Na Victor Masangu,Kibaha

ALIYEWAHI kuwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Sophia Simba ameitaka jamii kuwawezesha kiuchumi vijana wa kiume ambao wamesahaulika.

Simba ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya Kikundi cha Super Women 2017 na kuwa baada ya wanawake kufanikiwa vijana wakiume nao waangaliwe.

Amesema kuwa kwa muda mrefu jamii iliwekeza kudai haki za wanawake ambapo kwa sasa wamepiga hatua ya kimaendekeo baada ya nguvu kubwa kutumika huku wale wa kiume wakiwa wamesahaulika.

Naye mwanzilishi wa kikundi hicho Betty Msimbe amesema kuwa wamepata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kukopeshana fedha kwa riba nafuu kupitia mfuko wa kikundi kwa fedha wanazoweka ambapo mkopo ni mara tatu ya fedha waliojiwekea.

Kwa upande wake mwenyekiti kikundi hicho Betha Kimambo amesema kuwa wanatarajia kuanzisha mradi wa kukodisha vyombo ili kuongeza kipato ndani ya kikundi.

Naye mratibu wa kikundi hicho Maria Msimbe amesema kuwa wanahamasisha wanawake kujiunga ili kujikomboa kiuchumi.



Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

SERIKALI imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kuhakikisha Watu Wenye Ulemavu wanapata nafasi sawa katika nyanja zote za maendeleo, ikiwa ni pamoja na kijamii, kiuchumi na kisiasa, kupitia sera, sheria na mipango jumuishi inayotekelezwa nchini.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichowakutanisha viongozi wa vyama vya Watu Wenye Ulemavu na mashirika yasiyo ya kiserikali kujadili utekelezaji wa sera, sheria na miongozo ya ujumuishaji nchini.

Amesema hatua kubwa zimeendelea kuchukuliwa katika kuhakikisha hakuna mwananchi anayeachwa nyuma, ambapo Sera ya Taifa ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2004 pamoja na Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 zimekuwa msingi muhimu wa utekelezaji wa haki na usawa kwa kundi hilo.

“Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa kila sera, mpango na huduma inayotekelezwa nchini inazingatia ujumuishaji wa Watu Wenye Ulemavu tangu hatua ya upangaji, utekelezaji, ufuatiliaji hadi tathmini, ili kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma,” amesema Dkt. Jim Yonazi.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa mawasiliano bora na uratibu imara kati ya Serikali, vyama vya Watu Wenye Ulemavu na mashirika yasiyo ya kiserikali, akibainisha kuwa ushirikiano huo ni msingi muhimu wa kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Amesema ujumuishaji si jukumu la sekta moja pekee, bali ni wajibu wa kila taasisi, kila sekta na kila mdau wa maendeleo. “Tunapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha huduma zote zinamfikia kila mwananchi kwa usawa,” alisisitiza.

Dkt. Yonazi pia ametoa wito wa kuimarishwa kwa mifumo ya mawasiliano inayowezesha Watu Wenye Ulemavu kupata taarifa kwa urahisi, ikiwemo matumizi ya lugha ya alama, maandishi ya Breli, teknolojia saidizi na mifumo mingine jumuishi.

“Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na vyama vya Watu Wenye Ulemavu pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali katika kutoa huduma za utetezi wa haki, elimu kwa umma, mafunzo ya kujenga uwezo, uwezeshaji kiuchumi, huduma za afya, elimu jumuishi na ushauri wa kitaalamu,” amesema.

Katika hatua nyingine, Dkt. Yonazi amesema kuwa pamoja na jitihada ambazo Serikali imeendelea kuzichukua, bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji ushirikiano wa wadau wote.

Amesema changamoto hizo ni pamoja na uelewa usioridhisha kuhusu masuala ya ujumuishaji katika baadhi ya sekta, utekelezaji usiofanana wa sera na sheria, pamoja na changamoto za upatikanaji wa huduma jumuishi zinazokidhi mahitaji ya Watu Wenye Ulemavu.

“Kutokana na hali hiyo, kikao hiki ni muhimu sana kwa kuwa kinatoa fursa ya kujadili kwa kina namna bora ya kuimarisha ujumuishaji wa huduma katika sekta zote.”

Awali, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Bi. Tungi Mwanjala, ameiomba Serikali kuendelea kuangalia uwezekano wa kuwatambua watoto wa wazazi wenye ulemavu ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali za maendeleo, ikiwemo kupata mikopo ya elimu ya juu kwa urahisi.

