Na Mwandishi Wetu
WANANCHI wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) wanaendelea kunufaika na huduma mbalimbali za mawasiliano na ofa maalum zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia banda lake lililopo katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere.

Katika banda hilo, maafisa wa TTCL wanatoa elimu kuhusu huduma na suluhisho mbalimbali za mawasiliano pamoja na teknolojia za kidijitali, huku wakiwawezesha wananchi kujionea uwezo wa intaneti ya kasi ya juu na huduma zinazolenga matumizi ya nyumbani, taasisi na biashara.

Mbali na elimu hiyo, TTCL imeandaa ofa maalum za Sabasaba zinazowawezesha wateja kupata vifaa vya mawasiliano kwa bei zilizopunguzwa pamoja na huduma mbalimbali za kidijitali zinazorahisisha mawasiliano na shughuli za kila siku.

Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Banda la TTCL, Bi. Janeth Maeda, alisema ushiriki wa shirika hilo katika Sabasaba 2026 unalenga kuwasogezea wananchi huduma karibu zaidi, kuongeza uelewa kuhusu bidhaa na huduma za TTCL, pamoja na kuimarisha mahusiano na wateja na wadau.

Alisema maonesho hayo pia yanatoa nafasi muhimu kwa TTCL kupokea maoni na mrejesho kutoka kwa wateja ili kuendelea kuboresha huduma zake na kuendana na mahitaji ya soko la mawasiliano linalokua kwa kasi.

Aidha, wananchi na wadau wanaotembelea banda hilo wanapata fursa ya kutumia huduma ya Public Wi-Fi bila malipo, hatua inayowawezesha kujionea ubora na kasi ya intaneti inayotolewa na TTCL.

TTCL imeendelea kuwahamasisha wananchi kutembelea banda lake katika kipindi chote cha maonesho ili kujionea teknolojia bunifu, kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu huduma za mawasiliano na kunufaika na ofa mbalimbali zilizoandaliwa mahsusi kwa maonesho ya Sabasaba 2026



Lusaka, Julai 8, 2026
AFISA Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel Africa, Sunil Taldar, ametangaza dhamira ya kuunganisha shule 5,000 na mtandao wa intaneti ifikapo mwaka 2027 katika nchi 14 barani Afrika ambapo kampuni hiyo inatoa huduma. Hatua hii inatekelezwa kupitia taasisi yake ya hisani, Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF).

Hadi sasa, mradi huo wa ushirikiano wenye thamani ya dola milioni 57 uliozinduliwa mwaka 2021, umefanikiwa kuunganisha shule 3,296 na kutoa fursa ya mtandao kwa zaidi ya wanafunzi milioni 2 na walimu takribani 40,000. Maeneo 64 ya kujifunzia kwa njia za mtaondao yameondolewa malipo (zero-rated), na kuwawezesha watumiaji zaidi ya milioni 11 kupata maudhui ya elimu bila gharama yoyote.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Shule ya Wasichana ya Mtakatifu Monika (St. Monica) mjini Lusaka, ambayo ni moja ya shule 300 zilizokwishaunganishwa na intaneti nchini Zambia, Afisa Mtendaji Mkuu huyo wa Airtel Africa alieleza kuwa mpango huo una mchango mkubwa katika kuboresha ubora wa elimu kwa kupanua fursa ya kupata rasilimali za kidijitali za kujifunzia kwa watoto wa Afrika, kwa kushirikiana na serikali husika.

Bw. Taldar aliongeza: "Wanafunzi wanapata elimu ya kiwango cha juu kutoka kwenye mtaala ulioandaliwa na UNICEF kwa kushirikiana na Wizara mbalimbali za Elimu, inayopatikana kupitia mtandao wa Airtel. Pia tunawajengea uwezo walimu ili waweze kutumia njia za kidijitali kwa ufanisi kutoa elimu. Lengo letu ni kuendelea kuimarisha upatikanaji wa mtandao wenye tija mashuleni kwa kutoa intaneti ya bure, majukwaa yasiyotozwa gharama za data, na kuwanoa walimu kote barani."

Akitoa shukrani zake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Wasichana ya Mtakatifu Monika (St. Monica), Sr. Matilda Soloko alisema: "Sisi ni miongoni mwa mwa shule za kwanza kabisa kuunganishwa katika awamu ya kwanza na wanafunzi wetu wameweza kusoma kwa kutumia njia za kidijitali kujifunzia na uelewa wao katika masomo umeimarika sana. Tunwashukuru sana Airtel na UNICEF."

Mwakilishi wa UNICEF nchini Zambia, Dkt. Saja Farooq Abdullah alisema: "Ushirikiano wet una Airtel Africa ni kuziba pengo la ujumuishi wa kidijitali. Tunataka kuhakikisha kwamba kila mtoto anaweza kujifunza sehemu yoyote alipo. Kwetu, jambo la kujivunia sana kuona wanafunzi hawa wasichana wanavyoweza kujifunza kwa wakati na kasi yao wenyewe, jinsi wanavyoweza kupitia upya masomo, na jinsi wanavyofanya kazi zao za nyumbani (homework) kwa urahisi."

Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari katika Wizara ya Elimu nchini Zambia, Yvonne Mwemba Chuulu, aliwapongeza UNICEF na Airtel kwa ushirikiano huo akisema: "Sisi kama Wizara ya Elimu hatuwezi kufanya haya peke yetu, na tunashukuru kwa ushirikiano tulio nao na wenzetu wa Airtel Africa na UNICEF. Watoto wetu wana uwezo wa kujifunza kwa mfumo mseto, ambapo tuna mwalimu ambaye pia anatumia vifaa vya kidijitali. Pia tumesikia kutoka kwa wanafunzi kwamba wana uwezo wa kuingia kwenye mifumo ya kidijitali wakiwa nyumbani, jambo ambalo ni zuri kwa sababu wanafunzi wetu wanaendelea kujifunza wakiwa katika mazingira ya majumbani mwao."

Mpango huu wa Kuunganisha Shule unatoa uwanja mpana kwa wanafunzi kujifunza kwa njia za kidijitali katika nchi 13: Chad, Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Gabon, Kenya, Madagascar, Malawi, Niger, Nigeria, Rwanda, Tanzania, Uganda, na Zambia. Kwa kuzipatia shule hizi huduma ya intaneti na kuwapatia walimu mafunzo ya matumizi ya zana za kidijitali, mpango huu unawapa watoto, hasa katika maeneo ya pembezoni mwa miji na ya vijijini, zana na ujuzi wa kidijitali wanaouhitaji ili kufanikiwa.

Taasisi ya Airtel Africa Foundation inaendelea kuboresha maendeleo jumuishi kupitia nguzo nne za kimkakati: Ujumuishi wa Kifedha, Elimu, Uendelevu wa Mazingira, na Ujumuishi wa Kidijitali. Ripoti ya Mwaka ya Airtel Africa Foundation ya 2025/26 inapatikana katika www.airtelafricafoundation.org.

Kamati ya Siasa na Utekelezaji ya CCM Mkoa wa Geita imeridhishwa na mwendo wa ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe.

Jengo hilo lililokwama kwa muda mrefu baada ya mkandarasi kushindwa kumaliza mkataba, sasa linaendelezwa na Halmashauri kupitia force account na limefikia asilimia 68 ya ukamilishaji.

Pesa zilizopokelewa kwa ajili ya mradi huo ni takribani shilingi bilioni 1.8.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi wa mradi huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nicholous Kasendamila ameipongeza Halmashauri kwa hatua madhubuti zilizochukuliwa kuhuisha mradi huo.

Amesema kwa sasa mwendo wa ujenzi ni wa kuridhisha.

Mwenyekiti Kasendamila amewataka watendaji wa Halmashauri hiyo kuwa tayari kupokea ushauri na maelekezo kutoka kwa viongozi ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati bila kusuasua.














Families, architects, students and members of the public gathered at dawn on Saturday, 11 July 2026, for a memorial walk honouring the late Beda Amuli, one of Tanzania’s pioneering architects whose work helped shape Dar es Salaam’s built identity.

Organised by Amuli’s family in collaboration with the Architectural Association of Tanzania (AAT), the walk was held under the theme, “Designing Tanzania: Architecture for People, Place, and Purpose.”

The journey began at the Old Boma Building along Sokoine Drive before proceeding, under police and traffic escort, to selected landmarks associated with the city’s architectural history, including the Kilimanjaro Hotel, the Institute of Finance Management, the National Cooperative Building and Kariakoo Market.

AAT President Architect T’Chawi said Amuli did more than design buildings; he created civic spaces where Tanzanians could work, learn, trade and gather.

The walk concluded at Kariakoo Market with reflections, media engagement and closing remarks, followed by a memorial church service at St Alban’s Anglican Church.

Ten years after his passing, Beda Amuli’s legacy remains embedded in Dar es Salaam’s streets, institutions and public spaces, inspiring a new generation to appreciate architecture as national identity and public service.














 

Na. Mwandishi Wetu, Dar.

MKUU wa Wilaya ya Kisarawe Mhe. Petro Magoti ameipongeza Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa namna ilivyofanya maboresho ya Mitaala ya Elimu nchini yenye lengo la kumfanya muhitimu kuweza kujiajiri au kuajiriwa mara anapomaliza masomo  yake.

Mhe. Magoti ameyasema hayo leo tarehe 12/7/2026 katika maonesho ya Sabasaba ambapo amesema kuwa TET inafanya kazi nzuri ya kuboresha elimu nchini.

