Ushirikiano huo umetangazwa jijini Dar es Salaam, ukiwa ni sehemu ya mkakati wa PigaBet kuendeleza michezo kama chachu ya mshikamano wa jamii, ukuaji wa uchumi na kuinua hadhi ya taifa kupitia soka.
Hatua hiyo pia inaenda sambamba na mwanzo wa enzi mpya kwa Fountain Gate FC, ambayo sasa imehamishia makazi yake jijini Arusha, eneo linalozidi kujijenga kama kitovu cha michezo nchini kuelekea michuano ya Africa Cup of Nations 2027.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Meneja wa Masoko wa PigaBet, Arthur Kazola, alisema kampuni hiyo inaamini nguvu ya soka katika kuunganisha jamii na kuhamasisha vijana.
“Ushirikiano wetu na Fountain Gate FC si udhamini wa kawaida, bali ni uwekezaji katika mustakabali wa mpira wa miguu na kuinua hadhi ya Arusha kama jiji la michezo,” alisema Kazola.
Aliongeza kuwa Tanzania inaendelea kujijengea heshima barani Afrika katika soka, hivyo ni muhimu kwa sekta binafsi kuunga mkono juhudi hizo kwa vitendo.
Kwa upande wake, Rais wa klabu hiyo, Japhet Makau, alisema ujio wa PigaBet ni hatua kubwa si kwa klabu pekee bali kwa maendeleo ya soka la Tanzania kwa ujumla.
“Uwekezaji huu unaonesha wazi kuwa soka limekuwa chanzo cha ajira na fursa kwa vijana wetu. Tunakaribisha wadau wengine kuja kuunga mkono juhudi hizi,” alisema Makau.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, PigaBet itashiriki katika kusaidia maendeleo ya klabu ndani na nje ya uwanja, ikiwa ni pamoja na kuimarisha uhusiano na mashabiki na wadau wa soka.
Ushirikiano huo utaanza kuonekana rasmi Aprili 9, 2026, ambapo Fountain Gate FC itakuwa mwenyeji wa Simba SC katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Stadium, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wengi.
Kwa ujumla, hatua hii inaonekana kuwa kichocheo kipya cha maendeleo ya soka nchini, huku Arusha ikiendelea kujipambanua kama jiji muhimu katika ramani ya michezo Tanzania.


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)









