.jpg)
.jpg)
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Shigeki Komatsubara akizungumza leo Machi 17, 2026 wakati wa kusaini hati ya Makubaliano (MoU) itakayolenga kuendeleza mifumo bunifu ya ufadhili wa maendeleo, hatua inayotarajiwa kuchochea mageuzi ya kijamii na kiuchumi nchini. Mikataba huo umesainiwa leo Machi 17, 2026 jijini Dar es Salaam.
TTCL YALETA FURAHA KWA WATUMIAJI WA INTANETI, YAJA NA FAIBA ‘SUPERSONIC EXPERIENCE’ YENYE KASI BALAA
SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika hali ya kuendelea kuijenga sekta ya mawasiliano yenye nguvu zaidi na kuboresha huduma za vifurushi kwa wateja wake imekuja na kifurushi kipya kijulikanano kama TTCL Faiba ‘Supersonic Experience’ Kasi Balaa.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Biashara wa TTCL, Bw. Vedastus Mwita alisema kifurushi hicho maalum chenye intaneti vyenye Kasi ya Ajabu kitamuwezesha mteJa kufanya kazi zake bila ya kuwa na wasiwasi (No Stress).
“Kama tunavyofahamu, dunia inaendelea kubadilika kwa kasi kubwa katika enzi ya hizi za kidijitali. Leo hii, huduma za intaneti zenye kasi, ubora na uhakika zimekuwa mhimili muhimu katika kuendesha shughuli za kijamii na kiuchumi – kuanzia biashara, elimu, afya hadi ubunifu wa vijana wetu.”
“Sasa ni mwendo wa Supersonic Experience” – kasi ya ajabu, kasi isiyopimika, kwa wateja wote wa huduma ya “Faiba Mlangoni kwako”. TTCL Faiba Supersonic Experience ni vifurushi vinavyokupa nguvu ya kufanya kila kitu kidijitali bila mipaka.
“..Kuanzia Smart Home, Smart Office, gaming, streaming, biashara mtandaoni hadi mawasiliano ya uhakika, sasa yote yanawezekana kwa kasi ya ajabu kutoka TTCL,” alisema Bw. Mwita akizungumza na wanahabari.
Akifafanua zaidi juu ya vifurushi hivyo vipya, alivitaja ni pamoja na T-Fiber BUSTA chenye kasi ya 60/60 Mbps (Download and upload), Dakika 250 simu ya mezani kinachopatikana kwa Tsh 55,000 kwa mwezi, T-Fiber Triple Hub Plus chenye kasi ya 100/100 Mbps, dakika 300 simu ya mezani na GB 20 za mawasiliano ya simu ya mkononi kinachopatikana kwa Tsh 70,000 kwa mwezi. Huku mteja akipata Simcard moja Buree.
Aliongeza vingine ni T-Fiber Triple Hub Extra – Kasi ya 150/150 Mbps, Dakika 700 simu ya mezani na GB 30 za mawasiliano - kwa Tsh 100,000 kwa mwezi. mteja akipata Simcard ya TTCL mbili, bure, T-Fiber Triple Hub Balaa – Kasi ya 200/200 Mbps, chenye dakika 1200 na GB 40 za mawasiliano - kwa Tsh 150,000 kwa mwezi. Na mteja anapata Simcard tatu buree pamoja na T-Fiber Triple Hub Jumbo – Kasi ya 250/250 Mbps, dakika 2500 na GB 50 za mawasiliano - kwa Tsh 200,000 kwa mwezi. na mteja akipata Simcard tatu za buree
Alibainisha kuwa katika mazingira haya mapya ya kidijitali, upatikanaji wa intaneti yenye kasi, gharama nafuu na uhakika si anasa tena, bali ni hitaji la msingi kwa maendeleo ya taifa; hivyo ndiyo sababu Shirika hilo limeendelea kuweka nguvu kubwa katika kuboresha miundombinu ya mawasiliano na kupanua wigo wa huduma ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
“..Dira yetu ni kuona kila Mtanzania anapata fursa ya kutumia huduma ya Faiba Mlangoni Kwako itakayosaidiai kikamilifu katika ujenzi wa uchumi wa kidijitali – kwa kupata huduma bora, salama na za kuaminika zinazochochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla,”
*Yafikia Asilimia 91, Kukamilika Desemba 2026
Na MWANDISHI WETU,
Dar es Salaam. Serikali imesema mradi wa uwekezaji wa ujenzi wa jengo la kitega uchumi la Mzizima Towers unaotekelezwa jijini Dar es Salaam na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umefikia asilimia 91 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo Desemba 31, 2026.
