Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, amesema thamani ya fedha itaendelea kuwa imara kuelekea kipindi cha mavuno ili kuwawezesha wakulima kupata thamani stahiki ya mazao yao kulingana na shughuli za kiuchumi wanazozifanya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) Julai 10, 2026, Tutuba amesema kiwango cha riba ya Benki Kuu cha asilimia 6.25 kinalenga kuhakikisha kunakuwa na utulivu wa bei na mfumuko wa bei unaendelea kubaki kati ya asilimia 3 hadi 5.

Amesema kiwango hicho pia kitawezesha Mabenki kuwa na ukwasi wa kutosha kwa ajili ya utoaji wa mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara, hivyo kusaidia shughuli mbalimbali za uzalishaji na biashara nchini.

Tutuba amesema wakulima wanapoanza kuvuna mazao yao, thamani imara ya fedha itasaidia kuhakikisha wanapata malipo yanayolingana na thamani halisi ya mazao yao sokoni.

Ameongeza kuwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa nje ya nchi pia watanufaika kwa kupata fedha za kigeni kulingana na thamani ya fedha walizotumia katika uzalishaji, huku tathmini ikionyesha kiwango cha riba cha asilimia 6.25 kinatosha kuendelea kuimarisha shughuli za kiuchumi.

Aidha, amesema BoT hutumia Maonesho ya Sabasaba kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kiwango cha riba ya Benki Kuu katika kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza ukwasi katika mzunguko wa uchumi na kuwezesha upatikanaji wa fedha kwenye mabenki ya biashara.

Tutuba amesema maonesho hayo pia ni fursa kwa Watanzania kujifunza, kupata bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na mbinu mpya za kufanya shughuli za kiuchumi zinazochangia ukuaji wa uchumi wa nchi.






Na Mwandishi Wetu

MECHI kati ya timu ya soka ya Chuo cha Future World na timu ya Chanika Veteran umemalizika kwa sare 1-1 huku ujumbe mkubwa katika mechi hiyo ni kuhamasisha vijana kujiunga na Chuo hicho kupata ujuzi.

Katika mechi hiyo iliyochezwa leo Julai 11,2026 katika uwanja wa VODP uliopo Chanika kata ya zingiziwa wilayani Ilala jijini Dar es Salaam umeshuhudiwa na mamia ya wananchi wa Chanika na viunga vyake.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mechi hiyo Ofisa Masoko kutoka chuo Cha Future World Vocational David Msumba amesema lengo la mechi hiyo ni kukitambulisha chuo kwa wananchi hasa katika kata za Chanika na Zingiziwa

“Tumecheza mechi kati yetu Future World na Chanika Veterani na lengo kuu ni kuhamasisha wananchi kujiunga na chuo chetu ili kupata ujuzi kupitia kozi mbalimbali tunazitoa.”

Ametaja kozi zinazotolewa na chuo hicho ni ufundi wa magari na pikipiki, umeme wa majumbani,ulezi wa watoto wadogo,mafunzo ya urembo na ususi,Hotel Management pamoja na Computer Applications.

“Future World ni chuo chenye uzoefu wa karibu miaka 30 sasa, tangu kilipoanzishwa kwenye utoaji wa Mafunzo ya ufundi stadi katika fani mbalimbali.

“Hivi Karibuni, chuo hiki kimefungua tawi lake jipya eneo la Chanika kwa Ndevu eneo ambalo lina mandhari bora kabisa kwa utoaji wa elimu ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa hosteli nzuri za wanafunzi.

“Vijana hasa wahitimu wa kidato cha nne mnakaribishwa chuoni au kuingia kwenye Tovuti ya chuo na kupata fomu ya kujiunga na mafunzo uyapendayo, au kwa mawasiliano 0715 015778 ”amesema Msumba




















Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa Kusikiliza makundi mbalimbali ya kijamii, leo tarehe 11/07/2026 amesikiliza makundi ya kijamii 52 ndani ya Mkoa wa Songwe.

