

.jpeg)


AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw.Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika uwanja wa Nyamhongolo Jijini Mwanza Agosi 2,2026
Dodoma, Agosti 2, 2026
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unashiriki katika Maonesho ya Nanenane 2026 kwa kutoa huduma mbalimbali na elimu kuhusu Hifadhi ya Jamii kwa wanachama wake na wananchi kupitia mabanda yake yaliyopo katika kanda tano nchini, ikiwemo Zanzibar.

Msanii maarufu nchini ,Mrisho Mpoto (wa pili kushoto) akiwa ameshika mkanda ,moja ya bidhaa zinazozalishwa katika kiwanda cha KLICL,Kinachomilikiwa na PSSSF kwa ushirikiano na Jeshi la Magereza ,alipotembelea Banda la Mfuko wa PSSSF kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026,kushoto ni Afisa Mkuu wa Uhusiano wa Mfuko wa PSSSF Bw.Abdul Njaidi na kulia ni Afisa Mauzo kiwanda cha KLICL ,Bi,Mary Muna
Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko wa PSSSF, Bw. Abdul Njaidi, PSSSF imeshiriki maonesho hayo katika Kanda ya Kati viwanja vya Nanenane mkoani Dodoma, ambako Maonesho ya Nanenane 2026 yanafanyika kitaifa na tayari yamezinduliwa na Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Agosti 1, 2026. Kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘Tambua Soko; Ongeza Tija na Thamani ya Kuelekea Dira 2025’.

Wanachama wa Mfuko wa PSSSF wakihudumiwa kwenye Banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti2,2026
Katika maonesho ya mwaka huu, PSSSF inashiriki; Zanzibar katika viwanja vya Dole, Kanda ya Magharibi mkoani Tabora katika viwanja vya Ipuli Mnadani, Kanda ya Ziwa jijini Mwanza katika viwanja vya Nyamhungolo, Kanda ya Kusini mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini jijini Mbeya, viwanja vya Nanenane.

Afisa Matekelezo wa Mfuko wa PSSSF Bi.Esther Mpemba (kulia ) akimuunganisha Mwanachama wa PSSSF ,Bi.Maliasa Sajoho na Mfumo wa PSSSF Member Portal ambao unamuwezesha kupata huduma za mfuko Kidijitali,kwenye maonesho ya Nanenane Viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026
"Tunawakaribisha wanachama wetu na wananchi wote kutembelea mabanda ya PSSSF katika kanda hizo ili kupata huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu kuhusu mafao, kuhakiki taarifa zao na michango, pamoja na kuwaunganisha katika huduma zetu za kidijitali, huku tukiwahakikisha kesho ya uhakika wanachama wetu’" alisema Bw. Njaidi

Afisa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa PSSSF ,Bi .Saluna Ally (kushoto) akimuhudumia Mstaafu anayepokea Pensheni PSSSF ,Bw.Mwakibete G.Kasilati,kwenye banda la mfuko huu katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwenye viwanja vya Nanenane Jijini Mbeya,Agosti 2,2026
Aidha, watakaotembelea kwenye mabanda ya PSSSF watapata nafasi ya kuona fursa za uwekezaji wa Mfuko ambazo ni pamoja na bidhaa za ngozi zinazotengenezwa na Kiwanda cha KLICL na nyama kutoka machinjio ya Kimataifa ya Nguru.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba akitoa hotuba ya ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa katika viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 1,2026

Meneja wa PSSSF Kanda ya Magharibi Bw.Eliadi Mndeme akitoa elimu kwa mwanachama wa PSSSF wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi ambayo yanafanyika viwanja vya Ipuli mkoani Tabora Agosti 2,2026

.png)
Meneja wa EWURA Kanda ya Magaharibi, Mha. Karim Ally(kushoto) akitoa maelezo ya majukumu yanayotekelezwa na Mamlaka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua(kulia) ikiwemo utoaji wa leseni na vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta, vituo vya CNG, utatuzi wa migogoro na malalamiko na nafasi ya EWURA katika kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi ( LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, wakati kuongozi huyo alipotembelea banda la EWURA katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo 02/08/2026.
Na.Mwandishi Wetu-Tabora
Wakuu wa Wilaya za Tabora, Mh. Upendo Wella, na Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua, wameipongeza EWURA kwa usimamizi mzuri wa huduma za nishati na maji nchini. Wametoa pongezi hizo walipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo, 02.08.2026.
Viongozi hao wameitaka EWURA kuongeza hamasa kwa wananchi ili kubadili mtazamo na kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia ili azma ya kufikia 80% ya watumiaji ifikapo 2034 itimie.
Aidha, wameisisitiza EWURA kuendelea kuhamasisha uwekezaji wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini, wakieleza kuwa huduma hiyo inahitajika kutokana na kushamiri shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi.
Meneja wa EWURA Kanda ya Magharibi, Mha. Karim Ally, alitumia fursa hiyo kueleza nafasi ya EWURA ya kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi (LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, ambapo kwa sasa ni 19 pekee.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magaharibi, Mha. Karim Ally(kushoto) akitoa maelezo ya majukumu yanayotekelezwa na Mamlaka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua(kulia) ikiwemo utoaji wa leseni na vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta, vituo vya CNG, utatuzi wa migogoro na malalamiko na nafasi ya EWURA katika kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi ( LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, wakati kuongozi huyo alipotembelea banda la EWURA katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo 02/08/2026.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magahribi, Mha. Karim Ally(kulia) akimweleza Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mh. Upendo Wella (kushoto), Mamlaka inavyoendelea kutoa elimu na kuhamasisha ujenzi wa vituo maeneo ya vijijini ambapo uhitaji bado ni mkubwa hususan katika maeneo ya pembezoni na hivyo kuendelea kuwepo uuzaji holela wa bidhaa za petroli, ambao ni hatari kwa afya, mazingira na maisha ya watu, wakati kiongozi huyo alipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya NaneNane, viwanja vya Ipuli, Tabora, leo, 02/08/2026.
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Needpeace Wambuya, amepongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), hususan hatua ya kuanzisha mpango wa kuuza mifugo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.
Akizungumza alipotembelea banda la WRRB katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea viwanja vya John Malecela jijini Dodoma leo Agosti 2, 2026, Wambuya amesema "Niwapongeze sana, kwa kazi nzuri mnayofanya, nimeona mpango wenu kuingiza mifugo kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, natumai mpo hatua nzuri kwasasa."
Kwa upande wake, Ofisa Leseni wa WRRB, Nasri Khea, amesema maandalizi ya mnada wa kwanza wa mifugo kupitia Mfumo huu yamefikia hatua za mwisho, huku mnada huo ukitarajiwa kufanyika hivi karibuni katika Wilaya ya Mvomero.
Amesema pia mfumo huo unakwenda kuingiza kuwezesha biashara za bidhaa mbalimbali ikiwamo Mwani na mahindi.

