Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MFUMO wa kufuatilia, kudhibiti na kukusanya taarifa za mafuta yanayoingia nchini kwa wakati halisi (Supervisory Control and Data Acquisition -SCADA) umeendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha usimamizi wa mafuta nchini kwa kuongeza uwazi, usahihi wa taarifa na ufanisi katika ushushwaji wa mafuta yanayoingia kupitia bandari zetu hadi kufika kwenye maghala ya kuhifadhia.

Kupitia mfumo huo, Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umefanikiwa kuimarisha udhibiti wa upotevu wa mafuta na kuongeza uhakika wa takwimu zinazotumika katika kufanya maamuzi ya kiutendaji.

Akizungumza katika mahojiano na gazeti la Uhuru kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, Afisa Lojistiki wa Mafuta wa PBPA, Bi. Hilda Kowero, alisema mfumo wa SCADA umeleta maboresho makubwa katika usimamizi wa mafuta kwa kuwezesha ufuatiliaji wa shughuli zote muhimu kwa wakati halisi.

"Teknolojia hii inatuwezesha kupata taarifa sahihi kwa wakati kuhusu mwenendo wa mafuta yanayoingia nchini. Hivyo, tunakuwa na uwezo wa kufuatilia mnyororo mzima kwa usahihi na kuongeza uwajibikaji katika usimamizi wa mafuta," alisema Bi. Kowero.

Aliongeza kuwa pamoja na kuratibu uagizaji wa mafuta kupitia Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (Bulk Procurement System - BPS), PBPA pia ina jukumu la kuhakikisha nchi inakuwa na akiba na upatikanaji wa mafuta unaoaminika wakati wote hivyo kuimarisha usalama wa hali ya upatakinaji wa mafuta nchini.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Sabasaba Kitaifa upande wa JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi akizungumza waandishi wa habari kuhusiana na JKT kuibuka mshindi wa Kwanza katika Bidhaa za Kilimo na Uvuvi kwenye Maonesho ya 50  Biashara ya Biashara Kimataifa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Sabasaba Kitaifa upande wa JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi, akiwa katika picha ya pamoja na maafande wa JKT  mara baada ya kushangilia ushindi wa ubunifu wa jeshi katika bidhaa za Kilimo na Uvuvi.

Na Mwandishi Wetu
JESHI  la Kujenga Taifa (JKT) limeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la bidhaa za kilimo na uvuvi kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), mafanikio ambayo yameelezwa kuwa ni matokeo ya uzalishaji wenye ubora, ushirikiano na utekelezaji wa maelekezo ya viongozi wa jeshi hilo.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Sabasaba Kitaifa upande wa JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi, alisema ushindi huo unathibitisha kuwa bidhaa zinazozalishwa na JKT zinakidhi viwango vya ushindani na zimeendelea kutambulika nchini.

Alisema tuzo hiyo si ya kwanza kwa JKT, kwani taasisi hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika maonesho hayo kwa miaka iliyopita kupitia bidhaa zinazozalishwa na Shirika la SUMA JKT.

"Hata mwaka jana tulikuwa washindi wa kwanza kwa bidhaa za samani na mwaka huu tumeamua kushindana katika kundi la bidhaa za kilimo na uvuvi na tumefanikiwa kuibuka washindi wa kwanza. Hii inatupa hamasa ya kuendelea kuboresha bidhaa zetu ili tuendelee kufanya vizuri kila mwaka," alisema.

Brigedia Jenerali Lupi alisema mafanikio hayo yanatokana na utekelezaji wa maelekezo ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Rajabu Bunduku Mabeyo, ambaye amekuwa akisisitiza uzalishaji wa bidhaa bora kupitia vikosi vya JKT na Shirika la SUMA JKT.

Alisema ushirikiano uliopo katika mnyororo mzima wa uzalishaji umeiwezesha JKT kuendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora na ushindani mkubwa sokoni.

Akizungumzia mchango wa JKT katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Brigedia Jenerali Lupi alisema taasisi hiyo imekuwa mstari wa mbele katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuzalisha chakula na mazao ya biashara pamoja na kutoa mafunzo kwa wananchi.

Alieleza kuwa JKT inamiliki mashamba makubwa ya uzalishaji na ranchi mbalimbali, ikiwemo Ranchi za Misenyi, Orujoro na Mafinga, huku ikiendelea na ujenzi wa kiwanda cha kisasa cha uzalishaji wa maziwa kitakachoongeza thamani ya bidhaa za mifugo.

