NA MWANDISHI WETU

TIMU ya wanawake ya mchezo wa Hockey ya Royal Queens kutoka Zanzibar, imeanza kujiandaa na michuano ya Mapinduzi Cup inayotarajiwa kufanyika mapema mwakani ambapo imefanya mazoezi ya pamoja na wachezaji wa mchezo hao Tanzania Bara.

Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama cha Hockey Zanzibar , Juma Hassan Juma,amesema ni kwa mara ya kwanza timu ya Hockey ya wanawake kutoka Zanzibar kutua jijini humo kufanya mazoezi ya pamoja na wachezaji wa mchezo huo Tanzania bara.

Amesema , mazoezi hayo ya wiki moja yamekuwa na ufanisi mkubwa katika kuwanoa wachezaji wa timu hiyo ya wanawake.

"Tunaahidi kufanya vizuri katika michuano ya Mapinduzi Cup inayotarajiwa kufanyika Januari mwakani,"amesema Juma.

Ameeleza, changamoto iliyokuwepo awali Zanzibar ni kukosekana kwa viwanja maalumu vya mchezo huo ingawa

kuna mwamko wa jamii kushiriki na kuupenda mchezo huo huku akiishukuru Serikali chini ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuanza ujenzi wa viwanja mbalimbali na hamasa kubwa ya kuinua sekta ya michezo.

Ametoa wito kwa jamii na wahisani kusaidia kukuza mchezo huo wa Hockey hususan timu za majeshi Zanzibar kutoa wachezaji ambao watashiriki katika timu za wanawake za Hockey.

Kipa timu hiyo ya Royal Queens , Idaya Hassan, amesema mazoezi hayo ya pamoja yaliyofanyika katika viwanja vya JMK Youth Park, jijini Dar es Salaam, yamekuwa na ufanisi na yamesaidia wachezaji wa timu yake kujinoa kikamilifu.

Mratibu wa mchezo wa Hockey katika shule za Tanzania Bara , Elieza Mwankemwa, amesema mazoezi hayo ya wiki moja yameambatana na mafunzo mbalimbali kuiimnarisha timu hiyo ya wanawake kwani Zanzibar ilikuwa na timu nyingi za wanaume.








SINGIDA: Mwananchi na mamlaka nchini Tanzania zimetakiwa kuanza kuchukua hatua za mapema kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua kubwa na mafuriko yanayoweza kuambatana na hali ya hewa ya El Niño.

Rai hiyo imetolewa na Ndugu Ahmed Misanga wakati akizungumza mkoani Singida, ambapo amesisitiza umuhimu wa maandalizi ya mapema ili kupunguza madhara kwa maisha ya watu, afya, mifugo na mali.

Amesema iwapo mvua kubwa na mafuriko yatatokea, maandalizi ya dharura yanapaswa kuanza kabla ya hali kuwa mbaya, akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza madhara na kuokoa maisha.

Miongoni mwa hatua alizopendekeza ni kuongeza hifadhi ya chakula na maji salama, pamoja na kuhakikisha hospitali zina dawa na vifaa tiba vya kutosha na kuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa wengi endapo kutatokea ongezeko la mahitaji ya huduma za afya.

Aidha, Misanga amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uwezo wa kudhibiti magonjwa ya mlipuko ambayo yanaweza kujitokeza baada ya mafuriko, huku akipendekeza kuandaliwa kwa kambi za dharura kwa ajili ya wananchi watakaoweza kuathirika.

Amesema pia ni muhimu kuandaa Mobile Health Facilities (Mobile Clinics) zitakazoweza kuwafikia wananchi katika maeneo ambayo huduma za kawaida za afya zinaweza kuvurugwa kutokana na mafuriko.

Katika hatua nyingine, ameitaka jamii na mamlaka kuhakikisha kuna maandalizi ya kutosha ya neti za mbu, mablanketi, mashuka, magodoro na matenti kwa ajili ya waathirika wa mafuriko.

