Wanajumuiya wa Shirika la INADES Formation Tanzania wamelitaka shirika hilo kubuni miradi ya kilimo itakayosaidia kuwavutia vijana kuingia katika sekta hiyo, wakiamini inaweza kuwa njia ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

Wito huo umetolewa jijini Dodoma na Patrick Lameck wakati wa Washa iliyofanyika kuelekea mkutano mkuu wa mwaka wa wanajumuiya na wadau wa shirika hilo, unaoenda sambamba na uchaguzi wa viongozi.

Lameck amesema ili kupanua wigo wa utendaji wa shirika hilo, ni muhimu kuanzishwa kwa miradi ya kilimo itakayowapa vijana fursa ya kushiriki shughuli za uzalishaji na kujiongezea kipato.

Amesema bado vijana wengi wanaogopa kujihusisha na kilimo kutokana na dhana iliyozoeleka kuwa sekta hiyo haina faida, hali inayochangia kupungua kwa ushiriki wao.

“Tunaomba viongozi wetu wabuni miradi ya kilimo, kwa sababu itasaidia kushawishi vijana kujiunga na shughuli hizo na kuboresha maisha yao.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa INADES Formation Tanzania, Jacqueline Nicodemus, amesema wanajumuiya wanapaswa kuwa na mshikamano na ushirikiano ili kuwezesha shirika hilo kufikia malengo na mikakati iliyojiwekea.

Amesema mafanikio ya shirika yatategemea ushiriki wa pamoja wa wanachama katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazopangwa.

“Tunapaswa kuwa kitu kimoja na kushirikiana katika utekelezaji wa mipango yetu ili kuhakikisha shirika linaendelea kupiga hatua.”







 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri (kulia), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
▪️︎ Dkt. Mwigulu asema maghala yawafuate wakulima badala ya wakulima kufuata maghala

▪️︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inapanga kufanya maboresho katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima hususan gharama na usumbufu wa kufuata huduma za maghala yaliyo mbali na maeneo yao ya uzalishaji.

Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.

Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mfumo huo na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha mfumo huo unawanufaisha wakulima kama ilivyokusudiwa.

“Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ni wananchi wasiyafuate maghala, maghala yawafuate wananchi pale walipo,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema ataitisha kikao maalumu kitakachowahusisha wakuu wa mikoa pamoja na sekta zinazohusika kutoka maeneo yanayozalisha mazao yanayotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kufanya tathmini ya changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua.

“Nitaitisha kikao cha wakuu wa mikoa ya maeneo haya yanayozalisha mazao ambayo wananchi wake wamekuwa wakipata changamoto ili tupate mpango kazi wa namna ya kumaliza tatizo hili,” amesema.

Ametaja baadhi ya mikoa inayohusika kuwa ni Dodoma, Singida, Simiyu, Tabora pamoja na baadhi ya mikoa ya Kusini inayozalisha mazao ya biashara ikiwemo ufuta na dengu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza wanunuzi wa mazao kutumia taasisi za kifedha kupata mikopo badala ya kuwakopesha wakulima kabla ya mauzo ya mazao yao.

“Wenzetu wanaokwenda kununua haya mazao wasiwakope wakulima, wao wakakope benki. Benki ndiyo taasisi zinazotoa mikopo,” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mfumo huo ili kuhakikisha wakulima wanapata huduma kwa urahisi na kunufaika ipasavyo na mazao yao.












︎ Dkt. Mwigulu asema maghala yawafuate wakulima badala ya wakulima kufuata maghala
︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inapanga kufanya maboresho katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima hususan gharama na usumbufu wa kufuata huduma za maghala yaliyo mbali na maeneo yao ya uzalishaji.

Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.

Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mfumo huo na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha mfumo huo unawanufaisha wakulima kama ilivyokusudiwa.

“Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ni wananchi wasiyafuate maghala, maghala yawafuate wananchi pale walipo,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema ataitisha kikao maalumu kitakachowahusisha wakuu wa mikoa pamoja na sekta zinazohusika kutoka maeneo yanayozalisha mazao yanayotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kufanya tathmini ya changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua.

“Nitaitisha kikao cha wakuu wa mikoa ya maeneo haya yanayozalisha mazao ambayo wananchi wake wamekuwa wakipata changamoto ili tupate mpango kazi wa namna ya kumaliza tatizo hili,” amesema.

Ametaja baadhi ya mikoa inayohusika kuwa ni Dodoma, Singida, Simiyu, Tabora pamoja na baadhi ya mikoa ya Kusini inayozalisha mazao ya biashara ikiwemo ufuta na dengu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza wanunuzi wa mazao kutumia taasisi za kifedha kupata mikopo badala ya kuwakopesha wakulima kabla ya mauzo ya mazao yao.

