Watoto 1,337,079, wanatarajiwa kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio mkoani Dar es Salaam.
Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa mkoa huo, Abdul Mhite, alipozindua kampeni ya chanjo hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dares Salaam, Albert Chalamila leo.
Mhite amesema kampeni hiyo itamalizika Agosti 30 mwaka huu na inalengakuwafiia watoto wote walio chini ya umri wa miaka 10.
Amesema , chanjo hiyo itahusisha watoto ambao pia waliwahi kupata chanjo hiyo awali.
“Tunawataka wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo hii hata kama awali mtoto aliwahi kuchanjwa. Chanjo itatolewa kwa mfumo wa matone,”amesema.
Ameeleza serikali imeandaa kampeni hiyo kwa lengo la kuongeza na kuimarisha kinga ya jamii dhidi ya ugonjwa wa polio kwa kuhakikishawatoto wote walengwa wanafikiwa.
Mhite amebainisha chanjo hiyo itatolewa nyumbakwa nyumba, mtaa kwa mtaa, shuleni, vituo vya afya, zahanati, hospitali , sehemu za ibada, stendi, katika vituo vya kulea watoto, viwanja vya michezo na maeneo mbalimbali katika jamii.
“Nawaomba wazazi na walezi mshirikiae na timu za chanjo zinapofika katika maeneo yenu.Pia muwaruhusu watoto kupata matone ya chanjo hii,”ameeleza Mhite.
Katibu Tawala huyo, ametoa wito kwa viongozi wa halmashauri, serikali za mitaa, viongozi wa dini, walimu , wahamasishaji wa jamii na wadau wote kushiriki kikamilifu katikakampeni hyo ili kufikialengo.
Awali Ofisa wa Wizara ya Afya Mpango wa Chanjo Salama, Zainab Nyamgumi, alisema chanjo hiyo ni muhimu kwa Watoto hata kama waliwahi kuchanjwa awali.
Amesema chanjo hiyo ni muhimu na inaelekezwa na Shiria la Afya Duniani (WHO) kwa nchi kuitumia.
“Hii chanjo inatolewa kama nchi inaonekana inahatari ya mlipuko wa ugonjwa wapolio. Ni chanjo ambayo kwenye ratiba ya kawaida ya utoaji wa chanjo haipo.
Ndiyo mana tunasema hatakama mtoto amekamilisha chanjo lazima na hii chanjo apewe,”amesema Zainab.Alibainisha ni chanjo maalumu ambayo WHO inaelekeza nchi kuitumia pindi kunapo kuwa na hatari hiyo.
“Kwa hiyo hata mtoto ambaye amekamilisha chanjo bado anahatari kama hatapewa hii chanjo iliyopendekezwa na Shirikala Afya Duniani,”amebainisha.
Mganga Mkuu wa Mkoawa Dar es Salaam, Mohamed Mang’una, amehamasisha wazazi, walezi na wananchi. Kuhakikisha Watoto walengwa wanafikiwa na kupata huduma hiyo itakayo tolewa bila malipo.