Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM: Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO), Boniventura F. Mwalongo, ametoa salamu za pole na rambirambi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia msiba wa mume wake, Marehemu Hafidh Ameir.

Katika salamu zake, Mwalongo ameeleza masikitiko na huzuni kubwa kufuatia msiba huo, huku akimtakia Rais Samia, watoto, familia, ndugu, jamaa pamoja na wote walioguswa na msiba huo kupata faraja, nguvu, subira na moyo wa uvumilivu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Amesema katika kipindi hicho kigumu cha majonzi, familia inahitaji nguvu na faraja ili kukabiliana na wakati huo wa huzuni.

“Tunamuomba Mwenyezi Mungu, kwa rehema na upendo wake, ailaze roho ya Marehemu mahali pema na amsamehe makosa yake yote. Amina,” amesema Mwalongo.

Ameongeza ujumbe wa pole kwa Rais Samia, familia pamoja na Taifa kwa ujumla, akiwataka kuwa na moyo wa subira katika kipindi hicho cha majonzi.

“Pole sana Mheshimiwa Rais. Pole kwa Familia. Pole kwa Taifa. Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja katika kipindi hiki cha majonzi,” amesema.

Boniventura F. Mwalongo Katibu Mkuu – TRAMEPRO

Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania.

Dar es Salaam

Katika kile kinachoelezwa kuwa ni hatua madhubuti ya kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika makao makuu ya muda ya Tanzania Bloggers Network (TBN) yaliyoipo Dar es salaam, Kijitonyama na kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wakuu wa mtandao huo.

Mazungumzo hayo yaliyolenga kujenga ushirikiano wa manufaa ya pande zote mbili yamejikita katika kuimarisha uhusiano wa kisekta kwenye masuala ya habari, uelimishaji wa umma, na usambazaji wa maarifa sahihi kuhusu mifumo ya pensheni na uwekezaji nchini.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alieleza utayari wa mtandao huo kusimama kidete kama chombo cha kutoa elimu na kusambaza maarifa sahihi kwa umma na katika nyanja za kidijitali (space). Hata hivyo, alisisitiza kuwa ili kufikia malengo hayo kwa ufanisi zaidi, ni muhimu wanachama wa TBN wenyewe wakapatiwa kwanza mafunzo ya kina na ya kutosha kuhusu shughuli na uendeshaji wa mfuko huo.

Ushirikiano huo unatazamiwa kufungua ukurasa mpya katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni kufikisha elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi wengi zaidi nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa msafara huo kutoka PSSSF, Abdul Njaidi, alieleza kuwa ziara hiyo inalenga kujenga uhusiano wa karibu na wadau wa sekta ya habari pamoja na kutoa elimu kwa jamii. Aliwahakikishia viongozi wa TBN kuwa maombi na hoja zote zilizowasilishwa zitafanyiwa kazi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo mpya unalenga kuhakikisha wananchi wanapata uelewa mpana na sahihi kuhusu masuala ya pensheni na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, ambaye alishiriki katika mkutano huo, alieleza kuwa mtandao huo wenye historia kubwa unajivunia weledi na ufanisi mkubwa.

Alisema TBN ipo kwa ajili ya kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali ili kuchochea na kutanua zaidi gurudumu la maendeleo ya taifa.

Katibu wa TBN, Rahel Pallangyo, aliongeza kuwa mtandao huo upo tayari kutoa waandishi wake mahiri na kutumia majukwaa yake mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na za kuaminika zitakazowezesha kufanikiwa kwa utekelezaji wa majukumu ya wananchi na wadau wa maendeleo.

Katika mkutano huo, ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na Abdul Njaidi, ulijumuisha maofisa wengine akiwemo Regina Kumba, Grayson Mgunda, na Doreen Lyimo.

Kwa upande wa TBN, viongozi waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti Beda Msimbe, Katibu Rahel Pallangyo, mtaalamu wa mawasiliano, Cathbert Kajuna na Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi.











Na Mwandishi Wetu. Ubungo, Dar es Salaam

MBEZI. Shule ya Msingi Godiana iliyopo Mtaa wa Mpigi Mgoe, Kata ya Mbezi, Wilaya ya Ubungo, imeadhimisha mahafali yake ya tisa ya kuwapokeza wahitimu wa Darasa la Saba.

