
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo,(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi) Luhaga Joelson Mpina pamoja na Maaskofu Katoliki katika mazishi Mwadhama Askofu Mstaafu Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina pamoja na Mwenyekiti wa Zamani wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia katika mazishi ya Askofu Mkuu Mstaafu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina akisalimiana na Waziri Msaafu wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Profesa Anna Kajumulo Tibaijuka mara baada Adhimisho la Misa Takatifu ya Kumuombea Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Februari 2026Na Seif Mangwangi, Michuzi TV Arusha
WAKUU wa nchi wanachama wa umoja wa Afrika ambazo bado hazijaridhia itifaki ya uanzishwaij wa mahakama ya Afrika ya Haki za binaadam na Watu(AfCPHR), wametakiwa kuharakisha itifaki hiyo Ili kuruhusu Haki na demokrasia kutendeka katika nchi zao.
Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mwaka wa mahakama ya Watu na Haki za binaadam 2026 pamoja na maadhimisho ya miaka20 tangu kuanzishwa Kwa mahakama hiyo leo 2Machi 2026, Rais wa Jamhuri ya Ghana, John Dramani Mahama amesema hakuna jambo la kuogopa Kwa kuwa mahakama hiyo Ina lengo la kutenda haki pekee.
Amesema Baba yake ambaye alishawahi kuwa Waziri katika utawala wa Rais Kwame Nkuruma alishawahi kuwekwa kizuizini Kwa zaidi ya miaka 14 kwa kusema ukweli na baadae kuachiliwa lakini kungekuwa na mahakama hiyo familia ingeweza kufikisha mashtaka katika mahakama hiyo.
“ Nipende kutoa wito kwa wakuu wa nchi ambazo bado hawajaridhia itifaki ya mahakama hii kuridhia Kwa kuwa hakuna cha kuogopa, waridhie Ili kuwezesha wananchi wao pamoja na asasi za kiraia kufikisha malalamiko Yao pale wanapoona Sheria hazijafuatwa,” amesema.
Amesema ukiukwaji wa Haki za binaadam husababisha athari kubwa kwa familia na jamii na hivyo uwepo wa mahakama hiyo husaidia kupatikana kwa haki dhidi ya wale ambao wamekuwa wakizikiuka.
Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za binaadam na Watu, Jaji Blaisse Tchikaya amesema katika kuadhimisha miaka 20 ya mahakama hiyo, bado kumekuwepo na changamoto nyingi ikiwemo watu wengi kutofahamu majukumu ya mahakama hiyo.
Aidha amesema upungufu wa fedha umekuwa ni kikwazo kingine kinachosababisha mahakama hiyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ikiwemo kutoa elimu Kwa wadau wa mahakama hiyo.
“Wakati tunaadhimisha miaka 20 ya mahakama bado tunakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinahitajii ufumbuzi wa haraka Kwa ushirikiano wa wadau mbalimbali hususani wakuu wa nchi, mfano Afrika tuna nchi 55 lakini zilizoridhia itifaki ya mahakama hii ni nchi 35 pekee, utaona hapa bado Kuna kazi ya kufanya,” amesema Jaji Tchikaya.
Amesema changamoto nyingine ni nchi wanachama kushindwa kutekelezaji maamuzi yanayoamuliwa na mahakama hiyo jambo ambalo limekuwa likififisha demokrasia na kurudisha nyuma malengo ya kuanzishwa Kwa mahakama hiyo.
Kwa upande wake Wakili Mkuu wa Serikali Dkt Ally Posi amesema Serikali ya Tanzania inaendelea kufanyiakazi itifaki ya kuruhusu asasi za kiraia kuweza kufikisha mashauri yao katika mahakama hiyo baada ya kujiondoa katika kipengele hicho.
Hata hivyo Wakili Dkt Posi amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa msaada wake kwa mahakama hiyo kwa kuwa ni chombo kilichoanzishwa Kwa lengo la Kukuza demokrasia katika bara la Afrika.

