Na WMMJW- New York Marekani.
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, inaendelea kuimarisha hatua za kinga na huduma kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia na watoto kupitia utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (NPA–VAWC II) wa mwaka 2024/25 hadi 2028/29 pamoja na Mkakati wa Kitaifa wa Kisekta wa Kutokomeza Ukeketaji wa mwaka 2025/26 hadi 2029/30.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima wakati akishiriki Mkutano wa pembeni ulioandaliwa na nchi ya Liberia uliolenga kutathmini maendeleo na changamoto katika mapambano dhidi ya ukeketaji ndani ya Mkutano wa 70 wa Hali ya Wanawake Duniani unaoendelea jijini New York nchini Marekani.

Waziri Dkt. Gwajima amesema, Serikali ya Tanzania inaendelea kuimarisha juhudi za kutokomeza ukeketaji nchini huku akisema ukeketaji ni kitendo cha ukatili wa kijinsia na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kwa wanawake na watoto wa kike.

Ameongeza kuwa, kwa mujibu wa takwimu za Utafiti wa Afya na Viashiria vya Malaria wa Tanzania wa mwaka 2022 (TDHS-MIS), kiwango cha ukeketaji kwa wanawake wenye umri wa miaka 15 hadi 49 kimepungua kutoka asilimia 10 hadi asilimia 8 huku kukiwa bado na maeneo yenye viwango vya juu hususan mikoa ya Arusha na Manyara yenye asilimia 43 kila mmoja ikifuatia na mingine.

Akifafanua athari za ukeketaji, Waziri Dkt. Gwajima amesema kitendo hicho husababisha madhara makubwa ya kiafya na kisaikolojia, ikiwemo maumivu makali, kutokwa na damu nyingi, maambukizi ya magonjwa, matatizo wakati wa kujifungua na wakati mwingine kusababisha vifo vya Wanawake.

“Katika ngazi ya utekelezaji, Serikali imeanzisha nyumba salama kwa wasichana walio katika hatari ya kukeketwa, vituo vya huduma jumuishi kwa ajili ya kuwahudumia waathirika, pamoja na dawati za jinsia na watoto katika vituo vya polisi ili kuhakikisha waathirika wanapata ulinzi na haki zao zinasikilizwa.” ameeleza Waziri Dkt. Gwajima

Hata hivyo, Waziri Dkt. Gwajima amebainisha kuwa, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado kuna changamoto ya rasilimali zinazohitajika kupanua huduma huku akiwataka wadau wa maendeleo kuendelea kushirikiana na Serikali katika juhudi za kutokomeza ukeketaji.

Mkutano huo ulifunguliwa na Waziri wa Masuala ya Jinsia wa Liberia Mhe. Gbeme Horace-Kollie huku ukihudhuriwa na Mawaziri wa masuala ya Jinsia kutoka nchi za Liberia, Kenya, Tanzania, Gambia na Wawakilishi wa Shirika la UN Women.




Na Mwandishi wa OMH Arusha. 
MSAJILI  wa Hazina, Nehemiah Mchechu, ametoa wito kwa wakurugenzi wa bodi na watendaji wakuu wa kampuni ambazo Serikali ina umiliki wa hisa chache kuachana na usimamizi wa kawaida na kuelekea kwenye uongozi wa kimkakati unaotazama mbele.

Wito huo umetolewa wakati wa Mkutano wa Wakurugenzi wa Kampuni ambazo Serikali ina hisa hisa chache (MIF 2026) unaofanyika kwa siku tatu jijini Arusha, kuanzia Jumatatu, Machi 16, 2026.

Akizungumza katika mkutano huo, Bw. Mchechu alisema mabadiliko haya ni muhimu ili kampuni ziweze kukabiliana na kasi ya mabadiliko ya kiuchumi na kiteknolojia, sambamba na kutumia kikamilifu fursa zinazojitokeza.

Alisisitiza kuwa taasisi zitakazojenga utamaduni wa ubunifu, fikra za mbele na maamuzi ya haraka ndizo zitakazofanikiwa zaidi na kuchangia kwa ufanisi katika kufikia malengo ya Dira 2050.

Bw. Mchechu alisema jukwaa hilo, ambalo linafanyika kwa mara ya tatu tangu kuanzishwa kwake mwaka 2024, limekuwa sehemu muhimu kwa viongozi wa kampuni kujadili masuala ya utawala bora, utendaji na mchango wao katika mageuzi ya uchumi wa Tanzania.