Aidha, alisema kupitia kampuni zake, ikiwemo SUMA JKT, taasisi hiyo imeendelea kuzalisha bidhaa mbalimbali za viwandani pamoja na kutoa huduma za kitaalamu katika sekta ya kilimo na uvuvi.

Alitaja pia mchango wa kampuni ya SUMA Poni, inayojihusisha na ujenzi wa mabwawa ya kisasa ya ufugaji wa samaki na usimikaji wa mifumo ya uzalishaji, huku wataalamu wa JKT wakiendelea kutoa ushauri wa kitaalamu bila malipo kwa wananchi wanaohitaji kuwekeza katika kilimo, mifugo na uvuvi.

Brigedia Jenerali Lupi aliwataka wananchi kutembelea banda la JKT katika Maonesho ya Sabasaba ili kujionea bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na taasisi hiyo pamoja na kupata elimu kuhusu fursa za uzalishaji na uwekezaji katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na viwanda.
Mgeni Rasmi Katika Ufunguzi Maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa   Rais wa Msumbiji Daniel Francisco Chapo akimkabidhi Mwakilishi wa Kampuni ya GF Truck Salman Karmal  Tuzo ya Mshindi wa Kwanza wa Banda Bora katika Maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa ,jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya GF Trucks imesema katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) imepata mafanikio ya kuaminika kwa ubora baada ya kutwaa tuzo ya banda bora kwa mwaka wa pili katika maonesho hayo

Mafanikio hayo yanaelezwa kutokana na kuendelea kuendelea katiika kuleta teknolojia bunifu na rafiki kwa mazingira nchini.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mwakilishi wa kampuni hiyo, Salman Karmali, amesema mafanikio hayo ni ishara ya imani ambayo kampuni imejijengea kwa wadau na wananchi kupitia ushiriki wake wa muda mrefu katika maonesho hayo.

Amesema GF Trucks and Equipment imekuwa mshiriki wa maonesho ya Sabasaba kwa miaka mingi na imeendelea kutumia jukwaa hilo kuwatambulisha Watanzania bidhaa na teknolojia mpya zinazolenga kuongeza ufanisi katika sekta Usafirishaji pamoja na mitambo.

Mwaka huu wa maadhimisho ya miaka 50 ya Sabasaba, GF Trucks and Equipment imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuleta suluhisho za kisasa katika sekta ya usafirishaji, ujenzi na uchimbaji, huku ikijikita katika matumizi ya teknolojia endelevu na rafiki kwa mazingira.


“Ni heshima kubwa kwetu kupata tuzo hii kwa mwaka wa pili mfululizo. Tunawashukuru viongozi wa TanTrade kwa kutupa heshima hii na kutuongezea hamasa ya kuendelea kuboresha huduma na bidhaa zetu,” amesema.

Amebainisha kuwa katika maonesho ya mwaka huu kampuni imewasilisha bidhaa mbalimbali zikiwemo magari madogo, malori, mitambo mizito pamoja na mashine za kisasa za utafiti na uchimbaji maji.

Amesema vivutio vikubwa katika banda lao ni mitambo pamoja na mashine za utafiti na uchimbaji zinazojulikana kama drilling rigs au exploration rigs, ambazo hutumika katika tafiti za vyanzo vya maji na shughuli nyingine za uchimbaji.

Amesema baadhi ya mitambo hiyo imebuniwa kwa kuzingatia mazingira na mahitaji ya Tanzania baada ya kufanyiwa tafiti za kina ili kuhakikisha inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Karmali amesema kampuni hiyo inaendelea kuunga mkono juhudi za kuhifadhi mazingira kwa kuleta teknolojia zinazopunguza matumizi ya mafuta na kupunguza athari kwa mazingira.

“Kwa sasa dunia inaelekea kwenye matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira. Sisi tumekuja na bidhaa zenye matumizi madogo ya mafuta na pia tumewaletea magari yanayotumia umeme ya chapa ya Hyundai, ambayo tayari yameanza kutambulishwa nchini,”amesema.

Ameongeza kuwa kampuni hiyo itaendelea kutoa ofa maalum kwa wateja wake hadi mwisho wa maonesho hayo na kuwahimiza wananchi pamoja na wadau wa sekta mbalimbali kutembelea banda lao ili kujionea teknolojia mpya zinazowasilishwa na kampuni hiyo.

Mwakilishi wa Kampuni GF Truck & Equipment akiwa katika ufunguzi wa maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa


Na Mwandishi Wetu
AFISA Mtendaji Mkuu wa MIXX, Angelica Pesha, amesema kampuni hiyo imejipanga kikamilifu kuwahudumia wananchi wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kuwapatia huduma mbalimbali za kifedha na mawasiliano kwa urahisi na usalama.

