Na Mwandishi Wetu Dar es Salaam.

Tume ya Ushindani (FCC) imesema wazalishaji wa vifaa vya ujenzi wana wajibu wa kumlinda mlaji kwa kuhakikisha wanazalisha na kuuza bidhaa zenye ubora unaolingana na thamani ya fedha anayolipa mnunuzi.

FCC imeeleza kuwa ni muhimu kwa wazalishaji kuzingatia viwango vinavyotakiwa katika uzalishaji wa vifaa vya ujenzi ili kuepusha uwepo wa bidhaa zisizo na ubora sokoni, ambazo zinaweza kusababisha hasara kwa watumiaji na kudhoofisha imani ya wananchi katika bidhaa hizo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina kwa wazalishaji wa vifaa vya ujenzi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani, Mkurugenzi wa Udhibiti wa Mienendo ya Bidhaa Inayokatazwa na Sheria ya Ushindani wa FCC, Bi. Magdalena Utouh, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, amesema ulinzi wa mlaji ni miongoni mwa majukumu makuu ya Tume hiyo.

Amesema FCC itaendelea kufuatilia mwenendo wa soko la bidhaa za ujenzi ili kuhakikisha haki za walaji zinalindwa na wananchi wanapata bidhaa salama na zenye ubora unaokidhi viwango vinavyotakiwa.

Bi. Utouh amewataka wazalishaji wa vifaa vya ujenzi kuendesha biashara zao kwa kuzingatia sheria na kanuni za ushindani wa haki, hatua ambayo itasaidia kujenga soko lenye ushindani wa kweli unaolinda maslahi ya walaji pamoja na kuchochea maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini.

Ameeleza kuwa sekta ya ujenzi ni mhimili muhimu wa ukuaji wa uchumi wa taifa, hivyo uzalishaji wa vifaa vya ujenzi unapaswa kufanyika kwa kuzingatia viwango stahiki na thamani halisi ya fedha inayolipwa na mlaji.

“FCC ina jukumu la kufuatilia mwenendo wa ushindani katika soko ili kuhakikisha hakuna makubaliano ya kupanga bei miongoni mwa wafanyabiashara ambayo yanaweza kumuathiri mlaji,” amesema Bi.Magdalena

Amesema Tume haitavumilia vitendo vyovyote vinavyomuumiza mlaji, akisisitiza kuwa sheria na miongozo ya ushindani ipo wazi na wazalishaji wanapaswa kuizingatia kikamilifu.

Hata hivyo amesema mikutano na majadiliano kati ya FCC na wadau wa sekta ya ujenzi itaendelea kufanyika mara kwa mara ili kuimarisha ushindani wa soko na kuhakikisha walaji wanapata bidhaa na huduma bora.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama wa Shirikisho la Wamiliki wa Viwanda Tanzania (CTI), Bi. Neema Mhondo, amesema sekta ya ujenzi ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi pamoja na kutoa ajira kwa wananchi.

Hata hivyo, amesema wazalishaji wa ndani wanakabiliwa na changamoto ya uwepo wa bidhaa bandia sokoni, hali inayofanya viwanda vya ndani kupata ugumu katika ushindani kutokana na gharama kubwa za uzalishaji na uendeshaji wa biashara.

Semina hiyo ya siku moja imefanyika Machi 11, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ngorongoro katika Ofisi za FCC, Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Udhibiti wa Mienendo ya Bidhaa inayokatazwa na Sheria ya Ushindani wa FCC Bi.Magdalena Utouh akizungumza wakati akifungua Semina ya Wadau wa Uzalishaji wa Vifaa vya Ujenzi ,jijini Dar es Salaam.Meneja wa Kumlinda Mlaji wa FCC Joshua Msoma akitoa mada kwa wadau wa uzalishaji wa vifaa vya Ujenzi ikiwa ni muendelezo wa FCC kukutana na wadau kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani,jijini Dar es Salaam.


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa FCC,Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusiana na Semina ya wadau uzalishaji wa vifaa vya Ujenzi ikiwa ni muendelezo wa FCC kukutana na wadau kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama wa CTI Neema Mhondo akizungumza kwa niaba ya wadau kuhusiana na semina ya Wadau wa Uzalishaji wa wa vifaa vya Ujenzi ,jijini Dar es Salaam.




















