Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. Subira Mgalu leo Machi 03, 2026 amekabidhi magari mapya kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kuwahudumia Wateja wilayani Bagamoyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema hayo leo Machi 03,2026 katika chuo cha ufundi stadi Daon Bosco jijini Dodoma wakati akifungua Awamu ya Nane ya Mafunzo ya Stadi za Kazi kwa Njia ya Uanagenzi kwa Vijana 5,746 waliodahiliwa katika Vyuo 46 nchini kwa mwaka 2025/26 ambapo utekelezaji wa programu umewezesha jumla ya wanufaika 168,657 hadi kufikia Februari, 2026.
Waziri Sangu amesema mafunzo hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa katika kuwapa vijana uzoefu wa kazi kwa nadharia na vitendo, kupunguza pengo la ujuzi kati ya mafunzo ya kitaaluma na mahitaji ya waajiri na kuongezeka kwa ajira kwa vijana kuajiriwa au kujiajiri.
“Hii ni dhamira ya dhati ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kujenga nguvukazi yenye ushindani na tija kwa maendeleo endelevu ya Taifa.” amesema.
Aidha, amesisitiza kuwa kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Tanzania inahitaji nguvukazi yenye ujuzi, weledi na uwezo wa kutumia teknolojia ili kuhimili ushindani wa kikanda na kimataifa, huku Serikali ikiendelea kuboresha sera, sheria na mifumo ya mafunzo kuongeza fursa za ajira kwa vijana.
Awali akitoa salamu za wananchi wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa huo Rosemary Senyamule ameipongeza serikali kwa kuendelea kutenga bajeti maalum kwa ajili ya mafunzo ya uanagenzi hatua ambayo inaonyesha wazi kuwa serikali inawekeza katika rasilimali muhimu za taifa hususani Vijana.
Kwa upande wake Naibu Katibu, Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Zuhura Yunus amesema Serikali kupitia Ofisi hiyo, inatekeleza Mafunzo ya Uanagenzi kupitia Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi Nchini kuanzia mwaka 2016/17 na dhumuni la programu hiyo ni kukuza ujuzi wa nguvukazi iliyopo katika soko la ajira ili kuongeza tija kwenye uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma.
Naye, Mkuu wa Chuo cha Don Bosco Dodoma, Mhandisi Dkt. Justine Mulebya, ameshukuru Serikali kwa kukipatia chuo hicho wanafunzi 650 na ameiomba kuwawezesha vifaa wahitimu wa mafunzo ya uanagenzi ili kuwawezesha kujiajiri na kuajiri vijana wengine wakihitimu mafunzo yao.







Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewashauri viongozi kujenga utamaduni wa kuwasaidia wananchi hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuweka uwiano sawa wa mahitaji.
Ametoa wito huo mara baada ya zoezi la kuwagawa Iftar kwa wananchi wa jimbo la kiwani shehia ya kendwa yenye nyumba zaidi ya 1156 hafla iliyofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Mauuwani Jimbo la Kiwani.
Amesema ataendeleza utamaduni wake wa kugawa Iftari kwa wananchi wote hasa wenye mahitaji Maalum ili kupunguza ukali wa maisha na kupata chakula katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Amefahamisha kuwa mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni Maalum kwa waumini wa Dini ya kiislamu kufanya matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu,hivyo ni vyema kwa kila mwenye uwezo kutoa na kuwapa wahitaji ili kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi huu.
Aidha, Mhe. Hemed amesema anatarajia kuzifikia shehia zote saba ( 7 ) zilizomo ndani ya Jimbo hilo na kuzipatia Iftari jambo ambalo litaongezea umoja na mshikamano kwa wannachi wa jimbo hilo.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewaomba wafanya biashara kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu wakiweo Masikini, Wajane, Mayatima na watu wasiojiweza hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani ili kuzidi kuzitakada biashara zao na kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi wa ramadhani.
Kwa upande wake mfanya biashara SAID NASSIR NASOR ( BOBAR ) ameishukuru serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kumpatia ushirikiano ambapo kwa mwezi huu wa ramadhani amepatiwa usafiri wa kusafirisha bidhaa mbali mbali ambazo atawakabidhi wananchi wa kisiwani Pemba wakiwemo waannchi wa jimbo la kiwani.
Amesema kuwa lengo lake ni kuwafikia wananchi mbali mbali wasio na uwezo kwa Unguja na Pemba ili kila mwananchi apate sadaka itakayowasaidia kwa Iftari lakini pia aweze kupata fadhila hapa duniani na kesho akhera.
Nao wananchi waliopatiwa sadaka hizo wamemshukuru mwakilishi wao kwa kuendelea kuwatumikia kwa moyo wa upendo, huruma na usawa kwa wananchi wote jimboni humo jambo ambalo linawapa faraja na imani kubwa juu yake.
Wamesema hawana shaka na utendaji kazi wa Mhe. Hemed na matumaini yao makubwa ni kuzidi kuwaletea maendeleo jimbo humo kama vile alivyoanza kuzitekeleza ahadi mbali mbali alizoziahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwa mwakilishi wa Jimbo la Kiwani.
Mkutano huo wa Tume na Kinana umefanyika katika ukumbi wa Tanganyika uliopo jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Tume kukusanya taarifa, maoni na ushauri kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo wataalamu, watu wa kawaida, viongozi wa sasa na wastaafu.
Katika mkutano huo hoja zilizojadiliwa zilihusu maeneo ya tathmini ya athari za matukio hayo ndani ya nchi na kimataifa na ushauri wa hatua za kijamii na kisheria zinazochukuliwa ili kuimarisha amani, mshikamano wa kitaifa.
Tume inaendelea na mahojiano na waathirika wa Matukio hayo baada ya hivi karibuni Mamlaka ya Uteuzi kuiongezea Tume muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia tarehe 20 Februari, 2026 ili Tume iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025 na kuitaka ikamilishe kazi na kuwasilisha Taarifa yake kabla au ifikapo tarehe 3 Aprili, 2026.
Hatua hii mpya inalenga, pamoja na mambo mengine, kuimarisha ushirikishwaji wa kifedha na kupanua fursa za uwekezaji kwa Watanzania.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa hizi mpya, Mgeni Rasmi, ambaye ni Gavana wa Benki Kuu Tanzania, Emmanuel Tutuba, aliyewakilishwa na Emmanuel Akaro wa BoT alisema kwamba mifuko ya Imara na KeshoTulivu inatoa fursa zenye utaratibu maalumu kwa wananchi kushiriki katika masoko ya mitaji..
Alitoa wito wa kipekee kwa Watanzania kujenga utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza kwa uwajibikaji, akibainisha kwamba kufanya hivyo kutaimarisha ustahimilivu wao wa kifedha, kukuza masoko ya mitaji, na kuharakisha maendeleo endelevu ya kiuchumi.
"Ujuzi wa kifedha ndio msingi wa ustawi wa mtu binafsi na wa taifa. Watu binafsi wanapoelewa jinsi ya kuweka akiba, kuwekeza, na kudhibiti vihatarishi, wanakuwa katika nafasi nzuri ya kulinda maisha yao ya baadaye na kuchangia kwa maana katika ukuaji wa uchumi. Taifa linalowekeza kwa busara hujenga utajiri si kwa ajili ya leo tu, bali kwa vizazi vijavyo," alibainisha.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa TSL, George R. Shumbusho alisema mifuko hiyo miwili ina muundo tofauti, lakini imeunganishwa na dhumuni moja — kuwawezesha Watanzania kukuza, kulinda, na kupanga utajiri wao kwa kujiamini.
Akifafanua zaidi, Afisa Mtendaji huyo alisema, "Mfuko wa Imara ni mpango wa wazi ulioundwa kutoa ukwasi wa juu na kupunguza vihatarishi, na kuufanya uwe bora kwa wawekezaji wanaotafuta ukuaji wa mtaji wa muda mfupi kupitia mseto wa hati za madeni."
Aliongeza kwamba Mfuko wa Imara umeanzishwa kwa ajili ya wawekezaji wanaotaka ukuaji huku wakihitaji uwezo wa kupata fedha zao haraka, na ambao wako tayari kushiriki katika fursa za soko huku wakinufaika na usimamizi wa kitaalamu wa mfuko pamoja na udhibiti thabiti wa vihatarishi.
Kwa upande mwingine, kwa mujibu wa Bw. Shumbusho, Mfuko wa KeshoTulivu ni mfuko wa wazi wenye uwiano ulioundwa kuwasaidia Watanzania kujenga uwekezaji wa muda mrefu kwa ajili ya kustaafu. Unatoa muda wa uwekezaji wa miaka 5, 10, au 15 na kuendelea, faida shindani za muda mrefu, na njia rahisi kama vile makato ya kiotomatiki kutoka kwenye mshahara. Wawekezaji pia wako huru kuchagua jinsi na wakati wa kupokea faida zao — kila mwezi, robo mwaka, mwaka, na mchanganyiko (hybrid) — kulingana na malengo yao ya kustaafu na mahitaji ya kifedha.
Naye mwakilishi kutoka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Alfred Mkombo aliipongeza TSL kwa hatua hiyo muhimu na kusisitiza dhamira ya CMSA ya kukuza soko la mitaji ambalo ni thabiti, shirikishi, na endelevu.
"Kuanzishwa kwa Mipango ya Uwekezaji wa pamoja kunaonyesha jinsi uvumbuzi unavyoweza kupanua ufikiaji wa fursa za uwekezaji huku ukidumisha ulinzi unaostahili," alisisitiza na kuongeza kuwa soko linalodhibitiwa vyema halizuii ukuaji, bali huwezesha, hujenga uaminifu, huvutia ushiriki, na kusaidia maendeleo ya uchumi wa taifa.
TSL imepewa leseni na CMSA kama dalali wa hisa, meneja wa mifuko, na mshauri wa uwekezaji. TSL pia ni mwanachama wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) na muuzaji mkuu aliyeidhinishwa wa dhamana za Serikali, zikiwemo Dhamana za Muda Mfupi na Hati Fungani.








.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)




.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)










