Mwenyekiti wa umoja wa wanawake (UWT) Mkoa wa Pwani Zainabu Vullu amewahimiza wanawake kuweka misingi imara ya kutumia fursa za mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na Hamashauri kwa lengo la kuweza kujikwamua kiuchumi na kuondokana na wimbi la umasikini.
Vullu ameyabainisha hayo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha ambapo ameweza kutembelea katiika kata mbili za Tumbi pamoja na Kata ya Kongowe ambapo ameambatana na kamati ya utekelezaji ya Mkoa pamoja na vingozi ngazi ya Wilaya.
Katika ziara hiyo Mwenyekiti huyo ameweza kupata fursa ya kutembelea baadhi ya miradi ikiwemo katika sekta ya elimu ambapo ameweza kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa choo salama katika wa sekondari ya Kibaha pamoja na kituo cha afya Kongowe.
Mwenyekiti huyo amesema kwamba lengo kubwa la kufanya ziara hiyo ni kwa ajili ya kuwashukuru umoja wa wanawake UWT kwa kuweza kuwa pamoja na mshikamano wa kukiwezesha chama cha mapinduzi kuweza kushinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kuwapoitisha viongozi katika ngazi mbali mbali ikiwemo udiwani, Ubunge pamoja na nafasi ya Urais.
Naye Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha mjni Cesilian Ndaru amesema kwamba lengo lako kubwa ni kuhakikisha wanaweka mikakati madhubuti ya kuwa na vitega uchumi ambavyo vutaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa katika kijikwamua kiuchumi.
Katibu Ndaru amebainisha kwamba umoja huo wameweka mipango madhubuti ya kuwa na miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo kuanzisha miradii ya kuwa na nyumba za makatibu kila kata kwa ajili ya kuwawezesha makatibu kuwa na sehemu na makazi ya kusihi ili kuweza kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Naye mlezi wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Mama Selina Koka ambaye pia ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini amesema kwamba ataendelea kushirikiana bega kwa bega na wanawake katika kuhakikisha kwamba wanaimarisha jumuiya hiyo.
Mama Koka amebainisha kwamba lengo lake kubwa ni kuendelea kushirikiana kwa pamoja na viongozi wenzake katika kufanya kazi kwa bidii na kumuunga mkono Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuleta chanchu ya maendfeleo ikiwa pamoja na kuwainua kiuchumi wanawake wenzake.
Ziara ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani imefanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha ambapo ameweza kupata fursa ya kutembnelea baadhi ya mikradi ya maendeleo ikiwemo katika shule ya sekondari ya wasichana Kibaha pamoja na kituo cha afya Kongowe ikiwa pamoja na kuzungumza na wanawake wa umoja huo.
Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na wazazi na walezi mkoani Geita wametakiwa kuthamini na kulinda haki za watoto kwa kuwakinga dhidi ya ukatili na unyanyapaa.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika. Maadhimisho hayo ya kimkoa yamefanyika katika Kata ya Nyawilimilwa, Wilaya ya Geita.
Mhe. Komba amesema Serikali haitaona aibu kuwachukulia hatua za kisheria wazazi au walezi wanaowanyima watoto wao haki ya msingi ya kupata elimu na haki nyingine zilizowekwa na sheria za nchi. Amesema ulinzi wa mtoto ni wajibu wa kila mzazi na jamii kwa ujumla.
Akitoa taarifa ya utekelezaji, Ofisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Geita, Bw. Frank Moshi, ameeleza mafanikio yaliyopatikana pamoja na mikakati inayoendelea kutekelezwa ili kudhibiti vitendo vya ukatili na uhalifu unaofanywa dhidi ya watoto mkoani humo. Amesema jitihada hizo zimeleta matumaini kwa watoto wengi waliokuwa katika mazingira hatarishi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la NELICO linalojihusisha na utetezi na ulinzi wa haki za watoto mkoani Geita, Bi. Paulina Alex Majogoro, amesema shirika hilo linaendelea kutoa msaada kwa watoto. Msaada huo ni pamoja na ushauri wa kisheria, sare za shule na mahitaji mengine muhimu kwa familia zenye kipato duni.
Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kaulimbiu ya kuhimiza jamii kutoa kipaumbele kwa ustawi na usalama wa mtoto ili kujenga taifa lenye vizazi vijavyo vyenye maadili na elimu.
