Jane Mwakyoma - Rukwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Missana Kwangura amehitimisha mafunzo ya utoaji wa elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi yaliyofanyika wilayani humo mkoani Rukwa.
Kwangura aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Nyakia Chirukile kama mgeni rasmi amesema mafunzo hayo yanapaswa kuwa chachu ya maendeleo kwa washiriki na jamii kwa ujumla kwa kutumia maarifa waliyoyapata kuboresha shughuli zao za kiuchumi.
"Kupitia mafunzo haya mliyoyapata, hakikisheni yanakuwa chachu ya maendeleo katika jamii. Tumiaeni maarifa haya kuongeza thamani ya shughuli zenu za kiuchumi, kujiongezea kipato na kuchangia maendeleo ya Taifa," alisema Kwangura.
Aidha amesema programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi zina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi, kupunguza umaskini na kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa Jacqueline Chrisant Mzindakaya amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uwezo wa kutambua na kunufaika na fursa mbalimbali za mitaji ili waweze kuanzisha, kuendeleza na kupanua shughuli zao za kiuchumi.
Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Gwakisa Bapala amesema mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa NEEC wa kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuwapatia elimu kuhusu fursa za mitaji, namna ya kuandaa miradi inayoweza kupata ufadhili pamoja na matumizi sahihi ya mikopo ili kukuza biashara.
Mafunzo hayo yamewakutanisha wadau mbalimbali wa uwezeshaji wananchi kiuchumi, wakiwemo SELF Microfinance Fund (SELF MF), Benki ya CRDB, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Agricultural Inputs Trust Fund (AGITF), Azania Bank pamoja na PASS Trust, ambao wametoa elimu kuhusu huduma na fursa za kifedha zinazopatikana kwa wananchi .

Pendekezo la Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Songea (SOUWASA) la kuongeza bei ya maji kwa matumizi ya nyumbani kutoka shilingi 1,730 hadi shilingi 2,700 kwa kila mita ya ujazo limejadiliwa katika mkutano wa wadau ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) uliofanyika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.
Mkutano huo umefanyika Julai 16, 2026, ukiwa na lengo la kukusanya maoni ya wananchi na wadau kuhusu ombi hilo la marekebisho ya bei za huduma za majisafi na uondoaji wa majitaka kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2026/27 hadi 2030/31.
Akifungua mkutano huo, Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa EWURA, Mhandisi Walter Christopher, amesema zoezi hilo ni sehemu ya utaratibu wa kisheria unaolenga kuhakikisha maamuzi ya bei yanafanywa kwa kuzingatia maoni ya wananchi pamoja na hali halisi ya utoaji wa huduma.
Mhandisi Christopher amesema SOUWASA imeomba marekebisho ya bei kutokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji na matengenezo, upanuzi wa mtandao wa maji na majitaka pamoja na ukarabati wa miundombinu chakavu.
Ameeleza kuwa EWURA itachambua maoni yote yatakayopokelewa kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho, huku akisisitiza kuwa lengo ni kupata uwiano kati ya uwezo wa wananchi kumudu gharama za maji na uwezo wa mamlaka kuendelea kutoa huduma bora na endelevu.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amesema sekta ya maji ni msingi wa maendeleo ya jamii na uchumi, hivyo maamuzi kuhusu bei yanapaswa kufanyika kwa ushirikishwaji wa wananchi.
Kwa upande wake, Mhandisi Jafari Kinjalambaya wa SOUWASA amesema mapendekezo ya marekebisho ya bei yanalenga kuwezesha mamlaka kukarabati kilomita 32 za mabomba chakavu, kujenga vyanzo vipya vya maji, matenki na mtambo wa kutibu maji, kusambaza mabomba kwa urefu wa kilomita 194.7, kupanua mtandao wa majitaka kwa kilomita 14 pamoja na kufunga mita mpya za malipo ya awali na kubadilisha mita chakavu ili kuboresha ukusanyaji wa mapato na huduma kwa wateja.
Hata hivyo, wananchi na viongozi mbalimbali waliohudhuria mkutano huo wametoa maoni tofauti kuhusu pendekezo hilo, wakitaka Serikali na EWURA kuzingatia uwezo wa wananchi wenye kipato cha chini kabla ya kuidhinisha ongezeko la bei.
Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, tarehe 7 Julai 2026 aliongoza Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili yaliyofanyika katika Bunge la Uingereza (House of Lords), jijini London.