Pesha alitoa kauli hiyo alipotembelea banda la MIXX katika maonesho hayo yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Alisema MIXX imeweka mazingira rafiki yatakayowawezesha wananchi kufanya miamala mbalimbali ya kifedha bila ulazima wa kubeba fedha taslimu, hatua ambayo inalenga kuongeza usalama na urahisi wa huduma kwa watumiaji.

"Hatuna sababu ya wananchi kutembea na fedha taslimu wakati huduma zetu zinapatikana hapa bandarini. Tunawahimiza wote wanaotembelea Sabasaba kufika banda la MIXX ili wapate huduma za kifedha kwa haraka na kwa usalama," alisema Pesha.

Aliongeza kuwa, pamoja na huduma za kifedha, MIXX pia inatoa huduma mbalimbali za mawasiliano, ikiwemo ununuzi wa bando na huduma nyingine zinazowarahisishia wateja kuendelea kuwasiliana popote walipo.

Pesha aliwataka wananchi kutumia fursa ya maonesho hayo kutembelea banda la MIXX ili kujionea huduma zinazotolewa na kupata elimu kuhusu suluhisho mbalimbali za kidijitali zinazorahisisha maisha ya kila siku.

Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yamewakutanisha taasisi za Serikali na sekta binafsi zikionyesha bidhaa, huduma na ubunifu mbalimbali unaochochea maendeleo ya biashara na uchumi nchini.

Afisa Mtendaji Mkuu wa MIXX Angelica Pesha akizungumza na waandishi wa habari walivyojipanga kuhudumia wananchi maonesho ya Sabasaba


NAIBU Katibu Mtendaji Tume ya Taifa ya Mipango - Biashara na Ubunifu, Dkt. Blandina Kilama amesema anaitegemea Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya maendeleo 2050 iliyoanza Julai Mosi mwaka huu.

Akizungumza katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa - Sabasaba katika banda la PURA Dkt Kilama amesema ana matumaini makubwa kwamba PURA itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha utekelezaji wa DIRA 2050 unakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake Bw. Ebeneza Mollel kutoka PURA amesema kufuatia utekelezaji wa DIRA 2050 tayari PURA imehuisha Mpango Mkakati wa Taasisi kwa mwaka 2026/27 - 2030/31 ili kuendana na matakwa ya DIRA 2050.

Nishati ni moja ya kichocheo katika vichocheo vitano kufanikisha malengo ya DIRA 2050, ambapo PURA inaendelea kutoa elimu kuhusu utafutaji uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia nchini katika Maonyesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba.
-Yatwaa tuzo mbili ikiwemo mshindi wa tatu wa jumla

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitazama huduma mbalimbali zilizokuwepo ndani ya banda la Vodacom, wakati wa kutembelea banda hilo muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), baada ya kupata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire, kuhusu huduma zinazotolewa na kampuni hiyo.

Rais Samia aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho hayo. Katika hafla hiyo, Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu katika Kundi la Washindi wa Jumla wa Maonesho hayo na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Tukio hilo lilifanyika Julai 3, 2026, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo wakipokea maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire, kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) walipotembelea banda la Vodacom muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa maonesho hayo. Maonesho hayo yamefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo Julai 3, 2026, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili, ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire (kulia), kuhusu huduma ya simu mpya ya smati kitachi inayouzwa na kampuni hiyo ili kuwawezesha Watanzania kuingia katika ulimwengu wa kidijitali wakati Marais hao walipotembelea banda la Vodacom muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA). Katika hafla hiyo, Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu katika Kundi la Washindi wa Jumla wa Maonesho hayo na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo.

Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa katika picha ya pamoja kwenye banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), wakifurahia ushindi baada ya kampuni yao kutunukiwa tuzo mbili: Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi Julai 3, 2026, na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye kabla ya hafla ya ufunguzi aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutembelea banda la Vodacom na kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.



Na Mwandishi Wetu, Shelisheli
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Chande (Mb.) ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 69 wa Shirika la Utalii Duniani Kamisheni ya Afrika uliofanyika mjini Mahe, Jamhuri ya Ushelisheli.

Mkutano huo ulifunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Ushelisheli, Mhe. Dkt. Patrick Herminie Julai 2, 2026 ukiwa na dhima ya "Kuimarisha Rasilimali Watu ili Kuchochea Ukuaji wa Utalii Barani Afrika.”

