Taswira ya Hospitali Kuu ya Rufaa ya Rais Julius Nyerere (Hospital dos Queimados Presidente Julius Nyerere) iliyopo Kilamba, jijini Luanda, nchini Angola.
Taswira ya Hospitali Kuu ya Rufaa ya Rais Julius Nyerere (Hospital dos Queimados Presidente Julius Nyerere) iliyopo Kilamba, jijini Luanda, nchini Angola.
.jpeg)
.jpeg)

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi, akizungumza wakati wa semina maalum ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
*Mmoja atoa ushuhuda wa ‘Tunalipa Jana’
*Bunge: tunawashukuru PSSSF kwa elimu
Morogoro, Julai 31, 2026
Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.
Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.
“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Bi. Angelina Sanga.

Mtumishi kutoka Ofisi ya Bunge, Bi. Angelina Sanga (kushoto), akiwa na Afisa Matekelezo kutoka PSSSF, Bi. Upendo Chilewa, wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bi. Sanga alipokuwa akijisajili kaaika huduma ya mifumo ya kidijitali.
Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.
Katika semina hiyo Mtumishi Mstaafu wa Bunge Bw. Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto, akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa ajili ya Makatibu wa Kamati za Bunge mjini Morogoro.
Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Bw. Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine

Mtumishi Mstaafu wa Bunge, Bw. Gerald Magili, akitoa ushuhuda wake wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bw. Magili aliipongeza PSSSF kwa kulipa mafao yake kwa wakati
“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Bw. Hajji Moshi.
Kwa upande wake, Bw. Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi (kushoto), akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto (kulia), mara baada ya kuhitimishwa kwa semina ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro.
Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kwa umakini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajj Moshi (kulia), wakati wa semina ya kujenga uelewa wa Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
VIWANJA vya Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Mbeya vilitikiswa na shangwe na nderemo kufuatia mkutano mkubwa uliowakutanisha maelfu ya madereva wa bodaboda na bajaji wa Jiji hilo ana kwa ana na Mkuu wao wa Wilaya, Mhe. Solomon Itunda kuzungumzia amani na utulivu.
Mkutano huo, ambao ulitawaliwa na hali ya kirafiki na maelewano, haukuwa tu wa kutoa maagizo, bali ulikuwa ni jukwaa la kimkakati la kuwakumbusha vijana hao nafasi yao nyeti katika uchumi na usalama wa Jiji la Mbeya.
Akizungumza huku akishangiliwa na umati huo, Mhe. Itunda aliwaeleza madereva hao ukweli usiofichika kuwa wao ni injini muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa mustakabali wa nchi.
Alisema kutokana na asili ya kazi yao ya kukutana na mamia ya wananchi kila siku, wana nguvu kubwa ya kujenga au kubomoa taswira ya jiji katika sekta ya usafiri kwa kuwaeleza tofauti na uhalisia wa nchi inavyoendeshwa.
Hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya, ambaye amekuwa akisifika na wananchi wa Mbeya kama 'Mzee wa busara', aliwasihi madereva hao wa bodaboda na bajaji kuendesha vyombo vyao kwa umakini mkubwa na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kunusuru maisha yao na ya abiria wao.
"Ndugu zangu wa bodaboda na bajaji, sisi ni watu wa Mbeya, tunapokuwa kazini tulinde amani yetu. Nyie mkiwa mabalozi, lakini pia ni vizuri mkalinda amani ya nchi kwa kuhubiri amani kwa abiria wenu," alisema Itunda.
Katika kile kilichoonyesha kutambua mazingira wezeshi ya biashara, Mkuu huyo wa Wilaya alitumia jukwaa hilo kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Itunda aliweka wazi kuwa msingi imara wa amani, utulivu, na uhuru wa kiuchumi uliojengwa na Rais Samia ndio unaowapa vijana wengi fursa ya kujitafutia kipato mitaani bila bughudha.
Akifafanua kuhusu fursa za kiuchumi, DC Itunda aliwafafanulia wananchi hao kuwa awali mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji haikuwa ikiwafikia walengwa, lakini Rais Samia ameweka utaratibu mpya unaohakikisha kila kijana aliyekuwa kwenye kikundi ananufaika.
Aliwataka vijana hao, kama miongoni mwa wanufaika, kulinda fedha za mikopo wanayopewa na kuirejesha kwa wakati, ili asilimia hiyo 10 iweze kuwanufaisha vijana wengi zaidi wa Jiji hilo baada ya maboresho hayo makubwa.