Semina ikiendelea




Picha ya pamoja ya makundi mbalimbalj ya Mkurugenzi wa Udhibiti wa Mienendo ya Bidhaa inayokatazwa na Sheria ya Ushindani wa FCC Bi.Magdalena Utouh na Wadau wa Uzalishaji wa Vifaa vya Ujenzi ,jijini Dar es Salaam.



WAFANYAKAZI Wanawake kutoka Kampuni ya Sukari Kilombero walikusanyika kusherehekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake 2026 chini ya kauli mbiu “Give to Gain” Tukio hili lilijumuisha tafakuri za Uwezeshaji, kushirikishana maarifa, kutambua wafanyakazi walio hudumu muda mrefu na liliheshimiwa kwa uwepo wa Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Bi. Diana Mwakitwange, kama Mgeni Rasmi.

Kampuni ya Sukari Kilombero inajivunia wafanyakazi wetu wanawake wa kipekee na mchango mkubwa wanaoutoa katika biashara yetu na jamii kwa ujumla.






Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuongeza nguvu katika kudhibiti usahihi wa vipimo ili kuhakikisha huduma wanazopata wananchi zinaendana na thamani halisi ya fedha wanayotumia

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), Wakati Kamati hiyo ili pokea Taarifa ya Wizara ya Viwanda na Biashara kuhusu utekelezaji ya Miradi ya Maendeleo kwa mwaka 2025/26 kutoka Wakala wa Vipimo (WMA) na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Taasisi zake yake Machi 10, 2026 , Bungeni jijini Dodoma.

Mwanyika amesisitiza kuwa vita dhidi ya lumbesa haipaswi kuachiwa WMA pekee, bali inahitaji nguvu ya pamoja kati ya Halmashauri, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na Serikali Kuu ili kufanya oparesheni za nchi nzima.

Nao, Wajumbe wa Kamati hiyo walizipongeza WMA na CBE kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali na kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali yaliyolenga kuboresha utekelezaji wa Miradi hiyo kwa ufanisi.

Naye, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), alifafanua kuwa msingi wa Tanzania ya Viwanda ni kilimo ambapo WMA inatekeleza jukumu la kumlinda mkulima, huku akibainisha kuwa idadi kubwa ya watumishi wa Wakala huyo wanazalishwa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), jambo linaloashiria kuwepo kwa uhusiano mkubwa wa kikazi baina ya taasisi hizo mbili.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Kihulla, amesema kuwa taasisi hiyo, kwa wakishirikiana na mamlaka nyingine za Serikali pamoja na sekta binafsi, wanaenda kupata suluhisho la kudumu la malalamiko ya wananchi ambayo yamekuwa yakiwasilishwa kwa muda mrefu kuhusu ukosefu wa usahihi wa vipimo katika maeneo mbalimbali ikiwemo lumbesa.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Edda Lwoga amesema miradi ya majengo inayojengwa kwenye Kampasi mbalimbali za Chuo hicho mara itakapokamilika itaboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza udahili wa wanafunzi katika chuo hicho.


NA FARIDA MANGUBE, MOROGORO 

Kampeni ya "Soma na Mkarafuu," inayotekelezwa na Serikali ya Mkoa wa Morogoro, inatoa fursa mpya ya kiuchumi kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza Baada ya kuwapatia miche kumi ya  mkarafuu. 

Kampeni hii, ambayo inalenga kukuza kilimo cha zao la mkarafuu, inawapa wanafunzi na familia zao njia ya kujitegemea kifedha baada ya miaka minne, wakati ambapo zao hilo linapozalisha.


KILIMO CHA MKARAFUU NA FAIDA ZAKE KIMATAIFA

Mkarafuu ni zao lenye soko kubwa duniani, na linapandwa katika maeneo mbalimbali duniani kwa faida yake kubwa kiuchumi, kwa mujibu wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Musa Ali Musa, kila mkarafuu unazaa kilo tano na kuendelea na kilo moja inauzwa kati ya shilingi 15,000 hadi 20,000. 

"Miche ya mkarafuu inakua kwa kasi na inaanza kutoa mazao wakati mwanafunzi anapomaliza mtihani wa kidato cha nne, hivyo atakuwa na uwezo wa kujimudu kifedha akiwa katika kidato cha tano au anapojiunga na mafunzo ya ufundi," alisema Musa.

