TUME ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Februari 11, 2026, imekutana na Profesa Palamagamba Kabudi.

Mkutano huo wa Tume na Kabudi umefanyika katika Ukumbi wa Tanganyika uliopo katika ofisi za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) jijini, Dar es Salaam.

Miongoni mwa yaliyojadiliwa ni pamoja na namna matukio hayo yalivyoanza, athari zake kwa watu, mali na miundombinu pia ushauri wa namna ya kuondokana na matukio hayo.

Tume inaendelea kukutana na makundi mbalimbali wakiwemo waathirika wa Matukio hayo lengo ni kupata kiini cha chanzo cha matukio hayo na kuyawasilisha kwa ajili ya hatua zaidi.




▪️Benki ya Dunia yafurahishwa na mchango wa Sekta ya Madini wa kuchochea Uchumi Tanzania

📍 Cape town – Afrika Kusini

Sekta ya Madini Tanzania kupitia Kongamano la Mining Indaba 2026 imeendelea kuimarisha nafasi yake kimataifa, huku Tanzania ikiendelea kujidhihirisha kama kimbilio la uwekezaji katika Sekta ya Madini kwa kuvutia mashirika ya kimataifa, kampuni mbalimbali na wawakilishi wa kidiplomasia. 

Februari 10, 2026, Waziri wa Madini alikutana na wadau muhimu ikiwemo Benki ya Dunia katika vikao vya pembeni vya kongamano linaloendelea jijini Cape Town, Afrika Kusini, pamoja na kushiriki Mkutano wa Mawaziri wa Madini wa SADC.

Australia Yaipa Kipaumbele Tanzania Sekta ya Madini

Katika kikao kilichofanyika baina ya ujumbe wa Australia na Tanzania, Naibu Balozi wa Australia Christopher Ellinger alieleza kuvutiwa na mwenendo wa Sekta ya Madini nchini na kusema kwamba kwa kampuni za Australia, Tanzania ni moja ya machaguo ya kwanza kwa uwekezaji. Pia, amesisitiza utayari wa nchi hiyo kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza miradi ya madini kupitia kampuni za Australia, na kuomba ufafanuzi wa Kanuni za Madini za ushirikishwaji wa Watanzania katika sekta, hasa katika utoaji wa huduma migodini.

Benki ya Dunia yaiweka Tanzania kama Msingi wa  Uwekezaji Afrika

Benki ya Dunia imetambua sekta ya madini Tanzania kama eneo la kimkakati lisilopaswa kuachwa pembeni katika juhudi za maendeleo na uwekezaji, ikiashiria uhitaji wa kuendelea kuwekeza na kushirikiana na serikali katika kuboresha mazingira ya uwekezaji na kuongeza faida za kiuchumi.

Benki hiyo imeunga mkono mpango wa Tanzania kujiimarisha katika shughuli za utafutaji na utafiti wa rasilimali madini na dhamira ya uongezaji thamani madini ndani ya nchi badala ya kutegemea uzalishaji na usafirishaji wa madini ghafi nje ya nchi. Hii inaonesha umuhimu wa sekta ya madini katika mipango ya maendeleo ya Tanzania na uhusiano wake na wadau wa kimataifa. 

Waziri wa Madini alisisiza dhamira ya Serikali kuimarisha ushirikiano wa kufanya tafiti za kina za jiosayansi ambazo zitaongeza wingi wa taarifa na kuchochea uwekezaji  nchini. Aidha, Waziri Mavunde amesisitiza umuhimu wa kipaumbele cha kuongeza thamani madini ndani ya nchi kama njia ya kuongeza manufaa yatokanayo na rasilimali madini badala ya kuuza madini ghafi kwa waongezaji thamani nje ya nchi.