Serikali imeonyesha utayari wa kuangalia uwezekano wa mashindano ya Ligi ya Muungano kuanza kuchezwa pia Tanzania Bara, hatua inayolenga kuimarisha ushiriki wa pande zote mbili za Muungano na kukuza maendeleo ya michezo nchini.
Hoja hiyo iliibuliwa bungeni leo na Mbunge wa Jimbo la Mlalo, Rashid Shangazi, ambaye alihoji sababu za mashindano hayo kuendelea kufanyika Zanzibar pekee kwa muda mrefu na kusisitiza umuhimu wa kuyapanua ili yajumuishe Tanzania Bara.
Akichangia mjadala huo, Shangazi alisema kuwa kuchezwa kwa mashindano hayo katika pande zote za Muungano kutasaidia kuimarisha mshikamano wa kitaifa, kuongeza ushindani wa michezo na kutoa fursa sawa kwa wanamichezo wa Bara na Visiwani.
Akijibu hoja hiyo kwa niaba ya Serikali, Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Hamisi Mwinjuma, alisema hakuna sheria wala kanuni inayozuia Ligi ya Muungano kuchezwa Tanzania Bara, bali hali iliyopo kwa sasa ni matokeo ya mazoea yaliyojengeka kwa miaka mingi.
Mwinjuma alieleza kuwa suala hilo linaweza kujadiliwa na kufanyiwa maboresho kupitia mazungumzo na makubaliano ya wadau husika ili kuhakikisha mashindano hayo yanawanufaisha wananchi wa pande zote za Muungano.
“Serikali ipo tayari kuendelea kushirikiana na wadau wa michezo kujadili uwezekano wa mashindano haya kufanyika pia Tanzania Bara endapo kutakuwa na makubaliano ya pamoja,” alisema.
Aidha, alibainisha kuwa moja ya sababu zilizochangia mashindano hayo kufanyika zaidi Zanzibar ni kutokana na ukweli kwamba Tanzania Bara tayari ina idadi kubwa ya ligi na mashindano mbalimbali ya soka, hivyo Zanzibar imekuwa ikipewa nafasi ya kuwa mwenyeji wa matukio hayo ili kuongeza shughuli za michezo visiwani.
Hatua hiyo ya Serikali imepokelewa kama ishara ya kufungua ukurasa mpya katika uendeshaji wa Ligi ya Muungano, huku wadau wa michezo wakitarajia kuona mashindano hayo yakipanuliwa zaidi ili kuleta usawa wa ushiriki na kuongeza chachu ya maendeleo ya soka katika pande zote za Muungano.

Na Mwandishi Wetu
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeanza kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 yaliyoanza rasmi leo, tarehe 16 mpaka 23 Juni, yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma
Akizungumza kuhusu ushiriki wa EWURA katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa EWURA, Bi. Hawa Ramadhan Mniga, amesema maonesho hayo ni fursa muhimu kwa Mamlaka hiyo kuwafikia Watanzania na kuwapatia uelewa kuhusu majukumu yake katika usimamizi wa sekta za nishati na maji.
“Wananchi watakaotembelea banda la EWURA watapata fursa ya kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo mifumo mbalimbali ya kidijitali inayotumiwa na Mamlaka katika utoaji wa huduma kwa wateja, pamoja na maboresho yanayoendelea kufanyika kwa lengo la kuongeza ufanisi, kasi na ubora wa utoaji wa huduma,” amesema Bi. Mniga.
Ameongeza kuwa eneo lingine lililopatiwa kipaumbele ni uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kufanikisha lengo la Taifa la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Aidha, ametoa rai kwa wananchi, wadau wa sekta mbalimbali na washiriki wa maonesho hayo kutembelea banda la EWURA ili kupata elimu, kuuliza maswali na kufahamu kwa undani huduma zinazotolewa na Mamlaka hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya NMB, Ruth Zaipuna (katikati), akiwa na Menejimenti Kuu ya benki hiyo wakionyesha ishara ya furaha mara baada ya uzinduzi wa NMB Mkononi Super App jijini Dar es Salaam, Jumanne, Juni 16, 2026.
Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (kushoto), akijaribu huduma za NMB Mkononi Super App wakati wa uzinduzi wake jijini Dar es Salaam, Jumanne, Juni 16, 2026. Anayemwelekeza kwa kutumia iPad ni Mtaalamu wa Bima wa NMB, Sangwani Mkandawile (katikati).
Mfumo Mpya Waunganisha Mikopo, Bima, Uwekezaji na Huduma za Vikundi
Benki ya NMB imezindua rasmi NMB Mkononi Super App, jukwaa jipya la kidijitali linalounganisha huduma mbalimbali za kifedha katika mfumo mmoja, hatua inayolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma za benki na kuimarisha ujumuishaji wa kifedha nchini.
Kupitia jukwaa hilo, wateja wataweza kupata huduma za mikopo, bima, uwekezaji, malipo, huduma za vikundi pamoja na ununuzi wa bando la mawasiliano bila ulazima wa kutembelea matawi ya benki kwa huduma za kawaida.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna, alisema kuwa NMB Mkononi Super App ni zaidi ya programu ya kibenki, bali ni jukwaa la fursa na uwezeshaji linalolenga kuwahudumia makundi mbalimbali ya Watanzania.
“Jukwaa hili limeundwa kuwawezesha wanafunzi, wafanyakazi, wakulima, wafanyabiashara, wajasiriamali na wawekezaji kusimamia mahitaji yao ya kifedha kwa urahisi kupitia simu zao za mkononi,” alisema Zaipuna.
Katika hatua ya kuongeza upatikanaji wa mitaji, NMB imesema wateja binafsi wanaokidhi vigezo wataweza kuomba mikopo ya hadi Shilingi milioni mbili kupitia programu hiyo, huku wafanyabiashara wadogo wanaostahili wakipata mikopo ya hadi Shilingi milioni tano.
Hata hivyo, wataalamu wa sekta ya fedha wanaona kuwa ongezeko la upatikanaji wa mikopo kidijitali linaifanya elimu ya fedha kuwa muhimu zaidi, hasa katika kuwawezesha wananchi kuelewa gharama za mikopo, masharti ya mikataba, muda wa marejesho na uwezo wao wa kulipa kabla ya kukopa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Ubunifu wa NMB, Josina Njambi, alisema ufunguaji wa akaunti kupitia NMB Mkononi Super App umeboreshwa kwa kiwango kikubwa, ambapo mteja anaweza kufungua akaunti kwa kutumia namba ya simu na namba ya NIDA ndani ya dakika tano pekee.
Alibainisha kuwa mafanikio ya jukwaa hilo hayatategemea tu upana wa huduma zake, bali pia uwezo wake wa kuwasaidia wateja kufanya maamuzi sahihi ya kifedha, kuongeza utamaduni wa kuweka akiba na kutumia huduma za kifedha kwa uwajibikaji.
Uzinduzi wa NMB Mkononi Super App unaashiria hatua nyingine muhimu katika safari ya mageuzi ya kidijitali ya sekta ya benki nchini Tanzania, huku ukionyesha namna teknolojia inavyoendelea kubadilisha upatikanaji na matumizi ya huduma za kifedha kwa wananchi wa kada mbalimbali.
Mkononi Patamu.
Aidha, wamepongeza uwekezaji uliofanywa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) katika Kiwanda cha Kimataifa cha Bidhaa za Ngozi cha Kilimanjaro (KLICL), wakisema mradi huo una mchango mkubwa katika kukuza viwanda, kuongeza thamani ya mazao ya mifugo na kutengeneza ajira.
Pongezi hizo zilitolewa jijini Dodoma wakati wa semina ya wabunge kuhusu Skimu ya Hifadhi kwa Wananchi Waliojiajiri na Mradi wa Kiwanda cha Kimataifa cha Bidhaa za Ngozi cha Kilimanjaro.
Akizungumza kwa niaba ya Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu, Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, aliipongeza NSSF pamoja na PSSSF kwa kuendelea kutoa elimu kwa wabunge kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na mifuko hiyo.
Mhe. Sillo alisema elimu hiyo ni muhimu kwa wabunge kwani itawawezesha kuwa mabalozi wa kuhamasisha wananchi katika majimbo yao kujiunga na mifumo ya hifadhi ya jamii na kufahamu uwekezaji unaofanywa na mifuko hiyo.
