-Waziri Mkuu asema anatosha, kiti kimempata mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais.


BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo (Ijumaa, Agosti 28, 2026) limemthibitisha Mheshimiwa Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Ndejembi amepitishwa kwa asilimia 100 ya kura zote 324 zilizopigwa na waheshimiwa wabunge, ambapo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani aliyoionesha kwake kwa kumteua kuwa Makamu wa Rais na katika nafasi nyingine mbalimbali za uongozi.

Pia Mheshimiwa Ndejembi amelishukuru Bunge kwa imani kubwa waliyompa kiasi cha kumpigia kura kwa asilimia mia moja.

Mapema akiwasilisha hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Mheshimiwa Deogratius Ndejembi anatosha na ni mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais katika nafasi ya Makamu wa Rais,

akiitaja kuwa ni nafasi yenye dhamana na majukumu makubwa katika uongozi wa nchi.

"Majukumu hayo yanahitaji mtu mwenye uzoefu wa uongozi, uelewa mpana wa shughuli za Serikali, uwezo wa kufanya kazi kwa karibu na Rais, busara katika kushughulikia masuala ya kitaifa, pamoja na uwezo wa kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Serikali," amesema Dkt. Mwigulu.

"Mheshimiwa Rais amemteua Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, uzoefu alioujenga katika uongozi wa kisiasa na katika nafasi mbalimbali za Serikali," ameongeza Waziri Mkuu.

Dkt. Mwigulu amesisitiza kuwa uzoefu wa uongozi alionao Mheshimiwa Deogratius Ndejembi unadhihirisha kuwa ni mtu sahihi kutumikia wadhifa wa Makamu wa Rais.

"Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi si mgeni katika uongozi wa Umma na katika siasa za nchi yetu. Kabla ya kuwa Mbunge, Mheshimiwa Ndejembi alihudumu kama Mkuu wa Wilaya katika Wilaya ya Kongwa. Mheshimiwa Spika, baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge, Mheshimiwa Ndejembi ameendelea kuaminiwa na Mheshimiwa Rais na kupewa majukumu mbalimbali ndani ya Serikali."

"Amehudumu katika nafasi ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa; Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu; Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kuhudumu kama Waziri wa Nishati," ameongeza Waziri Mkuu.

Dkt. Mwigulu amesema katika kipindi ambacho amehudumu ndani ya Serikali, Mheshimiwa Ndejembi ameonesha uwezo wa kubeba majukumu mbalimbali na kufanya kazi katika sekta zenye mahitaji na changamoto zinazotofautiana, akisisitiza kuwa uzoefu huo ni muhimu kwa Makamu wa Rais ambaye, kwa nafasi yake, anatakiwa kuwa tayari kumsaidia Rais katika masuala mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano na kutekeleza majukumu yoyote atakayokabidhiwa kwa mujibu wa Katiba.

"Kwa kuzingatia majukumu ya Kikatiba ya Makamu wa Rais niliyoyaeleza, pamoja na uzoefu wa kisiasa, kiutawala na kiutendaji wa Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi, Serikali inaamini kuwa ana uwezo wa kutekeleza kwa uaminifu na ufanisi majukumu ya nafasi ya Makamu wa Rais na kumsaidia Mheshimiwa Rais katika kuendeleza shughuli za Serikali na maendeleo ya Taifa letu," amefafanua Dkt. Mwigulu.













MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imepokea jumla ya mawazo 9,545 ya ubunifu kutoka kwa wananchi ikiwa ni awamu ya pili ya mpango wa mawazo ya ubunifu, katika mchakato wa uchambuzi na tathmini ya mawazo ili kuwapata washindi 1020.

Mwenyekiti wa Kamati Huru ya Tathmini ya Wazo Bunifu, Zawadia Nanyaro amesema hayo leo Agosti 28, 2026.

Zawadia ameeleza kuwa awamu ya kupokea mawazo hayo ilizinduliwa Aprili Mosi, 2026 na kufungwa Julai 31, 2026 huku jumla ya wananchi 13,096 wakijisajili katika Mfumo wa Usimamizi wa Mawazo ya Ubunifu, ambapo mawazo 9,545 yaliwasilishwa.

Ameongezea kuwa Idadi hiyo imeongezeka kwa takribani asilimia 68 ikilinganishwa na mawazo 5,681 yaliyowasilishwa katika Awamu ya Kwanza.

Amefafanua kuwa mchakato huo wa uchambuzi na tathmini unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba 2026.

"Katika mchakato huo, mawazo 1,020 yatakayofikia hatua ya tathmini ya kina yatapata fursa ya kushindania zawadi mbalimbali, ambapo mshindi wa kwanza atapata shilingi milioni 50, washindi wawili wa nafasi ya pili watapata shilingi milioni 30 kila mmoja, washindi wawili wa nafasi ya tatu watapata shilingi milioni 20 kila mmoja na washindi 15 wa nafasi ya nne watapata shilingi milioni 10 kila mmoja". Amesema.

Ameongeza kuwa mawazo 1,000 yatakayobakia yatazawadiwa Shilingi 100,000 kila moja, pamoja na kutambuliwa kwa kupatiwa Cheti cha Ushiriki.

