Kaimu Meneja wa Mkoa wa TRA Dodoma, Bw. Obrey Sillayo, akiambatana na Kaimu Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi pamoja na maafisa wengine wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wametoa mkono wa Eid Fitri kwa watoto yatima na wenye mahitaji maalumu katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima Rahmani, ikiwa ni sehemu ya kuonesha upendo na kuimarisha mshikamano na jamii.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Bw. Sillayo amepongeza juhudi za kituo hicho kwa kulea watoto katika misingi bora ya maadili na malezi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwajali watoto hao kwa ustawi wa taifa.

Aidha, ameeleza kuwa TRA itaendelea kushiriki katika shughuli za kijamii kama sehemu ya kuwajibika kwa jamii na kujenga uhusiano mzuri na wananchi.

Kwa upande wake, Bi. Rukia Hamisi Abdallah ameishukuru TRA kwa mkono huo wa Eid, akieleza kuwa umeleta faraja na matumaini kwa watoto wanaolelewa katika kituo hicho.

Tukio hilo limeacha ujumbe wa upendo, mshikamano na uwajibikaji kwa jamii.







 

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 19,2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Mafunzo hayo pia yameenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho hayo ni “Bidhaa Salama, Imani kwa Mlaji,” ikisisitiza umuhimu wa kuhakikisha bidhaa zote zinazotumiwa na wananchi zinakidhi viwango vya usalama na ubora.

Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC, Thecla Kitosi, amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wazuri wa elimu hiyo kwa jamii zinazowazunguka.

Aidha Bi.Kitosi amewaasa wanafunzi hao kuelewa haki zao kama walaji, pamoja na wajibu wao wa kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini au kuwa na mashaka kuhusu usalama wa bidhaa au huduma wanazotumia.

Hata hivyo amewahimiza wanafunzi kuwa mabalozi wazuri kwa jamii zao kwa kuwafahamisha wazazi na ndugu zao juu ya hatari za bidhaa bandia na namna ya kuzitambua.

"FCC itaendelea kutoa   elimu kwa makundi mbalimbali ya jamii, hususan wanafunzi, ni njia muhimu ya kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa, wanaoweza kujilinda dhidi ya bidhaa bandia na huduma zisizo na ubora."amesisitiza Bi.Kitosi

Kwa upande wake Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine, amieleza kuwa bidhaa bandia zinaweza kuwa na athari kubwa kiafya, kiuchumi na hata kijamii. Alifafanua kuwa baadhi ya bidhaa hizo, hususan vipodozi, dawa na vifaa vya umeme, vinaweza kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji kutokana na kutokidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa.

“Ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuwa makini na bidhaa tunazonunua. Hakikisheni mnachunguza nembo za ubora na kununua bidhaa kutoka kwa wauzaji wanaoaminika,” amesisitiza Bi. Diana.

Kwa upande wao, wanafunzi walionesha shauku kubwa kwa kuuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia. Walishukuru kwa elimu hiyo na kuahidi kuitumia ipasavyo katika maisha yao ya kila siku.

Elimu hii ni sehemu ya juhudi za FCC za kuendelea kulinda haki za mlaji pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na zenye ubora unaokubalika, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

 Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

   

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Maafisa kutoka Tume ya Ushindani(FCC) wakiwa katika picha ya pamoja na  Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Bunge  mara baada ya kukamilisha utoaji wa elimu kwa wanafunzi kuhusiana masuala ya kumlinda mlaji.

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP), kwa kushirikiana na taasisi ya Sightsavers na YOWDO, umeandaa jukwaa maalumu la vijana na watu wenye ulemavu kwa lengo la kujadili fursa, changamoto na mikakati ya kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

Akizungumza leo Machi 19, 2026 jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Programu wa TGNP, Bi. Anna Sangai, amesema jukwaa hilo linafanyika ikiwa ni sehemu ya kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Mwezi wa Wanawake, likilenga kuwapa vijana nafasi ya kujadili masuala yanayowahusu na kupata uelewa mpana zaidi.

