WAKULIMA wakubwa, wa kati na wadogo nchini wanatarajiwa kupata fursa zaidi ya kutumia teknolojia ya ndege nyuki katika shughuli za kilimo, ikiwemo kunyunyiza viuatilifu na kufuatilia afya ya mazao.
Hatua hiyo inakuja baada ya kampuni ya Mati Technologies Company Ltd na Mazao Hub kusaini hati ya makubaliano ya ushirikiano (MOU), kwa lengo la kuwawezesha wakulima, hususan wakulima wadogo, kupata huduma za teknolojia hiyo inayozalishwa nchini.
Akizungumza baada ya kusainiwa kwa MOU hiyo, Mkurugenzi wa Mati Technologies, Benjamin Mollel, amesema kampuni hiyo imekuwa ikishirikiana na majukwaa mbalimbali ya wakulima ili kupanua upatikanaji wa huduma za ndege nyuki na kuongeza tija katika kilimo.
Amesema Mazao Hub ni miongoni mwa majukwaa yanayowafikia wakulima wengi kupitia huduma zake za ugani na mfumo wa usambazaji wa pembejeo za kilimo, hivyo ushirikiano huo utasaidia kuunganisha wakulima na teknolojia kwa urahisi zaidi.
Mollel amesema lengo ni kuwafikia zaidi ya wakulima laki moja kote nchini ifikapo mwaka 2027, huku teknolojia hiyo ikilenga kusaidia wakulima kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuongeza uzalishaji.
Kwa upande wake afisa mahusiano wa Mazao Hub Alexandra Ngaiza, amesema matumizi ya ndege nyuki katika kilimo yamekuwa yakihusishwa zaidi na wakulima wenye mashamba makubwa, lakini ushirikiano huo unalenga kubadilisha hali hiyo kwa kuwapa wakulima wadogo fursa ya kutumia teknolojia hiyo kupitia mifumo rahisi ya upatikanaji huduma ya Ndege nyuki hizo zinazozalishwa nchini.
Amesema teknolojia hiyo inaweza kusaidia kuongeza ufanisi katika unyunyiziaji wa viuatilifu, kuboresha uzalishaji na kupunguza uwezekano wa wakulima kukumbana moja kwa moja na kemikali wakati wa kunyunyizia mazao kwa njia za kawaida.
Mazao Hub, ambayo ni kampuni ya teknolojia ya kilimo (Agri-Tech), ambayo hutoa huduma za ugani kwa wakulima pamoja na kuwa na mfumo wa kuwaunganisha wakulima na pembejeo muhimu za kilimo, jambo linalowezesha teknolojia hiyo ya ndege nyuki zinazozalishwa nchini na Mati Technologies company ltd kuwafikia wakulima kupitia mtandao uliopo.
Lengo kubwa la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watoa huduma wa kujitolea na askari wa zimamoto ili wawe tayari kutoa msaada wa haraka wakati wowote na mahala popote. Hii ni maandalizi ya kukabiliana na athari za mvua kubwa za El-Nino zinazotabiriwa kuanza Oktoba 2026.
Akizungumza baada ya mafunzo hayo, Red Cross Mkoa wa Simiyu ilisema imechukua jukumu la kuhakikisha jamii inakuwa tayari kukabiliana na majanga. Taasisi hiyo imesisitiza kuwa itaendelea kuimarisha utamaduni wa kujitolea kwa kuzingatia Kanuni Saba za Kimataifa za Red Cross ambazo ni Ubinadamu, Uadilifu, Kutokupendelea, Uhuru, Kujitolea, Umoja na Ulimwengu.
Katika mafunzo hayo ya pamoja, washiriki walipata elimu ya jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa majeruhi, kuzuia damu, kutoa huduma kwa waliopata majeraha madogo na makubwa, pamoja na namna ya kuwasili katika tukio haraka na kwa usalama.
Watoa mafunzo walikuwa ni Hamis Shaban Mrisho, Barnabas Charles Daud, Aziz Abeod na Isaya Mganule. Walitoa masomo mbalimbali kwa vitendo na kinadharia ili kuhakikisha kila mshiriki anaelewa na anaweza kutekeleza.
Mafunzo haya yanakuja wakati Serikali ikitangaza kuwa mvua za El-Nino zinatarajiwa kuanza mwezi Oktoba na kuleta athari katika baadhi ya mikoa ikiwemo Simiyu. Hivyo ushirikiano kati ya Red Cross na Jeshi la Zimamoto unalenga kuhakikisha hakuna upotevu wa maisha utakaotokea wakati wa majanga hayo.
