Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Paul Christian 

Makonda kwa kushirikiana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo wa 
Zanzibar Mhe. Dkt. Riziki Pembe Juma wameteua Wajumbe wa Kamati ya Ndani 
(LOC) ya uratibu wa maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu Barani Afrika
(AFCON 2027).


 




Na; Mwandishi Wetu, Dodoma
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi ni nyenzo muhimu ya kujadili utekelezaji wa majukumu, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.

Amesema ili kuendelea kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu, ni muhimu kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja, bidii na weledi. Tunapaswa kujipambanua kwa utendaji wa hali ya juu unaoendana na hadhi ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika nchi.

Mhe. Masauni ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026 akieleza kuwa Ofisi imeendelea kufanya vizuri katika kudumisha Muungano, hususan kupitia utoaji wa elimu kwa umma kwa makundi mbalimbali.

“Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, Ofisi imefanikiwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, hususan kwa kuimarisha vifungu vinavyohusu mabadiliko ya tabianchi na kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Aidha, ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa kitaalam na kitaasisi, upatikanaji wa rasilimali na kuongeza jitihada za uhamasishaji wa rasilimali fedha, ikiwemo kupitia maandalizi bora ya miradi ya uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi alisema lake kuu tangu kuanzishwa kwake baraza hilo lilikuwa kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini mipangokazi, pamoja na kuboresha uhusiano kati ya Menejimenti na watumishi.

“Madhumuni ya Mkutano huu ni kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa lengo la kupata Taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Ofisi.”
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiagana na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, Dkt. Ndiame Diop, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo katika Ofisi za Benki ya Dunia, jijini Washington D.C Nchini Marekani, katika Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayofanyika, Jijini humo, ambapo Balozi Omar alishukuru uamuzi wa Benki ya Dunia, Kupitia Bodi yake ya Wakurugenzi, kuidhinishia Tanzania dola za Marekani milioni 550 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya kimkakati katika sekta za elimu na kusaidia kaya masikini.


Na Benny Mwaipaja, Washington D.C
BENKI ya Dunia, Kupitia Bodi yake ya Wakurugenzi, imeiidhinishia Tanzania dola za Marekani milioni 550 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 1.4 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya kimkakati katika sekta za elimu na kusaidia kaya masikini.

Uamuzi huo wa Benki umetangazwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, Dkt. Ndiame Diop, alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, Makao Makuu wa Taasisi hizo Jijini Washington D.C, nchini Marekani.

Kati ya fedha hizo, dola za Marekani milioni 300 zitatumika kusaidia program ya elimu ya kuongeza ujuzi hususana kwa vijana na kiasi kingine cha dola za Marekani milioni 250 kitatumika kwa ajili ya kusaidia program ya kusaidia kaya masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF

Dkt. Diop alisema kuwa uamuzi huo unafuatia uhusiano imara uliopo kati ya Tanzania na Benki hiyo pamoja na utekelezaji mzuri wa miradi inayofadhiliwa na Benki, pamoja na usimamizi mzuri wa sera zake za uchumi na fedha.

Makamu huyo wa Rais wa Benki ya Dunia aliahidi kuwa Benki inaendelea kuchakata miradi mingine ya kimkakati iliyowasiliashwa na Tanzania kwa ajili ya kupata ufadhili wa Benki ikiwemo sekta ya nishati, kilimobiashara, miradi ya afya Zanzibar na mingine ili kuiwezesha Tanzania kufikia malengo iliyojiwekea katika kukuza uchumi na maisha ya wananchi.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, aliishukuru Benki ya Dunia kwa kupitisha miradi hiyo miwili ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya nchi pamoja na majadiliamo yenye tija kwenye maeneo ya miradi muhimu ya maendeleo kwacnchi.

