Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, Julai 24, akipata maelezo wakati alipotembelea chuo cha Usafirishaji Tanzania (NIT) jijini Dar es Salaam leo Julai 24, 2026.


Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imekitaka Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kuhakikisha kinakamilisha miradi yote ya maendeleo inayoendelea na kuongeza juhudi za kuzalisha wataalamu wenye uwezo wa kufanya kazi ndani na nje ya nchi ili kuunga mkono utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ya usafiri inayotekelezwa nchini.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, Julai 24, wakati alipotembelea chuo hicho kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, kwa lengo la kukagua maendeleo ya miradi na kujionea namna serikali ilivyowekeza katika kuimarisha mafunzo ya sekta ya usafiri.

Kihenzile amesema Serikali inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya usafiri wa anga, barabara, reli na majini, hivyo kuna umuhimu wa kuwa na wataalamu wa kutosha watakaosimamia na kuendesha miradi hiyo.

Amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya chuo hicho, ikiwemo majengo yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 70 yaliyofadhiliwa na Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuongeza uwezo wa chuo kutoa mafunzo ya kisasa.

"Rai yangu kwa uongozi wa chuo ni kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati na muendelee kubuni programu zitakazozalisha wataalamu wa sekta ya anga, majini na ardhini. Hatupaswi kuendelea kutegemea wataalamu kutoka nje wakati tuna vijana wenye uwezo mkubwa," amesema.

Pia amesema miongoni mwa miradi aliyotembelea ni jengo maalumu la mafunzo ya matengenezo ya ndege, jengo la mafunzo kwa wahudumu wa ndege, madarasa ya marubani pamoja na mabweni ya kisasa yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1,500.

Aidha, amesema idadi ya wanafunzi chuoni hapo imeongezeka hadi kufikia zaidi ya 19,000, jambo linaloonesha kukua kwa mahitaji ya wataalamu wa sekta ya usafirishaji nchini.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Prof. Ulingeta Obadia Mbamba, amesema ziara ya Naibu Waziri imewapa hamasa ya kuongeza ubunifu na kuhakikisha chuo kinaendelea kuwa kinara katika kuzalisha wataalamu wa sekta ya usafiri.

Amesema Serikali imewekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya usafiri, hivyo chuo kina wajibu wa kuhakikisha kinaandaa wataalamu watakaoweza kuendesha maendeleo hayo na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

"Naibu Waziri ametusisitiza tusiridhike na mafanikio tuliyofikia, bali tuendelee kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza ubora wa mafunzo ili wataalamu wanaohitimu hapa waweze kushindana katika soko la ajira la kimataifa," amesema Mbamba.

Aidha, amesema chuo kitaendelea kutekeleza maelekezo hayo ili kuendana na kasi ya maendeleo ya sekta ya usafiri, ambayo imeendelea kuwa mhimili muhimu wa kukuza uchumi na utoaji wa huduma nchini.





Matukio mbalimbali katika 
picha za pamoja.

WANANCHI wa Jimbo la Monduli wamempokea kwa shangwe Mlezi wao wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) na kutuma salamu kuwa wako bega kwa bega na Serikalini katika kuleta maendeleo nchini.

Salamu hizo zimetolewa tarehe 23 Julai 2026 wakati wa mkutano wa hadhara wa Mhe. Waziri Chongolo na maelfu ya wananchi waliojikusanya katika eneo la Soko la Losirwa, Kata ya Esilalei, Wilaya ya Monduli.

“Hongereni kwa kujibiidiisha kwa kazi. Nimepokea kilio chenu cha kujengewa soko la kisasa la Losirwa, niwahakikishie Wizara itafanyia kazi hilo; sambamba na kukamilisha ukarabati wa skimu ya umwagiliaji ya Mto wa Mbu kwa gharama ya shilingi bilioni 17 chini ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ili kutatua matatizo ya kilimo cha umwagiliaji katika Kata za Wilaya ya Monduli,” amesema Mhe. Chongolo.

