TBN Chairman Beda Msimbe speaks during a meeting with a delegation from the Public Service Social Security Fund (PSSSF) on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam


TBN Chairman Beda Msimbe speaks with Mr Abdul Njaidi, delegation leader from the Public Service Social Security Fund (PSSSF), during their meeting on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam.



Mr Abdul Njaidi, delegation leader from the Public Service Social Security Fund (PSSSF), speaks with TBN leadership during their meeting on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam

TBN Trustee Issa Michuzi makes a point during the meeting


TBN Chairman Beda Msimbe receives PSSSF publications from Mr Abdul Njaidi, delegation leader from the Public Service Social Security Fund, during their meeting on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam.

By TBN Reporter

The Tanzania Bloggers Network (TBN) has reaffirmed its commitment to working with public and private institutions to produce and disseminate constructive content that educates the public and projects a positive image of Tanzania across digital platforms.

Speaking during a meeting between TBN leaders and a delegation from the Public Service Social Security Fund (PSSSF) at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam, TBN Chairman Beda Msimbe said there had never been a more important time for Tanzania’s development achievements to receive greater prominence in the digital space.

He said this had become particularly important in an era when artificial intelligence enables information to be searched, retrieved and circulated more rapidly than ever before.

“It is embarrassing to see that much of the information about Tanzania dominating digital platforms and spreading around the world is driven by online gossip rather than meaningful development stories,” Msimbe said.

Citing a recent example, he said that while President Dr Samia Suluhu Hassan was commissioning the Julius Nyerere Hydropower Project—an undertaking of immense importance to the country—some of the most widely circulated online stories from Tanzania concerned the private lives and childbirth experiences of film and music celebrities.

Msimbe said the situation demonstrated the urgent need for institutions, media organisations and other stakeholders to work together to ensure that Tanzania’s development achievements receive the prominence they deserve on digital platforms.

“TBN is ready to collaborate with different institutions to increase the volume of positive information available across digital platforms. Tanzania should not be known merely for stories concerning people’s private lives, but also for its considerable economic and social achievements,” he said.

Msimbe welcomed PSSSF’s commitment to working with TBN to broaden public education on social security, pension systems and investments undertaken by the Fund.

He said TBN has more than 200 members based in Tanzania and the diaspora, all capable of reaching large audiences through a wide range of digital platforms.

“We are prepared to use the expertise, experience and extensive reach of our members’ platforms to provide accurate information about PSSSF’s activities, services, investments and the various systems it administers,” Msimbe said.

TBN Trustee Issa Michuzi said the network has played an important role in the development of digital journalism in Tanzania and is proud to have members possessing considerable professionalism, experience and capacity to reach audiences across the country and beyond.

Michuzi said TBN was established to ensure Tanzania is properly represented in the digital arena by disseminating accurate, constructive information that stimulates development and contributes to the growth of the national economy.

“TBN is ready to work with PSSSF to ensure that information about social security reaches the public in clear, accurate and easily understood language through digital platforms,” Michuzi said.

TBN Secretary Rahel Pallangyo said the network was prepared to deploy its experienced writers and members’ platforms to ensure that citizens receive accurate and reliable information.

She said such information would enable the public to understand its rights and responsibilities, as well as the opportunities available through the country’s social security systems.

Pallangyo added that collaboration between TBN and PSSSF could provide an important bridge between the Fund and the public, particularly at a time when digital platforms have become some of the country’s principal sources of news, education and knowledge.

Speaking on behalf of PSSSF, delegation leader Abdul Njaidi said the visit formed part of the Fund’s continuing efforts to build closer relations with media stakeholders and strengthen the provision of public education.

Njaidi assured TBN leaders that the requests, proposals and observations presented during the meeting would be carefully considered and acted upon.

He said PSSSF was committed to ensuring that Tanzanians receive comprehensive and accurate information about pensions, social security and the Fund’s investments for the benefit of its members and the nation at large.

