

Amemwelekeza Mkurugenzi wa Muhimbili kuimarisha usimamizi wa huduma za afya kupitia viongozi walioko chini yake wakiwemo wakurugenzi, mameneja na wasimamizi wote na endapo kutakuwa na watumishi wowote wasiowajibika achukue hatua zilizo chini ya mamlaka yake na mengine yanayohitaji Wizara kufanyia kazi, ayawasilishe ili hatua stahiki zichukuliwe.
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.
Bw. Kessy ameongeza kuwa Mamlaka ya Rufani inawaelekeza wazabuni wote wa ndani na nje ya nchi kutumia Moduli ya kuwasilisha Malalamiko na Rufaa kwa kuzingatia Sheria ya Ununuzi wa Umma pamoja na kanuni zake pindi wanapoona hawakutendewa haki katika zabuni walizoomba.
Na.Mwandishi Wetu-Babati, ManyaraMamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kaskazini imeendesha semina ya kuwajengea uwezo Maafisa wa Huduma kwa Wateja, Mahusiano na Sheria kutoka TANESCO na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira za Kanda ya Kaskazini kuhusu huduma kwa wateja na uzingatiaji wa matakwa ya kisheria.
Akifungua semina hiyo katika Hoteli ya White Rose, Babati, Meneja wa EWURA Kanda ya Kaskazini, Bw. George Mhina, aliwasisitiza washiriki kuyafahamu vyema majukumu yao ili waweze kutoa majibu sahihi, ya wakati na yanayozingatia sheria, hivyo kuboresha huduma kwa wateja.
Kwa niaba ya washiriki, Bi. Devotha Mayala kutoka Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tanga na Bw. Samwel Mandari kutoka TANESCO waliishukuru EWURA kwa mafunzo hayo, wakieleza kuwa yamewaongezea uelewa na uwezo wa kuwahudumia wateja kwa weledi zaidi.
Semina hiyo ni sehemu ya juhudi za EWURA za kuimarisha uwezo wa watoa huduma na kulinda haki za watumiaji wa huduma za nishati na maji kupitia Udhibiti wa Haki kwa Matokeo Chanya.
Akizungumza Julai 30, 2026, wakati wa kufunga mafunzo maalum ya siku tatu kwa viongozi wa AMCOS, wajumbe wa bodi na viongozi wa DORECU jijini Dodoma, Chitinka alisema Mkoa wa Dodoma umejipanga kuhamasisha uzalishaji wa ufuta mweupe wenye thamani kubwa sokoni badala ya kuendelea kutegemea aina za ufuta wa rangi zinazolimwa kwa wingi hivi sasa.
Aidha, aliwataka viongozi wa vyama vya ushirika kuhakikisha matumizi yote ya fedha yanaidhinishwa na maafisa ushirika pamoja na Ofisi ya Mrajisi, huku mikataba yote ya watoa huduma ikifuata taratibu za kisheria ili kuzuia vitendo vya udanganyifu na ubadhirifu wa fedha za wanachama.
Chitinka amesisitiza umuhimu wa kufuata sheria za manunuzi, kuandaa mipango ya kimkakati na kuhakikisha AMCOS zinafanya kazi mwaka mzima badala ya kuwa vyama vya msimu, amewahimiza viongozi kushirikiana na jamii kuongeza wanachama, kuimarisha uzalishaji wa mazao na kutumia kikamilifu mfumo wa stakabadhi za ghala.
Kuhusu uchaguzi wa viongozi wa ushirika, alisema ni wakati wa kutoa nafasi kwa viongozi wapya wenye sifa na kuacha mfumo wa viongozi kukaa madarakani kwa muda mrefu, ameeleza kuwa mchakato wa uchaguzi utaanza mwezi Agosti baada ya maadhimisho ya Nanenane.
Kwa upande wa usimamizi wa fedha, amesema matumizi yote ya fedha za mfumo wa stakabadhi za ghala yatapaswa kupitishwa kwenye bajeti za mwaka ili kuondoa mianya ya matumizi mabaya, amevitaka vyama vilivyoshiriki minada msimu uliopita kuhakikisha vinalipa tozo zote zinazodaiwa kwa wakati.