“Wenzetu wanaokwenda kununua haya mazao wasiwakope wakulima, wao wakakope benki. Benki ndiyo taasisi zinazotoa mikopo,” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mfumo huo ili kuhakikisha wakulima wanapata huduma kwa urahisi na kunufaika ipasavyo na mazao yao.
Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Kongamano la 13 la Jukwaa la Miji Duniani (13th World Urban Forum) litakalofanyika Baku, Azerbaijan kuanzia tarehe 17-22 Mei 2026.

Kongamano hilo litakalofanyika katika Uwanja wa Olimpiki wa Baku kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Makazi Duniani (UN-Habitat), linabeba kaulimbiu isemayo: “Makazi kwa Dunia: Miji na Jamii Salama na Imara.”

Jukwaa hilo la Miji Duniani litazikutanisha nchi mbalimbali zikijadili na kuweka mikakati ya pamoja ya namna miji inavyoweza kuwa chachu ya kuchochea maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, Kongamano hilo la siku sita litahusisha ushiriki wa viongozi katika ngazi ya Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wataalamu mbalimbali watakaojadili changamoto za kimataifa za makazi pamoja na kukuza maendeleo endelevu ya miji.

Kupitia kongamano hilo la Miji Duniani kutakuwa na mawasilisho na mijadala kutoka kwa Mawaziri ambapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatarajia kutoa tamko litakalotolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo.

Mawasilisho na mijada ya mawaziri katika kongamano hilo la Miji Duniani yatatoa fursa kwa Tanzania kujifunza kutoka nchi nyingine mbinu bora zinazoweza kuboresha utekelezaji wa sera mbalimbali za maendeleo pamoja na kutoa uzoefu wake.

Ujumbe wa Tanzania katika Kongamano hilo la Jukwaa la miji Duniani unahusisha pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Profesa Riziki Shemdoe, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemera pamoja na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila.


GABORONE, BOTSWANA
RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amewasili nchini Botswana leo tarehe 15 Mei 2026 kumwakilisha Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika shughuli za Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Botswana, Hayati Festus Gontebanye Mogae.

Hayati Mogae alifariki dunia tarehe 08 Mei 2026 akiwa na umri wa miaka 86. Mazishi hayo yanatarajiwa kufanyika kesho, tarehe 16 Mei 2026, jijini Gaborone.

Mara baada ya kuwasili nchini humo, Mheshimiwa Dkt. Kikwete alifika katika Ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Botswana ambako alisaini katika Kitabu cha Rambirambi kuenzi mchango mkubwa wa Hayati Mogae kwa taifa la Botswana na bara la Afrika kwa ujumla.

Pichani Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Kikwete anaonekana akisaini kitabu cha rambirambi huku nyuma yake akiwa amesimama Mheshimiwa James Bwana, Balozi wa Tanzania nchini Botswana.

Katika picha ya pili, Mheshimiwa Dkt. Kikwete anaonekana akiwa pamoja na Mheshimiwa Dithapelo Keorapetse, Spika wa Bunge la Botswana, pamoja na Dkt. Gabriel Goitsemodimo Gosiame Malebang, Katibu wa Bunge la Botswana.

Wengine ni Mheshimiwa Balozi James Bwana pamoja na Balozi Mstaafu Dkt. Athalia Molokomme ambaye alimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Botswana wakati wa mapokezi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu.
Mkurugenzi Mkuu wa ESRF Profesa Fortunata Makene akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Makutano wa kufungua fursa za uwekezaji utaofanyika mwezi ujao Mjini Arusha.
Mwakilishi Mkazi wa UNDP Shogeki Komatsubara akizungumza kuhusiana nafasi ya UNDP katika ushiriki wa mkutano wa kufungua fursa za uwekezaji katika mkutano utaofanyika Mjini Arusha Juni Mwaka huu.
Baadhi washiriki katika mkutano huo

*Miradi 60 ya Kimkakati Kuwasilishwa Kongamano la Uwekezaji Tanzania

Na Mwandishi Wetu
TANZANIA inatarajia kuwa mwenyeji wa Makutano wa Uwekezaji unaolenga kuvutia uwekezaji wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 2.85 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi ESRF Profesa Fortunata Makene alisema kongamano hilo litafanyika Juni 1 hadi 2, 2026 katika Gran Meliá Arusha mkoani Arusha na Mgeni rasmi Waziri wa Mpingo na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo

Profesa Makene alisema mkutano huo utaunganisha wawekezaji wa kimataifa, taasisi za fedha, wadau wa maendeleo pamoja na waendelezaji wa miradi ya uwekezaji ya serikali iliyokamilisha maandalizi kwa ajili ya kupata mitaji.