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
Serikali imesema udanganyifu katika mitihani ya kitaifa umepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kuimarishwa kwa usimamizi wa mitihani nchini.
Kauli hiyo imetolewa Septemba 7, 2026 mkoani Ruvuma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Prof. Carolyne Nombo, alipofika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na kuazungumzia utekelezaji wa masuala mbalimbali ya elimu ikiwemo maandalizi ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba unaotrajia kufanyika nchini kote Septemba 9 na 10, 2026.
Ameeleza kuwa mitihani ya kitaifa ni suala nyeti linalohitaji usimamizi madhubuti, hivyo viongozi wa elimu katika ngazi zote wanapaswa kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinafuatwa.
“Udanganyifu umepungua kwa kiasi kikubwa, nawasihi wanafunzi wa darasa la saba manaotarajia kufanya mitihani yenu kutojiingiza katika udanganyifu wowote wa mitihani, tuzingatie taratibu zote za mitihani,” amesisitiza Prof. Nombo
Aidha, amezitaka kamati za mitihani za mikoa na viongozi wa elimu kuendelea kushirikiana katika kusimamia mitihani, huku akiwapongeza kwa hatua ambazo tayari zimechukuliwa katika kupunguza udanganyifu.
Amebainisha kuwa, Serikali itaendelea kuchukua hatua pale inapobaini vitendo vya udanganyifu, hasa vile vinavyohusisha kupanga kwa pamoja kati ya wanafunzi, walimu au wasimamizi wa mitihani.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Songea Mhe. Wilman Kapenjama amesema mkoa umejiandaa vema katika kusimamia mtihani huo kwa hali ya usalama bila changamoto yoyote.

Vyama vya siasa nchini vimetakiwa kutumia majukwaa yao kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote, kwa kuwa afya ni haki ya kila mwananchi bila kujali itikadi, umri, jinsia au nafasi yake katika jamii.
Wito huo umetolewa na Kaimu Waziri wa Afya Dkt. Saada Mkuya Salum na Mbunge wa Welezo, wakati wa semina iliyowakutanisha wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa na wataalamu kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa ajili ya kuwajengea uelewa kuhusu Bima ya Afya kwa Wote.
Dkt. Mkuya alisema wanasiasa wana mtandao mpana wa kuwafikia wananchi kuanzia ngazi ya jamii hadi taifa, hivyo wana nafasi muhimu ya kuwa mabalozi wa elimu kuhusu afya na bima ya afya.
Alisema ushiriki wa vyama vya siasa katika kutoa elimu hiyo unaweza kusaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya na namna inavyoweza kusaidia kulinda afya na ustawi wa familia.
“Bima ya afya inalinda mwananchi na familia dhidi ya gharama kubwa za matibabu. Hili si suala la chama cha siasa, bali ni suala la maisha na ustawi wa wananchi,” alisema Dkt. Mkuya.
Aliongeza kuwa wanasiasa wanapokutana na wananchi katika maeneo mbalimbali, ikiwemo mikutano ya hadhara na majukwaa mengine, wanaweza kutumia fursa hizo kutoa elimu sahihi kuhusu umuhimu wa bima ya afya.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Juma Ally Khatib, alisema elimu iliyotolewa katika semina hiyo itawafikia viongozi wa vyama vya siasa kuanzia ngazi ya taifa, mikoa, wilaya na kata, pamoja na wanachama wao.
Alisema viongozi hao watakuwa na jukumu la kuifikisha elimu hiyo kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini, ili kuongeza uelewa na ushiriki katika mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
“Tunachojifunza hapa hakitaishia kwa wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa. Tutakwenda kuwaelimisha viongozi wetu wa kitaifa, mikoa, wilaya, kata na wanachama, ambao nao wataifikisha elimu hii kwa wananchi,” alisema Khatib.
Naye Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mohamed Ahmed, alisema semina hiyo inalenga kuwawezesha viongozi na wawakilishi wa vyama vya siasa kupata uelewa sahihi kuhusu mifumo ya bima ya afya nchini, ili waweze kutoa elimu sahihi kwa wananchi.
Alisema uelewa wa viongozi wa kisiasa ni muhimu kwa kuwa wana nafasi kubwa ya kuhamasisha wananchi kushiriki katika mipango mbalimbali ya Serikali inayolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya.