MKUU wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha,Prof. Epaphra Manamba,akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 2,2026 kwenye banda la chuo hicho akimwakilisha Mkuu wa Chuo, Profesa Eliamani Sedoyeka,wakati wa Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela Nzuguni jijini Dodoma kwa niaba ya
.....
MKUU wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha,Prof. Epaphra Manamba,amesema wanaendelea kuandaa wataalamu wenye ujuzi na uwezo wa kutumia teknolojia za kisasa katika uzalishaji, usimamizi na biashara ya mazao, hatua itakayochangia kuongeza tija, ushindani na thamani ya sekta ya kilimo nchini.
Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt.John Malecela Nzunguni jijini Dodoma, Mkuu wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Prof.Epaphra Manamba, akimwakilisha Mkuu wa Chuo, Profesa Eliamani Sedoyeka, amesema IAA imeamua kushiriki maonesho hayo ili kuwa karibu na wakulima, kutoa elimu na kuonesha mchango wa taaluma katika kuimarisha uzalishaji wa kilimo nchini.
Amesema sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania kwa kuwa inategemewa na takribani asilimia 65 ya nguvu kazi ya Taifa, lakini bado mchango wake katika Pato la Taifa ni takribani asilimia 26 pekee, hali inayoonesha kuwa kuna nafasi kubwa ya kuongeza tija kupitia matumizi ya maarifa, teknolojia na usimamizi bora wa biashara.
"Kilimo kinahitaji nguvu kazi yenye ujuzi, ubunifu na maarifa ya kisasa. Ndiyo maana Chuo cha Uhasibu Arusha kinaendelea kutoa programu mbalimbali za biashara, uchumi, fedha na teknolojia ili kuwajengea uwezo wataalamu watakaosaidia kuifanya sekta ya kilimo iwe yenye ushindani na yenye mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa," amesema Prof.Manamba.
Ameeleza kuwa pamoja na changamoto za mitaji zinazowakabili wakulima wengi pamoja na utegemezi wa zana duni za kilimo, bado kuna fursa kubwa ya kuongeza uzalishaji endapo wakulima wataunganishwa na taasisi za kifedha pamoja na huduma za kitaalamu zitakazowezesha upatikanaji wa mitaji na uwekezaji katika teknolojia za kisasa.
Prof.Manamba amesema IAA imejikita pia katika kufundisha teknolojia zinazoibukia ikiwemo Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), ambapo wanafunzi wa chuo hicho tayari wamebuni mifumo inayotumia AI kuboresha uzalishaji wa mazao kama vitunguu kwa lengo la kuongeza tija, kupunguza gharama za uzalishaji na kuifanya kilimo kuwa biashara yenye faida zaidi.
"Hatutaki kuona kilimo kinabaki kwa ajili ya kujikimu pekee. Tunataka wakulima walime kwa mtazamo wa biashara, waongeze thamani ya mazao yao na kuongeza kipato cha familia zao pamoja na kuchangia zaidi katika uchumi wa Taifa," amsisitiza.
Akizungumzia kaulimbiu ya Nanenane ya mwaka huu isemayo "Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya Taifa 2050," Prof.Epaphra Manamba amesema dira hiyo inalenga kujenga nguvu kazi yenye ujuzi na maarifa inayoweza kuleta mapinduzi katika sekta mbalimbali za uchumi, hususan kilimo.
Amebainisha kuwa taasisi za elimu zina jukumu la kuhakikisha zinatoa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na mabadiliko ya teknolojia ili kuongeza ufanisi katika uzalishaji na kuifanya Tanzania kufikia malengo ya maendeleo ya Dira ya Taifa 2050.
Amesema kupitia ushiriki wa Maonesho ya Nanenane, Chuo cha Uhasibu Arusha kinaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu programu zake mbalimbali na namna zinavyoweza kuwaandaa vijana kuwa wataalamu watakaochangia maendeleo ya kilimo, biashara na uchumi wa kidijitali nchini.






.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)







.jpeg)