


MichuziBlogV2
Most read Swahili blog on earth
Bonyeza play kuangalia Michuzi TV LiVE
BONYEZA PLAY KUANGALIA AZAM TV LIVE
BONYEZA KUANGALIA CHANNEL TEN LIVE




Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Prof. Riziki Shemdoe (Wa pili kushoto) akizungumza katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.Naibu Waziri Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Dkt. Pius Chaya (Kulia) akisisitiza jambo wakati kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji kwenye wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga. Katikati ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza Dkt. Jumaa Mhina akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.
Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani, Dkt. Selemani Jafo, ametangaza mpango wa kuweka kambi maalum katika eneo la ujenzi wa Daraja la Kitomondo lililopo katika barabara ya Mzenga–Gwata, akilenga kuharakisha ukamilishaji wa mradi huo na kuondoa adha wanazokumbana nazo wananchi hasa nyakati za mvua.
Dkt. Jafo alitoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kata za Mzenga na Mafizi ndani ya Jimbo la Kisarawe, ambapo alikagua maendeleo ya mradi huo na kusikiliza changamoto za wananchi wanaotegemea daraja hilo kwa shughuli za kila siku.
Daraja la Kitomondo linajengwa na kampuni ya Neloyt Tanzania Limited kwa gharama ya shilingi milioni 359.67 chini ya usimamizi wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), hata hivyo ujenzi wake umechelewa kukamilika hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wa Mzenga na Mafizi.
Mbunge huyo amesema daraja hilo ni kiungo muhimu kwa wakazi wa kata hizo na vijiji vya Mafizi, Nyani, Gwata na Ving’andi, akieleza kuwa kuchelewa kwake kumeathiri shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo usafiri wa wanafunzi, wagonjwa na wafanyabiashara.
Amesisitiza kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutarahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao na bidhaa, hivyo kuchochea maendeleo katika Jimbo la Kisarawe.
Kwa upande wake, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kisarawe, Eng. Africano Orota, amemhakikishia Dkt. Jafo kuwa wataongeza usimamizi na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.

Na. Vero Ignatus,Arusha.
Serikali imepiga marufuku watumishi wa Uma Kutumia mitandao isiyo rasmi ambayo ni tofauti na ile iliyounganishwa na mfumo wa Serikali mtandao katika kutuma nyaraka na taarifa mbalimbali za serikali kwani si salama kwa usalama wa nchi na wananchi
Marufuku hiyo imetolewa l9 April 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete wakati akifunga kikao kazi cha 6 cha serikali mtandao kilichofanyika kwa siku Tatu mkoani Arusha nakusema kwamba watumishi wa Umma kutumia mifumo isiyo rasmi ni hatari kwani inasababisha nyaraka za siri za serikali kuonekana mtandaoni.
Bado tunao wafanyakazi wa Serikali wanatumia Mtandao binafsi kurusha taarifa za Serikali jambo ambalo siyo sawa kwa taarifa hizo za Serikali kuwekwa wazi jambo hilo liwe narufuku kuanzia Leo taarifa za Serikali kutumwa kwa Mtandao binafsi. Alisema
Kikao Kazi hicho cha siku tatu, kimewakutanisha takribani washiriki 1,000 kutoka sekta za umma na binafsi, na kimejadili kwa kina masuala muhimu yanayohusu ujenzi, uendelezaji na usimamizi wa jitihada za Serikali Mtandao. Ambapo Kupitia mijadala hiyo wamepata fursa ya: Kutathmini utekelezaji wa maazimio ya Kikao Kazi kilichopita,, Kubainisha mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa miradi ya TEHAMA Serikalini,
Pia waliweza Kujadili changamoto zilizopo na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana nazo,Na kuweka maazimio mapya yatakayotuongoza katika hatua zinazofuata za kuendelea kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma za umma kwa njia ya kidijitali.
Kikwete amesema amefarijika kuona kuwa, mijadala yote imejikita katika uzingatiaji wa Sheria, Kanuni,Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, jambo ambalo ni msingi muhimu wa kuhakikisha miradi ya TEHAMA Serikalini inakuwa salama, endelevu na yenye kujali Katika kikao kazi hiki,
Sambamba na hayo Serikali kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), itatoa tuzo kwa taasisi zilizofanya vizuri katika kuzingatia Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, kwenye utekelezajiwa miradi ya TEHAMA.ambapo amezipongeza taasisi zote zilizotunukiwa tuzo hizo na kusema Tuzo hizo si za heshima tu, bali ni chachu ya kuhamasisha ubora, uwajibikaji na uzingatiaji wa misingi ya Serikali Mtandao katika taasisi zote za umma.








