-Aomba Watanzania wafanye tathmini kwenye maeneo wanayoishi
-Ampongeza Mhe. Ndejembi kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imejipanga vema kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza wakati wa mvua kubwa za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi ujao hasa katika maeneo yanayopata mvua nyingi.
Ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma, leo (Alhamisi, Agosti 27, 2026) wakati akijibu swali la Mbunge wa Bukoba Mjini, Mha. Johnston Mutasingwa, kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu aliyetaka kujua Serikali imejipangaje kukabiliana na changamoto ya uharibifu wa miundombinu ya barabara na makazi ya wananchi kulingana na tahadhari ambayo imetolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) juu ya uwepo wa El-Nino yenye nguvu.
“Ni kweli tumepata tahadhari kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini juu ya uwepo wa mvua kubwa za El-Nino na hasa kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa ambako mvua hizo zinatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Septemba ama Oktoba mwanzoni. Serikali imejipanga kwa kuandaa mifereji katika maeneo hayo ili kuondoa uwezekano wa maji kurundikana.”
Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza TANROADS na TARURA zifanye ukaguzi wa barabara, madaraja, makalavati na mifereji ya maji ili kubaini mapema maeneo korofi yanayoweza kuathiriwa ili kuhakikisha wananchi hawakosi miundombinu kutokana na mafuriko.
“Bunge lako tukufu lilielekeza fedha za mifuko ya barabara ziwe zinakwenda moja kwa moja kwenye mifuko ya barabara badala ya Serikali kuu. Nimpongeze Waziri wa Fedha pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kuanza kutekeleza uamuzi huo ambapo kwa mwezi zaidi ya sh. bilioni 320 zinaenda moja kwa moja kweye mifuko na kuiwezesha kukabiliana na mambo kama haya,” amesema.
Amewataka Watanzania wachukue tahadhari kwa kila mmoja kufanya tathmini ya mahali wanapoishi kwa kuangalia mazingira ya mahali walipo kwani wanajua ni wapi maji huwa yanapita au yanatuama. “Tuendelee kuchukua hizo tahadhari ili maafa yasitokee ilhali tumeshatahadharishwa,” amesisitiza.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu amempongeza Deogratius John Ndejembi kwa kuaminiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kamati Kuu ya CCM na Halmashauri Kuu ya CCM na kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dkt. Mwigulu ameitumia nafasi hiyo pia kumpongeza Rais Samia kwa kuwa na jicho la kipekee hadi akamuona Mheshimiwa Ndejembi. Amesema kiongozi huyo anazo sifa zinazomfanya astahili kupewa dhamana hiyo kubwa ya kitaifa.
“Mheshimiwa Naibu Spika, Deogratius Ndejembi ni kiongozi mahiri sana, ni kiongozi makini, ni kiongozi mchapakazi anayefanya kazi bila kuchoka ili Watanzania waweze kupata manufaa. Ndejembi pia ana sifa za unyenyekevu na upole, ni mtu rahimu asiye na hiana ndani yake,” amesema.
Waziri Mkuu amemhakikishia Mheshimiwa Ndejembi kuwa yeye pamoja na mawaziri wenzake wako tayari kushirikiana naye wakati akitekeleza majukumu yake mapya katika kuijenga Tanzania.
MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Udhibiti wa Visumbufu Tanzania (TPHPA) imesema hatua za kudhibiti visumbufu na magonjwa ya mimea zimewezesha kuokoa mazao kwa kiwango kikubwa na kuimarisha uwezo wa Tanzania kufikia masoko ya kimataifa.
Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph Ndunguru, amesema hayo jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mamlaka kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na mipango ya mwaka 2026/27.
Amesema katika kipindi hicho, TPHPA iliweka nguvu katika kuimarisha afya ya mimea, kudhibiti visumbufu na magonjwa, kuboresha huduma za maabara, kutumia teknolojia za kisasa na kuhakikisha mazao yanayozalishwa nchini yanakidhi viwango vinavyohitajika katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wa udhibiti wa ndege waharibifu, Prof. Ndunguru amesema hatua zilizochukuliwa na Mamlaka zimefanikisha kuokoa takribani tani milioni moja za mazao, yakiwemo nafaka, mahindi, ngano na mpunga.
