
Na Victor Masangu, Kibaha
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa Ndg Fadhili Maganya amempongeza Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Kibaha Dkt Rogers Shemwelekwa kwa kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo kwa kuweza kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo kupitia mapato yake ya ndani.
Pongezi hizo amezitoa wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha yenye lengo la kuweza kuangalia uhai wa chama cha mapinduzi (CCM) ikiwa sambamba na kuimarisha jumuiya zake zote za vijana, wazazi, na wanawake na kufuatilia utekelezji wa Ilani ya chama.
Katika ziara hiyo Mwenyekiti huyo ambaye pia ameweza kupata fursa ya kutembelea mradi wa Zahanati ya Kilimahewa ambapo ameridhishwa kuona ujenzi wa majengo yaliyopo yamejengwa katika kiwango kinachotakiwa na kwamba fedha zaidi ya kiasi cha shilingi milioni 285 zimetokana na mapato ya ndani.
"Nampongeza kwa dhati Mkurrugenzi mtendaji wa Manispaa ya Kibaha mji Dkt. Rogers Shemwelekwa kwa kuweza kuchapa kazi kwa bidii katika suala zima la utekelezaji wa ilani kwa vitendo kwani ameweza kutekeleza baadhi ya miradi kwa kutumia fedha za mapato ya ndani nampa hongera sana,"amebainisha Mwenyekiti wa Wazazi Taifa
Pia Mwenyekiti huyo akiwa katika mkuitano wake wa ndani na viongozi wa CCM pamoja na jumuiya za ke ambao umeefanyika katika shule ya Uongozi ya mwalimu Julias Nyerere amempongeza Mkurugenzi huyo kwa uwajibikaji na kusimamia vema utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na Halmashauri.
"Nimeridhishwa na huduma mnayotoa, nimeona mna idadi nzuri ya watumishi pia vifaa tiba sambamba na maji jambo ambalo ni muhimu sana katika zahanati, naipongeza Manispaa na nampongeza Mkurugenzi kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kujenga Zahanati hii kwa kutumia mapato ya ndani," amesema Maganya.
Maganya akizungumzia suala la zima la utoaji wa fursa za mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Manispaa, Maganya amesema pamoja na kazi kubwa waliyoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata mikopo hiyo isiyokuwa na riba bado kuna jukumu la kushuka chini zaidi ili kuwafikia wananchi wengi.
"Kitu kikubwa mkurugenzi pamoja na kufanya kazi nzuri sana katika mambo mbbali mnbali lakini kwa sasa hakuna budi kuwafikia wananchi wengi zaidi ili kupunguza malalamiko yanayotolewa na wananchi, nataka nione hii idadi uliyosema ya wajasiriamali 3000 vikundi 457 vinaongezeka na kuwa vingi zaidi"
Maganya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt Shemwelekwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kushirikiana na Viongozi wa CCM Wilaya ili kuendelea kuimarisha mahusiano mazuri baina ya Chama pamoja na Serikali.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt Shemwelekwa amesema katika kuhakikisha mikopo ya asilimia 10 inafika kwa wananchi yeye pamoja na tilmu yake walienda kwenye Kata 7 za Manispaa kwa ajili ya kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujiunga na vikundi vya wajasiriamali ili kuweza kupata mikopo hiyo isiyokuwa na riba.
"Mimi na timu yangu tulifika katika Kata 7 za Manispaa, tukatoa elimu ya mikopo na hadi kufikia mwaka 2026, tumevifikia vikundi zaidi ya 457 sawa na wajasiriamali 3,000 waliokidhi vigezo na tumewapatia mikopo hiyo na wanairudisha kwa wakati ili wananchi wengine waendee kuchukua,"amesema Dkt Shemwelekwa.
Ameongeza kuwa, wamekuwa na utaratibu mzuri wa kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi katika matukio yote na hata kwenye utoaji wa mikopo hiyo wa vikundi wamekuwa bega kwa bega katika kuimarisha mahusiano ya Chama na Halmashauri kwa ujumla.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe, Silvestry Koka amesema kwamba ataendelea kushirikiana bega kwa bega na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa lengo la kuweza kuendelea kukusanya mapato kwa lengo la kupata fedha ambazo zitatumika katika miradi mbali mbali ya maendeleo.
