Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi akitembelea maeneo ambayo wakazi wake wamekataa kufanyiwa tathmini kwa ajili ya upanuzi wa shughuli za mgodi

Mkuu wa Mkoa wa Mara,Kanali Evans Mtambi akitembelea moja ya sehemu inapojengwa nyumba ya mwananchi ambaye amepatiwa fidia kupisha upanuzi wa mgodi wa Barrick North Mara,aliongozana na viongozi mbalimbali wa Serikali mkoani humo na maofisa waandamizi wa mgodi.

Meneja Mkuu wa mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko akieleza programu ya kulipa wananchi kwa ajili ya kupisha shughuli za mgodi inavyoendelea wakati wa ziara ya Mkuu wa mkoa wa Mara alipofanya ziara ya kikazi karibuni


*
-Awapa muda wa siku 90 wananchi ambao tayari wamelipwa fidia kupisha shughuli za upapanuzi wa mgodi.


Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, ameeleza kuridhishwa na ujenzi wa makazi mapya ya wananchi walioguswa na upanuzi wa Mgodi wa dhahabu wa Barrick North Mara pia amewapa siku 90 wananchi ambao tayari wamelipwa fidia ya maeneo yao kuondoka ili kupisha shughuli za upanuzi wa mgodi.


Akizungumza wakati alipokwenda kukagua ujenzi wa nyumba hizo katika eneo la Magena, Nyamongo wilayani Tarime karibuni, Kanali Mtambi aliupongeza mgodi huo kwa uwekezaji unaokwenda sambamba na ustawi wa wananchi.


Alitumia nafasi hiyo pia kusisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya mgodi huo na jamii inayouzunguka kwa maendeleo endelevu ya pande zote mbili na kuwataka wananchi ambao tayari wamelipwa fidia ya maeneo yao wawe wameondoka ndani ya siku 90 na wale waliogomea kulipwa fidia kukaa pamoja na wadau kutoka pande zozote kumaliza changamoto hiyo.


“Mkuu wa Wilaya na watu wa ardhi nawapa siku saba , mje kwa hawa wananchi, mkae nao muwaelimishe wakubali kufanyiwa uthamini na kupokea fidia kwa mujibu wa sheria,” alisema Kanali Mtambi.


Alionya kuwa kugomea uthamini na fidia kunakiuka sheria za nchi na kunachelewesha shughuli za mgodi huo pamoja na miradi ya maendeleo inayotegemea uwekezaji huo.


Baadaye, RC Mtambi alikwenda kuzindua moja ya nyumba za waguswa ambayo imejengwa na mgodi huo katika kijiji cha Mjini Kati.


Awali, Meneja Mkuu wa mgodi huo, Apolinary Lyambiko, alimweleza Mkuu wa Mkoa kwamba kampuni inaendelea kulipa fidia kwa kaya 254 zinazotakiwa kupisha ekari 59 kwa upanuzi wa shimo Nyabirama,hatua inayolenga kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama.


Lyambiko alisema waguswa 654 kati ya 728 walifanyiwa uthamini na kwamba hao tayari wamekwishapokea fidia zao ili kupisha upanuzi wa shimo la wazi la Nyabirama.


“Mradi huu unalenga si tu kuongeza ufanisi wa uzalishaji bali pia kuhakikisha usalama kwa kupata eneo la mita 200 la hifadhi kinga (buffer zone) kutoka kwenye shimo kama sheria inavyoelekeza,” alisema.


Aidha, Lyambiko alisema waguswa walipewa fursa ya kuchagua aina ya fidia wanayoitaka; kati ya fedha taslimu, kujengewa nyumba na ardhi mbadala.


“Wananchi 571 walichagua fedha taslimu, 36 walichagua ardhi na nyumba mbadala, 37 walichagua ardhi mbadala na 10 walichagua nyumba mbadala, na mchakato umezingatia ushirikishaji na hiari ya wananchi,” alifafanua.