Kwa upande wa uokoaji, Misanga amesisitiza kuimarishwa kwa timu pamoja na vifaa vya uokoaji, huku akitaka maeneo hatarishi yatambuliwe mapema na njia salama za uokoaji ziwekwe wazi.

Amesema mfumo wa tahadhari na utoaji wa taarifa za mapema kwa wananchi nao unapaswa kuimarishwa ili jamii iweze kuchukua hatua kwa wakati pindi kunapokuwa na dalili za hatari.

“Tanzania tusisubiri dharura itokee, tujandae mapema ili tuokoe maisha, afya, mifugo na mali za wananchi,” amesisitiza Misanga.

Akizungumzia mifugo, Misanga amesema maandalizi yanapaswa kuhusisha pia ulinzi wa mifugo dhidi ya mafuriko, magonjwa na upotevu, ikiwa ni pamoja na kuandaa maeneo salama ya kuhamishia mifugo pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa chakula, maji na dawa za mifugo.

Amesema mafuriko yanaweza kuleta changamoto mbalimbali kwa jamii, hivyo maandalizi yanapaswa kuwa ya pamoja na kuhusisha sekta za afya, chakula, maji, mifugo na uokoaji.

Amehimiza wananchi na mamlaka kuchukua tahadhari mapema badala ya kusubiri madhara yatokee, akieleza kuwa maandalizi ya wakati yanaweza kuwa hatua muhimu katika kupunguza athari za mafuriko na kulinda maisha pamoja na mali za wananchi.

 

Na Vero Ignatus, Michuzi Tv Arusha

Tanzania imeendelea kuchukua hatua za kuimarisha usalama wa nyuklia na mionzi kuelekea Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ikiwemo matumizi ya vifaa vya kugundua mionzi katika maeneo muhimu na mipakani, pamoja na kuwajengea uwezo maofisa walio mstari wa mbele katika kubaini na kukabiliana na matukio yanayoweza kuhusisha vyanzo vya mionzi.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), Profesa Najat Kassim Mohammed, amesema Tanzania kwa kushirikiana na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) imeanza kuimarisha maandalizi ya usalama wa nyuklia kuelekea AFCON 2027. Amesema Tanzania ni kiongozi na kinara katika kuhakikisha usalama wa nyuklia na mionzi unazingatiwa katika maandalizi ya mashindano hayo.

Profesa Najat amesema Serikali imewekeza katika wataalamu, vifaa na kujenga uwezo wa kitaifa, huku akisisitiza kuwa ukubwa na hadhi ya AFCON 2027 vinahitaji maandalizi ya kina na ushirikiano wa taasisi mbalimbali. Amesema warsha hiyo inayofanyika Agosti 31 hadi Septemba 4, 2026, imewakutanisha wataalamu na maofisa kutoka JWTZ, Jeshi la Polisi, vyombo vya usalama, mamlaka za forodha na uhamiaji pamoja na wasimamizi wa viwanja vya michezo.

Amesema washiriki wa warsha hiyo watapata mafunzo ya nadharia na vitendo kuhusu utambuzi wa mionzi, tathmini ya tahadhari, upekuzi na matumizi ya vifaa vya kugundua mionzi, ikiwemo Personal Radiation Detectors (PRDs) na Radioisotope Identification Devices (RIDs)

_Mazoezi hayo pia yatahusisha uchunguzi wa kimionzi katika mazingira ya uwanja wa michezo na maeneo ya watazamaji ili kuongeza utayari kuelekea AFCON 2027.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka IAEA, Lacina Saro, amepongeza Tanzania kwa kuanza mapema maandalizi ya usalama wa nyuklia kuelekea AFCON 2027.

Amesema kuchaguliwa kwa Tanzania kuwa miongoni mwa wenyeji wa mashindano hayo ni jambo la kujivunia, lakini pia kunaambatana na wajibu wa kuhakikisha usalama unaandaliwa mapema, unafanyiwa majaribio na kutekelezwa kwa ufanisi. Ameongeza kuwa IAEA itaendelea kutoa miongozo, mafunzo na msaada wa kiufundi kwa Tanzania.