Maadhimisho hayo yalifanyika kwa mwaliko maalum wa Mheshimiwa Lord Paul Boateng, Mjumbe wa Baraza la Juu la Bunge la Uingereza (House of Lords), na yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali, wanadiplomasia, wabunge, wadau wa elimu pamoja na wapenzi wa lugha ya Kiswahili kutoka mataifa mbalimbali.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mheshimiwa Salma Kikwete alisisitiza umuhimu wa Kiswahili kama chombo cha kuimarisha mshikamano, utamaduni na maendeleo ya kijamii na kiuchumi barani Afrika na duniani kwa ujumla. Alieleza kuwa kuendelea kwa matumizi ya Kiswahili katika majukwaa ya kimataifa ni ushahidi wa nafasi yake kubwa katika kuunganisha watu wa tamaduni na mataifa mbalimbali.
Mheshimiwa Salma Kikwete, ambaye pia ni Balozi wa Heshima wa Kiswahili Barani Afrika, alibainisha kuwa lugha ya Kiswahili imeendelea kupata heshima na kutambulika duniani, hatua inayochangiwa na juhudi za viongozi, taasisi na wadau mbalimbali wanaoendelea kuikuza na kuieneza lugha hiyo katika nyanja za elimu, biashara, diplomasia na teknolojia.
Maadhimisho hayo pia yalihudhuriwa na Mabalozi wa nchi mbalimbali za Afrika nchini Uingereza wakiongozwa na Mheshimiwa Christiane Katsande, Balozi wa Zimbabwe nchini Uingereza na Amidi wa Mabalozi wa nchi za Afrika wanaowakilisha mataifa yao nchini humo. Ushiriki wa mabalozi hao uliakisi mshikamano wa Afrika katika kuendeleza na kuipa hadhi lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya mawasiliano na utangamano wa bara hilo.
Kwa upande mwingine, maadhimisho hayo yalipambwa pia na uwepo wa mwanamuziki maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kanda Bongo Man, ambaye ni miongoni mwa wasanii wa Afrika waliotoa mchango mkubwa katika kueneza matumizi na umaarufu wa Kiswahili kupitia muziki wake uliovuka mipaka ya bara la Afrika na kufikia hadhira ya kimataifa.
Aidha, Mheshimiwa Salma Kikwete aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na wadau wengine kwa juhudi zao za kuendeleza na kuhamasisha matumizi ya Kiswahili kimataifa, akisisitiza kuwa lugha hiyo ni sehemu muhimu ya urithi wa Afrika na nyenzo ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.
Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Bunge la Uingereza yameendelea kuonesha kukua kwa hadhi na ushawishi wa Kiswahili duniani, huku Tanzania ikiendelea kuwa kinara katika juhudi za kukuza na kueneza lugha hiyo katika ngazi ya kimataifa.
Na Janeth Raphael - MichuziTv
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa ili kuboresha huduma za afya na kuhakikisha Watanzania wanapata matibabu ya kibingwa na ya kisasa yenye ubora ambayo yatakuwa kivutuo kwa nchi jirani
Dkt. Mwigulu ameyasema hayo wakati wa hafla ya Okoa Maisha Gala iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa kushirikiana na Hospitali ya Benjamin Mkapa, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele Hall, jijini Dodoma.
Dkt. Mwigulu amewashukuru wadau mbalimbali waliofanikisha kuchangia kiasi cha shilingi Bilion 5.5 ikiwa ni zaidi ya asilimia 80% ya lengo, kwa muda mfupi, kwani lengo ilikuwa ni ipatikane shilingi Bilioni 7 ndani ya miaka miwili.
Akitoa mchanganuo wa matumizi ya fedha hizo, na upatikanaji wa huduma za kibingwa na kibobezi hospitalini hapo, Mkurugenzi wa hospitali ya Benjamini Mkapa Profesa Abel Makubi amesema fedha hizo zitasaidia upanuzi wa matibabu kwa watoto 100 wanaosubiri matibabu hayo ambapo kwa sasa vipo vyumba viwili tu vyenye vifaa tiba kwa upandikizaji uloto Jambo linalochelewesha sana huduma hiyo kwa watoto wenye matatizo hayo.
Profesa Makubi amesema hospitali hiyo inampango wa kupanua huduma hiyo kwa kuongeza vyumba kutoka viwili hadi vinne, ambapo chumba kimoja huwa kinaghalimu kiasi cha shilingi milioni 200.
