-Singida

Wawekezaji wa ndani na nje ya Mkoa wa Singida wamehimizwa kujitokeza kuwekeza katika viwanda vya uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini ili kunufaika na rasilimali zilizopo, kuongeza ajira na kukuza uchumi wa wananchi.

Wito huo umetolewa na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Mhandisi Sabai Nyansiri, akisema mkoa huo una fursa kubwa ya uwekezaji katika sekta ya madini kutokana na ongezeko la shughuli za uchimbaji na mazingira bora ya uwekezaji yaliyowekwa na Serikali.

Akizungumza wakati wa ziara yake kwa wachimbaji wadogo katika Mgodi wa Matongo uliopo Kata ya Ikungi, Wilaya ya Ikungi, Mhandisi Nyansiri amesema Singida inaendelea kufanya vizuri katika uchimbaji wa madini ya dhahabu, shaba, madini ya ujenzi pamoja na jasi, hivyo kuwepo kwa viwanda vya uchenjuaji ni hatua muhimu ya kuongeza thamani ya madini hayo kabla ya kuuzwa.

Amesema uwekezaji katika viwanda vya uongezaji thamani wa madini utaongeza ajira kwa vijana na wanawake, kuongeza mapato ya Serikali na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa mkoa huo.

“Uwepo wa viwanda vya uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini utaongeza ajira, mapato ya Serikali na kukuza uchumi wa kila mwananchi,” amesema.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha masoko ya madini na kuendeleza biashara rasmi ya madini, akibainisha kuwa hatua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la mapato ya mkoa.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Singida ulipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 30 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kutoka Shilingi Bilioni 24 mwaka wa fedha 2024/2025, na hadi kufikia Desemba 2025 tayari umefanikiwa kufikia asilimia 54 ya lengo hilo sawa na Shilingi Bilioni 16.

Mhandisi Nyansiri amesema mafanikio hayo yanatokana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na kutoa kipaumbele kwa wachimbaji wadogo wazawa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mgodi wa Matongo, Japhet Madusa, ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wa wachimbaji wadogo katika maendeleo ya sekta ya madini na kuiomba iendelee kuwawezesha kwa kuwapatia vitendea kazi vya kisasa pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara ili kurahisisha upatikanaji wa migodi.

Ameongeza kuwa mgodi huo unaendelea kushirikiana na jamii inayouzunguka kwa kutoa ajira kwa vijana wa eneo hilo, kuchangia vifaa vya ujenzi katika Shule ya Sekondari Matongo, Ofisi ya Kijiji cha Matongo pamoja na ujenzi wa ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hatua inayochangia maendeleo ya kijamii katika eneo hilo.






Na Pamela Mollel Arusha,

Mradi wa ujenzi wa Stendi ya Mabasi Bondeni City unaendelea kuwa miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuboresha huduma za usafiri na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Jiji la Arusha, baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mhe. Paul Christian Makonda, kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo.

Akizungumza katika eneo la ujenzi wa stendi hiyo, Mhe. Makonda amepongeza uongozi wa Mkoa wa Arusha kwa utendaji kazi mzuri na usimamizi thabiti wa miradi ya maendeleo, akibainisha kuwa kasi ya ujenzi inaakisi dhamira ya serikali katika kuboresha huduma za kijamii na kiuchumi kwa wananchi.

Pia, amemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi huo kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka na kwa kuzingatia viwango vya ubora vinavyotakiwa, ili stendi hiyo iweze kutoa huduma bora, salama na za kisasa kwa wananchi pamoja na wageni wa Jiji la Arusha.

Aidha, Waziri Makonda ameuagiza uongozi wa mkoa kushirikiana kwa karibu na wataalamu wa mipango miji ili kunufaika na fursa zitakazotokana na mradi huo, ikiwemo ujenzi wa maeneo ya biashara na shughuli za kiuchumi zitakazosaidia kuongeza ajira na kukuza uchumi wa jiji.

