Mbogwe, Geita


‎Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imetenga kiasi cha shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi 554 wanaoathiriwa na ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 58 kwa kiwango cha lami wilaya ya Mbogwe mkoani Geita.

‎Zoezi hilo linahusisha wananchi ambao mali zao ikiwemo nyumba, mazao na maeneo mengine zimeathiriwa na utekelezaji wa mradi huo unaolenga kuboresha miundombinu ya usafirishaji na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii katika wilaya ya Mbogwe.

‎Akizungumza wakati akitoa taarifa kuhusu utekelezaji wa zoezi hilo, Meneja wa TARURA wilaya ya Mbogwe Mhandisi Patrick Chacha amesema tathmini ya mali za wananchi wanaoathiriwa na mradi imefanyika kwa lengo la kuhakikisha wanapata stahiki zao kabla ya kupisha utekelezaji wa mradi.

‎Mhandisi Chacha amesema ulipaji wa fidia ni sehemu muhimu ya utekelezaji wa mradi kwani unalenga kuwawezesha wananchi wanaoathiriwa na mradi kurejesha maisha yao na kuendelea na shughuli zao baada ya kupisha ujenzi wa barabara.

‎"Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetenga kiasi hiki cha fedha ili kuwezesha wananchi kujenga nyumba mpya na kuendelea na maisha yao baada ya kuondolewa makazi yao ya awali kwa ajili ya kupisha ujenzi wa barabara", amesema Mhandisi Chacha.

‎Aidha, Mhandisi Chacha amesema wilaya ya Mbogwe ni miongoni mwa maeneo yatakayopata manufaa makubwa kutokana na mradi huo akieleza kuwa ujenzi wa kilomita 58 kwa kiwango cha lami utaboresha usafiri na usafirishaji, huku ukifungua fursa mpya za biashara na kuongeza thamani ya shughuli za kiuchumi kwa wananchi.

‎Amesema barabara hizo zitakapokamilika zitasaidia kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na mazao, kupunguza changamoto za usafiri na kuongeza ufanisi wa shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

‎Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kijiji cha Kabanga Bw. Joseph Masanja amesema zoezi la tathmini ya mali za wananchi katika eneo lake limefanyika kwa ufasaha huku wananchi wakieleza kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa na serikali katika kuhakikisha wanapata fidia zao.

‎Masanja amesema awali baadhi ya wananchi walikuwa na mashaka kuhusu uwezekano wa utekelezaji wa mradi huo lakini hatua iliyofikiwa sasa imewapa matumaini makubwa.

‎"Mwanzoni watu walidhani suala hili haliwezekani lakini sasa tumefikia hatua ya mwisho ya kulipwa fidia na kila mmoja wetu anapongeza jitihada za serikali", amesema.

‎Ametoa wito kwa wananchi wa Kabanga na maeneo mengine ya Mbogwe kutumia fursa zitakazojitokeza baada ya kukamilika kwa mradi huo hususan katika biashara, kilimo, usafirishaji na huduma mbalimbali.

‎Mradi wa ujenzi wa barabara hizo unatekelezwa na TARURA kupitia mradi wa RISE unaogharamiwa na mkopo nafuu toka Benki ya Dunia.







Bodi ya Wakurugenzi ya INADES Formation Tanzania imefanya kikao chake cha kwanza tangu ichaguliwe mwezi Mei, kikilenga kupitia utekelezaji wa bajeti na shughuli za taasisi kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2026, pamoja na kujadili mipango ya utekelezaji kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2026.

Akizungumza Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Alphonce Katunzi, Jijini Dodoma, amesema lengo ni kuhakikisha kuwa mipango ya taasisi inaendana na mahitaji halisi na kwamba rasilimali zilizopo zinatumika kwa ufanisi katika kutekeleza majukumu na kufikia matokeo yaliyokusudiwa.

Amesema taasisi hiyo inataka kuendelea kuboresha namna inavyotekeleza shughuli zake, ikiwemo kuhakikisha huduma na programu zinazotolewa zinaendana na mahitaji ya jamii na wanufaika, kwa kuzingatia mfumo unaoangalia mahitaji halisi.

