Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeibuka mshindi kwenye Tuzo za Kimataifa za Ujenzi Zanzibar (ZICA Awards) baada ya kutunukiwa tuzo ya Benki Bora katika Kuwezesha Miradi ya Ujenzi Zanzibar (Excellence in Financing Construction Projects in Zanzibar), hatua inayothibitisha mchango wake mkubwa katika kukuza sekta ya ujenzi visiwani humo.

Hafla ya utoaji wa tuzo hizo ilifanyika mwishoni mwa wiki visiwani Zanzibar, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chemba ya Taifa ya Biashara Zanzibar (ZNCC), Bw. Ali Suleiman Amour, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya ujenzi kutoka serikalini na sekta binafsi. Benki ya NBC iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa na Uwekezaji, Bw. Elvis Ndunguru, aliyeongoza ujumbe wa maofisa wengine wa benki hiyo katika hafla hiyo.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Ndunguru alisema ushindi huo ni muendelezo wa mafanikio na uthibitisho wa jitihada endelevu za NBC katika kuwezesha miradi ya ujenzi nchini - Tanzania Bara na Zanzibar. Alitaja miongoni mwa miradi mikubwa iliyofanikishwa kwa ushiriki wa benki hiyo visiwani humo kuwa ni ujenzi wa Kituo cha Abiria cha Vivuko cha Maruhubi (Mpiga Duru) kilichozinduliwa hivi karibuni, pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kizimkazi.

“Kwa upande wa Tanzania Bara, NBC imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwezesha miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo miradi ya reli, madaraja na viwanja vya ndege. Tunatambua sekta ya ujenzi ni mhimili muhimu katika kukuza uchumi wa taifa, hivyo tutaendelea kushirikiana na serikali na sekta binafsi kuhakikisha miradi hiyo inafanikiwa, sambamba na kudhamini matukio muhimu ya wadau wa sekta hii,” alisema Bw. Ndunguru.

Benki ya NBC pia ilikuwa miongoni mwa wadhamini wakuu wa tuzo hizo za ZICA, ikionyesha dhamira yake ya dhati katika kuunga mkono maendeleo ya sekta ya ujenzi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa ZNCC, Bw. Ali Suleiman Amour, aliwapongeza waandaaji wa tuzo hizo — CSW Group na Zanzibar Marketing — pamoja na washindi wote, akizitaja tuzo za ZICA kama jukwaa muhimu la kuhamasisha ubora, ushindani wa kitaaluma na uwajibikaji katika sekta ya ujenzi.

Kutokana na mchango mkubwa wa sekta ya ujenzi katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi kupitia ukuaji wa miundombinu, biashara, utalii, makazi bora na uwekezaji, Bw. Amour aliziomba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuimarisha ushirikiano zaidi, hususan katika kuweka sera na mazingira rafiki kwa wawekezaji wa sekta hiyo.

“Serikali pia ihakikishe inawajengea uwezo wazawa kupitia mafunzo, teknolojia na mitaji, sambamba na kusimamia viwango, ubora na ujenzi unaozingatia usalama na utunzaji wa mazingira. Kwa upande wa wadau wa sekta ya ujenzi, ni muhimu kuzingatia maadili, uwazi na sheria ili kujenga imani kwa jamii na serikali ambayo ndiyo mdau wao mkuu,” alisisitiza Bw. Amour.

Awali, akielezea mchakato wa utoaji wa tuzo hizo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa CSW Group, Bi. Annelise Nyangusi, aliwashukuru wadhamini wote wakiwemo Benki ya NBC, akibainisha kuwa vigezo vya kuwapata washindi vilijikita katika ubora wa huduma, ushirikiano wa soko pamoja na mbinu za kipekee za ufanisi wa kampuni.


Mwenyekiti wa Chemba ya Taifa ya Biashara Zanzibar (ZNCC), Bw. Ali Suleiman Amour (kushoto) akikabidhi tuzo ya Benki Bora katika Kuwezesha Miradi ya Ujenzi Zanzibar (Excellence in Financing Construction Projects in Zanzibar) kwa Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa na Uwekezaji wa benki ya NBC Bw. Elvis Ndunguru baada ya benki hiyo kuibuka kinara wa tuzo hiyo kwenye Tuzo za Kimataifa za Ujenzi Zanzibar (ZICA Awards) zilizofanyika mwishoni mwa wiki Zanzibar. Wanaoshuhudia ni maofisa wengine wa benki hiyo.