Aidha, amesisitiza kuwa mpango huo haujajikita katika kutoa zawadi pekee, bali unalenga kubaini na kuendeleza mawazo yenye uwezo wa kutatua changamoto halisi na kuleta maboresho yanayoonekana katika usimamizi wa kodi, utoaji wa huduma na ufanisi wa Mamlaka.




Wakulima wa mahindi nchini wametahadharishwa dhidi ya kutumia mbegu zisizothibitishwa ubora, wakihimizwa kuhakikisha mbegu wanazonunua zimehakikiwa kabla ya kuzipanda ili kuepuka hasara na kupunguza hatari ya kupata mavuno duni.

Tahadhari hiyo imetolewa na Bayer Tanzania kupitia kampeni yake ya kitaifa ya uhamasishaji kwa wakulima inayolenga kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kutumia na kuhakiki mbegu halisi kabla ya msimu wa kilimo.

Kampeni hiyo inayojulikana kama “DEKALB Mafanikio Shambani” imeendelea Mkoani Morogoro baada ya kuzinduliwa mapema mwezi huu, ikiwa na lengo la kuwafikia wakulima katika maeneo mbalimbali nchini na kuwapatia elimu kuhusu mbegu bora na suluhisho za kisasa za kilimo.

Mkurugenzi wa Bayer Tanzania, Sango Mwinyi, alisema matumizi ya mbegu zisizothibitishwa yanaweza kuwaweka wakulima katika hatari ya kupoteza uwekezaji wao, hasa katika kipindi ambacho kilimo kinakabiliwa na changamoto zinazotokana na mabadiliko ya tabianchi na hali ya hewa isiyotabirika.

“Wakulima wanapaswa kuwa makini wanaponunua mbegu na kuhakikisha wanazihakiki kabla ya kupanda. Bila kupata taarifa sahihi na kufanya uhakiki, wakulima wanaweza kununua na kupanda mbegu zisizo sahihi na hatimaye kupoteza sehemu kubwa ya uwekezaji wao kutokana na mavuno duni,” alisema Mwinyi.

Alisema wakulima wadogo, ambao ni sehemu muhimu ya mfumo wa chakula nchini, wanahitaji kupata taarifa sahihi ili kufanya maamuzi sahihi kuhusu pembejeo wanazotumia katika mashamba yao.

Kwa mujibu wa Mwinyi, mabadiliko ya tabianchi yameongeza umuhimu wa wakulima kutumia mbegu zilizothibitishwa na zinazofaa kwa mazingira husika ili kuongeza uwezekano wa kupata mavuno yenye uhakika.

“Wakulima wadogo wanaendelea kukabiliwa na changamoto kubwa zinazotokana na mabadiliko ya tabianchi na hali ya hewa isiyotabirika. Katika mazingira haya, matumizi ya mbegu zilizothibitishwa ni muhimu zaidi kwa sababu zinawasaidia wakulima kuongeza tija na kujenga ustahimilivu wa kilimo,” alisema.

Kupitia kampeni hiyo, Bayer inahamasisha matumizi ya aina tano za mbegu chotara za mahindi za DEKALB, ambazo zimetengenezwa kwa kuzingatia maeneo mbalimbali ya kilimo nchini, ikiwemo maeneo yenye mvua chache na yale yenye uwezo mkubwa wa uzalishaji.

Mbali na elimu kwa wakulima, kampeni hiyo pia imeambatana na promosheni yenye zawadi mbalimbali kwa wakulima wanaonunua na kuhakiki mbegu halisi za DEKALB. Zawadi hizo ni pamoja na pampu za kunyunyizia dawa za mgongoni, simu janja, mashine za kupandia mahindi zinazoendeshwa kwa mkono, pikipiki, mifumo ya umeme wa jua na mashine za kumenya mahindi.

Aidha, wakulima wawili watakaobahatika watajishindia gari aina ya Toyota pick-up kila mmoja mwishoni mwa kampeni hiyo.

Ili kushiriki, wakulima wanatakiwa kununua mbegu za DEKALB kutoka kwa wauzaji wa pembejeo walioidhinishwa, kisha kukwangua kibandiko cha TOSCI kilichopo kwenye kifungashio ili kupata namba ya kipekee ya uhakiki.

Baada ya hapo, mkulima anatakiwa kupiga *148*52# na kuingiza namba ya uhakiki yenye tarakimu 12. Baada ya mbegu kuthibitishwa, mkulima atapokea ujumbe mfupi wa uthibitisho na kuingizwa moja kwa moja kwenye droo ya promosheni.

Mwinyi, ambaye pia ni Kiongozi wa Biashara ya Sayansi ya Mazao nchini Tanzania katika Bayer East Africa, alisema kampeni hiyo inalenga zaidi kumwezesha mkulima kufanya uamuzi sahihi kabla ya kuwekeza katika uzalishaji.

“Kila msimu wa kilimo ni uwekezaji mkubwa kwa kaya za wakulima. Hivyo, kuhakikisha mbegu ni halisi na zenye ubora kabla ya kupanda ni hatua muhimu ya kulinda uwekezaji huo. Tunawahamasisha wakulima wasinunue mbegu kwa kuangalia bei pekee, bali wahakikishe pia uhalali na ubora wake kabla ya kupanda,” alisisitiza.