Mkutano huo umeratibiwa Kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) ,Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) Tanzania, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji Tanzania (TISEZA) pamoja na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar I(ZIPA).

Aidha, usajili kwa washiriki wa mkutano huo umefunguliwa rasmi ambapo wamiliki wa miradi ya umma, wawekezaji, waendelezaji wa miradi pamoja na taasisi za fedha za maendeleo wametakiwa kujisajili kupitia mfumo rasmi wa TIGF.

Profesa Makene alisema kongamano hilo litawakutanisha viongozi wa serikali, taasisi za fedha, mifuko ya hifadhi ya jamii, wawekezaji binafsi pamoja na taasisi za kifedha kutoka ndani na nje ya nchi.

Alisema lengo kuu ni kuhakikisha mazungumzo ya uwekezaji yanazaa matokeo halisi kupitia miradi 60 iliyopitiwa na kuthibitishwa yenye thamani ya takribani dola bilioni 2.85 za Marekani.

Miradi hiyo inahusisha sekta mbalimbali za kipaumbele ikiwemo utalii na miundombinu ya asili, nishati jadidifu, usafirishaji, uchumi wa buluu Zanzibar, usindikaji wa mazao, miundombinu ya maji pamoja na miradi ya maendeleo ya ngazi za chini.

Waandaji wa kongamano hilo pia wametangaza kuwepo kwa miradi kati ya nane hadi 10 yenye kipaumbele kikubwa inayotarajiwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola milioni 100 za Marekani kila mmoja.

Profesa Makene alisema Tanzania ipo tayari kubadilisha fursa zilizopo kuwa miradi yenye tija ya kibiashara kwa manufaa ya taifa.

“TIGF 2026 ndiyo jukwaa ambalo jumuiya ya wawekezaji wa kimataifa itaweza kupata fursa hizi na kufuatilia kila hatua ya uwekezaji hadi pale makubaliano yatakapokamilika,” alisema Profesa Makene.

Amesema Tanzania inatarajia kunufaika zaidi na uwekezaji endelevu kupitia mkutano huo unaolenga kuharakisha mtiririko wa uwekezaji nchini na kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha uwekezaji barani Afrika.

Aidha, alisema kongamano hilo litakuwa daraja muhimu kati ya vipaumbele vya maendeleo ya taifa na mtaji wa kimataifa unaohitajika katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Mataifa Nchini Tanzania (UNDP) Shigeki Komatsubara alisema taasisi hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania katika kukuza maendeleo yanayoendeshwa na uwekezaji.

“UNDP Tanzania ipo tayari kusaidia Tanzania kuwezesha jukwaa linalokidhi viwango vya wawekezaji wa kimataifa,” alisema Komatsubara.
Na Said Mwishehe,Michuzi TV

OFISA Maendeleo ya Jamii ambaye ni Mratibu wa Programu ya Kizazi chenye usawa, John Mapunda ameeleza kwamba Tanzania imechagua eneo la haki na usawa wa kiuchumi katika Programu ya Kizazi Chenye Usawa.

Amesema eneo hilo lina mchango mkubwa katika kutatua changamoto mbalimbali za kijinsia nchini huku akifafanua kinara wa utekelezaji ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mapunda ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi cha kujadili namna kusuma ajenda ya Kizazi chenye Usawa ,kilichoandaliwa na Shirika la UN Women na kuwashirikisha Wahariri wa vyombo vya habari, waandishi na vijana Generation.

“Katika lengo hilo Tanzania imejiwekea maeneo manne makubwa ya utekelezaji ambayo ni kuongeza huduma za jamii zinazolenga kumpunguzia mwanamke mzigo wa kazi zisizo na malipo, kukuza ajira na kazi zenye staha hususan kwa wanawake, kuongeza uwezo wa wanawake kumiliki rasilimali za uzalishaji ikiwemo ardhi na biashara pamoja na kuandaa bajeti zenye mrengo wa kijinsia.

“Programu ya Kizazi Chenye Usawa ilianza mwaka 2021 na inatarajiwa kukamilika mwaka 2026 .Programu hiyo inatekelezwa Tanzania Bara na Zanzibar chini ya uratibu wa wizara zenye dhamana ya jinsia kwa kushirikiana na UN Women.”

Kwa upande wake Mchambuzi wa Programu za Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kutoka UN Women, Jackline Chami amesema kwa mwaka huu programu hiyo itajikita katika maeneo saba muhimu.

Ameyataja maeneo hayo ni ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi, uchumi wa malezi, ujuzi, ujumuishaji wa kidijitali, bajeti na ufadhili wenye mrengo wa kijinsia, kizazi chenye usawa katika taasisi na uendelevu pamoja na ujumuishaji wa watu wenye ulemavu na mabadiliko ya kijinsia.