"Mimi kama Mbunge wa Jimbo hili nitahakikisha naendelea kushirikiana kwa dhati na watendaji wengine pamoja na mkurugenzi na lengo kubwa ni ni kuendelea kuwaletea wananchi chachu kubwa ya kimaendeleo na mimi nampongeza sana Mkurugenzi wetu Dkt. Rogers Shemwelekwa kwa kazi nzuri ambayo anaifanya ya ukusanyaji wa mapato ya ndani," amebaainisha Mbunge Koka.
Naye Meya wa Manispaa ya Kibaha Mjini Mhe. Dr Nicas Mawazo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazinkubwa anayoifanya na kuleta fedha kwa ajili ya maendeleo ya Manispaa ya Kibaha.
Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa upande wa suala la utoaji wa fursa za mikopo ya asilimia 10, kwa makundi ya vijana, walemavu na wakinamama hadi kufika mwaka 2026 imefanikiwa kutoa kiasi cha jumla ya Shilingi bilioni 3.1 katika vikundi vipatavyo 457.
Udhamini huo unalenga kumpunguzia Simbu changamoto za kifedha wakati wa maandalizi, ili aweze kuelekeza nguvu zake zote kwenye mazoezi na kuiwakilisha Tanzania vyema katika mashindano hayo ya kimataifa.
Akimkabidhi Simbu hundi ya udhamini huo jijini Arusha, Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, alisema benki hiyo imeamua kuwa sehemu ya safari ya mwanariadha huyo kutokana na rekodi yake ya kuendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Alisema NMB inaamini mchango huo utampa utulivu wa kufanya maandalizi yake bila vikwazo vya kifedha.
"Tunamwamini Simbu kwa sababu ameendelea kuiandikia Tanzania historia katika mchezo wa riadha. Tunaamini hata safari hii atafanya makubwa na kuendelea kulitangaza taifa letu," alisema Ladislaus.
Alimtakia Simbu maandalizi mema na mafanikio makubwa katika mashindano hayo.
Mbali na fedha hizo, NMB pia ilimkabidhi Simbu kadi ya benki pamoja na NMB Band, bangili ya malipo ya kidijitali inayotolewa kwa ushirikiano na Mastercard, ambayo itamwezesha kufanya malipo salama na kwa urahisi katika maeneo mbalimbali duniani yanayokubali Mastercard au Visa.
Kwa mujibu wa Ladislaus, huduma hiyo itarahisisha miamala ya kifedha ya mwanariadha huyo wakati wote wa safari na kipindi cha mashindano.
Akizungumza baada ya kupokea udhamini huo, Simbu alisema maandalizi yake yanaendelea vizuri na afya yake ipo katika hali nzuri huku akieleza kuwa analenga kutwaa medali ya dhahabu nchini Australia.
"Maandalizi yanaendelea vizuri na nina afya njema. Niko tayari kwa changamoto ya Sydney Marathon na nina imani kubwa ya kufanya vizuri. Lengo langu ni kurudi nyumbani na medali ya dhahabu," alisema Simbu.
Aliwataka Watanzania kuendelea kumuombea ili afanikiwe kutimiza ndoto hiyo na kuiletea nchi heshima.
Katika hatua nyingine, Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Rogath Steven, alisema maandalizi ya wanariadha yanaendelea vizuri chini ya usimamizi wa shirikisho.
Alisema Simbu pamoja na mwanariadha Magdalena Shauri wamekuwa wakifanya mazoezi katika eneo la Ilboru, Arusha, kutokana na mazingira na hali ya hewa inayofanana kwa kiasi kikubwa na ile ya Sydney.
"Maandalizi yanaendelea vizuri na tuna imani kubwa na wanariadha wetu. Tunaamini Tanzania ina nafasi nzuri ya kupigania medali ya dhahabu katika mashindano hayo," alisema Steven.
TCS Sydney Marathon ni miongoni mwa marathon kubwa duniani na mwaka huu inatarajiwa kushirikisha zaidi ya wakimbiaji 40,000 kutoka mataifa mbalimbali. Mbio za kilomita 42 zitaanzia Miller Street na kumalizikia katika eneo la Sydney Opera House Forecourt.
NAJUA wengi wetu tunamfahamu Mwanasheria maarufu nchini Fatma Karume ambaye anajulikana zaidi kwa jina la Shangazi.
Shangazi ambaye pia ni mwanaharakati alikuwa mstari wa mbele katika kuikosoa Serikali ya Awamu ya Tano iliyokuwa inaongozwa na Hayati Dk.John Magufuli.