Baadhi ya wabunge walioshiriki semina hiyo, akiwemo Mhe. Said Salimu na Mhe. Rashid Shangazi, waliipongeza NSSF kwa juhudi zake za kuwafikia wananchi waliojiajiri na kuimarisha huduma za hifadhi ya jamii nchini.
Walisema skimu hiyo itasaidia kujenga utamaduni wa kuweka akiba, kuongeza usalama wa kipato na kuwapa wananchi waliojiajiri fursa ya kunufaika na huduma za hifadhi ya jamii.
Kwa upande wa uwekezaji wa PSSSF, wabunge Jackson Kiswaga na Rashid Shangazi waliipongeza PSSSF kwa uwekezaji kwenye kiwanda hicho, huku wakiishauri sekta binafsi ikaribushwe katika uendeshaji wa kiwanda ili kuongeza nguvu katika masoko na uzalishaji.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, alisema Serikali inaendelea kuimarisha huduma za hifadhi ya jamii kwa kuwajumuisha wananchi waliojiajiri, ambao kwa muda mrefu walikuwa nje ya mifumo rasmi ya hifadhi ya jamii licha ya mchango wao mkubwa katika uchumi wa taifa.
Kuhusu PSSSF, Mhe. Sangu alisema mradi wa kiwanda hicho unamilikiwa kwa ubia kati ya Mfuko huo na Jeshi la Magereza kupitia kampuni yake ya Prisons Corporation Sole (PCS) na kuwa umekuwa na manufaa makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema mfuko huo unalenga kuandikisha wananchi waliojiajiri milioni 3.7 ifikapo Juni 2031 kupitia Skimu ya Hifadhi ya Jamii. Alisema takribani asilimia 85 ya nguvu kazi nchini, sawa na wananchi milioni 20.98 wenye uwezo wa kufanya kazi, wamejiajiri, jambo linaloifanya skimu hiyo kuwa nyenzo muhimu ya kuwafikia makundi mbalimbali ya wananchi.
Bw. Mshomba alisema wanachama wa skimu hiyo watanufaika na mafao mbalimbali yakiwemo pensheni ya uzee, mafao ya urithi, ulemavu, uzazi na matibabu. Alisema wananchi sasa wanaweza kujiunga, kuchangia na kufuatilia taarifa zao kwa njia za kidijitali kupitia simu za mkononi, huku kiwango cha chini cha mchango kikiwa shilingi 30,000 kwa mwezi.
Naye, Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Fortunatus Magambo, amesema kiwanda hicho kinazalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na kimekuwa na mchango mkubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla.
Alisema kiwanda hicho kimeongeza ajira kwa wananchi, kimeboresha kipato cha wananchi hususan wafugaji kupitia upatikanaji wa soko la uhakika la ngozi, na kuchochea mnyororo wa thamani wa sekta ya mifugo nchini.
“Kiwanda chetu kinazalisha bidhaa zenye ubora mkubwa, kimeongeza ajira kwa wananchi na kimefungua soko la uhakika la ngozi kwa wafugaji wetu, jambo linalonufaisha jamii na taifa kwa ujumla,” alisema Bw. Magambo.
.jpeg)
Baada ya mazungumzo yao, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) alimkabidhi Mhe. António Guterres zawadi ya kitabu kuhusu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutambua kuvutiwa kwa muda mrefu kwa Katibu Mkuu huyo na maono, uongozi na mchango wa Mwalimu Nyerere katika kuhimiza amani, maendeleo na ushirikiano wa kimataifa.
Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Uzinduzi na utambulisho rasmi wa mfuko huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau wa sekta ya fedha, masoko ya mitaji, wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi, pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari.
Hafla hiyo iliongozwa na Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba, huku Afisa Mtendaji Mkuu wa CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, akiwaongoza viongozi wengine wa kampuni hiyo kuelezea manufaa na fursa zinazotokana na mfuko huo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Mwangalaba aliipongeza CORE Securities Limited kwa kuanzisha mfuko huo, akieleza kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na kupanua wigo wa huduma za uwekezaji kwa wananchi wengi zaidi.
Alisema kwa muda mrefu mipango ya kustaafu nchini imekuwa ikihusishwa zaidi na watu wenye ajira rasmi ambao ni takribani asilimia chache zaidi ya wananchi wote, hali iliyosababisha sehemu kubwa ya wananchi, hususan walio katika sekta isiyo rasmi, kukosa fursa za maandalizi ya maisha ya baadaye.