Mwenyekiti wa Chemba ya Taifa ya Biashara Zanzibar (ZNCC), Bw. Ali Suleiman Amour (kushoto) akijadili jambo na Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa na Uwekezaji wa benki ya NBC Bw. Elvis Ndunguru (kulia) wakati wa hafla ya Tuzo za Kimataifa za Ujenzi Zanzibar (ZICA Awards) zilizofanyika mwishoni mwa wiki Zanzibar. Benki ya NBC iliibuka kinara wa tuzo ya Benki Bora katika Kuwezesha Miradi ya Ujenzi Zanzibar (Excellence in Financing Construction Projects in Zanzibar).


Mwenyekiti wa Chemba ya Taifa ya Biashara Zanzibar (ZNCC), Bw. Ali Suleiman Amour (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi mbalimbali wa tuzo Tuzo za Kimataifa za Ujenzi Zanzibar (ZICA Awards) zilizofanyika mwishoni mwa wiki Zanzibar. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa na Uwekezaji wa benki ya NBC Bw. Elvis Ndunguru ambae benki yake iliibuka kinara wa tuzo ya Benki Bora katika Kuwezesha Miradi ya Ujenzi Zanzibar (Excellence in Financing Construction Projects in Zanzibar).





Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa na Uwekezaji wa benki ya NBC Bw. Elvis Ndunguru (wa tatu kushoto) sambamba na maofisa wengine wa benki hiyo wakifurahia tuzo hiyo.


Jumla ya shilingi milioni 40 hukusanywa Kila mwezi kutoka kwa jumuiya za watoa huduma za maji ngazi ya jamii (CBWSO) katika wilaya ya Geita.

Hayo yamesemwa na meneja wa Wakala wa Maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA wilaya ya Geita  Injinia Sande Batakanwa katika mkutano wa nusu mwaka wa jumuiya za watoa huduma za maji ngazi ya jamii Yani CBWSO katika wilaya hiyo.

Batakanwa alisema kuwa kumekuwa na mafanikio makubwa tangu kuanzishwa kwa jumuiya hizo katika wilaya hiyo ambapo Sasa wananchi wanapata huduma Bora za maji ambazo zimefuikisha asilimia 60 ya upatikanaji wake katika wilaya ya Geita.

Lusekelo Mwaikenda afisa mtendaji kata ya Nyarugusu amekiri uwepo wa manufaa makubwa kupitia CBWSO hizi ambapo Sasa wananchi wanapata huduma za maji kwa wakati. 

Aidha aliongeza kuwa kufuatia kuwepo kwa mradi wa RUWASA katika kata ya Nyarugusu wananchi wameepukana na adha ya maji katika eneo Hilo ambapo hapo awali walitumi maji ya kwenye mabwawa ambayo si safi na salama.

Nae diwani wa kata ya Kaseme Andrew Kalamula alisema kuwa viongozi katika kata ya Kaseme wamekuwa wakihamasisha utunzajibwa mazingira ili kulinda na kuvitunza vyanzo vya maji na katika kata hiyo.








 

  

*Sekta ya mafuta na gesi kama nguzo ya maendeleo ya Taifa*

Na Rashid Mtagaluka.

Tarehe 14 Novemba 2025, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliwasilisha hotuba yake ya kwanza ya muhula mpya mbele ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hotuba iliyobeba maelekezo ya kimkakati kuhusu mwelekeo wa Serikali katika kusimamia uchumi na rasilimali za Taifa.

Katika hotuba hiyo, Rais aliweka bayana dhamira ya Serikali ya kutumia ipasavyo rasilimali zilizopo, hususan mafuta na gesi asilia, kama chachu ya maendeleo ya viwanda, ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi. Alisisitiza kuwa rasilimali hizo ni mhimili muhimu wa safari ya Taifa kuelekea maendeleo endelevu.

Ndani ya siku 100 za mwanzo wa muhula huo, sekta ya mafuta na gesi imeendelea kujitokeza kama moja ya nguzo kuu za utekelezaji wa dira hiyo, chini ya uangalizi wa Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizojaaliwa akiba kubwa ya gesi asilia, rasilimali ambayo ina uwezo mkubwa wa kubadili taswira ya uchumi wa Taifa endapo itasimamiwa kwa weledi, uwazi na uwajibikaji. 