Pamoja na mambo mengine mkutano huo ulijadili hali ya Sekta ya Utalii Barani Afrika na Duniani kwa ujumla ikijumuisha mwenendo wa ukuaji wa watalii, changamoto na fursa zilizopo; pamoja na hatua zinazochukuliwa katika utekelezaji wa programu na mipango ya Shirika la Utalii la Umoja wa Mataifa (UN Tourism) katika ngazi ya Kimataifa na Kikanda; utalii endelevu; maendeleo ya rasilimali watu na elimu ya utalii; uwekezaji na ubunifu katika sekta; pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama na wadau mbalimbali.

Kupitia Mkutano huo Mkurugenzi wa Shirika la Utalii Kanda ya Afrika Bi. Elcia Grandcourt aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Afrika kwa kipindi cha Mwaka 2025/26 iliyosheheni shughuli zilizotekelezwa kwa kushirikiana na nchi wanachama na wadau mbalimbali, ikiwemo kuimarisha uwezo wa rasilimali watu, kukuza utalii endelevu, kuendeleza ubunifu na matumizi ya teknolojia, kuongeza uwekezaji na ushindani katika Sekta ya Utalii, pamoja na kuimarisha ushirikiano wa Kikanda ili kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo jumuishi kupitia utalii.

Sambamba na taarifa hiyo Bi. Grandcourt, aliwasilisha matokeo ya Utafiti kuhusu Kukuza Upatikanaji wa Elimu ya Utalii na Maendeleo ya Rasilimali Watu Barani Afrika.

Aidha, nchi wanachama walijadili kwa kina kuhusiana na uwezeshaji wa usafiri ndani ya nchi za Afrika kuwa na muunganiko wa safari ya pamoja, kurahisisha upatikanaji wa Visa, sambamba na utoaji wa elimu na maendeleo ya rasilimali watu.






WENGE wa Uhuru umewasili wilaya Siha ukitokea Hai mkoani Kilinanjaro ambapo unatarajiwa kukimbizwa kilomita 144 katika wilayani humo na kutembelea miradi ya maendeleo saba.

Akizungumza katika mapokezi hayo, yakiyofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Ormelili, Mkuu wa wilaya ya Siha, Christophe Timbuka alisema kuwa, Mwenge huo utazindua, kuweka mawe ya msingi pamoja na kutembelea miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo.

Miradi itakayotembelewa ni uwekaji wa jiwe la msingi kituo cha afya Ormelili chenye thamani ya milioni 250, uzinduzi wa mradi wa maabara za kemia na fizikia katika shule ya sekondari ya Sikirari wenye thamani ya shilingi milioni 104.71.

Miradi mingine ni kutembelea mradi wa vijana kazi iendelee Lawate wenye thamani ya shilingi milioni 25, uwekaji wa jiwe la msingi daraja la upinde wa mawe Songu (milioni 153.7.), uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa maji Gararagua kwenda vijiji 8 (Bilioni 1.59).

Aidha Mwenge huo utaweka jiwe la msingi mradi wa upanuzi wa shamba la kuku wazazi la Tanbreed (Bilioni 9.71) na kuzindua shule mpya ya sekondari Mitimirefu (milioni 584.28).






Na Mwandishi Wetu


NCHI za Tanzania na Urusi zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya utalii, hatua inayolenga kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili na kuongeza fursa za utalii, biashara na uwekezaji.

Makubaliano hayo yanaenda sambamba na kuanza kwa safari za moja kwa moja za kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) zinazounganisha Moscow na Tanzania Bara pamoja na Zanzibar, hatua itakayorahisisha usafiri wa watalii na wafanyabiashara kati ya masoko hayo mawili.

Katika safari hiyo ya kihistoria ya kwanza, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji, aliongoza ujumbe wa Tanzania uliojumuisha Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na wadau zaidi ya kampuni 47 za utalii.

Ujumbe huo ulikutana na wadau wa sekta ya utalii kutoka Urusi kupitia mikutano ya biashara baina ya wafanyabiashara (B2B), iliyowapa fursa ya kujadiliana, kujenga ushirikiano mpya wa kibiashara na kutangaza vivutio vya kipekee vya utalii vya Tanzania kwa soko la Urusi.

Hatua hii inatarajiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka Urusi, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya utalii, na kuchangia utekelezaji wa malengo ya Tanzania ya kukuza sekta ya utalii na uchumi wa nchi kupitia masoko mapya ya kimkakati.