Aliongeza kuwa ujenzi wa nyumba 10 mbadala umeshakamilika, nyumba 24 ujenzi umefikia asilimia 70, 16 ziko katika hatua za awali na 18 ziko kwenye hatua za manunuzi.


Kwa mujibu wa Lyambiko, mradi huo wa ujenzi wa nyumba za waguswa unatekelezwa na wakandarasi watatu waliopitishwa na Tume ya Madini Tanzania.


“Tunaendelea kuhakikisha kuwa kasi inaongezwa ili wahusika wahamie kwenye makazi yao mapya kwa wakati na kuruhusu mgodi kuendelea na shughuli zake kwenye eneo la Nyabirama,” alisema.


Taarifa za Serikali kuhusiana na program hiyo zinabainisha kuwa wananchi 728 wa eneo hilo walifanyiwa tathmini ya kulipwa fidia kwa ajili ya upanuzi wa eneo la mgodi ambapo hadi sasa wananchi 571 tayari wamelipwa fidia ya fedha taslimu na wengine 74 hawajasaini nyaraka za kulipwa fidia ambapo wananchi 11 wamegomea kufanyiwa tathmini.


Katika ziara hiyo, RC Mtambi aliambatana na Mkuu wa Wilaya, Meja Edward Gowele na Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Mwita Waitara, miongoni mwa viongozi wengine.


Mgodi wa Dhahabu wa North Mara unaendeshwa na Kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia Kampuni ya Twiga Minerals na ni miongoni mwa uwekezaji mkubwa wa uchimbaji wa madini nchini, ambao unachangia utekelezaji wa miradi ya kijamii, mapato ya taifa na ajira kwa Watanzania.
Mgodi wa Barrick North Mara umefanikisha miradi mbalimbali ya kijamii katika eneo la vijiji vinanyozunguka mgodi hususani katika sekta ya elimu,afya,maji,ujenzi wa miundombinu ya barabara,uwezeshwaji wa vijana na kuongeza wigo wa ajira.


*Zimo dawa aina ya Pethidine, Morphine na Fentanyl ni dawa tiba zenye asili ya kulevya

*Basi linalofanya safari Tanzania ,Uganda ,Congo lahusishwa,pia Scania lenye namba za Afrika Kusini 

Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imekamata tani 9.93 za dawa za kulevya aina mbalimbali, chupa 1,795 za dawa tiba zenye asili ya kulevya na kuteketeza ekari 87.5 za mashamba ya bangi. 

Aidha imekamata Magari 6 na pikipiki 29 vilikamatwa katika operesheni
hizo huku watuhumiwa 151 wakikamatwa kuhusika na uhalifu huo.
Aidha, kwa kushirikiana na maafisa wa kituo cha forodha cha Mutukula, 

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imekamata dawa tiba zenye asili ya kulevya aina ya Pethidine boksi 105 zenye chupa 1,045, Morphine Sulphate boksi 31 zenye chupa 310 na Fentanyl boksi 44 zenye chupa 440.

Akizungumza leo Machi 4,2026 jijini Dar es Salaam Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana a Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amesema dawa hizo zilikamatwa katika basi la abiria la kampuni ya SR Classic lenye usajili wa nchi ya Congo namba 5673AB04.

Amesema basi hilo linalofanya safari zake kati ya nchi za Uganda, Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Dawa zilizokamatwa zilibainika wakati wa upekuzi wa basi hilo katika kituo cha forodha cha Mutukula lilipokuwa likiingia chini Tanzania.

Amewataja watuhumiwa waliokamatwa katika tukio hilo ni Hassan Omary Mwambashi maarufu kama Macheni (50) mkazi wa Mbezi, Dar es Salaam, Ibrahim Saidi Malindi (36), manzania anayeishi Kampala Uganda, Yassa Said Hamood (38) mkazi wa Magomeni Dar es Salaam.

Wengine ni Hamad Said Hamad (46) mkazi wa Mombo Tanga, Abdul Athuman Khamis (31) mkazi wa Amana, Dar es Salaam, Mohamed Abdallah Sako (34) mkazi wa llala, Mwinshaa Mohamed Abdalla (47) mkazi wa Magomeni Dar es Salaam.

