Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba mara baada ya kufungua Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa mbele ya Soko Kuu jipya la Kariakoo mara baada ya ufunguzi uliofanyika Sokoni hapo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Matukio mbalimbali katika hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya picha mara baada ya kufungua Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.



Katika kuadhimisha miaka 19 ya kuanzishwa kwa kiwanda cha kuunganisha magari cha GF, uongozi wa kiwanda hicho umesema unajivunia kuwa sehemu ya kuzalisha ajira, huku ukieleza kuwa asilimia 90 ya wafanyakazi wake ni wazawa.

Akizungumza na waandishi wa habari, leo Februari 07, 2026, makao makuu ya kiwanda hicho yaliyopo Kibaha mkoani Pwani, Meneja Mkuu wa kiwanda cha GF, Ezra Mereng, amesema miaka 19 ya dira na matumaini yalianza kama ndoto, lakini hadi sasa kiwanda hicho kinajivunia kuzalisha magari ya aina mbalimbali.

“Leo tunajivunia kusherehekea miaka 19 ya GF, na sisi kama kiwanda tunajivunia kuwa zaidi ya asilimia 90 ya wafanyakazi ni vijana wazawa wa hapa Tanzania waliotoka katika vyuo mbalimbali hapa nchini."

Naye Meneja Chapa na Masoko wa GF Group, Salman Karmal  pamoja na kufurahia mafanikio ya kiwanda hicho, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufungua fursa za uwekezaji zinazowavutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza nchini.

Amesema katika kuadhimisha miaka 19 ya GF, kiwanda hicho kimekuja na mpango wa kurudisha kwa jamii, ambapo wameanza kwa kutembelea watu wenye mahitaji maalumu pamoja na kufadhili timu ya mpira wa miguu ya Nyumbu FC iliyopo jirani na kiwanda hicho, ambayo imekuwa ikifanya vizuri kwenye michezo yake mbalimbali.

“Tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuweza kufungua milango rafiki ya uwekezaji inayotufanya tuwe na uthubutu wa kujiimarisha zaidi katika maeneo mbalimbali ya kibiashara".

Kwa upande wake, Sefroza Mwizarubi, ambae ni mnufaika wa program ya kuchukua wanafunzi vyuoni , amewashukuru viongozi wa GF kwa kutoa nafasi kwa wahitimu wa vyuo mbalimbali kwenda kujifunza namna ya kuunganisha magari, jambo linalowafanya kuwa wabobezi katika nyanja hiyo.

“Mimi ni mnufaika wa mpango wa GF wa kuchukua wanafunzi kutoka vyuoni kwa ajili ya kuja kupata ujuzi wa kuunganisha magari, lakini pia kupata ajira,” amesema Mwizarubi.
Meneja Mkuu wa kiwanda cha GF Vehicle Assemblers,  Ezra Mereng akizuingumza na wafanyakkazi wa kiwanda hicho wakati wa hafla ya madhimisho ya miaka 19 ya kampuni ya GF mkoani Pwani





Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana,akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza,ili  kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara yaliyoandaliwa na Baraza la Ushindani wa Soko (FCT).

Na.Mwandishi Wetu-MWANZA

 BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara.

Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

“Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Baraza la Ushindani na nafasi yake katika kulinda haki za mlaji pamoja na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”Alisema Bw.Elikana

Akizungumza katika mafunzo hayo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Bw. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza lipo kwa ajili ya kulinda masuala yote yanayohusu ushindani wa soko na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini. Alieleza kuwa utekelezaji wa majukumu ya Baraza unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha sheria za ushindani zinatekelezwa kikamilifu, kwa haki na kwa uwazi.

Aidha, aliongeza kuwa Baraza huhakikisha mamlaka za udhibiti zinazingatia taratibu na kanuni za ushindani wakati wa utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kutoa majibu sahihi na ya haraka katika migogoro ya kibiashara. Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kumlinda mlaji dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha ushindani, hivyo kuchangia katika ujenzi wa uchumi shindani, jumuishi na wenye tija kwa Watanzania.

Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa Chemba ya Wafanyabiashara, Bw. Hassan Karambi, alisema kuwa amepata elimu yenye manufaa makubwa kupitia programu ya Baraza ya kuwajengea uwezo wadau.

Alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia wafanyabiashara kufahamu kuwa endapo hawataridhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti kama LATRA, TCRA, TCAA, EWURA, PURA pamoja na Tume ya Ushindani (FCC), wana haki ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yao.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa, Bi. Imelda Salumu, alifafanua utaratibu wa Baraza katika kupokea rufaa kutoka kwa wadau.

Alisema kuwa malalamiko huanza kwa mtoa huduma husika, na endapo hayatapatiwa ufumbuzi, hufikishwa katika mamlaka ya udhibiti kama hatua ya kwanza ya rufaa. Aliongeza kuwa iwapo mlalamikaji hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hiyo, utaratibu humruhusu kuwasilisha rufaa katika Baraza la Ushindani kwa hatua zaidi za kisheria.



Na Mwandishi Wetu, Manyara.

SERIKALI imeanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji 267 vya Mkoa wa Manyara kwa gharama ya Shilingi bilioni 45.8 kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.


Akizungumza wakati wa hafla ya kumtambulisha mkandarasi wa mradi huo, mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina, amesema mkataba wa utekelezaji wa mradi huo ni wa miaka mitatu na utatekelezwa katika halmashauri zote za Mkoa wa Manyara.



Mhandisi Mhina amesema mradi huo unalenga kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji ambavyo bado havijafikiwa, hatua itakayosaidia kuboresha maisha ya wananchi, kukuza shughuli za kiuchumi pamoja na kuimarisha upatikanaji wa huduma za kijamii kama afya na elimu.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amewaagiza Wakuu wa Wilaya zote za mkoa huo kutoa ushirikiano wa karibu kwa mkandarasi ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.


Mhe. Sendiga pia amesisitiza umuhimu wa viongozi kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utekelezaji wa mradi huo, akieleza kuwa mradi wa kusambaza umeme hauna fidia, hivyo ni muhimu wananchi kuelewa taratibu zake ili kuepusha changamoto zisizo za lazima.



Naye mkandarasi aliyekabidhiwa utekelezaji wa mradi huo, Bw. Patrick Mong, amesema lengo lao ni kuukamilisha mradi huo ndani ya miezi 33, huku akibainisha kuwa kazi za utekelezaji zinaanza rasmi Februari 9 mwaka huu.

Amesema mkandarasi amejiandaa kikamilifu kuhakikisha mradi unakamilika kwa ubora na kwa muda uliopangwa ili wananchi wa Mkoa wa Manyara wanufaike na huduma ya umeme kwa maendeleo endelevu.

Na Kassim Nyaki, Ngorongoro.

Mabadiliko makubwa katika ushirikishwaji wadau wa sekta ya utalii yameibuliwa na uongozi Mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro ikianza mwanzo wa safari mpya ya simulizi kwa chapa ya Destination Ngorongoro kwa kuzungumza sauti moja, iliyo thabiti, yenye kujiamini na kukumbukwa.

Ngorongoro imeamua kuzindua shindano la upigaji  picha kwa waongoza watalii (Tour Guides)  lijulikanalo kama “The Birth of Wonders photo competition” katika eneo la Ndutu hususan msimu huu wa mazalia ya Nyumbu.

Akitangaza kampeni hiyo Kamishna Msaidizi Mwandamizi anayesimamia huduma za Utalii na Masoko Mariam Kobelo ameeleza kuwa shindano hilo linahusu eneo la Ndutu ambapo ndipo Safari Kuu ya Nyumbu huzaliwa na maisha kuanza ambapo eneo hilo hadithi ya Ngorongoro hujirudia upya kila mwaka.

“Waongoza Watalii ni mabalozi wetu muhimu katika kuisimulia Ngorongoro kwa dunia, katika msimu huu wa uzaaji wa nyumbu hapa Ndutu, tunawaalika kutumia lenzi zao kunasa pumzi za kwanza za uhai wa ndama, hatua za kwanza za ndama, mahusiano ya mama na mwana, 

Waongoza watalii watapaswa kupiga picha na kuzituma kupitia akaunti zao za instagram, _tag_ na kushiriki (collaborate) na akaunti rasmi ya  _instagram_ ya ngorongoro ijulikanayo kama (@visitngorongoro

Katika shindano hilo  la upigaji picha ( _The Birth of Wonders photo competition)_ Washindi watachaguliwa kwa kuzingatia ushiriki (engagement) wa watazamaji pamoja na kufuata masharti yote ya shindano ambapo mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita kinono cha shilingi Milioni  3,000,000, mshindi wa pili shilingi milioni 2,000,000 na mshindi wa tatu atajishindia shilingi milioni 1,000,000 mtawalia.

