Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeandaa futari maalum kwa watoto wenye uhitaji kutoka Kituo cha Kulea Watoto wenye Uhitaji cha Zili, tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuendeleza ujumuishi kwa makundi yenye mahitaji maalum.
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeandaa futari maalum kwa watoto wenye uhitaji kutoka Kituo cha Kulea Watoto wenye Uhitaji cha Zili, tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuendeleza ujumuishi kwa makundi yenye mahitaji maalum.
Amesema mfumo huo, uliozinduliwa rasmi Januari 26, 2026, unalenga kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma za afya na kuhakikisha maamuzi ya serikali yanaendana na mahitaji halisi ya wananchi.

Waziri Mchengerwa ametoa kauli hiyo Machi 13, 2026 wakati wa ziara yake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala jijini Dar es Salaam, ambapo pia alishiriki katika tukio la “Ongea na Waziri” lililowakutanisha watumishi wa afya na wananchi kwa lengo la kusikiliza changamoto na kupokea maoni kuhusu utoaji wa huduma za afya.
Amesema kuanzishwa kwa mfumo huo kunaonesha dhamira ya serikali ya kuweka kipaumbele katika kusikiliza wananchi kama msingi wa kuboresha huduma na kuimarisha uwajibikaji katika sekta ya afya.
Aidha, Waziri Mchengerwa amesema serikali ipo mbioni kuandaa mwongozo utakaotumika katika hospitali zote za serikali ili kukabiliana na malalamiko ya wananchi kuhusu gharama kubwa za matibabu na upatikanaji wa dawa.
Dkt. Shekalaghe amesema kupitia mfumo huo wananchi wanapata nafasi ya kuwasilisha changamoto na maoni yao moja kwa moja kwa Waziri, jambo linalosaidia kupatikana kwa ufumbuzi wa haraka na kuimarisha utoaji wa huduma za afya.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Mwananyamala, Evancy Asenga, amemshukuru Waziri Mchengerwa kwa ziara yake hospitalini hapo na kuahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa ili kuboresha huduma, hususan katika eneo la mapokezi ya wananchi.
Pia ameomba serikali kufanikisha ujenzi wa jengo kubwa la ghorofa katika hospitali hiyo ili kurahisisha utoaji wa huduma.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala, Dkt. Mercy Maya, amesema hospitali hiyo inaendelea kuimarisha na kupanua huduma za kibingwa kwa kuboresha miundombinu na kuongeza vifaa tiba ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.