Akizungumza kwa niaba yao, Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe. Joseph İsack Copiriano amesema kuwa wananchi wa Monduli wanaipongeza Serikali kwa kusogeza huduma za kijamii na kupeleka miradi ya maendeleo ikiwemo elimu, afya na kilimo.

“Kilio chao ni mbolea ipatikane, wanahitaji maji na ujenzi wa barabara, ikiwa ni pamoja na kupata elimu zaidi kuhusu kilimo cha malisho ya mifugo,” ameeleza Mhe. Copiriano.

Akijibu hoja za wananchi, Mhe. Chongolo ameahidi kuwa zitafanyiwa kazi na Wizara ya Kilimo na Taasisi zake, huku akisisitiza kwa wananchi umuhimu wa kulinda miundombinu na vyanzo vya maji kwa kuwa mabwawa madogo yanaweza kujengwa maeneo hayo kwa ajili ya shughuli za kilimo na kunywesha mifugo.

Katika nyakati tofauti, Waziri Chongolo pia ametembelea Shule ya Sekondari ya Manyara yenye wanafunzi zaidi 1,800 na kuzindua bweni la wanafunzi wavulana.











Na Mwandishi Wetu
JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limetekeleza matendo ya huruma kwa kutembelea na kuwafariji wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika Kituo cha Afya Kambarage, kilichopo Manispaa ya Shinyanga, huku likitoa ujumbe wa matumaini, maadili na usalama kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Fraterine Tesha amesema Jeshi la Polisi linatambua kuwa wagonjwa ni sehemu ya jamii inayolihudumia na kulilinda, hivyo limeona ni muhimu kufika kituoni hapo kuwapa pole na kuwatia moyo.

ACP Tesha, amewaasa wagonjwa kuwa na uvumilivu wakati wa matibabu, akisisitiza kuwa jamii inaendelea kuwaombea ili wapone na kurejea katika shughuli zao za kila siku za kushiriki ujenzi wa Taifa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Shinyanga, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Zainabu Mangara, amewapongeza wanawake waliojifungua katika kituo hicho cha afya na kuwakumbusha umuhimu wa kulea watoto wao katika misingi ya maadili mema.

ASP Mangara, ametoa elimu ya usalama barabarani kwa wazazi hao, akiwakumbusha kutowaruhusu watoto wao kupandishwa kwenye pikipiki zaidi ya mtoto mmoja kwa wakati mmoja, akieleza kuwa kitendo hicho kinaongeza hatari ya ajali na kuhatarisha maisha ya watoto pamoja na watumiaji wengine wa barabara.

Akizungumza kwa niaba ya uongozi wa Kituo hicho, Mganga Mfawidhi Dkt. Ernest Kurwa amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kutenga muda wa kutembelea na kuwafariji wagonjwa.

Dkt. Kurwa amesema ziara za aina hiyo huwapa wagonjwa faraja na matumaini, huku akitoa wito kwa jamii kujenga utamaduni wa kutembelea wagonjwa hospitalini ili kuwapa moyo na kuwafanya wajione kuwa hawapo peke yao katika kipindi cha changamoto za kiafya.


Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limesema litaendelea kutekeleza mkakati wa kuwafikia wananchi kwa kuwapatia taarifa sahihi kuhusu elimu na mafunzo ya ufundi stadi ili kuongeza uelewa na ushiriki wa wadau katika sekta hiyo.

Hayo ameyasema Meneja wa NACTVET Zanzibar, Elitha Mbedule, wakati akizungumza katika Banda la NACTVET kwenye Maonesho ya Saba (7) ya Wiki ya Elimu ya Juu yanayoendelea katika Viwanja vya Gombani Mpya, Pemba.

Amesema maonesho hayo ni jukwaa muhimu kwa NACTVET kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na baraza hilo, ikiwemo taratibu za kuanzisha vyuo vya elimu na mafunzo ya ufundi stadi pamoja na usajili na udhibiti wa taasisi hizo.