Katika hatua nyingine mkurugenzi wa hospital hiyo Profesa Abel Makubi amesema ameishukuru serikali kwa ujenzi wa jengo la saratani linaloghalimu kiassi cha shilingi Bilioni 32 ambalo limefikia asilimia 70% ambalo litakuwa ni la pili nchini Tanzania kwa utoaji wa huduma hiyo. Na jengo la upandikizaji figo linalotarajiwa kujegwa hispitalini hapo ambalo kitaghalimu kiasi cha shilingi Bilioni 28.
Nae Mwenyekiti wa UWT ndugu Mery Chatanda amesema anamshukuru mwenyekiti wa chama cha mapinduzi taifa na Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani kwani ndiye muasisi wa mpango huo wa kutaka kutokomeza ugonjwa huo kwa kuanzisha huduma ya upandikizaji uloto katika hospital ya BMH na wao kama UWT wameona wa muunge mkono kwa kuandaa harambee ya kuwezesha huduma hiyo, na kutumia fursa hiyo kuwaalika wadau mbalimbali kuendelea kuchangia fedha ili huduma hiyo ianze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
SUBIRA IMEKWISHA! 😱⚽
Fainali ya FIFA WORLD CUP 2026 inakuja na Oryx Energies tuko tayari kuitazama pamoja nawe!
Tukutane Mbagala Zakhem
Jumapili | 19 July 2026
Tunayo kwa ajili yako:
🎉 Screen kubwa
🎧 Live DJ & Burudani
🍔 Vyakula na vinywaji
💯 Hakuna kiingilio
Wacha mpira unoge! Tujaze uwanja tucheke, tupige kelele na tushangilie pamoja 🇹🇿
Tag rafiki zako wa mpira hapa chini 👇
#OryxEnergies #FIFAWorldCup2026 #Fainali #MpiraNiFursa #Mbagala #Tanzania #WorldCupFinal
Kabla ya uteuzi huo, Kipimo alikuwa Meneja Mwandamizi wa Nchi, akisimamia shughuli za Bolt for Business nchini Afrika Kusini, Tanzania, Tunisia na Ghana. Alijiunga na Bolt mwaka 2018 akiwa miongoni mwa wafanyakazi wa kwanza wa kampuni hiyo nchini Tanzania.
Katika nafasi yake mpya, Kipimo atasimamia maendeleo ya biashara katika masoko yote ya Bolt barani Afrika pamoja na kukuza uwezo wa timu za ndani ili kuhakikisha kampuni na taasisi zinapata huduma zenye ubora, unyumbufu na usimamizi bora wa akaunti kupitia Bolt for Business kama mbadala wa mifumo ya kawaida ya usafiri wa kikazi.
Akizungumzia uteuzi huo, Mkurugenzi wa Kanda wa Bolt for Business, Juliano Fatio, alisema:
"Tunafurahia kumkabidhi Milu jukumu la kuongoza shughuli za Bolt for Business barani Afrika. Uzoefu wake katika masoko ya Afrika Kusini, Tanzania, Tunisia na Ghana utakuwa mchango mkubwa tunapoendelea kupanua huduma zetu barani na kuwahudumia wateja wetu wa biashara kwa ubunifu na ufanisi zaidi. Uteuzi huu unaonesha dhamira yetu ya kuendelea kuwekeza katika soko la Afrika."
Kwa upande wake, Kipimo alisema:
"Nimeheshimika kupewa nafasi ya kuongoza Bolt for Business Afrika. Natarajia kutumia uzoefu nilioupata katika masoko ya Afrika Mashariki, Kusini na Kaskazini kuimarisha ukuaji wa biashara katika bara zima, huku tukiendelea kutoa huduma bora ambazo wateja wetu wa biashara wanazitarajia kutoka Bolt Business."
Bolt for Business ni sehemu ya dhamira ya Bolt ya kujenga miji inayoweka watu mbele kuliko magari. Huduma hiyo ilizinduliwa mwaka 2018 na huwasaidia waajiri kurahisisha usafiri wa wafanyakazi kwa safari za kila siku na shughuli za kikazi, huku ikipunguza urasimu wa malipo na madai ya marejesho ya fedha. Kufikia Desemba 2024, Bolt for Business ilikuwa inapatikana katika zaidi ya masoko 50 duniani, ikihudumia zaidi ya kampuni 50,000.
