Na Hassan Kimweri, WAF - Addis Ababa

Tanzania imeendelea kusisitiza  ushirikiano wa Umoja wa Afrika (AU) katika kuimarisha juhudi za kupunguza vifo vya mama na mtoto barani Afrika, hususan kupitia utekelezaji wa mikakati na hatua madhubuti zinazolenga kuboresha afya na ustawi wa makundi hayo.
Hayo yameongelewa  leo Agosti 25, 2026 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe alipofanya kikao na Kamishna wa Afya, Masuala ya Kibinadamu na Maendeleo ya Jamii wa Tume ya Umoja wa Afrika Mhe. Balozi Amma Twum-Amoah, pembezoni mwa Mkutano wa 76 wa Kamati ya Kanda ya Afrika ya Shirika la Afya Duniani (WHO-AFRO), unaofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Dkt. Magembe amemshukuru Mhe. Balozi Amma Twum-Amoah na Tume ya Umoja wa Afrika kwa ushirikiano  unaoendelea kutolewa kwa Tanzania katika sekta ya afya, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano huo ili kukabiliana na changamoto za afya na kuharakisha hatua za kupunguza vifo vya mama na mtoto barani Afrika.

Aidha, Dkt. Magembe amepongeza imani kubwa iliyowekwa kwa   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumfanya kuwa kinara wa Afya ya Uzazi na Mtoto wa Umoja wa Afrika akieleza kuwa nafasi hiyo ni fursa muhimu ya kuhamasisha dhamira na hatua za pamoja za viongozi wa Afrika katika kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Katika hatua nyingine, Dkt. Magembe amesema kuwa Tanzania iko katika hatua za mwisho za maandalizi ya uzinduzi wa Mpango Mkakati wa utekelezaji (Roadmap) ya Kinara wa Umoja wa Afrika wa Afya ya Mama na Mtoto, unaotarajiwa kufanyika Arusha Septemba 9, 2026, na amemwalika Mhe. Balozi Amma Twum-Amoah kushiriki katika maandalizi na uzinduzi huo. 

"Lakini pia, tunaomba ushirikiano wa Tume ya Umoja wa Afrika katika maandalizi ya Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Viongozi wa Nchi na Serikali kuhusu Uhai wa Mama na Mtoto Barani Afrika, utakaofanyika Jijini New York Septemba 23, 2026, pembezoni mwa Mkutano wa 81 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa," amesema Dkt. Magembe




 

Na Hassan Kimweri, WAF - Addis Ababa

Tanzania imeunga mkono juhudi za kuimarisha Shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia maboresho ya Muundo wa Mfumo wa Afya Duniani (Global Health Architecture), huku ikisisitiza umuhimu wa WHO kuendelea kutekeleza jukumu lake la msingi kama mamlaka ya kiufundi ya afya duniani. 

Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Florence Samizi, amesema hayo leo Agosti 25, 2026 kwenye Mkutano wa 76 wa Kamati ya Kanda ya Afrika ya Shirika la Afya Duniani (WHO-AFRO), unaofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia.

"Tanzania inapongeza uongozi wa WHO katika kuratibu ushiriki wa Kanda ya Afrika kwenye utekelezaji wa marekebisho ya Kanuni za Kimataifa za Afya (International Health Regulations – IHR 2024) pamoja na kukamilishwa kwa viambatisho vyake katika Mkataba wa WHO," amesema Dkt. Samizi 

Aidha, Dkt. Samizi amesema Tanzania inatambua mchango wa WHO katika kutoa msaada wa kiufundi ili kuimarisha mifumo ya afya, kuboresha ufuatiliaji wa magonjwa, kukabiliana na milipuko, kuendeleza huduma jumuishi za afya kwa wote pamoja na kuboresha afya ya mama na mtoto pamoja na vijana.

Tanzania imeeleza dhamira yake ya kuendelea kushirikiana kwa karibu na WHO, taasisi za kikanda, washirika wa maendeleo na nchi wanachama katika kujenga mifumo ya afya imara, yenye usawa na inayomlenga mwananchi. 

Pai, Dkt. Samizi amesema Tanzania imedhamiria kukabiliana na changamoto za magonjwa yanayojitokeza na kuibuka upya, mabadiliko ya tabianchi, usugu wa vimelea dhidi ya dawa pamoja na upungufu wa rasilimali.