Bi.Mwanjala ameeleza kuwa, Serikali imepiga hatua kubwa kwa kukamilisha muongozo na mfumo wa utambuzi wa watu wenye ulemavu, lakini bado kuna haja ya kupanua utambuzi huo kwa watoto wa wazazi wenye ulemavu.

"Tunashukuru Serikali kwa kukamilisha muongozo na mfumo wa kutambua watu wenye ulemavu. Hata hivyo, tunaomba pia watoto wetu watambuliwe kupitia mfumo maalumu utakaowezesha kupata vitambulisho, jambo litakalowarahisishia kupata mikopo ya elimu ya juu na fursa nyingine za maendeleo ikiwamo ajira kwa kuzingatia utaratibu uliopo," amesema.












Na Janeth Raphael MichuziTv 

Sekta ya Maliasili na Utalii imetajwa kuwa miongoni mwa sekta muhimu zinazochangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya taifa kupitia ukuaji wa uchumi, upatikanaji wa ajira, mapato ya serikali na ustawi wa jamii zinazoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi.

Hata hivyo, mafanikio ya sekta hiyo yameendelea kuambatana na changamoto ya kuhakikisha kuwa uhifadhi wa wanyamapori unaendana na ulinzi wa maisha, mali na shughuli za kiuchumi za wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi. Kutokana na hali hiyo, Serikali imeendelea kuweka kipaumbele katika kutafuta suluhisho endelevu la migongano kati ya binadamu na wanyamapori wakali na waharibifu.

Akizungumza leo jijini Dodoma wakati akimwakilisha Waziri wa Maliasili na Utalii kufunga Mkutano wa Mwaka wa Wahifadhi wa Wanyamapori nchini, Mkurugenzi wa Wanyamapori Tanzania, Dkt. Alexander Lobora, amesema Serikali imeimarisha mifumo ya usimamizi wa migogoro hiyo kupitia sera mbalimbali, mikakati pamoja na matumizi ya teknolojia ya kisasa.

Amesema mfumo huo mpya unalenga kuongeza uwazi na uwajibikaji katika mchakato wa kushughulikia madai ya fidia ya “kifuta jasho na machozi” kwa wananchi wanaoathirika na wanyamapori.

Dkt. Lobora amesisitiza kuwa kuanzia tarehe 1 Julai 2026, Wizara haitapokea tena madai ya fidia kwa njia ya karatasi, bali yote yatapokelewa kupitia mfumo wa kidigitali ulioboreshwa. Ameelekeza maafisa wote kuhakikisha wanatumia mfumo huo kikamilifu katika maeneo yao ya kazi, kuingiza taarifa kwa usahihi na kuwasilisha kwa wakati.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya mfumo huo, kuhakikisha taarifa zote zinakuwa sahihi, pamoja na kuhakikisha mawasiliano ya waombaji yanathibitishwa ipasavyo kupitia namba za simu zinazotambulika. Pia amekumbusha watumishi wa umma kuzingatia maadili na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Wanyamapori, Dkt. Fortunata Msoffe, amesema ongezeko la shughuli za kibinadamu kuelekea maeneo ya hifadhi na kwenye shoroba za wanyamapori limechangia kuongezeka kwa matukio ya migogoro hiyo na kusababisha madhara kwa jamii.

Ameeleza kuwa Wizara imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kupunguza changamoto hizo, ikiwemo kufanya doria za mara kwa mara, kuongeza kasi ya mwitikio wa matukio, kutoa elimu kwa wananchi na kuimarisha usimamizi wa maeneo ya hifadhi pamoja na shoroba za wanyamapori kwa kutumia teknolojia za kisasa kufuatilia mienendo ya wanyama.

Kwa upande wa Serikali za Mitaa, Afisa Misitu Mkuu kutoka TAMISEMI, Rogasian Philip, ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kuendelea kutekeleza sera ya ugatuaji wa madaraka, akisema hatua hiyo imeongeza ufanisi katika usimamizi wa rasilimali za misitu na wanyamapori.

Naye Afisa Kilimo wa Kata ya Kiambai, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Anna Roki, amesema mfumo huo mpya utarahisisha utendaji kazi ikilinganishwa na mfumo wa awali wa kutumia fomu za karatasi, ambao ulikuwa unachukua muda na kuongeza ugumu wa huduma kwa wananchi.

