WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewahimiza watendaji wa Serikali kuwahudumia kikamilifu Watanzania ili miradi inayojengwa na Serikali itoe matokeo chanya.
“Tunachokijenga hapa, si jengo pekee, bali tunajenga mazingira bora ya utendaji wa mfuko. Kupitia uwekezaji huu tunachochea na tunaharakisha utekelezaji wa dhamira ya dhati aliyoionesha Mheshimiwa Rais kumsaidia mkulima mdogo kwa kuwezesha kupata mikopo.”
“Watumishi wote wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa bidii ili uwekezaji huu uwe na manufaa kwa Taifa. Tusiweke ofisi nzuri halafu huduma zikawa duni, tutakua hatujafikia malengo yaliyokusudiwa, ofisi nzuri lakini mwananchi akija kupata huduma anaambiwa njoo kesho, njoo kesho, majengo haya hayatakuwa na maana,” amesema Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili Agosti 2, 2026) Iyumbu jijini Dodoma wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa makao makuu ya ofisi za Mfuko wa Udhamini wa Pembejeo za Kilimo (AGITF).
Dkt. Mwigulu amesisitiza kuwa uwekezaji huo unaofanywa na Serikali katika utafiti wa kilimo ni mwelekeo sahihi wa mageuzi katika sekta ya kilimo. “Kuwekeza kwenye utafiti ni njia sahihi ya kufanya mageuzi katika sekta husika, tumetoka kufanya uzinduzi wa makao makuu ya taasisi yetu ya utafiti wa kilimo, na pembeni yake kuna jengo zuri la maabara ya kilimo, kuonesha jinsi Rais anamaanisha kwa dhati kufanya mageuzi katika kilimo.”
“Kwa nchi nyingine maabara ile ya kisasa ingekuwa kwenye moja ya chuo kikuu, lakini ile ni maabara ya wizara na ipo hapa makao makuu ya nchi,” ameongeza Waziri Mkuu.
Awali akiwa katika mji wa Serikali - Mtumba, kwenye halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi za makao makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), Waziri Mkuu alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendeleza uwekezaji jijini Dodoma hali iliyochochea ukuaji wa mkoa huo.
Dkt. Mwigulu ameongeza kuwa hatua hiyo ya Rais Samia imeenda sambamba na kuwaamini wakandarasi wazawa jambo lililowakuza wakandarasi hao.
“Mheshimiwa Rais aliweka imani kwao, akasema waacheni wajenge. Tumeona majengo na miradi ikimeremeta….nilipita katika miradi ya sekta nyingine, nikakuta madaraja yenye urefu wa ghorofa yamejengwa na wakandarasi wazawa, zaidi ya madaraja 81, sasa ukiangalia kwa jicho la kibinafsi utasema si ni yule mmoja tu ndiyo akapata mradi, lakini niwaambieni huo ni mzunguko wa uchumi wa ndani ya nchi, ndiyo maana mabenki yanapata wateja na yamepunguza mikopo chechefu,” amesisitiza Waziri Mkuu.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha wizara hiyo kupata bajeti ya kutosha kuendesha shughuli zake, ikiwemo kuwaongezea bajeti kila mwaka.



.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)










.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