Aliongeza kuwa kaulimbiu ya mwaka huu, “Kutoka Ufuatiliaji wa kawaida hadi Uongozi wa Kimkakati unaotazama mbele,” inaakisi umuhimu wa bodi na viongozi wakuu kuacha usimamizi wa kawaida na badala yake kuendeleza uongozi unaoweza kutambua mapema changamoto na fursa za baadaye.

“Katika dunia ya leo inayobadilika kwa kasi kiuchumi na kiteknolojia, uongozi hauwezi tena kujikita tu kusimamia hali ya sasa, bali unapaswa kutazama mbele na kujiandaa kwa siku za usoni,” alisema.

Alisisitiza kuwa taasisi zinazojenga utamaduni wa kufikiri mbele, ubunifu na maamuzi ya haraka ndizo zitakazofanikiwa zaidi na kuchangia kwa ufanisi katika kufikia malengo ya Dira 2050.

Bw. Mchechu pia alieleza kuwa uwekezaji wa Serikali katika kampuni zenye hisa chache umeongezeka kutoka Sh821 bilioni hadi Sh3.6 trilioni, huku michango ya gawio ikipanda kutoka Sh58 bilioni hadi Sh266 bilioni, ongezeko la asilimia 357 katika kipindi cha miaka mitano.

Mkutano wa MIF 2026 umewakutanisha zaidi ya washiriki 200, wakiwemo wakurugenzi wa bodi, Maafisa wakuu, watunga sera na wataalamu kutoka ndani na nje ya Tanzania kujadili mikakati ya kuimarisha utendaji na utawala wa kampuni hizo, ili ziweze kuchangia kwa ufanisi katika maendeleo ya uchumi wa taifa.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Maendeleo (TIB), Deogratius Kwiyukwa  na  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Shigeki Komatsubara wakisaini hati ya Makubaliano (MoU) itakayolenga kuendeleza mifumo bunifu ya ufadhili wa maendeleo, hatua inayotarajiwa kuchochea mageuzi ya kijamii na kiuchumi nchini. Mikataba huo umesainiwa leo Machi 17, 2026 jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Maendeleo (TIB), Deogratius Kwiyukwa  na  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Shigeki Komatsubara wakibadilishana hati ya Makubaliano (MoU) itakayolenga kuendeleza mifumo bunifu ya ufadhili wa maendeleo, hatua inayotarajiwa kuchochea mageuzi ya kijamii na kiuchumi nchini. Mikataba huo umesainiwa leo Machi 17, 2026 jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Maendeleo (TIB), Deogratius Kwiyukwa akizungumza leo Machi 17, 2026 wakati wa  kusaini hati ya Makubaliano (MoU) itakayolenga kuendeleza mifumo bunifu ya ufadhili wa maendeleo, hatua inayotarajiwa kuchochea mageuzi ya kijamii na kiuchumi nchini. Mikataba huo umesainiwa leo Machi 17, 2026 jijini Dar es Salaam. 
Mwakilishi Mkazi wa
 Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Shigeki Komatsubara akizungumza leo Machi 17, 2026 wakati wa  kusaini hati ya Makubaliano (MoU) itakayolenga kuendeleza mifumo bunifu ya ufadhili wa maendeleo, hatua inayotarajiwa kuchochea mageuzi ya kijamii na kiuchumi nchini. Mikataba huo umesainiwa leo Machi 17, 2026 jijini Dar es Salaam. 


Na Avila Kakingoi, Michuzi Tv
BENKI ya Maendeleo TIB kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) wamesaini Hati ya Makubaliano (MoU) itakayolenga kuendeleza mifumo bunifu ya ufadhili wa maendeleo, hatua inayotarajiwa kuchochea mageuzi ya kijamii na kiuchumi nchini.

Makubaliano hayo yaliyosainiwa jijini Dar es Salaam leo Machi 17, 2026 yatafungua fursa mpya za kuibua na kuendeleza miradi bunifu yenye tija na uwezo wa kuvutia uwekezaji, sambamba na vipaumbele vya taifa.

Sekta zitakazonufaika ni pamoja na nishati jadidifu, maendeleo ya biashara ndogo na za kati (SMEs), uchumi wa buluu pamoja na miradi inayoongozwa na vijana.

