Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Wanu Hafidh Ameir amesema kuwa Serikali imezidi kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Kidijitali kama nyenzo muhimu katika kuongeza ufanisi wa utoaji Elimu,dhamira ikiwa ni kuwa kichocheo cha ubunifu na kuzalisha maarifa kwa Wanafunzi.

Ambapo amesema ili kufanikisha hilo Serikali imeandaa na kuanza kutekeleza mkakati wa Kitaifa wa matumizi ya Teknolojia ya Kidijitali katika Elimu pamoja na miongozo yake ikiwemo muongozo wa matumizi ya Tehama katika Shule na Vyuo vya Ualimu na muongozo wa akili unde katika Elimu hiyo.

Mhe Naibu Waziri huyo ameyasema hayo mapema leo hii Jijini Dodoma Machi 30,2026 katika hafla ya ugawaji vifaa vya Tehama kwaajili ya kufundishia na kujifunzia katika Shule za Msingi na Sekondari Nchini.

"Serikali ya awamu ya sita inaendelea kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Kidijitali kama nyenzo muhimu ya kuongeza ufanisi wa utoaji wa Elimu,dhamira ikiwa ni kuhakikisha kuwa Teknolojia haitumiki tu kama chombo cha kujifunzia bali pia inakuwa kichocheo cha ubunifu na uzalishaji wa maarifa kwa vijana wetu".

Aidha katika zoezi hilo la ugawaji wa vifaa vya Tehama Naibu Waziri Wanu ametoa wito kwa Walimu,Wanafunzi na Wadau wa Elimu kwa ujumla kutumia na kuvitunza vifaa hivyo ipasavyo ili viweze kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa kama ambavyo inaelekezwa katika Sera ya Elimu na katika Dira ya Maendeleo ya 2050,Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuboresha Elimu kwa kuzingatia mahitaji ya karne ya 21 ikiwemo kuimarisha matumizi Teknolojia za Kidijitali katika ufundushaji na ujifunzaji.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi Lyra in Afrika ambayo imeshirikiana na Serikali katika upatikanaji wa vifaa hivyo Mhandisi Kulaya Henry ameeleza kuwa Shirika hilo limekuwa likishirikiana na Serikali na hata jamii katika mambo mbalimbali ikwemo ujenzi wa mabweni ya wasichana katika shule za Sekondari za Kata za Vijijini kwa Mkoa wa Iringa na Dodoma ambapo mpaka sasa wamejenga mabweni 16 katika shule 11 kwa Wilaya 3 za Mkoa wa Iringa na 1 kwa Wilaya ya Chamwino Dodoma.

Akitoa neno la Shukurani kwa niaba ya Wakuu wa Shule 9 zilizopoke vifaa vya Tehama Mwalimu Ignus Komba kutoka Shule ya Sekondari ya amali Iyunga amesema vifaa hivyo vinakwenda kuongeza umahiri na ufaulu mkubwa kwa wanafunzia,pamoja na kuahidi kwenda kusimamia matumizi sahihi na bora ya vifaa hivyo ili wanafunzi waweze kupata umahiri na kupandisha ufaulu wa Shule zao.

Leo vimetolewa jumla ya vifaa 1510 vikiwemo uhalisia pepe na simu janja ambavyo vimegawanyika katika makundi 15 vikiwa vimegharimu Shilingi Milioni 769 na laki 390 na vitakwenda katika Shule za msingi na Sekondari katika Mikoa 9 kwa Tanzania Bara na Visiwani ikiwemo Kusini Unguja,Dodoma,Mtwara, Geita na Arusha.




 

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi, Hassan Saidy amewataka Watumishi wa Wakala kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha ndani ya muda uliopangwa wanafikisha umeme kwenye vitongoji vyote vya Tanzania Bara.

Ametoa maelekezo hayo Makao Makuu ya REA, Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi na Watumishi wote, ambapo amesema baada ya kusaini Mradi mkubwa wa HEP II (B); Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 tarehe 17 Januari, 2026 na kuongeza kuwa kazi iliyombele ya kila Mtumishi ni kuhakikisha vitongoji hivyo vinafikishiwa umeme katika kipindi cha miaka mitatu yaani hadi 2029.