“Dawa aina ya Pethidine, Morphine na Fentanyl ni dawa tiba zenye asili ya kulevya zilizopo kwenye kundi la afyuni (opioids) ambazo hutumika hospitalini kwa ajili ya kupunguza maumivu makali wakati wa operesheni, kwa wagonjwa wa saratani, ajali, pamoja na wagonjwa wa selimundu.

“Aidha, dawa hizi zikichepushwa zinaweza kutumika kama dawa za kulevya na kusababisha uraibu kwa haraka zaidi kutokana na kuwa na nguvu kubwa. Dawa hizi zipo katika kundi la vipumbazi na zinauwezo mubwa wa kusababisha vifo kwa haraka kwa mtumiaji kwani huharibu mifumo ya mwili hasa mapigo
ya moyo, mfumo wa fahamu na fumo wa upumuaji.

“Hapa chini, dawa zilizokamatwa zinadhibitiwa kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Sura ya 95 na Sheria ya Dawa na Vifaa Tiba ya TMDA Sura ya 219. 

“Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imeorodhesha dawa hizo katika Jedwali la Kwanza (First Schedule) na Sheria ya Dawa na Vifaa Tiba inabainisha kuwa, muingizaji na msambazaji wa dawa aina ya nakotiki ni Medical Store Department (MSD) pekee.”

Kwa upande wa dawa za kulevya, bangi aina ya skanka Kamishina Jenerali Lyimo amesema Mamlaka imeendelea kukamatwa kwa wingi nchini. Katika operesheni zilizofanyika Dar es Salaam, muhumiwa Jontwa Samwel Mwaikonyole (43) mkazi wa Gogoni Kibamba, alikamatwa kiwa na kilogramu 81.883 za skanka.

Amefafanua dawa hizo zilikutwa ndani ya gari aina ya Scania lenye namba za usajili wa chi ya Afrika ya Kusini CAA 129054 na trailer namba CAA 22911 lililokuwa limebeba matunda aina ya apples.

Aidha amesema katika eneo la Chanika Buyuni watuhumiwa Masudi Rajabu (38) na mwenzake Shafii Mohamed (30) walikamatwa wakiwa na kilogramu 488.64 za skanka.

Aidha, katika ukaguzi wa mabasi ya abiria jijini Mbeya, watuhumiwa sita walikamatwa kwa nyakati tofauti wakisafirisha bangi aina ya skanka. Watuhumia hao ni Lenard Paulo (21) mkazi wa Sirali Mara, alikamatwa na kilogramu 46.46, Maria Kandonga (18) na wenzake Monica Kandonga (41) na Ibrahim Mwakibete (26) wote wakazi wa Mbeya.

Amesema watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na kilogramu 9.68, mtuhumiwa Joseph Mkwala (30) raia wa Malawi alikamatwa na kilogramu 4.62 na Esther Mbise (22) mkazi wa Mbeya alikamatwa na kilogramu 16.1 za skanka.

Wakati huo huo mkoani Arusha, watuhumiwa Fatuma Mussa Mohamed (45) maarufu kwa jina la Mama Arapha na mwenzake Elibaraka Martin Kingu (29) maarufu kwa jina Baraka walikamatwa wakiwa na bunda 937 za mirungi zenye uzito wa kilogramu 363.45. 

“Mama Arapha ni mhalifu wa muda mrefu aliyekuwa akiendesha mitandao ya safirishaji wa mirungi.”

Katika hatua nyingine amesema katika operesheni zilizofanyika mikoa ya Tabora, Tanga, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Katavi, Mtwara, Mara, Morogoro, Kigoma, Ruvuma na Kilimanjaro zilikamatwa tani 5.24 za dawa za kulevya aina ya bangi, tani 4.04 za mirungi pamoia na gramu 72 za heroin.

Hata hivyo katika operesheni zilizofanywa na mamlaka hiyo pia wamefanikiwa kukamata magari sita 6 na pikipiki 29 vilikamatwa katika operesheni hizo huku watuhumiwa 151 wakikamatwa kuhusika na uhalifu huo.