Kupitia ushirikiano huo, taasisi hizo mbili zitashirikiana kutambua na kuandaa miradi ya kimkakati itakayoongeza utayari wa uwekezaji, kuhamasisha matumizi ya mifumo ya ufadhili mseto (blended finance) na kuchochea ukuaji wa uchumi jumuishi.

Aidha, makubaliano hayo yanatarajiwa kuimarisha uwezo wa taasisi, kukuza ujasiriamali na kupanua fursa za kiuchumi kwa jamii.

Akizungumza wakati wa kusaini mikata hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Deogratius Kwiyukwa amesema ushirikiano huo unaakisi dhamira ya pamoja ya kuharakisha maendeleo endelevu nchini kwa kuunganisha mitaji ya muda mrefu na suluhisho bunifu za kifedha.

“Ushirikiano huu utachochea uwekezaji wenye mageuzi katika sekta muhimu za uchumi wetu, na kuiwezesha TIB kuendelea kutekeleza wajibu wake wa kusaidia miradi ya maendeleo yenye tija kwa taifa,” amesema.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini, Shigeki Komatsubara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za maendeleo na taasisi za kifedha za ndani katika kuongeza athari za maendeleo.

Amesema kupitia makubaliano hayo, UNDP inalenga kufungua mifumo mipya ya ufadhili itakayochochea ukuaji jumuishi, kuimarisha ustahimilivu wa uchumi na kupanua fursa za maendeleo kwa Watanzania.

Ushirikiano huo unaendana na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na juhudi za serikali chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassan za kuharakisha mageuzi ya kiuchumi, kuimarisha uwekezaji na kulinda rasilimali za mazingira.

Hati hiyo ya makubaliano imeweka msingi wa utekelezaji wa miradi ya pamoja, ushirikiano wa kitaalamu na uhamasishaji wa rasilimali, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuunda ajira, hususan kwa vijana, na kujenga uchumi endelevu na shindani nchini.

Picha ya pamoja.


 

LEO ni leo asemaye kesho muongo, Huu ni msemo ambao Wahenga walimaanisha kuwa jambo linalotakiwa kufanyika leo limailzike leo, na Meridianbet wanakwambia pesa inapatikana kwenye mechi za Uefa leo hivyo ingia na ubeti hapa.

Mapema kabisa Sporting Lisbon atakuwa nyumbani kukipiga dhidi ya Bodo/Glimt ambao walishinda mechi yao ya kwanza walipokutana. Mlima ni mrefu wa kushinda kwa wenyeji kwani mpaka sasa aggregate ni (3-0). Bodoe wamekuwa bora msimu huu huku wakitaka kushinda siku ya leo. Je Sporting atafanya nini nyumbani?. Suka jamvi hapa.

Mechi nyingine ya kibabe ni hii ya Chelsea vs PSG ambao ndio mabingwa watetezi wa kombe hili. Mechi ya kwanza kule Ufaransa The Blues walipigika haswa huku wakiwa magoli 3 nyuma. Vijana hao wa Darajani wanataka kufanya comeback nyumbani. Je Chelsea wanaweza kupindua meza na kusonga hatua ya Robo Fainali leo?. Jisajili hapa.

Ukiacha mechi za UEFA pia unaweza kutengeneza pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa upande wa Real Madrid baada ya kupata ushindi mnono kule Bernabeu, leo hii atakuwa kibaruani dhidi ya Manchester City pale Etihad. Mpaka sasa Agrregate ni (3-0) hivyo City anahitaji kushinda mechi ya leo kwa magoli kuanzia 4 ili avuke hatua ya Robo Fainali kwenye michuano hii. Je Pep Guardiola na vijana wake wanaweza kufuzu siku ya leo?. Bashiri hapa.

Nao Arsenal watakuwa nyumbani kusaka nafasi ya ushindi dhidi ya Bayer Leverkusen ya kule Ujerumani. Mtanange wa kwanza wametoa sare baada ya Havertz kusawazisha goli dakika za jioni za mchezo. Vinara hawa wa EPL wanahitaji ushindi pale Emirates ili kujiweka kwenye nafasi ya kufuzu hatua ya Robo Fainali. Je Arteta atasonga mbele kwenye michuano hii?. Tengeneza jamvi hapa.


Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Vedastus Mwita akizungumza na vyombo vya habari katika hafla ya uzinduzi wa kifurushi kipya kijulikanano kama TTCL Faiba ‘Supersonic Experience’ Kasi Balaa. Huduma hiyo ya vifurishi inampa mteja fursa ya kupata intaneti yenye kasi, gharama nafuu pamoja na muda wa maongezi ya simu.







Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Vedastus Mwita (kulia) akifuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa kifurushi kipya kijulikanano kama TTCL Faiba ‘Supersonic Experience’ Kasi Balaa. Huduma hiyo ya vifurishi inampa mteja fursa ya kupata intaneti yenye kasi, gharama nafuu pamoja na muda wa maongezi ya simu.

SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika hali ya kuendelea kuijenga sekta ya mawasiliano yenye nguvu zaidi na kuboresha huduma za vifurushi kwa wateja wake imekuja na kifurushi kipya kijulikanano kama TTCL Faiba ‘Supersonic Experience’ Kasi Balaa.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Biashara wa TTCL, Bw. Vedastus Mwita alisema kifurushi hicho maalum chenye intaneti vyenye Kasi ya Ajabu kitamuwezesha mteJa kufanya kazi zake bila ya kuwa na wasiwasi (No Stress).

“Kama tunavyofahamu, dunia inaendelea kubadilika kwa kasi kubwa katika enzi ya hizi za  kidijitali. Leo hii, huduma za intaneti zenye kasi, ubora na uhakika zimekuwa mhimili muhimu katika kuendesha shughuli za kijamii na kiuchumi – kuanzia biashara, elimu, afya hadi ubunifu wa vijana wetu.”

“Sasa ni mwendo wa Supersonic Experience” – kasi ya ajabu, kasi isiyopimika, kwa wateja wote wa huduma ya “Faiba Mlangoni kwako”. TTCL Faiba Supersonic Experience ni vifurushi vinavyokupa nguvu ya kufanya kila kitu kidijitali bila mipaka.

“..Kuanzia Smart Home, Smart Office, gaming, streaming, biashara mtandaoni hadi mawasiliano ya uhakika, sasa yote yanawezekana kwa kasi ya ajabu kutoka TTCL,” alisema Bw. Mwita akizungumza na wanahabari.

Akifafanua zaidi juu ya vifurushi hivyo vipya, alivitaja ni pamoja na T-Fiber BUSTA chenye kasi ya 60/60 Mbps (Download and upload), Dakika 250 simu ya mezani kinachopatikana kwa Tsh 55,000 kwa mwezi, T-Fiber Triple Hub Plus chenye kasi ya 100/100 Mbps, dakika 300 simu ya mezani na GB 20 za mawasiliano ya simu ya mkononi  kinachopatikana kwa Tsh 70,000 kwa mwezi. Huku mteja akipata Simcard moja Buree.

Aliongeza vingine ni T-Fiber Triple Hub Extra – Kasi ya 150/150 Mbps, Dakika 700 simu ya mezani na GB  30 za mawasiliano - kwa Tsh 100,000 kwa mwezi. mteja akipata Simcard ya TTCL mbili, bure, T-Fiber Triple Hub Balaa – Kasi ya 200/200 Mbps, chenye dakika 1200 na GB 40 za mawasiliano - kwa Tsh 150,000 kwa mwezi. Na mteja anapata Simcard tatu buree pamoja na T-Fiber Triple Hub Jumbo – Kasi ya 250/250 Mbps, dakika 2500 na GB 50 za mawasiliano - kwa Tsh 200,000 kwa mwezi. na mteja akipata Simcard tatu za buree

Alibainisha kuwa katika mazingira haya mapya ya kidijitali, upatikanaji wa intaneti yenye kasi, gharama nafuu na uhakika si anasa tena, bali ni hitaji la msingi kwa maendeleo ya taifa; hivyo ndiyo sababu Shirika hilo limeendelea kuweka nguvu kubwa katika kuboresha miundombinu ya mawasiliano na kupanua wigo wa huduma ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi.

“..Dira yetu ni kuona kila Mtanzania anapata fursa ya kutumia huduma ya Faiba Mlangoni Kwako itakayosaidiai kikamilifu katika ujenzi wa uchumi wa kidijitali – kwa kupata huduma bora, salama na za kuaminika zinazochochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla,”



*Yafikia Asilimia 91, Kukamilika Desemba 2026


Na MWANDISHI WETU,

Dar es Salaam. Serikali imesema mradi wa uwekezaji wa ujenzi wa jengo la kitega uchumi la Mzizima Towers unaotekelezwa jijini Dar es Salaam na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umefikia asilimia 91 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo Desemba 31, 2026.