 

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Viongozi wapya wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) wameapishwa rasmi jijini Dar es Salaam, huku wakitakiwa kusimamia Katiba ya chama na kulinda maslahi ya wanachama katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza wakati wa kuwaapisha viongozi hao, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, aliwataka kuzingatia Katiba ya TAPSEA na kuitumia kama mwongozo katika uongozi wao ili kuhakikisha wanachama wanaongozwa kwa haki na ufanisi.

Kiswaga amesema TAPSEA ni chama kikubwa chenye wajibu wa kuwatumikia wanachama wake, hivyo viongozi wanapaswa kuwa imara katika kusimamia maslahi yao na kuhakikisha chama kinaendelea kusonga mbele.

“Niwaombe viongozi mnapotoka hapa mkasimamie vyema Katiba yenu ili kuweza kuondoa migogoro itakayojitokeza,” alisema Kiswaga.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa TAPSEA, Leah Mwamba, aliwashukuru wanachama kwa kumpa dhamana ya kuwaongoza na kuahidi kushirikiana nao katika kuhakikisha chama kinafikia malengo yake. Amesema tukio la uapisho ni hatua muhimu katika safari ya uongozi na kuomba wanachama waendelee kuwaunga mkono.

“Ninatoa shukrani zangu za pekee kwa wote walioungana nasi katika historia hii. Jambo hili la uapisho ni kubwa sana, hivyo tunaomba mzidi kutuombea tufanye vyema katika uongozi,” alisema Mwamba.

Naye Katibu Mkuu wa TAPSEA, Hellen Magati, aliwashukuru wageni na wadau waliohudhuria hafla hiyo, akiahidi kuwa uongozi mpya utashirikiana na wanachama na wadau mbalimbali katika kutekeleza majukumu yake na kuimarisha chama.

Viongozi wengine walioapishwa ni pamoja na Makamu Mwenyekiti, Zainab Ibrahim Ally, Naibu Katibu Mkuu, Halima Twaha Mgulo, Mweka Hazina, Nyanza Msongela, pamoja na wajumbe wengine waliochaguliwa katika uongozi huo.












Na Dulla Uwezo
Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 zinatarajia kuingia Mkoani Kagera Agosti 30, Mwaka huu zikitokea Mkoa wa Geita, zikipokelewa rasmi katika Wilaya ya Muleba na Viongozi wa Mkoa huo wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Kagera Kanali Yahya Ramadhani Kido.

Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa mbele na Wanahabari na Mkuu wa Mkoa Kagera Kanali Kido, amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani humo utatembelea miradi 54 yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 23.07 ikiwemo miradi ya Serikali, Binafsi (wawekezaji) pamoja na ili inayotekelezwa kwa Kushirikiana na Nguvu ya Jamii.

Aidha Kanali Kido ameongeza kuwa kati ya Miradi 54, Miradi 25 itawekewa Mawe ya Msingi, Miradi 5 itafunguliwa, Miradi 11 itazinduliwa, na Miradi 13 Itatembelewa na Kukaguliwa. Miradi hiyo ni pamoja na Miradi ya Maji, Afya, Elimu, Miundo Mbinu, Maendeleo ya Vijana, Nishati, Mazingira wezeshi kwa wawekezaji pamoja na Uhifadhi Mazingira.

Pamoja na hayo Mkuu wa Mkoa Kagera Kanali Kido ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa Wingi kule kote ambapo Mwenge utapita, maeneo ya miradi pamoja na maeno ya Mikesha ya Mwenge, huku Mwenge wa Uhuru ukiwa na Umebeba Ujumbe wa Masuala ya UKIMWI, Malaria, Dawa za Kulevya, Masuala ya Lishe, Rushwa Sambamba na Kauli mbiu isemayo "Tanzania ni yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo."
Interim Dean of the Aga Khan Institute of Education Development, East Africa (IED,EA), Prof Jane Rarieya, during a regional learning exchange at the University’s campus in Dar es Salaam.
Delegates at the Aga Khan University Institute for Educational Development’s Tanzania Regional Learning Exchange observe a demonstration at the Marketplace Exhibition, where young engineers showcased innovative approaches to STEM education.