“Pia tumejadili kuhusu maendeleo ya ushoroba wa usafirishaji ambao ni suala muhimu pia ambapo tumeangazia namna korido ya usafirishaji ambayo nchi imewekeza kiasi kikubwa cha fedha ikiwemo reli ya SGR inavyoweza kuchochea uchumi kujumishi na endelevu” alisema Mhe. Balozi Omar.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkaazi wa Benki ya Dunia anayemaliza muda wake Bw. Nathan Belete, alisema kuwa kikao cha Mhe. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia, Dkt. Mdiame Diop kilikuwa cha manufaa makubwa na kinaendelea kuonesha namna Benki inavyothamini mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii yanayoendelea nchini Tanzania.

“Ninaondoka Tanzania nikiwa na furaha kubwa na nimaamini uhusiano wa Benki na Tanzania utaendelea kuwa imara na nchi itaendelea kuwa moja ya nchi kubwa kiuchumi katika bara la Afrika kutokana na rasilimali nyingi ilizonazo” alisema Bw. Belete.

Uwekezaji wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Kupitia Dirisha la IDA umefikia dola za Marekani bilioni 8.96 ukihusisha miradi 35 ambapo miradi 32 yenye thamaniya dola za Marekani ni ya kitaifa na miradi mitatu yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 0.18 ni ya kikanda.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Fedha na Mipango kutoka Ofisi ya Rais-Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi, na Viongozi wengine waaandamizi wa Taasisi za Serikali.



Farida Mangube Morogoro
KATIKA hatua mpya ya kuimarisha sekta ya utalii nchini, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Mhe. Hamida Mussa Hamis, amebainisha mkakati wa kipekee wa kuendelea kuwavutia watalii wanaotembelea Zanzibar kuongeza safari zao kwa kutembelea vivutio vya Tanzania Bara, hususan Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kutokana na upekee wake

Akizungumza baada ya kutembelea hifadhi hiyo iliyopo mkoani Morogoro, Mhe. Hamida alisema ipo haja ya kutumia fursa ya wingi wa watalii wanaoendelea kumimina Zanzibar kama daraja la kuutangaza utalii wa Bara ikiwemo hifadhi za taifa kama Mikumi.

“Zanzibar ni lango kubwa la utalii, lakini tunataka wageni hawa wasiishie visiwani pekee bali wavuke na kuja kuona hazina ya vivutio tulivyonavyo Bara,” alisema.

Katika kile alichokiita uzoefu wa kipekee, Mhe. Hamida alieleza kufurahishwa na tukio la kuona simba ndani ya muda mfupi mara tu baada ya kuingia hifadhini hapo, Tena wakiwa chini ya Ndege zilizoegeshwa ndani ya hifadhi zinazotumika kuleta wageni Mikumi kutokea Zanzibar akisema hali hiyo inaonesha ubora wa vivutio vya Tanzania.

Aliongeza kuwa miundombinu iliyopo ikiwemo reli ya kisasa ya SGR, usafiri wa anga na barabara pamoja na miundo mbinu mizuri ya ndani inayofikika kirahisi licha ya Mvua, imeifanya Mikumi kuwa miongoni mwa hifadhi bora zinazofikika kirahisi kwa watalii wa ndani na nje.

Katika hatua nyingine, aliwahimiza Wazanzibari kubadili mtazamo na kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya ndani, akisisitiza kuwa utalii si wa wageni pekee bali ni fursa kwa Watanzania wote.

“Ni wakati sasa kwa Watanzania kuwekeza katika kujitambua na kuthamini vivutio vyetu; utalii wa ndani ni msingi imara wa sekta hii,” alisisitiza.

Aidha akawahimiza watanzania kutokea Upande wa Bara kutembelea vivutio vya Utalii wa Zanzibar ikiwemo utalii wa fukwe, kuogelea na dolphins na matamasha mbalimbali likiwemo la Kizimkazi ili kufurahia upekee uliopo.

"Hata Rais wetu Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Zanzibar Dkt Husein Ali Mwinyi, wanahimiza utalii wa Ndani, Rais Samia alifanya Kazi kubwa kutangaza Royal Tour, tuwaunge mkono kivitendo viongozi wetu"Alisisitiza.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Augustine Masesa, alifichua kuwa idadi kubwa ya watalii wanaotembelea hifadhi hiyo wanatoka Zanzibar.

