Shirika la Madini la Taifa ( STAMICO) katika muendelezo wa kuhakikisha linaendelea kuwa kinara katika kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi Tanzania nzima, leo tarehe 11/8/2026 imeingia mkataba mnono wa pande tatu kati ya STAMICO, Chuo cha Mafunzo na taasisi ya FDH ya kuhakikisha magereza yote ya Zanzibar yanaanza kutumia Nishati ya Rafiki Briquettes.
Makubaliano hayo yamefanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar na kushuhudiwa na Kamishna wa Magereza Zanzibar Khamis Abdalah Khamis pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Dkt Venance Mwasse na Mkurugenzi wa FDH Bwn Michael Salali.
Akiongea katika hafla hiyo, Dkt Mwasse ameipongeza taasisi ya FDH kwa kufanikisha kuingia makubaliano haya ambayo yatawezesha Magereza zote za Zanzibar kupata Nishati hii ya Rafiki Briquettes ambayo inaenda kuleta afueni kwenye gharama za Nishati kwa Magereza lakini pia kuanza kutekeleza agenda ya Nishati Safi kwa taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100.
"Suala la Nishati Safi ni Agenda ya Kitaifa na sisi STAMICO tumeibeba kwa mikono miwili kuhakikisha tunatumia Nishati yetu ya Rafiki Briquettes kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi" amesema Dkt Mwasse
Dkt Mwasse pia ameahidi kusaidia kuleta mafunzo na Kongamano la kuhamasisha matumizi ya Nishati Nzima kwa Watumishi wa Magereza na Wananchi wote wa Zanzibar.
Awali akiongea na kutoa salamu kutoka FDH, Bwn Salali ameahidi kuhakikisha taasisi yake kwa kushirikiana na STAMICO itahakikisha Nishati hii inafika kwenye Magereza yote kwa wingi na inafika katika ubora unaostahili.
Naye, Kamishna Khamis ameishukuru na kuipongeza STAMICO kwa kuhakikisha Nishati hii inafika Zanzibar.
Ameomba pia STAMICO iangalie kuwapa fursa hii ya kusambaza Nishati hii kwa wale wafungwa ambao wamemaliza vifungo vyao ili iwe njia ya kujitengenezea Kipato baada ya kumaliza vifungo vyao.
Kamishna ametoa rai kwa taasisi nyingine kuhakikisha ziznaanza kutumia Nishati Safi kuendana na agenda ya kitaifa ya Nishati Safi ili kulinda mazingira.
Naye, Mwenyekiti wa Wanawake na Samia Bi Fatuma Madidi ameipongeza STAMICO kwa juhudi za kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi na akapigia msumari kwenye suala la kuhakikisha na taasisi yake hiyo inashiriki kikamilifu kuisambaza Nishati ya Rafiki Briquettes katika kona zote za Tanzania.
STAMICO imejipanga kuhakikisha inaendelea kuwa kinara katika kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi Tanzania Nzima.
Na Farida Saidi Morogoro
Wanafunzi 6,800 kutoka nchi tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamewasili mkoani Morogoro kushiriki Mashindano ya Michezo ya Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEASSA) 2026, yanayotarajiwa kuanza rasmi kesho, Agosti 12, hadi Agosti 23, mwaka huu.
Mashindano hayo, yanayofanyika kwa mara ya 23 katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na mara ya tano nchini Tanzania, yatawakutanisha wanafunzi kutoka Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro, Mkuu wa Mkoa huo, Adam Kighoma Malima, amesema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imejipanga kuhakikisha mkoa huo unakuwa mwenyeji bora wa mashindano hayo.
Amesema jumla ya viwanja 21 pamoja na maeneo manane ya malazi vimetengwa kwa ajili ya washiriki wa mashindano hayo.
Malima amewahakikishia washiriki kuwa ulinzi na usalama umeimarishwa vya kutosha, huku akiwataka wananchi wa Morogoro kuchangamkia fursa za kiuchumi zitakazotokana na ujio wa maelfu ya wageni.
Aidha, amewataka wakazi wa mkoa huo kuwakaribisha wageni kwa ukarimu na kutumia mashindano hayo kujenga mahusiano mazuri kati ya Tanzania na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Amesema Tanzania itawakilishwa na wanafunzi 1,510 kutoka mikoa 26 ya Tanzania Bara, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya washiriki kutoka nchini humo katika historia ya mashindano hayo.
Kwa upande wa Morogoro, Malima amesema mkoa huo utashiriki katika michezo 13 baada ya kufanya vizuri katika mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA yaliyofanyika mkoani Iringa Juni mwaka huu.