Ziara ya Waziri Makonda ilihusisha miradi ifwatayo ukaguzi  ujenzi wa Stendi ya Mabasi Bondeni City, ujenzi wa Barabara ya ESO, mradi wa Soko la Kilombero, pamoja na mradi wa ujenzi wa jengo jipya la Halmashauri ya Jiji la Arusha unaotekelezwa kwa mapato ya ndani.






📍Azindua wiki ya Sheria Mbeya 

NA MWANDISHI WETU, MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utashi wake wa kisiasa na uwekezaji mkubwa uliowezesha mapinduzi ya kidijitali ndani ya Muhimili wa Mahakama, hatua inayorahisisha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Mhe. Itunda ametoa pongezi hizo wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, katika uzinduzi wa Wiki ya Sheria mkoani hapa.

Alisema kuwa uboreshaji wa miundombinu na mifumo ya kisasa ya TEHAMA ni matokeo ya fedha nyingi ambazo Rais Samia amekuwa akizielekeza mahakamani ili kuleta ufanisi, uwazi na uwajibikaji.

Akielezea ufanisi huo, Mhe. Itunda amebainisha kuwa kupitia utekelezaji wa maono ya Rais Samia, Mahakama imeweza kuongeza kasi ya kusikiliza na kumaliza mashauri kwa wakati, jambo linalopunguza kero kwa wananchi na kuimarisha utawala wa sheria nchini.

"Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuipa kipaumbele Sekta ya Sheria. Si tu kwa upande wa majengo na teknolojia, bali pia kwa kuidhinisha ajira za watumishi wa mahakama ambazo zimekuja kuongeza nguvu kazi na kupunguza mrundikano wa kesi," alisema Mhe. Itunda.

Aidha, Mhe. Itunda alitoa wito kwa watumishi wa mahakama na wadau wa sheria kutumia maboresho hayo yaliyowekwa na serikali kutenda haki kwa kuzingatia maadili na hofu ya Mungu. 

Alisisitiza kuwa uwekezaji huu wa serikali lazima uende sambamba na uadilifu wa hali ya juu kwa maamuzi yenye tija kwa jamii.

Mkuu huyo wa wilaya alihitimisha kwa kusema kuwa Wiki ya Sheria ni wakati muhimu wa kutathmini jinsi nchi inavyopiga hatua chini ya uongozi wa Rais Samia katika kujenga Taifa linaloheshimu haki na wajibu wa kila raia. 






Wawekezaji wa ndani na nje ya Mkoa wa Singida wamehimizwa kujitokeza kuwekeza katika viwanda vya uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini ili kunufaika na rasilimali zilizopo, kuongeza ajira na kukuza uchumi wa wananchi.

Wito huo umetolewa na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Mhandisi Sabai Nyansiri, akisema mkoa huo una fursa kubwa ya uwekezaji katika sekta ya madini kutokana na ongezeko la shughuli za uchimbaji na mazingira bora ya uwekezaji yaliyowekwa na Serikali.

Akizungumza wakati wa ziara yake kwa wachimbaji wadogo katika Mgodi wa Matongo uliopo Kata ya Ikungi, Wilaya ya Ikungi, Mhandisi Nyansiri amesema Singida inaendelea kufanya vizuri katika uchimbaji wa madini ya dhahabu, shaba, madini ya ujenzi pamoja na jasi, hivyo kuwepo kwa viwanda vya uchenjuaji ni hatua muhimu ya kuongeza thamani ya madini hayo kabla ya kuuzwa.

Amesema uwekezaji katika viwanda vya uongezaji thamani wa madini utaongeza ajira kwa vijana na wanawake, kuongeza mapato ya Serikali na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa mkoa huo.

“Uwepo wa viwanda vya uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini utaongeza ajira, mapato ya Serikali na kukuza uchumi wa kila mwananchi,” amesema.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha masoko ya madini na kuendeleza biashara rasmi ya madini, akibainisha kuwa hatua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la mapato ya mkoa.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Singida ulipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 30 kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kutoka Shilingi Bilioni 24 mwaka wa fedha 2024/2025, na hadi kufikia Desemba 2025 tayari umefanikiwa kufikia asilimia 54 ya lengo hilo sawa na Shilingi Bilioni 16.