Taarifa hiyo imetolewa Machi 16, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, alipowasilisha taarifa ya maendeleo ya mradi huo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii.

Kwa mujibu wa Waziri Sangu, mradi huo wa uwekezaji unahusisha ujenzi wa minara miwili, ikiwemo mnara wa biashara wenye ghorofa 35 na mnara wa makazi wenye ghorofa 32, ukiwa na jumla ya eneo la ujenzi la mita za mraba 95,018.15.

Amesema majengo hayo yamebuniwa kwa kuzingatia viwango vya kisasa vya usanifu wa kimataifa ili kukidhi mahitaji ya biashara, makazi na huduma za utalii katika jiji la Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa mradi huo utakapokamilika utakuwa na hoteli ya hadhi ya nyota tano itakayoendeshwa na Radisson Hotel Group, yenye jumla ya vyumba 156 vya kulala pamoja na vyumba 132 vya makazi ya muda mfupi (hotel apartments).

Mhe. Sangu alisema mradi huo unatekelezwa kwa asilimia 100 na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kama sehemu ya mkakati wa Mfuko huo kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati yenye tija kwa wanachama na taifa kwa ujumla.

Alibainisha kuwa uwekezaji huo unalenga kuongeza thamani ya mali za Mfuko pamoja na kuimarisha uwezo wake wa kulipa mafao kwa wanachama.

Akizungumza baada ya ziara ya kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Mchafu Chakoma, alisema wajumbe wa kamati wanamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua mradi huo uendelee kutekelezwa ili uweze kuleta tija kwa Mfuko na Taifa kwa ujumla.

“Sisi kamati tumefika hapa na kujionea kazi inayofanyika katika mradi huu. Kazi ni nzuri sana na inaonesha kuwa uongozi wa NSSF chini ya Mkurugenzi Mkuu, Bw. Masha Mshomba, umekuwa mfano wa kuigwa katika usimamizi wa miradi,” alisema Mhe. Hawa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, aliwashukuru wajumbe wa kamati hiyo kwa kufanya ziara ya kikazi na kujionea maendeleo yaliyofikiwa katika mradi huo.

Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo akiwemo Mhe. Kafiti Kafiti waliipongeza NSSF kwa uwekezaji wa mradi huo mkubwa unaotarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa taifa na jamii kwa ujumla.

Naye Mhe. Kangi Lugola alisema mradi wa Mzizima Towers ni uwekezaji muhimu wenye tija kubwa kwa Mfuko na Taifa kwa ujumla, akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa NSSF kwa usimamizi mzuri wa Mfuko na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mradi wa Mzizima Towers unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kiuchumi ikiwemo kuongeza mapato ya Mfuko na Serikali, kuimarisha sekta ya biashara na utalii jijini Dar es Salaam pamoja na kuongeza ajira, ambapo zaidi ya wafanyakazi 300 wameajiriwa wakati wa ujenzi wa mradi huo, huku ajira zaidi ya 250 zikitarajiwa kupatikana mara baada ya kuanza kwa shughuli za hoteli na biashara ndani ya jengo hilo.




















Na Seif Mangwangi, Michuzi TV, Arusha

SERIKALI imesema vikundi vya Malezi na Makuzi vinavyoendelea kuanzishwa nchini vimekuwa chachu ya kupunguza tatizo la ukatili wa watoto kwa kuongeza ulinzi na usalama dhidi yao.

Aidha jamii imetakiwa kuungana kwenye suala zima la malezi na makuzi ya mtoto na kwamba Baba anapaswa kuungana na mke wake kuhakikisha mtoto anapata malezi bora, salama na yenye upendo tangu mimba inapotungwa.

Akizungumza kwenye kongamano lililokutanisha makundi ya malezi na makuzi yaliyoko chini ya  taasisi ya malezi ya SOS Children's Village kutoka katika Halmashauri nne za Mkoa wa Arusha za Meru, Arusha DC, Karatu na Jiji, Machi 16 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa malezi bora kwa watoto ni nguzo muhimu katika kuhakikisha jamii inapata maendeleo endelevu na yenye ustawi.

Amesema kuwa serikali inaendelea kushirikiana na taasisi zisizo za kiserikali ili kuhakikisha mwongozo wa malezi bora unatekelezwa kwa ufanisi katika jamii.