Akihutubia Bunge, Rais Samia alisisitiza kuwa rasilimali hizi ni mali ya wananchi wote, hivyo matumizi yake lazima yaongozwe na maslahi ya Taifa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Katika muktadha huo, TPDC imeendelea kutekeleza majukumu yake ya kisheria na kikatiba kama wakala wa Serikali katika sekta ya mafuta na gesi, kwa kuzingatia kikamilifu maelekezo na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Katika siku 100 za mwanzo wa muhula mpya wa Rais Samia, juhudi zimeelekezwa katika kuimarisha usimamizi wa rasilimali za gesi asilia, kusimamia mikataba ya utafutaji na uzalishaji, kuimarisha ushirikiano na wawekezaji, pamoja na kuhakikisha kuwa rasilimali hii inaleta manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi.

Moja ya maeneo yaliyopata uzito mkubwa katika hotuba ya Rais ni matumizi ya gesi asilia kama nishati safi, nafuu na salama kwa ajili ya viwanda, uzalishaji wa umeme na matumizi ya majumbani. 

Ndani ya kipindi hiki cha siku 100, Serikali kupitia taasisi zake ikiwemo TPDC, imeendelea kusimamia na kuimarisha miradi ya uzalishaji na usambazaji wa gesi asilia katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Hatua hizi zinalenga kupunguza gharama za uzalishaji viwandani, kukuza uchumi wa ndani na kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania, sambamba na kupunguza utegemezi wa nishati zisizo rafiki kwa mazingira.

Aidha, Rais Samia alisisitiza umuhimu wa sekta ya mafuta na gesi kuchangia maendeleo ya jamii zinazozunguka maeneo ya uzalishaji. Katika siku 100 hizi, dhana ya Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR) imeendelea kupewa kipaumbele katika utekelezaji wa majukumu ya TPDC.

Kupitia miradi ya kijamii katika sekta za elimu, afya, maji na miundombinu, juhudi zimeelekezwa katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata manufaa ya moja kwa moja ya uwepo wa rasilimali hizi katika maeneo yao.

Katika hotuba yake, Rais Samia aligusia pia umuhimu wa kujenga uwezo wa Watanzania kushiriki kikamilifu katika sekta ya mafuta na gesi. Ndani ya siku 100, jitihada zimeendelea kuimarisha ushiriki wa wazawa (local content) kwa kutoa fursa kwa wataalamu wa ndani, makampuni ya Kitanzania na vijana wanaosomea masuala ya nishati.

Hatua hii inaakisi dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kuwa sekta ya mafuta na gesi haiwanufaishi wawekezaji pekee, bali inakuwa jukwaa la kukuza ajira, ujuzi na teknolojia kwa Watanzania.

Sambamba na hilo, masuala ya ulinzi wa mazingira na usalama yameendelea kupewa uzito unaostahili. 

Akihutubia Bunge, Rais Samia alisisitiza kuwa maendeleo ya kiuchumi hayawezi kupatikana kwa gharama ya mazingira. Ndani ya siku 100, TPDC imeendelea kusimamia shughuli za utafutaji, uzalishaji na usambazaji wa gesi kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa vya uhifadhi wa mazingira, afya na usalama kazini.

Kwa ujumla, siku 100 za mwanzo wa muhula mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan zimeonesha mwelekeo thabiti wa Serikali katika kusimamia sekta ya mafuta na gesi kwa maslahi mapana ya Taifa. 

Kupitia TPDC, Serikali imeendelea kuimarisha misingi ya usimamizi bora wa rasilimali, kuongeza uwazi na kuimarisha mchango wa sekta hii katika uchumi wa Taifa.

Ingawa safari ya maendeleo ya sekta ya mafuta na gesi bado ni ndefu na yenye changamoto, dalili zilizojitokeza ndani ya siku 100 hizi zinaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha kuwa rasilimali hii inakuwa baraka kwa Watanzania wote.