Amesema jukwaa hilo pia linatoa fursa kwa vijana kuuliza maswali, kubadilishana mawazo na kujifunza kuhusu haki, fursa na wajibu wao katika kuchangia maendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, idadi ya watu wenye ulemavu imeongezeka kutoka asilimia 9.3 mwaka 2012 hadi asilimia 11.2 mwaka 2022, hali inayoonesha umuhimu wa kuongeza juhudi za ujumuishaji katika mipango ya maendeleo.

“Mchakato huu unaonesha wazi kuwa taifa linaelekea kwenye kuhakikisha ujumuishaji katika fursa, mipango na bajeti kwa watu wote, hususan vijana wenye ulemavu,” amesema Sangai.

Ameongeza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, katika nguzo ya uchumi imara, jumuishi na shindani, inalenga kuwa na mfumo wa kifedha unaowezesha wananchi wote kushiriki kikamilifu, huku ukitoa kipaumbele kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake, mmoja wa washiriki wa jukwaa hilo, Ridhiwani Burhani, amesema anatarajia kuona wanawake, hususan wenye ulemavu, wakipewa nafasi kubwa zaidi katika nyanja zote za maendeleo kutokana na uwezo wao mkubwa.

Naye Maimuna Saidi amesema matarajio yake ni kuona kundi la watu wenye ulemavu, hasa wanawake, likinufaika zaidi na fursa mbalimbali ifikapo mwaka 2050, akieleza kuwa juhudi za serikali zimeanza kuleta mabadiliko kupitia elimu inayotolewa kwa jamii.

Akizungumza katika jukwaa hilo, Afisa Mradi wa Sightsavers, Sabina Maheke, amesema mjadala huo utasaidia kuweka mikakati madhubuti ya kuwasaidia vijana wenye ulemavu, hasa wanawake, kupata fursa za ajira na kujikwamua kiuchumi.

Jukwaa hilo limewakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka Wizara ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Watu wenye Ulemavu) pamoja na asasi za kiraia.








Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Songea (SOUWASA) imewatunukia tuzo wateja wake kinara katika makundi matatu ambayo ni majumbani, maeneo ya biashara na taasisi pamoja na Tuzo maalumu kwa mdau anashirikiana bega kwa bega na Mamlaka kwenye utoaji taarifa na ushauri, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha ulipaji wa bili kwa wakati na kuboresha ushirikiano katika utoaji wa huduma ya maji.

Utoaji wa tuzo hizo umefanyika Machi 19, 2026 katika maeneo mbalimbali ya mji wa Songea, ambapo mamlaka imewafuata katika maeneo yao ya kazi na makazi kwa lengo la kuthamini mchango wao katika matumizi ya huduma ya maji na uwajibikaji wa malipo.

Akizungumza katika zoezi hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SOUWASA, Baby Biko, amesema hatua hiyo inalenga kuwatambua wateja wanaolipa ankara za maji kwa wakati na kuhamasisha wengine kuiga mfano huo. Amesema mamlaka imeweka vigezo vinavyozingatia matumizi ya maji yanayoendana na ulipaji sahihi wa bili katika makundi yote ya wateja.

Ameongeza kuwa utoaji wa tuzo hizo pia umehusisha wadau wanaoshirikiana na mamlaka katika kulinda miundombinu ya maji kwa kutoa taarifa za uharibifu, wizi wa mita pamoja na uvujaji wa mabomba, hali inayochangia kuboresha huduma kwa wananchi.

Katika kundi la biashara, Nipo Guest House imetunukiwa tuzo kutokana na rekodi nzuri ya ulipaji wa bili kwa wakati, huku Chuo cha Ualimu Songea kikipewa tuzo ya Taasisi kubwa kwa ulipaji wa ankara za maji kwa wakati.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkuu wa Chuo cha Ualimu Songea, Catherine Thomas Kimboka, ameipongeza SOUWASA kwa huduma wanazozitoa, akieleza kuwa taasisi hiyo imekuwa ikinufaika na upatikanaji wa maji ya uhakika. Amesema hali hiyo imewezesha chuo chenye zaidi ya wanafunzi 400 kudumisha usafi wa mazingira na mazingira bora ya kujifunzia.