Staili ya Shangazi katika kuikosoa Serikali uliwakwaza baadhi ya viongozi na hali hiyo ilisababisha kuingia kwenye changamoto mbalimbali katika shughuli zake za kisheria na za uwanaharakati.
Miongoni mwa changamoto ambazo Shangazi alizipitia ni pamoja na tukio la kupigwa bomu katika Ofisi za IMMMA Advocates ambapo Fatma Karume alikua Mshirika.
Wakati Fatma Karume a.k.a Shangazi anaendelea na harakati hizo alikuwa na Maria Sarungi na wawili hao walishiriki kufichua mengi ya Serikali ya Hayati John Magufuli.
Ndio waliofichua tuhuma za upotevu wa fedha Sh. Trilioni 1.5 trillion ambao Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)profesa Mussa Asad aliuandika kupitia ripoti yake.
Ripoti ya upotevu wa fedha hizo ukasababisha Profesa Asad kuondolewa kazini.Hivyo Dk.Magufuli akawa Rais wa kwanza tangu Uhuru kumfukuza CAG.
Fatma na Maria wakajipa kazi ya kuwa watetezi katika matukio yaliyokuwa yanatokea kwa mfano malalamiko ya watu kutekwa na wale waliokuwa wanaitwa wasiojulikana.
Waliotekwa kwa wakati ule walikuwepo pia kama kina Mo Dewji, Roma Mkatoliki, Mdude, Azory Gwanda.
Kwa wanaokumbuka vizuri baada ya Mama kuingia madarakani Shangazi aliamua kuwa mwanaharakati full time.Na wakati huo tayari Shangazi alikuwa amenyang’wanya kibali cha uwakili na IMMMA advocates walimtimua maana alikua hana muda wa kufanya kazi zao za uwakili.Kazi za uwanaharakati zilikua nyingi mno.
Hivyo katika awamu ya mama (Rais Dk.Samia) Shangazi na Maria walikua wameingia mfumo wa kulipwa fedha na NGOs kufanya uwanaharakati (Ford Foundation ikiwa moja wapo).
Hapo Fatma Karume alikubali hizo fedha lakini kumbuka alikua hana shida sana na hizo fedha kutokana na historia ya familia yake maana Babu yake Abeid Karume ndio aliyekuwa baba wa Taifa Zanzibar na baba yake akaja kuwa Rais wa Zanzibar.
Pia Shangazi bado alikuwa anapokea fedha za pango kwenye Jengo la IMMMA advocates, na pango za apartments alizojenga mume wake wa zamani ambazo wakagawana .Hivyo Shangazi hakuwa na dhiki ya fedha kama ilivyo kwa Maria.Kwa Maria yeye biashara inayomuweka mjini ni Uanaharakati.
Sasa Shangazi Fatma wakati nchi inaelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 akagundua biashara ya uanauharakati ina manufaa zaidi kwa watu ambao anawapigania kuliko manufaa yake.
Kuna makundi yaliyokuwa yametokea ndani ya CCM kuutaka Urais tulipokuwa tunaelekea 2025. Majina yaliyokuwa katika makundi kwa sasa tunayahifadhi kwa ile staili Nguruwe pita mkuki sina.
Katika uchaguzi ule mwaka 2025 baadhi ya waliokuwa ndani ya makundi kuutaka Urais walipanga na safu katika ngazi mbalimbali na hata kwa wabunge.
Harakati za hovyo na zisizo na tija kwa Taifa ndizo zilizosababisha na vurugu za Oktoba 29 mwaka 2025.Kupitia wanaharakati uchwara waliokuwa wanatumwa na wakubwa wao huko nje wakaja na Samia Must Go.
Hata hivyo wakati hayo yalipokuwa yakiendelea Shangazi aliona mwelekeo unavyoenda kuna damu zinakuja kumwajika kwenye uchaguzi wa mwaka 2025.Waliokuwa wanatoa fedha kufadhili hayo yote akili yao iko kwenye madini na gesi iliyoko Lindi na Mtwara.
Kwa Shangazi wakati wote alikuwa anawaza na kuangalia kama ndio Samia Must Go halafu nani anachukua madaraka na kwa manufaa gani yeye mwenyewe akaogopa zaidi!!!
Shangazi akajitafakari na kuona anayoyafanya hayana tija kwake wala kwa Taifa lake hivyo aliamua kwenda Hija na alivyorudi akaamua kuachana na Uwanaharakati na mambo machafu yote ya Dunia.