"Kwa kweli nawapongeza kwa kazi nzuri ya kuboresha Elimu nchini hasa hivi karibuni katika maboresho ya mitaala yaliyofanyika, ni tumaini langu kwamba wanafunzi nchi nzima wataendelea kufanya vyema, " Amesema mhe. Magoti.

Pia ameeleza, anafurahia namna wanafunzi wanaendelea kupatiwa vitendea kazi kama vitabu vinavyowapelekea kuendele kufanya vyema wakati wa masomo yao na kuendelea kuipongeza TET kwa uratibu mzuri na upatikanaji wa vitabu  mashuleni.

TET inashiriki katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya  biashara maarufu kama Sabasaba  yaliyoanza tarehe 28, Juni ambapo yanatarajiwa kufungwa hapo kesho, Julai 13.









Dar es Salaam, Julai 12, 2026

Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. William Kafiti, amesema Hifadhi Skimu ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) imeendelea kuwa mkombozi kwa wananchi waliojiajiri kwa kuwapa fursa ya kujiwekea akiba kwa ajili ya maisha ya baadaye, huku akiipongeza NSSF kwa kuimarisha huduma kwa wanachama kupitia mifumo ya kidijitali na utoaji wa huduma wenye viwango vya juu.

Akizungumza baada ya kutembelea banda la NSSF katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Mhe. Kafiti alisema ameridhishwa na kiwango cha huduma kinachotolewa na Mfuko huo, akibainisha kuwa wananchi wanapokelewa na kuhudumiwa kwa weledi, haraka na kwa kutumia teknolojia ya kisasa inayorahisisha upatikanaji wa huduma.

"Nimefurahishwa sana na huduma nilizoziona hapa, kila mfanyakazi yuko tayari na ana ari ya kumhudumia mwananchi kwa weledi na kwa wakati. Hili linaonesha dhamira ya kweli ya NSSF ya kuwahudumia Watanzania kwa viwango vya hali ya juu," alisema Mhe. Kafiti.

Alisema mafanikio hayo yanaakisi jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuimarisha sekta ya hifadhi ya jamii na kupanua wigo wa huduma kwa wananchi wote, hususan waliojiajiri ambao kwa miaka mingi walikuwa nje ya mfumo rasmi wa hifadhi ya jamii.

Mhe. Kafiti alieleza kuwa kuanzishwa kwa Hifadhi Skimu kumefungua ukurasa mpya kwa makundi mbalimbali ya wananchi waliojiajiri, wakiwemo bodaboda, mama na baba lishe, wafanyabiashara wadogo, wavuvi, wachimbaji wadogo wa madini, mafundi na makundi mengine ya wajasiriamali, kwa kuwawezesha kujiwekea akiba itakayowawezesha kuwa na uhakika wa kipato wanapofikia uzee.

"Kila mmoja atazeeka. Kesho iliyo bora hujengwa na maamuzi ya leo. Kupitia Hifadhi Skimu, NSSF imewapa wananchi waliojiajiri fursa ya kujenga maisha yenye uhakika baada ya kipindi chao cha kufanya kazi. Huu ni mpango unaostahili kuungwa mkono na kila Mtanzania," alisisitiza.

Aidha, aliipongeza NSSF kwa maboresho makubwa ya mifumo ya kidijitali yanayowawezesha wanachama kupata taarifa za michango yao kwa urahisi kupitia simu za mkononi, hatua aliyoielezea kuwa ni mapinduzi makubwa katika utoaji wa huduma za hifadhi ya jamii.

Mhe. Kafiti aliongeza kuwa NSSF inaendelea kutekeleza kwa vitendo azma ya Serikali ya kujenga taifa lenye wananchi wanaojitegemea kiuchumi kwa kuwawezesha kuweka akiba wakiwa bado wana nguvu za kufanya kazi ili wanapostaafu waendelee kuishi kwa heshima kupitia mafao na pensheni wanazostahili.

Naye, Theonasy Ngunga, mmoja wa wananchi waliotembelea banda la NSSF alieleza kuridhishwa na huduma alizopata, akisema alipokelewa kwa heshima, akaelekezwa katika kila hatua na ndani ya muda mfupi akapatiwa elimu kuhusu Hifadhi Skimu na kukamilisha taratibu za kujiunga na NSSF Portal.

"Nilipoingia nilipokelewa vizuri na kupewa maelekezo katika kila hatua. Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimehudumiwa na kuelewa namna ya kuchangia kupitia mifumo popote nilipo," alisema.

Kupitia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, NSSF inaendelea kuwahamasisha wananchi, hususan waliojiajiri, kujiunga na Hifadhi Skimu ili kujenga akiba kwa ajili ya maisha ya baadaye. Juhudi hizo zinaendana na azma ya Serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya hifadhi ya jamii na kujenga kesho yenye uhakika kupitia mfumo endelevu wa hifadhi ya jamii.















Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi  ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.

















Top News