Katika kutekeleza maono aliyoyatoa bungeni tarehe 14 Novemba 2025, Rais Samia ameendelea kusisitiza mshikamano kati ya Serikali, taasisi zake, sekta binafsi na wananchi. Sekta ya mafuta na gesi, chini ya usimamizi wa TPDC, inaendelea kubaki kuwa moja ya nguzo muhimu katika safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kati wa juu na maendeleo jumuishi. Siku 100 hizi ni mwanzo tu, lakini ni mwanzo unaobeba matumaini makubwa kwa mustakabali wa Taifa.




SERIKALI imezidisha kasi ya kujenga uchumi wa kidijitali kwa kusisitiza matumizi mapana ya mfumo wa anwani za makazi, hatua inayolenga kurahisisha utoaji wa huduma, kuimarisha utambuzi wa wananchi na kuongeza ufanisi wa shughuli za kiuchumi nchini. Wito huo umetolewa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angella Kairuki, akizihimiza wizara na taasisi zote za umma kuutumia kikamilifu mfumo huo kama nyenzo muhimu ya maendeleo ya kisasa.

Akizungumza jijini Dar Es Salaam leo Januari 08, 2026 katika kilele cha Wiki ya Anwani za Makazi na Maonyesho ya Teknolojia ya Posta jijini Dar es Salaam, Kairuki ameeleza kuwa mfumo huo ni mhimili wa kutambua makazi ya wananchi, kurahisisha huduma za kijamii na kiuchumi pamoja na kuboresha ukusanyaji wa mapato ya serikali. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa wakiwemo Hassan Juma, Anne Semamba Makinda na Profesa Joyce Mzalishako.

Waziri Kairuki amebainisha kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya mawasiliano na mifumo ya kidijitali ili kuiwezesha Tanzania kufikia uchumi unaotegemea ubunifu, teknolojia na maarifa. Alisema hadi sasa anwani za makazi takribani milioni 12.9 zimeshasajiliwa, huku mifumo 29 kutoka taasisi 23 za umma na binafsi ikiunganishwa ili kuboresha utoaji wa huduma.

Ameeleza kuwa manufaa ya mfumo huo yameonekana katika sekta za elimu, fedha, usalama, biashara mtandao na huduma za dharura, ambapo taasisi kama Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu na Jeshi la Zimamoto zimeongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu yao. Pia mfumo umeisaidia serikali kufikisha misaada kwa haraka wakati wa majanga kwa kutambua kaya zilizoathirika.

Kwa upande wa ushiriki wa sekta binafsi, Kairuki amezihimiza benki, kampuni za mawasiliano na taasisi za fedha kuutumia mfumo wa anwani za makazi katika utambuzi wa wateja, hatua itakayorahisisha huduma za kifedha na kuongeza ujumuishi wa wananchi katika uchumi rasmi. Sambamba na hilo, wizara ilikabidhi zaidi ya vishikwambi 5,000 kwa watendaji wa mitaa, kata na vijiji ili kuharakisha uingizaji na usasishaji wa taarifa za makazi.

Aidha, ameipongeza TAMISEMI, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar na Wizara ya Ardhi kwa ushirikiano uliofanikisha utekelezaji wa mradi huo kwa muda mfupi. Amesisitiza kuwa Wiki ya Anwani za Makazi itaadhimishwa kila Februari 8 kama jukwaa la tathmini, ubadilishanaji uzoefu na uhamasishaji wa matumizi ya teknolojia katika huduma za posta na mawasiliano.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mohammed Hamisa Abdullah, amesema mfumo wa anwani za makazi ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kuimarisha utambuzi wa makazi na kurahisisha huduma za serikali na sekta binafsi. Aliongeza kuwa mfumo huo uliobuniwa na wataalamu wa ndani unapatikana kupitia tovuti na programu ya simu ya NAPA, huku idadi ya watumiaji ikiongezeka kwa zaidi ya asilimia 70 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hassan Juma, amesisitiza dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendeleza ushirikiano katika utekelezaji wa mfumo huo Unguja na Pemba. Alisema licha ya changamoto za awali za uelewa mdogo, elimu kwa umma na ushiriki wa viongozi wa mitaa umeongeza matumizi ya huduma za kidijitali, zikiwemo mikopo ya elimu, huduma za benki na utambuzi sahihi wa makazi.








Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) imeipongeza Sanlam Allianz kwa kuanzisha Mfuko mpya wa 'USD Fixed Income Fund' utakaowawezesha wawekezaji na wananchi kuweka akiba ya fedha za kigeni (sola ya Marekani).