📍Yasifu uwekezaji wa shilingi bilioni 429
NA MASHAKA MHANDO, Tanga
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeiashauri Serikali kuongeza kasi ya utatuzi wa changamoto za miundombinu wezeshi katika Bandari ya Tanga, ili kuendana na kasi ya ongezeko la shehena na meli kubwa zinazoingia bandarini hapo kufuatia maboresho makubwa yaliyofanyika.
Ushauri huo umetolewa Leo Machi 13 na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Profesa Joyce Ndalichako, wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utendaji na ufanisi wa bandari hiyo, ambayo hivi sasa imekuwa mbadala muhimu katika kupunguza msongamano wa mizigo kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kukagua gati jipya, Profesa Ndalichako alipongeza uwekezaji wa Shilingi Bilioni 429 uliowekwa na Serikali ya Awamu ya Sita, akisisitiza kuwa ni lazima kasi ya ujenzi wa barabara za kuingia na kutoka bandarini iongezwe ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo kwenda kwa walaji.
“Kamati inampongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake ya kuifungua Tanga. Tunaunga mkono mpango wa kuunganisha bandari hii na reli ya kisasa ya SGR kutoka Tanga hadi Musoma, hatua itakayochochea tija na ajira kwa wingi,” alisema Profesa Ndalichako.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, alibainisha kuwa Serikali inaendelea na mpango wa kuunganisha bandari hiyo na mtandao wa reli wa kilomita 248 (Tanga–Mruazi–Ruvu) na hatimaye kufika Arusha. Alieleza kuwa reli ya SGR kupitia Minjingu na Engaruka hadi Musoma itakuwa kiunganishi muhimu cha kiuchumi.
Meneja wa Bandari ya Tanga, Salehe Mbega, alieleza kuwa maboresho hayo yameongeza kina cha maji kufikia mita 12, hali inayoruhusu meli kubwa zenye urefu wa hadi mita 200 kutia nanga, tofauti na hapo awali.
“Ufanisi umeongezeka kiasi kwamba meli sasa zinahudumiwa ndani ya siku tatu hadi tano. Hata hivyo, kutokana na ubora wa huduma zetu, mahitaji yameongezeka na wakati mwingine hadi meli 14 husubiri nje ya bandari. Ili kutatua hili, tuna mpango wa kujenga magati matatu mapya na kituo cha kisasa cha abiria (Terminal) katika awamu ya tatu ya mradi,” alisema Mbega.
Maboresho hayo yanatajwa kuwa kichocheo kikubwa cha uchumi wa mkoa wa Tanga, yakigusa sekta za usafirishaji, biashara ndogondogo, na kuimarisha nafasi ya mkoa huo kama kitovu cha uwekezaji nchini.
Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua maeneo yaliyoathiriwa na mvua Kata ya Nzuguni Halimashauri ya Jiji la Dodoma, leo Machi 13, 2026, amesema ni muhimu kwa wazazi kuhakikisha watoto hawachezi kwenye madimbwi au maeneo yenye maji mengi kipindi hiki cha mvua ili kuwalinda dhidi ya hatari zinazoweza kutokea.
Aidha, amewataka wananchi kutunza mazingira na kuepuka kuchafua mifereji ya maji kwa kutupa taka ovyo, akieleza kuwa hali hiyo huchangia kuziba mifereji na kusababisha maji kujaa katika makazi ya watu pamoja na barabarani.
Amesema pamoja na changamoto zinazosababishwa na mvua, bado wananchi wanapaswa kuona kuwa mvua ni neema kwa Jiji la Dodoma kwa kuwa inaongeza uzalishaji wa chakula na kuleta ukijani kwenye mazingira.
Katika hatua nyingine, amewataka baadhi ya wananchi waliovamia na kujenga kwenye njia za maji kuzingatia sheria za mipango miji ili kuepusha madhara yanayotokea wakati wa mvua, ikiwemo nyumba kujaa maji.
Ametoa pole kwa wananchi waliokumbwa na athari za mvua na kuwataka kuwa na uvumilivu wakati Serikali ikiendelea na jitihada za kutatua changamoto hizo. Amesema suluhisho la kudumu litatekelezwa mara mvua zitakapopungua kunyesha ili kuruhusu utekelezaji wa maboresho ya miundombinu ya barabara na mifereji ya maji.
Akisoma taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Mtendaji wa Kata ya Nzuguni, Edgar Fungo, amesema kuanzia Januari 21, 2026 hadi Machi 13, 2026, jumla ya kaya 271 zimeathirika na maafa ya mvua katika kata hiyo. Kati ya hizo, nyumba 42 zimeezuliwa na upepo, nyumba 170 zimeingiliwa na maji na nyumba 59 zimebomoka.
Ameeleza kuwa mvua kubwa iliyonyesha Februari 9, 2026 iliathiri maeneo ya Mtaa wa Kitelela, Nzuguni C na Mahomanyika ambapo katika eneo la Kitelela barabara ziliharibika na kusababisha kushindwa kupitika, hali iliyosababisha wanafunzi kushindwa kwenda shule baada ya korongo kujaa maji pamoja na wananchi kukosa huduma za msingi.
Kwa upande wa Mahomanyika, daraja lilivunjika na kusababisha shughuli mbalimbali kusimama, huku katika eneo la Nzuguni C mfereji wa maji uliochimbwa kuzunguka ukuta wa Nane Nane ulijaa na kusababisha maji kusambaa hadi kwenye makazi ya wananchi.
Aidha, amesema Mbunge wa Jimbo la Mtumba, Anthony Mavunde, kwa kushirikiana na uongozi wa kata pamoja na diwani wa kata hiyo walitembelea maeneo yaliyoathirika na kutoa pole kwa wananchi pamoja na kusikiliza changamoto zao.
Amesema ushirikiano kati ya Serikali, viongozi wa eneo pamoja na taasisi mbalimbali ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanaopata madhara wanapatiwa msaada na hatua za kudumu zinachukuliwa ili kupunguza athari za mafuriko katika maeneo hayo siku zijazo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga amewataka watumishi wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoani Singida kutambua kuwa sekta ya barabara ni kiungo muhimu cha maendeleo ya sekta nyingine kama elimu, afya na uchumi, hivyo wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa bidii na weledi ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
Ameyazungumza hayo leo 13 Machi 2026, katika kikao kazi cha TARURA kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Ukaguzi mkoa wa Singida ambapo Dkt. Mganga amesema TARURA ni taasisi mtambuka na inategemewa na sekta nyingi, hivyo utekelezaji mzuri wa majukumu yao ni muhimu kwa maendeleo ya jamii.
Amesema moja ya changamoto kubwa inayowakabili wananchi ni uwepo wa barabara zisizopitika, hivyo watumishi wa TARURA wanapaswa kuhakikisha wanakuwa karibu na maeneo ya kazi hasa katika kipindi cha mvua ili kufuatilia hali ya barabara na kuhakikisha zinaendelea kupitika.
Pia, amesisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, kuwa na mawasiliano mazuri na kuwahudumia wananchi kwa heshima akisisitiza kuwa “mteja ni mfalme”.
Aidha, amewakumbusha watumishi kupambana na vitendo vya rushwa, kuheshimu muda wa kazi na kujaza taarifa katika mfumo wa PEPMIS ili kufikia malengo ya utendaji kazi.
Dkt. Mganga pia amesisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kutunza afya zao kwa kufanya mazoezi, kupima afya mara kwa mara na kuepuka matumizi ya pombe kupita kiasi, akieleza kuwa serikali inawekeza rasilimali nyingi katika kuwajenga watumishi wake hivyo wanapaswa kulinda afya zao ili kuendelea kulitumikia taifa.
Awali, Meneja wa TARURA Mkoa wa Singida, Mhandisi Claver Mwinuka, amesema kikao kazi hicho kinalenga kujadili mipango ya kazi, bajeti ya mwaka ujao wa fedha pamoja na mikakati mipya ya utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia maelekezo ya Bodi ya Barabara mkoa wa Singida.
Ameongeza kuwa kikao hicho pia kitatoa fursa ya kuimarisha mahusiano na mawasiliano kati ya watumishi, hususani wapya pamoja na kujadili matumizi ya teknolojia ya mawe katika ujenzi wa barabara ili kupunguza gharama na kuboresha ubora wa miundombinu.
Baadhi ya washiriki wa kikao hicho wakiwemo Meneja wa TARURA Wilaya ya Iramba Mhandisi Evance Kibona na Meneja wa TARURA Wilaya ya Mkalama Mhandisi Rahabu Thomas, wamesema kikao hicho kitasaidia kuboresha utendaji kazi na kuongeza ubunifu katika ujenzi wa barabara, hususani kwa kutumia rasilimali za mawe zinazopatikana kwa wingi mkoani Singida ili kuongeza ubora wa barabara na kurahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo.


































.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)