Mahafali hayo yalihudhuriwa na viongozi wa Kata ya Mbezi, uongozi wa shule, walimu, wazazi pamoja na wanafunzi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Diwani wa Kata ya Mbezi, Mheshimiwa Pius Nyatori, aliipongeza shule hiyo kwa juhudi zake katika kutoa elimu na kuahidi kushirikiana na uongozi wa shule pamoja na wadau kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili shule hiyo.

Miongoni mwa changamoto hizo ni barabara, umeme na maji, ambazo zinaathiri mazingira ya kujifunzia na shughuli za kila siku za shule.

Nyatori alisema suala la maji ni miongoni mwa changamoto zinazohitaji kufanyiwa kazi, akieleza kuwa atazungumza na wadau na mwekezaji ili kuona namna ya kupata ufumbuzi.

“Tunatambua shida ya maji hapa. Tutaongea na mwekezaji ili tuone jinsi ya kuwekeza, kwa sababu watu wengi wanategemea shule hii,” alisema Nyatori.
Kwa upande wake, mmiliki wa Shule ya Godiana alisema ataendelea kushirikiana na serikali, walimu na wazazi kuhakikisha watoto wanapata elimu katika mazingira bora.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Godiana, Bw. Macmin  Silumbu, alisema shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika matokeo ya kitaifa na anaamini wahitimu wa mwaka huu watafanya vizuri zaidi.

“Leo tumefanikiwa kuwa na mahafali ya tisa. Ukweli ni Mungu ametujalia. Tuna walimu ambao wameshafundisha na tunaamini watoto wetu wanaenda kufanya vizuri,” alisema Silumbu.

Uongozi wa shule umetoa wito wa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Kata ya Mbezi pamoja na wadau mbalimbali ili changamoto za barabara, umeme na maji zipatiwe ufumbuzi na kuwezesha wanafunzi kusoma katika mazingira bora.







 

ALGIERS: Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, leo amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda vya Dawa wa Algeria, Dkt. Wassim Kouidri, katika ofisi za Wizara hiyo jijini Algiers, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizo katika sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba.

Mazungumzo hayo yamejikita katika namna ya kukuza ushirikiano wa kitaalamu na uwekezaji katika sekta hiyo, ambayo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeipa kipaumbele katika jitihada za kuongeza uzalishaji wa dawa nchini na kukidhi mahitaji ya soko la ndani pamoja na masoko ya ukanda wa Afrika.

Akizungumza katika mazungumzo hayo, Balozi Matinyi alimweleza Waziri Kouidri kuwa Serikali ya Tanzania imeweka vivutio maalum kwa ajili ya uwekezaji katika sekta ya viwanda vya dawa, huku viwanda vitano vikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi na vingine zaidi vikitarajiwa kujengwa.

“Serikali imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha viwanda vya dawa na vifaa tiba katika ukanda wa nchi za Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika wenye watu takribani milioni 350,” alisema Balozi Matinyi.

Kwa upande wake, Waziri Kouidri aliahidi ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria kwa Tanzania, hususan katika eneo la utaalamu na teknolojia za kisasa za utengenezaji wa dawa na vifaa tiba.

“Ni kweli, Tanzania ipo kwenye eneo zuri la kimkakati la ukanda mkubwa wa Afrika na Algeria iko tayari kushirikiana nayo kitaalamu ili kuhakikisha inafikia malengo yake,” alisema Waziri Kouidri.

Aidha, Balozi Matinyi aliikaribisha nchini Algeria kupitia Mamlaka ya Taifa ya Bidhaa za Dawa (ANPP), ambayo inatarajiwa kuwasili Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu kwa mwaliko wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA).

Ziara hiyo inatarajiwa kutoa fursa kwa mamlaka hizo kujadili na kuweka mikakati ya namna bora ya kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kitaalamu, ikiwemo udhibiti na uzalishaji wa dawa na vifaa tiba.

Tanzania inaheshimika barani Afrika katika eneo la udhibiti wa dawa, ikiwa ni nchi ya kwanza barani Afrika kufikia kiwango cha ML3 mwaka 2018 chini ya mfumo wa tathmini ya viwango vya udhibiti wa dawa (GBT) wa Shirika la Afya Duniani (WHO), unaopima ubora na ufanisi wa mifumo ya udhibiti wa dawa katika nchi.

Tangu mwaka 2020, nchi nyingine tisa za Afrika zimefikia kiwango hicho cha ML3, huku hakuna nchi barani Afrika ambayo imefikia kiwango cha juu zaidi cha ML4.