Aidha, Ndg Rabia Abdalla Hamid amesema kuwa ameridhishwa na utendaji kazi wa viongozi wa Serikali ndani ya Mkoa wa Songwe baada ya wananchi katika makundi mbalimbali ya kijamii, makundi 52 kuuliza maswali, ushauri, maoni, changamoto, kero na baadae kujibiwa kwa usahihi na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe Jabir Makame aliyeambatana na Viongozi mbalimbali wa Serikali kwa ajili ya kujibu hoja za wananchi.

#KaziNaUtuTunasongaMbele

#CCMKimbilioLaWananchi

#CCMTabasamuLaWatanzania










Bonanza la kimichezo lililohusisha vyombo vya ulinzi na Usalama na watumishi wa halmashauri katika Wilaya ya Ulanga Mkoa wa Morogoro lafana huku likiwaleta karibu vyombo hivyo na watumilishi wa halmashauri wilayani humo.

Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ulanga Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Deogratius Challe, ambapo alifungua bonanza hilo huku akiwataka watumishi hao na maafisa wa vyombo hivyo kutumia michezo hiyo kama sehemu ya kuimarisha afya zao pamoja na kujenga udugu utakaosadia kudumisha ushirikiano pamoja na kukomesha vitendo vya kiharifu Wilayani humo.

Ameongeza kuwa mafanikio katika utendaji wa kazi yanategemea mshikamano na ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali pamoja na wananchi ili kuifanya Wilaya hiyo iendele kuwa shwari muda wote.

Kwa Upande wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nalolikatumia fursa hiyo kutoa elimu kuhusu kinga na namna ya kukabiliana na majanga ya moto, huku maafisa wa Jeshi hilo wakitoa elimu kuwa moto una manufaa katika maisha ya kila siku, lakini unaweza kuwa hatari usipotumika au kudhibitiwa kwa usahihi na kwa wakati.

Nao idara ya Uhamiaji Wilayani humo ikatoa elimu kuhusu masuala ya uhamiaji, ikiwemo taratibu za utoaji wa hati za kusafiria na umuhimu wa wageni wote wanaoingia na kutoka nchini kufuata sheria na taratibu zilizowekwa.

Sambamba na hilo afisa Utamaduni wa Wilaya ya Ulanga George Kayora, alieleza kufurahishwa na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Halmashauri na vyombo vya ulinzi na usalama huku akiweka wazi kuwa bonanza hilo limeimarisha mahusiano, mshikamano na afya za washiriki kupitia michezo hiyo.

Timu shiriki katika Bonanza hilo zilikuwa ni vyombo vya ulinzi na usalama vya Wilaya ya Ulanga dhidi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, ambapo Katika bonanza hilo, Jeshi la Polisi kupitia kitengo cha Polisi Jamii kilitoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kubaini,kuzuia, na kutanzua uhalifu, pamoja na kutoa taarifa kwa wakati kuhusu vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa jamii.

Michezo iliyowakutanisha watumishi hao ni Mpira wa miguu, pete, bao, karata huku matokeo katika mpira miguu timu ya vyombo vya ulinzi ikiichapa goli tatu kwa mbili timu ya halmashauri.










 
 

Mr Walter Makundi (in blue shirt), a Tanzanian Civil and Structural Engineer who has lived in Singapore with his family since 1994, has described his recent meeting with senior government officials from several African countries as a great honour.


The engagement, organised by the Chandler Academy of Governance, brought together delegates from Rwanda, Kenya, Uganda, Mauritius, Malawi, Somalia, Zambia, Tanzania and South Africa.


“I am sincerely grateful to the Chandler Academy of Governance for allowing me to share my personal reflections on Singapore’s remarkable transformation,” Mr Makundi said.


He noted that during his more than three decades in Singapore, he had witnessed first-hand how visionary leadership, long-term planning, strong institutions and disciplined implementation had helped transform the country into one of the world’s most advanced and prosperous nations.