Mhandisi Saidy amesema kukamilika kwa Mradi huo wa HEP II (B) pamoja na miradi mingine inayoendelea kutafanya jumla ya vitongoji ambavyo tayari vitakuwa vimefikishiwa umeme kuwa takriban 51,000 kufanya vitongoji vitakavyobakia bila umeme na bila kuwa katika mradi wowote kuwa taklibani 13,000 ambavyo vimepangwa kuanza kusambaziwa umeme ifikapo mwaka 2030 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2025 – 2030.

Awali ilielezwa kuwa Mradi huo wa HEP II (B) ni muendelezo wa jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) za kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme kwa Wananchi wote wa Tanzania Bara.

Mradi huo unatarajiwa kutoa manufaa ya moja kwa moja kwa Wananchi kwa kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme vitongojini; kuboresha huduma za kijamii hususan katika sekta za afya, elimu na maji; kuwezesha matumizi ya umeme katika shughuli za uzalishaji na kuongeza kipato cha Wananchi pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa maeneo ya vitogojini pamoja na kuimarisha ustawi wa jamii.

 Aidha; Mhandisi, Saidy aliongoza Watumishi wa REA katika zoezi la kuchagua Viongozi wa TUGHE tawini hapo ambapo kwa kauli moja Watumishi waliwachagua Viongozi wao katika ngazi tofauti kama ifuatavyo: - Mwenyekiti wa Tawi ni Swalehe Kiloza, Katibu wa Tawi ni Mhandisi, Annet Malingumu; Mjumbe wa Halmashauri ya Tawi ni Bwana Issa Sabuni na Mwakilishi wa Kundi la Vijana, Mhandisi, Issac Sanga.

Viongozi wengine ni pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Wanawake ya Tawi la TUGHE REA ni kama ifuatavyo: - Mwenyekiti ni  Wilhelmina Cheyo; Katibu ni Ruth Emmanuel; Mweka Hazina ni Bi. Aveline Wilfred; Wajumbe Kamati ya Wanawake ni Bi. Happiness Ndunguru na Mhandisi, Bertha Mwaituka.

Vilevile Watumishi wa REA pia walichagua Viongozi kwa upande wa Klabu ya Michezo ya REA ambapo itaongozwa na Bwana Selemani Mtunzy kama Mwenyekiti na Mwenyekiti Msaidizi ni Bwana Samwel Sumwa; Katibu ni Bwana Praygod Ng’hunda; Mweka Hazina ni Bwana Daniel Kisaka wakati Wajumbe wa Kamati Tendaji kwa upande wa Wanaume atakuwa Mhandisi, Thomas Mmbaga na kwa upande wa Wanawake atakuwa Bi. Beatrice Shelukindo.

Wakati huo huo Watumishi wa REA walishiriki kwenye zoezi la kuchagua Viongozi wa Chama cha Kijamii cha Wafanyakazi (REA Social Club) chenye lengo la kusaidiana wakati wa raha na changamoto mbalimbali. Viongozi wa Chama hicho waliochaguliwa ni kama ifuatavyo: Mwenyekiti ni Bwana Elias Gunzer; Katibu ni Bi. Theresia Mang’ung’ula; Mweka Hazina ni Bwana Shukuru Malebeto; Wajumbe wa Kamati Tendaji ni Bwana Pastory Mwijage na Bi. Emmy Chali.





 


Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba leo Machi 31, 2026 amewasili Iringa Mjini akiwa njiani kwenda Idodi kumuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mazishi ya aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. William Lukuvi.

Kwenye uwanja wa Ndege wa Iringa, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu alipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James.







‎Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza kutekeleza ujenzi wa barabara zaidi ya Kilomita 56 kwa kiwango cha lami na zege kupitia mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala mkoani humo.

