Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amekutana na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini ikiwa ni mkakati wa Mkoa huo kuimarisha uelewa kwa wananchi kuhusiana na usafi jijini humo, tahadhari ya mvua za Elnino, upangaji wa wafanyabiashara wadogo pamoja na maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2018
Akizungumza leo Septemba 17, 2026 jijini Dar es Salaam na wahariri wa vyombo vya Habari RC Chalamila amesema moja ya mambo ambayo Mkoa huo umekusudia kuyafanya ili kuimarisha usafi ni pamoja na kubadili mitazamo ya wananchi ili wawe na utamaduni wa kupenda kufanya usafi na kutenganisha taka kwa kutumia wataalamu kuelimisha jamii pamoja na kusimamia sheria za usafi ipasavyo
Chalamila amesema kuwa katika mkakati huo pia wametoa muda wa miezi mitatu kwa wakandarasi wa uzoaji taka kuwa na vifaa vya kisasa na teknolojia inayoendana na uhitaji wa Mkoa huo, sanjari na kuwezesha usafi kufanyika nyakati za usiku na kuwa na mifumo bora ya uondoshaji maji taka ambapo pia amezungumzia mpango wa kutumia taasisi binafsi kufanya uchakataji taka kupata mbolea na bidhaa zingine.
Akizungumzia suala la wafanyabiashara wadogo RC Chalamila amesema Mkoa huo imeweka mikakati bora ya kuhakikisha biashara ikiwemo za mama lishe zinafanyika kwenye maeneo rasmi na kuondoka maeneo yasio rasmi huku akielekeza TANROAD kuimarisha upandaji miti na utunzaji bustani za barabarani na ametoa muda wa wiki mbili kwa barabara ya uwanja wa ndege (Nyerere Road)
Aidha Mkuu wa Mkoa amezungumzia tahadhari ya uwepo wa Mvua za Elnino kama zilivyotabiriwa na mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini TMA na kusema kuwa ni muhimu kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa kutoziba mitaro, kuepuka utupaji taka hovyo, kusafisha mito sanjari na kuhifadhi chakula huku akisisitiza kuwa s Mkoa huo unaendelea kuboresha miundombinu
Vilevile Chalamila ameeleza mikakati ya Mkoa huo kwa kushirikiana na wadau wa Sekta binafsi kukabiliana na uwepo wa idadi kubwa ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2018 kutokana na mabadiliko ya mitaala ambapo mwaka 2017 darasa la sita na la saba watahitimu hivyo mbali na ujenzi wa madarasa unaoendelea pia madarasa ya shule binafsi yatatumika
Kwa upande wa Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri Tanzania TEF Deudatus Balile amezungumzia taarifa za kidunia zinazoashiria uwepo wa majanga ya mvua kubwa huku akisisitiza usimamizi wa sheria kwenye kuimarisha usafi wa mazingira.


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)












.jpg)


.jpg)















