HUDUMA  ya Airtel Money School Pay imeendelea kurahisisha ulipaji na ukusanyaji wa ada za wanafunzi nchini, huku shule zaidi ya 800 kutoka mikoa 16 zikiwa tayari zimejiunga na kutumia mfumo huo wa kidigitali unaolenga kurahisisha malipo kwa wazazi na uendeshaji wa kifedha kwa shule.

Akizungumza wakati wa ziara katika Salaam Pre and Primary School, iliyopo Chamazi, Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Afisa Huduma wa Airtel Money School Pay, Roda William Mganga, alisema huduma hiyo ilianzishwa mwaka 2024 ikiwa na lengo la kutoa njia rahisi, salama na yenye ufanisi katika ulipaji wa ada na usimamizi wa taarifa za malipo.

Mganga alisema tangu kuanzishwa kwake, School Pay imefanikiwa kufikia shule zaidi ya 800 katika mikoa 16 nchini, huku lengo likiwa ni kuunganisha shule 1,000 kila mwaka. Mikoa ambayo tayari imefikiwa na huduma hiyo ni pamoja na Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma, Mbeya, Arusha, Mwanza na Mtwara.

Alisema miongoni mwa shule zinazotumia mfumo huo ni pamoja na St. Anne Maria Academy, Fountain Gate Schools, St. Anthony’s Secondary School, Salaam Pre and Primary School, Living Minds Pre and Primary School, Memon Pre and Primary School na Mbwawa Lutheran Secondary School, huku Airtel pia ikishirikiana na taasisi mbalimbali za kidini zinazoendesha shule.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Salaam Pre and Primary School, Kalunji Mkasa Idris, alisema shule hiyo imekuwa ikitumia School Pay tangu Septemba mwaka jana na kwamba mfumo huo umeleta mabadiliko makubwa katika ukusanyaji na usimamizi wa ada.

Alisema awali shule ilikuwa ikikabiliwa na changamoto za kupokea fedha taslimu, jambo ambalo liliongeza hatari ya fedha kupotea na kufanya ufuatiliaji wa malipo kuwa mgumu.

“School Pay imetusaidia sana katika ukusanyaji wa ada. Sasa fedha zinazoingizwa kupitia mfumo zinaonekana na kuingia benki, hivyo tunapata kumbukumbu sahihi na tunakuwa na uwezo wa kuzitumia kwa mahitaji ya shule,” alisema Idris.

Aidha, alisema mfumo huo umewarahisishia wazazi kwa kuwa hawalazimiki tena kwenda benki na kusimama kwenye foleni ili kulipia ada. Kwa mujibu wake, mzazi anaweza kufanya malipo kupitia simu yake wakati wowote, ikiwemo nyakati za usiku, na taarifa ya malipo kuonekana kwenye mfumo wa shule ndani ya muda mfupi, hivyo kurahisisha utoaji wa risiti na ufuatiliaji wa malipo.

Mhasibu wa Salaam Pre and Primary School, Fatma Yusuf, alisema School Pay imekuwa na mchango mkubwa katika kuweka kumbukumbu sahihi za malipo ya ada na kuwawezesha wazazi kupata risiti mara baada ya kufanya malipo.

Alisema mfumo huo umepunguza ulazima wa wazazi kufika shuleni kwa ajili ya kufanya malipo au kufuatilia risiti, kwani wanaweza kukamilisha mchakato huo wakiwa nyumbani.

Naye mzazi wa mwanafunzi wa Salaam Pre and Primary School, Hassan Said Malipa, alisema mfumo huo umemsaidia yeye na wazazi wengine kufuatilia kwa urahisi kiasi cha ada kilicholipwa na salio lililobaki. Alisema uwezo wa kufanya malipo kwa awamu kulingana na upatikanaji wa kipato umekuwa msaada mkubwa kwa wazazi, huku taarifa za malipo zikipatikana kwa wakati.

 



Na Mwandishi wetu-Iringa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe. Prof, Palamagamba Kabudi amesema Serikali itaendelea kuheshimu na kuthamini mchango wa kiuongozi uliotolewa na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu William Lukuvi.

Hayo ameyasema  wakati wa ibada ya Misa Takatifu ya kumaliza Msiba  iliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Idodi Mkoani Iringa na kuhudhuriwa na wananchi na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali.