Waongoza Watalii ambao ni washiriki wa kampeni hii wanakuwa wasimulizi wa sauti ya chapa ya _Destination Ngorongoro_ Kwani wao ndiyo mashuhuda wa kwanza wa simulizi ya uzao wa nyumbu.









 

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), amekipongeza Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwa kuweka mipango na mikakati inayotembea katika maono ya  dira Taifa ya mwaka 2025-2050, ikiwemo mageuzi ya Kidijitali na Utafiti na Maendeleo.

Mhe. Luswetula ameyasema hayo Februari 06, 2026 katika mahafali ya 27 ya IAA duru ya Pili, yaliyofanyika Ngurodoto jijini Arusha akimwakilisha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Omar Mussa.

Mhe. Luswetula amesema mipango inayofanywa na IAA ya kuboresha miundombinu ya TEHAMA, mifumo ya kujifunzia kwa njia ya mtandao hususani kwa Shahada ya Uzamili (master’s degree), usimamizi wa kitaaluma ni nguzo muhimu katika kuongeza ufanisi na ushindani wa Chuo kitaifa na kimataifa.

“Mageuzi ya Kidigitali ni kichocheo muhimu cha maendeleo hususani katika kuboresha ukuaji wa uchumi na kuimarisha huduma za jamii ikiwemo elimu. Serikali inatambua na kupongeza juhudi za IAA katika kuwekeza kwenye mifumo ya kidigitali”, amesema Mhe.Luswetula.

Aidha, ameipongeza IAA kwa kuendelea kuzalisha wataalam mahiri wa fedha, uhasibu, uchumi, kodi, utalii, usimamizi biashara, benki, ununuzi na ugavi, masoko, bima, TEHAMA na nyingine nyingi; ambao wamekuwa mhimili muhimu katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, usimamizi wa fedha za umma, sekta binafsi, taasisi za kifedha na miradi ya maendeleo.

Vile vile, Mhe.Luswetula awasisitiza wanafunzi na wahitimu wa Shahada ya Uzamili kuimarisha zaidi tafiti zao za kitaaluma kwa kuzielekeza katika kutoa majibu ya changamoto halisi zinazoikabili jamii na Taifa letu, ikiwemo masuala ya usimamizi wa fedha za umma, ukuaji wa uchumi jumuishi, ajira, ubunifu, na matumizi sahihi ya teknolojia.

Mkuu wa Chuo IAA, Prof. Eliamani Sedoyeka amesema IAA wanajivunia kuwa miongoni mwa taasisi za elimu ya juu nchini zinazotekeleza mwelekeo wa Kitaifa wa kupanua upatikanaji wa elimu ya juu kwa kuanzisha na kuimarisha mfumo jumuishi wa utoaji wa shahada ya Uzamili (Master’s degree) unaochanganya masomo ya ana kwa ana darasani (Physical classes) na ya mtandaoni  kwa wakati mmoja yaani ‘blended mode’.

Prof Sedoyeka ameongeza kuwa IAA imeweka mkakati  kuwawezesha wahadhiri wengi zaidi kusomea Shahada ya Uzamivu, ili kukidhi ongezeko la idadi ya wanafunzi wa Uzamili linaloendelea kushuhudiwa kila mwaka, ambapo jumla ya wahadhiri 115 wamepelekwa kusoma Shahada ya Uzamivu (PhD) katika vyuo mbalimbali nchini na nje ya nchi katika mwaka wa masomo 2025/2026.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo IAA, Dkt. Mwamini Tulli amesema Katika mahafali ya 27 duru hii ya pili  jumla ya wahitimu 2,250 kati yao wanaume ni 1,369 sawa na asilimia 60.8 na wanawake 881 sawa na asilimia 39.2 wametunukiwa Shahada ya Uzamili ya Chuo cha Uhasibu Arusha(IAA) katika fani 15.








 


Top News