Nchi hizo ni Afrika Kusini, Ethiopia, Ghana, Misri, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal na Zimbabwe.

Kwa upande mwingine, Algeria ni miongoni mwa nchi zinazoongoza barani Afrika katika sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba, ikiwa na jumla ya viwanda 230, sawa na takribani theluthi moja ya viwanda 690 vya aina hiyo vilivyopo barani Afrika.


Na Karama Kenyunko - Michuzi tv

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeelezwa kuwa Mwenyekiti CHADEMA, Tundu Lissu, hakuwa na ufahamu wa uwepo wa waandishi wa habari katika mkutano wa chama hicho na watia nia uliofanyika Aprili 3, 2025.

Shahidi wa nne wa utetezi, Brenda Rupia, ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, amedai hayo leo Septemba 7, 2026 mbele ya jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru akisaidiana na jaji Fednand Kiwonde na James Karayemaha alipokuwa akitoa ushahidi katika kesi ya uhaini inayomkabili Lissu.

Brenda amedai kuwa, Lissu hakuwa ameandaa mkutano huo wala aliyealika vyombo vya habari, akieleza kuwa jukumu hilo lilifanywa na Sekretarieti ya CHADEMA chini ya Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika.

Amesema yeye ndiye aliyeandika taarifa kwa umma na watia nia kuhusu mkutano huo Machi 27, 2025, na kuiweka katika kurasa za chama kwenye mitandao ya kijamii, huku waandishi wa habari wakialikwa kufanya coverage ya mkutano huo.

Kwa mujibu wa Brenda, takribani watu 250 walihudhuria mkutano huo, wakiwemo watia nia, wajumbe wa Sekretarieti, viongozi wakuu wa CHADEMA pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali, akiwemo Jambo TV.

Brenda amedai Lissu alikuwa mzungumzaji mkuu katika mkutano huo na alitoa hotuba kuhusu msimamo wa chama wa “No Reforms, No Election”, huku akisisitiza kuwa hakumuona akifanya jukumu lingine lolote katika mkutano huo.

Kuhusu maudhui yaliyorushwa na Jambo TV, shahidi huyo amesema yaliyorekodiwa na chombo hicho yalikuwa mali ya Jambo TV na kwamba Lissu hakuwa mfanyakazi wa chombo hicho wala hakuhusika na kurusha matangazo hayo.

Baada ya ushahidi huo, Mahakama iliahirisha kesi hadi kesho saa tatu asubuhi huku Jaji Dustan Ndunguru akieleza kuwa kesi hiyo imeongezewa siku 14 kuanzia leo kwa ajili ya kukamilisha mwenendo wake.



Na Mwandishi wetu Dodoma

Wanawake katika Jeshi la Magereza wametakiwa kuongeza ujuzi, maarifa na uwezo wa kutumia teknolojia za kidijitali ili kuendana na mabadiliko ya kiutendaji na kuongeza nafasi yao katika uongozi pamoja na majukumu ya kitaaluma ndani ya Jeshi hilo.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, Septemba 7, 2026, jijini Dodoma, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mtandao wa Wanawake wa Jeshi la Magereza Tanzania (TPSWNet) 2026.

Mhandisi Mahundi amesema dunia ya sasa inahitaji watumishi wenye uwezo wa kujifunza na kubadilika kulingana na maendeleo ya teknolojia, akisisitiza kuwa wanawake wanapaswa kutumia fursa zinazotokana na mabadiliko ya kidijitali katika kuboresha utendaji wao wa kazi na huduma zinazotolewa na Jeshi la Magereza.

Amesema uwezeshaji wa wanawake hauishii katika kuwapa nafasi, bali unapaswa kwenda sambamba na kuwaandaa kwa elimu, ujuzi na uwezo wa kushindana kwa haki katika nafasi mbalimbali za uongozi na kitaaluma.

“Nawahimiza wanawake wa Jeshi la Magereza kujiamini, kuongeza elimu na ujuzi na kujiandaa kwa ushindani wa haki katika nafasi za uongozi na kitaaluma. Katika dunia ya sasa, watumishi wanapaswa kuendelea kujifunza na kutumia teknolojia katika kuboresha huduma,” amesema Mhe. Mahundi.

Kwa mtazamo huo, Naibu Waziri amesema wanawake wa Jeshi la Magereza wana nafasi muhimu ya kuwa sehemu ya mageuzi yanayoendelea katika sekta ya urekebishaji wa wafungwa, huku wakitakiwa kutumia uwezo na uzoefu wao kuchangia katika kujenga Jeshi linalokwenda sambamba na mahitaji ya wakati.