Dar es Salaam, Tanzania, August 25, 2026:
The Aga Khan University’s Institute for Educational Development, East Africa (IED, EA) hosted a Regional Learning Exchange bringing together teacher educators, policymakers, researchers, school leaders, development partners, student teachers and education practitioners from across East Africa and beyond to exchange knowledge and explore the future of teacher education.

The learning exchange under the theme “Reimagining Teacher Preparation: An East African Learning Exchange on Innovation and Practice,” provided a collaborative platform for participants to share experiences, explore innovative practices, and co-create practical solutions to strengthen teacher preparation across the region.

The exchange comes at a critical moment for education in East Africa. As the teaching profession is being reshaped by efforts to improve learning and equity, the rapid growth of digital technology and artificial intelligence, climate disruption, increasing diversity and inclusion, and changing expectations of what education should achieve.

“The future of education in East Africa depends not only on having enough teachers, but on how well we prepare, support and empower them throughout their careers. This conference gives us an important opportunity to learn from one another, strengthen partnerships across schools, universities, communities and education systems, and rethink teacher preparation for the realities of today’s classrooms,” said Prof Jane Rarieya, Interim Dean, Institute for Educational Development, East Africa.

A key focus of the learning exchange was ensuring teachers have the professional agency to shape education reform. As education systems increasingly embrace competency-based approaches, teachers need to be equipped to understand learners’ needs, make informed professional decisions, assess learning, adapt their teaching and collaborate effectively with communities they serve.

For IED, EA, the learning exchange is also a call to action to work with teachers, governments, universities, schools, communities and development partners to reimagine teacher preparation across East Africa. This includes strengthening meaningful classroom practice and mentoring for student teachers, building supportive professional learning communities for early-career teachers, and creating opportunities for experienced educators to lead, mentor and contribute to innovation and inquiry.



Na Janeth Raphael - MichuziTv - Bungeni Dodoma

Serikali imesema haina mamlaka ya kuzipangia benki za biashara viwango vya riba za mikopo, kwa kuwa gharama hizo huamuliwa na mwenendo wa soko pamoja na sababu mbalimbali za kiuchumi na kiutendaji.

Kauli hiyo imetolewa leo, Agosti 26, 2026, na Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula, wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpanda Mjini, Haidary Sumry, Bungeni kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali kupunguza riba za mikopo ya biashara ili kuwawezesha wafanyabiashara kulipa madeni yao kwa wakati.

Luswetula amesema Serikali haiingilii moja kwa moja upangaji wa riba katika benki za biashara, kwa sababu viwango hivyo huwekwa kwa kuzingatia misingi ya soko.

Ameeleza kuwa miongoni mwa mambo yanayochangia kuamua kiwango cha riba ni mfumuko wa bei, hatari ya mkopaji kushindwa kurejesha mkopo, gharama za uendeshaji wa benki pamoja na kiwango cha faida kinacholengwa na taasisi husika ya fedha.

Hata hivyo, amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua za kisera na kiusimamizi zinazolenga kupunguza gharama za mikopo na kuongeza fursa kwa wananchi na wafanyabiashara kupata huduma za fedha kwa masharti nafuu.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri, Serikali inaendelea kutekeleza sera za fedha zinazolenga kudhibiti mfumuko wa bei, ambao ni miongoni mwa vigezo vinavyozingatiwa katika upangaji wa viwango vya riba.

Amesema Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imekuwa ikirekebisha kiwango cha Riba ya Benki Kuu (CBR) kulingana na mwenendo wa uchumi, hatua inayolenga kudhibiti mfumuko wa bei na kuhakikisha kunakuwa na ukwasi wa kutosha katika uchumi.

Luswetula pia ametaja kuanzishwa kwa Price Comparator System, mfumo unaolenga kuongeza uwazi katika sekta ya fedha kwa kuwawezesha wananchi kulinganisha viwango vya riba na gharama nyingine za mikopo zinazotozwa na taasisi mbalimbali za kifedha.

Amesema mfumo huo unatarajiwa kuongeza ushindani miongoni mwa benki na taasisi za fedha, jambo ambalo linaweza kuchangia kupunguza gharama za mikopo na kuwasaidia wakopaji kufanya maamuzi sahihi kabla ya kukopa.

