
Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi akitembelea maeneo ambayo wakazi wake wamekataa kufanyiwa tathmini kwa ajili ya upanuzi wa shughuli za mgodi

Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Meneja Mkuu wa mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko akieleza programu ya kulipa wananchi kwa ajili ya kupisha shughuli za mgodi inavyoendelea wakati wa ziara ya Mkuu wa mkoa wa Mara alipofanya ziara ya kikazi karibuni
*
-Awapa muda wa siku 90 wananchi ambao tayari wamelipwa fidia kupisha shughuli za upapanuzi wa mgodi.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, ameeleza kuridhishwa na ujenzi wa makazi mapya ya wananchi walioguswa na upanuzi wa Mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara pia amewapa siku 90 wananchi ambao tayari wamelipwa fidia ya maeneo yao kuondoka ili kupisha shughuli za upanuzi wa mgodi.
Akizungumza wakati alipokwenda kukagua ujenzi wa nyumba hizo katika eneo la Magena, Nyamongo wilayani Tarime karibuni, Kanali Mtambi aliupongeza mgodi huo kwa uwekezaji unaokwenda sambamba na ustawi wa wananchi.
Alitumia nafasi hiyo pia kusisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya mgodi huo na jamii inayouzunguka kwa maendeleo endelevu ya pande zote mbili na kuwataka wananchi ambao tayari wamelipwa fidia ya maeneo yao wawe wameondoka ndani ya siku 90 na wale waliogomea kulipwa fidia kukaa pamoja na wadau kutoka pande zozote kumaliza changamoto hiyo.
“Mkuu wa Wilaya na watu wa ardhi nawapa siku saba , mje kwa hawa wananchi, mkae nao muwaelimishe wakubali kufanyiwa uthamini na kupokea fidia kwa mujibu wa sheria,” alisema Kanali Mtambi.
Alionya kuwa kugomea uthamini na fidia kunakiuka sheria za nchi na kunachelewesha shughuli za mgodi huo pamoja na miradi ya maendeleo inayotegemea uwekezaji huo.
Baadaye, RC Mtambi alikwenda kuzindua moja ya nyumba za waguswa ambayo imejengwa na mgodi huo katika kijiji cha Mjini Kati.
Awali, Meneja Mkuu wa mgodi huo, Apolinary Lyambiko, alimweleza Mkuu wa Mkoa kwamba kampuni inaendelea kulipa fidia kwa kaya 254 zinazotakiwa kupisha ekari 59 kwa upanuzi wa shimo Nyabirama,hatua inayolenga kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama.
Lyambiko alisema waguswa 654 kati ya 728 walifanyiwa uthamini na kwamba hao tayari wamekwishapokea fidia zao ili kupisha upanuzi wa shimo la wazi la Nyabirama.
“Mradi huu unalenga si tu kuongeza ufanisi wa uzalishaji bali pia kuhakikisha usalama kwa kupata eneo la mita 200 la hifadhi kinga (buffer zone) kutoka kwenye shimo kama sheria inavyoelekeza,” alisema.
Aidha, Lyambiko alisema waguswa walipewa fursa ya kuchagua aina ya fidia wanayoitaka; kati ya fedha taslimu, kujengewa nyumba na ardhi mbadala.
“Wananchi 571 walichagua fedha taslimu, 36 walichagua ardhi na nyumba mbadala, 37 walichagua ardhi mbadala na 10 walichagua nyumba mbadala, na mchakato umezingatia ushirikishaji na hiari ya wananchi,” alifafanua.
Aliongeza kuwa ujenzi wa nyumba 10 mbadala umeshakamilika, nyumba 24 ujenzi umefikia asilimia 70, 16 ziko katika hatua za awali na 18 ziko kwenye hatua za manunuzi.
Kwa mujibu wa Lyambiko, mradi huo wa ujenzi wa nyumba za waguswa unatekelezwa na wakandarasi watatu waliopitishwa na Tume ya Madini Tanzania.
“Tunaendelea kuhakikisha kuwa kasi inaongezwa ili wahusika wahamie kwenye makazi yao mapya kwa wakati na kuruhusu mgodi kuendelea na shughuli zake kwenye eneo la Nyabirama,” alisema.
Taarifa za Serikali kuhusiana na program hiyo zinabainisha kuwa wananchi 728 wa eneo hilo walifanyiwa tathmini ya kulipwa fidia kwa ajili ya upanuzi wa eneo la mgodi ambapo hadi sasa wananchi 571 tayari wamelipwa fidia ya fedha taslimu na wengine 74 hawajasaini nyaraka za kulipwa fidia ambapo wananchi 11 wamegomea kufanyiwa tathmini.
Katika ziara hiyo, RC Mtambi aliambatana na Mkuu wa Wilaya, Meja Edward Gowele na Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Mwita Waitara, miongoni mwa viongozi wengine.
Mgodi wa Dhahabu wa North Mara unaendeshwa na Kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia Kampuni ya Twiga Minerals na ni miongoni mwa uwekezaji mkubwa wa uchimbaji wa madini nchini, ambao unachangia utekelezaji wa miradi ya kijamii, mapato ya taifa na ajira kwa Watanzania.
Mgodi wa Barrick North Mara umefanikisha miradi mbalimbali ya kijamii katika eneo la vijiji vinanyozunguka mgodi hususani katika sekta ya elimu,afya,maji,ujenzi wa miundombinu ya barabara,uwezeshwaji wa vijana na kuongeza wigo wa ajira.




















.jpeg)



.jpeg)










