Na Munir Shemweta, Dar es Salaam
Serikali imetangaza kuanza kutoa vibali vya ujenzi na kufanya majadiliano na wamiliki wa ardhi na nyumba ambao wapo tayari kushiriki kwenye Mpango wa Uendelezaji Upya eneo la Sinza, huku ikisisitiza kuwa mchakato uliopita umefutwa ili kutoa nafasi ya kuanza upya kwa misingi ya uwazi, ushirikishwaji na kujenga maridhiano.
Kauli hiyo ilitolewa Julai 1, 2026 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo, alipokutana na wamiliki wa ardhi na nyumba wa Sinza kwa lengo la kuwafafanulia hatua za utekelezaji wa mpango huo na kusikiliza maoni yao.
Dkt. Akwilapo alisema Serikali imeamua kufungua ukurasa mpya baada ya kubaini kuwa mchakato uliopita uliacha malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi, hivyo vikao vyote vya awali vimefutwa na sasa mazungumzo yanaanza upya kwa ushirikiano na wananchi.
Alieleza kuwa ukuaji wa miji ni jambo lisiloepukika kutokana na ongezeko la watu na mahitaji ya makazi, hivyo Serikali ina wajibu wa kupanga matumizi ya ardhi kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na ya baadaye.
Waziri huyo alisema Sinza ya sasa imebadilika kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na ilivyokuwa miaka ya nyuma, jambo ambalo linahitaji mpango mpya wa maendeleo utakaoendana na hadhi yake kama eneo muhimu la makazi na biashara ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
"Kama mwananchi anaona mpango huu haufai, hiyo ni haki yake, lakini ipo siku ataona umuhimu wake. Tusiporatibu maendeleo ya miji, tutakuwa na maeneo yasiyo na mpangilio na yenye miundombinu isiyokidhi mahitaji ya wananchi," alisema.
Dkt. Akwilapo alibainisha kuwa uendelezaji upya wa maeneo ya makazi si jambo geni nchini, kwani maeneo kama Posta, Kariakoo, Upanga, Oysterbay na Masaki yamepitia hatua kama hizo na yameendelea kuwa na thamani kubwa zaidi kutokana na upangaji mzuri wa matumizi ya ardhi.
Waziri huyo aliwataka wananchi kuwa makini na watu wasio waaminifu wanaoweza kutumia mchakato huo kuwahadaa au kuwasambazia taarifa zisizo sahihi kwa manufaa binafsi.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, alisema mafanikio ya mpango huo yatategemea kiwango cha ushirikishwaji wa wananchi na kuzingatia maoni yao.
Alipendekeza muda wa ukusanyaji wa maoni uongezwe kwa miezi mitatu ili wananchi wengi zaidi wapate nafasi ya kuelewa mpango huo na kutoa maoni yao kabla ya hatua za utekelezaji kuanza.
"Wananchi wasikilizwe, maoni yao yazingatiwe na rasimu iboreshwe ili iakisi matakwa yao. Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan haiwezi kupora haki za wananchi bali itafuata sheria, kanuni na taratibu zote zinazotambuliwa," alisema Profesa Mkumbo.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga aliwataka wamiliki wa ardhi na nyumba wa Sinza kuwa watulivu na kutochukua maamuzi ya haraka ya kuuza maeneo yao kutokana na taarifa zisizo rasmi.
Alisema thamani ya ardhi katika eneo la Sinza imeongezeka maradufu hivyo wananchi wanapaswa kutambua fursa iliyopo badala ya kufanya maamuzi yatakayowagharimu baadaye.
Akizungumza kwa niaba ya Kamati ya Wamiliki wa Ardhi na Nyumba wa Sinza, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Bw. Asibwene Lumuli, alisema ushirikiano kati ya Serikali na wananchi ndio utakaohakikisha mpango huo unatekelezwa kwa mafanikio na kwa manufaa ya pande zote.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akizungumza na wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza wakati wa Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akizungumza na baadhi ya wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza mara baada ya Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga akizungumza katika kikao kati ya waziri wa Ardhi na wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza wakati wa Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Meya wa Manispaa ya Ubungo Mstahiki Lawrence Mlaki akizungumza wakati wa kikao kati ya waziri wa Ardhi na wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza wakati wa Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Mwenyekiti wa Kamati ya wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza Bw. Asibwene Lumuli akizungumza katika kati ya waziri wa Ardhi na wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza wakati wa Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Ubungo Bw, Albert Msando wakati wa Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akiwa katika picha ya pamoja na kamati ya wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza mara baada ya Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wamiliki wa ardhi na Nyumba Sinza mara baada ya Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo akizungumza wakati wa Kikao kujadili uendelezaji upya eneo la Sinza Dar es Salaam tarehe 1 Julai 2026. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)











.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)










.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)