Kwa ujumla, FEASSA 2026 itahusisha michezo 20 kwa wanafunzi wa shule za sekondari, michezo sita kwa shule za msingi na michezo minne kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Malima amesema ujio wa maelfu ya washiriki na wageni unatoa fursa kubwa kwa wananchi kunufaika kiuchumi kupitia biashara, usafiri, chakula, malazi na huduma mbalimbali.
Ameongeza kuwa mashindano hayo pia yatatoa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vya Morogoro na Tanzania kwa ujumla kwa wageni kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki.
Ufunguzi rasmi wa mashindano hayo unatarajiwa kufanyika Agosti 16, ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia mashindano hayo na kuwakaribisha wageni kwa ukarimu, huku akivitaka vyombo vya habari kutumia fursa hiyo kuitangaza Morogoro na Tanzania kwa ujumla.
Akizungumza mara baada ya upasuaji huo, Dkt. Victor Ngotta, Bingwa wa Upasuaji wa Watoto wa MNH, amesema mafanikio hayo yanaonyesha uwezo wa hospitali kushughulikia kesi ngumu na adimu zinazohitaji utaalamu wa hali ya juu, na ni hatua muhimu katika kuendelea kuimarisha huduma za upasuaji wa kibingwa nchini.
Dkt. Ngotta amesema upasuaji huo ulihitaji maandalizi ya kina na ushirikiano wa wataalamu kutoka fani mbalimbali kutokana na hali ya kipekee ya mtoto huyo, ambaye alikuwa na pacha aliyekuwa na mikono, miguu na sehemu ya kiuno pekee huku akimtegemea mwili wa mwenzake kwa ukuaji na uhai.
Mafanikio ya upasuaji huo yanaendelea kuimarisha nafasi ya Hospitali ya Taifa Muhimbili kama kituo kinachoongoza nchini katika utoaji wa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi.
Mtoto anaendelea vizuri na yupo chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari
Na: Calvin Gwabara – Dodoma.
Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria
(OCPD) imeendelea kuwekeza katika kuwaendeleza watumishi wake kitaaluma kwa
kuwapatia fursa za mafunzo ndani na nje ya nchi, hatua inayolenga kuongeza
idadi ya wataalamu wenye weledi, utaalamu wa kisekta na uwezo wa kuandaa sheria
bora zinazowezesha utekelezaji wa sera na mipango ya Serikali.
![]() |
| Mwandishi Mkuu wa Sheria (CPD) Bwana Onorius John Njole wakati akiongea na Mwandishi wetu kuhusu mpango huo wa mafunzo. |
Hayo yamebainishwa na Mwandishi
Mkuu wa Sheria (CPD) Bwana Onorius John Njole wakati akiongea na Mwandishi wetu
kuhusu jitihada zinazochukuliwa na ofisi yake katika kuiwezesha nchi kupata
sheria bora zinazokwenda na wakati.
Bwana Njole amesema Uandishi wa Sheria
ni taaluma maalumu yenye misingi, kanuni na viwango vyake, hivyo inahitaji
mafunzo mahsusi na uwekezaji endelevu katika kujenga uwezo wa wataalamu.
“Ingawa Waandishi wa Sheria ni
Wanasheria, si kila Mwanasheria ni Mwandishi wa Sheria mtu anakuwa Mwandishi wa
Sheria baada ya kupata taaluma maalumu ya uandishi wa Sheria,” amesema Njole.
Amesema mkakati wa Ofisi hiyo
haujajikita katika kuwafundisha waandishi namna ya kuandika sheria pekee bali
pia kuwajengea utaalamu katika sekta ambazo sheria wanazoandika zinalenga
kuzisimamia kwa kuwa uelewa huo huwasaidia kutambua mahitaji halisi ya sekta na
kuandaa sheria zinazoweza kutatua changamoto na kuwezesha utekelezaji wa
mipango ya Taifa.
Mwandishi huyo Mkuu wa Sheria
amesema kwa kutambua umuhimu wa taaluma hiyo, Ofisi ya Mwadishi Mkuu wa Sheria
(OCPD) imekuwa ikiwapeleka watumishi kupata mafunzo katika vyuo na taasisi
mbalimbali ndani na nje ya nchi zilizobobea, huku baadhi wakipata utaalamu
katika maeneo mahsusi kama Kodi, Sheria za Bahari na Uandishi wa Sheria.