Naye Mkurugenzi wa Teknolojia na Huduma za Ufundi wa TAEC, Dkt. Remigius Kawala, amesema Tanzania ipo katika nafasi nzuri kutokana na uwekezaji wa Serikali katika wataalamu na vifaa vya usalama wa nyuklia na mionzi. Amesema zaidi ya asilimia 70 ya wataalamu wa TAEC wamebobea katika maeneo yanayohusiana na matumizi ya nguvu za atomu, nyuklia na mionzi, huku Tanzania ikiwa na vifaa vya kutosha vya kutekeleza majukumu ya kiusalama.

Dkt. Kawala amesema Tanzania imeomba msaada wa vifaa kwa kiwango cha chini ya asilimia 20 katika maandalizi ya AFCON 2027, jambo linaloonesha kuwa sehemu kubwa ya mahitaji inaweza kutekelezwa kwa kutumia uwezo na rasilimali zilizopo nchini. Amesema wataalamu wapatao 40 wanashiriki katika maandalizi hayo, huku Tanzania ikiwa ni miongoni mwa nchi wenyeji wa AFCON 2027 pamoja na Kenya na Uganda, ikiwa na lengo la kuhakikisha mashindano yanafanyika katika mazingira salama.

Washiriki wa warsha hiyo watapata mafunzo ya nadharia na vitendo kuhusu utambuzi wa mionzi, tathmini ya tahadhari, upekuzi na matumizi ya vifaa vya kugundua mionzi, ikiwemo Personal Radiation Detectors (PRDs) na Radioisotope Identification Devices (RIDs). Mazoezi hayo pia yatahusisha uchunguzi wa kimionzi katika mazingira ya uwanja wa michezo.









MOSHI, KILIMANJARO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasihi wananchi wa Mbuyuni, Wilaya ya Moshi, kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo leo, Septemba 1, 2026, wakati akiwasalimia wananchi wa Mbuyuni waliokusanyika kumlaki akiwa katika ziara binafsi mkoani Kilimanjaro.

Amesema kupitia maombi ya wananchi, ataweza kupata hekima na nguvu ya kumsaidia kwa utii Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia Watanzania.

Mhe. Ndejembi amesisitiza kuwa ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, huku akieleza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi katika kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema:

“Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama.”

Amesema kauli hiyo aliitoa pia mkoani Dodoma, kwa wananchi wa Chamwino, mara baada ya kuapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Awali, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambapo alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.






Na Janeth Raphael - MichuziTv Bungeni -Dodoma

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema Serikali zote mbili zimekubaliana kuondoa suala la mafuta na gesi asilia kwenye Orodha ya Masuala ya Muungano.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Reuben Kwagilwa, wakati akijibu swali la Mbunge Rashid Habib Ali Rashid (Mtambwe), aliyetaka kujua kama Serikali ina mpango wa kuondoa suala la mafuta na gesi kwenye Orodha ya Masuala ya Muungano.

Akijibu swali hilo, Kwagilwa amesema Serikali zote mbili zimekubaliana kuondoa Jambo la 15, linalohusu maliasili ya mafuta, mafuta yasiyochujwa ya motokaa, petroli na aina nyingine za mafuta au bidhaa pamoja na gesi asilia, kwenye orodha hiyo.

Amesema hatua hiyo inakwenda sambamba na hali ya sasa ambapo suala la mafuta na gesi asilia tayari linasimamiwa na kila upande wa Muungano kupitia sheria na mamlaka zake.

Kwa upande wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Naibu Waziri amesema imetunga Sheria ya Mafuta na Gesi Asilia ya Mwaka 2015, ambayo chini ya Kifungu cha 11 ilianzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kwa ajili ya kusimamia shughuli za sekta hiyo.