Amesema kikao hicho pia kimejadili na kupitisha makadirio ya bajeti ya mwaka 2027, huku kikifanya tathmini ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026 kwa kipindi cha Januari hadi Juni na kuangalia mipango ya utekelezaji kwa kipindi kilichobaki cha mwaka.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa INADES Formation Tanzania, Jacquline Nicodemas, amesema kabla ya kikao cha bodi, kwa takribani siku tatu kulifanyika vikao vya kiutendaji na kimaamuzi, ikiwemo vya Kamati ya Fedha, Rasilimali Watu na Utendaji Kazi pamoja na Kamati ya Mafunzo na Afya ya Jumuiya.

Amesema vikao hivyo ni sehemu ya kuimarisha utawala bora, uwajibikaji na utendaji wa taasisi, huku akieleza kuwa katika kipindi cha hivi karibuni taasisi imetekeleza programu kuu mbili zilizosaidia kuimarisha ushirikiano na Serikali, wadau mbalimbali pamoja na jamii, ikiwemo kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Specioza Kifuto, amesema baada ya kikao hicho wanatarajia wanajumuiya na wadau kuanza kuona mabadiliko katika utekelezaji wa shughuli za taasisi, ikiwemo kuboreshwa kwa huduma zinazotolewa kwa wakulima na jamii kwa ujumla, amesisitiza wadau kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa shughuli, kutumia mafunzo wanayopata katika vitendo na kushiriki katika kutekeleza maamuzi yaliyokubaliwa.








Na Vero Ignatus Michuzi Tv Arusha

Tanzania imepiga hatua nyingine katika kujiweka tayari kwa ulinzi na usalama kuelekea Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, baada ya kufungwa kwa mafunzo maalum ya siku tano mkoani Arusha yaliyolenga kuimarisha usalama wa nyuklia na mionzi.

​Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) kwa kushirikiana na Wakala wa Kimataifa wa Nguvu za Atomu (IAEA), yalihusisha vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na taasisi mbalimbali nchini ili kujenga uwezo wa kuzuia, kutambua na kukabiliana na vitisho wakati wa mashindano hayo.

​Akifunga mafunzo hayo ya siku tano Jijini Arusha Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya AFCON 2027, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Muliro J. Muliro, alisema kuwa maandalizi hayo ni chachu ya kuhakikisha nchi inakuwa na mifumo madhubuti ya kiusalama.

​SACP Muliro aliwataka washiriki kutumia maarifa waliyopata kufanya tathmini katika taasisi zao ili kubaini uwezo uliopo na kufanyia kazi mapungufu mapema, akisisitiza kuwa ukubwa wa mashindano ya AFCON 2027—yatakayoandaliwa kwa pamoja kati ya Tanzania, Kenya na Uganda—unahitaji maandalizi ya kina.

​Mafunzo hayo yalichanganya nadharia za darasani na mazoezi ya vitendo, ikiwa ni pamoja na zoezi la kutafuta na kutambua chanzo bandia cha mionzi kilichokuwa kimefichwa. Zoezi hilo lilipima uwezo wa washiriki katika kutumia vifaa, maarifa na taratibu za kiusalama walizofundishwa katika mazingira halisi.

​Kwa upande wa sekta ya michezo, Alex Mkenyenge kutoka Idara ya Michezo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, alieleza kuwa usalama wa viwanja na maeneo ya michezo ni nguzo kuu ya maandalizi hayo.

​"Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika ujenzi na uboreshaji wa viwanja vya mechi na mazoezi jijini Dar es Salaam, Arusha na Zanzibar. Ni muhimu kuhakikisha miundombinu hii na watu watakaoitumia wanalindwa ipasavyo ili kila anayekuja arejee nyumbani salama," alisema Mkenyenge huku akiishukuru TAEC na IAEA kwa kuongeza utayari wa nchi.

​Naye mwezeshaji wa mafunzo hayo kutoka Côte d’Ivoire, Lacina Soro, alibainisha kuwa ufanisi wa usalama katika matukio makubwa unategemea ushirikiano kati ya teknolojia na uwezo wa wataalamu, akisisitiza kuwa kuwa na vifaa pekee haitoshi bila uwepo wa mipango madhubuti, tathmini ya vitisho kabla ya tukio, na uratibu mzuri wa mawasiliano kati ya taasisi husika.