Kwa sasa Shangazi ameamua kuishi maisha yqnayompendeza Mungu,amesimama katika misingi ya imani yake ya dini ya Kiislamu na anaendesha maisha katika utaratibu wenye utu, ubinadamu.Sio Shangazi yule aliyekuwa moto na page yake ilikuwa ya Faya.Leo amepoa Shangazi na maisha yanaendelea.
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kulia), Mkuu wa Idara ya Biashara NMB, Deogratias Shirima (kushoto) wakifurahia tuzo za Benki Bora ya Huduma kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), zilizotolewa na Euromoney na Global Finance wakati wa hafla iliyowakutanisha NMB na Mtandao wa Wafanyabiashara Wakubwa Wanaohudumiwa na benki hiyo ‘NMB Business Executive Network’ iliyofanyika Ijumaa jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TTI, Leonard Shayo na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya High Quality, Selina Letara.WADAU wa mchezo wa uogeleaji Tanzania wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kiwango cha kimataifa kupitia programu ya wiki tatu iliyolenga kukuza vipaji vya waogeleaji vijana, kuimarisha uwezo wa makocha wa wazawa, pamoja na kuwaelimisha wazazi kuhusu namna bora ya kuwaunga mkono wanamichezo katika safari yao ya mafanikio.
Programu hiyo iliyopewa jina la Tanzania Performance Development Series 2026, imeandaliwa na RaceBetter kwa ushirikiano na Monti AquaForce, na itafanyika kuanzia Julai 28 hadi Agosti 14 katika Kampasi ya Mikocheni ya Shule ya Kimataifa ya Monti, jijini Dar es Salaam.
Mafunzo hayo yataongozwa na kocha mashuhuri wa kimataifa wa uogeleaji na mwanzilishi wa RaceBetter, Ben Lee, ambaye anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam Jumatatu kutokea nchini Marekani.
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Monti, Fatma Fernandes, alisema mpango huo unaashiria mwanzo wa ushirikiano wa muda mrefu unaolenga kuimarisha maendeleo ya mchezo wa uogeleaji nchini Tanzania kwa kuunganisha utaalamu wa kimataifa na uongozi wa ndani ili kujenga mfumo endelevu wa kukuza vipaji kuanzia ngazi ya msingi hadi ushindani wa kiwango cha juu.
Mfululizo wa mafunzo hayo utaanza kwa Warsha ya Maendeleo ya Makocha itakayofanyika Julai 28 hadi 30, ikiwakutanisha makocha wa uogeleaji, walimu na viongozi wa vilabu vya uogeleaji. Warsha hiyo inalenga kuboresha viwango vya ufundishaji huku ikiwapa makocha wa ndani fursa ya kujifunza na kufanya kazi bega kwa bega na Ben Lee katika kipindi chote cha kambi za mafunzo kwa wanamichezo.
Fatma alisema pia kutakuwa na kambi tatu za mafunzo kulingana na makundi ya umri wa washiri.
“Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 6 hadi 8, itafanyika kuanzia Julai 30 hadi Agosti 1. Itafuatiwa na Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 9 hadi 12 kuanzia Agosti 3 hadi 7. Programu hiyo itahitimishwa na Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 13 na kuendelea, itakayofanyika kuanzia Agosti 10 hadi 14.
“Aidha, kutakuwa na mfululizo wa mafunzo kwa wazazi, yatakayotolewa bila malipo sambamba na kambi hizo. Vipindi hivyo vitajikita katika lishe na urejeshaji wa nguvu kwa wanamichezo, kujenga kujiamini na ustahimilivu, pamoja na kuwasaidia wazazi kujenga utaratibu mzuri wa maisha unaowawezesha watoto wao kufanikiwa ndani na nje ya bwawa la kuogelea,” alisema.
Alisema programu hiyo itafanyika katika bwawa la kuogelea la mita 25 la Shule ya Kimataifa ya Monti, lenye viwango vya kimataifa kwa mashindano ya kozi fupi, na hivyo kuwapatia washiriki mazingira bora ya mafunzo.
Aliongeza kuwa idadi ya washiriki imewekewa ukomo ili kuhakikisha kila mshiriki anapata mafunzo ya karibu katika vikundi vidogo na ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa wakufunzi.
Akizungumza kuhusu programu hiyo, Ben Lee, ambaye ana uzoefu mkubwa wa kufundisha waogeleaji kuanzia ngazi ya maendeleo, vyuo vikuu hadi Olimpiki, alisema lengo kuu si kuwajengea waogeleaji kasi pekee, bali kuwajenga kama watu.