“It was a privilege to exchange ideas with such distinguished government leaders and to reflect on lessons that may be useful to African countries,” he said.


Mr Makundi expressed hope that Singapore’s development journey would continue to inspire African nations as they pursue sustainable growth, modern infrastructure, stronger institutions and improved governance.


He thanked the Chandler Academy of Governance and all participating delegates for the thoughtful discussions, warm fellowship and memorable experience.


The Chandler Governance Group (CGG) is an international non-profit organisation headquartered in Singapore. It works with governments to build capabilities through training, hands-on projects, partnerships, and knowledge creation and sharing.


CGG founder Richard F. Chandler established CGG in 2019 as the Chandler Institute of Governance (CIG), with the support of a group of seasoned former government leaders from several countries. He saw the value of an independent institute that would work with governments in highly practical ways. We are a practitioner-focused organisation, focusing on the “how” rather than just the “what” and “why”.

CIG rebranded in 2026 as CGG.


The Chandler Academy of Governance (CAG) is the Learning and Development division of CGG. We design and deliver training programmes for public sector leaders, equipping them with the skills to deliver high-performance government, with its signature programmes anchored in proprietary curriculum, practitioner-focused, and contextualised to local needs. 


It utilises a range of teaching techniques, including seminars, expert-led discussions, and site visits. We also work with clients to design customised programmes for public servants, tailored to the country context, objectives, and participant profiles.

.








BALOZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema lugha ya Kiswahili inaendelea kukua na kuenea duniani ambapo sasa inazungumzwa na watu zaidi ya milioni 200 katika nchi 14 duniani na kutumika rasmi katika jumuiya kadhaa za kikanda barani Afrika na kimataifa.

Balozi Matinyi aliyasema hayo kwenye sherehe za Siku ya Lugha ya Kiswahili Duniani zilizoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Algeria na kufanyika jijini Algiers tarehe 9 Julai zikihudhuriwa na mabalozi, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, taasisi za umma na binafsi, wanazuoni na waandishi wa habari walioongozwa na Katibu Mnadhimu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni na Sanaa ya Algeria, Bibi Nacera Ayaïchia.

“Mbali ya Tanzania, Kiswahili pia ni lugha ya taifa nchini Kenya, Uganda, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),” alisema Balozi Matinyi kwenye hotuba yake aliyoitoa kwa lugha ya Kiswahili na nakala yake katika tafsiri ya lugha za Kiarabu, Kifaransa na Kiingereza kusambazwa kwa wageni waalikwa waliopewa fursa ya kuifuatilia kwa sauti na maandishi kwenye skrini kubwa.

Sherehe hiyo ilinogeshwa na filamu fupi ya dakika kumi iliyoonesha marais wa zamani na wa sasa wa Tanzania na baadhi wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wakihutubia kwa lugha ya Kiswahili katika nyakati tofauti.

Filamu hiyo pia inamwonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia kwa lugha ya Kiswahili nchini Komoro mwaka 2025 kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru wa taifa hilo.

Balozi Matinyi aliongeza pia kwamba Kiswahili ni lugha rasmi ya Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Kadhalika, Balozi Matinyi aliitaja mifano ya redio za nchi za Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japan, China, Iran, India na wakati fulani Marekani ambazo hutumia lugha ya Kiswahili katika matangazo yake ya kila siku.

Akirejea kauli mbiu ya mwaka huu ya siku hiyo ya “Kiswahili kwa Amani, Mshikamano na Diplomasia ya Uchumi Duniani”, Balozi Matinyi alisema Kiswahili ni lugha ya kujivunia ambayo imetumika katika mapambano ya ukombozi barani Afrika na inaendelea kutumika kulinda amani, kuleta mshikamano na kujenga uchumi barani Afrika.