Alisema, “Enzi za uhai wake Waziri Lukuvi alinisaidia kufahamu shughuli mbalimbali za Bunge na serikali na hivyo kupata weledi mzuri mambo mengi kutokana na uzoefu aliyokuwa nao,”


Aidha uwezo wake wa kusimamia nidhamu ipasavyo Bungeni ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na Bunge ilimfanya aendelee kuaminiwa katika kazi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu.

Kwa Upande Mama Germana Lukuvi Mjane wa Marehemu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe, Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushikamana na familia tangu walipopata msiba.

Awali Mbunge wa Isimani Mhe, Emanuela Mtatifikolo alisema Marehemu Lukuvi ataendelea kuishi kwenye mioyo ya wananchi wa Isimani, kwa mageuzi makubwa ya maendeleo aliyoyafanya.


“Uwakilishi wake kwa wananchi wa Jimbo la isimani na kwa kushirikiana na Serikali aliwezesha Jimbo la Isimani kunufaika na ujenzi wa barabara ya lami uimarishaji wa Huduma za afya na kuendelea kuboresha miundo mbinu ya elimu szambamba na umeme,” alibainisha


Na Belinda Joseph-Tanga

Mradi wa Mafunzo ya Kitaaluma ya Ufundi Stadi katika Sekta ya Migodi (IMTT) umeendelea kuwa daraja muhimu kwa vijana kupata ujuzi unaohitajika katika sekta ya migodi, huku mfumo wake wa Uanagenzi ukiwawezesha wanafunzi kujifunza darasani na kufanya kazi za vitendo katika migodi, hatua inayochangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kujenga uchumi jumuishi unaoshirikisha wananchi katika shughuli za uzalishaji.

Akizungumza na Michuzi TV  Agosti 16, 2026, katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu inayoendelea jijini Tanga kuanzia Agosti 15 hadi 24, Mkufunzi na Mratibu wa Uanagenzi wa IMTT kutoka VETA Moshi, mkoani Kilimanjaro, Mwl. John Nathan, amesema mpango huo ulianzishwa kwa ushirikiano kati ya VETA na Chemba ya Migodi Tanzania yaani (TCM).

Amebainisha kuwa tofauti na mafunzo ya kawaida ya darasani, mradi wa IMTT unafanyika katika mazingira mawili muhimu ni chuoni na katika eneo la kazi kwa maana ya viwandani, na Mfumo huo unamwezesha mwanafunzi kupata maarifa ya kinadharia na ujuzi wa vitendo kwa wakati mmoja, hivyo anapohitimu huwa tayari ana uzoefu wa mazingira halisi ya kazi.

“Anapokwenda kwenye kazi, anakuwa si mgeni tena, hahitaji uzoefu mwingine wa ziada ili kukidhi mahitaji ya ajira kwa sababu tayari ana uzoefu uliojengwa kutokana na muundo wa mafunzo".

Amesema kwa sasa, IMTT inatolewa katika chuo cha  VETA Moshi peke yake, hii ni baada ya tafiti za awali  zilifanyika na kubaini kuwa chuo hicho kilikuwa na mazingira, vifaa na miundombinu iliyohitajika kuendesha mafunzo hayo. Hata hivyo baadhi ya kampuni za migodi zimekuwa zikisaidia vijana kutoka maeneo yanayozunguka migodi kusafiri hadi Moshi kwa ajili ya mafunzo kabla ya kurejea katika maeneo yao ya kazi.

Ameeleza kuwa kwa mtu yeyote anayehitaji kujiunga na IMTT anatakiwa kuwa na ufaulu wa Kidato cha Nne na kuwa mzawa wa Tanzania na taarifa zaidi kuhusu taratibu za kujiunga wanaweza kufika VETA Moshi au kupata taarifa kupitia tovuti ya VETA.

Kwa upande wa mafanikio, amesema zaidi ya vijana 1,668 wamepatiwa mafunzo kupitia IMTT tangu kuanzishwa kwake mwaka 2009, ambapo asilimia 79.1 wameajiriwa katika migodi mbalimbali nchini, huku asilimia 1.1 wamepata ajira katika migodi nje ya nchi hali  inayoonesha kuwa mafunzo ya ufundi stadi yanaweza kuwa njia muhimu ya kuwawezesha vijana kupata ajira.