Katika kukabiliana na viwavi jeshi, TPHPA ilifanya udhibiti katika maeneo yaliyoathirika kwa kushirikiana na wakulima pamoja na kampuni zinazozalisha viuatilifu.
Juhudi hizo zilifanyika katika eneo la takribani ekari 228,525 na kusaidia kuokoa takribani tani 342,737 za mazao mbalimbali, huku mahindi yakiwa miongoni mwa mazao yaliyonufaika.
Aidha, TPHPA ilichukua hatua za kudhibiti changamoto ya balae fanya katika maeneo yaliyoathirika, hatua iliyosaidia kulinda takribani ekari 70,136 za mazao.
Prof. Ndunguru amesema mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha uzalishaji wa mazao nchini unaendelea kuwa salama na wenye tija, huku Tanzania ikiimarisha uwezo wa kuuza mazao yake katika masoko ya kimataifa.
Kwa mwaka wa fedha 2026/27, Mamlaka inalenga kuendeleza udhibiti wa visumbufu na magonjwa ya mimea, kuimarisha mifumo ya afya ya mimea na kuongeza matumizi ya teknolojia ili kulinda uzalishaji na ushindani wa mazao ya Tanzania katika masoko ya kimataifa.
Hayo aliyasema Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri katika hafla fupi ya ufunguzi wa kampeni ya utoaji chanjo ya Polio iliyofanyika katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Alhaj Shekimweri alisema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za serikali chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha afya za watoto nchini, akieleza kuwa watoto wamekuwa sehemu muhimu ya programu mbalimbali za afya zinazotekelezwa na serikali.
Aliongeza kuwa kama Wilaya ya Dodoma imepewea lengo la kuwafikia watoto 207,096 katika zoezi hilo, ikiwa ni sehemu ya jumla ya watoto 1,003,061 katika Mkoa wa Dodoma wanaolengwa katika maeneo husika.
“Viongozi, watendaji wa serikali, shule, kamati na bodi za shule wamehamasishwa kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo, ikiwamo kuwafikishia wazazi ujumbe kuhusu umuhimu wa kuwapeleka watoto kupata chanjo ingawa hatuna changamoto ya mgonjwa wa Polio nchini, ni muhimu kujihami kwa kuwakinga watoto wetu,” alisema Alhaj Shekimweri.
Kwa upande wake, mkazi wa Dodoma, Rosmith Mkoko aliishukuru serikali kwa kuwezesha upatikanaji wa chanjo hiyo, akiwataka wazazi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo.
“Chanjo ni muhimu katika kuwalinda watoto dhidi ya magonjwa na kwamba wazazi wanapaswa kutumia fursa hii kuhakikisha watoto wao wanapata kinga. Nawashauri wazazi wawalete watoto wapate chanjo hizi ili ziweze kuwalinda,” alisema Mkoko.
Zoezi hilo linatarajiwa kuendelea hadi tarehe 30 Agosti, 2026 kwa kushirikisha jamii, hususani wazazi na walezi, ili kuhakikisha watoto wote waliolengwa wanapata chanjo kwa wakati.
HALMASHAURI ya wilaya ya Siha inatarajia kutoa chanjo ya ugonjwa wa Polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka 10 wapatao 42049 ambapo wazazi na walezi wametakiwa kuhakikisha zoezi hilo linawafikia watoto wote walengwa ili kukabiliana na ugonjwa wa Polio.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Mkuu wa wilaya hiyo, Dkt. Christophe Timbuka wakati wa uzinduzi uliofanyika katika shule ya msingi Wiri ambapo kampeni hiyo itafanyika kwa siku nne na kudai kuwa, serikali imeendelea kuweka mkazo katika kuimarisha na kulinda afya za wananchi hususan afyavna usalama wa watoto.
Dkt. Timbuka alisema kuwa, ugonjwa wa Polio ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya Polio ambapo huathiri mfumo wa fahamu na kusababisha kupooza kwa viungo na hivyo kupelekea ulemavu wa kudumu.
"Jambo la msingi mnalopaswa kuelewa ni kwamba Polio inazuilika kwa chanjo na ndio maana Serikali inaendelea kuchukua hatua za kuhakikisha watoto wote walio katika kundi lengwa la umri chini ya miaka kumi wanapatiwa chanjo kwa wakati" alisema Dkt. Timbuka.