Na. Vero Ignatus, Michuzi Tv -Arusha

Naibu Waziri wa Utalii, Hamad Hassan Chande, ametaja uwepo wa utalii wa maombi katika Hifadhi ya Msitu wa Ziwa Duluti, Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha,mazingira yake ya asili yana fursa kubwa ya kuendeleza aina mbalimbali za utalii,

Amesema utalii huo ndani ya Hifadhi ya Ziwa hilo unasaidia kukuza imani za watu na kuchangia maendeleo endelevu ya eneo hilo hivyo amewataka wananchi na wadau kuendelea kutunza mazingira na vivutio hivyo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho kwaajili ya maendeleo ya Kitaifa na kukuza uchumi.

Ametoa rai kwa wawekezaji wa ndani na nje kuchangamkia fursa katika eneo hilo, hususan katika miundombinu na huduma za utalii, ili kuongeza idadi ya watalii na mchango wa eneo hilo kwni Ziwa hilo halikauki na ni sababu kubwa ya kivutio huku akisisitiza Jamii kwa kushirikiana na Serikali pamoja na sekta binafsi katika kulilinda eneo hilo la utalii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Mbunge wa Korogwe Vijijini, Timotheo Mzava, aliwaongoza wajumbe wa Kamati hiyo katika ziara ya kutembelea Hifadhi hiyo kwa lengo la kukagua hali ya uhifadhi, kutathmini fursa za utalii wa ikolojia na kujadili changamoto zinazokabili eneo hilo la Ziwa Duluti

Mzava amepongeza na kuzisihi sekta binafsi kuboresha miundombinu na huduma kuelekea maandalizi ya Tanzania kuwa mwenyeji wa AFCON 2027 ,Sambamba na kuwa taka Watanzania kutembelea vivutio vilivyopo katika Hifadhi hiyo ya msitu wa ziwa Duluti

Peter Myonga ni Mhifadhi Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), amesema kuwa TFS imeendelea kuboresha huduma na miundombinu katika Hifadhi ya Msitu wa Ziwa Duluti, ikiwemo kuongeza maeneo ya malazi ili kuhudumia wageni wengi zaidi.

Myonga aliongeza kuwa hifadhi hiyo ina vivutio mbalimbali, ikiwemo utalii wa , matembezi ya kitalii, shughuli za majini,maombi, mandhari ya Mlima Meru , Kilimanjaro,kuna mnyama Kenge, hivyo amewasihi wananchi kutembelea eneo hilo kwa ajili ya kukuza utalii wa ndani.








Timu ya Ushirombo Warriors FC imetwaa ubingwa wa Wilaya ya Bukombe katika mashindano ya KNK CUP 2026, baada ya kuichapa Katome FC mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa tarehe 7 Septemba 2026 katika Uwanja wa Bukombe Stadium uliopo Mtaa wa Kilimahewa, Kata ya Katente, Tarafa ya Ushirombo, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita.

Ushirombo Warriors walionyesha kiwango kizuri na kutumia vyema nafasi walizopata. Bao la kwanza lilifungwa dakika ya 43 na mshambuliaji wao Hames Kigwangala kabla ya mapumziko.

Kama mabingwa, Ushirombo Warriors FC walikabidhiwa kombe, seti tatu za jezi, mipira mitatu pamoja na kitita cha shilingi milioni 5. Katome FC ambao walimaliza nafasi ya pili walikabidhiwa seti mbili za jezi, mipira miwili pamoja na shilingi milioni 3. Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Msasa FC ambao walikabidhiwa seti moja ya jezi, mpira mmoja pamoja na shilingi milioni 1.

Zawadi hizo zilikabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Paskasi Muragili, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita. Mashindano hayo yanafadhiliwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Dkt. Doto Biteko.