Kwa upande wake, Ibrahim Hakimu Faraji, aliyepokea tuzo ya mdau bora anaeshirikiana na Mamlaka kwa utoaji taarifa juu ya changamoto zinazohusu maji, amesema ushirikiano kati ya wananchi na mamlaka ni muhimu katika kulinda miundombinu ya maji. Amesisitiza umuhimu wa kutoa taarifa mapema pindi changamoto zinapojitokeza ili hatua zichukuliwe kwa haraka.

Amesisitiza kuwa mamlaka haiwezi kumzidishia bili mteja, kwani kila mteja hulipa kulingana na kiwango cha maji anachotumia, huku akiwataka wananchi kuendelea kulipa bili kwa wakati na kushirikiana na mamlaka katika kulinda miundombinu ya maji kwa manufaa ya wote.

Katika kuadhimisha Wiki ya Maji Duniani inayoendelea kuanzia Machi 16 hadi 22 chini ya kauli mbiu isemayo “Maji na Jinsia”, SOUWASA imeendelea na shughuli mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari pamoja na zoezi la upandaji miti katika bonde la Mto Luhira, ikiwa ni sehemu ya kulinda vyanzo vya maji na kuhakikisha huduma inaendelea kuwa endelevu.








Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam — Fundi wa mashine za photocopy kutoka Temeke, Mtega Thadei (33), sasa ana matumaini mapya ya kukuza kipato chake baada ya kushinda pikipiki kupitia kampeni ya #ShindaBoda ya PigaBet.

Kwa muda mrefu, Thadei alikumbana na changamoto ya usafiri wakati wa kuwafikia wateja wake, hali iliyokuwa ikiathiri kasi ya kazi na mapato yake. Akitumia daladala, mara nyingi alichelewa kufika kwa wateja na kupoteza fursa za kazi.

Akizungumza baada ya ushindi huo, Thadei alisema pikipiki hiyo itabadilisha namna anavyofanya kazi na kumwezesha kuwafikia wateja kwa haraka zaidi.

“Itanisaidia kuwafikia wateja kwa muda muafaka. Ilikuwa shida sana kufika kwa daladala, lakini sasa nitaweza kutoa huduma nzuri zaidi,” alisema.

Thadei, ambaye ni baba wa watoto watatu, alisema pia ushindi huo utamsaidia kuongeza kipato na kuboresha maisha ya familia yake.

“Kipato kitaongezeka, nitaweza ku-support familia yangu vizuri zaidi,” aliongeza.

Kampeni ya #ShindaBoda ya PigaBet inaendelea kutoa pikipiki kwa washindi kila wiki, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwapa wachezaji nafasi ya kushinda na kubadilisha maisha yao kupitia zawadi zinazoweza kuingiza kipato.

Kupitia ushindi huo, Thadei anaamini sasa ana nafasi ya kusukuma shughuli zake mbele kwa ufanisi zaidi na kujijengea msingi imara wa maisha.

18+ | Cheza kwa uwajibikaji

NA VICTOR MASANGU, PWANI

Mamlaka ya mapato (TRA) Mkoa wa Pwani katika kurudisha fadhila kwa jamii imeamua kuandaa Iftar maalumu kwa ajili ya kufuturisha makundi mbali mbali ikiwemo watoto yatima, viongozi wa madhehebu ya dini, viongozi wa serikali ikiwa pamoja na wananchi kutoka maeneo ya Mkoa wa Pwani.

Tukio hilo maalumu la Iftar limefanyika katika viwanja vya nje ya Ofisi ya TRA na kuongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Pwani Khamis Mtupa pamoja na kuhudhuliwa na viongozi wengine wa dini pamoja na watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kutoka kituo cha Fadhila kilichopo kata ya Misigusugu Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha.