Amesema operesheni zilizofanyika zinaonesha jitihada za Serikali katika kupunguza upatikanaji wa dawa za kulevya chini. Mamlaka itaendelea kupambana na wafanyabiashara haramu wa dawa za kulevya pamoja na dawa tiba zenye asili ya kulevya ili khakikisha hazichepushwi na zinawafikia wagonjwa wanaohitaji dawa hizo badala ya kutumiwa na wahalifu kama mbadala wa dawa za kulevya.

“Mamlaka itaendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, taasisi za Serikali, Mashirika, Asasi za kiraia pamoja na makundi mbalimbai ya kijamil kuhakikisha kwamba, tatizo la dawa za kulevya linadhibitiwa kikamilifu kwani mapambano dhidi ya dawa za kulevya ni jukumu la kila mmoja wetu.”











Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa Tarehe 04 Machi, 2026 amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa majengo ya Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam, akisisitiza umuhimu wa mradi huo katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga nchini.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo,Prof.Mbarawa amesema lengo la ziara hiyo ni kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mradi unaendelea kwa kasi inayotakiwa, kwa kuzingatia ubora, ratiba, viwango vya kitaalamu na kimataifa na kuakisi thamani halisi ya fedha.

Ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita imefanya mambo makubwa sana kwenye sekta ya anga ikiwemo ujenzi na uboreshaji wa viwanja vya ndege karibu kila mkoa, ununuzi wa ndege na sasa imejipanga kuendelea kuimarisha miundombinu ya mafunzo ya sekta ya anga ili kuzalisha wataalamu wenye ujuzi wa hali ya juu watakaokidhi mahitaji ya soko la ndani na kimataifa.

“Mradi huu unaotekelezwa kwa shilingi bil. 78 ambao sasa umefikia asilimia 10.3 ni muhimu sana kwa maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini,tunasisitiza utekelezaji wake kuzingatia ubora, ratiba na viwango vya kimataifa, na kuakisi thamani halisi ya fedha ili chuo hiki kiwe kitovu cha mafunzo ya anga katika ukanda huu,” amesema Waziri Mbarawa.

Mwisho Prof.Mbarawa ametoa rai kwa TCAA kuhakikisha wanawapatia fursa ya mafunzo kwa vitendo vijana wa ndani wanaosoma masomo ya uhandisi na kusisitiza miradi yotr mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa ndani ya nchi itumike kama darasa kwa vijana wetu wanaojifunza ili kuzalisha wataalamu wengi wa ndani kwa maendeleo ya Taifa

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bw. Salim Msangi amesema mradi huo ulioanza kutekelezwa Julai,2023 na unatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa mamlaka hiyo wa kuimarisha uwezo wa ndani katika mafunzo ya anga, sambamba na kuendana na miongozo na matakwa ya mashirika ya kimataifa ya usafiri wa anga.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi, Mha. Stephen Mwakasasa, amesema ujenzi unaendelea vizuri kulingana na michoro na usanifu uliokubaliwa.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akipata maelezo ya mradi wa Ujenzi wa  Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) kutoka kwa  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC). 
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa  Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam,
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa pamoja na Menejimenti ya TCAA ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi wakisiliza maelezo kuhusu ujenzi wa mradi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) yaliyokuwa yanatolewa na  Meneja mradi wa Chuo cha CATC, Mhandisi Stephen Mwakasasa.
Kazi zikiendelea kwenye mradi


Na John Mapepele

Waziri wa Afya, Mohammed Mchengerwa, amesema kuwa ushirikiano madhubuti kati ya Serikali na Washirika wa Mfuko wa Pamoja wa Afya (Health Basket Fund) umeendelea kuwa chachu ya maboresho makubwa katika utoaji wa huduma za afya nchini.