Alisema kuwa, Tanzania imeendelea kulinda mafanikio yake katika mapambano dhidi ya Polio, lakini bado tunapaswa kuwa waangalifu kutokana na uwepo na mzunguko wa virusi vya Polio katika baadhi ya maeneo ya Afrika na duniani.
Aliongeza kuwa, Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe inasisitiza kuwa, kampeni ya chanjo kwa watoto chini ya miaka 10 ni sehemu ya juhudi za kuongeza kinga ya jamii na kuzuia uwezekano wa maambukizi kwa hiyo, kampeni hiyo siyo jambo la kawaida la utoaji wa huduma za afya, bali ni juhudi ya kitaifa ya kulinda kizazi cha sasa na kijacho dhidi ya ugonjwa unaoweza kusababisha ulemavu wa kudumu na kupoteza nguvu kazi ya taifa letu.
Alibainisha kuwa, chanjo hiyo itatolewa katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha watoto wote wanafikiwa na timu ya wataalamu wa afya pamoja na wahamasishaji waliopata mafunzo watatoa chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya, Shule za Awali na Msingi, vituo vya malezi ya Watoto (Daycare), Makao ya Watoto, Maeneo ya mikusanyiko ya jamii, huduma za nyumba kwa nyumba na Maeneo mengine yatakayobainishwa katika mpango kazi wa Halmashauri za vijiji.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga mkuu wa wilaya ya Siha, Dkt. Nsubili Mwakapeje alisema kuwa, maandalizi yote ya utoaji chanjo yamekamilika kama serikali ilivyoelekeza ambapo timu za wataalam zipo tayari kuingia katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Siha kuwafikia watoto walengwa.
Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Siha, Dancan Urrasa alitumia nafasi hiyo kuwasihi Madiwani kutoa ushirikiano kwa wataalam hao wa afya kwa kuwaelimisha wananchi kuwatoa watoto waweze kupatiwa chanjo hiyo.
"Natambua sisi Madiwani ndio tupo karibu na wananchi wetu sasa tushirikiane na wataalam wetu wa afya kuwaelimisha wananchi wetu kutambua umuhimu wa chanjo hii ili waweze kuwatoa watoto wote walengwa wapatiwe chanjo kwa hizi siku nne za kampeni hii" alisema Urrasa.
Nkya, ambaye alipanda mlima Kilimanjaro kwa mara ya kwanza mwaka 2017 muda mfupi baada ya kumaliza chuo, anasema safari yake ya mwaka huu imekuwa ya tofauti kwa namna kadhaa. Amepanda mlima akiwa na uzoefu zaidi akiwa na maandalizi ya kutosha ya mwili na uelewa mzuri wa namna ya kukabiliana na uchovu, baridi na mabadiliko ya hali ya hewa kadri anavyopanda.
Tofauti nyingine kubwa ilikuwa mawasiliano; safari hii ameweza kuwasiliana na kutekeleza majukumu yake ya kikazi katika maeneo mengi ya mlima.
Akiwa katika safari hiyo, alitakiwa kurekodi na kutuma video, sauti, picha na taarifa mbalimbali kwa ajili ya matangazo ya redio na mitandao ya kijamii.
Anasema mtandao wa Viwango wa Yas ulimwezesha kuendelea kutekeleza majukumu yake katika maeneo mengi aliyopita kuelekea kileleni, huku pia akiendelea kuwasiliana na familia na marafiki.
“Tofauti na mwaka 2017 ambapo mawasiliano yalikua ni ya shida, safari hii mambo yalikua ni tofauti, nimeweza kutuma video, picha, sauti na kuwasiliana bila matatizo na watu wangu wa karibu,” anasema Nkya.
“Kupanda mlima Kilimanjaro si mchezo. Kuna wakati unahisi kabisa uko kwenye dunia nyingine. Mtandao wa viwango wa Yas ambao unapatikana vizuri kabisa katika maeneo mengi ya mlima tuliyopita umenisaidia kuendelea kutimiza majukumu ya kazi zangu bila shida.” anasema.
Nkya aliendelea na safari hiyo hadi kufika Uhuru Peak, mita 5,895 kutoka usawa wa bahari, kilele cha juu zaidi barani Afrika.
Anasema safari yake ya mwaka huu imempa picha tofauti na ile ya miaka tisa iliyopita, hasa kwa namna ambavyo mawasiliano yalivyorahisisha mambo mengi katika mazingira ya mlima huo wenye changamoto nyingi.