Aidha amesema kuwa OCPD pia
imeweka mkazo katika mafunzo ya ndani kwa kuwa sehemu kubwa ya uandishi wa
sheria hujifunzwa kupitia utekelezaji wa majukumu ya kila siku. Ofisi hiyo
imekuwa na mfumo wa kufundishana baina ya waandishi wa sheria, ikiwemo madarasa
ya maeneo mbalimbali ya uandishi wa sheria yanayofanyika kila Jumatatu.
“Katika mwaka uliomalizika, Waandishi
wawili walipelekwa Chuo cha West Indies, wengine tisa Chuo cha Sheria cha
Zambia kwa ajili ya mafunzo ya uandishi wa sheria, huku mpango wa mwaka 2026
ukilenga kupeleka waandishi wengine wawili Zambia na wawili katika Chuo cha
Sheria cha London” alieleza Njole.
Aliongeza “Uwekezaji huu pia
unalenga kuwa na wataalamu wenye utaalamu wa kisekta, ambapo katika mwaka
uliomalizika waandishi wawili walipata shahada za uzamili katika eneo la kodi,
huku waandishi wanne wakipata shahada za uzamili katika Sheria za Bahari nchini
Malta”.
Mwandishi huyo Mkuu wa Sheria alisema
lengo la muda mrefu ni kuhakikisha Tanzania inakuwa na wataalamu wa kutosha
katika uandishi wa sheria wenye uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndani na pia kutoa
huduma za uandishi wa sheria katika nchi nyingine, hususan ndani ya Jumuiya ya
Madola.
Miongoni mwa wanufaika wa mpango
huo ni Boniphas Mondu Giabe aliyepata
fursa ya kusoma Shahada ya Uzamili katika Uandishi wa Sheria katika Chuo Kikuu
cha West Indies, Kampasi ya Cave Hill, nchini Barbados ambaye amesema mafunzo
hayo yamemsaidia kuongeza ujuzi katika Uandishi wa Sheria na kumjengea uelewa
wa umuhimu wa kuandaa sheria kwa lugha inayoeleweka kwa urahisi na
inayozingatia misingi ya kikatiba na haki za binadamu.
“Moja ya mambo muhimu
niliyojifunza ni kwamba sheria zinapaswa kuandikwa kwa lugha na mtindo
unaowawezesha watumiaji kuzielewa kwa urahisi lakini pia zinapaswa kuzingatia
misingi ya kikatiba pamoja na haki za binadamu,” amesema Giabe.
Amesema maarifa aliyoyapata
katika maeneo ya sheria za utawala, sheria za katiba, mafuta na gesi
yanaendelea kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake, huku akishirikisha
ujuzi huo na waandishi wengine wa sheria katika kuandaa sheria bora na
zinazotabirika.
Nae mnufaika mwingine Bi. Loveness Jacob aliyepata ufadhili wa
Shahada ya Uzamili katika Sheria za Kimataifa za Baharini kutoka Chuo cha
Kimataifa cha Sheria za Baharini (IMO International Maritime Law Institute –
IMLI), nchini Malta, ambapo amesema mafunzo hayo yamemwongezea utaalamu katika
eneo muhimu la kimkakati kwa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.
“Utaalamu nilioupata utasaidia
katika uandaaji wa Sheria zinazotokana na mikataba ya kimataifa ya baharini,
uandaaji wa nyaraka za utekelezaji wa mikataba hiyo na kuimarisha usimamizi wa
masuala ya bahari na kuchangia katika kukuza uchumi wa buluu kupitia uandishi
wa sheria za sekta hiyo, alisema Jacob.
Amesema mafunzo hayo pia yamempa
fursa ya kupata uzoefu wa vitendo katika masuala ya sheria za kimataifa kupitia
ushiriki katika mkutano wa Kamati ya Kisheria ya Shirika la Kimataifa la Bahari
(IMO Legal Committee) ambapo alijifunza namna nchi zinavyoshiriki katika
mijadala ya kimataifa na kuwasilisha hoja za kisheria.
Aidha kwa upande wake Bi. Winfrida Mwera ambaye ni Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi wa Uandishi na Ufasiri wa Sheria Ndogo katika OCPD, aliyepata fursa ya
kusoma Postgraduate Diploma in Legislative Drafting, kwa lengo la kuimarisha
uwezo wake katika kuandaa na kurekebisha miswada ya sheria, amesema mafunzo
hayo yamemwongezea ujuzi katika matumizi ya mbinu na misingi mbalimbali ya
uandishi wa sheria, pamoja na uwezo wa kuandaa sheria zilizo wazi, sahihi na
zenye ufanisi.