Katika tuki hilo Sheikh wa Mkoa wa Pwani Khamis Mtupa ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi hakusita kuupongeza kwa dhati uongozi mzima wa TRA Mkoa wa Pwani kwa kuamua kurudish fadhila kwa jamii na kukusanya makundi mbali mbali ikiwemo watoto yatima na kula nao chakula cha jioni ikiwa ni moja na nguzo muhimu sana hasa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

"Kwa upande wangu mimi kipekee nipende kuchukua fursa hii kuwashukuru kwa dhati uongozi mzima wa TRA pamoja na meneja wake kwa kuona umuhimu mkubwa wa kutukutanisha siku ya leo katika hili tuko la Iftari kwa kweli mmefanya jambo la msingi sana na kingine nimependa mmekusanya makundi tofauti ikiwemo na watoto yatima ambao tumejumuika nao hapa katika tukio hilo na Mungu awabariki sana na muendelee na moyo huu wa kujitolea,"amebainisha Sheikh Mtupa.

Pia katika hatua nyingine amebaainisha kwamba katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadani taasisis na watu mbali mbali wanapaswa kufanya matendo ya huruma kwa wahitaji ikiwemo suala la kuwafuturisha watu wenye uhitaji na kuweza kutoa misaada mbaali mbali ambayo itaweza kuwasaidia walengwa na kwamba zoezi hilo liwe endelevu ikiwemo kusaidia jamii.

Kadhalika Sheikh Mtupa ameipongeza TRA Mkoa wa Pwani kwa kuweka mikakati madhubuti ambayo imeweza kusaidia kwa kiassi kikubwa katika suala zima la kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ambayo yanapelekea kuleta mabadiliko makubwa katika maendeleo kwa wananchi.

Kwa upande wake Meneja wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani Masawa Masawa amesema kwamba wameamua kufanya tukio la Iftar hiiyo na kuwakutanisha makundi mbali mbali ikiwa ni moja ya kurudisha fadhila kwa jamii pamoja na kukutana na watoto yatima na kula nao chakula cha jioni.

Meneja huyo amesema kwamba lengo kubwa la TRA Mkoa wa Pwani ni kuendelea kushirikiana begaa kwa bega na jamii katika mambo mbali mbali ikiwemo kukutana kwa pamoja na kubadilishanaa mawazo pamoja naa kula cha jioni kwani ni moja ya kuongeza wigo mpana ya katika kujenga mahusiano mazuri kwa jamii.,

Nao baadhi ya watoto yatima ambao wamehudhulia katika tukio hilo wamesema wamefurahishwa na uongozi mzima wa TRA kwa kuweza kuwakumbuka katika kuwakutanisha katika Iftar hiyo na kusema kwamba wamejisikia furaha na amani ya kukutana na jamii nyingine.







Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile, ameshiriki Mkutano wa Kimataifa wa masuala ya Uchukuzi (NCT), mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Gallagher Estate, uliopo Johannesburg, Afrika Kusini. Mkutano huo ulifunguliwa na Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa.

Sambamba na ushiriki huo, Naibu Waziri pia ameshiriki katika Mjadala wa Mawaziri wa Uchukuzi ukiwa na Mada isemayo: “Leadership and Governance in the Implementation of an Integrated, Sustainable and Safe Transport System that Promotes Inclusive Economic Growth, Job Retention and Social Development in Southern Africa.”

Wakati wa Mjadala huo, Naibu Waziri ameeleza hatua mbalimbali zilizofikiwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuendeleza miundombinu, ikiwemo Uwekezaji mkubwa katika Reli ya Kisasa (SGR); maboresho ya Bandari; Viwanja vya Ndege na miundombinu ya Barabara.

Aidha, ameeleza kuwa Serikali ya Tanzania inaendelea kuweka mazingira rafiki ya Uwekezaji na kuwakaribisha Wawekezaji kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya Sekta ya Uchukuzi, kwa lengo la kuimarisha biashara; kuongeza ushindani wa kiuchumi na kukuza maendeleo ya kikanda.












Top News