imekasimiwa na kupewa dhamana ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusimamia na kuendesha mashauri ya usuluhishi ndani na nje ya nchi kwa niaba ya Serikali.

Bi. Kyamba amesema kuwa uwepo wa mafunzo hayo na kongamano hilo ni dhamira ya pamoja ya TIAC na OWMS ya kuimarisha nafasi ya wanawake katika usuluhishi (arbitration), upatanishi (mediation) na mifumo mingine ya ADR. Mafunzo hayo yataendeshwa na wataalam wabobezi wa ndani na nje ya nchi na yamelenga kuwapatia wanawake maarifa, ujuzi wa vitendo na kujiamini kunakohitajika ili kushiriki kikamilifu katika michakato ya ADR.

Pia, Bi. Kyamba ameongeza kuwa maeneo muhimu yatajadiliwa kwenye mafunzo hayo yanahusu misingi ya usuluhishi (arbitration) na upatanishi (mediation); ujuzi wa vitendo katika majadiliano na usimamizi wa migogoro; viwango vya maadili na wajibu wa kitaaluma katika ADR; njia za kujenga taaluma na kupata ithibati katika ADR; na mikakati ya kujenga kujiamini na uwepo wa kitaaluma katika mashauri ya utatuzi wa migogoro.

Aidha, amesema kuwa kwa upande wa Kongamano, linatarajiwa kuwa jukwaa la kiwango cha juu la kujadili namna ya kuongeza ushiriki wa wanawake katika ADR ambapo majadiliano ya jopo la wataalamu yatawakutanisha wadau mashuhuri ili kuchambua masuala muhimu yakiwemo nafasi ya wanawake katika kuimarisha mifumo ya ADR; msaada wa taasisi katika kukuza wanawake katika usuluhishi na upatanishi; kujenga mitandao ya kitaaluma na fursa za ulezi (mentorship) kwa wataalamu wapya wa ADR; na athari pana ya utofauti wa kijinsia katika utoaji haki na imani ya kibiashara.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TIAC, Bi, Magreth Magoma amesema kuwa mafunzo na kongamano hilo ni sehemu ya juhudi pana za TIAC za kukuza matumizi na maendeleo ya utatuzi mbadala wa migogoro nchini Tanzania na katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki na kutachangia katika kujenga mfumo madhubuti na unaoaminika wa utatuzi wa migogoro unaosaidia upatikanaji wa haki, uhakika wa biashara na kuimarisha uwekezaji.

Bi. Magoma ameongeza kuwa kupitia uwepo wa Sheria ya Usuluhishi nchini ya mwaka 2020 ambayo inaelekeza kuwa mtu yeyote anayetaka kufanya usuluhishi lazima apate ithibati kutoka Wizara ya Katiba na Sheria. “Sheria hii ilianza utekelezaji wake mwaka 2021 ambapo hadi sasa Wizara imewapatia ithibati na kuwathibitisha jumla ya wanaume 444 katika eneo la usuluhishi na wanawake 89; majadiliano wanaume 162 na wanawake 38; wapatanishi wanaume 142 na wanawake 56; na upatanishi wanaume 77 na wanawake 14,” amefafanua Bi. Magoma.

Mafunzo na kongamano hilo litaangazia umuhimu wa uwiano wa kijinsia katika utatuzi wa migogoro, kujadili mikakati ya kuongeza uelewa na ushiriki na uongozi wa wanawake katika ADR ili kuwawezesha wanawake katika ADR na kuimarisha taaluma zao, kuchangia mfumo wa utatuzi wa migogoro ulio na uwiano, unaojumuisha wadau wote na unaoaminika zaidi.
Ndugu Godson Nyange, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (TIAC) akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Bi. Mercy Kyamba, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Udhibiti Ubora wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali akizungumzia ushirikiano uliopo kati ya Ofisi hiyo na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Bi. Magreth Magoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (TIAC) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.




Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (TIAC) wakimsikiliza ndugu Godson Nyange (hayupo pichani) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.


-WAZIRI DKT. GWAJIMA KUANZISHA JUKWAA LA MAJADILIANO ENDELEVU YA KISEKTA KUHUSU MIKUTANO YA WIZARA KIMATAIFA.

Na WMJJWM New York Marekani

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amesema, Serikali kupitia Wizara anayoiongoza itaanzisha Jukwaa endelevu la majadiliano ya Kisekta litakaosaidia kuongeza ufanisi wa ushiriki wa Nchi katika Mikutano ya kimataifa inayogusa maendeleo ya Wanawake na Jinsia.

Waziri Dkt. Gwajima ameyasema hayo jijini New York nchini Marekani mara baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano wa 70 wa Hali ya Wanawake Duniani (CSW 70) ambapo, Tanzania ilishiriki na kueleza mafanikio iliyopata katika kuhakikisha upatikanaji wa haki kwa wanawake na wasichana.

Waziri Dkt. Gwajima amesema jukwaa hilo litasaidia kuwepo kwa uelewe wa pamoja kati ya Serikali na wadau wengine wote katika kuratibu ushiriki wa nchi katika mikutano mbalimbali ya kimataifa hasa inayogusa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ili kuongeza ufanisi zaidi.

“Ni muhimu tuwe na Jukwaa hili ambalo litasaidia kuturatibu Serikali na wadau wetu wote ili, tunapotaka kushiriki katika Mikutano ya Kimataifa tuwe na uelewa wa pamoja na maandalizi ya pamoja ya kwenda kuitangaza nchi kimataifa” amesisitiza Waziri Dkt. Gwajima

Ameeleza kuwa, Tanzania imeshiriki mikutano mbalimbali iliyoandaa na iliyoalikwa ikiwa na lengo la kueleza mafanikio ya nchi katika suala la upatikanaji wa haki kwa wanawake na watoto wa kike na pia kujifunza namna mataifa mengine wanavyotekeleza suala hilo.

Aidha ameongeza kuwa, taarifa ya ushiriki wa Nchi katika Mkutano wa 70 wa Hali ya Wanawake Duniani itatolewa mara baada ya ujumbe ulioshiriki Mkutano huo kuwasili nchini.

Mkutano huo uliofunguliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres Machi 09, 2026 uliongozwa na Kaulimbiu isemayo "Kuhakikisha na Kuimarisha upatikanaji wa Haki kwa Wanawake na Wasichana wote, ikiwa ni pamoja na kukuza mifumo ya kisheria nyenye usawa na jumuishi, kuondoa sheria, sera, na desturi za kibaguzi na kushughulikia vikwazo vya kimuundo", (Ensuring and Strengthening access to justice for all Women and Girls, including by promoting inclusive and equitable legal system, eliminating discriminatory laws, policies, and practices and addressing structural barriers”).










 

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Ndugu Bakari Machumu akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Ndugu Gerson Msigwa katika Ofisi ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Machi, 2026.


Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Ndugu Bakari Machumu akiwa kwenye picha na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Ndugu Gerson Msigwa katika Ofisi ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Machi, 2026.

Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Ruvuma, Alan Njiro amewahimiza wananchi kujikita katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia majiko ya umeme ya kisasa, akibainisha kuwa hatua hiyo ni salama, nafuu na rafiki kwa mazingira.

Akizungumza Machi 20, 2026 wakati akiwasilisha mada kuhusu nishati safi ya kupikia katika mafunzo ya ndani ya watumishi wa Shirika la ukaguzi na usimamizi wa vyama vya ushirika COASCO, yaliyolenga kuwajengea uwezo katika masuala ya utumishi wa umma, rushwa, afya ya akili na UKIMWI.