Akieleza mchango wa programu hiyo katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, amesema IMTT inawawezesha vijana kushiriki moja kwa moja katika sekta ya migodi kwa kuwapatia ujuzi unaowawezesha kuwa sehemu ya nguvu kazi yenye tija, ambapo ajira wanazopata vijana hao haziwanufaishi wao pekee, bali pia familia zao na jamii zinazowazunguka.

Aidha, amegusia  mabadiliko ya teknolojia katika sekta ya migodi yameifanya VETA kuendelea kuboresha mitaala ili kukidhi mahitaji mapya, hususan katika uchimbaji wa chini ya ardhi, amesema wanatarajia kuja na Programu sita mpya ambazo ni Scoop Operation, Tele-remote Bogger Operation, Cubex Operation, Jumbo Operation, Lifting and Rigging pamoja na Mobile Charging Unit Operation ili kuongeza ujuzi wa vijana wataokwenda kuisaidia sekta ya migodi kikamilifu kulingana na kasi ya ukuaji wa teknolojia.

Akitoa ujumbe kwa vijana wanaotembelea Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu inayofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga, aliwataka kutumia fursa hiyo kupata taarifa kuhusu mafunzo ya ufundi stadi na kuchukua hatua badala ya kubaki na ndoto bila kuzifanyia kazi.

“Usiwe na wazo kichwani ukabaki na wazo, fanyia kazi, anza sasa,” akieleza kuwa vijana waliopitia IMTT wameweza kufikia fursa mbalimbali za ajira ndani na nje ya nchi, jambo linaloonesha kuwa ujuzi wa ufundi unaweza kuwa msingi wa mafanikio ya kiuchumi kwa vijana.






The rapid adoption of digital technologies is transforming the banking industry, making financial services faster, more convenient and increasingly accessible to customers. However, banks must now focus on closing a critical gap in the digital customer journey, effective digital complaint handling.

Absa Bank Tanzania Head of Application Management at Absa Bank Tanzania Nicky Mlelwa, said digital transformation has fundamentally changed how customers interact with banks, moving the industry away from traditional processes such as queues, paperwork and frequent branch visits.

“Digital transformation has fundamentally changed the face of banking. What was once an industry defined by queues, paperwork and branch visits is now powered by speed, convenience and experiences that fit seamlessly into customers’ daily lives,” Mlelwa said.

He said advances in automation, artificial intelligence, real-time data and other modern technologies have enabled banks to provide services that previously required days or weeks in a matter of minutes or even seconds.

Customers can now open bank accounts, apply for loans, make payments and access financial services through digital platforms, with technologies such as real-time payments, digital lending, straight-through processing and open banking becoming increasingly central to the modern banking experience.

“Banking is no longer just a place to store money or process transactions. Instead, it has become a trusted companion that supports customers throughout their financial journeys,” Mlelwa said.

He explained that customers increasingly expect to manage their finances anytime and anywhere, whether they are paying bills, transferring money, accessing credit, saving or investing.

According to Mlelwa, the transformation is being supported by a sophisticated digital infrastructure that enables banks to respond more quickly to changing customer expectations.

Technologies such as microservices and application programming interfaces (APIs) allow complex banking systems to be broken into smaller and more flexible components, while cloud computing provides scalable computing capacity to support faster innovation.

Artificial intelligence and machine learning are also enabling banks to understand customer behaviour, anticipate needs and develop more personalised financial solutions.

“Together, these innovations are creating a new era of banking, one that is more connected, intelligent and customer-centric,” he said.

However, Mlelwa said banks should not measure digital transformation only by the number of services they have successfully moved online.

He identified digital complaint handling as an area that requires greater attention if banks are to deliver a truly seamless digital experience.

“Digital customers expect digital service, not just when everything works perfectly, but also when something goes wrong,” Mlelwa said.

He explained that customers who open accounts online, apply for loans through mobile applications or make digital transactions naturally expect to be able to report and resolve problems through the same digital channels.

While traditional channels such as call centres and branch visits remain important, he said they may not always meet the expectations of customers who have become accustomed to instant digital services.

“The expectation goes even further. Today’s digital customers anticipate systems that are intelligent enough to detect failures proactively and resolve them before the customer even raises a complaint,” he said.

Mlelwa warned that when customers are forced to move between different support channels to resolve a digital banking problem, the experience can become frustrating and undermine trust.