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa Mfuko huo mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Masoko na Uchunguzi wa CMSA, Exaut Julius, alisema mfuko huo utachochea uchumi wa nchi na kuongeza akiba ya fedha za kigeni kwenye mzunguko.

"Tunawapongeza kwa kuzinduaa Mfuko huu kwa wakati muafaka kwani utachangia maendeleo yamasoko ya mitaji hapa nchini," alisema Julius.

Aidha, alisema Mfuko huo unaonyesha ushirikiano mzuri kati ya CMSA na wadau wake katika kukuza masoko endelevu na mitaji.

"Upatikanaji wa bidhaa bora za uwekezaji zinazoendana na viwango vya kimataifa ni nguzo muhimu katika kupanua ushiriki wa wawekezaji na kuendeleza masoko na mitaji hapa nchini," alisema Julius.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Muu wa kampuni hiyo, Jonathan Stichbury, alisema kuanzishwa mfuko huo ni hatua muhimu katika kuhamasisha utamaduni wa uwekezaji wenye tahadhari na kupanua fursa za uwekezaji zinazotumia dola ya marekani nchini Tanzania.

Alisisitiza pia dhamira yao katika kuzingatia uwazi, kufuata sheria na kanuni, pamoja na kuleta thamani ya muda mrefu kwa wawekezaji wote.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba mara baada ya kufungua Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa mbele ya Soko Kuu jipya la Kariakoo mara baada ya ufunguzi uliofanyika Sokoni hapo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Matukio mbalimbali katika hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya picha mara baada ya kufungua Soko Kuu jipya la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2026.



MERIDIANBET Tanzania inakuletea Super Heli Premium, mchezo unaokusanya msisimko, ujasiri na maamuzi ya haraka kwenye kila raundi. Hapa, bahati pekee haitoshi, kila sekunde ni fursa, kila uamuzi ni hatua kuelekea ushindi. Helikopta inapoanza kupaa, unakuwa katikati ya tukio, ukiamua ni lini kusimama na ni lini kupaa zaidi.

Safari ya Super Heli Premium inakufanya ujisikie kama rubani. Kila sekunde inahesabika, vizidishi vinavyoongezeka vinaongeza presha, na macho yako yako kwenye cash out. Je, utaendelea kushikilia kwa matumaini ya faida kubwa zaidi au utachukua ushindi wako sasa na kuanza raundi mpya? Huu ni mchezo unaokutaka ujipe nafasi ya kushinda kwa akili.

Mbali na mchezo huu, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kinachoifanya Super Heli Premium kuwa ya kipekee ni uhuru wa mchezaji. Unaweza kuweka dau hadi mara tatu kwa raundi moja, kuchagua vizidishi unavyoviamini, na kubadilisha mkakati kadri mchezo unavyobadilika. Hapa, hakuna sheria ngumu za kufuata, Meridianbet inakupa jukwaa, wewe unaamua safari yako ya ushindi.

Zaidi ya hilo, chaguzi za ziada zinakupa ladha ya kipekee. Jaribu Over/Under, tumia 50% Cashout ili kuchukua sehemu ya ushindi huku mchezo ukiendelea, au chagua mandhari tofauti huku helikopta ikiruka juu ya nchi mbalimbali. Kila raundi inakuwa mpya, kila mchezo unachukua sura tofauti, na kila kupaa kuna msisimko wa kipekee.

Na unaposhinda, dunia inajua. Wachezaji wanaocash out kwenye vizidishi vikubwa wanasherehekewa hadharani kwenye chati. Huu si mchezo tu, ni safari ya ushindi unaoonekana, unaoshirikishwa na unaopaswa kuchezwa. Cheza Super Heli Premium leo ndani ya Meridianbet, paa juu na acha kila sekunde iwe hatua yako kuelekea ushindi mkubwa.

Katika kuadhimisha miaka 19 ya kuanzishwa kwa kiwanda cha kuunganisha magari cha GF, uongozi wa kiwanda hicho umesema unajivunia kuwa sehemu ya kuzalisha ajira, huku ukieleza kuwa asilimia 90 ya wafanyakazi wake ni wazawa.

