TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imeendelea na vikao vyake leo Februari 14, 2026 kwa kukutana na Balozi wa Kudumu wa Tanzania Ofisi rasmi za Umoja wa Mataifa huko Geneva, Uswiswi, Dkt Abdallah Possi na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Ufalme wa Ubelgiji na Mkuu wa Ubalozi wa Tanzania kwa Umoja wa Ulaya (EU), Jestas Nyamanga.
Mkutano huo wa Tume na Mabalozi hao umefanyika katika ukumbi wa Tanganyika uliopo jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Tume kukusanya taarifa, maoni na ushauri kutoka kwa viongozi mbalimbali.
Kwa Pamoja Balozi Possi na Balozi Nyamanga walijadili namna matukio ya uvunjifu wa amani yalivyoanza, athari zake kwa wananchi, mali zao na miundombinu, pamoja na mapendekezo ya namna ya kudhibiti na kuzuia matukio kama hayo yasijirudie siku zijazo.
Vilevile, katika mkutano huo hoja zilizojadiliwa zilihusu maeneo ya tathmini ya athari za matukio hayo na ushauri wa hatua za kijamii na kisheria zinazoweza kuchukuliwa ili kuimarisha amani na mshikamano wa kitaifa.
Tume inaendelea kukutana na makundi mbalimbali ikiwemo waathirika wa matukio ya uvunjifu wa amani katika mikoa tofauti nchini, kwa lengo la kukusanya ushahidi na taarifa zitakazoiwezesha kuandaa ripoti ya kina.
Na Mwandishi wetu, Ngorongoro.
Kama wewe unahisi Penzi lako linalegalega na kuishiwa Pawa hujachelewa, mshawishi mpenzi, mume au mke wako mje Bustani ya Edeni katika hifadhi ya Ngorongoro. Shuhuda za wanyama wakubwa watano, mandhari ya kuvutia yaliyopambwa na sauti za ndege porini pamoja na harufu nzuri ya maua ya bustani ya Edeni yatalipa Nguvu Penzi lako kwa kulinogesha na kuligongelea Msumari.
Mamia wamejitokeza leo tarehe 14/02/2026, kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao (Valentine’s Day), wakichagua hifadhi hiyo kama sehemu maalum ya kuonesha mapenzi na kufurahia vivutio vya utalii kwenye kivutio cha utalii namba moja Afrika.
Watalii waliotembelea Ngorongoro wameshiriki matembezi ya utalii, upigaji picha za kumbukumbu na shughuli mbalimbali zilizowawezesha kufurahia mazingira ya hifadhi kwa namna tofauti na sherehe za mijini.
Mmoja wa watembezi hao Juma Shemoka na Mpenzi wake Radhia El-had wanaelezaa uzoefu huo umeongeza thamani ya sikukuu hiyo kwa kuunganisha burudani, mapumziko na kujifunza kuhusu uhifadhi wa mazingira na jinsi Wanyamapori wanavyoishi na kuthihirisha thamani ya upendo.
Hivi karibuni mamlaka hiyo ilizindua huduma mpya ya Wedding Tourism, inayowezesha wanandoa na wachumba kufanya harusi, kuvishana pete pamoja na sherehe nyingine za kimahaba ndani ya maeneo ya hifadhi ambapo huduma hiyo inalenga kupanua bidhaa za utalii na kuvutia makundi mapya ya wageni wa ndani na nje ya nchi kufurahia mapenzi ndani ya maeneo tulivu ya hufadhi.
Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Afisa Masoko Mkuu Ngorongoro, Michael Makombe, alisema mwitikio mkubwa wa wananchi unaonesha kuwa juhudi za kukuza utalii wa ndani zinaendelea kuleta matokeo chanya.
Karibu Ngorongoro ambapo maajabu saba yanayojumuisha asili ya binadamu, mazalia ya nyumbu, Kasoko ya Ngorongoro, maisha ya watu, wanyamapori, malikale, Jiolojia na vingine vingi vinakutana katika eneo moja.
-Ataka uchunguzi wa matumizi ya fedha na ununuzi wa vifaa hospitalini hapo.
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 14, 2026 ameweka jiwe la msingi la Hospitali ya Wilaya Kilindi iliyojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 2.64 ambapo kati ya fedha hizo shilingi 2.51 ni kutoka Serikali Kuu, Shilingi milioni 50 ni za mapato ya ndani ya Halmashauri na shilingi milioni 89.9 ni kutoka Benki ya Dunia
Ujenzi wa Hospitali hiyo umesaidia kuwapunguzia wananchi adha na gharama kubwa za matibabu ambazo walilazimika kuzifuata katika Wilaya za jirani.
Pamoja na kuridhishwa na ubora wa majengo katika hospitali hiyo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu amemtaka Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga kufuatilia na kujua ni kwanini idadi ya majengo yaliyopo ni machache kuliko yaliyokusudiwa ikiwa fedha yote ya utekelezaji wa mradi ilitoka.
“Majengo yapo kwenye viwango vizuri, ila fedha iliyokuja ilikuwa ijenge majengo mengi zaidi lakini mmejenga pungufu, fedha nyingine ipo wapi?, michezo ya upotevu wa fedha za Serikali hatuwezi ivumilia”
Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Mkoa wa Kagera kanali Yahaya Ramadhani Kido amesema suala la ulinzi na usalama litakuwa kipaumbele chake cha kwanza kutokana na mkoa huo una mipaka yenye uingiliano mkubwa na nchi jirani.
Katika hafla fupi ya hati ya makabidhiano kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Fatma Mwassa ,Kanali Kido amesema suala la ulinzi na usalama wa nchi sio la kubembelezana isipokuwa Kila mtanazania anapaswa kutoa taarifa haraka pale anapomtilia mashaka mgeni yeyote anayeingia nchini bila kibari.
"Kagera ni mkoa wa kimkakati nyote mtakuwa mlisikia maagizo ya Mheshimiwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kuhusu ulinzi na usalama hivyo naomba vyombo vya usalama tuchukue hatua kukabiliana na wimbi la wahamihaji wanaokimbilia katika mkoa huu kufuga ,kulima kujimilikisha,hii nchi ni yetu na sio Mali ya wageni kutoka nje "amesema.
Aidha amesema pia kipaumbele chake cha pili ni kuhakikisha miradi ya kimkakati yote inatekelezwa na kukamilika kwa wakati kwani miradi hiyo ndio yenye kuchochea Uchumi kwa wananchi.
“Miradi inayotekelezwa katika halmashauri lazima iendane thamani ya fedha na ikamilike ili kusogeza huduma Bora kwa wananchi wa mkoa wa Kagera.”
Awali kabla ya makabidhiano aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Fatma Mwassa amesema Mkoa wa Kagera unakabiliwa na changamoto ya wahamihaji kutoka nchi za Burundi,Rwanda,Uganda na nchi nyingine za Sudan Na congo
Amesema kwa mwaka 2024 hadi Novemba 2025 wahamihaji haramu walioingia nchini na kurudishwa walikuwa 17,200 na kati ya hao asilimia 85,ilitoka Burundi ,asilimia 5 Rwanda ,asilimia 5 Uganda na asilimia Nyinginezo .
“İdadi hiyo ni kubwa sana na inahitaji kuchukua hatua za haraka na weledi mkubwa kwani wengi ufata aridhi marisho na vibarua na baadhi wakifika wanaoa na kuolewa.”
Pia amesema mkoa huo unamiradi mingi inayotekelezwa huku akitaja kuwa uchumi wa Kagera kwa miaka mingi umekwama kutokana na kutokuwa na maamuzi ya kuwaweka vijana katika mpango mkakati wa kuwapatia kipato cha mwaka mzima kupitia sekta za kilimo mifugo na uvuvi na wengi wakitegemea ajira kutoka serikalini.
Fatma Mwassa amewashukuru wananchi na viongozi kwa ushirikiano na mipango thabiti ya kuendeleza mkoa huo ikiwemo mpango mkakati wa kuwapatia ajira vijana 2,000 Kila halmashauri kupitia Sekta ya kilimo ,mifugo,uvuvi na viwanda.
.jpeg)