Aidha, amesema maonesho hayo yanawapa fursa wahitimu wa ngazi ya stashahada wanaotarajia kuendelea na masomo ya elimu ya juu kufika na kupata maelezo ya kina kuhusu udahili, kwa kuwa vyuo vikuu mbalimbali vinashiriki katika maonesho hayo.

"NACTVET itaendelea kutoa elimu kwa wadau wake kuhusu huduma na taarifa mbalimbali zinazohusu elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi ili kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na kwa wakati," amesema Elitha.

Ameongeza kuwa ushiriki wa NACTVET katika maonesho hayo una lengo la kuhamasisha jamii kutambua mchango wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi unaohitajika katika soko la ajira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini.





KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel Africa imeanza mwaka wake mpya wa fedha wa 2026/27 kwa mafanikio makubwa, baada ya kuongeza mapato kwa asilimia 31 katika robo ya kwanza ya mwaka 2026/27, yakichochewa na kasi kubwa ya matumizi ya intaneti na huduma za kifedha kwa njia ya mtandao.

Akiwasilisha matokeo hayo, Mtendaji Mkuu wa Airtel Africa, Bw. Sunil Taldar, alisema mapato ya kampuni hiyo inayofanya kazi katika nchi 14 barani Afrika, ikiwemo Tanzania, yalifikia dola bilioni 1.853 za Marekani kwa robo mwaka iliyoishia Juni 30, 2026, ikilinganishwa na dola bilioni 1.415 katika kipindi kama hicho mwaka uliopita.

Faida baada ya kodi ilipaa kwa asilimia 27 na kufikia dola milioni 198. Kwa kuzingatia viwango vya fedha visivyobadilika (constant currency), mapato ya kampuni yalikua kwa asilimia 21.1, yakionyesha ukuaji thabiti katika huduma za sauti, intaneti na Airtel Money.

Ripoti hiyo inaonyesha ukuaji mkubwa katika maeneo yote makuu ya kibiashara ambapo soko la Nigeria liliongoza kwa kukua kwa asilimia 29.8, likifuatiwa na ukanda wa Afrika ya Kati na Magharibi inayozungumza Kifaransa (Francophone Africa) uliokua kwa asilimia 18, huku ukanda wa Afrika Mashariki ukikua kwa asilimia 17.8.

Ukuaji huo unachochewa na ongezeko kubwa la wateja ambapo katika nchi zote 14, jumla ya wateja wa Airtel iliongezeka kwa asilimia 11.6 hadi kufikia milioni 189.

Ripoti hiyo inaonyesha kuwa asilimia 51 ya wateja wote wa kampuni hiyo sasa wanatumia simu janja (smartphones). Hali hiyo imesababisha idadi ya wateja wa intaneti kuongezeka kwa asilimia 15.5 hadi kufikia milioni 87.3.

Kasi ya matumizi ya intaneti imeongezeka kwa kiwango kikubwa, ambapo wastani wa matumizi ya data kwa mwezi kwa kila mteja ulipaa kutoka Gigabaiti (GB) 7.8 hadi kufikia GB 10.6, na kupelekea matumizi ya intaneti (data traffic) kuongezeka kwa asilimia 56.3 ndani ya mwaka mmoja.

Upande wa huduma za kifedha, wateja wa Airtel Money waliongezeka kwa asilimia 23.3 hadi kufikia milioni 56.5.

Thamani ya miamala inayofanyika kupitia Airtel Money sasa imevuka dola bilioni 245 za Marekani kwa mwaka (ongezeko la asilimia 51.5), huku mapato ya huduma hiyo pekee yakikua kwa asilimia 38.9 na kufikia dola milioni 404.

Ili kuhimili kasi hii ya ukuaji na mahitaji makubwa ya wateja, Airtel Africa imewekeza kiasi cha dola milioni 389 za Marekani katika robo-mwaka hiyo kwa ajili ya kupanua miundombinu yake.

Airtel Africa pia ilifanikiwa kujenga minara na vituo vipya vya mawasiliano zaidi ya 920, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuwahi kujengwa katika robo ya kwanza ya mwaka katika historia ya kampuni hiyo, pamoja na kutandaza mtandao wa nyaya za mawasiliano (fibre) hadi urefu wa kilomita 82,100 ili kuimarisha upatikanaji wa huduma bora.