“Lengo letu si kuzalisha waogeleaji wenye kasi zaidi pekee. Tunataka kuwasaidia watu kuwa na uwezo zaidi, kujiamini zaidi na kuwa tayari kwa fursa na changamoto zitakazokuja mbele yao,” alisema.
Katika kipindi chake cha ukocha, Ben Lee amewafundisha wanamichezo wengi waliofanikiwa kujiunga na programu maarufu za NCAA nchini Marekani na kushiriki mashindano ya kimataifa. Pia amefanya kazi na vilabu vya uogeleaji, shule na mashirikisho ya kitaifa katika nchi mbalimbali duniani.
Na Victor Masangu, Kibaha
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Taifa Ndg. Fadhili Maganya amewaasa viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) ngazi za Wilaya pamoja na Mkoa wa Pwani kuhakikisha kwamba wanalivalia njuga suala la kero ya migogogoro ya ardhi sambamba na kusikiliza changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukijenga chama pamoja na kukagua uhai wake na kuimarisha jumuiya zake sambamba na kuangalia mwenendo mzima wa utekelezaji wa ilani ikiwemo kukagua na kutembelea baadhi ya miradi mbali mbali ya maendeleo.
Mwenyekiti huyo amebainisha kuwa katika ziara hiyo pia imelenga kukutana na viongozi mbali mbali wa serikali na kupokea taarifa zao zinazohusiana na suala zima la utekelezaji wa kazi zao ambazo wanazifanya katika maeneo yao kwenye nyanja mbali mbali za kimaendeleo.
"Nimeanza ziara yangu ya kikazi katika Wilaya ya Kibaha na lengo kubwa na kwamba ziara hii ni ya kikazi na lengo lake kubwa ni kuangalia uhai wa chama jinsi ilivyo, pamoja na jumuiya zake ikiwa sambamba na kuweza kuangalia na kutembelea miradi mbali mbali ya kimaendeleo na kuzungumza na wanachama," amebainisha Mwenyekiti huyo.
Pia Mwenyekiti huyo amewasihi wanachama na viongozi kuhakikisha kwamba wanaachana kabisa na tabia ya kuwasikiliza baadhi ya wanaharakati ambao wamekuwa wakibeza mambo mbali mbali ambayo yanatekelzwa na serikali ya awamu ya sita na badala yake wajikite zaidi katika kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi ambazo anazifanya.
Pia amewahimiza madiwani na viongozi wengine kuhakikisha wanaweka misingi imara ya kusimamia utoaji wa fursa za mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na halmashauri kwa lengo la kuwasaidia wajasiriamali waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini .
Aidha Mwenyekiti huyo hakusita kumpongeza kwa dhati Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwa kuweza kuchapa kazi kwa bidii pamoja na kuendelea kutekeleza ilani kwa vitendo katika suala zima la kusimamia fedha ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauru ya Manispaa ya Kibaha Dkt. Rogers Shemwelekwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge akitoa salama zake amesema kwamba Mkoa wa Pwani imeweza kuendelea kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu, afya, umeme, miundombinu ya barabara pamoja na ujenzi wa viwanda.
Naye Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa Hamoud Jumaa amesema kwamba lengo lake kubwa ni kuendelea kushirikiana bega kwa bega katika kuhakikisha chama cha serikali kinaendelea kuwa na mahusiano mazuri ikiwemo sambamba na kutekeleza ilani ya chama.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka amebainisha kuwa ni jukumu la wanachama kuendelea na kuweza kushikamana katika kukijenga chama ikiwa sambamba na kuiimarisha zaidi kwa vitendo jumuiya zake zote.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka amempongeza kwa dhati Mwenyekiti huyo kwa kuamua kufanya ziara ambayo itaweza kuleta uhai wa chama pamoja na kuimarisha jumuiya zake ikiwa pamoja na kutembelea miradi mbali mbali ya maendeleo.
Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka amempongeza Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Taifa kwa kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kuweza kuona umuhimu wa kufanya ziara yake ya kikazi ambayo itaweza kuleta matokeo chanya katika suala zima la kukiimarisha chama pamoja na jumuiya zake kwa pamoja.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ameanza ziara yake rasmi ya kikazi katika Mkoa wa Pwani ambapo ameanza katika Wilaya ya Kibaha ambapo ameweza kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo katika Zahanati ya Kilimahewa iliyopo kata ya Tangini, Kituo cha afya mlandizi pamoja na kutembelea mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi Mlandizi.

