Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma
Soko la ajira nchini Tanzania limeendelea kuimarika, baada ya kiwango cha ukosefu wa ajira kushuka hadi asilimia 6.2 mwaka 2024, ikilinganishwa na asilimia 8.7 iliyorekodiwa mwaka 2020/21.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, wakati akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2025 pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27.
Profesa Mkumbo amesema hali hiyo ni ishara ya kuimarika kwa mazingira ya biashara, uwekezaji na uzalishaji nchini, hali inayochochea ongezeko la nafasi za ajira katika sekta mbalimbali.
Kwa mujibu wa takwimu hizo, kasi ya ukuaji wa ajira pia imepanda kwa kiwango kikubwa, ambapo wastani wa ukuaji wa ajira kwa mwaka umefikia asilimia 7.8 mwaka 2024, kutoka asilimia 2.3 mwaka 2020/21.
Aidha, nguvu kazi nchini imeongezeka na kufikia watu milioni 27.3, sawa na asilimia 73.2 ya wananchi wote wenye uwezo wa kufanya kazi, ikilinganishwa na asilimia 72.1 ya mwaka 2020/21.
Kati ya nguvu kazi hiyo, takriban watu milioni 25.6 wanajishughulisha na shughuli za kiuchumi zinazowaingizia kipato, hali inayoonyesha ushiriki mpana wa wananchi katika uzalishaji.
Kwa upande wa sekta, kilimo kinaendelea kuwa mwajiri mkubwa zaidi nchini kwa asilimia 54.2, kikifuatiwa na sekta ya huduma yenye asilimia 35.5, huku sekta ya viwanda ikichukua asilimia 10.3 ya ajira zote.
Serikali imesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za kuboresha mazingira ya biashara, kuvutia uwekezaji na kuimarisha shughuli za uzalishaji katika sekta mbalimbali za uchumi.
Kwa ujumla, mwenendo huo unaonyesha mwanga mpya katika soko la ajira nchini, huku matarajio yakiwa ni kuendelea kupungua kwa ukosefu wa ajira na kuongezeka kwa fursa zaidi kwa wananchi katika miaka ijayo.



.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)






.jpeg)









.jpeg)