UWEKEZAJI WA FARU GRAPHITE MAHENGE KULETA MAPINDUZI MAKUBWA NCHINI

Waziri wa Madini

 Anthony Mavunde, alisisitiza kwamba kaulimbiu ya “Madini ni Maisha na Utajiri” inaweka kipaumbele cha kufanya tafiti za jiosayansi na kuongeza thamani ya madini ndani ya nchi. Amesema Serikali iko tayari kushirikiana na wawekezaji wote wanaochangia maendeleo ya sekta ya madini nchini kwa kuzingatia Kanuni, Sheria na miongozo iliyowekwa.  Aliyasema hayo  alipokutana na Kampuni ya Faru Graphite inayomilikiwa kwa ubia baina ya Serikali na Kampuni ya Black Rock Mining inayotarajia kuchimba madini ya kinywe, katika eneo la Mahenge, Wilayani Ulanga, Mkoani Morogoro. Katika kikao hicho, Kampuni hiyo imetangaza maendeleo mazuri kwenye mradi huo na kuwashukuru viongozi wa Serikali kwa ushirikiano unaowawezesha kufanikisha kazi.

PLANTCOR MINING, STAMICO Mguu Sawa Kuchimba Dhahabu KIGOSI

Katika kikao na Waziri Mavunde, kampuni ya uchimbaji madini na ukodishaji wa vifaa vya uchimbaji ya Plantcor Mining yenye makazi yake nchini Afrika Kusini ambayo ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kusaini Mkataba na Shirika la Madini laTaifa (STAMICO) ilimhakikishia Mhe. Mavunde kwamba mara baada ya kusaini mkataba huo wa ubia na STAMICO itaanza kushirikiana na STAMICO kuendeleza mradi wa uchimbaji madini ya dhahabu kwenye leseni inayomilikiwa na STAMICO katika eneo la Kigosi,Mkoani Geita.

Breakthrough Attorneys na Benki ya NMB washirikiana kuvutia uwekezaji Tanzania

Kampuni ya Breakthrough Attorneys na benki ya NMB, zimeshirikiana kuandaa na kutekeleza warsha ya kuitangaza sekta ya madini na kuvutia uwekezaji nchini Tanzania. Warsha hiyo iliyofanyika Februari 10, 2026 jijini Cape Town nchini Afrika Kusini na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya madini kutoka sehemu mbalimbali duniani.  Breakthrough Attorneys ni kampuni ya kisasa ya huduma za kisheria yenye makao yake Tanzania, inayotoa huduma mbalimbali za kisheria za kimataifa kwa kampuni, taasisi za fedha, taasisi za Serikali na watu binafsi.

Akizungumza katika warsha hiyo, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde ambaye alikuwa mgeni rasmi, alieleza kuwa Tanzania inahama kutoka kumiliki rasilimali za madini pekee kwenda kushiriki kikamilifu katika mnyororo mzima wa thamani wa madini. Alisisitiza  kuwa uongezaji thamani nchini Tanzania si kikwazo bali ni fursa, na kuwaasa wawekezaji kuitumia fursa hiyo kikamilifu. Alisema kuwa uongezaji thamani madini unaodhamiriwa Tanzania ni ule unaojengwa kupitia ushirikiano, unaoendana na Dira ya Madini ya Afrika (Africa Mining Vision) na sera za viwanda ambazo ni rafiki kwa wawekezaji.

Mhe.  Mavunde alipongeza ongezeko la mchango wa taasisi za fedha nchini, akitolea mfano wa Benki ya NMB, ambayo inashirikiana kikamilifu na wawekezaji wa madini katika hatua zote za mnyororo wa thamani na inashiriki kuvutia wawekezaji ndani nan je ya nchi. “Muunganiko kati ya ufadhili wa kifedha wa ndani na wa kimataifa ni ishara muhimu inayoashiria kuwa sekta ya madini ya Tanzania ina uwezo wa kufadhiliwa, kukopesheka, na kuvutia uwekezaji," alisema Waziri Mavunde.