Taarifa hiyo imetolewa Machi 16, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, alipowasilisha taarifa ya maendeleo ya mradi huo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii.
Kwa mujibu wa Waziri Sangu, mradi huo wa uwekezaji unahusisha ujenzi wa minara miwili, ikiwemo mnara wa biashara wenye ghorofa 35 na mnara wa makazi wenye ghorofa 32, ukiwa na jumla ya eneo la ujenzi la mita za mraba 95,018.15.
Amesema majengo hayo yamebuniwa kwa kuzingatia viwango vya kisasa vya usanifu wa kimataifa ili kukidhi mahitaji ya biashara, makazi na huduma za utalii katika jiji la Dar es Salaam.
Aliongeza kuwa mradi huo utakapokamilika utakuwa na hoteli ya hadhi ya nyota tano itakayoendeshwa na Radisson Hotel Group, yenye jumla ya vyumba 156 vya kulala pamoja na vyumba 132 vya makazi ya muda mfupi (hotel apartments).
Mhe. Sangu alisema mradi huo unatekelezwa kwa asilimia 100 na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kama sehemu ya mkakati wa Mfuko huo kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati yenye tija kwa wanachama na taifa kwa ujumla.
Alibainisha kuwa uwekezaji huo unalenga kuongeza thamani ya mali za Mfuko pamoja na kuimarisha uwezo wake wa kulipa mafao kwa wanachama.
Akizungumza baada ya ziara ya kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Mchafu Chakoma, alisema wajumbe wa kamati wanamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua mradi huo uendelee kutekelezwa ili uweze kuleta tija kwa Mfuko na Taifa kwa ujumla.
“Sisi kamati tumefika hapa na kujionea kazi inayofanyika katika mradi huu. Kazi ni nzuri sana na inaonesha kuwa uongozi wa NSSF chini ya Mkurugenzi Mkuu, Bw. Masha Mshomba, umekuwa mfano wa kuigwa katika usimamizi wa miradi,” alisema Mhe. Hawa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, aliwashukuru wajumbe wa kamati hiyo kwa kufanya ziara ya kikazi na kujionea maendeleo yaliyofikiwa katika mradi huo.
Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo akiwemo Mhe. Kafiti Kafiti waliipongeza NSSF kwa uwekezaji wa mradi huo mkubwa unaotarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa taifa na jamii kwa ujumla.
Naye Mhe. Kangi Lugola alisema mradi wa Mzizima Towers ni uwekezaji muhimu wenye tija kubwa kwa Mfuko na Taifa kwa ujumla, akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa NSSF kwa usimamizi mzuri wa Mfuko na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Mradi wa Mzizima Towers unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kiuchumi ikiwemo kuongeza mapato ya Mfuko na Serikali, kuimarisha sekta ya biashara na utalii jijini Dar es Salaam pamoja na kuongeza ajira, ambapo zaidi ya wafanyakazi 300 wameajiriwa wakati wa ujenzi wa mradi huo, huku ajira zaidi ya 250 zikitarajiwa kupatikana mara baada ya kuanza kwa shughuli za hoteli na biashara ndani ya jengo hilo.

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
Na Seif Mangwangi, Michuzi TV, Arusha
SERIKALI imesema vikundi vya Malezi na Makuzi vinavyoendelea kuanzishwa nchini vimekuwa chachu ya kupunguza tatizo la ukatili wa watoto kwa kuongeza ulinzi na usalama dhidi yao.
Aidha jamii imetakiwa kuungana kwenye suala zima la malezi na makuzi ya mtoto na kwamba Baba anapaswa kuungana na mke wake kuhakikisha mtoto anapata malezi bora, salama na yenye upendo tangu mimba inapotungwa.
Akizungumza kwenye kongamano lililokutanisha makundi ya malezi na makuzi yaliyoko chini ya taasisi ya malezi ya SOS Children's Village kutoka katika Halmashauri nne za Mkoa wa Arusha za Meru, Arusha DC, Karatu na Jiji, Machi 16 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Seleman Msumi, amesema kuwa malezi bora kwa watoto ni nguzo muhimu katika kuhakikisha jamii inapata maendeleo endelevu na yenye ustawi.
