Akizungumza na wananchi wa Kata ya Hogoro wilayani Kongwa mkoani Dodoma wakati wa ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, Senyamule alisema serikali inatarajia kupeleka umeme katika vitongoji sita vya kata hiyo katika mwaka ujao wa fedha.
Alieleza kuwa matarajio ya serikali ni kuhakikisha vitongoji vyote vinapata huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030, jambo litakalosaidia kuongeza maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi.
“Zamani wananchi walitegemea chemli na vibatari kwa ajili ya mwanga, lakini sasa serikali imeona umuhimu wa kupeleka umeme karibu na wananchi ili waweze kupata mwanga wa uhakika na kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazowaongezea kipato na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.”
Katika sekta ya elimu, Mkuu huyo wa Mkoa alisema Serikali ya Awamu ya Sita imefanikisha ujenzi wa shule nyingi zaidi kuliko vipindi vilivyotangulia, huku akiwataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote wanapata fursa ya elimu.
Alisisitiza kuwa dhamira ya serikali ni kuona kila Mtanzania anajua kusoma na kuandika katika miaka ijayo ili kuwaandaa wananchi kukabiliana na ushindani wa dunia ya sasa inayokua kwa kasi katika nyanja za sayansi na teknolojia.
“Dunia ya leo imekuwa kama kijiji kutokana na maendeleo ya teknolojia. Elimu na ujuzi ni nyenzo muhimu zinazoweza kumpa mtu fursa ya kufanya kazi na kuishi popote duniani”.
Aidha, Senyamule alisema serikali imeendelea kuboresha huduma za afya kwa kujenga na kuimarisha zahanati, vituo vya afya na hospitali pamoja na kuweka mazingira rafiki ya utoaji huduma.
Kutokana na maboresho hayo, alisema hakuna sababu ya wanawake wajawazito kujifungulia nyumbani kwani huduma bora za afya sasa zinapatikana karibu na wananchi, hatua inayolenga kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)















.jpeg)

.jpeg)

















.jpeg)