‎‎Akiwa katika ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo Kaimu Meneja wa TARURA wilaya ya Ilala, Mhandisi Grayson Nzunda amesema kuwa miradi inayojengwa ni barabara za lami na zege,  mifereji ya maji ya mvua, makalavati, njia za waenda kwa miguu, uwekaji wa taa za barabarani pamoja na kuweka alama za barabarani ambapo mradi unagharimu shilingi Bilioni 138.

‎“Hapa tulipo ni maeneo ya Kivule tupo  kukagua ujenzi wa barabara zenye urefu wa Kilomita 12, barabara ya Kivule-Majohe Junction Km 2.79 inajengwa kwa kiwango cha zege na barabara ya Kitunda-Kivule-Msongola Km 9.95 inajengwa kwa kiwango cha lami, mradi umegharimu shilingi Bilioni 30 kati ya Bilioni 138 za wilaya nzima ya Ilala", alisema.

‎‎Ameeleza kuwa barabara hizo zilikuwa na changamoto kubwa hivyo kukamilika kwake zitasaidia wananchi kufikia huduma mbalimbali kwa urahisi na kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji, pia barabara hizo zinatumika kama 'bypass' kwa wanaokwenda Chanika au Majohe kama barabara kubwa ikiwa na foleni.

‎Naye, Bi. Vicky Shayo mkazi wa Kitunda amesema kuwa wamekuwa wakikosa wateja katika biashara zao kutokana na changamoto ya barabara hasa kipindi cha mvua kutokana na maji mengi na matope ambapo inapelekea watu kuanguka kwasababu ya udongo kuteleza, lakini barabara ikikamilika itawasaidia kufanya biashara zao na kipato kitaongezeka.

‎Bi. Maria Petro mkazi wa Kivule ameishukuru serikali kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara kwani walikuwa wanapata changamoto kwenda hospitalini lakini sasa hivi usafiri umekuwa rahisi kufika mpaka Banana.

‎Aidha, Mwenyekiti wa mtaa wa Karume Bw. Hajibu China amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani anaiona Ilala inakwenda kubadilika kutokana na maboresho ya barabara kwani wananchi wanajenga nyumba zao, pia kutakuwa na taa za barabarani zitakazopendezesha mji na kuongeza ulinzi na usalama.









Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi, Hassan Saidy amewataka Watumishi wa Wakala kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha ndani ya muda uliopangwa wanafikisha umeme kwenye vitongoji vyote vya Tanzania Bara.

Ametoa maelekezo hayo Machi 30, 2026 Makao Makuu ya REA, Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi na Watumishi wote, ambapo amesema baada ya kusaini Mradi mkubwa wa HEP II (B); Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 tarehe 17 Januari, 2026 na kuongeza kuwa kazi iliyombele ya kila Mtumishi ni kuhakikisha vitongoji hivyo vinafikishiwa umeme katika kipindi cha miaka mitatu yaani hadi 2029.

Awali ilielezwa kuwa Mradi huo wa HEP II (B) ni muendelezo wa jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) za kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme kwa Wananchi wote wa Tanzania Bara.

Mhandisi Saidy amesema kukamilika kwa Mradi huo wa HEP II (B) pamoja na miradi mingine inayoendelea kutafanya jumla ya vitongoji ambavyo tayari vitakuwa vimefikishiwa umeme kuwa takriban 51,000 kufanya vitongoji vitakavyobakia bila umeme na bila kuwa katika mradi wowote kuwa taklibani 13,000 ambavyo vimepangwa kuanza kusambaziwa umeme ifikapo mwaka 2030 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2025 – 2030.

Mradi huo unatarajiwa kutoa manufaa ya moja kwa moja kwa Wananchi kwa kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme vitongojini; kuboresha huduma za kijamii hususan katika sekta za afya, elimu na maji; kuwezesha matumizi ya umeme katika shughuli za uzalishaji na kuongeza kipato cha Wananchi pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa maeneo ya vitogojini pamoja na kuimarisha ustawi wa jamii.