DC Itunda aliwataka bodaboda hao kuunga mkono juhudi hizo za Rais kwa vitendo, huku wakiweka maslahi ya Tanzania mbele, ili kuhakikisha makundi ya vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu yanawezeshwa na kuifanya Tanzania yenye watu milioni 65 kupiga hatua kiuchumi.
Hata hivyo, kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Wilaya, Mhe. Itunda hakusita kugusa mshipa wa usalama. Aliwapa onyo na kuwasihi vijana hao kutokubali kutumika kama daraja la uhalifu. Aliwaomba wawe walinzi wa kwanza wa Jiji kwa kutoa taarifa za siri kwa vyombo vya dola mara wanapobaini watu wasioeleweka.
"Jiepusheni na makundi yenye mwelekeo wa kuvunja sheria. Ushirikiano wenu na Serikali ndiyo nguzo pekee itakayotuhakikishia Mbeya inabaki kuwa salama kwa maendeleo endelevu," alisisitiza Mhe. Itunda.
Kauli hizo za DC ziliingia vizuri masikioni mwa madereva hao, ambao kwa upande wao hawakuwa na hiyana. Wakizungumza kwa niaba ya wenzao, viongozi wa bodaboda waliipongeza Serikali kwa kuendelea kuwathamini na kutatua changamoto zao.
Kama ishara ya kukubaliana na mwongozo wa DC Itunda, madereva hao waliweka ahadi nzito mbele ya mamlaka kuwa kuanzia sasa watakuwa mabalozi wazuri wa usalama barabarani, watafichua wahalifu wote wanaochafua taswira ya kazi yao, na watalinda amani ya Mbeya kwa nguvu zao zote.
Na Mwandishi wetu, Mirerani
WADAU wa madini ya Tanzanite, mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro, Mkoani Manyara, wamechangia Sh23.6 milioni kwa ajili ya kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha ya watoto wachanga njiti.
Lengo ni kuunga mkono mkoa wa Manyara, ambao umeandaa mbio za hisani za kuchangia ujenzi wa jengo la mama na mtoto na kuboresha huduma za afya zitakazofanyika mjini Babati, Agosti 22, 2026 mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba.
Wadau hao wa madini ya Tanzanite, wamechangia kiasi hicho mbele ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Cuthbert Sendiga kwa nia ya kukusanya kiasi cha Sh1.6 bilioni cha kuanza ujenzi kwenye hospitali ya wilaya ya Hanang'.
Sendiga amewashukuru wadau hao wa madini ya Tanzanite kwa kuchangia fedha hizo ili kufanikisha ujenzi huo wa wodi ya watoto njiti.
"Mmefanya jambo kubwa mno kwani watoto njiti 3,000 kila mwaka kwenye mkoa wetu huwa wanazaliwa kwa hiyo tunataka tufanye jambo la baraka kwa watoto wanaozaliwa chini ya miezi tisa," amesema RC Sendiga.
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro, Fakii Lulandala ameeleza kwamba wadau wa madini ya Tanzanite watajitokeza kwa wingi kuunga mkono mbio hizo za kusaidia watoto njiti.
"Mimi binafsi nitakimbia kilomita tano na wana Simanjiro kwa umoja wetu tutashiriki kwa wingi mbio hizo kuchangia matibabu ya watoto wetu," amesema Lulandala.
Mkurugenzi wa JS Magezi, William Magezi wanaochimba kitalu D extension kwa kushirikiana na Tanzanite Afrika, amesema wadau wanaochangia wanakuwa wanatoa sadaka ambayo pia inakuwa toba kwa makosa yaliyofanyika.
"Mkurugenzi mwenza wa Tanzanite Africa Will Mushi alichangia Sh2 milioni na mimi nachangia Sh2 milioni hivyo jumla tumetoa Sh4 milioni," amesema Magezi.
Mkurugenzi wa JN Mining Justin Nyari ambaye amechangia Sh2 milioni ameeleza kuwa wadau wa nyanja tofauti washirikishwe katika sadaka hiyo.
"Hili jambo ni zuri mno katika kuokoa maisha ya watoto wetu, ushauri wangu wote wapitiwe kwa kupitia viongozi wetu wa kata na vitongoji ili kila mmoja ashiriki vile alivyojaliwa," amesema Nyari.
Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara wa madini mkoa wa Manyara, Mokia Ole Mrefu amesema ili kuunga mkono tukio hilo, jumanne ijayo watafanya kikao na wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite ili kwa umoja wao nao wachangie.
"Pia nikiwa hapa hapa mdau wa maendeleo wa mkoa wa Manyara, Taiko Ole Kulunju, amechangia kwa kutuma Sh1 milioni na mimi binafsi nachangia Sh500,000 ili kumuunga mkono RC wetu Sendiga," amesema Ole Mrefu.
Mmiliki mwingine wa mgodi wa madini ya Tanzanite, Joseph Manga ambaye amechangia Sh1 milioni ametoa ombi la kurekebishwa changamoto ya bei ya kibali cha kununua zana za milipuko.
"Tunakuunga mkono RC wetu kwenye hili ila tunakuomba utuangalie suala la sisi wachimbaji kulipia Sh100,000 kwa kila kibali cha kununua milipuko siyo sawa, kibali kiwe kimoja kwa bei hiyo hiyo," amesema Manga.





.jpeg)


.jpeg)





.jpeg)






.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)







.jpeg)
.jpeg)