Mhandisi Nyansiri amesema mafanikio hayo yanatokana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na kutoa kipaumbele kwa wachimbaji wadogo wazawa.

Kwa upande wake, Meneja wa Mgodi wa Matongo, Japhet Madusa, ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wa wachimbaji wadogo katika maendeleo ya sekta ya madini na kuiomba iendelee kuwawezesha kwa kuwapatia vitendea kazi vya kisasa pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara ili kurahisisha upatikanaji wa migodi.

Ameongeza kuwa mgodi huo unaendelea kushirikiana na jamii inayouzunguka kwa kutoa ajira kwa vijana wa eneo hilo, kuchangia vifaa vya ujenzi katika Shule ya Sekondari Matongo, Ofisi ya Kijiji cha Matongo pamoja na ujenzi wa ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hatua inayochangia maendeleo ya kijamii katika eneo hilo.










SIKU ya kubadilisha maisha yako na Meridianbet imefika leo. Suka jamvi lako la ushindi siku ya leo na uingie kwenye wale washindi wakubwa ambao hutangazwa hapa kila wiki.

Copa del Rey kule Hispania kutakuwa na mechi mbili kali kabisa ambapo Deportivo Alaves atakipiga dhidi ya Real Sociedad ambapo kwenye ligi tofauti yako ni pointi 2 pekee na mwenyeji alishinda mechi ya kwanza walipokutana. Sasa kwenye Kombe hili mgeni anataka kulipa kisasi. ODDS KUBWA zipo kwenye mtanange huu ndani ya Meridianbet. Suka jamvi hapa.

Nao Valencia watakuwa uso kwa uso dhidi ya Athletic Bilbao ambao wapo nafasi ya 12 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 14. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo kufuzu kwenye hatua ya Nusu Fainali leo. Meridianbet inakwambia kuwa hii ndio nafasi ya wewe kuondoka na pesa leo. Bashiri hapa.

Tengeneza pesa kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Pale Uingereza, kutakuwa na mechi ya kukata na shoka ya Carabao Cup mzunguko wa pili kati ya Manchester City dhidi ya Newcastle United ambapo kwenye mechi ya kwanza kukutana vijana wa Eddie Howe walipasuka nyumbani kwao. Leo hii ni nafsi yao kulipa kisasi wakiwa ugenini. Je watweza mbele ya vijana wa Pep Guardiola?. Beti hapa.

Coppa Italia pia kuna mechi ya kubeti, Inter Milan atamenyana dhidi ya Torino ambao hawapewi nafasi kubwa ya kuondoka na ushindi siku ya leo pale Meridianbet. Vijana wa Chivu wanahitaji ushindi ili wasonge mbele kwenye hatua ya Nusu Fainali kwenye michuano hii. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii. Jisajili hapa.

Vilevile DFB CUP kule Ujerumani kuna mechi moja ya Robo Fainali kati ya Holstein Kiel dhidi ya VFB Stuttgart ambao wana mwendelezo mzuri wa ligi hadi sasa. Mechi ya mwisho kukutana hawa wawili, walitoa sare. Je nani kuondoka kifua mbele siku ya leo?. Beti hapa.

Na Mwandishi wetu, Amboni Tanga.

Osale Otango ni Paulo Hamisi walikuwa wakifanya kazi  katika mashamba ya mkonge mkoani Tanga ambapo  mwaka 1952 walitoroka kutoka kwenye himaya ya wakoloni wa kizungu na kwenda kujificha kwenye mapango ya Amboni Tanga kwa ajili ya harakati za kupigania uhuru

Kwa muda wa miaka minne hawakuweza kuonekana na mtu yoyote kutokana na kutumia dawa za asili ambazo ziliwafanya wasionekane na mtu yoyote ingawa walikuwa na uwezo wa kukaa na makundi mengine ya watu ila kutokana na nguvu ya dawa hiyo walikuwa hawaonekani mpaka pale watakapoamua kuaga na kuondoka katika kundi hilo la watu, sharti  la dawa hizo walizopewa   ilikuwa ni kutofanya zinaa (mapenzi)

Sehemu waliyoishi inapatikana ndani ya mapango ya Amboni Tanga yanayosimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ambapo waliweza kuishi katika mapango hayo kwa miaka minne ingawa kuna wakati waliweza kutoka na kwenda maeneo mengine kwa ajili ya harakati za kupigania uhuru lakini kwa nguvu ya  dawa waliyopewa watu walikuwa hawawaoni.