“Kwangu hii ndiyo maana ya Mtandao wa Viwango, mtandao unaokuwezesha kuendelea kufanya kile unachotaka kufanya hata ukiwa katika safari yenye changamoto. Nimepanda na Yas hadi Uhuru Peak na nimeendelea kuwasiliana na dunia,” anasema.
Kwa Nkya, kufika Uhuru Peak hakukuwa mwisho wa safari pekee, bali pia ujumbe kwamba kila mtu ana kilele anachotamani kukifikia.
“Kila mmoja wetu ana kilele anachopanda katika maisha yake. Cha kwangu safari hii kilikuwa Uhuru Peak.”
Na WMA - Mwanza
Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Mwanza umezitaka kampuni zinazojihusisha na uzalishaji wa mabati kuhakikisha zinazingatia matakwa ya sheria ya vipimo na viwango vya ubora vilivyowekwa, ili kulinda haki na fedha za wananchi.
Akizungumza mapema leo Agosti 27, 2026 mara baada ya zoezi la ukaguzi wa kushtukiza katika baadhi ya viwanda vya uzalishaji wa mabati mkoani Mwanza, Meneja wa Mkoa wa Wakala huo, Karim Zuberi, amesema kupitia kaguzi na taarifa zinazotolewa na wananchi, ndani ya kipindi cha mwaka huu, tayari wamebaini na kuchukua hatua dhidi ya wazalishaji watano waliobainika kuzalisha mabati yasiyokuwa na vipimo sahihi.
Zuberi amesema wananchi wanapaswa kuwa makini wanaponunua mabati na kutoa taarifa kwa mamlaka husika pindi wanapohisi kuuziwa bidhaa zisizokuwa na vipimo sahihi, akiwataka pia wafanyabiashara kuacha tabia ya kuwapotosha wateja kuhusu vipimo vya unene wa mabati.
Amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakitoa taarifa zisizo sahihi kwa wateja kwa kuwafanya waamini kuwa kadri namba ya 'Gauge' inavyokuwa kubwa ndivyo bati linavyokuwa bora, wakati kinyume chake ndicho sahihi, ambapo bati lenye namba ndogo ya "Gauge' huwa na unene mkubwa zaidi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu viwango vya bidhaa wanazonunua ili kuepuka udanganyifu unaoweza kusababisha hasara, hususan katika ujenzi wa makazi na miundombinu mingine.
Kwa upande wake, Biyolelo Ndaisaba, mmoja wa viongozi wa kampuni inayojihusisha na uzalishaji wa bidhaa hizo mkoani Mwanza, amesema udanganyifu katika vipimo vya mabati ni sawa na kuhujumu jasho la wananchi wanaotumia fedha zao kujenga makazi na kuendeleza shughuli nyingine.
Amesema kampuni yao imeendelea kuwa kinara katika kuzingatia usahihi wa vipimo vinavyotakiwa kisheria, akisisitiza kuwa wazalishaji wote wana wajibu wa kuhakikisha bidhaa wanazozipeleka sokoni zinakidhi viwango kwa manufaa ya walaji
Wakala wa Vipimo Mkoa wa Mwanza unaendelea na zoezi la ukaguzi wa bidhaa mbalimbali, linalofanyika kwa utaratibu wa kawaida pamoja na ukaguzi wa kushtukiza, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wananchi wanalindwa dhidi ya bidhaa zisizokidhi vipimo sahihi.
Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kumwona Deogratius Ndejembi kuwa miongoni mwa viongozi wanaoweza kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu ya kitaifa, akielezwa kuwa msaidizi wake mpya katika nafasi ya Makamu wa Rais.
Dkt Mwigulu ametoa pongezi hizo leo Alhamisi, Agosti 27, 2026, wakati akijibu maswali ya papo kwa papo katika Bunge jijini Dodoma, akianza kwa kumpongeza Ndejembi ambaye amependekezwa kushika nafasi hiyo.
Ndejembi, ambaye ni Mbunge wa Chamwino mkoani Dodoma, alipendekezwa jana Jumatano, Agosti 26, 2026, na vikao vya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pendekezo hilo limekuja baada ya Dk Emmanuel Nchimbi kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais, hatua iliyokubaliwa na Rais Samia.