Njiro amesema kuwa TANESCO imefanya tafiti juu ya matumizi ya majiko ya umeme ikiwemo induction cooker na pressure cooker, na kubaini kuwa vifaa hivyo vinatumia umeme kidogo (energy saver) na vinafaa kwa matumizi ya kila siku majumbani.

Alieleza kuwa tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo wananchi walikuwa na hofu ya gharama kubwa za umeme, teknolojia ya sasa imeboreshwa na kufanya majiko ya umeme kuwa na matumizi madogo ya nishati. Aidha, aliwataka wananchi kuepuka kutumia vifaa vya mtumba ambavyo mara nyingi hutumia umeme mwingi na kuongeza gharama zisizo za lazima.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano Msaidizi wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma, Emma Ulendo alisema majiko ya induction cooker ni salama zaidi kwani hutumia mfumo wa sumaku kati ya sufuria na jiko, hivyo kupunguza hatari ya mtumiaji kupigwa na shoti au kusababisha ajali za moto. Aliongeza kuwa majiko hayo yana uwezo wa kuweka muda wa kupika na kujizima yenyewe, jambo linalosaidia kuokoa umeme na kuongeza usalama kwa mtumiaji.

Ulendo pia alisisitiza kuwa matumizi ya pressure cooker yana mchango mkubwa katika kupunguza muda wa kupika na hivyo kutumia umeme kidogo, hali inayofanya majiko hayo kuwa suluhisho bora kwa kaya nyingi zinazotaka kupunguza gharama na kulinda mazingira.

Katika hatua nyingine, Njiro alibainisha kuwa Mkoa wa Ruvuma una umeme wa kutosha, ukiwa na matumizi  ya takribani megawati 28 huku ukisalia  na ziada ya megawati 42, hali inayowezesha wananchi kutumia umeme huo kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kupikia bila hofu ya upungufu wa nishati hiyo muhimu.

Kwa ujumla, TANESCO imeendelea kusisitiza umuhimu wa wananchi kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia umeme, hatua ambayo itasaidia kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa, kulinda mazingira na kuboresha afya pamoja na maisha ya wananchi kwa ujumla.







Na Mwandishi Wetu

KITUO cha kulea watoto yatima cha New Faraja Orphanage kilichopo Mburahati jijini Dar es Salaam kimepokea msaada mkubwa wa vyakula mbalimbali kutoka kampuni ya Oryx Gas ikiwa ni sehemu ya kuwapa mkono wa Eid na kupeleka tabasamu kwa watoto hao.

Msaada huo wa vyakula ni kwa ajili maandalizi ya sikukuu ya Iddi ambayo huenda ikaazimishwa kesho au keshokutwa kutegemea mwandamo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Mwanzilishi wa Kituo cha New Faraja Orphanage Zmla İdris amesema wanaishukuru Oryx Gas Tanzania kwa msaada huo ambao umepeleka faraja kwa watoto wa Kituo hicho wapato 120 ambapo asilimia 80 ni yatima.

“Misaada ni ishara ya upendo, na leo tumepokea upendo pamoja na burudani. Nani alijua leo mtaleta hiyo furaha kwa hawa watoto?”amesema na kuongeza kituo hicho kina miaka 17 tangu kuanzishwa kwake na watoto wanaoishi hapo wapo katika ngazi mbalimbali za kielimu kuanzia elimu ya msingi,Sekondari na wengine Chuo.

Mmoja ya watoto wanaolelewa katika kituo hicho amesema msaada huo si tu umepeleka faraja kwao bali umethibitisha upendo wa kweli wa kampuni hiyo kwa watu wenye uhitaji kama wao.“Hii ndiyo siku bora kabisa. Hatuli tu tunacheza, na tunaimba pia!”

Awali kampuni ya Orx Gas Tanzania imesema imetoa msaada huo kutokana juhudi za kituo hicho kwa kulea watoto katika misingi bora ya maadili na malezi mema huku ikisisitiza itaendelea kushirikiana na jamii kwa kuyagusa makundi mbalimbali.







Top News