“Kupitia FPRF, taifa linapata jukwaa jumuishi linalomwezesha kila Mtanzania — awe ameajiriwa rasmi, amejiajiri, mfanyabiashara au anayejishughulisha na shughuli za sekta isiyo rasmi — kuwekeza na kujiandaa kwa maisha ya baadaye kwa uhuru, unyumbufu na heshima,” alisema Dkt. Mwangalaba.
Aidha, aliwahimiza wananchi kujenga utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza kwa malengo ya muda mrefu, huku akisisitiza umuhimu wa kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kufanya maamuzi ya uwekezaji.
“Mipango ya kustaafu haipaswi kuonekana kama fursa ya watu wachache wenye ajira rasmi pekee. Kila Mtanzania anastahili kuwa na usalama na heshima ya kifedha baada ya miaka yake ya uzalishaji, na mfuko huu ni sehemu ya suluhisho la kufanikisha lengo hilo...nawapongeza sana CORE Securities kwa mpango huu” alisisitiza.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, alisema FPRF imeundwa kuziba mapengo yaliyopo katika mifumo ya kawaida ya pensheni kwa kutoa chaguzi zenye unyumbufu zaidi katika uwekezaji na upatikanaji wa mafao.
“Ingawa mifuko ya hifadhi ya jamii kama NSSF na PSSSF inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika ustawi wa wananchi, FPRF imeundwa kuikamilisha mifumo hiyo kwa kutoa fursa za ziada za uwekezaji kwa watu ambao awali hawakuwa na nafasi ya kushiriki,” alisema.
Alifafanua kuwa CMSA iliidhinisha mfuko huo tarehe 28 Aprili 2026 kwa mujibu wa Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana pamoja na Kanuni za Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja za mwaka 1997, huku NMB Bank PLC ikiidhinishwa kuwa Mdhamini na Mlezi wa mfuko huo.
Kwa mujibu wa CPA Fumbuka, mfuko huo umeidhinishwa kukusanya hadi shilingi bilioni 10 kupitia uuzaji wa vipande vya uwekezaji milioni 100, kila kimoja kikiwa na thamani ya shilingi 100.
Alisema muundo wa FPRF umeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji tofauti ya kifedha na viwango vya uvumilivu wa hatari za uwekezaji kwa makundi mbalimbali ya umri.
“Mahitaji ya kifedha ya kijana aliyeanza kazi ni tofauti na ya mtu anayekaribia kustaafu. Ndiyo maana tumeandaa mipango tofauti inayowawezesha wawekezaji kuchagua mkakati unaoendana na umri, kipato na matarajio yao ya muda mrefu,” alieleza.
Mfuko huo utakuwa na mipango mitatu ya uwekezaji ambayo ni Youngsters’ Plan kwa wawekezaji wenye umri chini ya miaka 35, Middle-Agers’ Plan kwa wenye umri kati ya miaka 35 na 50, na Seniors’ Plan kwa wawekezaji wenye umri zaidi ya miaka 50, ambao uwekezaji wake utazingatia zaidi dhamana za Serikali.
CPA Fumbuka alibainisha kuwa tofauti na mifuko mingi ya pensheni inayohitaji michango ya muda mrefu kabla ya mafao kupatikana, FPRF ina kipindi cha miaka mitano pekee ambapo baada ya hapo, mwekezaji ataweza kupata fedha zake kwa mkupuo, kwa malipo ya pensheni ya kawaida au kwa mchanganyiko wa njia hizo.
“Mahitaji ya kifedha ya watu hubadilika kadri muda unavyokwenda. Wapo wanaohitaji mapato ya kila mwezi baada ya kustaafu, na wapo wanaoweza kuhitaji sehemu ya akiba zao kwa ajili ya matibabu, familia au biashara. Mfuko huu unawapa uhuru wa kufanya maamuzi hayo kulingana na mahitaji yao,” alisema.
Aliongeza kuwa mwananchi anaweza kuanza uwekezaji kwa kiasi cha shilingi 10,000 tu, sawa na vipande 100 vya uwekezaji, na kuongeza uwekezaji wake taratibu kulingana na uwezo wake wa kifedha.