Aidha; Mhandisi, Saidy aliongoza Watumishi wa REA katika zoezi la kuchagua Viongozi wa TUGHE tawini hapo ambapo kwa kauli moja Watumishi waliwachagua Viongozi wao katika ngazi tofauti kama ifuatavyo: – Mwenyekiti wa Tawi ni Bwana Swalehe Kiloza, Katibu wa Tawi ni Mhandisi, Annet Malingumu; Mjumbe wa Halmashauri ya Tawi ni Bwana Issa Sabuni na Mwakilishi wa Kundi la Vijana, Mhandisi, Issac Sanga.

Viongozi wengine ni pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Wanawake ya Tawi la TUGHE REA ni kama ifuatavyo: – Mwenyekiti ni Bi. Wilhelmina Cheyo; Katibu ni Bi. Ruth Emmanuel; Mweka Hazina ni Bi. Aveline Wilfred; Wajumbe Kamati ya Wanawake ni Bi. Happiness Ndunguru na Mhandisi, Bertha Mwaituka.

Vilevile Watumishi wa REA pia walichagua Viongozi kwa upande wa Klabu ya Michezo ya REA ambapo itaongozwa na Bwana Selemani Mtunzy kama Mwenyekiti na Mwenyekiti Msaidizi ni Bwana Samwel Sumwa; Katibu ni Bwana Praygod Ng’hunda; Mweka Hazina ni Bwana Daniel Kisaka wakati Wajumbe wa Kamati Tendaji kwa upande wa Wanaume atakuwa Mhandisi, Thomas Mmbaga na kwa upande wa Wanawake atakuwa Bi. Beatrice Shelukindo.

Wakati huo huo Watumishi wa REA walishiriki kwenye zoezi la kuchagua Viongozi wa Chama cha Kijamii cha Wafanyakazi (REA Social Club) chenye lengo la kusaidiana wakati wa raha na changamoto mbalimbali. Viongozi wa Chama hicho waliochaguliwa ni kama ifuatavyo: Mwenyekiti ni Bwana Elias Gunzer; Katibu ni Bi. Theresia Mang’ung’ula; Mweka Hazina ni Bwana Shukuru Malebeto; Wajumbe wa Kamati Tendaji ni Bwana Pastory Mwijage na Bi. Emmy Chali.




Utaratibu mpya wa kutoa mafuta kwenye vituo vya kuhifadhia mafuta ya Dizeli na Petroli kwenda sokoni uliowekwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), umetajwa kuharakisha utoaji wa mafuta kwenye vituo vya kuhifadhia kwenda sokoni.

Utaratibu huo wa kikodi unawataka wamiliki wa mafuta hayo kuyalipia kodi kabla ya kuyaingiza sokoni ili yanapoingizwa sokoni yanaendelea na taratibu za uuzwaji hali ambayo inarahisisha usambazaji na kuwafikishia wateja huduma ya mafuta kwa wakati.

Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda amefanya ziara kwenye baadhi ya vituo vya kuhifadhia mafuta ya vyombo vya moto jijini Dar es Salaam leo tarehe 29.03.2026 kikiwemo kituo cha Camel Oil, Moil Energies na Mount Meru na kujiridhisha namna utaratibu huo mpya unavyofanya kazi.

Akiwa katika ziara hiyo Kamishna Mkuu Mwenda amezungumza na wasimamizi wa vituo hivyo ambao wamemuhakikishia uwepo na mafuta ya kutosha kwenye viyuo hivyo na namna utaratibu mpya wa TRA unavyorahisisha utoaji mafuta na kuweka udhibiti.

Amesema lengo la TRA kuweka utaratibu huo wa kulipia kodi mafuta kabla ya kuingia sokoni ni kuwezesha biashara ya mafuta ya Dizeli na Petroli kufanyika kwa urahisi na kuondoa changamoto zilizokuwepo huku akitoa wito kwa wafanyabiashara watakaokutana na chanagamoto kuwasiliana na TRA.