Na Pamela Mollel,Arusha 

Arusha inatarajia kuandika historia mpya kupitia Tamasha kubwa la Sanaa na Kazi za Ufundi litakalofanyika Oktoba 2026, tukio linalolenga kuipa nguvu sekta ya utalii na sanaa pamoja na kukuza uchumi na ubunifu nchini Tanzania

Tamasha hilo linaandaliwa na Tanzania International Tourism Festival (TITF) kwa kushirikiana na Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TASFA), likiwa limebeba dhamira ya kuwaunganisha wasanii, wabunifu na wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mkurugenzi wa TITF, Ibrahim Jamal, amesema lengo kuu la tamasha hilo ni kuinua thamani ya kazi za ubunifu na kuzifanya ziwe na ushindani katika masoko ya kimataifa kupitia sekta ya utalii

Amefafanua kuwa tamasha hilo litakuwa jukwaa muhimu litakalowakutanisha wachongaji, wachoraji, wabunifu wa mavazi, watengenezaji wa vito, wafinyanzi na wasanii wa kazi za mikono kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania

Mbali na maonesho ya sanaa, washiriki watapata fursa ya mafunzo maalum yatakayojikita katika uongezaji thamani wa bidhaa, ulinzi wa haki miliki za kazi za ubunifu pamoja na mbinu za kufikia masoko ya ndani na nje ya nchi

Aidha, kutakuwa na maonyesho ya moja kwa moja ya utengenezaji wa kazi za sanaa (live demonstrations) pamoja na mikutano ya kibiashara (B2B) itakayowaunganisha wasanii na wanunuzi wakubwa pamoja na wawekezaji wa kimataifa

Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA), Rukia Walele, amesema tamasha hilo linafungua ukurasa mpya kwa sekta ya sanaa za ufundi ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikichangia uchumi na kuhifadhi utamaduni wa Kitanzania

Ameongeza kuwa kupitia vyama zaidi ya 20 vinavyounda shirikisho hilo, maelfu ya wasanii nchini watapata nafasi ya kutambulika, kujifunza mbinu za kisasa za biashara na kujenga mitandao itakayowaingiza katika masoko ya kikanda na kimataifa

Aidha, amesema sanaa za ufundi ni nguzo muhimu ya uchumi wa ubunifu, hivyo tamasha hilo litasaidia kuongeza kipato kwa wasanii na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha sanaa na utalii barani Afrika

 Waandaaji wamesisitiza kuwa Arusha itakuwa kitovu cha ubunifu na utalii wakati wa tamasha hilo, ambalo linatarajiwa kuvutia maelfu ya washiriki na wageni kutoka mataifa mbalimbali, ikiwa ni chachu ya mageuzi ya kiuchumi kupitia sanaa na utamaduni.







Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, amesema Mkoa wa Iringa unaendelea kujipambanua kama mkoa wenye fursa ya utalii, kilimo, huku akiwakaribisha wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi kufika mkoani humo kutumia fursa zilizopo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Juni 3, 2026, mara baada ya kutembelea banda la Mkoa wa Iringa katika Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba, Mhe. Kheri amesema Iringa imebarikiwa vivutio vya kipekee vya utalii vinavyoifanya kuwa eneo lenye fursa kubwa za uwekezaji.

Ameitaja Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kuwa miongoni mwa vivutio vikubwa vinavyovutia watalii kutoka sehemu mbalimbali duniani, akisisitiza kuwa wawekezaji wenye ndoto ya kuwekeza katika sekta ya utalii wanapaswa kuichagua Iringa kutokana na mazingira yake rafiki kwa biashara.

Aidha, ameeleza kuwa Iringa ina maeneo mengi ya kimkakati yanayofaa kwa kilimo cha biashara na ndiyo mkoa unaoongoza nchini kwa kuwa na skimu kubwa za umwagiliaji, hali inayowezesha uzalishaji wa mazao kwa kiwango kikubwa mwaka mzima.

Mhe. Kheri amebainisha kuwa wawekezaji wanaolenga sekta ya mazao, hususan zao la mpunga na shughuli za kuongeza thamani ya mazao ya mbao , wana kila sababu ya kuwekeza Iringa, akieleza kuwa mkoa huo una mazingira yanayowezesha ukuaji wa uwekezaji wenye tija.