Na Oscar Assenga,MUHEZA

MKURUGENZI Bonde la Maji la Pangani Segule Segule amewaonya watu wanao kuchukua maji chini ya ardhi,juu ya ardhi bila kufuata utaratibu uliowekwa kisheria ikiwemo kuwa vibali kuacha mara moja kwani wakiwafikia watawakamata.

Segule aliyasema hayo wakati wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maji Mto Zigi uliofanyika mjini Muheza ambapo alisema iwe mtu binafsi au taasisi wanapaswa kuwa na vibali huku akiwashauri wafuate utaratibu na kuvichukua kwenye mamlaka husika .

Aliwaeleza wadau wa Jumuiya hiyo kuwa Bonde la Mto Pangani linasimamia vyanzo vilivyopo chini ya ardhi kupitia visima na katika eneo hilo watu wengi hawana ufahamu au wengine wanaelewa lakini hawafuati utaratibu uliowekwa

Aidha alisema watu hawana ufahamu wa kutosha katika eneo la visima kwamba ukipewa ridhaa na Mkurugenzi wa Halmshauri ukipewa hatia na Wizara ya Ardhi juu ya kutumia ardhi na unapotaka kutumia rasilimali maji lazima upate kibali kutoka kwenye Bonde husika na katika Kanda ya Kaskazini anayetaka kutimia maji kutoka chini ya ardhi lazima apate kibali kuyoka Bonde la Pangani.

Aidha alisema kwamba Serikali imefanya kwa nia njema na sio kuweka ugumu watu wasitumie lakini wasiposimamiana katika hilo ipo siku maji yote yatachafuliwa na yanaweza yasiwepo.

Alieleza kwamba wao hawatoi vibali pekee bali wanaratibu wachimbaji kujua wana utaalamu wa kutosha wanaanza kuratibu kwenye utafiti huyo anayefanya utafiti je ana taaluma hiyo mpaka wanapotoa kibali cha kuchimbiwa visima wanauhakika wanakuwa ni watu sahihi wanaotumia utaalamu sahihi hivyo uchimbahji wake hauwezi kuleta madhara kwenye jmii husika,

Awali akizungumza wakati akifungua mkutano huo kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Muheza, Katibu Tawala wa wilaya hiyo serikali inatambua ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika usimamizi na uhifadhi na uendelezaji wa rasimali za maji na mazingira.

Alisema lengo kuu katika juhudi hizo ni kuhakikisha rasilimali za maji zinazopatikana kwa wingi ikiwemo ubora unaokubalika na kwa uendelevu wa matumizi ya maji kwa sasa na vizazi vijavyo.

“Niwapongeze viongozi mliomaliza muda wenu kwa kazi nzuri na kubwa mlioifanya na kusimamia uendeshaji wa jumuiya ikiwemo usimamizi wa vyanzo vya maji”Alisema

Aliongeza kwa athari za mabadiliko ya tabia ya nchi na hali ya hewa hapa nchini ikiwemo Muheza joto kali mvua hazinyeshi hayo yote yamebadilika kutokana na uharibifu wa mazingira unaoendelea.

Alisisitiza utunzaji wa mazingira ni jambo muhimu ambalo limeendelewa kupewa kipaumbele na Rais na hata alipoazimisha siku ya kuzaliwa alipanda miti hivyo kupitia jumuya hiyo waendelee kuwahamasisha watu wapande miti katika kila sikukuu zao muhimu ikiwemo kuzaliwa.

Hata hivyo alieleza kwamba kuna umuhimu wa Jumuiya hizo kuendelea kujengewa uwezo ili kuweza kutunza mazingira ikiwemo mafunzo ya mara kwa mara ili waweze kuendana na kazi na mazingira kipindi cha sasa.











Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Maendeleo ya Usimamizi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, anashiriki warsha ya uthibitishaji iliyoandaliwa na Kituo cha Afrika cha Uongozi wa Shule (ACSL) jijini Nairobi, Kenya, kuanzia tarehe 10 hadi 13 Februari 2026.