Akizungumza katika mkutano wa nchi washirika wa Mfuko huo Machi 2, 2026 jijini Dar es Salaam Mhe. Mchengerwa alianza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuiwezesha Tanzania kufikia hatua ya kufanya majadiliano muhimu kuhusu mustakabali wa sekta ya afya. Alisisitiza kuwa pale washirika wa sekta ya afya wanapoungana kwa uwazi, dhamira na malengo ya pamoja, maisha ya wananchi huboreshwa kwa haraka zaidi.

“Mkutano huu si wa kawaida. Ni wakati wa kimkakati wa kuimarisha ushirikiano na kuthibitisha upya wajibu wetu wa pamoja wa kutoa huduma bora za afya kwa Watanzania,” alifafanua.

Mfuko wa Pamoja wa Afya Waimarisha Huduma za Msingi nchini

Waziri Mchengerwa alieleza kuwa tangu kuanzishwa kwa Mfuko wa Pamoja wa Afya mwaka 1999, zaidi ya dola za Marekani bilioni 1.3 zimechangishwa kusaidia utekelezaji wa mipango ya kimkakati ya sekta ya afya. Asilimia 90 ya fedha hizo zimeelekezwa katika huduma za Afya ya Msingi zinazosimamiwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Alibainisha kuwa kuanzia mwaka 2017, fedha za Mfuko zilianza kupelekwa moja kwa moja katika zaidi ya vituo 7,345 vya afya kupitia utaratibu wa ufadhili wa moja kwa moja kwa Vituo vya Afya, hatua iliyoongeza uwazi na ufanisi katika matumizi ya rasilimali.

“Kwa pamoja tumeimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba muhimu, tumepunguza vifo, na kuongeza uzazi salama katika Vituo vya Afya. Mageuzi haya yameweka msingi imara wa mfumo wa afya wenye ustahimilivu,” alisisitiza.

Msukumo Mpya: Bima ya Afya kwa Wote na Afya Kidijitali

Katika hatua nyingine, Mhe. Mchengerwa alisema Tanzania ipo katika kipindi cha mageuzi makubwa, huku lengo kuu likiwa utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Alifafanua kuwa wakati bima hiyo ikipanua ulinzi wa kifedha kwa wananchi, Mfuko wa Pamoja wa Afya unabaki kuwa mhimili wa kuhakikisha huduma bora na zenye usawa zinapatikana kwa wote.

Aidha, Waziri huyo alitoa wito kwa washirika kuunga mkono utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Afya Kidijitali uliounganishwa, akisisitiza umuhimu wa kuwa na mfumo mmoja wa kitaifa unaounganisha taarifa zote za afya.

“Huwezi kusimamia usichokiona, na huwezi kuboresha usichokipima. Mfumo wa kidijitali uliounganishwa ni mageuzi ya utawala, ufanisi na uaminifu,” alisema.

Kujenga Uwezo wa Ndani na Usalama wa Afya

Akizungumzia dira ya muda mrefu, Mhe. Mchengerwa alisema Tanzania inalenga kupunguza utegemezi mkubwa wa bidhaa za afya kutoka nje kwa kuwekeza katika uzalishaji wa ndani wa dawa, vifaa tiba na teknolojia za afya.

“Hili si suala la uchumi pekee, bali ni suala la usalama wa afya ya taifa. Mfumo imara wa afya lazima uunganishe ustahimilivu wa kifedha, kidijitali, rasilimali watu pamoja na uzalishaji na ugavi,” alifafanua.

Ushirikiano wa Kushinda kwa Pamoja

Waziri huyo alieleza kuwa mandhari ya maendeleo duniani yanabadilika, huku nchi zikielekea kwenye ushirikiano wa thamani ya pande zote na uendelevu wa muda mrefu.

“Tunaamini mustakabali wa ushirikiano haujengwi juu ya utegemezi, bali ubunifu wa pamoja na uwekezaji. Ushirikiano wenye busara haufiche changamoto; hujifunza kutoka kwake na hubuni mifumo bora zaidi,” alisema.

Alikiri kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa fedha kwa wakati, akieleza kuwa Serikali inafanya kazi kwa karibu na Wizara nyingine ikiwa ni pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI na Wizara ya Fedha ili kuondoa vikwazo vya kiutendaji na kuimarisha uwazi katika usimamizi wa fedha.