“The inability to lodge a complaint easily or receive swift digital resolution leaves customers feeling unheard and undervalued,” he said.

Mlelwa said the next phase of banking transformation should therefore focus on creating an end-to-end digital journey that continues beyond the completion of a transaction.

“The path forward is clear: banks must embrace a truly end-to-end digital journey, one that does not end at service delivery but extends seamlessly into customer support,” he said.

He said digital complaint management should be embedded within banking platforms, enabling customers to report problems instantly, track their complaints and receive updates without leaving the digital environment.

“This requires embedding complaint handling directly into the digital architecture of banking solutions. It means building systems that can capture issues instantly, track them transparently and resolve them efficiently,” Mlelwa said.

He added that effective digital complaint management should incorporate automated detection of anomalies, real-time notifications, self-service resolution options and swift escalation where human intervention is required.

“More importantly, it should provide customers with visibility and assurance that their concerns are being addressed,” he said.

Mlelwa said future competition in banking would increasingly be determined by the quality of customer experiences rather than the sophistication of products alone.

“In a market where customer expectations are continuously evolving, differentiation will no longer be driven solely by the sophistication of products but by the quality of experiences,” he said.

He stressed that banks need to listen to customers while continuing to innovate, arguing that technology should ultimately strengthen rather than weaken the human connection between financial institutions and their customers.

“Banks that succeed will be those that listen as well as they innovate, those that not only digitise services but also humanise the digital journey through responsiveness and empathy,” Mlelwa said.

He noted that unresolved complaints, failed transactions and delays can have a disproportionate impact on customer trust, making effective complaint management an essential component of the digital banking experience.

Mlelwa said the true measure of digital transformation should therefore extend beyond how quickly a bank can process a successful transaction.

“Ultimately, a truly transformed bank is one that ensures every interaction is digital, every complaint is resolved swiftly, and every customer feels heard,” he said.

According to Mlelwa, creating such an end-to-end experience will be essential for building trust, strengthening customer loyalty and securing long-term competitive advantage.

“Because in the end, a delighted customer is not just a satisfied user who is likely to spend more, it is an enduring source of value,” he said.





Wananchi wakipata elimu katika Banda la VETA aliyetembelea banda la kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga
Wananchi wakipata elimu katika Banda la VETA aliyetembelea banda la kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Korogwe Mkondo wa Amali Katika Fani ya Upishi wakiwa na Bidhaa zao walizitengeneza katika Banda la TEA kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano Bi.Julitha Mlay akizungumza na mwananchi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano Bi.Julitha Mlay akizungumza na Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Usagara  wakati walipotembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano wa Tume ya Taifa ya Unesco  Bi.Julitha Mlay akiwaonesha namna ya  fursa za Tume hiyo kwa Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Usagara  wakati walipotembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano wa Tume ya Taifa ya Unesco  Bi.Julitha Mlay akiwa katika picha  ya pamoja na  Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Usagara  wakati walipotembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano  Bi.Julitha Mlay akizungumza na mwananchi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimkabidhi Tuzo pamoja na Cheti, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Deogratius Kwiyukwa, kama Ishara ya kutambua mchango wa benki hiyo katika kushiriki kukuza na kuchochea shughuli za uchuki jumuishi na shukrani kwa ushiriki na kuwa tayari kuchochea maono ya Taifa ya kumkomboa mwananchi kwa kumtengenezea mazingira bora ya uwajibikaji kwa Taifa lake, katika Kilele cha Tamasha la Kizimkazi 2026, lililohitimishwa mwishoni wa Juma lililopita.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha, Kizimkazi, Zanzibar)

Na Benny Mwaipaja, Kizimkazi-Zanzibar
SAFARI ya mageuzi ya kiuchumi kuelekea Dira ya Taifa 2050 imeanza kushika kasi, huku mijadala kuhusu vichocheo vya uchumi ikiendelea kupewa uzito mkubwa nchini.

Miongoni mwa matukio yaliyoibua mjadala huo ni Tamasha la Kizimkazi 2026, lililofanyika kusini mwa Unguja na kukutanisha viongozi wakuu wa serikali, taasisi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Tamasha hilo lilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel John Nchimbi, pamoja na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, sambamba na viongozi wengine wa serikali akiwemo Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), vyama vya siasa, taasisi za umma na binafsi, pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Mbali na kuwa jukwaa la kukutanisha wadau, tamasha hilo pia lilikuwa sehemu muhimu ya mdahalo wa kitaifa kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, ambapo viongozi waandamizi walitoa maoni yao kuhusu umuhimu wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi kama sehemu ya maendeleo endelevu ya taifa.