Mratibu wa Kamati ya Mashindano ya KNK CUP 2026 Wilaya ya Bukombe, Bosco Mwidad, alisema mashindano hayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwaibua vijana wenye vipaji vya soka. Alisema tangu mashindano hayo yalipoanza mwezi Julai mwaka huu, jumla ya timu 248 zilishiriki, huku zawadi zikitolewa kuanzia ngazi ya kata hadi tarafa.

Nahodha wa Ushirombo Warriors FC, Damas Buyenze, alieleza furaha yake baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Wilaya kwa mara ya kwanza. Alisema “Nina furaha sana pamoja na wachezaji wenzangu kwa kutwaa ubingwa wa Wilaya, kwani si jambo dogo. Tulijipa moyo, tukajituma na kumsikiliza mwalimu wa timu, na leo tumetwaa ubingwa. Pia namshukuru Mungu kwa kunisaidia kuwa golikipa bora”.

Wananchi wa Bukombe pamoja na wapenda michezo kwa ujumla wamemshukuru Dkt. Doto Mashaka Biteko kwa kuendelea kugharamia mashindano hayo ambayo yamekuwa chachu kubwa ya kukuza na kuibua vipaji vya watoto na vijana katika Wilaya hiyo.











Jumla ya watoto wachanga 15 wenye changamoto ya manjano na watoto zaidi ya 30 njiti hupokelewa kila mwezi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita. Changamoto hizo zimekuwa zikisababisha vifo vingi kwa watoto wachanga.

Hali hiyo imeiibua Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Geita kuona ipo haja ya kuongeza nguvu katika mapambano ya kuwaokoa watoto hao.

TAKUKURU Mkoa wa Geita imetoa vifaa vya kuokoa watoto njiti na wenye manjano, ambavyo ni infant warmer pamoja na photo therapy kwa ajili ya kuzuia vifo vya watoto wachanga.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Nchini, Neema Mwakalyele amesema zoezi la kukabidhi mashine hizo katika hospitali mbalimbali limefanyika katika zaidi ya mikoa 20 nchini.

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita imepatiwa jumla ya mashine 6 za aina hiyo, wakati mahitaji ni jumla ya mashine 10 ili kumaliza kabisa vifo vya watoto njiti na wenye manjano.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, ameishukuru TAKUKURU kwa vifaa hivyo ambavyo vinaenda kuokoa maisha ya watoto wachanga. Amesema atahakikisha anachangia kupatikana kwa mashine zilizobaki ili kumaliza kabisa changamoto hiyo.






- Ushirikiano huu kupitia taasisi zinazosaidia wajasiriamali vyuoni unalenga kuwafikia zaidi ya wajasiriamali 1,000 na kusaidia biashara zaidi ya 40 kukua na kupanuka


Dar es Salaam, Septemba 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imetangaza kuingia katika ubia wa miaka mitatu na Bridge for Billions, mtandao wa kimataifa wa ujasiriamali, kwa lengo la kupanua wigo na kuongeza matokeo ya mpango wa Vodacom Digital Accelerator (VDA).

Katika kipindi cha miaka mitatu ya ubia huo, mashirika hayo mawili yatazijengea uwezo na kuziwezesha taasisi zinazosaidia wajasiriamali (ESOs) kote nchini Tanzania na hivyo kuwafikia zaidi ya wajasiriamali 1,000 na kusaidia biashara zaidi ya 40 kukua na kupanuka.

Ushirikiano huu unaashiria mabadiliko katika namna VDA inavyotekeleza na kuongeza matokeo yake. Pamoja na kuendelea na lengo la kusaidia biashara changa moja kwa moja, mpango huu sasa utawekeza pia katika vituo vya kulea na kukuza biashara, vituo vya ujasiriamali, vyuo vikuu na mashirika ya maendeleo ya biashara yanayowasaidia waanzilishi wa biashara kila siku. Hatua hii inalenga kuimarisha mifumo ambayo wajasiriamali nchini Tanzania wanaihitaji hata baada ya kumalizika kwa programu ya kundi fulani la washiriki.