Mbali na hilo, mfuko huo unatoa faida ya ukwasi (liquidity), ambapo baada ya kipindi cha miaka mitano, wawekezaji wataweza kuuza vipande vyao kwa thamani halisi ya mali za mfuko (NAV), huku malipo yakifanyika ndani ya siku mbili za biashara.
Uwekezaji katika mfuko huo utafanyika kwa njia ya kielektroniki kupitia mfumo wa CORE Securities Limited, matawi maalumu ya NMB Bank PLC pamoja na mawakala walioidhinishwa na kuunganishwa na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa wa chama hicho, Bw. Nelson Mabula, alisema CWT imejiridhisha kuhusu usalama, uwazi na manufaa ya mfuko huo kwa wanachama wake.
“Kiwango cha chini cha kuanzia uwekezaji cha shilingi 10,000 kinawapa fursa wanachama wetu wengi kushiriki. Tunaamini huu ni uwekezaji wenye manufaa kwa walimu na wafanyakazi wengine, na kama taasisi tutahamasisha wanachama wetu kushiriki ili wawe sehemu ya fursa hii ya kujenga ustawi wao wa kifedha wa muda mrefu,” alisema.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (kushoto) akimkabidhi Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Bw. Nelson Mabula (kulia) mfuko wenye nyaraka muhimu kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Anaeshuhudia katikati ni Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (kushoto) akimkabidhi Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba (kulia) mfuko wenye nyaraka muhimu kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (kulia) akimkabidhi Mwakilishi kutoka benki ya NMB Bw Avith Massawe (kushoto) mfuko wenye nyaraka muhimu kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi huku benki ya NMB ikiwa Mdhamini na Mlezi wa mfuko huo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka, (wa pili kushoto) sambamba na Mtaalamu Mbobevu wa Masoko ya Mitaji na Dhamana, Dkt. Ibrahimu Mwangalaba (wa pili kuli), Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Taifa wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Bw. Nelson Mabula (kulia) na Mwakilishi kutoka benki ya NMB Bw Avith Massawe (kushoto) wakionesha nyaraka ya muongozo kuhusu Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mfuko huo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Mfuko huo unasimamiwa na CORE Securities Limited na unalenga kupanua fursa za uwekezaji na maandalizi ya maisha ya baada ya kustaafu kwa Watanzania wa makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi huku benki ya NMB ikiwa Mdhamini na Mlezi wa mfuko huo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Mwangalaba (pichani) aliipongeza CORE Securities Limited kwa kuanzisha mfuko huo, akieleza kuwa ni hatua muhimu katika kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na kupanua wigo wa huduma za uwekezaji kwa wananchi wengi zaidi.
Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa CORE Securities Limited, CPA George Fumbuka (pichani) alisema FPRF imeundwa kuziba mapengo yaliyopo katika mifumo ya kawaida ya pensheni kwa kutoa chaguzi zenye unyumbufu zaidi katika uwekezaji na upatikanaji wa mafao.
Msimamizi wa Mfumo wa Teknolojia wa Mfuko Mpya wa Uwekezaji wa kustaafu unaofahamika kama Foresight Private Retirement Fund (FPRF), Bw Ibrahim Isack (pichani) akifafanua kuhusu uendeshwaji wa mfumo wa teknolojia wa mfuko huo wakati wa hafla hiyo.
Uzinduzi na utambulisho rasmi wa mfuko huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam, ukihudhuriwa na wadau wa sekta ya fedha, masoko ya mitaji, wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi, pamoja na wawakilishi wa vyombo vya habari.
Na Janeth Raphael MichuziTv
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema serikali imechukua hatua madhubuti kumaliza changamoto za kukatika kwa umeme zilizokuwa zikiathiri baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, hali iliyokuwa ikisababisha wilaya nzima kukosa umeme pindi hitilafu zinapotokea kwenye baadhi ya sehemu za mtandao.
Ndejembi amebainisha hayo leo wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Usambazaji Umeme (Switching Station) pamoja na transfoma mpya zilizojengwa kwa lengo la kuimarisha na kudhibiti mfumo wa usambazaji umeme katika wilaya hiyo.