Kwa upande wa Zanzibar, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetunga Sheria ya Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia Namba 6 ya Mwaka 2016, iliyoanzisha Mamlaka ya Udhibiti, Utafutaji na Uendelezaji wa Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar (ZPRA).

Aidha, sheria hiyo imewezesha kuanzishwa kwa Kampuni ya Maendeleo ya Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar (ZPDC).

Kwa mantiki hiyo, Serikali imeeleza kuwa hatua ya kuondoa mafuta na gesi asilia kwenye Orodha ya Masuala ya Muungano inaendana na mfumo ambao tayari umewekwa wa kila upande kusimamia shughuli za sekta hiyo kwa mujibu wa sheria na taasisi zake.


Na: OWM – TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameelekeza waliokuwa wafanyabiashara 30 wa soko la ndizi Mabibo (Mahakama ya Ndizi) kurejea kufanya biashara kwa udhamini wa maandishi kutoka ofisi za Serikali za Mitaa.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Agosti 31, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi Ndogo ya OWM- TAMISEMI jijini Dar es Salaam, mara baada ya kupokea taarifa ya timu ya ufuatiliaji wa malalamiko ya wafanyabiashara hao wa soko la ndizi Mabibo, wakati wa kikao kazi chake na wafanyabiashara hao.

Aidha, Prof. Shemdoe ameilekeza Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kufanya tathmini ya mali ya Bw. Frego Njovu aliyewasilisha madai ya kuomba kurejeshewa fedha alizotumia kukarabati choo kilichopo sokoni hapo ambacho alikuwa akikisimamia.

Katika kuhakikisha haki inatendeka, Prof. Shemdoe ameelekeza bidhaa za mfanyabiashara Bw. Enock Kimwayeya aliyekuwa Mwenyekiti wa Wafanyabiashara waliowasilisha malalamiko kwa Prof. Shemdoe, arejeshewe bidhaa zake alizoziacha kwenye kibanda cha biashara pindi alipoondolewa, kwani taarifa ya timu ya ufuatiliaji imeainisha kuwa Halmashauri imekiri kwamba bidhaa za mfanyabiashara huyo zipo.

Ili kuimarisha usimamizi wa soko, Prof. Shemdoe amemuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo kumpeleka meneja wa soko mwingine kulisimamia soko hilo na aliyepo kupangiwa majukumu mengine.

Maelekezo hayo ya Prof. Shemdoe yametokana na maafikiano baina ya pande zote katika kikao kazi cha Waziri huyo na walalamikaji (wafanyabiashara) na walalamikiwa ambao ni Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Malalamiko ya wafanyabiashara hao 30 yaliwasilishwa kwa Prof. Shemdoe kupitia andiko lao la tarehe 15/01/2026 lililohusu Sakata la soko la Ndizi Mabibo wakilalamikia kupigwa marufuku kuingia sokoni, kutaifishwa na kuuzwa kwa maeneo yao ya biashara, aidha Manispaa ya Ubungo iliwaondoka sokoni wafanyabiashara hao kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu na kutoitambua manispaa hiyo kama msimamizi wa soko.










Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amezitaka nchi wanachama wa Harakati za Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) kuunganisha sauti na misimamo yao ili kuongeza ushawishi katika maamuzi ya kimataifa na kutetea maslahi ya mataifa yanayoendelea.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 01 Septemba 2026, jijini Belgrade, Jamhuri ya Serbia, alipowasilisha hotuba kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano Maalum wa Ngazi ya Juu wa Kumbukumbu ya Miaka 65 tangu kufanyika kwa Mkutano wa Kwanza wa Wakuu wa Nchi wa NAM.

Amesema misingi ya NAM iliyoasisiwa mwaka 1961 bado ina umuhimu katika dunia ya sasa, huku akisisitiza kuwa kutofungamana na upande wowote hakumaanishi kutokuwa na msimamo, bali ni uhuru wa mataifa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maslahi yao na kulinda uhuru na mamlaka yao.

Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kutatua migogoro kupitia mazungumzo, upatanishi na kujenga kuaminiana, pamoja na kushughulikia vyanzo vya migogoro vinavyotokana na ukosefu wa haki, usawa na ujumuishi.

Aidha, ametoa wito wa kufanyika kwa mageuzi katika mfumo wa Umoja wa Mataifa, ikiwemo Baraza la Usalama, pamoja na taasisi za fedha za kimataifa, ili kuongeza uwakilishi, uwazi na kuzingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea. Amesema Afrika inastahili uwakilishi mkubwa na wa haki zaidi katika maamuzi ya kimataifa.

Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kuimarisha Ushirikiano wa Kusini pamoja na ushirikiano kati ya NAM na BRICS, hususan katika fedha za maendeleo na mageuzi ya mfumo wa utawala wa kimataifa, bila kuathiri misingi na utambulisho wa NAM.

Amesema Tanzania itaendelea kuunga mkono NAM yenye umoja na yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa, kwa kuhimiza amani, haki ya maendeleo, ushirikiano wa Kusini na mfumo wa dunia wenye usawa na uwakilishi wa haki.

Mkutano huo wenye kaulimbiu “Urithi wa Kutofungamana na Upande Wowote: Mafunzo kwa Dunia ya Leo” umefunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Serbia, Mhe. Aleksandar Vučić, na kuhudhuriwa na Viongozi Wakuu wa Serikali pamoja na Wakuu wa Ujumbe kutoka mataifa 34.



















Na Janeth Raphael - MichuziTv

Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imejipanga kikamilifu kuhakikisha inatoa huduma za matibabu na tiba za kibobezi kwa wanamichezo watakaoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Tanzania kuelekea mashindano hayo makubwa ya kimataifa.

MOI imesema imeweka mikakati mahsusi ya kuhakikisha wanamichezo watakaopata changamoto za majeraha wakati wa michuano hiyo, pamoja na wale watakaohitaji kupima afya zao, wanapata huduma za kisasa, za haraka na zenye viwango vya kimataifa.

Akizungumza leo jijini Dodoma kuhusu maandalizi hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, amesema taasisi hiyo iko tayari kutumia wataalamu, miundombinu na teknolojia ilizonazo kuhakikisha wanamichezo wanapata huduma bora wakati wote wa michuano.

Amesema MOI ina zaidi ya Madaktari Bingwa Bobezi sita (6) waliobobea katika tiba za michezo (Sports Medicine), ambao wamepata mafunzo katika mataifa mbalimbali duniani na kurejea nchini wakiwa na ujuzi na uzoefu unaowawezesha kutoa huduma maalum kwa wanamichezo.

Kwa mujibu wa Dkt. Ulisubisya, baadhi ya wataalamu hao pia wamekuwa wakihudumia timu ya Taifa pamoja na kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), jambo linaloongeza uwezo wa MOI katika kushughulikia mahitaji ya kiafya ya wanamichezo wa ngazi ya juu.


KLINIKI MAALUM KWA WAGONJWA WA KIMATAIFA


Katika maandalizi hayo, MOI imeeleza kuwa ina Kliniki Maalum ya Wagonjwa wa Kimataifa (Premier and International Patient Services) inayolenga kutoa huduma kwa haraka na kwa viwango vinavyokidhi mahitaji ya wagonjwa na wageni wa kimataifa.

Huduma hiyo inatarajiwa kuwa sehemu muhimu katika kuwahudumia wanamichezo na wajumbe wa timu mbalimbali watakaohitaji huduma za kitabibu wakati wa michuano.

Aidha, MOI ina vyumba 25 vya kisasa vya kulaza wagonjwa wa kimataifa (Premier Wards), ambavyo vimeandaliwa kutoa mazingira bora ya malazi na matibabu kwa wagonjwa wanaohitaji huduma za kiwango cha juu.