Kupitia makubaliano hayo, Bridge for Billions italeta nchini utaalamu wake katika programu za kulea na kukuza biashara changa (incubation), teknolojia za kidijitali na uzoefu wa kujenga uwezo wa taasisi zinazosaidia wajasiriamali. Taasisi zitakazochaguliwa zitapatiwa mafunzo maalumu, zitawezeshwa kutumia zana na mifumo ya Bridge for Billions, pamoja na kupata msaada katika kubuni programu na kuziendesha.

Aidha, taasisi hizo zitaunganishwa na mtandao wa kimataifa wa washauri na taasisi zinazosaidia wajasiriamali, hivyo kuwawezesha kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujenga mahusiano na taasisi nyingine.

Wajasiriamali watakaopatikana kupitia taasisi hizo watapitia mchakato maalumu wa kulea na kukuza biashara zao, huku biashara zitakazoonesha uwezo mkubwa wa kukua zikiendelea kwenye hatua ya acceleration, ambapo zitapatiwa msaada wa kina zaidi katika kukuza biashara na kujiandaa kwa fursa za uwekezaji.

Tangu kuzinduliwa kwake mwaka 2019, Vodacom Digital Accelerator imekuwa ikiunga mkono biashara changa na zinazokua zinazotumia teknolojia kutengeneza bidhaa na huduma zenye uwezo wa kukua, katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo, elimu na huduma za kifedha.

Kupitia awamu mbalimbali, programu hiyo imewapatia wajasiriamali mafunzo, ushauri wa kitaalamu, teknolojia, fursa za kuunganishwa na wawekezaji, pamoja na fursa za kufikia mitandao na washirika wa Vodacom.

Ubia huu wa miaka mitatu unaendeleza safari ya VDA kutoka kwenye programu zinazotekelezwa kwa awamu moja baada ya nyingine hadi kwenye uwekezaji wa muda mrefu katika kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini.

Kundi la kwanza la taasisi zitakazoshiriki katika mpango huu linatarajiwa kutangazwa Oktoba 2026, huku maombi kwa wajasiriamali yakitarajiwa kufunguliwa mwishoni mwa Septemba 2026.
Mkurugenzi wa Vodacom Business Nguvu Kamando (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Programu za Afrika wa Bridge for Billions, Liliosa Mbirimi (kulia), muda mfupi baada ya kutangazwa kwa ushirikiano wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na Bridge for Billions. Ushirikiano huo unalenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini kwa kuwafikia zaidi ya wajasiriamali na wabunifu 1,000 na kusaidia zaidi ya biashara 40 kukua na kupanuka, ushirikiano huu ulitangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3 jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Programu za Afrika wa Bridge for Billions, Liliosa Mbirimi (kulia), akizungumza wakati wa kutangazwa kwa ushirikiano wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na kampuni hiyo unaolenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini kwa kuwafikia zaidi ya wajasiriamali na wabunifu 1,000 na kusaidia zaidi ya biashara 40 kukua na kupanuka. Ushirikiano huo ulitangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Vodacom Business Nguvu Kamando.

Baadhi ya washiriki na wabunifu wakifuatilia uzinduzi wa ushirikiano wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na Bridge for Billions unaolenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini uliotangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3 jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Vodacom Business Biashara Nguvu Kamando, akizungumza wakati wa kutangazwa kwa ushirikiano mpya wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na Bridge for Billions, unaolenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini na kuwawezesha wajasiriamali na wabunifu kukua. Ushirikiano huo ulitangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3 jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Programu za Afrika wa Bridge for Billions, Liliosa Mbirimi.


Mkurugenzi wa Programu za Afrika wa Bridge for Billions, Liliosa Mbirimi (kulia) akifafanua kuhusu ushirikiano mpya wa miaka mitatu kati ya Vodacom Digital Accelerator (VDA) na kampuni hiyo unaolenga kuimarisha mfumo wa ujasiriamali nchini kwa kuwafikia zaidi ya wajasiriamali na wabunifu 1,000 na kusaidia zaidi ya biashara 40 kukua na kupanuka. Ushirikiano huo ulitangazwa wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Septemba 3 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Vodacom Business Nguvu Kamando.