Amesema uwepo wa miundombinu hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya mgao wa umeme wa ghafla, ambao hapo awali ulikuwa ukisababisha maeneo mengi ya Kongwa na wilaya jirani kuathirika pindi hitilafu inapotokea sehemu moja ya mfumo.
“Kwa muda mrefu, changamoto ya voltage ndogo na kukatika kwa umeme mara kwa mara ilikuwa kikwazo kikubwa kwa wananchi na wajasiriamali wadogo, hususan waliokuwa wakishindwa kuendesha shughuli za uzalishaji kama kusaga nafaka na kukamua mafuta kutokana na uhaba wa umeme wa uhakika,” amesema Ndejembi.
Ameongeza kuwa serikali, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuliweka sekta ya nishati katika kipaumbele cha juu, hali iliyowezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuboresha maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.
Amesema zaidi ya shilingi bilioni 10 zimewekezwa katika eneo la Mbande kwa ajili ya ujenzi wa Switching Station hiyo, hatua ambayo itanufaisha wakazi wa wilaya za Kongwa, Kiteto, Gairo, Chamwino na Mpwapwa kwa kupata umeme wa uhakika na wa kutosha.
“Lengo letu siyo tu kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa kuwasha taa, bali ni umeme wa kuendesha viwanda na shughuli za uzalishaji. Hii itasaidia kukuza uchumi wa maeneo haya na kuongeza fursa za ajira,” ameongeza.
Uzinduzi wa mradi huo unatajwa kuwa sehemu ya jitihada za serikali kuboresha miundombinu ya nishati nchini na kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika unafika kwa wananchi wengi zaidi, hususan maeneo ya vijijini na pembezoni.
Aidha limewataka ndugu wote wenye ualbino nchini Tanzania na duniani kote, wasikate tamaa na kuwakumbusha waendelee kuamini katika uwezo wao,kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutimiza ndoto zao na kwamba Dunia inahitaji mchango, vipaji na uwezo wenu.
Hayo yamesemwa na Boniventura Mwalongo ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO)
na Mjumbe wa Kamati Maalumu ya Pamoja ya Kushughulikia Changamoto za Watu Wenye Ualbino nchini alipokuwa akitoa salamu katika Maadhimisho ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika Juni 13,2026.
“TRAMEPRO inapenda kuwahakikishia watu wote wenye ualbino kwamba itaendelea kuwa sauti yao na mshirika wao katika kutetea haki, usawa, heshima na maendeleo yao. Ahadi yetu ni kwamba kamwe hatutawasaliti katika kusimamia haki zenu na haki za binadamu kwa ujumla.
“Tutaendelea kushirikiana na Serikali, Bunge, taasisi mbalimbali, wadau wa maendeleo na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha kuwa watu wenye ualbino wanapata ulinzi, heshima, fursa na haki zote wanazostahili kama raia wengine,”amesema na kuongeza "Utu, usawa, upendo na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa maendeleo endelevu na jamii yenye amani kwa wote."
Akieleza zaidi kuhusu maadhimisho hayo amesema TRAMEPRO inaamini siku hiyo ni fursa muhimu ya kuendelea kuelimisha jamii kuhusu haki, usawa, usalama, afya na ustawi wa watu wenye ualbino, pamoja na kupinga ubaguzi, unyanyapaa na vitendo vyote vya ukatili vinavyokiuka haki zao za msingi.
Pia maadhimisho hayo yanakumbusha wajibu wa pamoja wa kujenga jamii inayoheshimu utu, usawa na haki za kila mwanadamu bila kujali tofauti zake za kimaumbile.
“TRAMEPRO inatoa pongezi kwa Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS), Albinism Sports Club, Serikali, Bunge, wataalamu wa tiba asili, wadau wa afya, elimu, michezo na mazingira pamoja na wanachama wote wa TRAMEPRO kwa mchango wao katika kuimarisha ustawi, usalama na maendeleo ya watu wenye ualbino nchini.”
Wakati huo huo Mwalongo ametumia maadhimisho hayo kueleza wanatambua na kupongeza mechi ya kirafiki iliyochezwa Juni 6,2026 kati ya Bunge Sports Club na Albinism Sports Club, ambayo imeendelea kuwa mfano bora wa matumizi ya michezo katika kuhamasisha ushirikishwaji, mshikamano, uelewa na mapambano dhidi ya ubaguzi kwa watu wenye ualbino.