Alisema hali hiyo inaashiria mafanikio ya juhudi za kuitangaza Tanzania kupitia kampeni mbalimbali ikiwemo Royal Tour, huku akibainisha kuwa bado kuna fursa kubwa zaidi ya kuongeza idadi hiyo kupitia ushirikiano wa pande zote mbili.

Alisisitiza kuwa Mikumi inaendelea kuwa kivutio muhimu kinachochochea utalii wa ndani na wa kimataifa, huku akiwakaribisha Watanzania na wageni kufika kujionea vivutio hivyo kwa macho yao wenyewe hasa kutokana na miundo mbinu Rafiki na inayofikika kirahisi ikiwemo Reli ya SGR, Barabara na ndege ambazo kutoka Zanzibar ni dakika 40 tu kufika.

 

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Aprili 14, 2026 amekutana na kuzungumza na mjumbe maalum Jumuiya ya Madola (Commonwealth) Rais wa zamani wa Malawi Mhe.Lazarus McCarthy Chakwera ambaye alitembelea ofisi za Tume Njedengwa jijini Dodoma. Ziara hiyo maalum ya mjumbe huyo wa Jumuia ya Madola ililenga kuangalia namna Uchaguzi Mkuu wa 2025 ulivyofanyika. (Picha na INEC).








Dar es Salaam, Tanzania – Aprili 15, 2026
Punchline Africa imetangaza rasmi uzinduzi wa Tamasha la Kimataifa la Vichekesho la Punchline (PICF) 2026, litakalofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 25 hadi Juni 1, 2026.

Tamasha hilo la wiki moja linatarajiwa kuwakutanisha wachekeshaji kutoka nchi mbalimbali za Afrika, likijumuisha maonesho ya moja kwa moja, shughuli za vyombo vya habari pamoja na ubadilishanaji wa utamaduni. Tamasha litahitimishwa kwa onesho kubwa la fainali litakalofanyika katika ukumbi wa Superdome.

PICF 2026 itajumuisha maonesho ya vichekesho kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili, ikiwa ni juhudi za kuonesha utofauti na utajiri wa vipaji vya ucheshi barani Afrika.

Mbali na burudani, waandaaji wamesema tamasha hilo pia linalenga kuhamasisha ustawi wa afya ya akili kwa kuonesha umuhimu wa kicheko kama nyenzo ya kupunguza msongo wa mawazo na kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mwanzilishi Mwenza wa Punchline Africa, Evans Bukuku, alisema ucheshi una mchango mkubwa zaidi ya burudani.

“Comedy siyo kuchekesha tu, bali ni njia ya kuwasaidia watu kuelewa maisha, kupunguza msongo wa mawazo na kuunganishwa kijamii. Kupitia PICF tunataka kuunda jukwaa la watu kukutana, kucheka na kuondoka wakiwa na nafuu zaidi,” alisema.

Kwa upande wake, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Anne Sophie Ave, alisema wameamua kuunga mkono tamasha hilo kutokana na imani yao katika nguvu ya sanaa ya ubunifu, hasa kwa vijana.

“Vijana wengi wana vipaji vikubwa lakini hukosa kujiamini kujitokeza. Tunaamini tamasha hili litawasaidia kupata ujasiri na kufikia fursa za kimataifa,” alisema.

Aliongeza kuwa Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji kutokana na nafasi yake kama kitovu cha Afrika Mashariki pamoja na historia yake katika harakati za Pan-Afrika.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Filamu kutoka Tanzania Film Board, Emmanuel Ndumukwa, alilipongeza tamasha hilo akieleza kuwa ni hatua muhimu kwa ukuaji wa tasnia ya ucheshi nchini.

Alisema serikali ipo tayari kuunga mkono jitihada kama hizo kupitia mifuko ya utamaduni huku akisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa vigezo vya wazi kwa washiriki

Akizungumza kwa niaba ya wachekeshaji wa Tanzania, Humphrey Richard maarufu kama MC Kisoli, alisema tamasha hilo lina uwezo wa kubadilisha maisha ya wasanii wengi.