Aidha, Serikali imeendelea kuhimiza matumizi ya Credit Reference Bureau, mfumo unaohifadhi taarifa kuhusu historia ya ukopaji na ulipaji wa madeni ya wateja.

Naibu Waziri amesema matumizi ya taarifa hizo yanawezesha benki kutathmini kwa usahihi uwezo na historia ya mkopaji, hivyo kupunguza vihatarishi vya mikopo kutolipwa na gharama zinazotumika katika tathmini ya wakopaji.

Amesema hatua hizo, kwa pamoja, zinaweza kusaidia kupunguza gharama za mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara, licha ya Serikali kutokuwa na mamlaka ya kuweka moja kwa moja viwango vya riba vinavyotozwa na benki za biashara.

Kwa hiyo, Serikali imeeleza kuwa mkakati wake ni kutumia sera za fedha, kuongeza ushindani na uwazi katika sekta ya kifedha pamoja na kuimarisha mifumo ya taarifa za wakopaji, ili kuchochea upatikanaji wa mikopo yenye gharama nafuu zaidi.



Na Janeth Raphael - MichuziTv

Tume ya Madini imewapa siku 30 wamiliki wa baadhi ya miradi ya msaada wa kiufundi kurekebisha mapungufu yaliyobainika katika utekelezaji wa shughuli zao, huku ikionya kuwa kushindwa kutekeleza matakwa hayo ndani ya muda uliowekwa kunaweza kusababisha kuchukuliwa kwa hatua za kisheria, ikiwemo kufutwa kwa hati au idhini za msaada wa kiufundi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Katibu Mtendaji, Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwamo amesema hatua hiyo imekuja baada ya Tume kufanya ukaguzi wa miradi ya msaada wa kiufundi na kubaini kuwa baadhi yake haitekelezwi kwa kuzingatia matakwa ya sheria, kanuni na masharti yanayosimamia sekta ya madini nchini.

Kwa mujibu wa matokeo ya ukaguzi huo, jumla ya miradi 42 imebainika kuwa haifanyi kazi, wakati miradi mingine 86 inaendelea na shughuli zake lakini imeonekana kuwa na changamoto na mapungufu mbalimbali yanayohitaji kurekebishwa.

Kutokana na hali hiyo, Tume ya Madini imewapatia wamiliki wa miradi husika hati za makosa, zikiwaelekeza kurekebisha mapungufu yaliyoainishwa na kuwasilisha mrejesho ndani ya siku 30 tangu kutolewa kwa maelekezo hayo.

Tume imesisitiza kuwa muda huo si wa kupuuzwa, kwani iwapo wamiliki wa miradi watashindwa kutekeleza matakwa yaliyowekwa, hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria. Miongoni mwa hatua zinazoweza kuchukuliwa ni kufutwa kwa hati au idhini zinazohusiana na shughuli za msaada wa kiufundi.

Aidha, Tume imewataka wanufaika wa huduma za msaada wa kiufundi kuhakikisha shughuli zao zinafanyika kwa kuzingatia kikamilifu sheria, kanuni na masharti ya sekta ya madini, badala ya kusubiri hatua za utekelezaji zichukuliwe.

Katika maelekezo yake, Tume imekazia umuhimu wa kuzingatia masuala ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira, usalama na afya mahali pa kazi, pamoja na kuhakikisha shughuli zote za uchimbaji na huduma za kiufundi zinafanyika kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na mamlaka husika.

Tume imeeleza kuwa utekelezaji wa masharti hayo ni muhimu katika kuhakikisha shughuli za madini zinafanyika kwa usalama, zinazingatia mazingira na zinatoa manufaa yanayokusudiwa kwa wachimbaji, jamii zinazozunguka maeneo ya miradi na Taifa kwa ujumla.

Aidha, Tume imeonya kuwa itaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika miradi ya msaada wa kiufundi ili kubaini changamoto, kuhakikisha wamiliki wanazingatia matakwa ya kisheria na kuchukua hatua stahiki pale ambapo kutakuwa na ukiukwaji.

Hatua hiyo inalenga kuimarisha usimamizi wa shughuli za madini na kuhakikisha kuwa miradi yenye idhini inatekelezwa kwa ufanisi, kwa kuzingatia sheria na viwango vinavyotakiwa, huku ikihakikisha kuwa rasilimali za madini zinatumika kwa manufaa ya uchumi, jamii na Taifa.