Ajenda ya nishati safi inaenda sambamba na nguzo ya uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, ambayo ni sehemu ya msingi ya Dira 2050.

Kupitia nguzo hiyo, Tanzania inalenga kuwa kinara wa kimataifa katika uhifadhi wa mazingira kwa kusimamia matumizi endelevu ya rasilimali za asili na kuimarisha uwezo wa taifa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Miongoni mwa taasisi zilizojitokeza kwa nguvu katika tamasha hilo ni Benki ya Maendeleo TIB, iliyoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Deogratius Kwiyukwa. TIB ni benki ya maendeleo ya Serikali iliyoanzishwa mahsusi kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini kupitia utafutaji wa mitaji, uandaaji wa miradi ili iweze kuvutia uwekezaji, pamoja na usimamizi wa mifuko ya maendeleo kwa niaba ya serikali na sekta binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari kando ya tamasha hilo, Bw. Kwiyukwa alisema
Benki ya Maendeleo ya Tanzania TIB, imejipanga kuongeza ufadhili wa miradi ya nishati safi nchini, kama sehemu ya jitihada za Taifa za kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Amesema benki hiyo imetenga fedha maalum za kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa miradi ya nishati mbadala ikiwemo ya jua, upepo, gesi asilia na nishati ya maji.

“Tunafahamu kuwa nishati safi ndio mkombozi wa viwanda, kilimo na nyumba za Watanzania. Kupitia ufadhili huu tunalenga kupunguza utegemezi wa nishati chafu na kuchochea uchumi wa kijani,” amesema Bw. Kwiyukwa.

Kwa mujibu wa TIB, hatua hii pia inalenga kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kushiriki katika miradi mikubwa ya miundombinu ya nishati, ambayo itasaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ajira kwa vijana.

“Benki ya Maendeleo ya TIB imekuwa na mchango mkubwa hapa nchini katika kuleta mabadiliko chanya katika ukuaji wa sekta mbalimbali. Kupitia tamasha hili la Kizimkazi, tunaungana na Mheshimiwa Rais na wadau wengine kupambanua na kuonesha mchango wa sekta zote kufikia malengo ya Dira,” alisema.

Alieleza kuwa benki hiyo imejikita katika sekta mbalimbali muhimu ikiwemo miundombinu, nishati, utalii, uchumi wa buluu, vijana na wanawake, pamoja na utunzaji wa mazingira.

Kwa mujibu wa Bw. Kwiyukwa, TIB pia inasimamia mifuko mbalimbali ya maendeleo kwa niaba ya serikali na taasisi nyingine, ikiwemo mifuko ya maji, umeme vijijini, na nishati safi, katika Tanzania Bara na Zanzibar.

Alisema dhamira kuu ni kufikisha maendeleo kwa wananchi na kupunguza vihatarishi katika maeneo ambayo benki za biashara hushindwa kuyafikia.

Katika hatua nyingine, TIB kupitia kampuni yake tanzu ya TIB Rasilimali, imeendelea kufungua njia mbadala za upatikanaji na ukuzaji wa mitaji. Kampuni hiyo ni miongoni mwa mawakala wakubwa wa soko la hisa la Dar es Salaam, ikiwa na jukumu la kuuza na kununua hisa kwa niaba ya taasisi na watu binafsi. Pia hutoa huduma za elimu ya fedha, uwekezaji, pamoja na uwakala wa bima.

Bw. Kwiyukwa alisema kupitia TIB Rasilimali, taasisi na wananchi wamekuwa wakihamasishwa kutambua njia mbadala za kukuza mitaji yao bila kutegemea fedha za Serikali pekee.

Alibainisha kuwa Ofisi za Dar es Salaam na majukwaa ya mitandaoni zimekuwa zikiendesha madarasa maalumu ya kila wiki, hasa kwa vijana, ili kuwapa uelewa kuhusu njia salama na za uhakika za uwekezaji.