Warsha hiyo imewakutanisha wadau muhimu wa uongozi wa shule kutoka nchi mbalimbali barani Afrika, wakiwemo watunga sera, watoa huduma za maendeleo ya kitaaluma, watafiti, viongozi wa shule, pamoja na maafisa wa elimu. Jukwaa hilo linatoa fursa ya kupitia na kuboresha matokeo ya utafiti wa ramani ya uongozi wa shule, kwa lengo la kuhakikisha usahihi, muktadha stahiki, na matumizi yenye tija.

Lengo kuu la warsha ni kupitia, kuboresha, na kuthibitisha matokeo ya utafiti huo kupitia mashauriano shirikishi yanayohusisha wadau mbalimbali. Mchakato huu unalenga kuhakikisha ushahidi uliokusanywa ni sahihi, unaaminika, na unaendana na mazingira halisi ya mifumo ya elimu katika nchi za Afrika.

Aidha, warsha inalenga kujenga umiliki wa pamoja wa matokeo hayo na kuyatafsiri kuwa vipaumbele vinavyoweza kutekelezeka. Matokeo yaliyothibitishwa yanatarajiwa kusaidia maboresho ya sera katika ngazi ya kitaifa, pamoja na kuongoza mifumo na vipaumbele vya kimkakati katika ngazi za kikanda na bara zima.

Matokeo hayo pia yatachangia kuimarisha utendaji wa uongozi wa shule, kuunda mwelekeo wa programu za maendeleo ya kitaaluma, kuongoza tafiti na uzalishaji wa ushahidi, pamoja na kukuza ushirikiano na uratibu wa juhudi za kuboresha uongozi wa shule barani Afrika.

ACSL inaratibiwa na mashirika manne ya Kiafrika — Chama cha Maendeleo ya Elimu Afrika (ADEA), Education Sub-Saharan Africa (ESSA), Jukwaa la Wanawake Waelimishaji Afrika (FAWE), na VVOB – Education for Development — kwa ushirikiano na Taasisi ya Mastercard Foundation. ADEM inashiriki kama mdau kupitia ushirikiano wake na VVOB.




Dar es Salaam. Leo, Februari 9, 2026, Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Bw.Frederic Van de vyver Mkuu wa Jeune Afrique Media Group, kampuni inayoongoza ya habari ya ki-panafrika yenye makao yake makuu jijini Paris, Ufaransa.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, wamejadiliana ni kwa namna gani wanaweza wakafanya kazi pamoja katika fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini.

Bw. Mchechu alimhakikishia Bw. De vyver kuwa Tanzania ina mazingira mazuri ya uwekezaji na kwamba atapata ushirikiano wa kutosha.

“Kwa upande wa sekta ya umma utapata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa Ofisi ya Msajili wa Hazin ana kwa upande wa sekta binafsi utapata ushirikiano kutoka kwa CEOrt,” alisema Bw. Mchechu.

Kwa upande wake Bw. De vyver alieleza dhamira yake ya kuimarisha ushirikiano na Tanzania.

“Lazima tutafute namna bora ya kushirikiana,” alisema.


Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akizungumza na washiriki wa kikao kazibaina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini(hawapo pichani).

***************

Na Mwandishi Wetu

Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) umezindua mpango wake wakushirikiana na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya katika kuwezesha biashara nauwekezaji nchini.

Mpango huo unahusisha utaratibu wa kuunganisha mifumo na kubadilishana taarifa za biashara na miradi mbalimbali ya uwekezaji ili kurahisisha ufikishaji wa huduma za urasimishaji biashara na ukaguzi wa mifumo ya usalama na afya mahali pa kazi.

Mpango huo wa OSHA umewekwa wazi na Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo, Khadija Mwenda, alipohitimisha semina ya kujenga uelewa wa pamoja baina ya OSHA naMaafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya zote za Kanda ya Kaskazini ambao umefanyikakwa siku moja katika Ofisi za OSHA zilizopo Jengo la PAPU Jijini Arusha.