Sherehe hiyo iliyotumia lugha nne zikiongozwa na Kiswahili, ilipambwa pia na vinywaji vya chai na kahawa ya Tanzania, vyakula vya mapishi ya Kiswahili, maonesho ya mavazi ya wakaazi wa pwani ya Tanzania kama khanga, baibui, kanzu, vikoi na vitenge yaliyooneshwa na wanafunzi wa Tanzania.

Wanafunzi hao wa Tanzania wanaosoma kwenye vyuo vikuu nchini Algeria, walicheza pia ngoma mbili za makabila ya Tanzania ya Kimasai na Kihaya na kuimba shairi la Kiswahili.

Siku ya Lugha ya Kiswahili Duniani huadhimishwa mwezi Julai tangu mwaka 2022 kufuatia uamuzi wa UNESCO wa mwaka 2021 wa kuitangaza tarehe 7 Julai kuwa siku ya maadhimisho ya lugha hii pekee barani Afrika kuwahi kupewa hadhi hii kimataifa.


"....Mimi nikifa nitaaga siwezi kuondoka kimya kimya", Seif Kisauji amemwambia Ankal kwa utani wakati Mwanamuziki huyo maarufu kama Babu wa TikTok, akikanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa amefariki dunia.

Babu wa TikTok akiongea akiwa msikiti wa Maamur ulioko Upanga jijini Dar amekanusha taarifa hizo na kuwahakikishia mashabiki wake kuwa yuko hai na anaendelea vizuri.

Ameeleza kuwa chanzo cha mkanganyiko huo ni kifo cha mtoto wa familia yao, Mabrouk Kisauji, na si yeye, na kwamba wapo hapo Maamur kukamilisha mipango ya safari ya Tanga, na kwamba yeye na familia yake wanasafiri kuelekea huko leo kwa ajili ya kuhudhuria mazishi.

Kisauji kaongea haya yote baada ya kuona video yake akiimba kusambazwa mitandaoni ikiwa imeambatanishwa na madai ya uongo kwamba amefariki, jambo lililozua taharuki miongoni mwa mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Amewasihi watumiaji wa mitandao kuwa makini na taarifa za upande mmoja kwani katika zama hizi za kila mtu kujifanya mwandishi wa habari, taarifa zisizo sahihi ni nyingi mno.

Pia amewataka walio wanahabari wasiwe na papara za kuchapisha taarifa ammbazo hazijathibitishwa kwa kuwa hiyo inawavunjia heshima kwa kuonekana ni waongo na wadaku.


Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya NIC Insurance imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa Bima ya COMESA (COMESA Yellow Card), ikieleza kuwa huduma hiyo inarahisisha safari za kuvuka mipaka ya nchi wanachama wa Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) bila kulazimika kukata bima mpya ya lazima katika kila nchi.

Akizungumza katika Banda la NIC Insurance kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa Mwandamizi wa kampuni hiyo, Bi. Erika Nnko, amesema Bima ya COMESA ni mfumo wa kikanda wa bima ya vyombo vya moto unaowapa madereva uhuru wa kusafiri kwa usalama katika nchi wanachama wa COMESA huku wakitambuliwa kisheria kupitia kadi maalumu ya njano inayofahamika kama COMESA Yellow Card.

Amesema mmiliki wa chombo cha moto anapokata bima hiyo kupitia kampuni za bima zilizoidhinishwa nchini, hupatiwa Yellow Card ambayo hutambulika na mamlaka za nchi zote zinazoshiriki katika mfumo huo.

Erika amesema kadi hiyo hutoa kinga dhidi ya madai yanayotokana na majeraha kwa watu wengine au uharibifu wa mali za watu wengine unaoweza kusababishwa na chombo cha moto wakati wa safari katika nchi wanachama wa COMESA.

Ameeleza kuwa mfumo huo unarahisisha biashara na usafirishaji wa mizigo pamoja na safari za watu binafsi kwa kuondoa ulazima wa kukata bima mpya ya lazima ya mkataba wa tatu (Third Party) kila unapovuka mpaka wa nchi mwanachama.