“Jitihada hizo zinaunga mkono malengo makubwa ya Dira 2050, yanayolenga kujenga uchumi wa thamani ya dola trilioni moja, kuongeza wastani wa kipato cha Mtanzania hadi dola 7,000 kwa mwaka, pamoja na kuhakikisha sekta binafsi inachangia kwa kiwango kikubwa zaidi katika ukuaji wa uchumi wa Taifa” alisema Bw. Kwiyukwa.

Sambamba na ushiriki wake katika tamasha hilo, Benki ya Maendeleo TIB pia ilitunukiwa tuzo na cheti kutoka kwa Mheshimiwa Rais kama ishara ya kutambua mchango wake na utayari wake wa kuchochea maono ya Taifa ya kumkomboa mwananchi kiuchumi kupitia maendeleo jumuishi.

Akihitimisha, Bw. Kwiyukwa aliipongeza Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuandaa Tamasha la Kizimkazi, akieleza kuwa limefungua fursa pana kwa Watanzania kujadili masuala muhimu ya maendeleo. Pia aliahidi kuwa TIB itaendelea kushiriki katika matamasha na majukwaa mengine yenye lengo la kuchochea maendeleo ya Taifa.

Sambamba na hayo, katika Tamasha hilo la Kizimkazi 2026, Benki ya Maendeleo TIB ilitunikiwa tuzo pamoja na cheti na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama Ishara ya kutambua mchango wa benki hiyo katika kushiriki kukuza na kuchochea shughuli za uchuki jumuishi na shukrani kwa ushiriki na kuwa tayari kuchochea maono ya Taifa ya kumkomboa mwananchi kwa kumtengenezea mazingira bora ya uwajibikaji kwa taifa lake.

Kwa ujumla, ushiriki wa TIB katika Tamasha la Kizimkazi 2026 umeonesha wazi nafasi ya taasisi za maendeleo katika kusukuma mbele ajenda ya nishati safi, uhifadhi wa mazingira na uwezeshaji wa kiuchumi, yote ikiwa ni sehemu ya safari ya Tanzania kuelekea Dira 2050.

Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Mb), Ridhiwani Kikwete, amezitaka shule za msingi na sekondari kuwa na karakana zitakazokuwa chemchemi za ubunifu kwa vijana, huku akisisitiza kazi zitakazobuniwa zisajiliwe ili wabunifu wanufaike nazo.

Ridhiwani amesema usajili huo utawasaidia vijana kumiliki kazi zao na kuzitumia kama fursa za kiuchumi, badala ya watu wengine kuchukua mawazo yao na kujinufaisha huku wabunifu wakibaki bila manufaa.

Amesema hayo akimwakilisha Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Baobab, iliyopo Mapinga, Bagamoyo mkoani Pwani.

Mkurugenzi wa Baobab, Shani Swai, amesema kwa sasa shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 1,000 na tangu mwaka 2007 hadi 2026, jumla ya wanafunzi wa 4,495 wa kidato cha sita wamehitimu, huku asilimia 98 wakiendelea na elimu ya vyuo vikuu ndani na nje ya nchi na wanafunzi 3,270 wamehitimu kidato cha nne ambapo asilimia 95 wameendelea na sekondari na vyuo vya ufundi. 

Naye Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amewataka Watanzania kushikamana katika kuwalinda .

Makamu wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (wa tatu kushoto), akiongoza washiriki wa Mashindano ya CRDB Bank International Marathon leo katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam. Kijitonyama, Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam. Mashindano ya CRDB Bank International Marathon yamegeuka kutoka kuwa tukio la michezo na kuwa mpango mkubwa wa kuleta athari chanya katika jamii, baada ya kukusanya zaidi ya Sh5 bilioni tangu yalipoanzishwa mwaka 2020, fedha ambazo zimeelekezwa katika kuboresha huduma za afya, kuwawezesha vijana na maendeleo ya jamii nchini Tanzania.

Athari hizo zilibainika. wakati toleo la saba la marathon hiyo lilipohitimishwa katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam, likiwakutanisha washiriki takribani 17,000 chini ya kaulimbiu “Kasi Isambazayo Tabasamu.”
Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la CRDB Bank, Dk Abdulmajid Nsekela, alisema fedha zilizopatikana kupitia marathon hiyo zimeleta msaada unaoonekana kwa makundi yenye uhitaji, hususan watoto wenye matatizo ya moyo na wanawake wenye mimba hatarishi.