Mapato kabla ya Riba, Kodi, Kushuka kwa Thamani, na Malipo ya Madeni (EBITDA) iliongezeka kwa asilimia 36.6 hadi dola milioni 928, huku kiwango cha faida cha EBITDA kikiboreka hadi asilimia 50.1.

Aidha, fedha taslimu zitokanazo na uendeshaji ziliongezeka kwa asilimia 38.3 hadi dola milioni 786, zikionyesha uimara wa kampuni licha ya kupanda kwa gharama za nishati.

"Tumeanza mwaka huu kwa matokeo mazuri tena. Kuongezeka kwa matumizi ya simu janja, ushiriki mkubwa wa wateja katika huduma za kidijitali na uwekezaji unaoendelea katika miundombinu vinaendelea kuchochea ukuaji wetu," alisema Bw. Taldar.

Katika hatua nyingine ya kimkakati, Bw. Taldar alithibitisha kuwa kampuni hiyo inaendelea na mpango wake wa kuorodhesha biashara ya Airtel Money katika Soko la Hisa la London (London Stock Exchange - LSE), punde tu itakapopata idhini kutoka kwa mamlaka husika, lengo likiwa ni kuongeza thamani ya biashara hiyo na kuvutia wawekezaji wengi zaidi wa kimataifa.

Na Mwandishi Wetu

Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) limesema linasikitishwa kuhusu kuongezeka kwa vitendo vya utapeli wa mitandaoni vinavyotumia picha, majina, nembo na utambulisho wa viongozi wa Serikali na watu maarufu kwa lengo la kuwadanganya wananchi na kujipatia fedha kwa njia zisizo halali.

Limesema kumekuwepo na matangazo yanayodai kuwa viongozi mbalimbali, wafanyabiashara au taasisi zinatoa mikopo, ruzuku (grants), misaada au uwekezaji wa haraka na matangazo hayo huambatana na ushuhuda wa uongo ili kuwafanya wananchi waamini.

Akizungumza kuhusu utapeli wa mitandaoni Katibu Mkuu wa TRAMEPRO ambaye pia ni Mtaalam wa Tiba Asili Boniventura Mwalongo amesema shirika hilo linatoa tahadhari kwa wananchi wote kutokukubali kushawishiwa na matangazo hayo bila kuyathibitisha kupitia mamlaka au taasisi husika. 

Amesisitiza wananchi wanapaswa kutumia taarifa zinazotolewa kupitia njia rasmi pekee na kuepuka kutuma fedha, nyaraka au taarifa binafsi kwa watu wasiojulikana.

“Tunasikitishwa na matumizi mabaya ya nembo na majina ya vyombo vya habari pamoja na viongozi wa kitaifa katika kusambaza taarifa za uongo. Vitendo hivyo vinachochea upotoshaji wa umma, huondoa imani kwa taasisi na vinaweza kuhatarisha usalama, amani na mshikamano wa Taifa.

“TRAMEPRO inaona bado kuna haja ya kuimarisha juhudi za kutokomeza mila potofu zinazodhuru afya, utu na haki za binadamu.Zipo taarifa na tafiti zinazoonyesha baadhi ya mila potofu zinaendelea kufanyika kwa siri katika maeneo mbalimbali. Hali hii inaonyesha kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado elimu, ufuatiliaji na ushirikiano wa wadau vinahitaji kuimarishwa zaidi.”

Amesema TRAMEPRO inatoa rai kwa Serikali kuimarisha mapambano dhidi ya utapeli wa mtandaoni kupitia vyombo vya dola na mamlaka zinazohusika.Kuendelea kutoa elimu ya matumizi salama ya mitandao ya kijamii na huduma za kidijitali.

Pia kufufua au kuimarisha mifumo ya kitaifa ya uratibu wa mapambano dhidi ya mila potofu kwa kushirikisha sekta zote muhimu pamoja na kuongeza uwekezaji katika tafiti, elimu ya afya na kampeni za mabadiliko ya tabia.