Mkuu wa wilaya ya Bahi Mhe. Joachim Thobias Nyingo amekabidhi gari jipya aina ya ‘Toyota Pickup’ kwa Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa wilaya hiyo Mha. Hopeness Liundi huku akitoa wito wa kutumia vizuri kitendea kazi hicho kwa kuongeza kasi ya utendaji kazi kwa tija ili kufikia lengo la kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwafikishia huduma ya Majisafi ya bomba wananchi wa wilaya hiyo.
Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika ofisi ya Meneja RUWASA Mkoa wa Dodoma Julai 27, 2026 na kuhudhuriwa na Meneja wa Mkoa huo Mha. Beatrice Kasimbazi pamoja na watumishi wengine wa mkoa huo.
Akizungumza kabla ya kuzindua na kukabidhi gari hilo, Mhe. Nyingo aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuiwezesha RUWASA na kuboresha utendaji wao wa kazi ikionesha dhamira ya dhati ya serikali kuwafikishia wananchi huduma muhimu ya majisafi ya bomba.
Hivi karibuni, Serikali kupitia RUWASA ilinunua na kugawa magari 22 katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kuboresha na kuimarisha utendaji wa taasisi katika kusimamia na kufuatilia miradi na huduma ya maji katika maeneo ya vijijini.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa wilaya Nyingo amemkaribisha Meneja mpya wa RUWASA wa mkoa wa Dodoma Beatrice Kasimbazi ambaye amehamishiwa mkoani humo akitokea mkoa wa Pwani, huku akitoa wito kwa watumishi wa wilaya hiyo kumpokea na kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya serikali na kuwahudumia wananchi.









Na Mwandishi wetu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaapisha Naibu Makatibu Wakuu wawili na kushuhudia viongozi wanne wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma, huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, ushirikiano, uwajibikaji na kuzingatia maslahi ya wananchi.
Akizungumza katika hafla iliyofanyika Ikulu, Tunguu, Zanzibar, Rais Samia amesema uteuzi wa viongozi hao unaonesha imani ambayo Serikali imewawekea, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanatoa huduma bora, kufanya kazi kwa weledi na kuleta matokeo yanayogusa maisha ya Watanzania.
Rais Samia ameielekeza Ofisi ya Makamu wa Rais kuendelea kuimarisha usimamizi wa masuala ya Muungano kwa kushughulikia changamoto zinazojitokeza kupitia ushirikiano, ili kuendelea kuulinda na kuuimarisha Muungano wa Tanzania. Pia amesisitiza umuhimu wa kusimamia kwa karibu programu za uhifadhi wa mazingira na hatua za kukabiliana na changamoto zinazotishia ustawi wa Taifa.
Aidha, ameagiza Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuendelea kuboresha usimamizi wa watumishi wa umma kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuongeza ubora wa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika sekta ya uchukuzi, Rais Samia amesisitiza kuongezwa kasi ya utekelezaji wa miradi ya reli, barabara, bandari na meli, pamoja na kutathmini fursa za kupanua biashara ya anga ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ili kuongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi.
Kwa upande wa sekta ya sheria, ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kuendelea kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi kupitia kampeni za msaada wa kisheria, ili huduma hizo ziweze kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati.
Vilevile, Rais Samia ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuongeza juhudi katika kukuza biashara na kuboresha usimamizi wa maonesho ya biashara nchini. Pia ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuimarisha ulinzi na usimamizi wa hifadhi za taifa na rasilimali za utalii, akieleza kuwa sekta hiyo ni nguzo muhimu ya uchumi wa Taifa.
Kwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha nafasi yake kama chombo cha Serikali na sauti ya Taifa kwa kuongeza ubora wa maudhui, weledi wa watumishi na ufanisi katika utoaji wa huduma za habari.
Walioapishwa ni Dkt. Latifa Mohammed Khamis, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano, pamoja na Bi. Prisca Burton Lwangili, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Viongozi wengine walioapa Kiapo cha Uadilifu ni Bw. Ephraim Balozi Mafuru, Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE; Bw. Salum Nassor Mnuna, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA; Bw. Massana Gibril Mwishawa, Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA; na Bi. Asha Dachi Mbaruk, Mkurugenzi Mkuu wa TBC.


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)









.jpeg)
.jpeg)










.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