Ameongeza kuwa mfumo wa kidigitali utasaidia wananchi kupata stahiki zao kwa haraka zaidi na kupunguza malalamiko yaliyokuwa yakijitokeza hapo awali.

Serikali imesisitiza kuwa matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa migogoro ya binadamu na wanyamapori ni hatua muhimu kuelekea ufanisi zaidi, uwazi na uboreshaji wa huduma kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi.









Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kulia), akisalimiana na Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo, aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, akiambatana na wajumbe wengine wa benki hiyo, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili kati ya Benki hiyo na Serikali ya Tanzania ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
WAZIRI wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema Tanzania inaiona Benki ya Afrexim kama mshirika wa kimkakati katika safari ya mageuzi ya kiuchumi ya nchi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

Akizungumza Dar es Salaam wakati wa kikao na ujumbe wa Afreximbank ulioongozwa na Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Benki hiyo, Bw. Humphrey Nwugo, aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, Balozi Omar alimkaribisha rasmi na kumpongeza kwa uteuzi wake mpya, akieleza matumaini ya Tanzania kuimarisha zaidi uhusiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na taasisi hiyo ya kifedha ya Afrika.

Alisema kwa miaka mingi Afreximbank imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi muhimu za kifedha barani Afrika, huku Tanzania ikiwa sehemu ya safari hiyo na kwamba Serikali inathamini mchango wa benki hiyo katika kusaidia biashara, miundombinu, ukuaji wa viwanda na maendeleo ya sekta binafsi.

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, Tanzania imefarijika na dhamira ya Afreximbank ya kuhamasisha dola za Marekani bilioni moja zaidi ndani ya miezi 12 ijayo kwa ajili ya uwekezaji nchini, hasa katika sekta za viwanda, miundombinu na biashara ndogo na za kati.

Aidha, alisema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano unalenga kujenga uchumi shindani unaoongozwa na sekta binafsi na kwamba ili kufikia lengo hilo kutahitaji ubia madhubuti, uwekezaji wa muda mrefu na ushirikiano wa karibu na taasisi kama Afreximbank.

Alibainisha kuwa pamoja na mafanikio yaliyopo, bado kuna nafasi kubwa ya kupanua ushirikiano katika maeneo ya kimkakati yakiwemo miundombinu, viwanda, afya na uwezeshaji wa biashara. Aliongeza kuwa kikao hicho ni fursa muhimu ya kubadilishana mawazo kuhusu maeneo ya maslahi ya pamoja na kutafuta njia za vitendo za kuimarisha ushirikiano huo.
Alitaja maeneo yanayohitaji msukumo zaidi kuwa ni kusaidia ukuaji wa viwanda, kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi, kuendeleza mtaji watu na kuongeza ushindani wa biashara ya Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Benki ya Afriexim, Bw. Humphrey Nwugo, aliipongeza Tanzania kwa hatua kubwa iliyopiga kiuchumi na kuaghidi kuwa Benki yake iko tayari kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu ili kufikia matarajio yake ya agenda ya kufikia uchumi wa dola za Marekani trilioni moja kupitia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Alisema kuwa Afriexim ina nia ya kuwekeza kwenye miradi ya kimkakati ikiwemo mafuta, madini, chuma, magadi na imejipanga kuendelea kuisaidia sekta binafsi kwa kuipatia mikopo na mitaji ili iweze kuchangia katika kuwekeza kwenye sekta zitakazochochea zaidi ukuaji wa uchumi ikiwemo uongezaji wa thamani ya bidhaa.

Benki ya Afrexim imeendelea kuwa mshirika muhimu wa Tanzania katika kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo, ikitoa fedha na dhamana zenye thamani ya mabilioni ya dola za Marekani kwa ajili ya miundombinu, sekta ya fedha na miradi ya kimkakati.

Mwaka 2018 Benki ya Afrexim ilitoa dhamana yenye thamani ya dola za Marekani milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere katika bonde la Rufiji, hatua iliyowawezesha wakandarasi kutoka Misri kutekeleza mradi huo.

Mbali na hilo, benki hiyo imetoa jumla ya dola za Marekani milioni 700 kusaidia miradi mbalimbali ya miundombinu, ikiwemo sehemu za kwanza hadi za nne za reli ya kisasa ya SGR.