Wakati kwa mamlaka za mawasiliano na usalama zimeshauriwq kuchukua hatua za haraka dhidi ya akaunti na mitandao inayotumika kufanya utapeli na kusambaza taarifa za uongo.

Aidha kuongeza uwezo wa kufuatilia na kuwachukulia hatua wahalifu wa mtandaoni,kushirikiana na kampuni za mitandao ya kijamii kuondoa akaunti bandia zinazojifanya viongozi au taasisi.

Mwalongo pia ametoa rai kwa wananchi wasiamini matangazo yanayoahidi fedha, mikopo au ruzuku bila uthibitisho na kuwataka wathibitiahe taarifa kupitia ofisi au tovuti rasmi.

“TRAMEPRO inaamini jamii salama, yenye afya na maendeleo endelevu hujengwa kwa msingi wa ukweli, elimu, uwajibikaji na ushirikiano. Tunatoa wito kwa kila mwananchi kuwa sehemu ya mapambano dhidi ya utapeli wa mtandaoni, taarifa za uongo na mila potofu zinazokwamisha maendeleo ya Taifa.”

 

Na. Saidina Msangi, WF, Abidjan, Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Ali Munde (Mb), kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayoshughulikia Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano, pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati ya Mawaziri wa Biashara, Utalii, Viwanda na Madini.

Mkutano huo wa kimkakati ulioanza rasmi tarehe 24 Julai 2026 jijini Abidjan, Côte d’Ivoire, unalenga kuweka misingi imara ya ushirikiano wa kiuchumi barani Afrika.

Mkutano huo umejadili kwa kina umuhimu wa nchi za Afrika kuharakisha juhudi za kuendeleza sekta ya viwanda kwa kuongeza thamani ya malighafi za ndani badala ya kusafirishwa zikiwa ghafi, kuimarisha minyororo ya thamani ya kikanda, pamoja na kuweka mazingira bora na wezeshi yatakayovutia uwekezaji wenye tija kiuchumi.

Wajumbe wa mkutano huo walibainisha kuwa, kutokana na Bara la Afrika kuwa na rasilimali nyingi za asili, ardhi kubwa yenye rutuba kwa ajili ya kilimo, madini ya kimkakati na idadi kubwa ya vijana ambao ndio nguvu kazi kubwa katika uzalishaji, kuna umuhimu kwa Afrika kuwa kama kitovu cha uzalishaji na biashara duniani.

Aidha, mkutano huo umehimiza umuhimu wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani, kuboresha usimamizi wa rasilimali za asili, na kupambana na ukwepaji kodi ili kukabiliana na pengo kubwa la ufadhili wa maendeleo ya miundombinu ya kisekta.

Mawaziri na wataalamu hao walikubaliana kwa pamoja kuwa maendeleo ya viwanda hayawezi kufikiwa bila uwepo wa mfumo imara wa kifedha utakaowezesha upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu, kupunguza gharama za mikopo, na kuvutia sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akifuatilia mada zilizokuwa zikijadiliwa katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), (katikati) Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa (kulia) na Naibu Waziri wa Viwanda, Mhe. Dennis L. Londo (kushoto), wakifuatilia mijadala katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu Mtendaji, Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), Naibu Katibu Mkuu Mtendaji, Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama (wa pili kulia), na Kamishna Msaidizi Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. James Msina (kushoto), wakimsikiliza Afisa Usimamizi Fedha Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Glory Sindilo, akifafanua jambo katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.


Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), (katikati), Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa (kushoto) na Naibu Waziri wa Viwanda, Mhe. Dennis L. Londo (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufunguliwa kwa Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), (katikati), Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa (kushoto) na Naibu Waziri wa Viwanda, Mhe. Dennis L. Londo (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufunguliwa kwa Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Mtendaji, Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, na kulia ni Naibu Gavana wa Sera za Kiuchumi na Fedha, Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Yamungu Kayandabila.




Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akiteta jambo na Waziri wa Fedha wa Eswatini Mhe. Neal Rijkenberg, katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire. Katikati ni Katibu wa Naibu Waziri wa Fedha, Bw. Yambi Kinyaki.





(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Abidjan, Côte d’Ivoire.)


TIMU ya Barcelona wanatarajiwa kucheza mchezo wao wa kwanza wa maandalizi ya msimu mpya wa 2026/27 dhidi ya CE Europa, Ijumaa hii, Julai 24, saa 19:00 usiku katika kituo chao cha mazoezi cha Ciutat Esportiva Joan Gamper.

Mchezo huu utachezwa bila watazamaji (behind closed doors), muda mfupi kabla ya Barcelona kusafiri kwenda Uingereza kwa kambi ya mazoezi. Hii ni fursa muhimu kwa kocha Hansi Flick kuwapima wachezaji wake kabla ya msimu mpya kuanza rasmi.

CE Europa ni klabu ndogo inayotokea jijini Barcelona, yenye uhusiano wa karibu na eneo la Vila de Gracia, katika mkoa wa Catalonia, na huchezea ligi ya tatu ya Hispania, Primera Federación Kundi la 2, wakiongozwa na kocha Aday Benitez, aliyekuwa beki wa Girona. Msimu uliopita, CE Europa walimaliza nafasi ya tano katika ligi hiyo, hivyo si timu ya kudharauliwa licha ya tofauti kubwa ya ubora kati yao na Barcelona.

Kwa upande wa Barcelona, mchezo huu ndio wa kwanza kabisa katika msimu mpya. Ratiba ya maandalizi inaonyesha kuwa baada ya mchezo huu dhidi ya CE Europa, timu itaelekea St. George's Park nchini Uingereza tarehe 27 Julai kwa kuendelea na maandalizi.

Mchezo wa kwanza wa hadhara utakuwa dhidi ya Birmingham City tarehe 30 Julai, kisha mchezo mwingine wa siri dhidi ya Preston North End tarehe 3 Agosti. Hii inaonyesha kwamba mchezo dhidi ya CE Europa ni sehemu ndogo tu ya mpango mkubwa wa maandalizi.

mpira wa miguu, kubeti mpira wa miguu, bashiri soka, soka, beti kwenye soka, odds za soka, bashiri mpira wa miguu, beti za soka, beti mechi za soka, odds za kubeti mpira wa miguu

Kwa mtazamo wa kiufundi, mchezo huu utakuwa fursa kwa Flick kuwapa muda wachezaji vijana kutoka timu za chini (Juvenil U-18 na Barça Atlètic), huku baadhi ya nyota wakuu kama Lamine Yamal, Pedri, Raphinha na Jules Kounde bado wakiwa mapumziko mara tu baada ya kumalizika kwa fainali ya taji la Dunia.

Kwa hiyo, muundo wa kikosi kitakachocheza dhidi ya CE Europa unaweza kuwa na mchanganyiko wa vijana na wachezaji wachache wa kawaida waliopo tayari kambini.

Kwa ujumla, ingawa mchezo huu hautaonyeshwa moja kwa moja kwa umma kutokana na kufanyika bila watazamaji, umuhimu wake ni mkubwa kwa Barcelona kwani ndio hatua ya kwanza rasmi ya maandalizi ya msimu mpya.

Matokeo au takwimu za mchezo huu hazitarajiwi kutangazwa rasmi kwa vyombo vya habari mara moja, lakini taarifa fupi zinaweza kutolewa na klabu baadaye kuhusu jinsi mchezo ulivyoenda na mchango wa wachezaji vijana waliopewa nafasi.


NA MWANDISHI WETU, DAR

Mkandarasi anayetekeleza mradi wa Maduka ya Biashara ya Maria Nyerere (Maria Nyerere Shopping Mall) ulio chini Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), amehimizwa kuongeza kasi ya ujenzi ili mradi huo ukamilike kwa wakati.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda, Julai 22, 2026, Jijini Dar es Salaam, katika ziara ya Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT Taifa, kukagua uhai wa Chama na miradi ya Jumuiya hiyo.