Vodacom Tanzania PLC, kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited, imehitimisha mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yaliyofanyika katika Uwanja wa TPDF Lugalo Golf Club, yakiwakutanisha wachezaji wapatao 150 kutoka Tanzania na nchi jirani, wakiwemo viongozi wa biashara, wakurugenzi na wakuu wa makampuni pamoja na wapenzi wa mchezo wa golf.

Wachezaji gofu Khalid Shemndolwa na Yvonne Ondari wameibuka washinda kwa jumla shindano la Vodacom Corporate Masters kwa upande wa wanaume na wanawake. Katika shindano hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Lugalo, Shemndolwa alikusanya pointi 42 huku Ondari akikusanya pointi kama hizo katika mashindano hayo ya siku moja.

Mbali ya Shemndolwa na Ondari, Godfrey Abel aliibuka mhsindi katika daraja A, kwa kupata pointi 42, akifuatiwa na Likuli Juma aliyepata pointi 41 ambapo Sigfrid Urassa alitwaa ubingwa wa daraja B kwa pointi 40, akimzidi Godfrey Kilenga aliyemaliza na pointi hizo hizo, lakini Urassa akashinda kwa kanuni ya countback.

Boniface Japhet alitwaa ubingwa wa daraha C baada ya kupata pointi 39, huku Abdallah Singano akimaliza nafasi ya pili kwa pointi 37. Kwa upande wa wanawake, Neema Job alimaliza na pointi 42 na kutwaa ubingwa, akifuatiwa na Leticia Kapalia aliyepata pointi 40. Mashindano ya timu za kampuni nayo yalikuwa kivutio kikubwa, huku timu ya KQ ikiibuka mshindi baada ya kushindana na timu nyingine tisa za kampuni.

Zawadi maalum za mtu mmoja mmoja zilienda kwa Michael Norbert aliyeshinda Longest Drive kwa wanaume, huku Kapalia akitwaa tuzo hiyo kwa wanawake. Harshid Barmeda alishinda Nearest to the Pin kwa wanaume, wakati Vaileth James akitwaa tuzo hiyo kwa wanawake.

Mbali na ushindani, washiriki pamoja na familia zao walifurahia shughuli mbalimbali katika eneo la Corporate Village, lililokuwa na burudani, maonesho ya biashara, magari ya zamani pamoja na eneo maalum la watoto.

Mkurugenzi wa Vodacom Business wa Vodacom Tanzania PLC, Nguvu Kamando, alisema mashindano hayo yameendelea kuonyesha nafasi ya michezo katika kujenga mahusiano yenye tija katika biashara.

“Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup imethibitisha tena kwamba michezo ni jukwaa lenye nguvu katika kujenga mahusiano ya muda mrefu ya kibiashara. Tunafurahishwa na ushiriki mkubwa wa kampuni na kasi ya mahusiano mapya yaliyojengwa wiki hii,” alisema Kamando.

Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Kariuki, alizipongeza kampuni zilizoshiriki na kusema mashindano hayo yanaendelea kuchangia katika kujenga mtandao wa kibiashara na kukuza mchezo wa gofu.

“Mwaka huu tulishuhudia ushindani wa kiwango cha juu uwanjani na ushiriki wenye maana katika biashara nje ya uwanja. Hilo ndilo lengo kuu la Corporate Masters, kuzikutanisha kampuni katika mazingira rafiki yanayozalisha fursa halisi za ushirikiano,” alisema Kariuki.

Alisema ushirikiano kati ya Vodacom na Corporate Masters unaonyesha namna kampuni zinavyoweza kufanya kazi pamoja katika kutengeneza thamani kwa wateja na wadau, huku zikiunga mkono maendeleo ya mchezo wa gofu nchini Tanzania.