The PSSSF delegation was led by Njaidi and included Regina Kumba, Grayson Mgunda and Doreen Lyimo.

TBN was represented by Chairman Beda Msimbe, Secretary Rahel Pallangyo, communications specialist Cathbert Kajuna and Trustee Issa Michuzi.

 

Katika hatua inayolenga kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika Makao Makuu ya Muda ya Tanzania Bloggers Network (TBN), yaliyopo Kijitonyama, Dar es Salaam, kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wa mtandao huo.

Mazungumzo hayo yalilenga kujenga ushirikiano wenye manufaa kwa pande zote mbili, hususan katika masuala ya habari, uelimishaji wa umma na usambazaji wa taarifa na maarifa sahihi kuhusu mifumo ya hifadhi ya jamii, pensheni pamoja na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alisema mtandao huo uko tayari kutumia majukwaa yake kusimama kidete katika kutoa elimu na kusambaza taarifa sahihi kwa umma, hususan kupitia majukwaa ya kidijitali.

Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa wanachama wa TBN kupata mafunzo ya kina kuhusu shughuli, huduma na uendeshaji wa PSSSF, ili waweze kuwaelimisha wananchi kwa ufanisi na kwa usahihi zaidi.

“Ni muhimu kwanza sisi wanachama wa TBN kupata elimu ya kutosha kuhusu mfuko huu, ili elimu tutakayokwenda kuwapa wananchi iwe sahihi, yenye uelewa mpana na yenye tija,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa msafara wa PSSSF, Abdul Njaidi, alisema ziara hiyo imelenga kujenga uhusiano wa karibu na wadau wa sekta ya habari, pamoja na kuimarisha juhudi za kutoa elimu kwa jamii kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii.

Njaidi aliwahakikishia viongozi wa TBN kuwa hoja na mapendekezo yote yaliyowasilishwa katika mkutano huo yatafanyiwa kazi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo unalenga kuhakikisha wananchi wanapata uelewa mpana na sahihi kuhusu masuala ya pensheni na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, alisema mtandao huo wenye historia kubwa katika tasnia ya habari za mtandaoni unajivunia weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yake.

Alisema TBN ipo kwa ajili ya kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali, kwa kutoa taarifa zenye kujenga na kuchochea maendeleo ya taifa.

“Tunataka kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali na kwamba taarifa zinazotolewa zinakuwa na mchango katika kuchochea na kutanua zaidi gurudumu la maendeleo ya taifa,” alisema Michuzi.

Kwa upande wake, Katibu wa TBN, Rahel Pallangyo, alisema mtandao huo uko tayari kutoa waandishi wake mahiri na kutumia majukwaa yake mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, za kuaminika na zenye tija kwa jamii.

Alisema ushirikiano huo utasaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii na kuwawezesha wadau mbalimbali kuelewa kwa kina huduma na fursa zinazotolewa na PSSSF.

Ushirikiano huo unatazamiwa kufungua ukurasa mpya katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni katika kufikisha elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi wengi zaidi nchini.

Katika mkutano huo, ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na Abdul Njaidi ulihusisha pia maofisa Regina Kumba, Grayson Mgunda na Doreen Lyimo.

Kwa upande wa TBN, viongozi walioshiriki mkutano huo ni Mwenyekiti Beda Msimbe, Katibu Rahel Pallangyo, Mtaalamu wa Mawasiliano Cathbert Kajuna na Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi.










Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Aggrey Mwanri, amesema mazungumzo yaliyofanywa na wadau mbalimbali kuhusu hali ya kisiasa nchini yameonesha mwanga mkubwa wa maridhiano na utayari wa wadau hao katika kufikia mwafaka wa pamoja.

Mwanri amesema hayo leo, Septemba 7, 2026, wakati akizungumza katika Mkutano wa Kitaifa wa Wadau wa Kutafakari Hali ya Kisiasa Nchini, uliofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.