Naye Mrajisi Msaidizi kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Richard Izengo, amesema mafunzo hayo yamelenga kuimarisha usimamizi, ukaguzi na uwajibikaji wa vyama vya ushirika, amesisitiza umuhimu wa kuandaa hesabu na kuziwasilisha kwa mkaguzi wa nje ili kuongeza uwazi kwa wanachama.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa DORECU, David Mtimbi Mwaka, amesema mfumo wa stakabadhi za ghala Una matarajio ya mafanikio makubwa zaidi katika misimu ijayo, kufuatia kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti madalali wa mazao Mkoani Dodoma.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhitimisha mafunzo ya siku tatu kwa wanaushirika 80 kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Dodoma, Meneja Mkuu wa DORECU, Feruzi Hassan Mwindi, alisema mafunzo hayo yalilenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi za ghala kwa msimu uliopita, kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya ushirika katika usimamizi wa shughuli zao.
Mwindi alisema mafunzo hayo yatawanufaisha wakulima wengi ambao ni wageni katika matumizi ya mfumo wa stakabadhi za ghala, kwa kuwa yatawawezesha kuhifadhi kumbukumbu na takwimu kwa usahihi pamoja na kuendesha vyama vyao kwa ufanisi zaidi katika misimu ijayo.
Makamu Mwenyekiti wa DORECU, David Mtimbi Mwaka, alisema wanachama wa mkoa wa Dodoma wamenufaika na mfumo wa stakabadhi za ghala ambao umechangia kudhibiti madalali (aggregators), akieleza kuwa mafanikio yaliyopatikana yanatoa matumaini ya kufanya vizuri zaidi katika msimu ujao.
Naye Mrajisi Msaidizi anayesimamia vyama vya ushirika visivyo vya kifedha kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Richard Izengo, alisema mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa kila mwaka wa kuimarisha usimamizi na ukaguzi wa vyama vya ushirika.
Pia alisisitiza umuhimu wa kuandaa na kuwasilisha hesabu kwa mkaguzi wa nje ili taarifa za utekelezaji wa shughuli za vyama ziwasilishwe kwenye mikutano mikuu ya mwaka na kuongeza uwajibikaji kwa viongozi na wanachama.
MAHAKAMA ya Rufani Tanzania imetupilia mbali ombi la Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) lililotaka kuruhusiwa kuwasilisha ushahidi wa nyongeza katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, na hivyo kuacha uamuzi wa Mahakama Kuu ukiwa palepale.
Uamuzi huo ulitolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoundwa na Jaji Augustine Mwarija, Jaji Zahara Muruke na Jaji Amour Khamisi, ambao walikubaliana na uamuzi wa awali wa Mahakama Kuu uliotolewa na Jaji Dunstan Ndunguru, akisaidiana na Majaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde.
Akisoma hukumu, Jaji Mwarija alisema hoja kuu ilikuwa kubaini kama Mahakama Kuu ilikosea kwa kujadili na kukataa notisi ya ushahidi wa nyongeza bila kuipa Jamhuri nafasi ya kusikilizwa, lakini Mahakama ya Rufani ilibaini kuwa upande wa mashtaka ulipewa fursa ya kutosha kueleza msimamo wake.
Mahakama ilieleza kuwa notisi ya Jamhuri ililenga kuongeza maelezo ya ushahidi wa ACP Amini Mahamba kuhusu uchunguzi wa matukio ya Oktoba 29, 2025, maelezo ambayo hayakusomwa wakati wa mwenendo wa kupeleka shauri Mahakama Kuu (committal proceedings).
Hata hivyo, Lissu alipinga hatua hiyo akidai kuwa kifungu cha 308 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai hakiruhusu kuwasilishwa kwa ushahidi mpya kutoka kwa shahidi ambaye tayari ushahidi wake ulishawasilishwa wakati wa committal, bali kinahusu mashahidi ambao taarifa zao hazikusomwa kabisa.
Mahakama ya Rufani ilikubaliana na tafsiri hiyo, ikisema kifungu hicho kinatoa nafasi ya kumwita shahidi ambaye taarifa yake haikusomwa wakati wa committal, lakini hakitoi mamlaka ya kumrejesha shahidi aliyekwisha kutoa ushahidi ili kuongeza ushahidi mpya alioupata baadaye.
Kutokana na tafsiri hiyo, Mahakama ilisema notisi ya Jamhuri ilikuwa imewasilishwa kwa msingi usio sahihi wa kisheria na kwamba Mahakama Kuu ilikuwa sahihi kuifuta kwa kuwa haikukidhi matakwa ya kifungu cha 308 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.
