Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) Julai 10, 2026, Tutuba amesema kiwango cha riba ya Benki Kuu cha asilimia 6.25 kinalenga kuhakikisha kunakuwa na utulivu wa bei na mfumuko wa bei unaendelea kubaki kati ya asilimia 3 hadi 5.
Amesema kiwango hicho pia kitawezesha Mabenki kuwa na ukwasi wa kutosha kwa ajili ya utoaji wa mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara, hivyo kusaidia shughuli mbalimbali za uzalishaji na biashara nchini.
Tutuba amesema wakulima wanapoanza kuvuna mazao yao, thamani imara ya fedha itasaidia kuhakikisha wanapata malipo yanayolingana na thamani halisi ya mazao yao sokoni.
Ameongeza kuwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa nje ya nchi pia watanufaika kwa kupata fedha za kigeni kulingana na thamani ya fedha walizotumia katika uzalishaji, huku tathmini ikionyesha kiwango cha riba cha asilimia 6.25 kinatosha kuendelea kuimarisha shughuli za kiuchumi.
Aidha, amesema BoT hutumia Maonesho ya Sabasaba kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kiwango cha riba ya Benki Kuu katika kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza ukwasi katika mzunguko wa uchumi na kuwezesha upatikanaji wa fedha kwenye mabenki ya biashara.
Tutuba amesema maonesho hayo pia ni fursa kwa Watanzania kujifunza, kupata bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na mbinu mpya za kufanya shughuli za kiuchumi zinazochangia ukuaji wa uchumi wa nchi.


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)