New Delhi, Machi 2, 2026: GSMA imemtunuku Tuzo ya Maisha (Lifetime Achievement Award) Sunil Bharti Mittal, Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bharti Enterprises, kwa kutambua mchango wake mkubwa katika kubadili na kuunda upya taswira ya mawasiliano ya simu duniani pamoja na kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa waendeshaji, serikali, biashara na mabilioni ya watumiaji.
Tuzo hiyo, ambayo imetolewa kwa viongozi wachache tu katika historia ya GSMA, hutambua mchango wa kipekee ulioacha alama ya kudumu na yenye mwelekeo katika mfumo wa kimataifa wa mawasiliano.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa wakati wa mkutano wa Mobile World Congress uliofanyika Barcelona, mbele ya uwepo wa Mfalme Felipe VI wa Hispania, Waziri Mkuu wa Hispania Pedro Sanchez, Rais wa Catalonia Salvador Illa, pamoja na viongozi wakuu wa sekta hiyo kutoka duniani kote.
Akiwa miongoni mwa vinara wa maono katika sekta ya mawasiliano, Mittal ameijenga Bharti Airtel kuwa miongoni mwa waendeshaji wakubwa zaidi wa huduma za simu duniani, ikiwa na shughuli zake India na barani Afrika. Kampuni hiyo imeorodheshwa miongoni mwa waendeshaji watatu wakuu duniani na inahudumia zaidi ya wateja nusu bilioni.
Aliongoza upanuzi wa huduma za simu katika masoko yanayoibukia na pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa GSMA kati ya mwaka 2017 na 2018, ambapo alitetea sera zinazochochea uwekezaji na ubunifu, huku akiimarisha dhamira ya sekta ya kuunganisha wasiofikiwa na kukuza ujumuishwaji wa kidijitali.
Awali, Mittal alitunukiwa Tuzo ya Mwenyekiti wa GSMA mwaka 2008 na tena mwaka 2016 kwa mchango wake bora katika kukuza na kuendeleza sekta ya simu duniani, na aliheshimiwa tena wakati wa Mobile World Congress mwezi Februari 2019 kwa kutambua uongozi wake kama Mwenyekiti wa GSMA.
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mittal alisema:
“Nimeheshimiwa sana kupokea tuzo hii na ninaishukuru kwa dhati GSMA kwa kunitambua. Naipokea si tu kama mafanikio binafsi, bali kama heshima kwa safari ya sekta ya mawasiliano ya India, ari ya pamoja ya Bharti, na kuibuka kwa kampuni za mawasiliano za India katika jukwaa la kimataifa. Sekta ya mawasiliano ni nguvu inayopanua fursa, inayoweka huduma muhimu mikononi mwa kila mtu na kufungua uwezo wa kibinadamu. Kushiriki katika kuunda mageuzi yake na kuifanya kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kisasa ni jukumu la heshima kubwa. Kadiri ubunifu unavyozidi kushika kasi, tutaendelea kushirikiana na wadau wetu kuhakikisha ukuaji unaendeleza usawa na kuleta fursa endelevu kwa vizazi vijavyo.”
Tuzo ya Maisha ya GSMA ni heshima adimu inayotolewa kwa watu wachache tu waliodhihirisha uongozi na ubunifu uliobadili mwelekeo wa sekta kwa namna ya kudumu.
Mapinduzi ya Kahawa Mbinga Yawanufaisha Wakulima, Wawapongeza Wadau huku Wakiahidi Uzalishaji zaidi.
Wakulima wa zao la kahawa wilayani Mbinga, mkoani Ruvuma wameonyesha matumaini makubwa na jitihada pamoja na mikakati ya uboreshaji wa kilimo cha zao hilo wilayani humo huku wakiwashukuru wadau mbalimbali likiwemo serikali na shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) kwa jitihada zake hususani kwenye utoaji wa mafunzo ya mbinu bora za kilimo cha zao hilo.
Jitihida za shirika hilo zimewafikia wakulima wadogo wapatao 2,000 kupitia vikundi 65 na vyama vya Ushirika wa Msingi (AMCOS) 10 ambapo wamepatiwa mafunzo ya mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea.Wakizungumza wakati wa ziara ya maofisa wa HRNS wilayani humo, viongozi wa vikundi na AMCOS hizo zilizonufaika na jitihada za shirika hilo walisema matokeo ya jitihada za shirika hilo lililoanza mradi huo miaka mitatu iliyopita, yameanza kuonekana hususani kwenye ongezeko la bei ya zao hili kutoka wastani wa sh 7,000 hadi kufikia zaidi ya Sh 11,000 kwa kilo katika msimu uliopita.
Ongezeko hilo linalotafsiriwa moja kwa moja kuwa ni matokeo ya ubora wa kahawa inayozalishwa na ongezeko la uelewa wa wakulima hao kuhusu bei stahiki za zao hilo.
“Mabadiliko haya yanatafsiriwa moja kwa moja kuwa nafuu kwa wakulima na matumaini mapya kwa vijana wanaotazama kilimo kama ajira yenye heshima,” alisema Bw. Steven Milinga, Mwenyekiti wa Kikundi cha Ngwindi Group chenye wanachama 29 wenye uwiano unaokaribiana wa jinsia.