Kilichowaponza wawili hao ni kuvunja sharti la dawa kwa kuamua kutoka Amboni na kwenda Lushoto kutafuta mwanamke na kufanya naye mapenzi. Hali hiyo ilitokea mwaka 1956  ambapo mara baada ya kumaliza kufanya  mapenzi na mwanamke huyo nguvu ya nguvu ya dawa ilipotea  na kuanza kuonekana na hivyo kukamatwa na kuhukumiwa adhabu ya kupigwa risasi kwa makosa ya kutoroka kwenye mashamba ya mkonge kwenda kwenye harakati za kupigania uhuru.

Kukiuka masharti hayo inaenda sambamba na usemi usemao "asiyesikia la Mkuu huvunjika guu"na  ukiambiwa zinaa mbaya ndiyo uelewe na ndiyo maana baadhi ya vitabu takatifu vinatufundisha  kuwa usikaribie zinaa na ukimuangalia mke wa mwenzio kwa jicho la kumtamani basi umezini, Karibuni mapango ya Amboni mujionee mahali walipokuwa wakiishi jamaa hao wawili.



 

Na OWM - TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OWM- TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na uwakilishi wa Benki ya NMB na kujadili namna wanavyoweza kufanya maboresho katika mchakato wa kutoa fedha za mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi kupitia taasisi hiyo ya kifedha.

Prof. Shemdoe amekutana na ujumbe huo leo Februari 03, 2026 ofisini kwake jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa Serikali kutafuta namna bora ya kurahisisha utolewaji wa mikopo hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha makundi yote lengwa ya Wanawake, Vijana na wenye Ulemavu yananufaika na mikopo hiyo.

Msisitizo wa Prof. Shemdoe kwa ujumbe huo ulioongozwa na Mkuu wa Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo umekuwa ni kuhakikisha vikundi vya wanufaika vyenye sifa stahiki vinapata mikopo hiyo kwa wakati.

Sanjali na hilo, Prof. Shemdoe ameipongeza na kuishukuru Benki ya NMB kwa kuiunga mkono Serikali katika uboreshaji wa miundombinu ya afya msingi na elimu msingi pamoja na kurahisisha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa walengwa. 

Akitoa ufafanuzi kuhusu hoja ya walengwa kutakiwa kuweka dhamana ili kupata mikopo ya asilimia 10, Bi. Bishubo amesema kuwa, hoja hiyo si ya kweli kwani mikopo hiyo ni nafuu na inatolewa bila dhamana yoyote, hivyo amewataka walengwa kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo. 

Katika hatua nyingine, uwakilishi huo wa Benki ya NMB umekutana na Naibu Waziri OWM- TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, pamoja na Naibu Waziri, OWM - TAMISEMI, anayeshughulikia Afya, Mhe. Dkt. Jafal Seif kama sehemu ya Kuimarisha mahusiano baina ya Benki hiyo na OWM- TAMISEMI.




Na Mwandishi wetu Simanjiro


MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, wamempongeza Mbunge wa Jimbo la Simanjiro James Ole Millya kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Kaleiya Mollel akizungumza kwenye kikao cha Baraza la madiwani kilichofanyika mji mdogo wa Orkesumet amesema wanamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Ole Millya kushika nafasi hiyo.

"Tangu dunia iumbwe ni mara ya kwanza Simanjiro kutoa Naibu Waziri hivyo tumpe ushirikiano wa kutosha ili aweze kuitumikia vyema nafasi hiyo ambayo Rais Samia ameona inamfaa katika kuitumikia," amesema Kaleiya.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mwanjaa Jacob amesema Ole Millya amewapa heshima kubwa watu wa Simanjiro hivyo watamuunga mkono ili aitumikie nafasi hiyo ipasavyo.