Wito huo umetolewa na Mkaguzi Msaidizi Emmanuel Kisiri, ambaye ni Polisi wa Kata ya Ikoma, Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara,alipokuwa akitoa elimu ya Polisi Jamii katika nyumba ya Abwire Thomas hivi karibuni.
Mkaguzi Msaidizi Kisiri amesema wazazi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwalea, kuwafuatilia na kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuhatarisha ustawi wao.
Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya wazazi, jamii na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kujenga mazingira bora ya malezi na kuhakikisha haki za watoto zinazingatiwa.
Benki ya NMB Plc imetajwa kuwa Benki Bora Zaidi nchini kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati katika Tuzo za Euromoney za Ubora 2026, ikitambuliwa kwa mchango wake katika ufadhili, malipo ya kidijitali, huduma za miamala na ushauri wa kibiashara.
Tuzo hiyo ilitolewa katika hafla iliyofanyika Peninsula Hotel, London, Uingereza, na kupokelewa kwa niaba ya benki na Alex Mgeni, Mkuu wa Idara ya Biashara, Benki ya NMB. Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, alisema ushindi huo ni utambuzi kwa wajasiriamali wanaoendelea kujenga biashara, kutoa ajira na kuchochea uchumi wa Tanzania.
Uwezeshaji wa wafanyabiashara wadogo na wa kati ni eneo muhimu katika Agenda 2030 ya NMB, inayotekelezwa kuanzia mwaka 2026 hadi 2030. Mkakati huo unaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kujenga sekta binafsi yenye ushindani, kuongeza urasimishaji wa biashara na kuchochea ukuaji endelevu.
Benki ya NMB, inayohudumia wafanyabiashara katika mikoa yote 31 ya Tanzania, imesema itaendelea kupanua mikopo, malipo ya kidijitali na suluhisho za biashara zinazosaidia wajasiriamali kuimarisha mzunguko wa fedha, kujenga kumbukumbu rasmi za kifedha na kufikia masoko mapya.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea vifaa vya kisasa vya Chumba cha Kanzi Data, vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) pamoja na miundombinu iliyoboreshwa ya mtandao kutoka Mamlaka ya Taifa ya Nyaraka na Kumbukumbu ya Sultanate ya Oman.
Hatua hiyo inalenga kuimarisha usimamizi wa kumbukumbu na nyaraka za Serikali katika mfumo wa kidijitali, kuongeza usalama wa taarifa za Serikali, kuboresha upatikanaji wa nyaraka kwa wakati, kuimarisha uhifadhi wa muda mrefu wa kumbukumbu muhimu za taifa na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za umma.Akizungumza Julai 15, 2026 jijini Dar es salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete (Mb), amesema msaada huo ni ishara ya uhusiano wa kihistoria na ushirikiano imara uliopo kati ya Tanzania na Oman.
Mhe. Kikwete amesema makabidhiano hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) iliyosainiwa mwaka 2012 kati ya Tanzania na Oman kuhusu usimamizi wa kumbukumbu na nyaraka. “Ushirikiano huu unaakisi dhamira ya pamoja ya nchi hizo mbili katika kuendeleza mageuzi ya kidijitali, kuhifadhi urithi wa nyaraka za Taifa na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za umma. Uwekezaji katika miundombinu ya TEHAMA ni muhimu katika kuhakikisha uhalisia, uadilifu, usalama na uhifadhi wa muda mrefu wa kumbukumbu za umma sambamba na kulinda urithi wa taifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo” amesema.
Kwa upande wake, Kiongozi wa Ujumbe na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Taifa ya Nyaraka na Kumbukumbu ya Sultanate ya Oman, Dkt. Hamad Al-Dhawyani, amesema Oman itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa kumbukumbu na nyaraka kupitia kubadilishana uzoefu, mafunzo ya kitaalamu, tafiti, uhifadhi wa kidijitali na utekelezaji wa miradi ya pamoja itakayowanufaisha wananchi wa nchi zote mbili.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi wa Serikali za Tanzania na Oman, akiwemo Balozi wa Sultanate ya Oman nchini Tanzania, Mheshimiwa Said Hilal Al-Shidhani, Balozi Abdallah Kilima kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na viongozi na watumishi wa Idara ya Usimamizi wa Kumbukumbu na Nyaraka.

.jpeg)







.jpeg)


.jpeg)









.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)







.jpg)





