.jpeg)
.jpeg)
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mwang’onda amewapongeza uongozi wa Musasa Gold Mine kwa kugharamia ujenzi wa kituo hicho na kuiomba jamii kuendelea kushirikiana na wawekezaji katika kuleta maendeleo.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Kamishna Msaidizi wa Polisi Safia Jongo, amesema kituo hiki ndicho kitakuwa kikuu kwa Kata yote ya Runzewe. Amesema wananchi wa Musasa na Runzewe kwa ujumla watahudumiwa huduma zote za kipolisi kupitia kituo hicho.
Ujenzi wa kituo hiki ulianza tarehe 16 Machi 2026 na umegharimu *shilingi 150,000,000. Kati ya hizo shilingi 145,000,000 zimetolewa na Musasa Gold Mine huku wananchi wakichangia shilingi 5,000,000 kupitia nguvu zao. Mgodi pia umenunua samani zote za ofisi.
Uanzishwaji wa kituo hiki umetokana na ongezeko la watu katika eneo hilo kutokana na shughuli za uchimbaji madini. Viongozi wamesema uwepo wake utasaidia kuimarisha ulinzi, kupunguza uhalifu, kutoa mwitikio wa haraka na kukuza mazingira salama kwa uwekezaji.
Wananchi wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita na wawekezaji kwa hatua hiyo na wameahidi kulinda miundombinu hiyo.





Na Belinda Joseph – Dodoma
Walimu wenye ulemavu mkoani Dodoma wamepatiwa elimu ya fedha, uwekezaji na hifadhi ya jamii ili kuwajengea uwezo wa kusimamia kipato, kuwekeza na kujiandaa kwa maisha baada ya kustaafu, mafunzo hayo yameandaliwa na Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Akizungumza katika mafunzo hayo, Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Mwalimu Kiduma Mageni, wakati akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa, amesema elimu ya fedha ni muhimu kwa watumishi kwa kuwa inawasaidia kupanga matumizi, kuweka akiba na kuwekeza, akisisitiza kuwa changamoto za kifedha haziwezi kutatuliwa kwa kuongeza kipato pekee bila kuwa na uelewa wa kukisimamia.
Mwalimu Kiduma amesema walimu wanapaswa kuanza kujiandaa kwa maisha ya baada ya kustaafu mapema kwa kufanya maamuzi sahihi kuhusu matumizi, akiba na uwekezaji ili kuepuka changamoto za kifedha wanapomaliza utumishi.
Kwa upande wake, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa CWT, Alfred Alexander, amesema mafunzo hayo yamelenga pia kuwaandaa walimu kukabiliana na maisha baada ya kustaafu, akieleza kuwa baadhi ya wastaafu wamekuwa wakipoteza mafao yao kutokana na kuingia kwenye uwekezaji bila kuwa na uelewa wa kutosha.
Alfred amesema CWT imeialika Mwalimu Commercial Bank kutoa elimu kuhusu fursa za kifedha na uwekezaji, ili kuwasaidia walimu kuanza uwekezaji wakiwa bado kazini na kujenga vyanzo vya ziada vya kipato.
Mkuu wa Idara inayohudumia Walimu Wenye Ulemavu wa CWT, Mwalimu Robert Bundala Katuba, amesema mafunzo hayo yamewapa walimu uelewa kuhusu mabadiliko ya sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na fursa za uwekezaji, huku akizitaka taasisi nyingine kuunga mkono juhudi za kuwawezesha walimu wenye ulemavu.
Mwalimu Robert amesema CWT inathamini ushirikiano na NSSF katika kutoa elimu hiyo na kwamba maarifa yanayopatikana yanapaswa kuwafikia walimu wengine pamoja na jamii, hususan kuhusu umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii na kutumia fursa zinazopatikana.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Dodoma amesema mfuko huo utaendelea kushirikiana na CWT kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi, akieleza kuwa elimu hiyo ni muhimu katika kuwasaidia kuelewa huduma zinazotolewa na NSSF na fursa zinazopatikana kupitia hifadhi ya jamii.
Mafunzo hayo yameweka mkazo katika umuhimu wa walimu wenye ulemavu kuwa na uelewa wa fedha, uwekezaji na hifadhi ya jamii mapema, ili kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi ya kifedha, kujenga vyanzo vya ziada vya kipato na kuwa na maisha yenye utulivu wakati wa utumishi na baada ya kustaafu.
.jpeg)

Na Mwandishi Wetu, Morogoro Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umeeleza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja umeendelea kuhakikisha Tanzania inapata bidhaa za mafuta kwa uhakika, kwa wakati na kwa gharama shindani.
Akizungumza katika Maonesho ya Nne ya Kitaifa ya Utamaduni yanayoendelea mkoani Morogoro, Mchumi wa PBPA, Bw. Henry Kilenga, amesema mfumo huo unahusisha ukusanyaji wa mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta nchini kabla ya kutangazwa kwa zabuni za kimataifa.
Amesema PBPA hukusanya mahitaji hayo na kuyaunganisha ili mafuta yaagizwe kwa pamoja kwa kiwango kikubwa. Utaratibu huo huiwezesha nchi kunufaika na ununuzi wa pamoja na kupata gharama shindani za uagizaji na usafirishaji.
“PBPA hukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, huandaa zabuni na kuwashindanisha wazabuni waliokidhi vigezo. Utaratibu huu unasaidia kuhakikisha nchi inapata mafuta kwa uhakika na kwa gharama shindani,” amesema Kilenga.
Amefafanua kuwa zabuni hizo hushirikisha kampuni za kimataifa zilizohakikiwa na kukidhi vigezo vilivyowekwa na PBPA. Wazabuni hushindanishwa kwa uwazi, huku tathmini ikizingatia bei zilizowasilishwa, uwezo wa kusambaza mafuta na masharti mengine ya zabuni.
Kwa mujibu wa Kilenga, baada ya kukamilika kwa tathmini, kampuni zilizokidhi vigezo na kuwasilisha bei nzuri huchaguliwa kuleta mafuta nchini kulingana na kiasi na muda uliopangwa.
Kilenga amesema uwazi na ushindani katika uendeshaji wa zabuni unalenga kulinda maslahi ya taifa, kuongeza ufanisi na kuhakikisha bidhaa za mafuta zinaendelea kupatikana kwa ajili ya wananchi na shughuli mbalimbali za kiuchumi.
Amesisitiza kuwa Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja una mchango mkubwa katika kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)


.jpeg)