Msumi  amesema ushirikiano wa familia na jamii kwenye makuzi ya mtoto  utasaidia kupunguza vitendo vya ukatili vinavyotokea katika jamii, hasa kwa watoto, kwa kuwa jamii itakuwa na uelewa mpana kuhusu wajibu wa malezi na ulinzi wa mtoto.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee, wanawake na Makundi Maalum, Victor Rugarabamu, amesema uwepo wa makundi ya malezi ni mkakati wa Serikali wa kuwa na vikundi aki2 kote nchini ifikapo mwakani.

Amesema pamoja na mafanikio ya uanzishwaij wa makundi hayo, bado takwimu za uanzishwaji wake ni ndogo ambapo Hadi kufikia mwaka huu ni makundi 4060 pekee ambayo yameshaanzishwa nchini.

“ Mpaka Sasa takwimu zinaonyesha tuna vikundi vya Malezi na Makuzi 4060 pekee kote nchini wakati matarajio ni kuwa na vikundi laki2, kasi bado ni ndogo sana inapaswa kuongeza kasi zaidi Ili kufikia malengo,” amesema.

Aidha amelipongeza shirika la SOS Children’s Village kwa juhudi zake za kuanzisha vikundi vya malezi na Makuzi  katika mkoa wa Arusha na kutoa wito kwa taasisi na mashirika mengine kuungana na Serikali kuanzisha vikundi hivyo.

Amesema vikundi hivyo vina mchango mkubwa katika kuhamasisha na kuimarisha malezi bora, pamoja na kuongeza uelewa kwa jamii juu ya haki na ustawi wa mtoto.

Awali Meneja Programu wa taasisi ya SOS Children’s Village mkoa wa Arusha, Mpely Ally Kalonge, amesema kuwa lengo la shirika hilo ni kutoa malezi mbadala kwa watoto wanaohitaji msaada, pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto na kupinga vitendo vya ukatili katika jamii.

Amesema taasisi ya SOS Children village imekuwa kiunganishi Kikubwa kati yake na jamii kwa kusaidia kuanzisha makundi ya malezi katika Halmashauri nne ndani ya Mkoa wa Arusha sanjari na kuyapatia  elimu ya malezi na makuzi makundi hayo.

Kalonge amesema mpango wa taasisi ni kuendelea kuongeza makundi hayo Ili kuongeza ustawi na ulinzi wa watoto na kujenga jamii yenye upendo na isiyo na matendo ya kikatili.





Na Mwandishi Wetu


UZOEFU wa Tanzania katika kuunganisha uhifadhi wa maliasili na maendeleo ya sekta ya utalii umevutia wataalamu kutoka nchini Zambia, waliowasili nchini kwa ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu.

Ujumbe huo umetembelea Tanzania Machi 16,2026 kwa lengo la kujifunza namna nchi inavyotekeleza mikakati ya uhifadhi wa rasilimali za asili sambamba na kutangaza vivutio vyake vya utalii katika masoko ya kimataifa.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya ujumbe huo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii (TTB), Ephraim Mafuru amesema nchi imeendelea kuwa ya mfano barani Afrika kuunganisha juhudi za uhifadhi na maendeleo ya utalii, hatua inayochangia kukuza uchumi wa taifa.

Amesema mfumo wa usimamizi wa hifadhi, uendelezaji wa vivutio vya utalii pamoja na mikakati ya masoko ya kimataifa umeifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zinazoongoza kwa kuvutia watalii duniani.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Baraza la Mawaziri ( FED) kutoka nchini Zambia Siazongo Siakalenge, pamoja na wataalam kutoka sekta ya utalii, uhifadhi wa wanyamapori wameongoza ujumbe huo.

Wajumbe wa Zambia wameeleza kuvutiwa na juhudi zinazofanywa na Tanzania katika kulinda rasilimali za asili huku ikiendeleza utalii kama kichocheo muhimu cha maendeleo ya uchumi na ustawi wa jamii.

“Kama sehemu ya ziara yao ya mafunzo, ujumbe huo pia umetembelea Hifadhi ya Serengeti, kushuhudia uhamaji mkubwa wa nyumbu tukio la kipekee duniani linalovutia maelfu ya watalii kutoka mataifa mbalimbali kila mwaka,” amesema Siakalenge.











Top News