“Nitatumia ujuzi na maarifa
niliyoyapata kupitia mafunzo haya katika kuandaa rasimu za sheria zenye ubora
wa juu, kupunguza mapungufu katika uandishi wa sheria na kutoa mchango wenye
tija katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku ya OCPD,” amesema Mwera.
Amesema uwekezaji huo umechangia
kuongeza uwezo wa watumishi na kuboresha utendaji wa taasisi huku akitoa wito
wa kuendelea kutolewa kwa fursa za mafunzo kwa wataalamu wengine.
Katika kuhakikisha mafunzo
wanayoyapata kutoka ndani na nje ya nchi Ofisi hiyo ina siku maalumu kila wiki
kwa wahitimu kukutana na watumishi wenzao na kuwafndisha na kujengeana uwezo
kupitia mafunzo ya ndani ili wote wanufaike na kuchangia ubora wa kazi za ofisi
kwa maslahi mapana ya Taifa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amewasilisha Maelezo ya Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.2) wa Mwaka 2026 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments ) (No.2) Bill, 2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 11 Agosti, 2026 Bungeni Jijini, Dodoma.
Aidha, Mhe. Johari ametoa maelezo ya Serikali kuhusiana na Muswada huo unaolenga kufanya marekebisho katika Sheria kama vile Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, Sura ya 166, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka ya Wilaya) Sura ya 287, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288, Sheria ya Baraza la Usalama la Taifa, Sura ya 61, Sheria ya Uthamini na Usajili wa Wathamini, Sura ya 138 na Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria inayoongozwa na Mwenyekiti Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) imepokea na kujadili maelezo Serikali kuhusiana na Muswada huo.

Na Janeth Raphael - MichuziTv
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka wananchi wanaomiliki silaha kuhakikisha wanakamilisha taratibu zote za kisheria na vibali vinavyohitajika kabla ya Agosti 30, 2026, akieleza kuwa operesheni maalum ya ukaguzi wa silaha itaanza mara baada ya muda huo.
Chalamila ametoa agizo hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo , akisisitiza kuwa wamiliki ambao kwa sababu mbalimbali, ikiwemo kusahau au kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu taratibu, hawajakamilisha malipo ya vibali au hatua nyingine za kisheria, wanapaswa kutumia muda uliopo kufika katika mamlaka husika na kurekebisha hali hiyo.
Amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha silaha zinazomilikiwa na wananchi katika Mkoa wa Dar es Salaam zinakuwa na kumbukumbu na vibali halali vinavyotambulika kisheria, kabla ya kuanza kwa operesheni hiyo.
Kwa upande mwingine, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watu wanaomiliki silaha bila kufuata sheria kuzisalimisha kwa hiari katika Jeshi la Polisi au kituo cha Polisi kilicho karibu kabla ya operesheni kuanza. Amesisitiza kuwa hatua hiyo inaweza kusaidia wahusika kuepuka kukumbana na hatua za kisheria zitakazochukuliwa baada ya ukaguzi kuanza.
Aidha, Chalamila ametoa mwito kwa familia ambazo ndugu zao wamefariki huku wakiacha silaha zenye vibali halali kuhakikisha hazizifichi wala kuzihamisha bila kufuata utaratibu. Badala yake, amewataka kuwasilisha taarifa pamoja na silaha hizo kwa mamlaka husika ili kupata maelekezo ya kisheria kuhusu namna ya kushughulikia umiliki huo.
Kuhusu silaha zinazoripotiwa kuibiwa, amewataka wamiliki kutoa taarifa Polisi na kufuata taratibu zote zinazohitajika. Amesisitiza kuwa silaha hizo zinapopatikana, wahusika hawapaswi kuzificha au kuendelea kuzitumia bila kufuata maelekezo ya mamlaka.
Chalamila amesisitiza kuwa Agosti 30, 2026 ndiyo mwisho wa muda uliotolewa kwa wamiliki kuhakikisha wanakamilisha taratibu zao, akieleza kuwa baada ya tarehe hiyo operesheni maalum ya ukaguzi itaanza na yeyote atakayebainika kumiliki silaha kinyume cha sheria atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Amewataka wananchi kutotumia muda uliobaki kupuuza agizo hilo, bali kuhakikisha mapema kuwa umiliki wa silaha zao uko katika hali halali na unaotambulika na mamlaka, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha udhibiti na usalama wa silaha katika Mkoa wa Dar es Salaam.


.jpeg)
















.jpeg)

.jpeg)
%20%20Bwana%20Onorious%20John%20Njole.jpg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)










.jpeg)