"Mbunge wetu ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, hii ni heshima kubwa tumepewa wana Simanjiro tunatarajia wote tumuunge mkono mbunge wetu ili atimize vyema majukumu yake," amesema Mwanjaa.

Diwani wa Kata ya Mirerani Salome Mnyawi amesema kupitia nafasi hiyo anaimani kubwa Simanjiro itapiga hatua kubwa zaidi kwani wanaye mbunge ambaye yupo Serikali kupitia nafasi ya Naibu Waziri.

"Kwa sasa mbunge wetu yupo jikoni anaweza akafanikisha maendeleo hivyo tumpe ushirikiano mkubwa wana Simanjiro," amesema Salome.

Hata hivyo, Ole Millya akizungumza kwenye kikao cha baraza hilo amewashukuru madiwani hao kwa kumpa pongezi hizo na ushirikiano katika nafasi yake.

"Kipekee nimshukuru Mhe DC Simanjiro mwalimu Fakii Raphael Lulandala, DED Simanjiro Gracian Max Makota, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Kaleiya na viongozi wote kwa namna wanavyonipa ushirikiano wa kutosha," amesema Ole Millya.

Amesema japokuwa hivi sasa mara nyingi anaishi Dar es salaam na Dodoma ila anawasiliana kwa karibu na viongozi hao wa Simanjiro kwa njia ya simu hata usiku wa manane kwa ajili ya maendeleo ya eneo hilo.



SIKU ya kubadilisha maisha yako na Meridianbet imefika leo. Suka jamvi lako la ushindi siku ya leo na uingie kwenye wale washindi wakubwa ambao hutangazwa hapa kila wiki.

Copa del Rey kule Hispania kutakuwa na mechi mbili kali kabisa ambapo Deportivo Alaves atakipiga dhidi ya Real Sociedad ambapo kwenye ligi tofauti yako ni pointi 2 pekee na mwenyeji alishinda mechi ya kwanza walipokutana. Sasa kwenye Kombe hili mgeni anataka kulipa kisasi. ODDS KUBWA zipo kwenye mtanange huu ndani ya Meridianbet. Suka jamvi hapa.

Nao Valencia watakuwa uso kwa uso dhidi ya Athletic Bilbao ambao wapo nafasi ya 12 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 14. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo kufuzu kwenye hatua ya Nusu Fainali leo. Meridianbet inakwambia kuwa hii ndio nafasi ya wewe kuondoka na pesa leo. Bashiri hapa.

Tengeneza pesa kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Pale Uingereza, kutakuwa na mechi ya kukata na shoka ya Carabao Cup mzunguko wa pili kati ya Manchester City dhidi ya Newcastle United ambapo kwenye mechi ya kwanza kukutana vijana wa Eddie Howe walipasuka nyumbani kwao. Leo hii ni nafsi yao kulipa kisasi wakiwa ugenini. Je watweza mbele ya vijana wa Pep Guardiola?. Beti hapa.

Coppa Italia pia kuna mechi ya kubeti, Inter Milan atamenyana dhidi ya Torino ambao hawapewi nafasi kubwa ya kuondoka na ushindi siku ya leo pale Meridianbet. Vijana wa Chivu wanahitaji ushindi ili wasonge mbele kwenye hatua ya Nusu Fainali kwenye michuano hii. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii. Jisajili hapa.

Vilevile DFB CUP kule Ujerumani kuna mechi moja ya Robo Fainali kati ya Holstein Kiel dhidi ya VFB Stuttgart ambao wana mwendelezo mzuri wa ligi hadi sasa. Mechi ya mwisho kukutana hawa wawili, walitoa sare. Je nani kuondoka kifua mbele siku ya leo?. Beti hapa.

 Samsung Electronics East Africa has officially launched the Galaxy Tab A11 in Tanzania, reinforcing its commitment to making innovative technology more accessible to families, students, and everyday users across the country. As Tanzanian households increasingly juggle remote learning, digital entertainment, and productivity demands on limited devices, the Galaxy Tab A11 enters the market positioned as a versatile solution for modern family life.