Mabalozi wampongeza Rais Samia kwa kazi kubwa kwenye Sekta ya Afya

Akizungumza kwa niaba ya timu ya mabalozi walioshiriki katika kikao hicho, Mheshimiwa Elke Wisch, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Mratibu wa Wadau wa Mfuko wa Pamoja wa Afya alimshukuru Rais Samia kwa kazi kubwa katika kuokoa vifo vya mama wajawazito na mtoto wakati wa kujifungua.

Mhe. Wisch aliihakikishia Serikali ya Tanzania kuendelea kuchangia katika sekta ya afya.

Aidha, walisifu juhudi zilizofikiwa katika kuimarisha huduma bora za afya katika kipindi kifupi cha Serikali chini ya Rais Samia.

Shukrani kwa Washirika wa Maendeleo

Kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mchengerwa alitoa shukrani kwa Washirika wote wa Mfuko wa Pamoja wa Afya kwa ushirikiano wao thabiti. Aliitambua kwa kipekee UNICEF kama Mratibu wa Mfuko, pamoja na mchango wa Benki ya Dunia na wadau wengine wa maendeleo.

Waheshimiwa mabalozi walioshiriki kwenye mkutano huo ni pamoja na Mheshimiwa Nicole Providoli, Balozi wa Uswisi,

Mheshimiwa Nicola Brennan, Balozi wa Ireland,

Mheshimiwa Emily Burns, balozi wa Canada,

Mheshimiwa Marianne Young, balozi wa Uingereza,

Mheshimiwa Eunju Ahn, Balozi wa Korea,

Mheshimiwa Nathan Bellete, Mwakilishi wa Benki ya Dunia nchini

Mheshimiwa Mark Bryan Schreiner, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA),

Mheshimiwa Elke Wisch, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Mratibu wa Wadau wa Mfuko wa Pamoja wa Afya.

Mhe. Mchengerwa alisisitiza kuwa mafanikio hayapimwi kwa kiasi cha fedha kilichotolewa, bali kwa maboresho yanayopimika katika afya na ustawi wa jamii.

“Tanzania iko tayari kushirikiana, tayari kuvumbua, na tayari kusonga mbele kwa njia mpya inayozingatia uwajibikaji wa pamoja na matokeo yanayopimika,” alihitimisha.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, kuimarisha mifumo ya afya si tu kuboresha huduma, bali ni kulinda jamii, kuongeza tija ya taifa, kuimarisha taasisi na kujenga mustakabali wenye afya na usalama zaidi kwa nchi.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, Katibu Mkuu, Dkt. Seif Shekhalaghe, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia eneo la Dawa, Emmanuel Tayari, Mganga Mkuu na Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Maghembe.



Pembezoni mwa kikao hicho Mheshimiwa Mchengerwa alifanya balozi wa Uingereza, Canada na Marekani.

Ushirikiano baina ya Tanzania Uingereza na Canada

Mhe. Mchengerwa alifafanua kuwa Uingereza na Tanzania zina ushirikiano wa muda mrefu katika sekta ya afya, uliojengwa juu ya miongo kadhaa ya kazi ya pamoja ya kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, kuimarisha mifumo ya afya, na kukabiliana na changamoto kuu za kiafya. Ushirikiano huu unahusisha misaada ya kiserikali, msaada wa kitaalamu, ushirikiano wa tafiti, pamoja na msaada kupitia taasisi na mashirika yasiyo ya kiserikali ya Uingereza.