Kampeni hii ni muhimu si tu kwa kuongeza kipato kwa wanafunzi na familia zao, bali pia inahamasisha wanafunzi kufanya bidii katika masomo yao kwa kuwa wanajua kuwa wataweza kujimudu kifedha kupitia kilimo cha mkarafuu baada ya kumaliza masomo.

 Wanafunzi watakuwa na uhuru wa kuchagua ni njia gani ya maisha wanayotaka, bila kuathiriwa na changamoto za kifedha.


KUPUNGUZA NDOA ZA MAPEMA NA UTORO KWA WATOTO WA KIKE

Kampeni hii pia ina mchango mkubwa katika kupunguza utoro na ndoa za mapema, hasa kwa watoto wa kike. Kwa kuwa watoto wa kike sasa watakuwa na fursa ya kujitegemea kifedha, watakuwa na uwezo wa kugharamia masomo yao na kujiendeleza kimasomo, jambo ambalo linawapa uhuru zaidi wa kuchagua mustakabali wao. 

"Watoto wa kike, ambao mara nyingi walikosa fursa ya kujitegemea kutokana na ukosefu wa fedha, sasa watakuwa na njia ya kujimudu," aliongeza Katibu Tawala.

Fatuma Amri, mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Tawa, ameeleza furaha yake kuhusu mpango huu wa kipekee, akisema, "Hii itatufanya tusome kwa bidii na kuwa na uhakika wa kuendelea na masomo yetu baada ya kidato cha nne. Hatuwezi tena kuwa na wasiwasi kuhusu ada na gharama za shule."

MAFAKIO YA KAMPENI NA MATUMAINI YA BAADAYE

Kampeni ya "Soma na Mkarafuu" inaonyesha mafanikio ya awali, na kwa mwaka 2026, jumla ya miche 2,650 ya kokoa iligawiwa kwa wanafunzi wa Halmashauri ya Mlimba, na miche 9,680 imetolewa kwa wanafunzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

 Miche hii ya kilimo itasaidia wanafunzi kujiendeleza kimasomo na kiuchumi baada ya kumaliza kidato cha nne.

Dkt. Rozalia Rwegasira, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali, anasema kuwa kampeni hii itasaidia kuinua uchumi wa familia na pia itawawezesha wanafunzi kuanzisha miradi ya kilimo itakayowaingizia kipato.

 "Miche ya mkarafuu itachangia katika kukuza uchumi wa wanafunzi na familia zao, na itakuwa na manufaa makubwa kwa mkoa na taifa kwa ujumla," alisema Dkt. Rwegasira.

MOTISHA KWA WANAJUMUIYA BORA

Serikali ya Mkoa wa Morogoro pia imeandaa motisha kwa wanafunzi watakaofanya vizuri katika utunzaji wa miche ya mkarafuu. Wanafunzi watakaofanya vizuri watajipatia zawadi za sare za shule, madaftari, na zawadi kubwa ya safari ya kwenda Zanzibar kwa mwanafunzi atakayefanya vizuri zaidi.








Wanawake watumishi wa Mamlaka  Hifadhi ya Ngorongoro katika muendelezo wa  kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, wamedhihirisha kwamba mchawi wa mwanamke si mwanamke  kwa kutembelea  shule ya Sekondari ya wasichana Ngorongoro na kuwapa tabasamu la  msaada wa vifaa mbalimbali

Akiongea kwa Niaba ya Kamishna wa Uhifadhi, Afisa Uhifadhi Mkuu Sarah Lushu ameeleza kuwa vitu ambavyo Mamlaka vinajumuisha vyakula, Sabuni, vifaa vya kujifunzia, taulo la kike, Vyombo vya kuogea, kupikia na kufulia na mahitaji mbalimbali mahususi kwa wanafunzi wanawake ilo kuwaongezea tabasabu na kuonyesha nguvu ya mwanamke katika Jamii.

"Msaada huu ni sehemu ya jitihada za Shirika kupitia kamishna wa Uhifadhi kuimarisha uhusiano na jamii iliyopo ndani ya Hifadhi na kuhakikisha kuwa wanafunzi hasa wa kike wanapata mahitaji muhimu ya kuwapa utulivu wa kusoma na kupata ufaulu mzuri" alifafanua PCO Sarah.

Msaada huu unadhihirisha wazi kuwa wanawake ni watu wa kusaidiana na mchawi wa mwanamke sio Mwanamke. 







Top News