Kufanikiwa kwa mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 kunaendelea kuthibitisha mkakati wa Vodacom Tanzania wa kutumia michezo kama jukwaa la kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kuhamasisha ubunifu na kuwasogeza karibu viongozi wa biashara na suluhisho za kidijitali zinazochochea ukuaji wa uchumi wa Tanzania.
Mshindi wa jumla kwa upande wa wanawake, Yvonne Ondari (wa tatu kushoto), akipokea zawadi baada ya kutwaa taji katika Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament yaliyofanyika Lugalo Golf Club mwishoni mwa wiki. Ondari alikusanya pointi 42 (CB) katika mashindano yaliyoshirikisha wachezaji golf 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando (kushoto), akikabidhi zawadi ya tiketi ya kwenda na kurudi Mauritius kwa mshindi wa jumla kwa wanaume Khalid Shemndolwa (wa tatu kushoto) katika mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Shemndolwa alikusanya point 42 katika mashindano yaliyoshirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Washindi wa Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament katika makundi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea zawadi zao, Tukio hilo lilifanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki


Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, akishiriki mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, Septemba 5, 2026. Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.
Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Business Joseph Sayi, akishiriki mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, Septemba 5, 2026. Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

TBN Chairman Beda Msimbe speaks during a meeting with a delegation from the Public Service Social Security Fund (PSSSF) on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam


TBN Chairman Beda Msimbe speaks with Mr Abdul Njaidi, delegation leader from the Public Service Social Security Fund (PSSSF), during their meeting on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam.



Mr Abdul Njaidi, delegation leader from the Public Service Social Security Fund (PSSSF), speaks with TBN leadership during their meeting on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam

TBN Trustee Issa Michuzi makes a point during the meeting


TBN Chairman Beda Msimbe receives PSSSF publications from Mr Abdul Njaidi, delegation leader from the Public Service Social Security Fund, during their meeting on Monday, September 7, 2026, at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam.

By TBN Reporter

The Tanzania Bloggers Network (TBN) has reaffirmed its commitment to working with public and private institutions to produce and disseminate constructive content that educates the public and projects a positive image of Tanzania across digital platforms.

Speaking during a meeting between TBN leaders and a delegation from the Public Service Social Security Fund (PSSSF) at the TBN headquarters in Kijitonyama, Dar es Salaam, TBN Chairman Beda Msimbe said there had never been a more important time for Tanzania’s development achievements to receive greater prominence in the digital space.

He said this had become particularly important in an era when artificial intelligence enables information to be searched, retrieved and circulated more rapidly than ever before.

“It is embarrassing to see that much of the information about Tanzania dominating digital platforms and spreading around the world is driven by online gossip rather than meaningful development stories,” Msimbe said.

Citing a recent example, he said that while President Dr Samia Suluhu Hassan was commissioning the Julius Nyerere Hydropower Project—an undertaking of immense importance to the country—some of the most widely circulated online stories from Tanzania concerned the private lives and childbirth experiences of film and music celebrities.

Msimbe said the situation demonstrated the urgent need for institutions, media organisations and other stakeholders to work together to ensure that Tanzania’s development achievements receive the prominence they deserve on digital platforms.

“TBN is ready to collaborate with different institutions to increase the volume of positive information available across digital platforms. Tanzania should not be known merely for stories concerning people’s private lives, but also for its considerable economic and social achievements,” he said.

Msimbe welcomed PSSSF’s commitment to working with TBN to broaden public education on social security, pension systems and investments undertaken by the Fund.

He said TBN has more than 200 members based in Tanzania and the diaspora, all capable of reaching large audiences through a wide range of digital platforms.

“We are prepared to use the expertise, experience and extensive reach of our members’ platforms to provide accurate information about PSSSF’s activities, services, investments and the various systems it administers,” Msimbe said.

TBN Trustee Issa Michuzi said the network has played an important role in the development of digital journalism in Tanzania and is proud to have members possessing considerable professionalism, experience and capacity to reach audiences across the country and beyond.

Michuzi said TBN was established to ensure Tanzania is properly represented in the digital arena by disseminating accurate, constructive information that stimulates development and contributes to the growth of the national economy.

“TBN is ready to work with PSSSF to ensure that information about social security reaches the public in clear, accurate and easily understood language through digital platforms,” Michuzi said.

TBN Secretary Rahel Pallangyo said the network was prepared to deploy its experienced writers and members’ platforms to ensure that citizens receive accurate and reliable information.

She said such information would enable the public to understand its rights and responsibilities, as well as the opportunities available through the country’s social security systems.