“Maeneo hayo yanalenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika uchumi, teknolojia, maamuzi na kuhakikisha makundi yote yanapata fursa sawa katika maendeleo ya taifa,”amesema alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu programu hiyo.

Awali Mtaalamu wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kutoka UN Women, Lillian Mwamdanga amesema jukwaa hilo limewakutanisha serikali, mashirika ya kiraia, vijana, sekta binafsi, vyombo vya habari pamoja na washirika wa maendeleo kwa lengo la kugeuza ahadi za usawa wa kijinsia kuwa matokeo halisi kwa wanawake na wasichana.

“Kupitia Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa linaloongozwa kwa pamoja na UN Women na wadau mbalimbali duniani, nchi zimekuwa zikitoa ahadi za kifedha na utekelezaji wa programu zinazolenga kuimarisha haki na uwezeshaji wa wanawake na wasichana.

“Tanzania imeonesha uongozi mkubwa kwa kuwekeza katika haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake ambapo tangu mwaka 2021 serikali imekuwa ikitekeleza programu ya kitaifa chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum,”amesema.

Akizumgumzia baadhi ya mafanikio yaliyofikiwa kuwa ni pamoja na kuanzishwa kwa NMB Gender Bond, uwekezaji katika huduma za malezi ya watoto na matumizi ya nishati safi ya kupikia ambayo imesaidia kupunguza mzigo wa kazi kwa wanawake na kuwapa muda zaidi kushiriki shughuli za uzalishaji mali.

Pia amesema ahadi zaidi ya 200 zimepatikana kutoka serikalini, asasi za kiraia, sekta binafsi na taasisi za elimu huku majukwaa 10,000 ya uwezeshaji wanawake yakianzishwa nchini ili kuongeza upatikanaji wa taarifa, fursa za uongozi na mitandao ya kijamii kwa wanawake.








Na. Jawadu Kinyobwa
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka Wahitimu wa Taasisi ya Uongozi kuwa waadilifu, wenye nidhamu na uthubutu ili kuleta maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla.
Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo Mei 15, 2026 katika Sherehe ya Tisa ya Mahafali ya Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika Mlimani City, Jijini Dar es salaam.



Aidha, amesema katika ulimwengu wa sasa uadilifu ndio sifa kuu ya kiongozi bora na mwenye kuaminika, hivyo watumie maarifa na ujuzi walioupata chuoni kuwa viongozi wanaozingatia haki, uwajibikaji na weledi katika kila jambo.



“Nawakumbusha umuhimu wa kuwa Viongozi Wenye Uzalendo. Tukumbuke msemo wa wahenga: Adhabu ya msaliti ni malipo ya usaliti wake. Usaliti mkubwa katika uongozi wa umma ni sawa na ubadhirifu wa mali za Umma” amesema.



Akizungumza kuhusu umuhimu wa uadilifu katika uongozi, amewasihi wahitimu hao kuwa viongozi wenye maadili mema, wanaolinda mali za umma na kuweka mbele maslahi ya wananchi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.



Amesema Taifa linahitaji viongozi waaminifu, wenye uwajibikaji na wanaotumia nafasi zao kusukuma mbele maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa manufaa ya Watanzania wote.


Sambamba na hayo, Mhe. Ridhiwani amesisitiza kuwa, uongozi bora na wa kuzingatia misingi ya haki na uwazi utasaidia kuendelea kuitangaza vyema Tanzania pamoja na Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya nchi.

Awali akizungumza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Bw. Kadari Singo, amesema Taasisi hiyo imetimiza miaka kumi na tano tangu ilipoanzishwa rasmi Julai 2010 kwa Hati ya Rais kama Kituo cha Utaalamu wa Hali ya Juu (Centre of Excellence) cha kujenga na kuimarisha viongozi barani Afrika ili kuleta maendeleo endelevu.



Amebainisha kuwa, Taasisi hiyo imeendelea kufanya kazi kubwa na nzuri katika utoaji wa programu za mafunzo ya uongozi, uandaaji wa mijadala ya kisera, upanuzi wa dimbwi la maarifa kupitia tafiti na machapisho mbalimbali.



Akizungumza kwa niaba ya wahitimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Juma Burhan Mohamed amesema mafunzo hayo yamekuwa chachu ya mabadiliko makubwa katika fikra, uwezo wa uongozi na namna ya kufanya maamuzi yenye tija kwa taasisi na jamii.



Amesema mahafali hayo hayakuwa tu sherehe ya kukamilisha mafunzo, bali yalikuwa ishara ya mabadiliko na ukuaji wa kiuongozi walioupata washiriki ndani ya kipindi cha miezi sita ya programu hiyo.










Top News