Kwa wamiliki wa miradi iliyobainika kuwa na mapungufu, siku 30 zilizotolewa na Tume sasa ni muda wa kuchukua hatua za haraka kurekebisha kasoro hizo na kuwasilisha mrejesho, vinginevyo wanaweza kukabiliwa na hatua kali zaidi za kisheria, ikiwemo kupoteza hati au idhini zao.



Na Janeth Raphael - MichuziTv - Bungeni


Serikali imesema haina mpango wa kuunda Tume maalum ya Taifa ya kutatua migogoro ya ardhi nchini, badala yake imeandaa Mkakati wa Kudumu wa Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi Nchini utakaotumika na taasisi mbalimbali za Serikali katika kushughulikia migogoro hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kaspare Mmuya, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Asha Ramadhani Baraka, aliyetaka kujua lini Serikali itaunda Tume itakayokuwa na jukumu la kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Mmuya amesema Serikali imeona umuhimu wa kutumia mfumo wa pamoja unaowezesha taasisi zinazohusika kushughulikia migogoro ya ardhi kwa utaratibu unaofanana, badala ya kuanzisha Tume nyingine.

Amesema Mkakati huo utaiwezesha Serikali kuwa na kanzidata moja inayohifadhi taarifa za migogoro ya ardhi nchini, hatua itakayosaidia kuondoa changamoto ya mgogoro mmoja kushughulikiwa na taasisi zaidi ya moja na hatimaye kutolewa kwa maamuzi yanayotofautiana.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri, mfumo huo utasaidia kuongeza uelewa, uwazi na uwajibikaji miongoni mwa taasisi zinazohusika, huku ukiongeza kasi ya kushughulikia na kutatua migogoro ya ardhi.

Amesema Serikali inalenga kupitia mkakati huo kuimarisha amani, umoja na mshikamano katika jamii, sambamba na kuboresha mazingira ya uwekezaji katika ardhi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.

Naibu Waziri Mmuya amesema kwa sasa Mkakati wa Kudumu wa Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi Nchini upo katika hatua za ukamilishaji na mara utakapokamilika utaanza kutumiwa na taasisi zote husika.

Hatua hiyo inatarajiwa kuweka mfumo mmoja wa kitaifa wa kushughulikia migogoro ya ardhi, kwa kuimarisha uratibu wa taasisi za Serikali na kuhakikisha migogoro inashughulikiwa kwa ufanisi, uwazi na kwa maamuzi yanayokwenda sambamba.


Zaidi ya Shilingi milioni 700 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kashishi iliyopo Kata ya Nyakamwaga Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Shule hiyo inatarajiwa kuondoa adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata shule.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Ndugu Wazo Michael Mwang’onda, ndiye aliyeweka jiwe la msingi katika ujenzi wa shule hiyo wakati Mwenge ulipofika Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi, Mwang’onda amesema ameridhishwa na mradi huo ambao mpaka sasa umefikia asilimia 75 ya utekelezaji. Amesema ni shule ya kwanza ya Serikali yenye muonekano wa gorofa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Ameeleza kuwa shule hiyo ilianzishwa kwa nguvu za wananchi na baadaye kuungwa mkono na mdau wa maendeleo, Mhe. Evarist Gervas, ambaye ametumia zaidi ya Shilingi milioni 300 kukamilisha miundombinu.

Mwang’onda amesema mradi huo utakuwa na madarasa zaidi ya 8, matundu 12 ya vyoo pamoja na ofisi mbalimbali. Pia ametoa wito kwa wadau wengine kuiga mfano wa Mhe. Gervas kwa kuunga mkono juhudi za wananchi katika kukuza maendeleo ya elimu Kata ya Nyakamwaga.

Kwa upande wao wananchi wa Kijiji cha Kashishi wamesema walianzisha ujenzi wa shule hiyo ili kupunguza umbali wa watoto kwenda kusoma. Wamesema hapo awali wanafunzi walikuwa wakitembea umbali mrefu hadi Shule ya Sekondari Nyakamwaga na wengi waliishia kukatisha masomo.











Top News