Kwa mujibu wa Bw. Milinga, mafunzo ya kilimo cha kisasa na ujasiriamali waliyopata kupitia HRNS yamewawezesha kuzalisha miche 30,000 kati ya lengo la miche 150,000. Aidha, kikundi hicho kimefanikiwa kukopa Sh milioni 70 kutoka Halmashauri ya Wilaya, fedha zinazowezesha ujenzi wa nyumba ya kulala wageni katika Kata ya Mpapa, Mbinga Vijijini – hatua inayoashiria kupanuka kwa wigo wa uwekezaji wa wakulima hao.
“Tumepata hamasa kubwa. Tuna ndoto kubwa licha ya changamoto zilizopo, ikiwemo uhitaji wa neti za vivuli kulinda miche, viliba vya kutosha (tube za kuoteshea miche) na kuboresha mfumo wa maji kutoka milimani ili kurahisisha upatikanaji wa maji vitaluni,” aliongeza.
Kwa upande wake, Bi. Grace Ndunguru, Mwenyekiti wa AMCOS ya Kigoti katika kata hiyo, alisema mradi huo umeleta mageuzi ya dhahiri katika uzalishaji na usimamizi. “Tulianza kwa kujifunza kuanzisha vitalu vya miche kutumia mbegu bora tulizopewa kutoka Taasisi ya Utafiti wa zao la Kahawa nchini (TaCRI). Leo tunauza miche kwa wanachama na watu binafsi. Mapato hayo yametuwezesha kujenga ofisi ya kisasa ya AMCOS yetu. Huu ni uthibitisho kuwa tukipata maarifa na umoja, tunaweza,” alisema kwa furaha.
Naye Bw. January Komba, mwanachama na Bwana Shamba wa Kikundi cha Namwang’ina, Kata ya Kitanda, alisema msaada wa mbegu bora, pampu ya maji na viliba vya miche umepunguza kwa kiasi kikubwa upotevu wa miche wakati wa upandikizaji. “Tofauti kati ya zamani na sasa ni kubwa. Tunaona mashamba yenye afya na tija zaidi,” alisisitiza.
Akizungumzia hatua hiyo, Mtaalamu wa Kilimo wa HRNS, Bw. Isack Lungu, alisema kabla ya kuanza kwa mradi huo wakulima walikabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa miche bora, uelewa mdogo wa mbinu za kisasa za kilimo na mitaji haba.
“Walikuwa wanajitahidi, lakini bila zana sahihi na maarifa ya kisasa. Sasa wamejengewa uwezo wa kuanzisha na kusimamia vitalu, kutumia pembejeo kwa usahihi, kupulizia dawa kwa wakati na kuweka mbolea kwa mpangilio unaoongeza tija. Tunaona mashamba yenye afya, mavuno bora na ari mpya ya uzalishaji,” alisema.
Mbali na mafunzo, baadhi ya AMCOS zimepatiwa neti za vivuli (shed nets), viliba vya kuoteshea miche na mbegu bora. Hatua hiyo imeongeza uzalishaji wa miche yenye ubora na inayostahimili magonjwa ya kahawa, ikiweka msingi imara wa uzalishaji endelevu kwa miaka ijayo.
Kwa mujibu wa Bw. Benson Wanyuike, Mhamasishaji (Producer Organiser Trainer) wa HRNS, mafanikio hayo yametokana pia na kuimarika kwa ushirika na uelewa wa masoko. “Tumewekeza katika elimu ya uongozi, uwazi na usimamizi wa vyama. Wakulima sasa wanaelewa haki na wajibu wao, wanashiriki kikamilifu kwenye minada na wanafuatilia bei kwa uelewa mkubwa zaidi. Hata hivyo maboresho hayo kwenye mfumo wa ushirika yanawahakikishia wakulima kunufaika pale soko linapokuwa zuri zaidi,’’ alisema.
Mapinduzi haya hayakuishia shambani pekee. Vikundi 65 vilivyofikiwa vimeanzisha miradi mingine ya kiuchumi ikiwemo ufugaji wa nyuki, samaki, uzalishaji wa maparachichi, pamoja na ujenzi wa nyumba za kulala wageni na ofisi za AMCOS. Mkakati huo wa vyanzo mbadala vya mapato umepunguza utegemezi wa zao moja na kuimarisha ustahimilivu wa kaya kiuchumi.
Aidha, katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, HRNS imesambaza zaidi ya miti 200,000 ya kivuli na matunda kwa wakulima wa Mbinga. Miti hiyo inachangia kuongeza kivuli mashambani, kuboresha afya ya udongo na kufyonza hewa ya ukaa.
“Tunajenga mashamba yanayostahimili joto kali na mvua zisizotabirika. Huu ni uwekezaji kwa kizazi kijacho,” aliongeza Bw. Lungu.
Zaidi, wataalamu hao wa HRNS walitoa wito kwa Serikali na wadau wengine kuendelea kuhamasisha wakulima kujiunga na vikundi na vyama vya ushirika ili kuongeza tija, uwazi na nguvu ya pamoja katika kilimo na biashara ya kahawa.
“Uzoefu wa Mbinga unaonesha wazi kuwa uwekezaji katika elimu ya kilimo, kuimarisha ushirika na mikakati himilivu kwa tabianchi unaweza kugeuza changamoto kuwa fursa. Leo, kahawa ya Mbinga si zao la biashara tu – ni alama ya mageuzi, umoja na matumaini mapya kwa maelfu ya familia za wakulima, na injini mpya ya kuchochea uchumi wa vijijini.’’ Alihitimisha Bw Lungu.