Kwa upande wake, Kamishna wa Divisheni ya Sheria na Uendeshaji wa Magereza, CP Nicodemus Menyiansumba Tenga, amesema mafanikio yaliyofikiwa na wanawake wanaoshika nafasi mbalimbali ndani ya Jeshi hilo ni ushahidi wa uwezo wao na yanapaswa kuwa chachu kwa wanawake wengine kujituma na kuwania nafasi za uongozi na kitaaluma.

Akisoma taarifa ya Mtandao wa Wanawake wa Jeshi la Magereza Tanzania, Kamishna wa Huduma za Urekebishaji Jeshi la Magereza, CP Amina Jumanne Kavirondo, amesema TPSWNet imeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwawezesha wanawake, kukuza usawa wa kijinsia na kujenga mazingira rafiki ya kazi kwa watumishi wanawake.

Amesema mtandao huo pia unalenga kuhakikisha wanawake wanapata uwakilishi katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Jeshi pale inapowezekana, huku ukiendelea kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika majukumu ya urekebishaji wa wafungwa pamoja na masuala ya ulinzi na usalama.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mchango wa wanawake katika urekebishaji wa wafungwa unaonekana pia kupitia shughuli mbalimbali za kuwapatia wafungwa ujuzi na kuwaandaa kurejea katika jamii wakiwa na uwezo wa kuendesha maisha yenye tija.

Mkutano huo pia unajadili namna ya kuimarisha uwezo wa wanawake katika uongozi, kujitambua na kufanya maamuzi, sambamba na kubadilishana uzoefu na ujuzi wa kitaifa, kikanda na kimataifa kuhusu urekebishaji wa wafungwa.

Mbali na masuala ya uongozi na utendaji, washiriki wanajadili pia malezi, maendeleo ya awali ya mtoto, wajibu wa kijamii, uwezeshaji wa kiuchumi, maadili, afya na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii.

Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mtandao wa Wanawake wa Jeshi la Magereza Tanzania 2026 unafanyika jijini Dodoma kuanzia Septemba 7 hadi 9, 2026, ukiwakutanisha wanawake wa Jeshi la Magereza pamoja na wadau mbalimbali.

Mkutano huo umebeba kaulimbiu “Wanawake Mahiri, Jeshi la Magereza la Kisasa, na Taifa lenye Ustawi kuelekea Dira 2050.”









 



DODOMA, September 7, 2026:

UNESCO, in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, has launched a programme to establish and strengthen Information and Communication Technology (ICT) Clubs in public schools in Dodoma and Morogoro, aimed at equipping girls with digital skills, confidence and knowledge to pursue education and careers in technology.


The initiative is being implemented under the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls,” which seeks to reduce the gender gap in digital education and expand opportunities for women and girls to participate fully in the technology sector.












Speaking during the official launch held today at Edema Conference Hall in Kisasa, Dodoma, UNESCO Tanzania Head of Education Sector, Dr Faith Shayo, said the initiative was designed to encourage girls to develop an interest in technology, build confidence and explore opportunities in ICT-related education and careers.



She said the ICT Clubs would provide students with opportunities for practical learning, innovation and the development of skills to use technology to address challenges in their communities.

Dr Shayo said the programme would also involve ICT teachers and student teachers, with the clubs serving as platforms for extracurricular activities that give students practical experience beyond regular classroom lessons.



She said challenges contributing to the digital divide included disparities in access to technology, digital skills and competencies, as well as limited opportunities for girls to gain first-hand knowledge of education and career pathways in technology-related fields.



The programme is being implemented in collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), and the Tanzania Institute of Education (TIE).

A total of 20 public schools are expected to participate, with 10 from Morogoro Municipality and 10 from Dodoma City. The programme will directly benefit 500 girls and 40 teachers.



The official launch marks the beginning of a series of activities under the programme, with a four-day ICT Innovation Bootcamp scheduled to begin tomorrow, September 8, at Msalato, and run through Friday, September 11, 2026.

The Bootcamp will provide students with opportunities for practical learning, digital skills development and innovation, including developing and showcasing digital ideas and projects aimed at addressing real-life challenges in their communities.



In Dodoma, participating schools include Dodoma, Kisasa, Nara, Ihumwa, Makole, Mnadani, Hazina, Mtumba and Msalato, all secondary schools.