Naye Balozi wa, Uingereza Mhe. Young alisema nchi yake huchangia kwa kiasi kikubwa katika taasisi za kimataifa za afya kama Gavi, Mfuko wa Dunia (Global Fund), na Shirika la Afya Duniani (WHO) zinazofanya kazi nchini Tanzania na itaendelea kufanya hivyo

Mhe. Mchengerwa alifafanua kuwa kwa sasa, sekta ya afya inalenga maeneo yafuatayo ya kipaumbele ambayo ni pamoja na Kusaidia kuanzisha na kutekeleza mifumo ya Bima ya Afya kwa Wote ili kupunguza pengo la upatikanaji wa huduma;

Kuboresha huduma za mkoba, rufaa na huduma bingwa katika ngazi zote za utoaji huduma;

Kuimarisha huduma za uchunguzi, kinga, tiba, ukarabati na huduma za kupunguza maumivu katika ngazi zote;

Kuimarisha afya ya uzazi, mama na mtoto;

Kuimarisha kinga, udhibiti na usimamizi wa magonjwa yasiyoambukiza (NCDs);

Kuimarisha maandalizi na mwitikio wa dharura dhidi ya magonjwa ya milipuko;

Kuboresha utekelezaji wa tiba mtandao (telemedicine) na mifumo ya kielektroniki ya taarifa za afya katika ngazi zote;

Kusaidia utekelezaji wa tiba asili na mbadala nchini; na

Kuwekeza katika uzalishaji wa ndani wa chanjo, bidhaa na vifaa tiba

Kwa upande wake Balozi wa Canada nchini Mhe. Burn alisema ameridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Tanzania na ipo tayari kuendelea kuchangia katika sekta ya afya.



Na Mwandishi Wetu, Berlin, Ujerumani.
MKURUGENZI wa Mauzo wa Turaco Collection Tanzania, Florenso Kirambata akiziwakilisha hotel zao katika maonesho ya ITB- Berlin anasema kwamba, maonesho hayo ni eneo jema kabisa la kujitangaza kubadilishana uzoefu hasa katika dunia ambayo walaji (watumiaji wa huduma) wamekuwa wakibadilika kutokana na mazingira yanayotokea duniani.

Florenso amebainisha kuwa, Turaco Collection kwa upande wa Dar es Salaam wana Element By Westin Marriott na Delta By Marriott na kwa upande wa utalii wa kaskazini pamoja na bidhaa mbalimbali za utalii pia wana; Turaco Ngorongoro Valley Lodge Tribute portfolio under Marriott International na Turaco Manyara View Lodge Tribute portfolio under Marriott International na kwa Zanzibar wana Turaco Nungwi Beach Reasort Tribute portfolio under Marriott International na Turaco Spice Tree Stone Town Tribute portfolio under Marriott International na Beyt Aly Salaam-By Turaco

Katika jukwaa hili linalokutanisha wadau wa sekta ya utalii kutoka kila pembe ya dunia kwa lengo la kukuza ushirikiano, ubunifu na uwekezaji endelevu.

Katika hafla hii, napenda kusisitiza kuwa Serikali ya Tanzania imeendelea kukuza mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji, huku ikilenga kurahisisha michakato ya kiutawala, kuimarisha mifumo ya udhibiti, na kutoa motisha zinazovutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Hatua hizi ni sehemu ya mkakati mpana wa kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utalii wa kimataifa chenye ushindani na ubora wa hali ya juu.

Tanzania imefungua milango kwa fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji, tayari ikiwakaribisha wadau kushirikiana katika maono ya kukuza uchumi endelevu na ustawi wa muda mrefu katika sekta ya utalii. Turaco Collection tunaamini kuwa ushirikiano kati ya sekta binafsi na Serikali ni nguzo muhimu katika kufanikisha malengo haya.

Maonesho haya ni fursa adhimu ya kubadilishana uzoefu, kuhamasisha ushirikiano wa kimkakati, na kuweka misingi ya miradi mipya itakayoboresha miundombinu, huduma, na ubora wa uzoefu wa watalii. Kupitia jukwaa hili, tunaendelea kuitangaza Tanzania kama kivutio cha kipekee chenye utajiri wa mbuga Za wanyama,Mlima Kilimajaro,utamaduni, historia, fukwe za kuvutia na huduma bora za ukarimu.

Aidha, nawapongeza Bodi ya utalii kwa kuendeleza utamaduni wa kufanya maonesho ya utalii na uwekezaji katika medani za kimataifa.