The Galaxy Tab A11 has been developed with the needs of modern users in mind, offering a balance between performance, ease of use, and affordability. As digital tools continue to play a greater role in education and daily life, the new tablets provide Tanzanian consumers with reliable solutions for studying, working, and staying connected.

Designed to Support Learning, Work, and Family Life

The Galaxy Tab A11 offers a seamless experience for users looking to get more done. Its large, immersive display allows students to read, watch lessons, and complete assignments comfortably, while multitasking features enable users to open and work across multiple applications at the same time. This makes it easier for learners to research, take notes, and organise their work efficiently.

Powered by intelligent Samsung capabilities, the Galaxy Tab A11 supports smarter and more efficient learning. Users can download the Gemini AI app from the Play Store to assist with research, everyday tasks, and information discovery. Samsung Notes further enhances the learning experience through tools such as Solve Math, helping students work through everything from basic calculations to more advanced problems with greater ease.

Education advocates are taking note of these practical features, particularly the combination of offline capability and smart learning tools. Features like Solve Math and large storage for downloaded materials address real barriers Tanzanian students face, especially those without consistent internet access or who can't afford private tutoring.

Built for Entertainment and Everyday Enjoyment

Beyond learning and productivity, the Galaxy Tab A11 delivers a rich entertainment experience for the whole family. For parents navigating busy households where the TV is often occupied, the tablet's immersive audio and smooth visuals offer a personal entertainment solution - ideal for streaming movies, browsing content, or catching up on series without competing for the remote. Enhanced performance ensures fast and smooth operation, even when switching between applications.

Parents are also supported through Kids Mode, which allows them to manage screen time, control accessible content, and monitor usage, ensuring a safe and balanced digital experience for children with a feature particularly valued by parents investing in technology for learning purposes.

Practical Features for Daily Convenience

The Galaxy Tab A11 comes with improved front camera quality for clearer and more natural video calls, making it suitable for online classes and virtual meetings. With large storage capacity, users can save photos, videos, and important files without worrying about space which is particularly useful for downloading educational content when WiFi or mobile network is available to access later offline. Fast charging ensures the device stays powered throughout the day, while light adaptation allows comfortable use both indoors and outdoors.

These features combine to make the Galaxy Tab A11 a dependable companion for learning, entertainment, and everyday tasks.

Samsung’s Commitment to Accessible Technology

Commenting on the launch, Mobile Business Head at Samsung Electronics East Africa – Tanzania Mgope Kiwanga, said:

“At Samsung, we are focused on creating technology that fits seamlessly into people’s everyday lives offering a better way to get things done. The Galaxy Tab A11 has been designed to support learning, creativity, and entertainment in a simple and accessible way. As more families and students embrace digital tools, this device offers a reliable solution that meets their needs while maintaining the quality and innovation Samsung is known for.”

Supporting Digital Growth in Tanzania

The launch of the Galaxy Tab A11 reflects Samsung’s broader commitment to supporting Tanzania’s digital journey by enabling access to smart devices that enhance education, productivity, and connectivity. By offering technology that is practical, reliable, and designed for real-life use, Samsung continues to empower users to do more, whether at home, in school, or on the move.

Samsung is launching the Galaxy Tab A11, giving families options based on their specific needs and budget. The Galaxy Tab A11 series aligns with Samsung's brand promise that "Awesome is for Everyone", making modern technology easier to access and simpler to use for more people across Tanzania.

The Galaxy Tab A11 series is now available at Samsung authorized retailers across Tanzania and online on www.samsungstore.tz .


Na Mwandishi Wetu, Tabora

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara,John Mongella, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, ameshiriki katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa mstaafu, Ndugu Nassor Hamdani.

Mazishi hayo yamefanyika leo Februari  3,2026 katika makaburi ya Mihogoni, Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora mkoani Tabora. 

