Kanali Kolombo alitoa agizo hilo Machi 17, 2026, wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo kwa vikundi 20 kati ya 101 vilivyokidhi vigezo, ambapo jumla ya Sh milioni 266 zilitolewa kusaidia shughuli za uzalishaji.
Alisema licha ya Halmashauri kukopesha zaidi ya Sh bilioni 2 kwa vikundi mbalimbali, kiasi kilichorejeshwa hadi sasa ni takribani Sh bilioni 1 pekee, huku deni lililobaki likiwa bado kubwa.
“Fedha hizi si msaada, ni mtaji unaopaswa kurejeshwa ili kuwapa nafasi wananchi wengine kunufaika. Vikundi visivyorejesha vinakwamisha maendeleo ya wengine,” alisema Kolombo.
Aidha, alisisitiza kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya vikundi vinavyokiuka masharti ya urejeshaji, ikiwa ni pamoja na kuviita mbele ya uongozi wa wilaya ili kujua namna ya kushughulikia changamoto hiyo.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mpango huo, Kaimu Mratibu wa Mikopo, Mbilima Tungaraza alisema tangu mwaka wa fedha 2016/2017, Halmashauri imetoa mikopo yenye jumla ya Sh bilioni 2 kwa vikundi 490.
Alifafanua kuwa kati ya vikundi hivyo, 178 tayari vimemaliza kurejesha mikopo yao, huku vikundi 312 vikiwa bado vinadaiwa kiasi cha zaidi ya Sh bilioni 1.
Kwa mujibu wa Tungaraza, kati ya deni hilo, takribani Sh milioni 867 ni kwa vikundi vilivyo ndani ya muda wa marejesho, wakati zaidi ya Sh milioni 384 ni kwa vikundi vilivyochelewa kurejesha mikopo hiyo.
Aliongeza kuwa Halmashauri inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kisheria kuhakikisha marejesho yanafanyika, ambapo katika mwaka wa fedha 2024/2025, mashauri 95 yalifunguliwa katika mahakama za Kibiti, Bungu na Mohoro, na kufanikisha ukusanyaji wa zaidi ya Sh milioni 43.
Hatua hizo, alisema, zinalenga kuhakikisha nidhamu ya urejeshaji inaimarika na mikopo hiyo inaendelea kuwasaidia wananchi wengi zaidi kujikwamua kiuchumi.












.jpeg)

.jpeg)








.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