“Hili ni zaidi ya burudani; ni jukwaa la kujifunza, kubadilishana uzoefu na kukuza sanaa ya ucheshi. Ni tamasha la kila mtu,” alisema.

Tamasha hilo pia ni sehemu ya mradi wa Création Africa unaofadhiliwa na Ubalozi wa Ufaransa na kuratibiwa na Alliance Française Dar es Salaam, unaolenga kuwawezesha wasanii na taasisi za ubunifu nchini.

Uzinduzi rasmi ulifanyika kupitia mkutano na waandishi wa habari katika Punchline Comedy Club, Masaki, ukihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo SGA Security ambao watatoa huduma za ulinzi katika matukio yote ya tamasha.

Waandaaji wanatarajia tamasha hilo kuvutia hadhira kubwa, hususan vijana na wabunifu, pamoja na kuwafikia zaidi ya watu milioni moja kupitia majukwaa ya kidijitali.

Ratiba kamili ya matukio, majina ya wasanii pamoja na taarifa za tiketi zinatarajiwa kutolewa hivi karibuni.

Farida Mangube Morogoro

Katika hatua mpya ya kuimarisha sekta ya utalii nchini, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Mhe. Hamida Mussa Hamis, amebainisha mkakati wa kipekee wa kuendelea kuwavutia watalii wanaotembelea Zanzibar kuongeza safari zao kwa kutembelea vivutio vya Tanzania Bara, hususan Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kutokana na upekee wake 
Akizungumza baada ya kutembelea hifadhi hiyo iliyopo mkoani Morogoro, Mhe. Hamida alisema ipo haja ya kutumia fursa ya wingi wa watalii wanaoendelea kumimina Zanzibar kama daraja la kuutangaza utalii wa Bara ikiwemo hifadhi za taifa kama Mikumi.

“Zanzibar ni lango kubwa la utalii, lakini tunataka wageni hawa wasiishie visiwani pekee bali wavuke na kuja kuona hazina ya vivutio tulivyonavyo Bara,” alisema.

Katika kile alichokiita uzoefu wa kipekee, Mhe. Hamida alieleza kufurahishwa na tukio la kuona simba ndani ya muda mfupi mara tu baada ya kuingia hifadhini hapo, Tena wakiwa chini ya Ndege zilizoegeshwa ndani ya hifadhi zinazotumika kuleta wageni Mikumi kutokea Zanzibar akisema hali hiyo inaonesha ubora wa vivutio vya Tanzania.

Aliongeza kuwa miundombinu iliyopo ikiwemo reli ya kisasa ya SGR, usafiri wa anga na barabara pamoja na miundo mbinu mizuri ya ndani inayofikika kirahisi licha ya Mvua, imeifanya Mikumi kuwa miongoni mwa hifadhi bora zinazofikika kirahisi kwa watalii wa ndani na nje.

Katika hatua nyingine, aliwahimiza Wazanzibari kubadili mtazamo na kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya ndani, akisisitiza kuwa utalii si wa wageni pekee bali ni fursa kwa Watanzania wote.

“Ni wakati sasa kwa Watanzania kuwekeza katika kujitambua na kuthamini vivutio vyetu; utalii wa ndani ni msingi imara wa sekta hii,” alisisitiza.

Aidha akawahimiza watanzania kutokea Upande wa Bara kutembelea vivutio vya Utalii wa Zanzibar ikiwemo utalii wa fukwe, kuogelea na dolphins na matamasha mbalimbali likiwemo la Kizimkazi ili kufurahia upekee uliopo.

"Hata Rais wetu Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Zanzibar Dkt Husein Ali Mwinyi, wanahimiza utalii wa Ndani, Rais Samia alifanya Kazi kubwa kutangaza Royal Tour, tuwaunge mkono kivitendo viongozi wetu"Alisisitiza.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mikumi, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Augustine Masesa, alifichua kuwa idadi kubwa ya watalii wanaotembelea hifadhi hiyo wanatoka Zanzibar.