Katika sekta ya fedha, Benki ya Afrexim imeidhinisha jumla ya dola za Marekani milioni 230 kwa mabenki ya biashara nchini Tanzania. Vilevile, imewezesha sekta binafsi kwa kutoa mikopo na huduma za kifedha zenye thamani ya dola za Marekani milioni 80.


Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa kikao chake na Ujumbe wa Benki ya Afrexim ukiongozwa na Mkurugenzi wake Mpya wa Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo (hayupo pichani), aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili kati ya Benki hiyo na Serikali ya Tanzania ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.




Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa tatu kulia), Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo (wa tatu kushoto), na maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha na Benki ya Afrexim, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Huduma za Elimu nchini Zambia, Dkt. Kelvin Mambwe (wa pili kulia), akibadilishana nakala za Mkataba wa Ushirikiano (MoU) uliotiwa saini na Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Food4Education, Bi. Wawira Njiru (wa pili kushoto), kufuatia kurasimishwa kwa ushirikiano wa muda mrefu wa kutoa msaada wa kiufundi unaolenga kuimarisha na kupanua mpango wa kitaifa wa lishe shuleni nchini Zambia. Wanaoshuhudia ni Katibu Mkuu wa Utawala katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Lillian Kapusana (wa kwanza kulia), na Mwakilishi wa Food4Education nchini Zambia, Bw. Brian Kayongo (wa kwanza kushoto). Picha: Kwa Hisani.

WIZARA ya Elimu ya Zambia na shirika la Food4Education (F4E) zimetia saini Mkataba wa Ushirikiano (MoU) wenye lengo la kuimarisha mpango wa kitaifa wa lishe kwa wanafunzi wa shule za msingi za umma nchini Zambia. Kwa sasa, mpango huo unawanufaisha wanafunzi milioni 4.6 katika shule 8,193, huku serikali ikilenga kuongeza idadi hiyo hadi wanafunzi milioni 5.6 ifikapo mwisho wa mwaka 2026.

Mkataba huu unaweka msingi wa ushirikiano wa muda mrefu wa kiufundi, ambapo Food4Education itaunga mkono Wizara ya Elimu katika maeneo matano muhimu: uratibu wa sera na taasisi; usanifu wa programu na mifumo ya utekelezaji; matumizi ya data, teknolojia za kidijitali na ubunifu; upangaji wa bajeti, ufadhili na matumizi bora ya rasilimali; pamoja na maendeleo ya miundombinu na vifaa. Ushirikiano huu unalenga kusaidia Zambia kujenga mfumo endelevu wa lishe shuleni unaoongozwa na serikali, unaochangia kuboresha elimu, lishe ya watoto, kuimarisha kilimo cha ndani na kuchochea ukuaji wa uchumi.

"Mpango wa lishe shuleni kwa wote ni uwekezaji katika mustakabali wa watoto wetu na maendeleo ya uchumi wa taifa. Ushirikiano huu na Food4Education utatusaidia kuimarisha mifumo inayohakikisha uwekezaji huu unazalisha matokeo ya kudumu kwa Zambia," alisema Dkt. Kelvin Mambwe, Katibu Mkuu Mwandamizi wa Huduma za Elimu nchini Zambia.

Afrika hupoteza hadi asilimia 16.5 ya Pato la Taifa (GDP) kila mwaka kutokana na athari za utapiamlo kwa watoto. Hata hivyo, tafiti zinaonyesha kuwa kila dola moja inayowekezwa katika mpango wa lishe shuleni inaweza kuzalisha hadi dola 20 za faida kwa jamii na uchumi. Wakati theluthi mbili ya serikali za Afrika tayari zimetenga bajeti mahsusi kwa ajili ya lishe shuleni, changamoto iliyopo sasa si iwapo nchi zinapaswa kuwekeza, bali ni jinsi ya kubuni na kutekeleza programu hizo kwa ufanisi na kwa kiwango kikubwa. Mifumo madhubuti inayozingatia mazingira ya ndani ndiyo inayogeuza dhamira kuwa matokeo halisi.

"Zambia inaonyesha mfano ambao bara zima linaweza kuufuata. Kwa kuwekeza rasilimali zake na kushirikisha wizara mbalimbali katika kuwahudumia watoto wake, nchi hii inajenga mpango wa lishe shuleni kama nguzo muhimu ya maendeleo ya kiuchumi inayokuza kilimo, kuunda ajira zenye hadhi, kujenga mtaji wa watu na kuchochea ukuaji wa uchumi. Food4Education ipo hapa kuunga mkono juhudi ambazo tayari zimeanzishwa na uongozi wa Zambia, na kusaidia kuharakisha maendeleo ya uchumi unaotokana na lishe shuleni barani Afrika," alisema Wawira Njiru, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Food4Education.