Akizungumza katika semina hiyo, Dkt. David Mwanesano kutoka NHIF, alisema Serikali imeanza kutekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa awamu, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha wananchi wanapata kinga dhidi ya changamoto za gharama za matibabu.
Alisema hadi sasa jumla ya kaya 276,400 zimekwishaandikishwa katika mpango huo na kuanza kupata huduma za afya.
Alisisitiza kuwa ushirikiano wa wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa kisiasa, ni muhimu katika kufanikisha azma ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma za matibabu bila kukabiliwa na mzigo mkubwa wa gharama za matibabu.

Bima ya Afya kwa Wote, Jiunge Sasa
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetangaza kuanza kwa Awamu ya Pili ya udahili wa Shahada ya Kwanza kwa mwaka wa masomo 2026/2027, hatua inayowapa fursa nyingine waombaji ambao hawakuweza kuwasilisha maombi au hawakupata nafasi ya kudahiliwa katika Awamu ya Kwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Katibu Mtendaji wa TCU, Prof. Charles Kihampa, amesema Awamu ya Pili ya udahili imeanza Septemba 8 na itaendelea hadi Septemba 21, 2026, huku akiwataka waombaji kutumia fursa hiyo kutuma maombi katika vyuo na programu wanazozipendelea.
Prof. Kihampa amesema kukamilika kwa Awamu ya Kwanza kumebainisha kuwa jumla ya waombaji 149,645 waliwasilisha maombi ya kujiunga na Shahada ya Kwanza katika vyuo 93 vilivyoidhinishwa kudahili wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/2027, ambapo waombaji 117,334, sawa na asilimia 78.4 ya waombaji wote, wamepata udahili katika vyuo walivyoomba.
Amesema idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka baada ya kukamilika kwa Awamu ya Pili, ambayo imefunguliwa kwa waombaji ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kutuma maombi au hawakupata nafasi katika Awamu ya Kwanza.
Kwa mwaka wa masomo 2026/2027, TCU imeeleza kuwa kuna jumla ya programu 1,019 za Shahada ya Kwanza zinazotolewa na vyuo vilivyoidhinishwa, ikiwa ni ongezeko la programu 125 kutoka programu 894 zilizokuwepo mwaka wa masomo 2025/2026.
Aidha, nafasi za udahili zimeongezeka kutoka 205,652 mwaka uliopita hadi 227,555 mwaka huu, sawa na ongezeko la nafasi 21,903 au asilimia 10.7.
Katika hatua nyingine, waombaji waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja wametakiwa kuhakikisha wanathibitisha udahili wao katika chuo kimojawapo kuanzia Septemba 8 hadi 21, 2026. Uthibitisho huo utafanyika kwa kutumia namba maalum ya siri iliyotumwa kwa waombaji kupitia ujumbe mfupi wa simu au barua pepe walizotumia wakati wa kuomba udahili.
Prof. Kihampa amesema waombaji ambao hawajapokea namba hiyo kwa wakati wanapaswa kuingia katika mifumo ya udahili ya vyuo walivyodahiliwa na kuomba kutumiwa tena ujumbe wenye namba maalum ya siri ili waweze kukamilisha uthibitisho wa udahili.
Tume imesisitiza kuwa uthibitisho wa udahili unatakiwa kufanyika kupitia akaunti ambayo mwombaji alitumia wakati wa kuwasilisha maombi yake, huku orodha ya waombaji waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja ikipatikana kupitia tovuti rasmi ya TCU.
Wakati huo huo, TCU imevielekeza vyuo vya elimu ya juu nchini kutangaza programu ambazo bado zina nafasi za udahili ili kuwawezesha waombaji kupata taarifa sahihi na kutumia fursa hiyo katika Awamu ya Pili. Waombaji na vyuo pia wametakiwa kuzingatia kalenda, miongozo na taratibu za udahili wa Awamu ya Pili zilizowekwa na TCU.
Kwa upande wa waombaji watakaokutana na changamoto katika masuala ya udahili au uthibitisho wa nafasi zao, TCU imewataka kuwasiliana moja kwa moja na vyuo husika, huku vyuo vikielekezwa kupokea taarifa hizo na kutafuta ufumbuzi wa haraka kwa kuzingatia miongozo na taratibu zilizowekwa na Tume.
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza kuwa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) kwa mwaka 2026 utafanyika Septemba 9 na 10, ukihusisha watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 nchini.