TEKNOLOJIA NA VIFAA VYA KISASA

Dkt. Ulisubisya amesema uwezo wa MOI pia unaimarishwa na uwepo wa vifaa vya kisasa vya uchunguzi, tiba na upasuaji, vinavyowezesha wataalamu kutoa huduma za kibobezi kwa usahihi na kwa wakati.

Miongoni mwa vifaa hivyo ni MRI, CT Scan, Cathlab, Arthroscopic Towers, Brain Lab, Digital X-Ray, Ultrasound za kisasa, vifaa vya kisasa vya Microscopy kwa ajili ya upasuaji wa ubongo na mgongo, C-Arms pamoja na ETV Towers, sambamba na vifaa vingine vya kisasa.

Kwa kuwa michezo ya ushindani inaweza kuhusisha majeraha ya aina mbalimbali, MOI imesema uwepo wa teknolojia hizo unaipa uwezo wa kufanya uchunguzi wa haraka na kutoa matibabu yanayohitajika kulingana na aina na ukubwa wa jeraha.


KITENGO CHA DHARURA CHAWEKWA TAYARI


MOI pia imeweka mkazo katika maandalizi ya Kitengo cha Dharura, ambacho kimeandaliwa mahsusi kuhakikisha kinakuwa tayari kutoa huduma wakati wa kipindi cha michuano.

Dkt. Ulisubisya amesema MOI tayari ina uzoefu wa kuandaa huduma za dharura wakati wa mashindano makubwa ya michezo, akitoa mfano wa michuano ya CHAN, ambapo taasisi hiyo ilishiriki katika kutoa huduma za afya kwa maandalizi maalum.

Amesema uzoefu huo umejenga uwezo na utayari wa taasisi hiyo kukabiliana na mahitaji ya kitabibu yatakayojitokeza wakati wa AFCON 2027.

Kwa ujumla, MOI imesisitiza kuwa imejipanga kutumia wataalamu wake, huduma maalum, miundombinu na teknolojia ya kisasa kuhakikisha Tanzania inakuwa na mfumo madhubuti wa huduma za afya kwa wanamichezo wakati wa AFCON 2027.

“MOI tuko tayari kwa michuano ya AFCON Zanzibar na mikoa ya Arusha na Dar es Salaam,” amesema Dkt. Ulisubisya.

Kauli hiyo inaweka wazi dhamira ya MOI kuwa sehemu muhimu ya maandalizi ya Tanzania katika kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa maandalizi ya kutosha, ikiwemo uwepo wa huduma za afya zinazoweza kukidhi mahitaji ya wanamichezo wa ndani na wa kimataifa.

Taarifa hiyo imetolewa wakati wa kuwasilishwa kwa Taarifa ya Mafanikio ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Julai 2025 hadi Juni 2026, iliyotolewa jijini Dodoma, Septemba 1, 2026, na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya.


Na Janeth Raphael -MichuziTv -Bungeni Dodoma

SERIKALI imesema inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha taaluma na kazi ya udereva nchini zinapata staha, hadhi na heshima inayolingana na kada nyingine katika utumishi wa umma.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Regina Qwaray, wakati akijibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi (Mlalo) lililouliza kuhusu mkakati wa Serikali wa kuinua hadhi ya taaluma ya udereva.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Qwaray amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua kadhaa zikiwemo kuboresha Muundo wa Maendeleo ya Utumishi wa Kada ya Udereva, ili kuwawezesha watumishi wa kada hiyo kupata fursa za maendeleo ya kiutumishi.

Amesema Serikali pia inaendelea kuboresha mafunzo ya kitaaluma pamoja na viwango vya elimu kwa madereva, hatua inayolenga kuongeza weledi, ufanisi na uwezo wa watumishi hao katika kutekeleza majukumu yao.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, Serikali pia imeendelea kuimarisha motisha na maslahi ya kada ya udereva, kwa kuzingatia mazingira ya kazi na mahitaji ya utendaji, ili kuhakikisha madereva wanatekeleza majukumu yao katika mazingira yanayostahili.