Through the ICT Clubs, students will receive practical training in computer programming (coding), computational thinking and problem-solving, digital creativity, visual and audio content production, and the safe and responsible use of technology.



The girls will also be connected with women ICT professionals through mentorship programmes, enabling them to learn from their experiences and gain a broader understanding of education, employment and career opportunities in the technology sector.

PMO-RALG STRESSES COLLABORATION

Speaking on behalf of the Prime minister Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), Mr. Francis Gervas, from the Education Management Department, thanked UNESCO for partnering with the Government in implementing the initiative.

He stressed the importance of continued collaboration among stakeholders to ensure that the programme achieves its intended objectives and that the results and lessons generated are sustained beyond the implementation period.

Mr. Gervas also called for the initiative to be expanded to other parts of the country so that more girls could benefit, while urging participants and stakeholders to remain committed to its effective implementation.

TEACHER CALLS FOR ATTITUDE CHANGE
Meanwhile, Mr Godfrey Robin Mseti, a teacher at Mtumba, commended the Government and UNESCO for introducing the initiative, saying opportunities and training related to technology had for a long time been perceived as being more accessible to boys and men.

He said society needed to change the perception that ICT-related learning was mainly for boys, stressing that girls also had the ability and should be given equal opportunities to learn, participate in and benefit from technology.

Under the programme, the ICT Clubs are intended to provide safe and inclusive learning environments where students can develop their skills through learning, innovation, leadership and collaboration.
Girls are expected to account for at least 50 per cent of participation in the clubs, with stakeholders encouraged to promote even greater representation.

Overall, the initiative is expected to strengthen ICT Clubs in 20 schools and enable 500 girls to improve their digital skills, confidence, participation and leadership abilities, while increasing their awareness of education and career opportunities in ICT.

The programme seeks to ensure that girls acquire not only the skills to use technology, but also the confidence to view technology as a tool for innovation, education and building their future careers.



Na; Mwandishi wetu-Tanga.

Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa la Kuendeleza Kilimo (IFAD) na wataalamu kutoka katika sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) wamekutana Mkoani Tanga Tarehe 7 Septemba 2026 kwa lengo la kufanya mapitio ya Utekelezaji wa Programu hiyo.

Sambamba na hilo timu hiyo itatembelea maeneo yanayotekeleza Programu kwa Mkoa wa Tanga, ambapo kwa upande wa sekta ya kilimo timu hiyo itatembelea kata ya Msomela iliyopo katika Halmashauri ya Handeni Vijijini ambako programu imehamasisha na kutoa elimu ya kilimo bora kwa jamii ya kimasai ambao kiasili ni wafugaji ambapo wameweza kujishughulisha na kilimo cha mahindi chenye tija.


Programu imewezesha kuwepo kwa eneo la mashamba darasa (FFS) kwa mazao ya Alizeti, Mahindi na Maharage, na shamba Darasa hilo limeonesha mafanikio kwa kiasi kikubwa, ambapo hekta moja inaweza kuzalisha takribani magunia 20 ya kilo mia moja kila moja, na jamii ya wafugaji sasa inajishulisha na shughuli za Kilimo na kunufaika na upatikanaji wa mazao yanayolimwa.


Kwa upande wa Sekta ya Uvuvi, Programu inaendelea na ujenzi wa soko la kimataifa la Samaki Kipumbwi lililloko katika halmashauri ya Pangani ambapo mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 68% na linategemewa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.

Aidha, programu pia inaendelea na ujenzi wa vichanja 40 vya kukaushia dagaa ambavyo vinaweza kukausha takribani tani tano kwa za dagaa kwa wakati mmoja.


Kwa upande mwingine pia Programu ya AFDP inaendelea na ujenzi wa Ghala la baridi na mtambo wa barafu katika soko hilo kwa ajili ya kuhifadhi na kusafirisha samaki.




Awali Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la kimataifa la maendeleo ya Kilimo nchini (IFAD) Bw. Seth Meng alikutana na Kaimu Katibu tawala wa Mkoa wa Tanga Bw.Emmanuel Kisongo na kufanya mazungumzo kuhusiana na utekelezaji wa Programu katika Mkoa sambamba na mafanikio tarajiwa kwa wanachi wa maeneo husika ambapo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa alieleza kuwa Programu hiyo ni muhimu sana katika kuhamasisha maendeleo ya kilimo na uvuvi katika mkoa huo.