Na Mwandishi Wetu
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, ameipongeza Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwa juhudi zake za kuwawezesha vijana kujiajiri kupitia Kituo chake cha Kiatamizi cha IAA Business Start Up Centre, kinachowasaidia kubadili mawazo ya kibunifu kuwa biashara zenye mafanikio.

Tutuba alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la IAA katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema anafurahishwa na maendeleo ya kituo hicho, akieleza kuwa alishiriki katika hatua za mwanzo za kuanzishwa kwake na sasa anashuhudia matokeo chanya kupitia vijana wanaobuni na kuanzisha biashara zinazochangia maendeleo ya uchumi.

"Ninakumbuka tulipoanzisha kituo hiki. Leo ninafurahi kuona kinaendelea kuzalisha vijana wenye ubunifu na kuwageuza mawazo yao kuwa fursa za kiuchumi," alisema Tutuba.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa, Uhusiano na Masoko wa IAA, Sarah Goroi, alisema taasisi hiyo imeendelea kuwekeza katika kuwaandaa vijana kwa kujiajiri kupitia Kituo cha Kiatamizi, sambamba na kutoa elimu inayokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Alisema mbali na mafunzo ya darasani, IAA imeweka mazingira rafiki yanayowezesha wanafunzi kuanzisha biashara zao huku wakipata ushauri wa kitaalamu, mafunzo ya ujasiriamali na ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha mawazo yao yanakua na kuwa biashara endelevu.

Sarah alisema katika mwaka wa masomo 2024/2025 zaidi ya vijana 8,600 walinufaika na programu za ujasiriamali, huku vijana 1,520 wakiwasilisha mawazo mbalimbali ya biashara kupitia kituo hicho.

Aliongeza kuwa kati ya mawazo hayo, zaidi ya biashara 50 zilianzishwa na kampuni 12 zikafanikiwa kusajiliwa rasmi, zikijikita katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara, teknolojia, sanaa, uhifadhi wa mazingira na shughuli nyingine za kiuchumi.

Alisema kupitia Kituo cha Kiatamizi, wahitimu wengi wamefanikiwa kujiajiri na wengine kuanzisha kampuni zinazowaajiri vijana wenzao, hatua inayochangia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia ubunifu na ujasiriamali.









Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI  ya Mixx imeendelea kuwazawadia wateja wake kupitia kampeni ya Kombe la Dunia ya MiXX Super, ambapo washindi watatu wamekabidhiwa zawadi za shilingi milioni moja kila mmoja kwa kutumia aprication ya MiXX Super app kufanya malipo ya huduma mbalimbali.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi hizo katika banda la Yas kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Meneja wa Biashara Mixx Mkoa wa Dar es Salaam, Estony Venant, alisema kampeni hiyo imeendelea kuwagusa Watanzania wengi huku jumla ya washindi 48 wakinufaika hadi sasa.

Alisema kati ya washindi hao,zaidi ya washindi 20 wamejishindia vifaa mbalimbali kutoka kwa mshirika wa Mixx kampuni ya Hisense, huku washindi wengine zaidi ya 40 wakijishindia fedha taslimu za shilingi milioni moja kila mmoja.

Venant alisema kampeni hiyo bado inaendelea na kwamba mshindi wa mwisho atajishindia zawadi kubwa ya shilingi milioni 50, akiwahimiza wananchi kutumia Aprication ya MiXX Super app katika kufanya malipo ya huduma mbalimbali za kifedha ili kuongeza nafasi ya kushinda.

"MiXX Super ni zaidi ya Aprication malipo; ni jukwaa linalorahisisha huduma za kifedha huku likiwapa watumiaji nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali. Tunawahimiza wananchi kuipakua na kuitumia mara kwa mara," alisema Venant.



Top News