Wakulima wa zao la kahawa wa kikundi cha Mangwagala kilichopo kata ya Kitanda, wilayani Mbinga mjini wakihudumia kitalu cha miche ya zao walipotembelewa na maofisa wa Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho ni moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea.

Wakulima wa zao la kahawa wa AMCOS ya Kigoti iliyopo Kata ya Mpapa, Mbinga Vijijini wakionesha mbegu bora za zao hilo walizootesha kwenye kitalu chao walipotembelewa na maofisa wa Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. AMCOS hiyo ni moja ya AMCOS 10 na vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea. Kushoto Mtaalamu wa Mawasiliano wa Kanda kutoka HRNS Bw Muddy Kimweri.

Wakulima wa zao la kahawa wa kikundi cha Ngwindi kilichopo Kata ya Mpapa, Mbinga Vijijini wakionesha mbegu bora za zao hilo walizootesha kwenye kitalu chao walipotembelewa na maofisa wa Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho ni moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea. Pamoja nao yupo Mtaalamu wa Mawasiliano wa Kanda kutoka HRNS Bw Muddy Kimweri (wa tatu kushoto)

Wakulima wa zao la kahawa wa kikundi cha Uhai Uzena kilichopo Wilayani Mbinga wakionesha mbegu bora za zao hilo walizootesha kwenye kitalu chao walipotembelewa na maofisa pamoja na wataalamu wa kilimo kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho ni moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea. Pamoja nao yupo Mtaalamu wa Mawasiliano wa Kanda kutoka HRNS Bw Muddy Kimweri (kushoto)

Wakulima wa zao la kahawa wa kikundi cha Namwang’ina kilichopo kata ya Kitanda, wilayani Mbinga mjini wakihudumia kitalu cha miche ya zao walipotembelewa na maofisa na wataalam wa kilimo kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho ni moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea.

Wakulima wa zao la kahawa wa kikundi cha Amkeni Kitelea kilichopo wilayani Mbinga wakimsikiliza kwa umakini Mtaalamu wa Mawasiliano wa Kanda kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani Bw Muddy Kimweri wakati maofisa wa na wataalam wa kilimo kutoka shirika hilo walipowatembelea wakulima hao mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho ni moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea.

Wakulima wa zao la kahawa wa AMCOS ya Kigoti iliyopo Kata ya Mpapa, Mbinga Vijijini wakionesha maendeleo ya ujenzi wa ofisi za AMCOS hiyo walipotembelewa na maofisa wa Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. AMCOS hiyo ni moja ya AMCOS 10 na vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea. Pamoja nao yupo Mtaalamu wa Mawasiliano wa Kanda kutoka HRNS Bw Muddy Kimweri (wa tatu kushoto)

Mwenyekiti wa Kikundi cha wakulima cha Vumilia kilichopo Kata ya Mpapa, Mbinga Vijijini Bw Reginald Ndunguru (wa pili kushoto) akionesha maendeleo ya mradi wa bwawa la Samaki unaotekelezwa na kikundi hicho walipotembelewa na maofisa wa Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea.