Kampeni ya DEKALB Mafanikio Shambani inatarajiwa kudumu kwa miezi minne, ikilenga kuongeza uelewa miongoni mwa wakulima kuhusu umuhimu wa kutumia mbegu zilizothibitishwa, kuongeza tija ya kilimo na kuchangia katika kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Mkurugenzi wa Bayer Tanzania Sango Mwinyi ( mwenye namba 8) akiwa kwa picha ya pamoja na wadau wa mbegu kutoka Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) na wakulima wa mkoa wa morogoro, pamoja na wauza pembejeo kutoka Morogoro wakati wa uzinduzi wa kampeni yake ya kitaifa ya uhamasishaji kwa wakulima ili kuwaongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kutumia na kuhakiki mbegu halisi kabla ya msimu wa kilimo inayofahamika kama “DEKALB Mafanikio Shambani’’. Uzinduzi huo umefanyika katikati ya wiki hii.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar imeupongeza Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kazi kubwa inayofanya katika kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za bima ya afya nchini, pamoja na ushirikiano wake na Mfuko wa Huduma za Afya Zanzibar (ZHSF).

Pongezi hizo zimetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mariam Hamis Said, wakati Kamati hiyo pamoja na Menejimenti za ZHSF na NHIF ilipotembelea Makao Makuu ya NHIF kwa ajili ya kujifunza namna Mfuko huo unavyoendesha na kutoa huduma kwa wanachama.

Mhe. Mariam amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa, kwa kuwa Kamati imepata fursa ya kuelezwa na kujionea kwa vitendo mifumo na huduma zinazotolewa na NHIF, kupitia ziara kwenye Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH).

Pamoja na kutoa pongezi kwa NHIF, Kamati hiyo ilipata fursa ya kutaka kufahamu kwa kina masuala mbalimbali yanayohusu uendeshaji na maendeleo ya Mfuko, ikiwemo namna NHIF inavyopambana na udanganyifu, utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, pamoja na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wanachama wanapata huduma bora na kwa wakati.

Aidha, Kamati ilitaka kufahamu namna matumizi ya TEHAMA yameboresha utendaji wa NHIF na kusaidia kupunguza gharama za uendeshaji, pamoja na namna uwekezaji unavyosaidia kuimarisha Mfuko.

Masuala mengine yaliyotiliwa mkazo ni pamoja na vyanzo vya mapato ya Mfuko, viashiria vinavyotumika kupima mafanikio na uendelevu wa NHIF, pamoja na mafunzo na uzoefu ambao Mfuko umeupata katika kipindi cha miaka 25 ya utekelezaji wa majukumu yake.

Amesema ushirikiano kati ya NHIF na ZHSF umeleta matokeo makubwa katika hatua mbalimbali za uanzishaji na uendelezaji wa ZHSF, huku akieleza kuwa uzoefu na msaada uliotolewa na NHIF umeiwezesha Zanzibar kuanza na kuendelea vizuri katika safari ya kuimarisha huduma za bima ya afya.

“Kamati inapongeza NHIF na ZHSF kwa mashirikiano makubwa wanayoyafanya ambayo yamewezesha ZHSF kuanza na kuendelea vizuri,” amesema Mhe. Mariam.

Ameongeza kuwa kazi iliyofanywa na NHIF katika kusaidia uanzishaji wa ZHSF ilihitaji uvumilivu na kujitolea kwa kiwango kikubwa, akieleza kuwa Zanzibar imenufaika na uzoefu wa NHIF katika kujenga mfumo wa bima ya afya.

“Kazi iliyofanywa na NHIF ni kazi iliyofanyika kwa uvumilivu mkubwa, lakini kwa kutubeba Zanzibar katika uanzishaji wa Mfuko wetu,” amesema.

Aidha, Mhe. Mariam ameipongeza Menejimenti ya NHIF kwa kuwawezesha kutembelea Hospitali ya Benjamin Mkapa, ambako wamejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa.

Amesema ziara hiyo imewapa fursa ya kuona kwa vitendo ubora wa huduma zinazotolewa, hususan huduma za kibingwa na kibingwa bobezi, ambayo ni mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha huduma za afya nchini.

“Tumejionea namna wanachama wa NHIF wanavyopokelewa na kuhudumiwa. Hakika kazi hii ni kubwa na nzuri ambayo kwa ujumla tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, ambapo huduma za kibingwa na kibingwa bobezi zinapatikana hapa nchini,” amesema. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, amesema Mfuko utaendelea kushirikiana kwa karibu na ZHSF ili kuhakikisha wananchi na wanachama wanapata huduma bora za afya kwa wakati na kwa ufanisi.

Dkt. Isaka amesema NHIF itaendelea kutoa ushirikiano unaohitajika kwa ZHSF, hususan katika maeneo ya uzoefu, mifumo ya utoaji huduma na masuala mengine ya kitaalamu, kwa lengo la kuimarisha huduma za bima ya afya kwa wananchi wa Zanzibar.