Amesema awali, alipowasili kwenye mkutano huo, alikuwa na wasiwasi akidhani kuwa baadhi ya wadau wangekosoa CCM na kukielekezea chama hicho lawama kuhusu changamoto za kisiasa zinazoikabili nchi.

Hata hivyo, amesema mazungumzo yaliyofanyika yameonesha hali tofauti, huku akieleza kuwa utayari wa wadau kushiriki katika majadiliano ya kujenga ni ishara muhimu kuelekea maridhiano na mwafaka.

“Wakati nakuja nilikuwa na hofu kidogo, nikafikiria kwamba watarusha mawe CCM, chama tawala, kwamba hii shida yote tunayopata ni CCM. Tulikuwa na Mzee Wasira, nikamwambia kama mood yenyewe ni hii, unaweza kuwa na uhakika kuwa tuko tayari,” amesema Mwanri.




Mkuu wa Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam, Mhe. Edward Mpogolo, amewapongeza walimu wa Kata ya Ukonga kwa kazi kubwa wanayoifanya katika jamii, akisema walimu ni wazalishaji wa wataalamu na viongozi mbalimbali nchini.

Mhe. Mpogolo ameyasema hayo katika sherehe ya walimu wa Kata ya Ukonga inayojulikana kama UKONGA DAY, iliyofanyika Ukonga jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mpogolo amesema walimu wamekuwa nyenzo muhimu katika jamii kwa kuwaandaa viongozi na wataalamu mbalimbali wanaochangia maendeleo ya Taifa.

Aidha, Mhe. Mpogolo ametoa pongezi hizo kufuatia hotuba ya utangulizi iliyotolewa na mgeni maalum wa hafla hiyo, Mhe. Jerry Silaa, ambaye pamoja na kuwa mlezi wa walimu wa Kata ya Ukonga, pia ana historia ya kipekee na eneo hilo.

Mhe. Silaa amezaliwa katika Kata ya Ukonga na kusoma katika Shule ya Msingi Ukonga. Katika safari yake ya maisha, amekuwa akirejea na kutoa shukrani kwa walimu wa Kata ya Ukonga, akiwatambua kuwa miongoni mwa watu waliochangia mafanikio yake.

Mhe. Mpogolo ameongeza kuwa walimu ni miongoni mwa watu wasiokuwa na wivu katika jamii, kwani wanapowaona watu waliowafundisha wakifanikiwa, hufurahia kuona matunda ya kazi na mchango wao katika kuwaandaa.

Amesema hali hiyo ni tofauti na baadhi ya watu ambao wanapowaona wenzao wakifanikiwa huweza kuwa na wivu, huku walimu wakichukulia mafanikio ya wanafunzi wao kama sehemu ya mafanikio yao wenyewe.





Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na vyama vya siasa na wananchi, wakimfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, walipofika nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja.

Viongozi hao walifika kumfariji Rais Samia kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 07 Septemba 2026 katika Hospitali ya Mzena, Zanzibar.













Na Emmanuel Massaka, Michuzi TV

DAR ES SALAAM: Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imeimarisha ushirikiano na Jeshi la Polisi katika kudhibiti uingizaji, usambazaji na matumizi ya dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa za tumbaku zisizokidhi viwango nchini.

Mkurugenzi wa TMDA, Adam Fimbo, amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanatumia bidhaa zilizo na ubora, usalama na ufanisi unaokubalika.

Akizungumza katika kikao kazi kati ya TMDA na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam, Fimbo alisema mamlaka hiyo inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha bidhaa zisizokidhi viwango haziingii wala kuendelea kuwepo katika soko.

“Majukumu yetu makubwa ni kuhakikisha bidhaa hizo ni bora, salama na zina ufanisi kwa matumizi ya binadamu na mifugo,” alisema.

Alisema kabla ya bidhaa kuingia nchini, zinapaswa kusajiliwa na TMDA na kufanyiwa tathmini kupitia tafiti na uchunguzi wa kitaalamu ili kuthibitisha ubora, usalama na ufanisi wake.