Wanachama wa kikundi cha wakulima cha Agriculture Arusha kilichopo wilayani Mbinga wakionesha maendeleo ya mradi wa ufugaji nyuki unaotekelezwa na kikundi hicho walipotembelewa na maofisa wa Shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki. Kikundi hicho moja ya vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika hilo inayolenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea.

Muonekano wa kitalu cha kukuzia miche ya kahawa kinachomilikiwa na AMCOS ya Kigoti iliyopo Kata ya Mpapa, Mbinga Vijijini. AMCOS hiyo ni moja ya AMCOS 10 na vikundi 65 vyenye jumla ya wakulima 2000 walionufaika na program ya mafunzo na uwezeshwaji kutoka shirika lisilo la kiserikali la Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) la nchini Ujerumani Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wakulima hao kuhusu mbinu bora za kilimo cha kahawa, usimamizi wa vitalu vya miche bora ya kisasa na kuimarishwa kwa mifumo ya ushirika ili waweze kujiendesha kwa ufanisi na kujitegemea
Mbunge wa Jimbo la Katoro, Mhandisi Kija Limbu Ntemi, ametoa onyo kali kwa taasisi za kifedha zinazowadhulumu wananchi kupitia mikopo isiyo na tija, huku akiwataka wananchi kuwa makini na mikataba wanayoingia.
Agizo hilo la Mbunge limekuja baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi ambao nyumba zao zimekuwa zikipigwa mnada kwa bei ya hasara, kulinganisha na kiasi kidogo cha mkopo walichochukua.
Mhandisi Kija amebainisha kuwa hali hiyo imekuwa ikileta maumivu makali na kuwafanya wananchi wengi kubaki bila makazi huku wakikosa faida yoyote kutokana na mali zao.
Mbunge Kija ameyasema hayo leo wakati akizindua rasmi Ofisi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Kilimahewa, ambayo imeanza kutumika rasmi kwa ajili ya kuratibu shughuli za maendeleo na kero za wananchi wa eneo hilo.
Mhandisi Kija Amemuagiza Mtendaji wa Kata ya Ludete kuitisha mkutano wa mabalozi wa Kata za Katoro na Ludete.
Amesisitiza kuwa wananchi na mabalozi wanahitaji kupata elimu ya mahakama na taratibu za kisheria ili kutambua namna ya kutatua migogoro ya mikopo na uuzaji wa mali.
Amewatahadharisha wakopeshaji kuhakikisha taratibu zote za kiofisi na nyaraka (documents) zinazingatiwa wakati wa kukopesha na kurejesha.
"Tunaomba hili jambo lizingatiwe. Wanaokopesha wachukue tahadhari sasa; unapomkopesha mtu kwa documents, hakikisha anakulipa kwa documents. Sisi tutawashughulikia kweli ili kulinda heshima ya wananchi wetu," alisisitiza Mhandisi Kija.
Mhandisi Kija ameongeza kuwa hatanyamazia wote wanaowanyanyasa wananchi kwa kuwauzia nyumba zao bila kunufaika na chochote, na ameahidi kusimamia haki za wanyonge katika jimbo lake.
-Asisitiza amani na kuishi kindugu
WAZIRI MKUU Dkt Mwigulu Nchemba amewaomba Wabunge wa Mbulu na uongozi wa wilaya hiyo waendelee kutoa elimu kwa wananchi juu ya kuendeleza amani na kuishi kindugu.
Ametoa wito huo leo (Jumatatu, Machi 2, 2026) wakati akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye hospitali ya Lutheran ya Haydom, wilayani Mbulu, mkoani Manyara mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la afya ya mama na mtoto.
“Nimepata taarifa ya kuwepo kwa mizozo kule Yaeda Chini. Waheshimiwa Wabunge wa majimbo haya mawili na viongozi wa Halmashauri kaeni na wananchi muwaelimishe kuwa ardhi haiongezeki. Kaeni na wananchi muwaeleze kuwa suluhisho ni kupanga matumizi bora ya ardhi.”
“Endeleeni kuwaelimisha wananchi kuwa hata wakipigana ardhi haiongezeki. Hata mkiwaondoa kabila fulani, bado ardhi haiongezeki kwa sababu watu wanaendelea kuzaa.”
Akizungumzia kuhusu ujenzi wa jengo hilo, Waziri Mkuu amesifu kazi nzuri iliyofanywa na akamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya hospitali zinazoendeshwa na taasisi za dini ili kuboresha utoaji huduma kwenye hospitali hizo.
“Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alielekeza taasisi zinazotoa huduma kwa jamii (charitable organisations) zipewe nafuu ya kikodi. Hii ni kwa sababu hizi taasisi hazifanyi biashara na serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na hizo taasisi,” amesema.
Akitoa maelezo kuhusu fedha zinazotolewa na serikali kwenye hospitali hiyo, Naibu Waziri – OWM-TAMISEMI (Elimu), Reuben Kwagilwa alisema kumekuwa na ushirikiano wa mrefua ambapo kila mwezi, Serikali imekuwa ikilipa sh. milioni 188 kwa ajili ya watumishi 128 wa hospitali hiyo.
“Serikali pia imekuwa ikitoa ruzuku ya sh. milioni 545 kila mwaka ambazo hupitia MSD kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba. Vilevile, imekuwa ikitoa sh. milioni 57 kila mwaka kwa ajili ya uendeshaji wa hospitali,” amesema.
Mapema, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mbulu, Askofu John Nade alimweleza Waziri Mkuu kwamba wanashukuru kwa ushirikiano uliopo baina ya Serikali na kanisa kwenye utoaji wa huduma za jamii.
Alisema mbali na hospitali, wana Taasisi ya Afya ya Haydom ambayo inatoa mafunzo kwenye kozi tano ambazo ni Radiolojia, Famasia, Afisa Tabibu, Maabara na Uuguzi.
Akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Haydom, Dkt. Paschal Mdoe alisema ujenzi wa jengo hilo umegharimu sh. bilioni 6.3 ambazo zimetokana na vyanzo vya ndani na marafiki wa Haydom Norway.
Alisema hospitali hiyo ya Kanisa imekuwa mdau mkubwa na wa muda mrefu katika sekta ya afya, ikitoa huduma za rufaa na kibingwa kwa wananchi wa Mkoa wa Manyara na mikoa jirani, pamoja na kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za afya ya jamii.
TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Machi 2, 2026 imekutana na Mtaalamu wa Uchunguzi wa Kisayansi na Usalama wa Mtandao, Yusuph Kileo.
Mkutano huo wa Tume na Mchunguzi huyo umefanyika katika ukumbi wa Tanganyika uliopo jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Tume kukusanya taarifa, maoni na ushauri kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo wataalamu, watu wa kawaida, viongozi wa sasa na wastaafu.
Katika mkutano huo hoja zilizojadiliwa zilihusu maeneo ya tathmini ya athari za matukio hayo ndani ya nchi na kimataifa na ushauri wa hatua za kijamii na kisheria zinazochukuliwa ili kuimarisha amani, mshikamano wa kitaifa.
Hivi karibuni Mamlaka ya Uteuzi imeiongezea Tume muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia tarehe 20 Februari, 2026 ili Tume iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025 na kuitaka ikamilishe kazi na kuwasilisha Taarifa yake kabla au ifikapo tarehe 3 Aprili, 2026.
Tume inaendelea na mahojiano na waathirika wa Matukio hayo kwa ajili ya hatua zaidi kama Taifa ili Matukio kama hayo yasijirudie tena.
Msanii kutoka Zanzibar Bi Fatma Issa aliimba tahadhari na adui kiumbe, daima asikusibu na Mungu akuepushie.
Nyumbu wakiwa wanazaliwa katika eneo la Ndutu huomba sana Mungu awaepushie adui kiumbe kama Fisi, Simba, chui na mbweha ambao nao msimu huo huhamia katika eneo la Ndutu hifadhi ya Ngorongoro ili kuwavizia Nyumbu na watoto wao.
Hata hivyo kwa kuwa Mungu ni wa wote, huwaepusha nyumbu na adui hao kwa kuwa katika safari ya nyumbu, kuanzia wanapozaliwa Ndutu na kuanza mzunguko wa kuhama kila mwaka kuelekea Kenya, hukabiliana na changamoto nyingi za kuliwa na wanyama wala nyama lakini wengi husalimika.
Kila nyumbu mzima (adult) ni ushahidi wa ustahimilivu mkubwa kwamba alinusurika hatari wakati wa kuzaliwa, akapita salama katika mito yenye mamba na wanyama wanaokula Nyama (Predators) katika maisha ya kila siku. Kuishi hadi utu uzima kwa nyumbu ni matokeo ya ushindi dhidi ya vikwazo vingi vya asili vilivyojaa taabu, chuki, hila na madhila.



.jpg)



.jpg)









.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)



.jpeg)


