Mhe. Wanu ametoa agizo hilo Machi 03, 2026, wilayani Kisarawe wakati wa ziara ya ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi inayotekelezwa na Wizara katika wilaya hiyo.
Amewataka viongozi wa wilaya na wananchi wa eneo hilo kuona umuhimu wa mafunzo ya ujuzi na hivyo kuhamasisha vijana kujiunga na chuo hicho ili kupata ujuzi utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.
Amesema chuo hicho, pamoja na vyuo vingine vya maendeleo ya wananchi, vinapaswa kuzingatia mahitaji halisi ya kiujuzi ili vijana waweze kujiunga kwa wingi.
“Mmesema hapa mnazalisha zao la korosho, ufuta na mihogo; kwa nini sasa msianzishe kozi ya kusindika mazao hayo? Hii itawamasisha vijana kujiunga na chuo kwa kuwa wanasoma kile wanachofanyia kazi,” amesema Mhe. Wanu.
Aidha, ameutaka uongozi wa chuo hicho kusimamia ipasavyo mifumo ya usimamizi wa watumishi ili kuimarisha uwajibikaji.
Akiwa wilayani humo, Mhe. Wanu pia amekagua ujenzi wa VETA Kisarawe na kusema kuwa Serikali inaendelea kujipanga kupata rasilimali fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa chuo hicho ili malengo ya kutoa ujuzi kwa wananchi yafikiwe.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mhe. Petro Magoti, amemuhakikishia Naibu Waziri Wanu ushirikiano katika kusimamia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa, ikiwemo kuhakikisha huduma za umeme na maji zinafika katika eneo la chuo ili kurahisisha hatua inayofuata ya ujenzi.










Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Wanyamapori Duniani, siku maalum inayotambua mchango wa wanyamapori katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kimazingira.
Akizungumzia maadhimisho hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania, Ephraim Mafuru, amesema kuwa, kwa Tanzania wanyamapori si urithi wa asili pekee bali ni sehemu ya utambulisho wa taifa.
“Wanyamapori ni uti wa mgongo wa sekta yetu ya utalii. Ni chanzo cha ajira na kipato kwa maelfu ya wananchi. Ni fahari inayolitangaza taifa letu kimataifa,” amesema Mafuru.
Ameongeza kuwa kupitia rasilimali hizo, Tanzania imeendelea kuwa kivutio kinachoongoza duniani, kikivutia wageni kutoka pande zote za dunia kufurahia vivutio vya asili vilivyopo nchini.
Mafuru amesisitiza kuwa Bodi ya Utalii Tanzania itaendelea kuhamasisha na kukuza utalii endelevu unaolinda mazingira, unaoheshimu bioanuwai, na kuhakikisha wanyamapori wanahifadhiwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Maadhimisho ya mwaka huu yameongozwa na kaulimbiu isemayo, “Medicinal and Aromatic Plants: Conserving Health, Heritage and Livelihoods” (Mimea Tiba na Harufu: Kuhifadhi Afya, Urithi na Maisha), inayotukumbusha kuwa utajiri wa bioanuwai ya Tanzania si uzuri wa asili pekee, bali ni chanzo cha afya, maarifa ya jadi, ajira na ustawi wa jamii.
Kaulimbiu hiyo inaweka msisitizo katika umuhimu wa kulinda mimea tiba na rasilimali nyingine za asili kama sehemu ya mkakati mpana wa uhifadhi unaounganisha mazingira, urithi wa kitamaduni na maendeleo endelevu ya taifa.
Kupitia mazungumzo hayo, wawili hao walijadili kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano kwenye masuala ya olimpiki. Kadhalika, waliangazia namna ya kuimarisha ushirikiano wa michezo kwa ujumla kati ya Tanzania na Algeria kupitia Wizara za Michezo za nchi hizo mbili.
Viongozi hao, walisisitiza kwamba kukamilisha na kusaini Hati ya Makubaliano (MoU) kwenye eneo la michezo, kutaimarisha ushirikiano huo. Mhe. Balozi Njalikai alisisitiza umuhimu wa kutoa kipaumbele kwenye eneo la mafunzo sambamba na kuandaa programu maalumu za mafunzo ya olimpiki kwa ajili ya vijana ili kuwajengea uwezo wa kushiriki na kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Kwa upande wake Bw. Berraf alionesha utayari wa kutoa kipaumbele maalumu kwa Tanzania kwenye eneo la mafunzo na kuahidi pia kuchagiza ukamilishwaji wa MoU kwenye eneo la michezo kati ya Tanzania na Algeria.
Mhe. Balozi Njalikai, alihitimisha mazungumzo yake kwa kumshukuru Bw. Berraf kwa kuonesha nia thabiti ya kuimarisha ushirikiano pamoja na juhudi anazofanya za kukuza vipaji vya vijana wa kitanzania kimichezo.






Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe ameziagiza halmashauri zote kwenye mikoa ya Geita, Tabora na Iringa kuendelea kutenga kiasi cha sh 1,000 kwenye bajeti zao kwa kila mtoto wa chini ya miaka mitano ili kuboresha miradi ya lishe katika halmashauri hizo.
Ametoa maagizo hayo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kuimarisha Huduma za Lishe katika mikoa ya Geita, Iringa na Tabora ili kusaidia kupunguza changamoto za udumavu, ukondefu na utapiamulo wa watoto.
Profesa Shemdoe ameitaka mikoa ya Geita, Iringa na Tabora kuimarisha ufuatiliaji wa mradi jumuishi wa lishe na shughuli zote zinazotekelezwa katika jamii kwa ajili ya kukabiliana na matatizo ya lishe
Mradi wa Kuimarisha Huduma za Lishe unatekelezwa chini ya ufadhili wa taasisi ya BWP ya nchini Uingereza kwa thamani ya dola za kimarekani milioni 2 malengo makuu yakiwa ni kuimarisha lishe na maendeleo ya watoto.
Halmashuri zote zimetakiwa kuhakikisha zinatoa takwimu sahihi na kwa wakati ili kuzingatia utoaji huduma sahihi kwa kuzingatia ushahidi unaotokana na takwimu.
Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Profesa Tumaini Nagu amesema kuwa kupitia mradi huu serikali itaongeza kasi ya ufuatiliaji wa huduma bora za malezi na makuzi ya awali ya mtoto hususani katika vituo ya kulelea watoto mchana,
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Lishe Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Luitfrid Nnally amesema kuwa pamoja na nchi kuwa na kiwango kikubwa cha vyakula lakini bado watoto wanapata utapiamlo katika mikoa hii mitatatu kutokana na kukosa matunzo kutokana na shughuli nyingi za wazazi hususani kilimo
Mwakilishi wa taasisi ya BWP, Dr Taye Balcha alisisitiza kuwa mradi huo umezingatia tathimini ya serikali na hivo na kutambua kuwa wahanga wakubwa wa udumavu ni watoto.
Mkuu wa mkoa wa Geita, Martine Shigella aliahidi kuwa mkoa wa Geita kwa kushirikiana na mikoa inayonufaika na mradi huo watatumia fursa hiyo kupunguza kiwango cha lishe kilichopo.
Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. Subira Mgalu leo Machi 03, 2026 amekabidhi magari mapya kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kuwahudumia Wateja wilayani Bagamoyo.







Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewashauri viongozi kujenga utamaduni wa kuwasaidia wananchi hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuweka uwiano sawa wa mahitaji.
Ametoa wito huo mara baada ya zoezi la kuwagawa Iftar kwa wananchi wa jimbo la kiwani shehia ya kendwa yenye nyumba zaidi ya 1156 hafla iliyofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Mauuwani Jimbo la Kiwani.
Amesema ataendeleza utamaduni wake wa kugawa Iftari kwa wananchi wote hasa wenye mahitaji Maalum ili kupunguza ukali wa maisha na kupata chakula katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Amefahamisha kuwa mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni Maalum kwa waumini wa Dini ya kiislamu kufanya matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu,hivyo ni vyema kwa kila mwenye uwezo kutoa na kuwapa wahitaji ili kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi huu.
Aidha, Mhe. Hemed amesema anatarajia kuzifikia shehia zote saba ( 7 ) zilizomo ndani ya Jimbo hilo na kuzipatia Iftari jambo ambalo litaongezea umoja na mshikamano kwa wannachi wa jimbo hilo.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewaomba wafanya biashara kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu wakiweo Masikini, Wajane, Mayatima na watu wasiojiweza hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani ili kuzidi kuzitakada biashara zao na kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi wa ramadhani.
Kwa upande wake mfanya biashara SAID NASSIR NASOR ( BOBAR ) ameishukuru serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kumpatia ushirikiano ambapo kwa mwezi huu wa ramadhani amepatiwa usafiri wa kusafirisha bidhaa mbali mbali ambazo atawakabidhi wananchi wa kisiwani Pemba wakiwemo waannchi wa jimbo la kiwani.
Amesema kuwa lengo lake ni kuwafikia wananchi mbali mbali wasio na uwezo kwa Unguja na Pemba ili kila mwananchi apate sadaka itakayowasaidia kwa Iftari lakini pia aweze kupata fadhila hapa duniani na kesho akhera.
Nao wananchi waliopatiwa sadaka hizo wamemshukuru mwakilishi wao kwa kuendelea kuwatumikia kwa moyo wa upendo, huruma na usawa kwa wananchi wote jimboni humo jambo ambalo linawapa faraja na imani kubwa juu yake.
Wamesema hawana shaka na utendaji kazi wa Mhe. Hemed na matumaini yao makubwa ni kuzidi kuwaletea maendeleo jimbo humo kama vile alivyoanza kuzitekeleza ahadi mbali mbali alizoziahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwa mwakilishi wa Jimbo la Kiwani.


.jpeg)



.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)




.jpeg)