Alisema hali hiyo inaashiria mafanikio ya juhudi za kuitangaza Tanzania kupitia kampeni mbalimbali ikiwemo Royal Tour, huku akibainisha kuwa bado kuna fursa kubwa zaidi ya kuongeza idadi hiyo kupitia ushirikiano wa pande zote mbili.

Alisisitiza kuwa Mikumi inaendelea kuwa kivutio muhimu kinachochochea utalii wa ndani na wa kimataifa, huku akiwakaribisha Watanzania na wageni kufika kujionea vivutio hivyo kwa macho yao wenyewe hasa kutokana na miundo mbinu Rafiki na inayofikika kirahisi ikiwemo Reli ya SGR, Barabara na ndege ambazo kutoka Zanzibar ni dakika 40 tu kufika.



 

SHIRIKA La Mawasiliano Tanzania (TTCL,) limeendelea kutekeleza mpango mkakati kwa kuhakikisha watanzania wanapata huduma za kidigitali ili kuweza kuendana na kasi ya maendeleo ya teknolojia.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akizindua kituo cha Kijitonyama FTTx Experience Centre Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL,) David Nchimbi amesema kituo hicho cha ubunifu wa matumizi ya teknolojia ni cha kipekee na kinachotoa uzoefu wa pamoja na elimu kuhusu matumizi ya teknolojia za kidigitali ambapo kupitia kituo hicho wananchi watapa fursa ya kuona kwa vitendo namna ambavyo intaneti ya TTCL inavyoweza kubadilisha nyumba, ofisi au biashara kwa za kidigitali na zenye ufanisi.

Amesema kituo hicho kitakuwa jukwaa la kujifunza na kubadilisha uzoefu kuhusu matumizi teknolojia za kisasa nyumbani, mifumo ya ofisi za kidigitali, na suluhisho katika biashara za mtandaoni pamoja na kuchochea na kujenga uelewa kwa jamii juu ya umuhimu wa TEHAMA katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Nchimbi amesema,ubunifu unaoendelea kufanywa na Shirika hilo ni katika kuhakikisha wateja wanapata huduma bora kwa wakati na uhakika na zenye kurahisisha shughuli mbalimbali ikiwemo mtandao, biashara mtandao, huduma za kifedha na mawasilino yenye tija.

Amesema, Serikali itaendelea kuhakikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano nchini zinapewa kipaumbele na hiyo ni pamoja na kuongeza ubunifu na wigo wa utoaji huduma wa Shirika hilo kwa wananchi, kuongeza ufanisi, mapato na kujiendesha kibiashara ili kuendelea kuwahudumia wananchi kwa ubora zaidi,

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Moremi Marwa amesema kuwa, Shirika linatekeleza Mpango Mkakati wa miaka 10 ulioanza katika mwaka wa fedha wa 2025/ 2026 kwa lengo la kuleta mageuzi katika uwajibikaji, kuongeza uzalishaji wenye tija na kufanya uendelevu katika miradi waliyoianzisha.

“Pamoja na mageuzi mengineyo mradi huu wa ´Faiba ´Fiber to The X´( FTTx) ambao umelenga kusambaza huduma ya intaneti yenye kasi , uhakika na ubora katika makazi, ofisi na maeneo ya biashara na kupitia huduma ya ´Faiba Mlangoni Kwako´shirika linaendelea kutoa huduma katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Dar es Salaam, Unguja, Arusha, Dodoma, Mwanza, Geita, Iringa na Mbeya na kwa mwaka 2026/27 Shirika limejipanga kufikisha huduma hii ya Faiba katika mikoa iliyobaki.” Amesema.

Akieleza kuhusu FTTX Experience Centre, Marwa amesema kituo hicho ni mwendelezo wa ubunifu katika utoaji huduma za intaneti nchini ambapo kwa sasa wateja wanapata huduma za inataneti zilizounganishwa, ambapo mteja anaweza kupata huduma tatu katika kifurushi kimoja yaani intaneti bila kikomo akiwa nyumbani, dakika anazoweza kuzitumia katika simu ya mkononi au mezani pamoja na GB za intaneti katika simu ya mkononi.