KWA sasa, burudani si tu njia ya kupumzika, bali pia ni sehemu ya kujifunza, kushindana na kujitengenezea fursa mpya. Meridianbet imeelewa hilo vizuri kupitia promosheni hii maalum iliyoundwa kwa watumiaji wa Airtel Money. Kupitia Mzuka wa Mabingwa, kila mchezaji mwenye umri unaoruhusiwa kushiriki anaweza kuingia kwenye droo za kila siku, kila wiki na droo kuu kwa kutia dau la kuanzia shilingi 5,000 na kucheza michezo ya kasino au kuweka tiketi ya michezo yenye thamani hiyo au zaidi.

Kinachovutia zaidi katika promosheni hii ni aina ya zawadi zinazotolewa. Fikiria kuamka asubuhi na kupokea taarifa kwamba umejishindia mizunguko 250 ya bure, au kupigiwa simu na kuambiwa umejishindia smartphone mpya kupitia droo ya wiki. Lakini zaidi ya yote, kuna zawadi kuu ambazo zinamuweka kila mshiriki kwenye hali ya matarajio makubwa, Bajaj mpya kabisa, PlayStation 5 mbili na televisheni ya kisasa ya Hisense. Kwa kizazi kinachopenda teknolojia, michezo na maisha yenye ubunifu, hizi si zawadi za kawaida bali ni ndoto ambazo zinaweza kutimia kwa hatua chache tu.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba na nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10#.

Kwa mujibu wa wadau mbalimbali wa burudani za kidijitali, promosheni zinazounganisha teknolojia, michezo na zawadi za kweli zinaendelea kupata umaarufu mkubwa. Hii ni kwa sababu vijana wengi wanatafuta uzoefu unaowapa nafasi ya kushiriki, kuburudika na wakati huo huo kupata fursa ya kushinda. Meridianbet imefanikiwa kuleta hili kupitia Mzuka wa Mabingwa, ambapo kila mchezo unaweza kuwa mwanzo wa simulizi mpya ya ushindi. Promosheni hii ni jukwaa la kuonyesha kwamba bahati na maamuzi sahihi vinaweza kukutana.

Kwa wale ambao bado hawajajiunga, huu unaweza kuwa wakati sahihi wa kujaribu bahati yako. Ikiwa wewe ni mpenzi wa michezo ya kubashiri au kasino, Mzuka wa Mabingwa inaweza kuwa mlango wa kuelekea kwenye zawadi ambazo umekuwa ukizitamani. Unachotakiwa kufanya ni kutumia Airtel Money, kuweka dau la angalau shilingi 5,000 na kuanza safari yako ya ushindi.




NYASI zinaenda kuwaka leo kwenye mechi hii ya kibabe sana kati ya Canada dhidi ya Morocco ambapo wote wanatafuta nafasi ya kwenda hatua ya Robo Fainali. Odds kubwa zinakusubiri kwenye mechi hii ingia na ubeti sasa.

Hayawi hayawi sasa yamekuwa na leo hii tutaenda kushuhudia mechi ya kwanza ya hatuia ya 16 bora kwenye Taji hili la Dunia kati ya Canada dhidi ya Morocco, mchezo ambao unaweza kuwa na uzito mkubwa kutokana na ubora wa timu hizi mbili mpaka kufika hapo walipo.

Ushindi hii ni tiketi kwa timu mojawapo kwenda hatua ya Robo Fainali, alkini pia huu ni mchezo ambao unarejesha kumbukumbu za Taji la Dunia 2022 ambapo Simba wa Atlas yaani Morocco ilipoifunga Canada mabao 2-1 kwenye hatua ya makundi kwgaiyo hii ni mechi ya kisasi kwa enyeji.

Canada ambao ni moja ya nchi ambao ni wenyeji wa mashindano haya safari yao uelekea hatua hii imeonyesha mabadiliko makubwa ya timu hiyo. Katika hatua ya 32 bora, walishinda kwa ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Afrika Kusini baada ya bao la dakika za mwisho la Stephen Eustáquio. Timu hiyo ilionesha nidhamu kubwakwa wapinzani wao mpaka kipenga cha mwisho.

Nafasi ya kuondoka na pesa ndefu ipo kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa upande wa Morocco wao ilipitia mtihani mgumu zaidi. Ilihitaji dakika 120 pamoja na mikwaju ya penalti kuiondoa Uholanzi baada ya kutoka sare ya 1-1. Ushindi huo umeongeza kujiamini kwa kikosi hicho baada ya kuonesha kiwango kizuri kwenye michezo ambayo wamecheza. Odds kubwa zinakungoja leo. Ingia na ubashiri sasa.