Akizungumza katika ibada hiyo,Mongella amewasilisha salamu za rambirambi kutoka Chama Cha Mapinduzi, akimuelezea marehemu ndugu Nassor Hamdani kuwa alikuwa mshauri mwema wa Chama kwa kipindi chote cha uhai wake, sambamba na mchango wake mkubwa wa kujitolea kwa jamii.

Amesema CCM itaendelea kumkumbuka marehemu kwa uadilifu, hekima na mchango wake katika kukijenga Chama pamoja na ustawi wa jamii kwa ujumla.












 

Na FARIDA MANGUBE, MOROGORO

Baada ya mafuriko makubwa ya mwaka 2024 kukata mawasiliano na kuhatarisha maisha ya wananchi wa Kata ya Ngerengere, hali iliyosababisha adha kubwa ya usafiri na kudhoofisha shughuli za kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia wakala wa barabara mijini na vijijini TARURA mkoa wa Morogoro ililazimika kuchukua hatua za haraka kutatua changamoto hiyo ya muda mrefu.

Serikali ilitenga jumla ya shilingi 200,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa daraja la upinde wa mawe katika barabara ya Ngerengere – Sinyaulime lenye  urefu wa mita 30 na midomo miwili ya kupitisha maji, sambamba na uchongaji wa barabara yenye urefu wa kilometa moja, mradi uliolenga kurejesha mawasiliano ya uhakika na usalama wa usafiri kwa wananchi wa eneo hilo.

Akizungumza na Michuzi Blog kwenye ziara ya kamati ya siasa Mkoa wa Morogoro iliyokuwa ikikagua miradi ya barabra ndani ya Halmashauri hiyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Sinyaulime Shabani Ramadhani  amesema kwa muda mrefu walikuwa wakikabiliwa na adha ya usafiri na usafirishaji, hususani nyakati za mvua, baada ya daraja hilo kusombwa na maji  na kukatiza mawasiliano, kuhatarisha maisha ya wananchi na kudhoofisha shughuli za kiuchumi.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji iliyowasilishwa kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Morogoro katika maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa chama hicho, mkandarasi M/S Yesaca Civil and Building Works Company Limited anaendelea na kazi bila kuwasilisha madai ya malipo hadi sasa, huku thamani ya mradi ikifikia shilingi 199,668,112.

Mradi huo wa dharura unasimamiwa na TARURA Wilaya ya Morogoro hadi sasa, utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 80, huku unatarajiwa kukamilika Aprili 8, 2026, baada ya ratiba ya awali kuathiriwa na changamoto za mvua.

Kazi zinazoendelea ni pamoja na ujenzi wa kuta za daraja, uchongaji wa barabara, uwekaji wa kifusi, ujenzi wa kinga za daraja (gabions), uwekaji wa guard rail pamoja na kuvunja daraja la zamani, hatua zinazolenga kuhakikisha daraja linakuwa imara, salama na la kudumu.

Aidha baada ya kutembela na kukagua  kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Morogoro imelidhika na utekelezaji wa mradi huo na kuipongeza TARURA kwa usimamizi mzuri, ikisisitiza kuwa barabara ni kiungo muhimu katika kukuza uchumi na ustawi wa jamii.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Joseph Masunga, amesema kukamilika kwa daraja hilo kutarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wakazi wa maeneo hayo, hususani katika kusafirisha mazao ya kilimo na kufikia masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake, Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Ndyamukama amesema wakala huo umejipanga kuhakikisha maeneo yote korofi nyakati za mvua yanaboreshwa ili kurahisisha huduma kwa wananchi, kulingana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Nae Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Nuru Ngereja ameitaka TARURA na TANROADS kukamilisha miradi yote inakamika kwa wakati ili kukidhi hitaji la watanzania huku ikisisitiza kutoa kazi kwa wakandalasi wanaotekeleza miradi kwa wakati.

Wadau wa maendeleo wameeleza kuwa ujenzi wa daraja hilo ni ushahidi wa utekelezaji wa ahadi za Serikali ya Awamu ya Sita na Ilani ya CCM kwa vitendo, hasa katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuimarisha miundombinu ya vijijini.



 


Top News