Hatua hizo, amesema, ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha kada ya udereva inatambuliwa na kuthaminiwa kama taaluma yenye mchango muhimu katika utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.



 

SportPesa Tanzania sponsorship backs Rugby Union growth at Dar Rugby Saba 2026

SportPesa Tanzania sponsorship backs Rugby Union growth at Dar Rugby Saba 2026

Iringa Wild Dogs turned SportPesa Dar Rugby Saba 2026 into a final to remember after edging Dar Leopards 21–20 at Leaders Club in Kinondoni. The result gave the second leg of the SportPesa National Saba Circuit a dramatic finish, but the bigger story was the new partnership between SportPesa Tanzania and Tanzania Rugby Union. It was designed to grow rugby through regular competition, fan engagement, player development and national team support.

But this thrilling match was only the beginning. What makes this partnership truly special is the solid foundation being built for the future of rugby in Tanzania. SportPesa has stepped up as the National Rugby Sevens Circuit sponsor and the exclusive betting partner for five months. Beyond the games, the program is focused on raising the sport’s profile, engaging fans, developing players, and backing Tanzania’s national team, the Twiga Kings, with genuine commitment and energy.

Iringa Wild Dogs lifting the title

The Dar competition delivered the kind of contest that fans love. Iringa reached the final after a 27–0 semi-final victory over Kilimanjaro, while Dar Leopards defeated Arusha Rhinos 21–0. Arusha then secured third place by beating Kilimanjaro 19–7 before Iringa held off Dar 21–20 for the title.

Those results matter beyond the trophy. A close final creates a sporting memory, while the earlier matches showed the depth TRU is working to develop. For the SportPesa and Tanzania Rugby Union partnership, the weekend offered a credible starting point: regional rivalry, clear stakes and a champion tested to the final whistle.

National circuit gives clubs meaningful competition

Dar Rugby Saba was the second leg of the national circuit after the opening round in Dodoma. It featured men’s and girls’ teams from various regions, with over 150 players and officials participating. Teams competed for points ahead of the Grand Finale in Arusha in December. Officials from Kenya and Uganda supported local referees through officiating and knowledge-sharing.

That calendar is essential. Rugby cannot develop through isolated matches; clubs need regular competition, coaches need repeated tests and players need a route from regional teams to national selection. TRU President Jacob Jonas said the support should create more opportunities for players, coaches and young talent. By backing the SportPesa National Saba Circuit 2026, SportPesa Tanzania is helping build a system in which progress can be measured across several rounds.

SportPesa Tanzania rugby brings full support

The weekend also highlighted why making rugby visible and inviting public participation really matters. Hosting the event at Leaders Club gave the competition a vibrant, central stage in Dar es Salaam, while live social media updates brought the energy and excitement to fans beyond the venue. Honourable Zainab Issa, Special Seats Member of Parliament for Youth, joined as the official guest, lending important public support to a sport eager to reach a wider national audience.

SportPesa’s backing gives Tanzania rugby something every growing sport needs. This partnership also benefits from SportPesa’s rugby experience in Kenya and South Africa, adding valuable regional insight. The goal now is to build on that knowledge to create bigger events, boost exposure, and grow a passionate community around the game. Fans can follow rugby union markets on SportPesa’s digital platform, linking interest in the international game with awareness of local competition.

“We believe that a strong sports industry needs real support, and rugby has incredible potential to grow in Tanzania,” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.

Twiga Kings gives the SportPesa partnership next move

This agreement goes beyond just the local tournaments. SportPesa is also backing the Twiga Kings as they head to South Africa for the Obaro 7s in October. This shows the partnership’s true commitment to the national team and gives Tanzanian players a valuable chance to challenge themselves against tougher regional competition.