Je unajua kuwa tofauti kubwa zilizopo kwenye hizi timu ni kwenye aina ya uchezaji?. Canada hupenda kushambulia kwa kasi, kufanya presha mapema na kuwalazimisha wapinzani kufanya makosa. Chini ya kocha Jesse Marsch, timu hiyo imekuwa ikitumia nguvu nyingi katika kukaba na imekuwa ikiwazidi wapinzani kwa umbali wa kukimbia ndani ya uwanja. Hilo linaweza kuwa faida kubwa ikiwa Morocco itaonyesha dalili za uchovu kutokana na mechi yake ya awali.

Morocco, hata hivyo, imeonyesha ukomavu mkubwa katika michezo ya mtoano. Ina safu ya ulinzi iliyopangika vizuri, haipotezi umbo la timu kirahisi na inajua namna ya kusubiri nafasi sahihi kabla ya kuanzisha mashambulizi ya kushtukiza.

Hata ilipopata presha dhidi ya Uholanzi, iliendelea kuwa tulivu hadi iliposhinda kwa penalti. Tabia hiyo inaweza kuwa silaha muhimu dhidi ya Canada ambayo hupenda kupandisha wachezaji wengi mbele. Jisajili na Meridianbet hapa.

Je ni Canada ua Morocco kwenda hatua ya Robo Fainali leo?. Timu ambayo itakuwa imejipanga vyema na kutumia nafasi vizuri huenda ikawa na bahati zaidi ya kusonga mbele.

KATIKA kuendeleza juhudi zake za kuchangia ustawi wa jamii kupitia programu zake za uwajibikaji kwa jamii, Benki ya Absa Tanzania imetoa msaada wa Shilingi milioni 20 kwa ajili ya kusaidia matibabu ya watoto wanaoishi na magonjwa ya moyo nchini Tanzania.

Msaada huo umetolewa kupitia Heart Team Africa Foundation (HTAF), taasisi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), yenye lengo la kuwasaidia watoto wanaotoka katika mazingira yenye uhitaji Ili kupata matibabu na huduma za moyo hivyo kuokoa maisha yao.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa Hati ya Makubaliano (MoU), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, alisema ushirikiano huo unaakisi dhamira ya benki hiyo ya kuwa chachu ya maendeleo mema katika jamii inazozihudumia.

"Dhamira yetu ni kuwa chachu ya maendeleo mema katika kila tunachofanya, na ushirikiano huu ni uthibitisho wa dhamira hiyo kwa vitendo. Tunatambua kazi kubwa inayofanywa na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo kwa watoto na familia nchini Tanzania. Kupitia Hati hii ya Makubaliano, tunaongeza fursa kwa watoto wanaoishi na magonjwa ya moyo kupata matibabu yanayookoa maisha na kuzipa matumaini familia zinazokabiliwa na changamoto kubwa za kiafya na kifedha.

"Kila mtoto anastahili nafasi ya kuishi maisha yenye afya na yenye tija. Kwa kuwekeza katika afya zao leo, tunawekeza katika mustakabali wao, ustawi wa familia zao na maendeleo endelevu ya jamii zetu. Tunajivunia kushirikiana na JKCI katika mpango huu muhimu unaolenga kuboresha maisha ya watoto kote nchini Tanzania”, alisema Bw. Laiser.

Akipokea msaada huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, aliishukuru Benki ya Absa Tanzania kwa mchango huo, akieleza kuwa utasaidia kuongeza upatikanaji wa matibabu muhimu ya moyo kwa watoto wanaoishi na magonjwa ya moyo.

Alisema magonjwa ya moyo yanaongezeka kwa kasi duniani ikiwa ni pamoja na Tanzania, waathirika pia wakiwa ni watoto ambao wengi wao zaidi ya asilimia 70 wanazaliwa wakiwa na changamoto za magonjwa hayo licha ya wale wanaoyapata baada ya kuzaliwa.

"Msaada huu umekuja wakati muhimu kwa watoto wengi na familia zinazohitaji huduma maalumu za matibabu ya moyo," alisema. "Mbali na kutusaidia kuokoa maisha, unadhihirisha nafasi muhimu ya ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za afya katika kuimarisha utoaji wa huduma za afya na kuboresha matokeo ya matibabu kwa wagonjwa nchini Tanzania.

“Namshukuru Mheshimiwa rais na serikali yake kwa kusaidia zaidi ya asilimia 70 ya gharama, kwa niaba ya bodi ya JKCI, kwa niaba ya serikali kwa jinsi mnavyofanya kumuunga mkono mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kurudisha matumaini na kuwapa watu upendo, Absa mmefanya,mmetekeleza kile ambacho rais anakihitaji”, aliongeza Dk. Kisenge.