Amesema ushirikiano huo ni sehemu ya dhamira ya NHIF ya kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa wananchi popote walipo nchini, huku mifuko hiyo ikiendelea kujifunza na kubadilishana uzoefu katika kuboresha huduma kwa wanachama.

Ziara hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu baina ya taasisi zinazohusika na utoaji wa huduma za bima ya afya Tanzania Bara na Zanzibar.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa!
Na Janeth Raphael - Michuzi Tv Bungeni Dodoma


Wakati Bunge limepitisha jina la Makamu wa Rais Mteule, Deogratius John Ndejembi, Mbunge wa Nzega Mjini Hussein BASHE amesema Ndejembi ni kiongozi mwenye uzoefu, nidhamu na uwezo wa kuunganisha watu, huku Watanzania wakihimizwa kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake mapya.

Akizungumza katika kikao cha Mbunge wa Nzega Mjini amesema uteuzi huo wa Ndejembi ni zao la Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye amelelewa ndani ya chama hicho na kufahamu vyema misingi, dhamana na wajibu wa chama kwa Taifa.

Amesema Ndejembi amekuwa ndani ya CCM kwa muda mrefu na amelelewa katika misingi ya kuheshimu viongozi na kutekeleza majukumu aliyopewa kwa nidhamu na uaminifu.

“Deo ni zao la Chama Cha Mapinduzi. Ni mtu aliyetokana na CCM na siyo aliyepita tu ndani ya chama. Anafahamu misingi ya chama, dhamana ya chama hiki na wajibu wake kwa Taifa,” amesema.

Aidha, ameeleza kuwa Ndejembi ni miongoni mwa wajumbe wachache ndani ya Baraza Kuu ambao wamekuwa na uwezo wa kuwakutanisha pande zinazotofautiana na kuzifanya zisikilize hoja kwa lengo la kutafuta suluhu.

“Deo ni mjumbe miongoni mwa wachache ambao pande mbili zinapokuwa zinavutana, ana uwezo wa kukutana na pande zote mbili, zikamsikiliza. Anafahamu misingi ya chama na amelelewa kwa misingi ya kuheshimu viongozi na walio juu yake,” amesema.

Kwa upande mwingine, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaamini vijana waliotokana na Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na kuwapa nafasi za kushika dhamana kubwa za uongozi.

Amesema hakuna wasiwasi kuhusu uwezo, tabia, nidhamu na uzoefu wa Ndejembi, akisisitiza kuwa uteuzi huo umefika katika wakati wake.

“Ombi letu ni moja; hatuna wasiwasi juu ya uwezo wake, tabia yake, nidhamu yake na uzoefu wa kujifunza. Ni mvumilivu. Mwenyezi Mungu humuandikia kila mtu kwa wakati wake,” amesema.

Ameongeza kuwa dhamana aliyopewa Ndejembi inakuja katika kipindi ambacho Taifa linahitaji mshikamano, hivyo Watanzania wanapaswa kumpa moyo, kumuombea na kumpa ushirikiano ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Amesema Tanzania imepitia changamoto mbalimbali huko nyuma na kwamba ili kukabiliana na changamoto zinazoikabili nchi, Watanzania wanapaswa kuwa kitu kimoja na kuwaunga mkono viongozi wao.

“Jambo la msingi tumpe ushirikiano. Amepewa dhamana katika nyakati ngumu na ni tofauti na nyakati nyingine zote katika nchi yetu. Anahitaji kupewa moyo, anahitaji kuombewa,” amesema.

Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kudumisha umoja na mshikamano, akisisitiza kuwa Tanzania ni moja na hakuna Taifa jingine kwa Watanzania.

“Taifa letu limetoka kwenye changamoto kubwa sana huko nyuma. Tuna Taifa moja, tuunganeni sote kuwaunga mkono viongozi wetu ili tuweze kukabiliana na changamoto zinazolikabili Taifa letu. Kila nyakati zinapitia changamoto zake na kila nyakati Mungu huwapatia viongozi wake,” amesema.

Amehitimisha kwa kuwataka Watanzania kuwasaidia viongozi waliopo madarakani katika kukabiliana na changamoto za Taifa na kujenga Tanzania yenye umoja, akisisitiza kuwa Mungu amewapa Watanzania viongozi hao kwa wakati huu.

“Tuwaunge mkono viongozi wetu ili tukabiliane na changamoto za Taifa letu na tuweze kujenga Taifa moja, kwa sababu hatuna Tanzania nyingine zaidi ya hii. Leo Tanzania hii Mungu ametupa viongozi hawa,” amesema.




LEO Ijumaa, Agosti 28, 2026, saa 22:00 usiku, Crystal Palace watapambana na Manchester City katika uwanja wao wa nyumbani wa Selhurst Park. Mechi hii ni sehemu ya wiki ya pili ya msimu wa Ligi Kuu Uingereza (Premier League), na inatarajiwa kuwa na mvuto mkubwa kutokana na hali tofauti za timu hizi mbili tangu mwanzo wa msimu.