Mpango wa lishe shuleni unaoongozwa vizuri na serikali huleta manufaa yanayozidi utoaji wa chakula kwa wanafunzi. Unaunganisha wakulima wadogo na masoko ya uhakika, huongeza ajira na kipato katika mnyororo mzima wa thamani wa chakula—hasa kwa wanawake na vijana—huimarisha mifumo ya chakula ya ndani na kuendeleza matumizi ya teknolojia za kidijitali katika utoaji wa huduma za umma. Ushirikiano huu unalenga kuonyesha namna serikali za Afrika zinavyoweza kujenga, kufadhili na kuendesha mifumo ya umma iliyo endelevu kwa kiwango kikubwa.

Kampuni ya mawasiliano ya Halotel Tanzania imezindua rasmi na kwa kishindo ushiriki wake katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu kama SabaSaba, ikiwa na uwepo thabiti unaoambatana na uzoefu wa kipekee wa kidigitali katika banda lake la maonesho.

Ikiwa chini ya kauli mbiu “Teknolojia kutoka Moyoni”, Halotel inaendelea kuonesha dhamira yake ya kuendeleza mageuzi ya kidigitali nchini Tanzania kupitia huduma bunifu za mawasiliano, kidigitali na kifedha zinazolenga kurahisisha maisha ya kila siku na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Wageni wanaotembelea banda la Halotel watapata nafasi ya kujionea suluhisho mbalimbali za kisasa zikiwemo huduma za mtandao wa 5G, huduma ya intaneti ya kasi ya juu ya HaloFibre, suluhisho za kidigitali kwa biashara pamoja na huduma rahisi za kifedha zinazotolewa kupitia HaloPesa.

Kupitia HaloPesa, wateja wanaendelea kufurahia huduma salama, rahisi na zenye ufanisi za kifedha kidigitali zikiwemo kutuma na kupokea fedha, kuweka na kutoa fedha, pamoja na kufanya malipo kwa urahisi, hatua inayochangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha ujumuishaji wa kifedha nchini.

Kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya HaloPesa, Halotel imeandaa zawadi maalum, ofa za kipekee na shughuli mbalimbali za kuwashirikisha wateja, zinazolenga kuboresha zaidi uzoefu wa wageni katika kipindi chote cha maonesho.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho katika banda la Halotel, Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara wa Halotel Tanzania, Bw. Abdallah Salum, amesema:

“Saba Saba inatupatia jukwaa muhimu la kuwasiliana moja kwa moja na wateja wetu na kuonesha ubunifu unaoendelea kuboresha maisha yao kupitia teknolojia.”

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Halotel Tanzania, Bi. Tran Thi Thuy Dung, aliendelea kusisitiza dhamira ya kampuni katika ubunifu na maendeleo ya kidigitali akisema:

“Halotel inaendelea kujitolea kuwekeza katika suluhisho bunifu zinazoboresha uzoefu wa wateja na kuharakisha mageuzi ya kidigitali nchini Tanzania. Kupitia maonesho haya, tunawapa wageni nafasi ya kushuhudia kwa vitendo huduma zetu na kuona athari zake halisi katika maisha ya kila siku.”

Kwa upande wa HaloPesa, Meneja wa Masoko, Bi. Aidat Lwiza, alibainisha:

“Kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya HaloPesa, tunafuraha kuleta ofa na uzoefu wa kipekee kwa wateja ili kuimarisha zaidi upatikanaji wa huduma za kifedha kidigitali zilizo rahisi na zenye uhakika katika kipindi chote cha maonesho ya SabaSaba.”

Halotel inawaalika wageni wote, wadau na washiriki wa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam kutembelea banda lao na kujionea ubunifu wa huduma pamoja na ofa maalum zitakazopatikana katika kipindi chote cha maonesho kuanzia 28 Juni hadi 13 Julai 2026.
















































Katika juhudi za kuhakikisha Tanzania inafikia azma ya kuwa nchi ya kijani ifikapo mwaka 2050, Shirika la INADES-Formation Tanzania kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira limeandaa kikao kazi cha kuandaa Mpango wa Usimamizi wa Mazingira wa Wilaya ya Bahi, kwa kushirikisha wataalamu kutoka Wilaya za Chemba na Kondoa.