Katibu Mtendaji wa NECTA, Prof. Said A. Mohamed, amesema kati ya watahiniwa hao, wavulana ni 531,467 sawa na asilimia 45, huku wasichana wakiwa 637,182 sawa na asilimia 55.
Amesema watahiniwa 1,081,204 sawa na asilimia 93 watafanya mtihani kwa Kiswahili, huku 87,445 sawa na asilimia saba wakifanya kwa lugha ya Kiingereza.
Kwa mujibu wa Prof. Mohamed, watahiniwa wenye mahitaji maalumu 4,867 pia wamesajiliwa kufanya mtihani huo. Kati yao, 82 ni wasioona, 1,591 wenye uoni hafifu, 999 wenye uziwi, 576 wenye ulemavu wa akili na 1,619 wenye ulemavu wa viungo.
Amesema masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, English Language, Sayansi na Teknolojia, Hisabati, Maarifa ya Jamii na Stadi za Kazi, pamoja na Uraia na Maadili.
Prof. Mohamed amesema mtihani huo ni wa mwisho kufanyika kwa kutumia mtaala wa sasa, huku ukilenga kupima maarifa na ujuzi walioupata wanafunzi katika miaka saba ya elimu ya msingi na kutumika katika mchakato wa uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari.
Amesema maandalizi yote ya mtihani huo yamekamilika, yakiwemo usambazaji wa karatasi za mitihani na nyaraka muhimu katika halmashauri zote nchini, mafunzo kwa wasimamizi pamoja na kuweka mikakati ya kuhakikisha usalama wa vituo vya mitihani.
Amewataka wasimamizi wa mitihani kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuzingatia kanuni za mitihani, huku wakihakikisha watahiniwa wote wanapata fursa ya kufanya mtihani kwa muda uliopangwa.
Kwa watahiniwa wenye mahitaji maalumu, amesema NECTA imeweka utaratibu wa kuwapatia maandishi ya nukta nundu kwa wasioona, maandishi yaliyokuzwa kwa wenye uoni hafifu na muda wa ziada wa dakika 20 kwa kila saa katika somo la Hisabati na dakika 10 kwa kila saa kwa masomo mengine.
Aidha, amewataka watahiniwa kuepuka vitendo vya udanganyifu, akisisitiza kuwa matokeo ya mwanafunzi atakayebainika kufanya udanganyifu yatafutwa kwa mujibu wa kanuni.
Amewataka wamiliki na wakuu wa shule kutokuingilia majukumu ya wasimamizi wakati wa mtihani, akionya kuwa NECTA inaweza kufuta kituo cha mtihani endapo itabaini uwepo wake unahatarisha usalama wa mtihani.
Pia ameitaka jamii kutoa ushirikiano kwa kuhakikisha mitihani inafanyika kwa amani na utulivu, ikiwemo kuheshimu maeneo ya mitihani na kuepuka kuingia shuleni wakati wa uendeshaji wa mtihani.
NECTA imetoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za vitendo vya udanganyifu kupitia namba 0759 360 000 au barua pepe esnecta@necta.go.tz.
Mtihani huo utafanyika Jumatano, Septemba 9, na Alhamisi, Septemba 10, 2026.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 08 Septemba 2026, Ikulu Zanzibar, wakati akikabidhiwa Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2025 na Mwenyekiti wa ZEC, Mhe. Jaji George Joseph Kazi.
Amesema Serikali na ZEC zinapaswa kuendelea kushirikiana kutatua changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi huo ili zisijirudie katika chaguzi zijazo.
Aidha, ameipongeza ZEC kwa kuongezeka kwa idadi ya wapiga kura walioandikishwa kutoka 566,352 mwaka 2020 hadi 717,557 mwaka 2025, sawa na ongezeko la asilimia 26.7, pamoja na Serikali kugharamia uchaguzi huo kwa asilimia 100 kwa mara ya kwanza.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa ZEC, Mhe. Jaji George Joseph Kazi, amesema mafanikio mengine ni kuendelea kutumia Tactile Ballot Folder kuwawezesha watu wenye ulemavu wa kuona kupiga kura bila msaada, pamoja na kupatikana kwa jengo la kisasa la One Stop Center na majengo sita ya Afisi za Uchaguzi za Wilaya.
Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi ameishukuru ZEC kwa kazi iliyofanyika na kuwataka viongozi na watendaji wake kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na weledi, huku Serikali ikiendelea kushirikiana na Tume kuimarisha mazingira ya chaguzi zijazo.




