Crystal Palace wanaingia kwenye mechi hii wakiwa na hali ngumu baada ya kufungwa 2-0 dhidi ya Everton katika mechi ya kwanza ya msimu, kwa mabao ya Kiernan Dewsbury-Hall na Thierno Barry katika kipindi cha kwanza. Timu ya Pierre Sage kwa sasa iko nafasi ya 16 kwenye msimamo bila pointi yoyote, hivyo watahitaji kuonyesha nguvu mbele ya mashabiki wao ili kuanza kukusanya pointi.

Kwa upande wa Manchester City, timu inaongozwa sasa na Enzo Maresca, akichukua nafasi baada ya kipindi cha Pep Guardiola. City waliingia msimu huu kwa ushindi wa kusisimua dhidi ya Bournemouth, ambapo walifunga mabao mawili ya mwisho kupitia Marc Guéhi (dakika ya 83) na Joško Gvardiol (dakika ya 90) kugeuza matokeo kutoka kufungwa na kuibuka washindi 2-1. Kwa sasa City wako nafasi ya saba wakiwa na pointi tatu.

Kuhusu mifumo inayotarajiwa kuchezea, Crystal Palace wanatarajiwa kuwa na muundo wa 3-4-2-1 ukiongozwa na Dean Henderson kwenye lango, huku Jean-Philippe Mateta akitarajiwa kubeba jukumu la ushambuliaji mstari wa mbele.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema. Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Manchester City nao wanatarajiwa kutumia muundo wa 4-2-3-1, huku Erling Haaland akiwa mchezaji wa kutegemewa mbele na Phil Foden pamoja na Antoine Semenyo wakimsaidia. Ni muhimu kutambua kuwa Chadi Riad wa Palace na Jérémy Doku wa City wote hawatashiriki kutokana na majeraha.

Kihistoria, Manchester City wamekuwa wakiitawala Crystal Palace, ambapo rekodi ya jumla ya mechi zao za awali inaonyesha ushindi 20 kwa City, ushindi 4 kwa Palace, na sare 5. Msimu uliopita pia City walishinda mara mbili kwa bao 3-0, jambo linaloonyesha pengo kubwa la ubora kati ya timu hizi mbili.

 


KAMPUNI ya Bayer Tanzania imeendelea na kampeni ya kitaifa ya uhamasishaji kwa wakulima, inayolenga kuwahamasisha wakulima wa mahindi kuhakiki mbegu zilizothibitishwa kabla ya kupanda, ili kuongeza tija, kuimarisha usalama wa chakula na kujenga ustahimilivu wa kilimo.


Akizungumza katika kampeni hiyo mkoani Morogoro, Mkurugenzi wa Bayer Tanzania, Sango Mwinyi, amesema wakulima wadogo wanahitaji kupata taarifa sahihi kuhusu mbegu bora na zilizothibitishwa ili kuepuka hasara na kuongeza uzalishaji.


Mwinyi amesema mabadiliko ya tabianchi na hali ya hewa isiyotabirika yanaendelea kuwa changamoto kwa wakulima, hivyo matumizi ya mbegu zilizothibitishwa ni muhimu katika kuongeza tija na ustahimilivu wa kilimo.


Amesema kampeni hiyo inayojulikana kama “DEKALB Mafanikio Shambani” itadumu kwa miezi minne na inalenga kuhamasisha matumizi ya aina tano za mbegu chotara za mahindi za DEKALB, zinazolenga mazingira mbalimbali ya kilimo nchini.


Aidha, Bayer imeanzisha promosheni yenye zawadi mbalimbali kwa wakulima watakaonunua mbegu halisi, ikiwemo pampu za kunyunyizia, simu janja, mashine za kupandia mahindi, pikipiki, mifumo ya umeme wa jua na mashine za kumenya mahindi.


UKO tayari kuingia kwenye safari mpya ya burudani yenye msisimko, bahati na nafasi ya ushindi? Thunder Riches: Fortune Eagle imewasili rasmi, ikiwa ni mchezo mpya kabisa kutoka Games Global unaopatikana kwa kipekee kupitia Meridianbet. Hapa si suala la kucheza tu, bali ni kuikaribisha bahati yako na kumruhusu tai wa Fortune Eagle kutandaza mabawa yake huku akikuongoza kwenye ulimwengu wa kusisimua wenye fursa za ushindi.

Kinachoufanya Thunder Riches: Fortune Eagle kuwa wa kipekee ni safari yake inayokualika kugundua kile ambacho bahati imekuandalia. Tai wa bahati anapotandaza mabawa yake, msisimko unapanda na kila hatua inakuwa sehemu ya safari yako ya kutafuta utajiri. Mchezo huu umeletwa kwa mtindo unaolenga kuwapa wachezaji burudani mpya, huku Meridianbet ikiwa imeufanya upatikane kwa wateja wake pekee.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Na sasa, usibaki kuwa mtazamaji wakati wengine wakigundua burudani hii mpya. Jisajili Meridianbet, ingia kwenye kasino ya Thunder Riches: Fortune Eagle na anza kucheza sasa. Tai wa bahati tayari ameshatandaza mabawa yake, na safari yako inaanzia hapa. Kila mchezaji ana nafasi ya kufurahia uzoefu huu mpya huku akigundua ni wapi bahati inaweza kumpeleka.