Amefafanua kuwa kupitia kituo hicho wateja watapata fursa ya kuona matumizi ya kidigitali kwenye smart home, uwekaji wa huduma ya intaneti ya Faiba majumbani, ofisini na maeneo ya biashara pamoja na teknolojia inayotumika katika utoaji wa huduma hizo.

Kuhusiana na faida kwa Shirika hilo Marwa amesema kwa mwaka wa fedha 2024/25 lilipata faida ya Shilingi Bilioni 22.9 kabla ya kodi na ni faida ambayo imethibitishwa na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG,) na wamejipanga zaidi katika kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja pamoja na kuliendesha Shirika hilo kibiashara na kuwashukuru wadau wao kutoka kampuni za Hisence na Huawei kwa ushirikiano wao katika ujenzi wa kituo hicho.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL,) Moremi Marwa akizungumza wakati wa uzinduzi huo na kueleza kuwa kupitia kituo hicho wananchi watapata fursa ya kuona kwa vitendo namna TTCL inavyotumia teknolojia katika utoaji wa huduma. Leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL,) David Nchimbi akizungumza mara baada ya kuzindua kituo hicho na kueleza kuwa upekee na ubunifu wa kituo hicho ni jukwaa la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu matumizi ya teknolojia. Leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Biashara wa TTCL Vedastus Mwita akieleza namna TTCL inavyotumia teknolojia katika utoaji huduma. Leo jijini Dar es Salaam.




Na; Mwandishi Wetu

Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi ni nyenzo muhimu ya kujadili utekelezaji wa majukumu, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.

Amesema ili kuendelea kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu, ni muhimu kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja, bidii na weledi. Tunapaswa kujipambanua kwa utendaji wa hali ya juu unaoendana na hadhi ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika nchi.

Mhe. Masauni ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026 akieleza kuwa Ofisi imeendelea kufanya vizuri katika kudumisha Muungano, hususan kupitia utoaji wa elimu kwa umma kwa makundi mbalimbali.

“Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, Ofisi imefanikiwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, hususan kwa kuimarisha vifungu vinavyohusu mabadiliko ya tabianchi na kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Aidha, ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa kitaalam na kitaasisi, upatikanaji wa rasilimali na kuongeza jitihada za uhamasishaji wa rasilimali fedha, ikiwemo kupitia maandalizi bora ya miradi ya uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi alisema lake kuu tangu kuanzishwa kwake baraza hilo lilikuwa kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini mipangokazi, pamoja na kuboresha uhusiano kati ya Menejimenti na watumishi.

“Madhumuni ya Mkutano huu ni kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa lengo la kupata Taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Ofisi.”
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauniakizungumza wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu waRais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyikaDodoma, Aprili 15, 2026. Wa pili kutoka kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu waRais, Mhe. Reuben Kwagilwa, wa Kwanza kulia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi na wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Bw. Abdallah Mitawi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati) akiwa na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo Ofisi ya Makamu wa Rais mara baada ya kufungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Raisuliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

NA Mwandishi Wetu

HALMASHAURI ya Jiji la Dar es salaam linaendelea kutekeleza agizo la Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Sukuhu Hassan la kuhakikisha wanafunzi wote wa darasa la 6 na 7 wanaotarajia kumaliza elimu ya msingi kwa mkupuo (Double Cohort) 2027 wanapata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2028.

Katika kuhakikisha agizo hilo linafanikiwa, Halmashuri hiyo imeendelea na ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa kujenga shule kwa mtindo wa ghorofa ambapo nyingine zimekamilika na nyingine zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Kwa mfano kwa mwaka wa fedha 2025/26,Halmashuri ya Jiji la Dar es salaam imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 19 katika sekta ya elimu Sekondari kuhakikisha adhima hiyo inafanikiwa.

Jumla ya shule za ghorofa 9 mpaka sasa zimejengwa zikiwemo mpya na zile zilizoboreshwa ili kuweza kukidhi mahitaji ya sasa.