Pallangyo added that collaboration between TBN and PSSSF could provide an important bridge between the Fund and the public, particularly at a time when digital platforms have become some of the country’s principal sources of news, education and knowledge.

Speaking on behalf of PSSSF, delegation leader Abdul Njaidi said the visit formed part of the Fund’s continuing efforts to build closer relations with media stakeholders and strengthen the provision of public education.

Njaidi assured TBN leaders that the requests, proposals and observations presented during the meeting would be carefully considered and acted upon.

He said PSSSF was committed to ensuring that Tanzanians receive comprehensive and accurate information about pensions, social security and the Fund’s investments for the benefit of its members and the nation at large.

The PSSSF delegation was led by Njaidi and included Regina Kumba, Grayson Mgunda and Doreen Lyimo.

TBN was represented by Chairman Beda Msimbe, Secretary Rahel Pallangyo, communications specialist Cathbert Kajuna and Trustee Issa Michuzi.

 

Katika hatua inayolenga kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika Makao Makuu ya Muda ya Tanzania Bloggers Network (TBN), yaliyopo Kijitonyama, Dar es Salaam, kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wa mtandao huo.

Mazungumzo hayo yalilenga kujenga ushirikiano wenye manufaa kwa pande zote mbili, hususan katika masuala ya habari, uelimishaji wa umma na usambazaji wa taarifa na maarifa sahihi kuhusu mifumo ya hifadhi ya jamii, pensheni pamoja na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alisema mtandao huo uko tayari kutumia majukwaa yake kusimama kidete katika kutoa elimu na kusambaza taarifa sahihi kwa umma, hususan kupitia majukwaa ya kidijitali.

Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa wanachama wa TBN kupata mafunzo ya kina kuhusu shughuli, huduma na uendeshaji wa PSSSF, ili waweze kuwaelimisha wananchi kwa ufanisi na kwa usahihi zaidi.

“Ni muhimu kwanza sisi wanachama wa TBN kupata elimu ya kutosha kuhusu mfuko huu, ili elimu tutakayokwenda kuwapa wananchi iwe sahihi, yenye uelewa mpana na yenye tija,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa msafara wa PSSSF, Abdul Njaidi, alisema ziara hiyo imelenga kujenga uhusiano wa karibu na wadau wa sekta ya habari, pamoja na kuimarisha juhudi za kutoa elimu kwa jamii kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii.

Njaidi aliwahakikishia viongozi wa TBN kuwa hoja na mapendekezo yote yaliyowasilishwa katika mkutano huo yatafanyiwa kazi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo unalenga kuhakikisha wananchi wanapata uelewa mpana na sahihi kuhusu masuala ya pensheni na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, alisema mtandao huo wenye historia kubwa katika tasnia ya habari za mtandaoni unajivunia weledi na ufanisi katika kutekeleza majukumu yake.

Alisema TBN ipo kwa ajili ya kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali, kwa kutoa taarifa zenye kujenga na kuchochea maendeleo ya taifa.

“Tunataka kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali na kwamba taarifa zinazotolewa zinakuwa na mchango katika kuchochea na kutanua zaidi gurudumu la maendeleo ya taifa,” alisema Michuzi.

Kwa upande wake, Katibu wa TBN, Rahel Pallangyo, alisema mtandao huo uko tayari kutoa waandishi wake mahiri na kutumia majukwaa yake mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, za kuaminika na zenye tija kwa jamii.

Alisema ushirikiano huo utasaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii na kuwawezesha wadau mbalimbali kuelewa kwa kina huduma na fursa zinazotolewa na PSSSF.

Ushirikiano huo unatazamiwa kufungua ukurasa mpya katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni katika kufikisha elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi wengi zaidi nchini.

Katika mkutano huo, ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na Abdul Njaidi ulihusisha pia maofisa Regina Kumba, Grayson Mgunda na Doreen Lyimo.

Kwa upande wa TBN, viongozi walioshiriki mkutano huo ni Mwenyekiti Beda Msimbe, Katibu Rahel Pallangyo, Mtaalamu wa Mawasiliano Cathbert Kajuna na Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi.










Top News