Kwa wapenzi wa burudani za kasino wanaopenda vitu vipya, Fortune Eagle ni jina la kulifuatilia. Ni fursa ya kuachana na mazoea na kujaribu mchezo mpya ambao umeletwa moja kwa moja kutoka Games Global. Meridianbet inakupa nafasi ya kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuupitia na kujionea mwenyewe kile ambacho tai huyu wa bahati amekibeba.

Thunder Riches: Fortune Eagle imefika, na mabawa ya bahati yako yanaweza kuanza kutandazwa leo. Jisajili Meridianbet, chagua mchezo na ucheze ili kugundua dunia mpya ya burudani na msisimko. Bahati inaweza kukupeleka mbali zaidi ya unavyotarajia.

Vodacom Tanzania PLC kupitia programu ya Classroom for Community Impact iliyo chini ya Vodacom Tanzania Foundation imekabidhi madarasa mawili yaliyokarabatiwa, madawati 30 pamoja na vifaa muhimu vya shule kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihowanja, wilayani Malinyi mkoani Morogoro, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za msingi za umma.

Makabidhiano hayo yaliyofanyika jana yanalenga kuchangia uboreshaji wa miundombinu na mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi, hususan wenye mahitaji maalum.

Kupitia mpango huo, katika awamu hii Vodacom Tanzania imekarabati na kujenga jumla ya madarasa sita pamoja na kutoa madawati 90 katika shule tatu za msingi za umma za Vikindu, wilayani Mkuranga mkoani Pwani; Ihowanja, Malinyi mkoani Morogoro na Mahilo, wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Katika Shule ya Msingi Ihowanja, msaada huo umehusisha ukarabati wa ujenzi wa madarasa mawili na utoaji wa madawati 30. Aidha, wanafunzi wamepatiwa mahitaji muhimu ya shule, ikiwemo madaftari, chupa za kubebea maji, kalamu na mabegi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania PLC, Chiha Nchimbi, alisema mpango huo ni sehemu ya mchango wa kampuni katika kusaidia jamii na kuboresha mazingira ambayo watoto wanapata elimu.

Alisema uwepo wa madarasa salama, madawati ya kutosha na mazingira rafiki ya kujifunzia ni muhimu katika kuwawezesha wanafunzi hasa wenye mahitaji maalum, kushiriki kikamilifu katika masomo yao.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ihowanja, Iddy Mgonja aliishukuru Vodacom Tanzania kwa msaada huo, akisema utakuwa na mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia shuleni hapo, hasa kwa kupunguza changamoto ya upungufu wa madarasa na madawati.

Mgonja alisema ukarabati wa madarasa mawili pamoja na kupatiwa madawati 30 na vifaa muhimu vya shule kutawawezesha wanafunzi kupata mazingira salama na rafiki zaidi ya kujifunzia, huku walimu wakipata mazingira bora ya kutekeleza majukumu yao ya kufundisha.

Kwa upande wa serikali na uongozi wa jamii, makabidhiano hayo yalishuhudiwa na Diwani wa Kata ya Kilosampepo, Boniventure Killian Mwanga, pamoja na Mtendaji wa kijiji cha Ihowanja, Gotard Garus Mitti pamoja na viongozi na wadau wengine wa elimu.

Viongozi hao wamepongeza uwekezaji huo wakisema utasaidia kupunguza changamoto za miundombinu ya elimu na kuweka mazingira bora na salama zaidi kwa wanafunzi na walimu. Wamesisitiza kuwa ushirikiano kati ya sekta binafsi, serikali na jamii ni muhimu katika kuharakisha upatikanaji wa miundombinu bora na jumuishi ya elimu, hususan kwa watoto wenye mahitaji maalum.

Mpango wa Classroom for Community Impact ni sehemu ya jitihada za Vodacom Tanzania kupitia Vodacom Foundation za kushirikiana na jamii katika kuboresha mazingira ya elimu na kusaidia kujenga mazingira jumuishi zaidi ya kufundishia na kujifunzia kwa watoto nchini.

Mkuu wa Kanda ya Kati wa Vodacom Tanzania PLC, Chiha Nchimbi (kulia), akikabidhi dawati kwa Diwani wa Kata ya Kilosampepo, Boniventure Killian Mwanga (kushoto), dawati hilo ni mojawapo ya madawati 30 yaliyokabidhiwa katika Shule ya Msingi Ihowanja, Malinyi mkoani Morogoro, kupitia mpango wa Classroom for impact ulioko chini ya Vodacom Tanzania Foundation. Kupitia mpango huo, Vodacom Tanzania imekarabati na kujenga madarasa sita pamoja na kutoa madawati 90 katika shule tatu za msingi za umma za Vikindu (Mkuranga - Pwani), Ihowanja (Malinyi - Morogoro) na Mahilo (Ruvuma) kwa lengo la kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, hususan kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika Shule ya Msingi Ihowanja, wilayani Malinyi mkoani Morogoro. Wengine katika picha ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ihowanja, Iddy Mgonja (wa pili kushoto), na Mtendaji wa kijiji cha Ihowanja, Gotard Garus Mitti (wa pili Kulia).

Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakitayarisha mahitaji ya shule, ikiwemo madaftari, mabegi na kalamu kwa ajili ya kutoa msaada kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihowanja, Malinyi-mkoani Morogoro wakati wa hafla ya makabidhiano ya madarasa mawili na madawati 30 yaliyofanyika shuleni hapo kupitia Vodacom Tanzania Foundation. Msaada huo unalenga kuwapa wanafunzi vifaa muhimu vya kujisomea, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya kampuni hiyo kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia yanaenda sambamba na upatikanaji wa vifaa vya elimu kwa watoto.

Baadhi ya vikapu vyenye mahitaji muhimu ya shule kwa ajili ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihowanja, iliyoko wilaya ya Malinyi, mkoani Morogoro, vikiwemo madaftari, chupa ya maji, kalamu, soksi na mabegi, vikiwa tayari kwa ajili ya kugawiwa kwa wanafunzi. Vifaa hivyo vilitolewa na Vodacom Tanzania PLC sambamba na makabidhiano ya madarasa mawili na madawati 30 yaliyofanyika shuleni hapo, chini ya mpango wa kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, hususan kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Ihowanja, Malinyi-mkoani Morogoro, wakiwa katika baadhi ya madawati yaliyotolewa na Vodacom Tanzania Foundation ndani ya moja ya madarasa yaliyokarabatiwa kupitia mpango unaolenga kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi. Kupitia mpango huo, Vodacom Tanzania Plc imekarabati na kujenga madarasa sita pamoja na kutoa madawati 90 katika shule tatu za msingi za umma za Vikindu (Pwani), Ihowanja (Morogoro) na Mahilo (Ruvuma).

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwajulisha wananchi na walipakodi wote kuwa ofisi zake katika mikoa yote nchini zitakuwa wazi kesho, Jumamosi, tarehe 29 Agosti 2026 Kuanzia saa 2:30 asubuhi mpaka saa 11 jioni kwa ajili ya kutoa huduma za kikodi.

Wananchi na walipakodi wote mnakaribishwa kufika katika ofisi ya TRA iliyo karibu nawe kupata huduma mbalimbali . Pamoja tunajenga Taifa Letu.



Serikali ya Tanzania na Ujumbe wa Mabalozi wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Akiongea baada ya kikao hicho, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Kitila Mkumbo, amesema pande zote mbili zimejadili hatua zilizofikiwa katika kuboresha masuala ya sheria, kodi, utaratibu na urasimu unaowakabili wawekezaji.


"Kumetokea maendeleo katika kuboresha mazingira ya uwekezaji. Tumejadili pia hatua zaidi za kuchukua ili kuwavutia wawekezaji zaidi kutoka Umoja wa Ulaya kuja kuwekeza hapa Tanzania," amesema Waziri Mkumbo.

Ameongeza kuwa Serikali inatekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu kutoa kipaumbele kwa sekta ya kilimo ili kuongeza thamani ya mazao na kuvutia uwekezaji zaidi katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa Waziri Mkumbo, mazungumzo kama haya yamekubaliwa kufanyika kila baada ya miezi sita. Kikao kinachofuata kimepangwa kufanyika tarehe 20 Februari 2027



Farida Mangube Morogoro 

Serikali imewataka watanzania   kuitumia vizuri fursa  ya Tanzania kuwa mwenyeji  wa  mashindano ya AFCON 2027 kwa kutangaza   tamaduni za makabila mbalimbali  kama sehemu ya vivitio adimu vinavyopatikananchini humo  sambamba na  kufanya vizuri kwenye michezo hiyo.

Kauli hiyo Imetolewa na  Mkuu wa Mkoa  Morogoro,Adam Malima  wakati akifungua Tamasha la Nne la Kitaifa la Utamaduni linalofanyika mjini Morogoro  ambapo jumla ya wahiriki 150,000 kutoka mikoa mbalimbali wanaonyesha  tamaduni.zao.

Amesema katika michuano hiyo  licha ya Tanzania kushiriki nchi zingine ni Kenya na Uganda ambazo  zinaendelea na maandalizi ya michezo  hiyo ambapo kwa Tanzania itafanyika Arusha,Dar es salaam na Zanzibar.

Aidha amewataka watanzania kuendelea kuheshimu utamadani kwani bila kuwepo Kwa  utamaduni huwezi kuwa na  heshima.

Naye  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema tamasha Hilo la Kitaifa la Utamaduni lilianzia Mkoani Dar Salaam,likaenda Songwe na Ruvuma na Mwaka huu linafanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumzia kuhusu  michuano ya AFCON  Msigwa amewataka watanzania watanzania  kuachiana  maneno yanaenezwa na baadhi ya watu wasioitakia mema   kwa kueneza uongo kuwa  michuano ya AFCON inayotarajiwa kufanyika mwakani kwa nchi tatu za Tanzania,Kenya na Uganda kuwa Kwa Tanzania imehamishwa sio taarifa za kweli.







Na Janeth Raphael – MichuziTv

Mwalimu wa Shule ya Awali DCT Canon Andrea Mwaka, Rose Isaka, aliyewahi kumfundisha Makamu wa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, mwaka 1986, amemuelezea kiongozi huyo kuwa tangu akiwa mtoto alikuwa na tabia ya furaha, ucheshi, upole na kujali watu waliomzunguka.