Tukio hilo limeonesha michezo ni nyenzo muhimu ya kuunganisha jamii na kuimarisha mshikamano wa kitaifa.Tunatoa shukrani za dhati kwa viongozi wa Bunge Sports Club, Waheshimiwa Wabunge na wadau wote walioshiriki kufanikisha tukio hilo muhimu.
Aidha, wanaguswa na moyo wa upendo, utu na kujali uliooneshwa na Salma Kikwete, ambaye baada ya kuguswa na hali halisi ya baadhi ya wachezaji wa Albinism Sports Club alionesha moyo wa kuwafariji na kuwasaidia. Kitendo hicho ni mfano wa kuigwa katika kujenga jamii yenye huruma, mshikamano na usawa.
“Pia tunatoa shukrani kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)kwa kuwezesha upatikanaji wa miche iliyotumika katika zoezi hilo. Mchango huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za Serikali, mashirika ya kiraia na wananchi katika kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”
Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma, ameishauri Serikali kupitia upya masharti mapya yanayowataka madereva walioko kazini kufanyiwa mafunzo na mitihani upya ili kuhuisha leseni zao, akisema utaratibu huo unaweza kuhatarisha ajira na maisha ya maelfu ya wananchi wanaotegemea udereva kama chanzo cha kipato.
Akichangia mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali bungeni, Musukuma amesema kuna madereva wengi nchini ambao wamefanya kazi kwa zaidi ya miaka 30 bila kusababisha ajali kubwa, hivyo hawapaswi kulazimishwa kurudi darasani na kufanya mitihani inayoweza kuwaondoa kazini.
Amesema utekelezaji wa masharti hayo mapya unaweza kuwaongezea mzigo mkubwa madereva wenye kipato cha chini, ambao tayari wanakabiliwa na changamoto za kifamilia na maisha ya kila siku yanayotegemea mshahara wao wa kila mwezi.
Mbunge huyo pia ametumia nafasi hiyo kuikosoa Serikali kuhusu baadhi ya miradi ya maendeleo, hususan ujenzi wa masoko na stendi za kisasa, akidai kuwa baadhi ya miradi hiyo haitimizi mahitaji halisi ya wananchi katika maeneo husika.
Katika hoja nyingine, Musukuma amepinga matumizi makubwa ya fedha za umma katika maonesho, mikutano na warsha za watumishi wa umma, akisema shughuli hizo zinagharimu Serikali fedha nyingi kupitia safari, malazi na posho, fedha ambazo angependa zielekezwe zaidi kwenye huduma za maendeleo.
Badala yake, ameshauri Serikali kuimarisha matumizi ya teknolojia za mawasiliano, ikiwemo mikutano ya mtandaoni, ili kupunguza gharama zisizo za lazima na kuongeza ufanisi katika utendaji wa shughuli za serikali.
📍Dodoma
Tume ya Madini imeanza kutoa elimu kwa wananchi kuhusu sekta ya madini katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu rasilimali madini na fursa zinazotokana na sekta hiyo.
Maonesho hayo yaliyoanza leo Juni 16, 2026 yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 23, 2026, yakikutanisha taasisi mbalimbali za umma kwa lengo la kuonesha huduma wanazotoa kwa wananchi chini ya kaulimbiu isemayo, “Kuchochea Uwajibikaji kwa Huduma Endelevu.”
Kupitia banda lake, Tume ya Madini inatoa elimu kuhusu aina mbalimbali za madini yanayopatikana nchini, mchango wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa taifa, pamoja na fursa za uwekezaji, ajira na ushiriki wa wananchi katika shughuli za uchimbaji na biashara ya madini.
Aidha, wananchi wanaotembelea banda la Tume wanapata fursa ya kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi kwa wadau wa sekta ya madini, sambamba na kupata ufafanuzi kuhusu taratibu na miongozo inayosimamia shughuli za madini nchini.
Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho Juni 17, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.
Wananchi wamehimizwa kutembelea mabanda mbalimbali ili kujionea huduma zinazotolewa na taasisi za umma na kupata elimu itakayowawezesha kunufaika na fursa zilizopo katika sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo sekta ya madini.





.jpeg)
.jpeg)

















.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)


.jpeg)