Katika uamuzi huo, Mahakama pia ilikataa ombi la Lissu la kulipwa fidia kwa madai ya kukaa mahabusu kwa siku 139 kutokana na kusimamishwa kwa mwenendo wa kesi wakati maombi hayo yalipokuwa yakisikilizwa.
Jaji Mwarija alisema Mahakama ya Rufani haina mamlaka ya kushughulikia ombi hilo kwa kuwa si Mahakama ya kwanza kusikiliza shauri, akifafanua kuwa fidia ya aina hiyo inaweza kutolewa tu endapo mshtakiwa ataachiwa huru na kubainika kuwa shtaka lilikuwa la kipuuzi au la kumsumbua bila sababu.
Kutokana na sababu hizo, Mahakama ya Rufani ilihitimisha kuwa ombi la DPP halikuwa na msingi wa kisheria na hivyo likatupiliwa mbali, hatua inayomaanisha uamuzi wa Mahakama Kuu wa kuzuia kuwasilishwa kwa ushahidi huo wa nyongeza unabaki kuwa halali.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali itaendelea kuimarisha maridhiano ya kisiasa kama msingi wa kuendeleza mchakato wa maboresho ya Katiba, huku akisisitiza kuwa hatua zote zitafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi kwa maslahi mapana ya Taifa.
Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Julai 30, 2026, alipokutana na viongozi wa vyama 18 vya siasa nchini katika Ikulu ya Dar es Salaam, kwenye mkutano uliolenga kujadili masuala ya maridhiano ya kisiasa, mageuzi ya kisiasa, uchumi, huduma za jamii, ajira, uwekezaji na ulinzi wa amani nchini.
Akizungumza katika mkutano huo, Rais Samia alisema Serikali imejipanga kuendelea kushirikiana na vyama vya siasa ili kuhakikisha mchakato wa maridhiano unazaa matokeo yenye manufaa kwa Taifa, ikiwa ni pamoja na kufungua njia kuelekea hatua zinazofuata za maboresho ya Katiba.
Aidha, amewafahamisha viongozi hao kuhusu hatua zilizofikiwa katika maandalizi ya mchakato wa maridhiano visiwani Zanzibar, akieleza kuwa Serikali itaendelea kusimamia mchakato huo kwa uwazi na kwa kuzingatia misingi ya kisheria.
Rais Samia pia alitangaza kuwa Serikali itaendelea kufanya mikutano ya mazungumzo na viongozi wa vyama vya siasa angalau mara tatu kwa mwaka, akisema hatua hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano, kujenga uelewano na kutatua changamoto mbalimbali kupitia majadiliano.
Mbali na masuala ya kisiasa, Rais Samia alielezea hali ya uchumi wa nchi, akisema Tanzania imeendelea kushuhudia ukuaji wa uchumi wa asilimia sita katika mwaka uliopita, huku ukuaji wa asilimia 6.3 ukitarajiwa kufikiwa mwaka huu.
Amesema Serikali inaendelea kuweka mkazo katika kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo iliyoanza kutekelezwa pamoja na kuwekeza zaidi katika miundombinu ya kimkakati, ikiwemo reli, barabara, bandari na sekta nyingine muhimu kwa maendeleo ya uchumi.
Kuhusu uwekezaji, Rais Samia alisema maboresho yaliyofanyika katika Bandari ya Dar es Salaam yameongeza uwezo wa bandari hiyo kuhudumia biashara ya ndani na kikanda, huku Serikali ikiendelea kupanua na kuboresha shughuli za bandari za Bahari ya Hindi pamoja na zile za maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa.
Aidha, amewataka viongozi wa vyama vya siasa kushirikiana katika kulinda amani, umoja na maslahi ya Taifa, akisisitiza kuwa ulinzi wa Tanzania ni jukumu la pamoja linalohusisha Serikali, vyama vya siasa na wananchi wote.
Katika mkutano huo, viongozi wa vyama vya siasa waliwasilisha maoni na mapendekezo yao kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Serikali iliahidi kuendelea kuyapokea na kuyafanyia kazi kupitia majukwaa rasmi ya majadiliano na mifumo ya maamuzi.
Mkutano huo ni wa pili kuitishwa na Rais Samia tangu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Mkutano wa kwanza ulifanyika Machi 31, 2026, Ikulu ya Dar es Salaam, ukiwakutanisha wagombea wa urais na wagombea wenza kutoka vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi huo.






























.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)