Akizungumza kuhusu kumbukumbu zake za kipindi hicho, Rose amesema Ndejembi alikuwa mwanafunzi mwenye nidhamu na tabia njema, aliyependa kushirikiana na wenzake pamoja na kushiriki katika michezo, hususan mpira wa miguu.

“Alikuwa mwanafunzi mzuri sana, mcheshi na mwenye furaha wakati wote. Nimefurahi sana kwa sababu alikuwa ni mwanafunzi wangu,” amesema.

Amesema moja ya matukio ambayo yameendelea kubaki kwenye kumbukumbu yake ni pale Ndejembi alipomsaidia mwanafunzi mwenzake aliyeanguka na kuumia wakati wa michezo.

Kwa mujibu wa Rose, baada ya kuona mwanafunzi huyo ameumia, Ndejembi alimfuata na kumsaidia, jambo ambalo aliliona kama ishara ya kujali na kuwathamini wenzake tangu akiwa katika umri mdogo.

“Alikuwa hana matukio mabaya ya kutisha, hapana. Tukio ninalolikumbuka ni siku ambayo mwanafunzi mwenzake alianguka na kuumia, Ndejembi akaenda kumsaidia na kumhudumia vizuri sana. Hicho ndicho ninachokumbuka mpaka leo,” amesema.

Rose amesema tukio hilo lilimfanya kumtambua Ndejembi kama mtoto mwenye moyo wa kuwajali wengine, akieleza kuwa hulka ya kusaidia na kushirikiana na watu ilionekana wazi tangu utotoni.

Amesema anaamini tabia hizo njema alizokuwa nazo akiwa mtoto zimeendelea kuwa sehemu ya maisha yake hadi sasa, huku akimtakia mafanikio na kumwombea aendelee kuwa kiongozi mwenye moyo wa kuwasaidia wengine.

“Ninamwombea baraka kibao. Ninamwombea kwa Mungu aendelee kuwa mwema. Mungu azidi kumbariki sana na aendelee na tabia yake ileile ya kusaidia watu wote kama alivyokuwa utotoni,” amesema Rose.


Na MWANDISHI WETU


Watoto 1,337,079, wanatarajiwa kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio mkoani Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa mkoa huo, Abdul Mhite, alipozindua kampeni ya chanjo hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dares Salaam, Albert Chalamila leo.

Mhite amesema kampeni hiyo itamalizika Agosti 30 mwaka huu na inalengakuwafiia watoto wote walio chini ya umri wa miaka 10.

Amesema , chanjo hiyo itahusisha watoto ambao pia waliwahi kupata chanjo hiyo awali.

“Tunawataka wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo hii hata kama awali mtoto aliwahi kuchanjwa. Chanjo itatolewa kwa mfumo wa matone,”amesema.

Ameeleza serikali imeandaa kampeni hiyo kwa lengo la kuongeza na kuimarisha kinga ya jamii dhidi ya ugonjwa wa polio kwa kuhakikishawatoto wote walengwa wanafikiwa.

Mhite amebainisha chanjo hiyo itatolewa nyumbakwa nyumba, mtaa kwa mtaa, shuleni, vituo vya afya, zahanati, hospitali , sehemu za ibada, stendi, katika vituo vya kulea watoto, viwanja vya michezo na maeneo mbalimbali katika jamii.

“Nawaomba wazazi na walezi mshirikiae na timu za chanjo zinapofika katika maeneo yenu.Pia muwaruhusu watoto kupata matone ya chanjo hii,”ameeleza Mhite.

Katibu Tawala huyo, ametoa wito kwa viongozi wa halmashauri, serikali za mitaa, viongozi wa dini, walimu , wahamasishaji wa jamii na wadau wote kushiriki kikamilifu katikakampeni hyo ili kufikialengo.

Awali Ofisa wa Wizara ya Afya Mpango wa Chanjo Salama, Zainab Nyamgumi, alisema chanjo hiyo ni muhimu kwa Watoto hata kama waliwahi kuchanjwa awali.

Amesema chanjo hiyo ni muhimu na inaelekezwa na Shiria la Afya Duniani (WHO) kwa nchi kuitumia.

“Hii chanjo inatolewa kama nchi inaonekana inahatari ya mlipuko wa ugonjwa wapolio. Ni chanjo ambayo kwenye ratiba ya kawaida ya utoaji wa chanjo haipo.

Ndiyo mana tunasema hatakama mtoto amekamilisha chanjo lazima na hii chanjo apewe,”amesema Zainab.Alibainisha ni chanjo maalumu ambayo WHO inaelekeza nchi kuitumia pindi kunapo kuwa na hatari hiyo.

“Kwa hiyo hata mtoto ambaye amekamilisha chanjo bado anahatari kama hatapewa hii chanjo iliyopendekezwa na Shirikala Afya Duniani,”amebainisha.

Mganga Mkuu wa Mkoawa Dar es Salaam, Mohamed Mang’una, amehamasisha wazazi, walezi na wananchi. Kuhakikisha Watoto walengwa wanafikiwa na kupata huduma hiyo itakayo tolewa bila malipo.







Top News