Bi.Mwenda amesema mpango huo umeibuliwa ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa akielekeza Taasisi za serikalikushirikiana katika utendaji ikiwemo kuhakikisha kwamba mifumo mbalimbali ya serikaliinasomana.

Aidha, ameeleza kuwa mpango huo unalenga kutekeleza agizo la Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, alilolitoa Desemba 22, 2025 ambapo aliwataka waajiri/wamiliki wa maeneo ya kazi kote nchini kuhakikisha maeneoyao ya kazi yanasajiliwa OSHA ndani ya siku 90 kuanzia mwezi Januari 2026 ilikurahisisha usimamizi wa masuala ya usalama na afya katika maeneo husika.

“Lengo kuu la mpango huu ni kuhakikisha kuwa Taasisi ya OSHA inafanya kazi kwakushirikiana na wenzetu ambao ni Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya wote tukiwakama Taasisi wezeshi katika biashara na uwekezaji,” ameeleza Mtendaji Mkuu waOSHA na kuongeza:

“Tumekuwa na kikao kizuri sana ambacho kimetufungulia zoezi letu ambalo tumepangakulifanya nchi nzima. Mpango huu utakapokamilika sote tutakuwa na uelewa wa pamojaambao utapelekea taasisi zetu kuwa wawezeshaji zaidi badala ya kuwa wadhibiti washughuli za biashara na uwekezaji nchini.”

Kwa upande wao washiriki wa semina hiyo ambao ni Maafisa Biashara wa Mikoa naWilaya zote za Kanda ya Kaskazini ikihusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga, wamepongeza mpango huo na kuahidi kushirikiana na OSHA kufanikishampango huo.

“Tumefurahia sana mafunzo ya leo,hakika tumetoka na ufahamu mpana kuhusiana nakazi za OSHA na tumeona kuna umuhimu mkubwa sana kwa wafanyabiashara nawawekezaji kujisajili katika mfumo rasmi ili waweze kuweka salama sehemu zao za kazi,” ameeleza Bw. Elisha Erasto, Mkuu wa Idara ya Biashara wa Halmashauri yaWilaya ya Rombo.

“Tunaishukuru sana OSHA kwa semina ya leo na kwaniaba ya washiriki wenzanguninapenda kusema kwamba tutashirikiana na OSHA ili kufanikisha mpango huuunaolenga kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini na hivyo kufanikishamalengo ya Dira ya Taifa 2050,” amesema Bi. Lulu Kaaya, Afisa Biashara Mkoa waArusha.

OSHA ni Taasisi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) yenye jukumula kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003inayoweka utaratibu wa kitaifa wa usimamizi wa masuala ya usalama na afya katikamaeneo ya kazi.

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akizungumza na washiriki wa kikao kazibaina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini(hawapo pichani).
Meneja wa Usalama Mahali pa Kazi wa OSHA, Mhandisi Robert Mashinji, akiwasilishamada kuhusu usajili wa maeneo ya kazi na utekelezaji wa majukumu ya OSHA kwaujumla katika kikao kazi baina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini.
Meneja wa Kitengo cha Sheria OSHA, Bi. Pendo Berege, akiwasilisha mada kuhusuSheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 katika kikao kazibaina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini.

Washiriki wa kikao kazi baina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini wakifuatilia mawasilisho toka kwa wataalam wa OSHA kuhusuSheria na Usalama na Afya Mahali pa Kazi pamoja na utekelezaji wa majukumu yaOSHA kwa ujumla.


Na Pamela Mollel,Arusha 

Maandalizi ya Michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yameibua fursa mpya za kukuza sekta ya kilimo katika Kanda ya Kaskazini, huku viongozi wakihimizwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili kukidhi mahitaji yatakayoongezeka wakati wa mashindano hayo.