‎Akifungua kikao hicho Leo katika ofisi ya Makamu wa Rais, Mtumba mjini Dodoma, Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira, Dk. Paul Deogratius, alisema ushiriki wa Wilaya za Chemba na Kondoa utasaidia kubadilishana uzoefu katika mchakato wa kuandaa mpango huo kwa Wilaya ya Bahi.

‎‎Alieleza kuwa mipango ya usimamizi wa mazingira katika ngazi ya wilaya ni takwa la kisheria na ni nyenzo muhimu katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za mazingira zinazozikabili halmashauri nchini.

‎"Kitaifa, zimetambuliwa zaidi ya changamoto 13 za mazingira, huku kila wilaya ikiwa na changamoto zake kulingana na mazingira na shughuli za kiuchumi zinazofanyika katika eneo husika. Hivyo, uwepo wa mpango wa usimamizi wa mazingira ni muhimu katika kutoa mwongozo wa namna ya kuzikabili changamoto hizo," alisema Dk. Deogratius.

‎‎Aliongeza kuwa maandalizi ya mpango huo yataisaidia Tanzania kutekeleza mikakati ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kufikia lengo la kuwa nchi ya kijani ifikapo mwaka 2050.

‎‎Kwa upande wake, Mkurugenzi wa INADES-Formation Tanzania, Bi. Jacqueline Nicodemus, alisema ushirikiano na Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira ni muhimu ili kuhakikisha mipango hiyo inaandaliwa kwa kuzingatia miongozo, sera na mikakati ya kitaifa ya usimamizi na uhifadhi wa mazingira.

‎Aidha, aliomba Ofisi hiyo kushiriki katika uzinduzi wa mipango ya usimamizi wa mazingira ya Wilaya za Chemba na Kondoa, akisema ushiriki huo utatoa msukumo na kuhamasisha wadau mbalimbali kutambua umuhimu wa kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya nchi.

‎‎Nao washiriki wa kikao hicho walisisitiza kuwa mipango ya usimamizi wa mazingira katika wilaya hizo inapaswa kuendana na vipaumbele vya kitaifa, ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, mipango kabambe ya maendeleo, Sera ya Taifa ya Mazingira pamoja na miongozo mingine ya uhifadhi wa mazingira.

‎‎Vilevile, walieleza umuhimu wa kupata mwongozo wa kitaalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira katika hatua za kuandaa na kupitia rasimu ya Mpango wa Usimamizi wa Mazingira wa Wilaya ya Bahi, ili kuhakikisha unakidhi viwango na matakwa ya kitaifa.








Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Bodi ya Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA), Victor Tesha, amewataka wanakwaya wa Flying Family Choir (FFC) kuanzisha miradi ya maendeleo itakayokuwa chanzo cha kuongeza kipato na kuwasaidia kujikomboa kutoka katika umaskini.

Tesha amesema hayo jana, Jumapili, katika tamasha la kwaya hiyo lijulikanalo FFC Corporate Encore 2026, lililofanyika katika Ukumbi wa Cardinal Rugambwa, Oysterbay, jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na watu mbalimbali, akiwemo Askofu wa Jimbo Katoliki la Morogoro, Lazarus Msimbe.

FFC Kwaya inaundwa na wanakwaya kutoka madhehebu matatu ya Kikristo ambayo ni Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Kanisa la Anglikana na Kanisa Katoliki, wakishirikiana kupitia huduma ya uimbaji wa injili.

Akizungumza katika tamasha hilo, Tesha ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA), amesema wanakwaya wengi bado wanakabiliwa na changamoto za kiuchumi na hali zao za maisha si za kuridhisha, hivyo kuna umuhimu wa kuwa na mradi endelevu utakaoweza kuwanufaisha hata katika kipindi cha miaka 10 ijayo.

Amesema uwepo wa mradi mkubwa wa kwaya utasaidia kujenga ustawi wa wanakwaya na kuhakikisha huduma ya uinjilishaji inaendelea sambamba na kuimarika kwa maisha yao ya kiuchumi.

"Ningependa kuona wanakwaya wakifikiria zaidi kuhusu uwekezaji na miradi itakayowasaidia kujikomboa kiuchumi. Wengi bado hali zao si nzuri, hivyo tunahitaji kuwa na mradi ambao hata baada ya miaka 10 utakuwa umebadilisha maisha ya wanakwaya," amesema Tesha.