Alisema zaidi ya watoto 400 wenye matatizo ya moyo wamefanyiwa upasuaji, huku zaidi ya wanawake 240 wenye mimba hatarishi wakipatiwa huduma za afya na kujifungua salama.

“Kila mchango unawakilisha mtoto aliyepewa nafasi nyingine ya kuishi, mama aliyepata huduma salama zaidi wakati wa kujifungua na familia ambazo maisha yao yamebadilika,” alisema Dk Nsekela.
Athari katika sekta ya afya pia imepanuliwa kupitia ushirikiano na taasisi mbalimbali. Zaidi ya watoto 1,000 wamepatiwa matibabu ya moyo kupitia msaada uliowasilishwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), huku wanawake zaidi ya 450 wenye mimba hatarishi wakinufaika kupitia CCBRT.

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road nayo imenufaika kupitia ujenzi wa kituo cha huduma kwa wateja kwa njia ya simu, hatua iliyosaidia kuboresha upatikanaji wa msaada kwa wagonjwa wa saratani.

Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu Dk Mwigulu Lameck Nchemba, Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, alisema marathon hiyo imevuka mipaka ya michezo na kuwa harakati ya kitaifa inayochangia afya, ustawi wa jamii, uwezeshaji vijana na maendeleo ya kiuchumi.

“CRDB Bank International Marathon imevuka kuwa tukio la michezo na kuwa harakati ya kitaifa inayochangia afya, ustawi wa jamii, uwezeshaji vijana na maendeleo ya kiuchumi, alisema Abdulla.

Alisema mpango huo unaonyesha umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wananchi katika kukabiliana na changamoto za kijamii.

Abdulla aliipongeza CRDB Bank Foundation kwa kutumia michezo kukusanya rasilimali kwa ajili ya shughuli za kijamii, huku ikiendelea kupanua programu zake za vijana katika ujasiriamali, ubunifu, mazingira na maendeleo ya vipaji.

Kupitia programu zake kwa ujumla, taasisi hiyo inasema imewafikia zaidi ya wajasiriamali milioni tatu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kutoa zaidi ya Sh30 bilioni kama mtaji wa kuwawezesha.
Hatua hizo ni pamoja na zaidi ya Sh4.2 bilioni zilizotolewa kupitia mpango wa mikopo wa asilimia 10 wa halmashauri katika awamu yake ya kwanza kwa halmashauri tano, huku zaidi ya Sh3.5 bilioni zikitolewa kwa vijana kupitia changamoto ya Vijana Uchumi.

Mfuko wa Samia Commercialization Fund, unaotekelezwa kwa ushirikiano na COSTECH, pia umepokea Sh4.6 bilioni kusaidia vijana wabunifu kubadili mawazo yao kuwa biashara zinazoweza kujiendesha.

Aidha, Sh8 bilioni zimetengwa kupitia SIDO na TIRDO kwa ajili ya elimu ya fedha, mafunzo ya ujasiriamali, maendeleo ya biashara, huduma za ushauri wa kitaalamu na mtaji.

Sh5 bilioni nyingine zimetengwa kupitia programu za Go Green na IMBEJU kuwawezesha vijana na wanawake wanaoendesha biashara zinazozingatia mazingira, huku zaidi ya wanufaika 1,000 tayari wakiwa wamechaguliwa.
Abdulla alisema programu kama FursaHub, Imbeju UDSM Start-Up Challenge, Imbeju Ndondo Cup na Imbeju Zuchu MasterClass zimeendelea kupanua fursa kwa vijana wa Tanzania.

Pia aliipongeza taasisi hiyo kwa kuunganisha marathon na tamasha la IMBEJU Sauti Moja Concert, lililofanyika Dar es Salaam Ijumaa na kuvutia zaidi ya watu 15,000.

Tamasha hilo lilishirikisha wasanii wa kimataifa akiwemo mwimbaji wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, msanii wa Nigeria BNXN na DJ wa Afrika Kusini Kabza De Small, pamoja na wasanii wa Tanzania. Sehemu ya mapato ya tamasha hilo itaelekezwa katika kuwawezesha vijana, hususan katika sekta ya ubunifu.