Chatanda amesema, ipo haja ya mkandarasi huyo kuongeza kasi ya ujenzi, huku akimshauri kuongeza wakandarasi wengine ili kumsaidia baadhi ya kazi na kuongeza kasi ya ujenzi wa mradi huo.

"Mradi unakwenda vizuri, isipokuwa kwa mwenendo unavyokwenda na kwa muda tuliokubaliana huenda asikamilishe kwa wakati. Mkandarasi tunachomuhitaji aukamilishe mradi kwa mujibu wa tulivyokubaliana na kama kuna maeneo yeye hana uwezo wa kufanya, akabidhi kwa wakandarasi wengine (sub contractors) ili kazi ikamilike kwa wakati," amesema Chatanda.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti UWT Taifa, Zainabu Shomari, amesema mradi huo ni utekelezaji wa maagizo ya Chama wa kuzitaka Jumuiya zake kuwa na vitega uchumi.

"Chama kimeelekeza Jumuiya zake kujitegemea kiuchumi, kwahiyo, mradi huu ni utekelezaji wa maagizo na Chama na kwa hakika UWT tutafanikiwa kujitegemea," amesema Shomari.

Ikumbukwe kuwa, mradi wa Maria Nyerere Shopping Mall unatekelezwa eneo la Gerezani Jijini Dar es Salaam, ambapo unategemewa kuongeza mapato ili Jumuiya  hiyo iwe na uwezo wa kuendesha shughuli zake bila kutegemea uwezeshwaji kutoka Chama ngazi ya Taifa.

Pamoja na mradi huo, Kamati hiyo, ilipata fursa ya kukagua eneo lake lenye ukubwa wa hekta 8.2, lililopo mtaa wa Zogo, kata ya Zingiziwa, wilayani Ilala, ambapo linategemewa kuongeza uwekezaji wa Jumuiya hiyo.










MERIDIANBET Tanzania inaendelea kufungua milango mipya ya burudani na ushindi kwa kuileta rasmi Super Heli Premium, mchezo wa kasino unaochanganya kasi, mkakati na maamuzi ya papo kwa papo. Hapa, si suala la kubahatisha tu, ni kuhusu kusoma mchezo, kuhisi muda sahihi na kuchukua hatua kabla helikopta haijapotea angani.

Kila raundi ni hadithi mpya. Unaweka dau lako, helikopta inaanza kupaa, odds zinaongezeka, na macho yako yanabaki kwenye skrini. Ndani ya Super Heli Premium, msisimko uko kwenye sekunde chache za maamuzi, pale moyo unapodunda na ushindi ukionekana karibu.

Meridianbet imeufanya mchezo huu uwe wa uhuru kwa mchezaji kwa kukupa uhuru wa kuweka hadi dau tatu kwa raundi moja. Hii inamaanisha nafasi zaidi za kupanga mikakati tofauti ndani ya raundi ileile. Unaweza kucheza kwa tahadhari, au ukaamua kucheza kwa ujasiri mkubwa, chaguo liko mikononi mwako kila safari inapoanza.

Mbali na mchezo huu, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa wale wanaopenda mbinu, Super Heli Premium inatoa chaguo la makadirio kwa kuweka dau ndani ya vizidishi maalum, Over/Under kwa kubashiri mwelekeo wa safari ya helikopta, pamoja na 50% Cashout inayokuwezesha kuchukua sehemu ya ushindi mapema huku ukiendelea kucheza na kilichobaki.

Na pale ushindi mkubwa unapogonga, haufichiki. Cash out kwenye kizidishi zaidi ya 50 na jina lako linaonekana kwenye chati likipongezwa, likikupa heshima mbele ya wachezaji wengine. Super Heli Premium ni zaidi ya mchezo, ni jukwaa la ujasiri na zawadi. Jiunge sasa ndani ya Meridianbet na uanze safari yako ambapo kila uamuzi unaweza kukupeleka juu zaidi.

Top News