Aidha, ameahidi kukaa pamoja na bodi ya kwaya hiyo ili kujadili namna bora ya kupata mradi mkubwa na wenye tija ambao utalenga kuinua vipato vya wanakwaya na kuimarisha ustawi wao wa kiuchumi.

Kwa upande wake, Katibu wa kwaya hiyo, Brigita James amesema pamoja na kwaya hiyo kumiliki vifaa vyake vya muziki, bado inahitaji kuwa na chombo chake cha usafiri kitakachorahisisha shughuli za uinjilishaji na usafiri wa wanakwaya wanapopata mialiko ya kuhudumu katika maeneo mbalimbali.

Amesema upatikanaji wa chombo hicho utapunguza gharama za usafiri na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za kwaya, hususan katika huduma za uinjilishaji zinazofanyika ndani na nje ya Dar es Salaam.

Naye Mwenyekiti wa kwaya hiyo, Innocent Fundisha amesema kwaya hiyo imefanikiwa kufanya matamasha 10 tangu kuanzishwa kwake, jambo linalowapa fahari kutokana na kuendelea kudumu katika upendo, amani na mshikamano miongoni mwa wanakwaya wake.

Fundisha amesema wanakwaya wa FFC wanatoka katika madhehebu matatu ya Kikristo ambayo ni KKKT, Anglikana na Kanisa Katoliki, lakini tofauti zao za kimadhehebu hazijawahi kuwa kikwazo katika huduma yao ya uimbaji.

Amesema umoja, upendo na mshikamano walioujenga ni ishara kuwa licha ya kutofautiana madhehebu, wote wanamuabudu Mungu mmoja katika roho na kweli, huku wakitumia muziki wa injili kuhubiri amani na kuimarisha ushirikiano miongoni mwa waumini.









Jeshi la Polisi Tanzania lingependa kujulisha kuwa, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura, amemhamisha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Twaha Juma Lulengelule ambaye alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) Mkoa wa Tabora kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) Mkoa wa Tabora.


Uhamisho huo umefanyika ili kujaza nafasi iliyokuwa wazi baada ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Richard George Abwao, kufariki dunia Juni 20, 2026.


Imetolewa na;

Msemaji wa Jeshi la Polisi

Makao Makuu ya Polisi

Dodoma,Tanzania

Na Mwandishi Wetu
NDOTO za vijana wa Tanzania wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mbalimbali nje ya nchi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 zimeingia hatua muhimu baada ya Global Education Link kuwakutanisha wanafunzi hao pamoja na wazazi na walezi wao kwa ajili ya kuhakiki nyaraka na kukamilisha maandalizi ya safari.
Kikao hicho kilichofanyika katika Makao Makuu ya Global Education Link, Dar es Salaam, kililenga kuhakikisha kila mwanafunzi anakuwa na nyaraka sahihi, taarifa za kutosha na maandalizi muhimu kabla ya kuondoka nchini kwenda kuanza masomo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel, alisema lengo kuu la kikao hicho ni kuhakiki na kukamilisha nyaraka muhimu za wanafunzi, kujibu maswali ya wazazi na kuhakikisha changamoto zinazoweza kuchelewesha safari zinapatiwa ufumbuzi mapema.

Mollel alisema wazazi na walezi wanapaswa kujiridhisha kuhusu utambuzi wa kisheria wa chuo kilichochaguliwa kwa kupata uthibitisho rasmi kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, ili kuhakikisha sifa zitakazopatikana baada ya kuhitimu zinatambuliwa na mamlaka husika nchini.

Kwa mujibu wa Mollel, safari ya masomo nje ya nchi haiishii katika kupata nafasi ya kujiunga na chuo pekee, bali inahitaji maandalizi kuhusu visa, malazi, usafiri, usalama, sheria, utamaduni wa nchi husika na uwezo wa mwanafunzi kuishi kwa nidhamu na uwajibikaji.

Kwa upande wao, wazazi na walezi walioshiriki kikao hicho walisema wameridhishwa na namna Global Education Link ilivyowahudumia na kuwapatia majibu kuhusu hatua mbalimbali za udahili na maandalizi ya safari.
Mmoja wa walezi hao, Asuba Omary kutoka Zanzibar, alisema kikao hicho kimemsaidia kufahamu mambo ya kuzingatia kabla ya mzazi kuamua kumsomesha mtoto katika chuo kikuu cha nje ya Tanzania.







Top News