Aidha, alisema TMDA hufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maduka ya jumla na rejareja pamoja na maeneo mengine ya usambazaji, kuhakikisha bidhaa zinazouzwa ni zile zilizosajiliwa na kuruhusiwa kuingia sokoni.

Fimbo alisema TMDA pia huchukua sampuli za bidhaa kutoka maeneo mbalimbali na kuzipeleka katika maabara zake kwa uchunguzi wa kitaalamu ili kubaini kama zinakidhi viwango vilivyowekwa.

Alisema sampuli zinazokamatwa na Jeshi la Polisi wakati wa operesheni na doria mbalimbali pia huwasilishwa TMDA kwa ajili ya uchunguzi, hatua inayowezesha mamlaka kutoa ushahidi wa kitaalamu unaoweza kutumika katika kesi mahakamani.

“Jeshi la Polisi linapokamata sampuli mbalimbali, huletwa kwetu kwa ajili ya kuthibitisha kama zinakidhi viwango vya ubora. Uchunguzi huu hutuwezesha kutoa vielelezo vinavyoweza kutumika kwenye kesi mbalimbali mahakamani,” alisema.

Bidhaa zisizokidhi viwango kuondolewa sokoni

Fimbo alisema TMDA ina jukumu la kuondoa sokoni bidhaa zisizokidhi viwango na kuziteketeza katika maeneo maalumu ili kuzuia zisirejee tena sokoni na kuhatarisha afya za wananchi.

Alisema mamlaka hiyo pia hushirikiana na Jeshi la Polisi pamoja na taasisi nyingine za Serikali katika vituo vya mipakani, kwa lengo la kudhibiti uingizaji wa bidhaa hizo nchini.

Kikao hicho kiliwakutanisha viongozi na askari wa Jeshi la Polisi kutoka maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam, wakiwamo makamanda wa Polisi wa mikoa ya Temeke, Kinondoni na Ilala pamoja na wakuu wa upelelezi wa mikoa hiyo.

Fimbo alisema kikao hicho ni sehemu ya mpango wa TMDA wa kuimarisha uhusiano na Jeshi la Polisi, ambapo mamlaka hiyo imeanza kufanya vikao vya aina hiyo katika kanda zake na inatarajia kuviendesha pia katika mikoa mingine nchini.

“Tumekuwa tukifanya vikao kazi na waandishi wa habari katika kanda mbalimbali Tanzania, lakini hatujawahi kufanya vikao kama hivi na Polisi. Tumeona umuhimu wa kuanza utaratibu huu ili tukutane, tujenge uelewa na kujadili kwa pamoja namna ya kudhibiti bidhaa hizi,” alisema.

Alisema TMDA ina kanda nane nchini na inatarajia kufanya vikao hivyo kila mwaka ili kuongeza uelewa wa majukumu ya kila upande na kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa sheria.

Mbali na udhibiti wa bidhaa hizo, Fimbo alisema TMDA pia inasimamia majaribio ya dawa yanayofanyika kwa wanyama, pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi salama ya dawa na bidhaa nyingine zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo.







 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameshiriki katika maziko ya Marehemu Hafidh Ameir Hassan, mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, yaliyofanyika leo, tarehe 07 Septemba 2026, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja.

Maziko hayo yamehudhuriwa na Viongozi Wakuu wa Serikali, Viongozi Wakuu Wastaafu, viongozi wa dini, vyama vya siasa, Mahakama na Bunge, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, pamoja na ndugu, jamaa, familia, marafiki na waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Marehemu Hafidh Ameir Hassan amefariki dunia leo, tarehe 07 Septemba 2026, katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar, alipokuwa akipatiwa matibabu.

Nikiambiwa unalenga mtindo wa taarifa ya Ikulu/Ofisi ya Makamu wa Rais, naweza kuufanya uwe rasmi zaidi na wenye lugha ya kitaasisi.















Top News