Kabla ya kupewa nafasi hiyo, Ndejembi alikuwa Waziri wa Nishati, nafasi aliyohudumu akisimamia masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati nchini.
Akizungumza Bungeni, Dkt. Mwigulu amemtakia Ndejembi mafanikio katika jukumu hilo jipya, huku akimpongeza Rais Samia kwa kumuamini na kumteua kuwa sehemu muhimu ya uongozi wa Serikali.
Uteuzi wa Ndejembi sasa unafungua ukurasa mpya katika uongozi wa Serikali, huku akitarajiwa kuendelea na majukumu ya kitaifa kwa nafasi yake mpya baada ya taratibu za kikatiba kukamilika.
The cost for each LATRA licence is valued between TSh30,000 and TSh60,000, besides training fees, depending on vehicle category. This license allows drivers to lawfully carry passengers and access more public areas pick-ups and drop-offs. With a target of over 5000 drivers, Bolt’s investment may easily cross Tsh300,000,000, demonstrating public private partnership to ensure on-road compliance, safety, and peace of mind in the mobility sector.
The initiative comes as regulatory compliance continues to play a central role in strengthening road safety and consumer confidence. According to LATRA, the Authority issued 91,178 licences for private hire vehicles during the 2024/25 financial year, reflecting continued efforts to formalise and regulate the sector.
Speaking on the initiative, Dimmy Kanyankole, Senior General Manager, Bolt East Africa, said compliance should be viewed as a shared investment in safer mobility rather than simply a regulatory obligation.
"A licensed driver represents more than regulatory compliance—it demonstrates that the individual has met the standards required to provide safe and professional transport services. And we need more of these to meet growing demand for movement, a primary driver of Tanzania’s economy.
Bolt said the programme removes financial barriers that may prevent some drivers from completing licensing requirements and remain unqualified to become Bolt drivers and access income opportunities enjoyed by many drivers that partner with the nation’s largest ride-hailing player.
.jpeg)
.jpeg)


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Viongozi wapya wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) wameapishwa rasmi jijini Dar es Salaam, huku wakitakiwa kusimamia Katiba ya chama na kulinda maslahi ya wanachama katika utekelezaji wa majukumu yao.
Akizungumza wakati wa kuwaapisha viongozi hao, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, aliwataka kuzingatia Katiba ya TAPSEA na kuitumia kama mwongozo katika uongozi wao ili kuhakikisha wanachama wanaongozwa kwa haki na ufanisi.
Kiswaga amesema TAPSEA ni chama kikubwa chenye wajibu wa kuwatumikia wanachama wake, hivyo viongozi wanapaswa kuwa imara katika kusimamia maslahi yao na kuhakikisha chama kinaendelea kusonga mbele.
“Niwaombe viongozi mnapotoka hapa mkasimamie vyema Katiba yenu ili kuweza kuondoa migogoro itakayojitokeza,” alisema Kiswaga.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa TAPSEA, Leah Mwamba, aliwashukuru wanachama kwa kumpa dhamana ya kuwaongoza na kuahidi kushirikiana nao katika kuhakikisha chama kinafikia malengo yake. Amesema tukio la uapisho ni hatua muhimu katika safari ya uongozi na kuomba wanachama waendelee kuwaunga mkono.
“Ninatoa shukrani zangu za pekee kwa wote walioungana nasi katika historia hii. Jambo hili la uapisho ni kubwa sana, hivyo tunaomba mzidi kutuombea tufanye vyema katika uongozi,” alisema Mwamba.
Naye Katibu Mkuu wa TAPSEA, Hellen Magati, aliwashukuru wageni na wadau waliohudhuria hafla hiyo, akiahidi kuwa uongozi mpya utashirikiana na wanachama na wadau mbalimbali katika kutekeleza majukumu yake na kuimarisha chama.
Viongozi wengine walioapishwa ni pamoja na Makamu Mwenyekiti, Zainab Ibrahim Ally, Naibu Katibu Mkuu, Halima Twaha Mgulo, Mweka Hazina, Nyanza Msongela, pamoja na wajumbe wengine waliochaguliwa katika uongozi huo.



.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)





.jpeg)

.jpeg)




.jpeg)




.png)
.jpeg)
.jpeg)