Playing internationally shines a light on where players need to improve—in areas like fitness, decision-making, and preparation. It also gives both players and coaches experience they can bring back to strengthen the national circuit. For a growing rugby community, the connection between club play and the national team is vital: clubs build the talent pool, while the national team sets the bar for what players should aim for.

Conclusion

Dar Rugby Saba 2026 gave SportPesa and TRU the kind of start rugby needs. A competitive final, regional participation, visible fan engagement and a clear link between club competition and the national team. If the circuit maintains that momentum through the Arusha finale and beyond, SportPesa’s partnership with TRU could become a turning point for rugby development in Tanzania

 


Taasisi za LALJI FOUNDATION na BARAKA  FOUNDATION  kwa kushirikiana na  VISION 4 ALL EYE CENTER  imeendesha Kambi ya Matibabu ya Macho Bure katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Mkoa wa Tanga, kwa lengo la kuwasaidia wananchi kupata huduma za uchunguzi, matibabu na upasuaji wa macho bila gharama.

Kambi hiyo iliyofanyika kwa muda wa siku tatu imewafikia jumla ya wananchi 3,259, ambao walihudhuria na kupata huduma mbalimbali za afya ya macho.

Akizungumza baada ya kutamatika kwa kambi hiyo mwenyekiti wa LALJI FOUNDATION Imtiaz Lalji amesema kwa siku zote tatu, jumla ya wagonjwa 333 walifanyiwa  upasuaji wa macho, Kati yao, 291 walibainika kuwa na tatizo la mtoto wa jicho (cataract), huku 39 wakiwa na matatizo madogo ya macho yaliyohitaji huduma za upasuaji.

Aidha, jumla ya wananchi 1,723 walipewa dawa kulingana na mahitaji yao ya kiafya, huku wananchi 1,706  wakipatiwa miwani ya kusomea (reading glasses).

Imtiaz Lalji, amesema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali kuwasaidia Watanzania kupata matibabu ya macho bila malipo, kutokana na changamoto ya magonjwa ya macho ambayo imeendelea kuwaathiri wananchi wengi.

“Takwimu zilizopatikana katika kambi hiyo zinaonesha ukubwa wa changamoto ya magonjwa ya macho katika jamii, akibainisha kuwa wananchi wa maeneo ya vijijini ni miongoni mwa wanaokumbwa zaidi na changamoto ya upatikanaji wa huduma za macho kwa wakati" ameongeza

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bi. Zahara Msangi, ameishukuru LALJI FOUNDATION na Baraka FOUNDATION  kwa kuguswa na changamoto zinazowakabili wananchi na kuamua kufikisha huduma za matibabu ya macho katika Halmashauri hiyo.

Amesema huduma hiyo imekuwa na umuhimu mkubwa kwa wananchi, hususan wale ambao wamepata fursa ya kufanyiwa uchunguzi, kupata dawa, miwani pamoja na upasuaji bila kulipia gharama.

Naye Mratibu wa Huduma za Macho Mkoa wa Tanga, Dkt. Husein Abassy, amesema kuletwa kwa huduma hiyo mkoani Tanga ni hatua muhimu inayolenga kuwafikia wananchi wenye uhitaji, hususan wale ambao wanakabiliwa na changamoto ya kupata huduma za macho kwa wakati.

Nao baadhi ya wananchi walionufaika na kambi hiyo wameeleza namna huduma hizo zilivyowasaidia kupata matibabu ambayo huenda wasingeweza kuyapata kwa urahisi kutokana na gharama.

Wameishukuru LALJI FOUNDATION kwa huduma hiyo na kutoa wito kwa taasisi nyingine, mashirika na wadau mbalimbali kuendelea kujitokeza na kushirikiana na Serikali katika kuboresha afya na ustawi wa wananchi.

Huduma hiyo ya matibabu ya macho bila malipo ni sehemu ya juhudi za LALJI FOUNDATION  katika kusaidia jamii na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi.

 Taasisi hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine katika kuwafikia wananchi wenye uhitaji katika maeneo mbalimbali nchini.







Top News