WATAALAMU wa kilimo cha korosho nchini wamewaasa wakulima kuanza kuandaa mashamba yao kwa kufuata hatua kuu tatu na muhimu katika kuleta tija kwenye uzalishaji wa zao hilo.
Wakizungumza na waandishi wa habari Mkoani Mtwara, wataalamu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Nchini (TARI), kituo cha Naliendele wamesema zipo hatua kuu tatu ambazo wakulima wanapaswa kufuata ili kuongeza tija kwenye mavuno ya zao la korosho nchini.
"Hatua ya kwanza ni hatua ambayo mikorosho inakuwa imetulia baada ya kipindi cha mavuno, mikorosho inakuwa imetulia, ambapo ni kipindi hiki, hatua ya pili ni hatua ya mikorosho kuchipua na hatua ya tatu ni mikorosho kuanza kuzaa," amesema mtafiti na Mtaalamu wa Sayansi ya Udogo na Mimea kutoka TARI Naliendele Abdallah Makale.
Amesema hatua ya kwanza, wakulima wanapaswa kutibua mashamba ili kuruhusu mikorosho ipate maji kwa ajili ya kurutubisha majani ya uzalishaji.
"Lakini pia katika kipindi hiki ambapo mikorosho inakuwa imetulia, tunashuri wakulima kulima mazao kwenye hayo mashamba ya mikorosho, na tunahimiza zaidi mazao ya jamii ya kunde kama karanga , choroko na kunde," amesema.
Makale amesema kuchanganya mazao ya jamii ya kunde inasaidia mikorosho kupata maji na virutubisho na kufanya maua ya mikorosho kuwa imara kipindi cha kuchipua.
"Mikorosho isipopata maji na virutubisho itadondosha sana maua, inakuwa ya njano na wakati mwingine mbengu kuanguka," amesema.
Katika hatua ya pili Makale amesema wakulima wanapaswa kupogolea mikorosho ili kuipa nguvu, kwa kuondoa matawi ambayo yanakuwa hayazai.
Na hatua ya tatu ya uzalishaji, wakulima wanapaswa kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri wa hali ya hewa na kufuata utaratibu sahihi katika kuhudumia mikorosho ikiwemo kupulizia viuatilifu kudhibiti magonjwa ambayo huibuka wakati wa maua kuanza kuzaa korosho.
"Kipindi hiki tunashauri viuatilifu vya mazao ya korosho viandaliwe mapema ili kusaidia wakulima kujiandaa kupulizia mikorosho ambayo itakuwa imechipuka mapema kudhibiti wadudu," amesema.
Makale amesema wakulima wakizingatia hatua hizo tatu itawasaidia kuleta tija kwenye uzalishaji wa korosho nchini.
Katika hatua nyingine, Mtafiti na Mtaalamu wa mbegu bora kutoka TARI, Dwasi Gambo amewashauri wakulima kutoa mbegu bora za korosho kwa ajili ya kuleta tija zaidi kwenye zao la Korosho.
Dwasi amesema TARI Naliendele wanazo mbegu bora na miche ambayo iko tayari kwenda shambani na kuwataka wakulima ambao wanaanzisha mashamba mapya, kuboresha kutumia mbegu bora kutoka TARI NALIENDELE.
"Tunahimiza wakulima kutumia mbegu bora ili kupata mavuno mengi na yenye ubora zaidi, TAIR tuna mbegu bora zenye uwezo wa kuzalisha sana na kuhimili magonjwa na wadudu,"amesema.
Dwasi amesema pia kuwa mbegu bora kutoka TARI Naliendele zina uwezo wa kuhimili mabadiliko ya tabia nchi akisisitiza kuwa ni vyema wakulima kutumia mbegu hizo kuongeza uzalishaji wa korosho nchini.



.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