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia Mheshimiwa Abiy Ahmed pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika, tarehe 14 Februari, 2026 jijini Addis Ababa, Ethiopia.
KIGOMA
Baraza la Ushindani(FCT), moja ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, imeendesha kikao cha kuwajengea uwezo watumiaji wa huduma, wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za ushindani na taratibu za rufaa.
Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Lake Tanganyika Hotel na kuhudhuriwa na wadau kutoka sekta mbalimbali za biashara na huduma.
Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Ndg. Deogratias Sangu, aliwataka wananchi kutumia elimu waliyoipata kuelewa haki zao katika ushindani na udhibiti wa soko. Alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani utasaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima, kuimarisha uwajibikaji wa taasisi na kujenga mazingira ya Soko yenye usawa na haki.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa FCT, Mhe. Jaji Rose Ally Ebrahim, alisema Baraza lina jukumu la kusikiliza na kuamua rufaa zinazotokana na maamuzi ya Fair Competition Commission (FCC) pamoja na mamlaka za udhibiti wa sekta mbalimbali ikiwemo LATRA, EWURA, TCRA, TCAA na PURA.
Aliwahimiza wananchi wa Kigoma kulitumia Baraza hilo wanapokuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya vyombo husika, akisisitiza kuwa mfumo wa rufaa umewekwa kisheria ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati na kwa uwazi.
“Watu wakijua wapi pa kupata haki, wanapunguza gharama za kuhangaika kutoka sehemu moja ya huduma hadi nyingine,” alisema Mhe. Jaji Ebrahim, akisisitiza kuwa elimu ya sheria ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wananchi na wafanyabiashara kukua kiuchumi.
Wadau waliohudhuria kikao hicho waliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kuimarisha taasisi zinazolinda na kusimamia haki za wafanyabiashara na watumiaji wa huduma.
Walisema juhudi hizo zinaonyesha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi kupitia mfumo wa ushindani ulio wazi, shindani na wa haki, unaochochea ukuaji wa biashara na ustawi wa taifa.






.jpeg)

.jpeg)

