Nao baadhi ya wazazi wanufaika wa msaada huo, Mariam Athumani ambaye mtoto wake Lightness ameshafanyiwa upasuaji wa moyo na Adam Nuhu ambaye mtoto wake Ajmalbey anayesubiri upasuaji wametoa shukurani kwa Benki ya Absa huku wakiziomba taasisi nyingine kujitolea kuwasaidia kutokana na changamoto kubwa wanazozipata wazazi wenye watoto wenye magonjwa ya moyo.

Benki ya Absa inasema mchango huo unathibitisha dhamira ya benki hiyo ya ‘kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja... Hatua moja baada ya nyingine’, kupitia kusaidia upatikanaji wa matibabu yanayookoa maisha kwa watoto wenye magonjwa ya moyo, ikilenga kuboresha matokeo ya afya, kupunguza mzigo wa kifedha kwa familia zilizoathirika, na kuchangia kujenga jamii zenye afya bora na ustahimilivu zaidi nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), akizungumza katika hafla ya utiaji saini  Hati za Makubaliano (MoU) ya ushirikiano kati ya benki hiyo na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) , ambapo pia  benki hiyo ilitoa Shilingi Milioni 20 kusaidia matibabu ya watoto wenye changamoto ya magonjwa ya moyo wanaotoka katika familia zenye uhitaji. Hafla hiyo ilifanyika katika taasisi hiyo, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Katibu wa Kampuni kutoka Benki ya Absa Tanzania, Bw. Desmond Malyi, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge, Meneja Mkuu wa Taasisi ya Global Medicare, Bw. Daniel Lazaro, na Ofisa Huduma za Sheria wa JKCI, Bi. Ummukulthum Said.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge wakisaini Hati za Makubaliano (MoU) ya ushirikiano kati ya pande hizo mbili, katika hafla ambayo pia   benki hiyo ilitoa Shilingi Milioni 20 kusaidia matibabu ya watoto wenye changamoto ya magonjwa ya moyo wanaotoka katika familia zenye uhitaji. Hafla hiyo ilifanyika katika taasisi hiyo, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Katibu wa Kampuni kutoka  Benki ya Absa Tanzania, Bw. Desmond Malyi na Meneja Mkuu wa Taasisi ya Global Medicare, Bw. Daniel Lazaro.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge wakibadilishana Hati za Makubaliano (MoU) ya ushirikiano kati ya pande hizo mbili muda mfupi baada ya kuzisaini katika hafla ambayo pia  benki hiyo ilitoa Shilingi Milioni 20 kusaidia matibabu ya watoto wenye changamoto ya magonjwa ya moyo wanaotoka katika familia zenye uhitaji. Hafla hiyo ilifanyika katika taasisi hiyo, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Katibu wa Kampuni kutoka Benki ya Absa Tanzania, Bw. Desmond Malyi na Meneja Mkuu wa Taasisi ya Global Medicare, Bw. Daniel Lazaro.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge (wa nne kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia kwake), wakipiga picha ya pamoja pamoja na wazazi na watoto wao wanaopatiwa matibabu ya moyo katika taasisi hiyo mara baada ya tukio hilo jijini Dar es Salaam jana. 


Benki ya NMB imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za bima kidijitali kupitia Umebima Mini App, huduma iliyounganishwa ndani ya programu ya NMB Mkononi, inayowawezesha wateja kununua bima kwa urahisi kupitia simu zao za mkononi.

Akizungumza na waandishi wa habari, katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, maarufu kama Sabasaba, Mkuu wa Idara ya Bima Benki ya NMB, Martin Massawe, alisema huduma hiyo inaendana na kauli mbiu ndogo ya maonesho hayo, “Biashara za Tanzania Kidijitali Zaidi.”

Massawe alisema Umebima Mini App imeondoa ulazima wa mteja kufika tawi la benki au ofisi za bima, kwa kuwa sasa anaweza kuchagua na kununua bima inayokidhi mahitaji yake akiwa mahali popote, kwa njia rahisi, salama na ya haraka kupitia NMB Mkononi.

Alisema bima ni nyenzo muhimu ya usalama wa kifedha kwa mtu binafsi, familia na biashara, hasa katika kujikinga dhidi ya majanga yasiyotegemewa. Aliongeza kuwa NMB imeandaa bidhaa mbalimbali za bima kwa makundi tofauti, ikiwemo Matching Insurance kwa wafanyabiashara wadogo, ili kusaidia kulinda biashara zao kwa gharama nafuu na kupitia njia za kidijitali.









Top News