Jitihada hizi zinaimarisha taswira ya nchi yetu, kuongeza mtiririko wa watalii, na kufungua milango mipya ya masoko duniani.

Turaco Collection tunaendelea kujizatiti kutoa huduma za viwango vya kimataifa, tukizingatia ubora, ubunifu na uzoefu wa kipekee kwa wageni wetu. Tunaamini kuwa kwa pamoja, tutaweza kuifanya Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kuwa kitovu cha utalii endelevu na wenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho.









Na Khadija Kalili, Kibaha
MWENYEKITI wa Baraza la Wafanyakazi Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa huo, Pili Mnyema, amewataka wajumbe wa baraza hilo kujadili ajenda zenye tija kwa wananchi pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Mnyema ameyasema hayo leo, Machi 3, 2026, wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi Mkoa wa Pwani kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Kibaha.

Aidha, amesisitiza uwajibikaji, kufanya kazi kwa nidhamu na uadilifu, pamoja na kuhimiza ushirikiano ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

“Niwapongeze kwa mafanikio yaliyofikiwa, kwani Mkoa wa Pwani unaongoza katika mambo mengi yaliyoiwezesha kuwa kinara katika sekta mbalimbali. Hivyo, niwaombe tuendelee kushirikiana ili kuendeleza mafanikio hayo na kuufanya Mkoa wetu kuwa kinara katika kila sekta,” amesema Mnyema.

Katika hatua nyingine, amewataka wajumbe wa baraza hilo kuipa kipaumbele ajenda ya uwekezaji kwa kufanya kazi kwa ushirikiano, akieleza kuwa Mkoa wa Pwani ni mkoa wa kimkakati katika uwekezaji wa viwanda.

Aidha, kikao hicho kilipata fursa ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mpango wa bajeti wa mwaka 2025/2026, pamoja na kupokea na kupitisha rasimu yexa mpango wa bajeti ya mwaka 2026/2027. Vilevile, kilifanya uchaguzi wa Katibu na Katibu Msaidizi, ambapo Ramadhani Mwaiganju amechaguliwa kuwa Katibu, huku Mwajuma Mohamed amechaguliwa kuwa Katibu Msaidizi.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameutaka uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mzenga, kilichopo Kata ya Mzenga, Wilaya ya Kisarawe, kuhakikisha kinatoa mafunzo katika fani zinazoendana na shughuli za kiuchumi za eneo hilo.

Mhe. Wanu ametoa agizo hilo Machi 03, 2026, wilayani Kisarawe wakati wa ziara ya ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na Wizara katika wilaya hiyo.

Amewataka viongozi wa wilaya na wananchi wa eneo hilo kuona umuhimu wa mafunzo ya ujuzi na hivyo kuhamasisha vijana kujiunga na chuo hicho ili kupata ujuzi utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.

Amesema chuo hicho, pamoja na vyuo vingine vya maendeleo ya wananchi, vinapaswa kuzingatia mahitaji halisi ya kiujuzi ili vijana waweze kujiunga kwa wingi.

“Mmesema hapa mnazalisha zao la korosho, ufuta na mihogo; kwa nini sasa msianzishe kozi ya kusindika mazao hayo? Hii itawamasisha vijana kujiunga na chuo kwa kuwa wanasoma kile wanachofanyia kazi,” amesema Mhe. Wanu.

Aidha, ameutaka uongozi wa chuo hicho kusimamia ipasavyo mifumo ya usimamizi wa watumishi ili kuimarisha uwajibikaji.

Akiwa wilayani humo, Mhe. Wanu pia amekagua ujenzi wa VETA Kisarawe na kusema kuwa Serikali inaendelea kujipanga kupata rasilimali fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa chuo hicho ili malengo ya kutoa ujuzi kwa wananchi yafikiwe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mhe. Petro Magoti, amemuhakikishia Naibu Waziri Wanu ushirikiano katika kusimamia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa, ikiwemo kuhakikisha huduma za umeme na maji zinafika katika eneo la chuo ili kurahisisha hatua inayofuata ya ujenzi.









Top News