Amesema kuwa serikali inaendelea kushirikiana na taasisi zisizo za kiserikali ili kuhakikisha mwongozo wa malezi bora unatekelezwa kwa ufanisi katika jamii.
Msumi amesema ushirikiano wa familia na jamii kwenye makuzi ya mtoto utasaidia kupunguza vitendo vya ukatili vinavyotokea katika jamii, hasa kwa watoto, kwa kuwa jamii itakuwa na uelewa mpana kuhusu wajibu wa malezi na ulinzi wa mtoto.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee, wanawake na Makundi Maalum, Victor Rugarabamu, amesema uwepo wa makundi ya malezi ni mkakati wa Serikali wa kuwa na vikundi aki2 kote nchini ifikapo mwakani.
Amesema pamoja na mafanikio ya uanzishwaij wa makundi hayo, bado takwimu za uanzishwaji wake ni ndogo ambapo Hadi kufikia mwaka huu ni makundi 4060 pekee ambayo yameshaanzishwa nchini.
“ Mpaka Sasa takwimu zinaonyesha tuna vikundi vya Malezi na Makuzi 4060 pekee kote nchini wakati matarajio ni kuwa na vikundi laki2, kasi bado ni ndogo sana inapaswa kuongeza kasi zaidi Ili kufikia malengo,” amesema.
Aidha amelipongeza shirika la SOS Children’s Village kwa juhudi zake za kuanzisha vikundi vya malezi na Makuzi katika mkoa wa Arusha na kutoa wito kwa taasisi na mashirika mengine kuungana na Serikali kuanzisha vikundi hivyo.
Amesema vikundi hivyo vina mchango mkubwa katika kuhamasisha na kuimarisha malezi bora, pamoja na kuongeza uelewa kwa jamii juu ya haki na ustawi wa mtoto.
Awali Meneja Programu wa taasisi ya SOS Children’s Village mkoa wa Arusha, Mpely Ally Kalonge, amesema kuwa lengo la shirika hilo ni kutoa malezi mbadala kwa watoto wanaohitaji msaada, pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto na kupinga vitendo vya ukatili katika jamii.
Amesema taasisi ya SOS Children village imekuwa kiunganishi Kikubwa kati yake na jamii kwa kusaidia kuanzisha makundi ya malezi katika Halmashauri nne ndani ya Mkoa wa Arusha sanjari na kuyapatia elimu ya malezi na makuzi makundi hayo.
Kalonge amesema mpango wa taasisi ni kuendelea kuongeza makundi hayo Ili kuongeza ustawi na ulinzi wa watoto na kujenga jamii yenye upendo na isiyo na matendo ya kikatili.
UZOEFU wa Tanzania katika kuunganisha uhifadhi wa maliasili na maendeleo ya sekta ya utalii umevutia wataalamu kutoka nchini Zambia, waliowasili nchini kwa ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu.
Ujumbe huo umetembelea Tanzania Machi 16,2026 kwa lengo la kujifunza namna nchi inavyotekeleza mikakati ya uhifadhi wa rasilimali za asili sambamba na kutangaza vivutio vyake vya utalii katika masoko ya kimataifa.
Akizungumza wakati wa mapokezi ya ujumbe huo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii (TTB), Ephraim Mafuru amesema nchi imeendelea kuwa ya mfano barani Afrika kuunganisha juhudi za uhifadhi na maendeleo ya utalii, hatua inayochangia kukuza uchumi wa taifa.
Amesema mfumo wa usimamizi wa hifadhi, uendelezaji wa vivutio vya utalii pamoja na mikakati ya masoko ya kimataifa umeifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zinazoongoza kwa kuvutia watalii duniani.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Baraza la Mawaziri ( FED) kutoka nchini Zambia Siazongo Siakalenge, pamoja na wataalam kutoka sekta ya utalii, uhifadhi wa wanyamapori wameongoza ujumbe huo.
Wajumbe wa Zambia wameeleza kuvutiwa na juhudi zinazofanywa na Tanzania katika kulinda rasilimali za asili huku ikiendeleza utalii kama kichocheo muhimu cha maendeleo ya uchumi na ustawi wa jamii.
“Kama sehemu ya ziara yao ya mafunzo, ujumbe huo pia umetembelea Hifadhi ya Serengeti, kushuhudia uhamaji mkubwa wa nyumbu tukio la kipekee duniani linalovutia maelfu ya watalii kutoka mataifa mbalimbali kila mwaka,” amesema Siakalenge.



.jpg)




.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)