Shule hizo ni pamoja na shule mpya ya  Kitunda Relini iliyojengwa kwa gharama za Shilingi bilioni 4.2,Kipunguni B (bilioni 2.1),Bonyokwa(bilioni 2),Ukonga (bilioni 2.2),Minazi Mirefu (bilioni 2.3),Mnazi Mmoja (kumalizia ujenzi bilioni 1.8), Liwiti(bilioni 2.1) pamoja na kumalizia ujenzi Sekondari Kimanga(milioni 998).

Mbali na ujenzi huo, baadhi ya shule hizo zimefungiwa mfumo wa "lift" kuwawezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam inatarajia kuwa ifikapo muhula wa 2027/28 iwe imekamilisha mahitaji ya wanafunzi wote wanaotarajia kuanza kidato cha kwanza kwa muhula huo.


 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA

WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umeanzisha utaratibu mpya wa kupima utendaji wa madiwani kwa kuzingatia uwezo wao wa kuchochea ukuaji wa biashara katika kata zao hatua hiyo inalenga kuimarisha uwajibikaji na kuinua uchumi wa wananchi katika ngazi ya chini.

Hayo yamesemwa leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma ambapo amesema mfumo huo utazingatia idadi ya biashara mpya zinazoanzishwa pamoja na uwepo wa mazingira rafiki yanayowezesha wafanyabiashara kukua.

Amesema kupitia utaratibu huo, madiwani watahamasika zaidi kusimamia maendeleo ya biashara katika maeneo yao na kuhakikisha maafisa biashara wa halmashauri wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Aidha, Nyaisa amesisitiza kuwa ni wajibu wa madiwani kusimamia utekelezaji wa sheria za biashara, huku akionya dhidi ya uwepo wa shughuli haramu kama uzalishaji wa pombe bandia katika maeneo yao.

"BRELA inalenga kukuza biashara ndogondogo ili ziweze kurasimishwa, hatua itakayowawezesha wafanyabiashara kupata mikopo, kupanua shughuli zao na kufikia masoko mapana zaidi ndani na nje ya nchi."amesema Bw.Nyaisa

Nyaisa ameongeza kuwa vijana ndio kundi kubwa la wafanyabiashara nchini, hivyo kuna umuhimu wa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutumia ujuzi na elimu yao kujiajiri kupitia biashara endelevu.

Kwa mujibu wa takwimu za BRELA, kumekuwa na ongezeko kubwa la biashara katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, hali inayoashiria kuimarika kwa uchumi wa nchi.

Hata hivyo, amewahimiza wafanyabiashara kurasimisha shughuli zao ili kuongeza uwezekano wa kupata mikopo na kuepuka changamoto zinazotokana na mitaji isiyo rasmi.

Vilevile, amewashauri wamiliki wa biashara za kifamilia kuhakikisha wanawaorodhesha wanahisa wote wakati wa usajili ili kuepusha migogoro ya baadaye.

Katika hatua nyingine, Nyaisa amesema taasisi hiyo imeanza kufuatilia na kusajili bunifu zinazotokana na taasisi za elimu kuanzia ngazi ya chini hadi vyuo vikuu, hususan zile zinazolenga kuboresha shughuli za kibiashara.

Kwa upande wake, Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira, amesema mafunzo yaliyotolewa kwa madiwani yamewajengea uwezo wa kuelewa vyema taratibu za usajili wa biashara pamoja na aina mbalimbali za leseni.

"Madiwani sasa wana nafasi nzuri ya kuwaongoza wananchi kwa usahihi wanapohitaji kusajili biashara zao, hatua itakayosaidia kupunguza changamoto zilizokuwapo awali."amesema

Aidha, amefafanua kuwa leseni za biashara kundi “B” hutumika kwa biashara zinazofanyika ndani ya halmashauri moja, wakati leseni za biashara kundi “A” humruhusu mfanyabiashara kuendesha shughuli zake hadi ngazi ya kimataifa bila kutozwa tozo ya ziada za leseni za biashara kundi B.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma


Top News