Akizungumza na waandishi wa habari, leo Februari 07, 2026, makao makuu ya kiwanda hicho yaliyopo Kibaha mkoani Pwani, Meneja Mkuu wa kiwanda cha GF, Ezra Mereng, amesema miaka 19 ya dira na matumaini yalianza kama ndoto, lakini hadi sasa kiwanda hicho kinajivunia kuzalisha magari ya aina mbalimbali.

“Leo tunajivunia kusherehekea miaka 19 ya GF, na sisi kama kiwanda tunajivunia kuwa zaidi ya asilimia 90 ya wafanyakazi ni vijana wazawa wa hapa Tanzania waliotoka katika vyuo mbalimbali hapa nchini."

Naye Meneja Chapa na Masoko wa GF Group, Salman Karmal  pamoja na kufurahia mafanikio ya kiwanda hicho, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufungua fursa za uwekezaji zinazowavutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza nchini.

Amesema katika kuadhimisha miaka 19 ya GF, kiwanda hicho kimekuja na mpango wa kurudisha kwa jamii, ambapo wameanza kwa kutembelea watu wenye mahitaji maalumu pamoja na kufadhili timu ya mpira wa miguu ya Nyumbu FC iliyopo jirani na kiwanda hicho, ambayo imekuwa ikifanya vizuri kwenye michezo yake mbalimbali.

“Tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuweza kufungua milango rafiki ya uwekezaji inayotufanya tuwe na uthubutu wa kujiimarisha zaidi katika maeneo mbalimbali ya kibiashara".

Kwa upande wake, Sefroza Mwizarubi, ambae ni mnufaika wa program ya kuchukua wanafunzi vyuoni , amewashukuru viongozi wa GF kwa kutoa nafasi kwa wahitimu wa vyuo mbalimbali kwenda kujifunza namna ya kuunganisha magari, jambo linalowafanya kuwa wabobezi katika nyanja hiyo.

“Mimi ni mnufaika wa mpango wa GF wa kuchukua wanafunzi kutoka vyuoni kwa ajili ya kuja kupata ujuzi wa kuunganisha magari, lakini pia kupata ajira,” amesema Mwizarubi.
Meneja Mkuu wa kiwanda cha GF Vehicle Assemblers,  Ezra Mereng akizuingumza na wafanyakkazi wa kiwanda hicho wakati wa hafla ya madhimisho ya miaka 19 ya kampuni ya GF mkoani Pwani





Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana,akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza,ili  kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara yaliyoandaliwa na Baraza la Ushindani wa Soko (FCT).

Na.Mwandishi Wetu-MWANZA

 BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara.

Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

“Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Baraza la Ushindani na nafasi yake katika kulinda haki za mlaji pamoja na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”Alisema Bw.Elikana

Akizungumza katika mafunzo hayo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Bw. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza lipo kwa ajili ya kulinda masuala yote yanayohusu ushindani wa soko na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini. Alieleza kuwa utekelezaji wa majukumu ya Baraza unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha sheria za ushindani zinatekelezwa kikamilifu, kwa haki na kwa uwazi.

Aidha, aliongeza kuwa Baraza huhakikisha mamlaka za udhibiti zinazingatia taratibu na kanuni za ushindani wakati wa utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kutoa majibu sahihi na ya haraka katika migogoro ya kibiashara. Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kumlinda mlaji dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha ushindani, hivyo kuchangia katika ujenzi wa uchumi shindani, jumuishi na wenye tija kwa Watanzania.

Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa Chemba ya Wafanyabiashara, Bw. Hassan Karambi, alisema kuwa amepata elimu yenye manufaa makubwa kupitia programu ya Baraza ya kuwajengea uwezo wadau.

Alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia wafanyabiashara kufahamu kuwa endapo hawataridhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti kama LATRA, TCRA, TCAA, EWURA, PURA pamoja na Tume ya Ushindani (FCC), wana haki ya kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yao.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa, Bi. Imelda Salumu, alifafanua utaratibu wa Baraza katika kupokea rufaa kutoka kwa wadau.

Alisema kuwa malalamiko huanza kwa mtoa huduma husika, na endapo hayatapatiwa ufumbuzi, hufikishwa katika mamlaka ya udhibiti kama hatua ya kwanza ya rufaa. Aliongeza kuwa iwapo mlalamikaji hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hiyo, utaratibu humruhusu kuwasilisha rufaa katika Baraza la Ushindani kwa hatua zaidi za kisheria.


Top News