Aidha amesema TRA imejiwekea utaratibu wa kufanya kazi kwa saa 24 ili kuharakisha utolewaji wa huduma kwa walipakodi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti waratibu na wasimamizi wa vituo vya kuhifadhia mafuta akiwemo Omar Yusufu wa Mount Meru amesema utaratibu huo mpya wa TRA umeonyesha mafanikio makubwa kwa kusaidia uingizaji mafuta sokoni kwa urahisi.

Amesema wamekuwa wakisafirisha mafuta kwenda Rwanda, Burundi, Congo, Zambia na Malawi na kuwa wanayo mafuta ya kutosha huku wakisubiria shehena nyingine kuingia.

Omar Abeid kutoka Camel Oil amesema wanayo mafuta ya kutosha na wamekuwa wakiyauza kwa wateja wao kulingana na mahitaji ya miezi yote ambapo wateja wanaohitaji mafuta ya ziada hawapatiwi ili na wengine wapate huduma hiyo.

Kwa upande wa kituo cha Moil Energies Meneja wake hapa nchini Bw. Sanjar Rai amesema wao hawana upungufu wa mafuta na wanaendelea kutoa huduma zao kama kawaida na kuishukuru TRA kwa kuwapatia huduma kwa wakati.


Afisa Mwandamizi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Gladness Kirei, ametoa wito kwa jamii pamoja na mashirika mbalimbali nchini kuwasaidia wanafunzi waliokatisha masomo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ujauzito, ili waweze kurejea katika mfumo rasmi wa elimu na kukabiliana na changamoto wanazokumbana nazo, hususan unyanyapaa.

Dkt. Kirei alitoa wito huo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kukabiliana na unyanyapaa kwa wanafunzi wanaorejea shuleni, iliyoandaliwa na Taasisi ya Msichana Initiative.

Alisema hatua hiyo imechukuliwa kufuatia kubainika kuwa baadhi ya wanafunzi waliorejea shuleni kwa mujibu wa Waraka wa Elimu Na. 2 wa mwaka 2021 wamekuwa wakiacha tena masomo kutokana na unyanyapaa kutoka kwa jamii, walimu na wanafunzi wenzao.

“Wapo wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo kutokana na mazingira yasiyo rafiki yanayotokana na unyanyapaa. Muongozo unaeleza wazi kuwa mwanafunzi ana haki ya kuhamia shule nyingine endapo atakumbana na hali hiyo,” alisema Dkt. Kirei.

Aidha, aliipongeza Taasisi ya Msichana Initiative kwa juhudi zake za kupigania haki za wasichana, akieleza kuwa kampeni hiyo itasaidia kuhamasisha jamii kuwatambua wanafunzi hao kama wengine na kuwaunga mkono ili wafikie ndoto zao.

Alisisitiza umuhimu wa kuwasaidia wanafunzi hao kwa kuwapatia mahitaji muhimu ikiwemo vifaa vya shule pamoja na msaada wa kisaikolojia ili waweze kuendelea na masomo kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Msichana Initiative, Consolata Chikoti, alisema taasisi hiyo imekuwa ikiunga mkono juhudi za Serikali katika kuhakikisha changamoto zinazowakabili watoto wa kike zinatatuliwa na haki zao zinalindwa.

Alisema licha ya utekelezaji wa waraka unaoruhusu wanafunzi kurejea shuleni, bado wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo unyanyapaa.

Takwimu za Wizara ya Elimu zinaonesha kuwa wasichana 58 walirejea katika mfumo wa elimu baada ya kuacha shule, huku tafiti za taasisi ya Global Women Institute zikionesha kuwa wasichana milioni 60 duniani wamekumbana na ukatili wa kijinsia. Nchini Tanzania, takribani wasichana milioni 14.6 wanakabiliwa na changamoto zinazowazuia kupata haki ya elimu.

Aidha, alibainisha kuwa msichana mmoja kati ya watatu anaolewa kabla ya kufikisha miaka 18, huku mmoja kati ya wanne pekee akifanikiwa kumaliza elimu ya sekondari.