Abdulla alisema mchanganyiko wa michezo na burudani unaweza kusaidia Tanzania kujenga kalenda pana ya matukio makubwa, huku ukitengeneza ajira, kukuza utalii na kuzalisha fursa za uwekezaji.
Alisema michezo si burudani pekee bali ni sehemu muhimu ya uchumi, akitaja maandalizi ya Tanzania kuandaa kwa pamoja Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 na Kenya na Uganda.

Pia alisisitiza umuhimu wa Imbeju Ndondo Cup katika kugundua na kukuza vipaji vya soka, akiwataka waandaaji kuendelea kulinda dhima yake ya msingi katika ngazi za chini huku wakiimarisha mifumo ya maendeleo ya vipaji.

Abdulla alisema Serikali imetenga Sh519.6 bilioni kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika mwaka wa fedha 2026/27, huku vipaumbele vikijumuisha miundombinu ya michezo, maandalizi ya AFCON 2027, maendeleo ya vipaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi.
Aliwahakikishia wadau wa sekta binafsi kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili Watanzania wanufaike na fursa zilizopo katika michezo na sekta ya ubunifu.

Kwa zaidi ya Sh5 bilioni zilizokusanywa kupitia marathon hiyo na programu nyingine za CRDB Foundation zinazohusisha mabilioni ya shilingi, tukio hilo linazidi kuwa nyenzo ya kubadili ushiriki katika michezo kuwa matokeo yanayopimika katika jamii na uchumi.

Abdulla aliwapongeza viongozi wa CRDB Bank, akiwemo Mwenyekiti wa Bodi Prof Neema Mori, Dk Nsekela, Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank Foundation CPA (T) Oswald Urassa na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation, Tully Esther Mwambapa, kwa mchango wao katika maendeleo ya taifa.

Wakenya watawala CRDB Marathon

Wanariadha kutoka Kenya walitawala CRDB Marathon 2026 baada ya kushinda nafasi nyingi za juu katika mashindano makuu.

Katika mbio za kilomita 42 kwa wanaume, Abraham Kiptum alishika nafasi ya kwanza kwa muda wa saa 2:15:33, akifuatiwa na Mkenya mwenzake James Mwangi aliyemaliza kwa saa 2:16:11. Mtanzania Marco Sylvester alishika nafasi ya tatu kwa saa 2:16:33.

Kwa upande wa wanawake katika kilomita 42, Joyce Kemuma alishinda kwa saa 2:35:26, huku Mkenya Jacinta Chepkoech akimaliza wa pili kwa saa 2:36:57 na Mkenya mwingine Jane Chelagant akishika nafasi ya tatu kwa saa 2:39:18.
Washindi wa kilomita 42 kwa wanaume na wanawake walipata Sh12 milioni kila mmoja, washindi wa pili Sh5 milioni na waliomaliza nafasi ya tatu Sh2 milioni.

Katika nusu marathon, Mkenya Simon Kelenzyoki alishinda mbio za wanaume kwa saa 1:15:33, akifuatiwa na Mtanzania Ebei Francis aliyemaliza kwa saa 1:15:52, huku Mtanzania mwingine Boay Dawi akiwa wa tatu kwa saa 1:16:07.

Kwa wanawake, Mkenya Rebecca Chepkwemoi alishinda nusu marathon kwa saa 1:12:42, akifuatiwa na Mtanzania Failuna Matanga aliyemaliza kwa saa 1:13:21 na Mkenya Irine Mkungu aliyeshika nafasi ya tatu kwa saa 1:13:23.
Washindi wa nusu marathon walipata Sh6 milioni, washindi wa pili Sh2 milioni na waliomaliza nafasi ya tatu Sh1 milioni.

Wanariadha wa Tanzania walitawala mbio za kilomita 10 kwa wanaume, huku Jumanne Ngoya akishinda kwa muda wa dakika 29:53. Benard Geay alimaliza wa pili kwa dakika 29:58, huku Shedrack Hasani akiwa wa tatu kwa dakika 30:06.

Tanzania pia ilitwaa nafasi zote tatu za juu katika mbio za wanawake za kilomita 10, ambapo Transfora Mussa alishinda kwa dakika 34:00, Anna Dolomongo akimaliza wa pili kwa dakika 34:18 na Agnes Mwanghui akiwa wa tatu kwa dakika 34:45.

Washindi wa kilomita 10 walipata Sh2 milioni, washindi wa pili Sh500,000 na waliomaliza nafasi ya tatu Sh300,000.














Top News