Akifungua kikao kazi cha uhamasishaji na uendelezaji wa Shoroba za Kilimo leo Jumanne, Februari 10, 2026 Jijini Arusha, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian, amesema ni wakati wa mikoa ya Arusha, Tanga, Kilimanjaro na Manyara kutumia rasilimali walizonazo kuzalisha chakula cha kutosha badala ya kutegemea mazao kutoka mikoa mingine.

Amesema AFCON 2027 italeta ongezeko kubwa la mahitaji ya chakula, hivyo ni muhimu viongozi na wataalamu wa kilimo kuandaa mikakati madhubuti ya kuongeza uzalishaji, thamani ya mazao, ajira kwa vijana na mapato ya wananchi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi kutoka Ofisi ya Mageuzi ya Kilimo (ATO), Bi. Elizabeth Missokia, amesema maendeleo ya shoroba za kilimo yataunganisha uzalishaji, usindikaji, uhifadhi, usafirishaji na masoko, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kikao hicho kimefanyika katika Hoteli ya Mount Meru, Jijini Arusha, kikihusisha viongozi na wataalamu mbalimbali wa sekta ya kilimo kutoka ngazi za Mikoa na Halmashauri.








Leo Februari 10, 2026, Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Chamwino ikiongozwa na Mwenyekiti wake amabaye ni Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Mhe. Janeth Mayanja imefanya Ziara ya Kutembelea Mradi wa Maji wa Miji 28 unaotekelezwa na Wizara ya Maji kwa kushirikiana na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA).

Mhe. Mayanja amesema Kamati ya Siasa imeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo ambao utaenda kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Chamwino, hasa katika maeneo yenye mgao wa maji, ikiwemo Kata ya Chamwino, Msanga na Buigiri.

Amesema, wananchi wa Wilaya ya Chamwino wanamshukuru Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa aliyoifanya katika Wilaya ya Chamwino.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Chamwino, Mhe. George Malima, ameipongeza Wizara ya Maji na DUWASA kwa kusimamia mradi huo na kuomba Mkandarasi kukamilisha kwa wakati mradi huo.

Akisoma taarifa ya mradi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Meneja wa DUWASA Kanda ya Chamwino, Mha. Gray Mbalikila, amesema lengo la mradi huo ni kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi katika Mji wa Chamwino, ambapo kukamilika kwake kutachochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja kupunguza magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji.

Amesema gharama za mradi huo ni Shilingi Bilioni 17 ambazo zinahusisha uchimbaji wa visima virefu vinane ambavyo vimekamilika, ujenzi wa tenki la kuvunia maji la lita laki tano na miundombinu ya kusukuma na kutibu maji katika eneo la Chamwino.

Kazi nyingine zinazofanyika katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa tenki la laki mbili katika eneo la Msanga na uchimbaji na ulazaji wa Bomba za kipenyo kikubwa cha Inchi 6 hadi 16 kwa umbali wa kilometa 47.

Mradi umefikia asilimia 68 ya utekelezaji wake ambapo mkataba wa mradi huu ulisainiwa tarehe 6 Juni, 2022 na utekelezaji wake ulianza mwaka 2023 na unatarajiwa kukamilika tarehe 10 Agosti, 2026, huku Mkandarasi amepewa maelekezo na Katibu Mkuu, Wizara ya Maji kuhakikisha ifikapo tarehe 31 Machi, 2026 awe ameanza kufanya majaribio ya Mradi.

Kukamilika kwa Mradi huo utaongeza upatikanaji wa Majisafi kutoka asilimia 91 ya sasa hadi asilimia 100 na utaenda kuhudumia wananchi zaidi ya 59,085 katika eneo la kihuduma la DUWASA katika Mji wa Chamwino, ambapo Kata 4 zenye jumla ya Vijiji na Mitaa 7 na Vitongoji 48 watanufaika.














Top News