Aliishukuru IFAD kwa kuweza kuwafikia wananchi wa mkoa huo na kuwataka ikiwezekana kuongeza uwekezaji mkoani hapo.
Na MWANDISHI WETU


BALOZI wa Msumbiji nchini Tanzania, Ricardo Mtumbuida, amesema mataifa hayo yataendelea kuenzi, udugu, umoja na ushirikiano ulioasisiwa katika harakati za ukombozi wa mataifa hayo.

Amesema nchi za Tanzania na Msumbiji zinahistoria ya kipekee katika harakati hizo kwani Chama cha Ukombozi cha Msumbiji (FRELIMO) kiliasisiwa chini Tanzania .

Balozi Mtumbuida amryasema hayo leo Septemba 7,2026 Dar es Salaam, katika maadhimisho ya miaka 52 ya makubaliano ya Msumbiji na Ureno ya kumaliza vita yaliyosainia Lusaka, nchini Zambia mwaka 1974.

Ameeleza, vita ya ukombozi wa Msumbiji ilianza mwaka 1664 ambapo Septemba 7 mwaka 1974 Wareno wakatambua haki ya kufanya mapatano.

"Ndiyo maana sisi tunaita septemba 7 kila mwaka ni siku ya ushindi na ni kweli kwamba tulishinda vita hii kwani tulimshinda Mreno,"amesema Balozi Mtumbuida.

Amebainisha maadhimisho hayo ya miaka 52 ni muhimu hasa kwa jumuiya ya wananchi wa Msumbiji waishio hapa nchini .

"Tunapaswa kuwaambia historia watoto wetu, wajukuu na watu wote waliopo wakati huu kwani vita ya kukomboa Msumbiji ilianzia hapa Tanzania,"amesema.

Ameeleza Chama cha FRELIMO ambacho kimeongoza vita ya ukombozi wa Msumbiji, liliasisiwa hapa Tanzania.

"Kwa hiyo sisi jumuiya ya Wanamsumbiji tuishio Tanzania tunanafasi ya kipekee kukaa katika kitovu cha uhuru wetu,"ameeleza balozo huyo.

Amewataka wananchi wa Msumbiji waishio hapa nchini kuendelea kuenzi historia hiyo muhimu na kuwashirikisha watoto kujua historia hiyo muhimu.

"Nawapongeza wazazi walioleta watoto hapa na mimi nimekuwa nikieleza historia hii mara kwa mara, kuhusu umuhimu wa siku hii.,"amesema.

Mtumbuida alishukuru ushiriki wa Watanzania katika maadhimisho hayo hususan Kampuni ya Uhuru Publications Limited (UPL) wachapishaji wa magazeti ya Uhuru, Mzalendo, Burudani na Uhuru ya Kijani .

"Tunashukuru kuona chombo hiki cha habari kinachomilikiwa na Chama Cha Mapindizi (CCM) kiko hapa. Hii yote nio kuendeleza mshikamano na ushirikiano wetu. Pia wapo wananchi wa Tanzania hapa,"ameeleza Mtumbuida.

Katika maadhimisho hayo, Balozi Mtumbuida, aliwaongoza wananchi wa Msumbiji waishio hapa nchini kuweka mashada ya maua katika kaburi ya mashujaa wa mapambano ya kupigania uhuru wa taifa hilo.

Makaburi hayo ni kaburi la maziko ya kwanza ya Rais wa wa FRELIMO, Dk. Eduardo Chivambo Mondlane, kaburi la aliyekuwa mke wa kwanza wa Rais wa Msumbiji, Samora Machel, Jozina Machel na shujaa mpigania uhuru wa taifa Francisco Manyanga.

Kwa upande wa Mondlane alizikwa kwa mara ya kwanza mnamo Februari 6, 1969, katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, baada ya kuuawa kwa bomu la kwenye bahasha Februari 3, 1969 ambapo baadaye mabaki ya mwili wake yalifukuliwa na kwenda kuzikwa nchini Msumbiji.

Mpigania uhuru wa Msumbiji Paul Matete Lekanone, alisema siku hiyo ya Septemba 7 kila mwaka ni kumbukumbu muhimu ya Ushindi Msumbiji baada ya mkutano wa makubaliano uliofanyika jijini Lusaka, nchini Zambia katika ya serikali ya Ureno na Msumbiji na kusaini makubalano hayo ya Uhuru wa Msumjini ulipatikana Juni 25, 1975.











Top News