Pia, baadhi ya wasichana hukosa masomo kwa siku nne hadi tano kila mwezi kutokana na changamoto za hedhi.

Chikoti alisema kupitia mradi wa “Rudi Shule”, taasisi hiyo imefanikiwa kuwafikia zaidi ya wasichana 500, na inalenga kuwafikia wanafunzi 250 zaidi mwaka huu, huku ikibainisha kuwa unyanyapaa bado ni kikwazo kikubwa kwa wanafunzi wanaorejea shuleni.

Mmoja wa wanufaika wa kampeni hiyo, Theresa Juma (21), alisema alipata ujauzito akiwa na umri wa miaka 18 baada ya kumaliza kidato cha kwanza hali iliyomlazimu kuacha shule.

Alisema alifukuzwa nyumbani na kupitia changamoto nyingi, lakini aliamua kurejea shuleni huku akijitegemea kugharamia masomo yake.

“Nilifaulu kwa daraja la kwanza, lakini ujauzito ulinikatisha masomo.

Nimepitia changamoto nyingi, lakini nimeamua kujitafutia maisha na kuendelea na elimu yangu huku nikilea mtoto wangu,” alisema Theresa.





WAKALA wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu nchini (ADEM) kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) wamefanya warsha maalumu ya kuhakiki Matini ya uendeshaji wa Jumuiya za Kujifunza za walimu na viongozi wa elimu (JzK), ikiwa ni hatua muhimu ya kukusanya maoni ya wadau kwa ajili ya kuboresha nyenzo hiyo.

Warsha hiyo imelenga kuhakikisha matini inayotarajiwa kutumika kuzijengea uwezo Jumuiya za Kujifunza inakuwa bora, shirikishi na yenye kukidhi mahitaji halisi ya walimu na viongozi wa elimu nchini.

Akifungua warsha hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania, Dkt. Aneth Komba, amesisitiza umuhimu wa taasisi hizo mbili kuweka mpango madhubuti wa utekelezaji wa matumizi sahihi ya matini hizo ili kufanikisha lengo la kuimarisha Jumuiya za Kujifunza.

Ameeleza kuwa maandalizi ya matini hiyo ni jukumu muhimu la kitaifa, hivyo wadau walioshiriki wanapaswa kutoa maoni na ushauri wa kitaalamu utakaosaidia kuboresha nyenzo hiyo na kuhakikisha inaleta matokeo chanya yaliyokusudiwa.

“Niwapongeze sana mliochaguliwa kuandaa matini hii, nina imani mmeitekeleza kazi hii kwa weledi na ufanisi mkubwa. Ni muhimu pia kwa wadau wote kushiriki kikamilifu katika uhakiki huu ili kupata matini bora itakayosaidia kufikia malengo yaliyowekwa,” amesema Dkt. Komba.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid J. Maulid, amewashukuru wataalamu na wadau wote waliohusika katika uandaaji wa matini hiyo kwa kukamilisha kazi hiyo kwa wakati na kwa viwango vinavyohitajika.

Amesema matini hiyo itakuwa mwongozo muhimu wa utekelezaji wa shughuli za Jumuiya za Kujifunza nchini, sambamba na kusaidia kufikia azma ya Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya kuboresha mafunzo ya walimu na viongozi wa elimu kazini.

Aidha, amewahimiza wadau walioshiriki warsha hiyo kuendelea kutoa mchango wao kwa weledi ili kuhakikisha matini hiyo inakuwa na ubora unaokusudiwa.

Warsha hiyo imewakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wataalamu kutoka programu ya Shule Bora, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI, Taasisi ya Elimu Tanzania, pamoja na viongozi wa idara za elimu kutoka Halmashauri ya Mji Bagamoyo na Manispaa ya Singida. Wadau wengine walioshiriki ni pamoja na wawakilishi kutoka taasisi za CAMFED na Project Zawadi.



















Top News