SHIRIKA la Dawa Asili na Ulinzi wa Mazingira(TRAMEPRO) limesema linatambua na kuthamini mchango wao katika kukuza na kuendeleza sekta ya tiba asilia, ambayo imeendelea kuwa tegemeo muhimu kwa wananchi wengi katika huduma za afya.Akitoa salaam kuhusu maadhimisho hayo ya Siku ya Wafanyakazi duniani Katibu Mkuu wa TRAMEPRO Boniventura Mwalongo amesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa wanaungana na jumuiya ya kimataifa kusisitiza kuwa kazi ni msingi wa utu, heshima na maendeleo ya binadamu.Amesema Kaulimbiu ya Mei Mosi mwaka huu inasema Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050,hivyo wanasisitiza umuhimu wa kazi zenye staha.“Mafundisho ya kijamii na kiroho, kama yanavyoakisiwa na World Health Organization, yanaeleza kuwa kazi si tu njia ya kujipatia kipato, bali pia ni wito wa kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa jamii yenye haki, mshikamano na ustawi wa wote.“Sekta ya tiba asilia na mbadala inaendelea kuwa mhimili muhimu wa mfumo wa afya, ikichangia utoaji wa huduma, ajira, uhifadhi wa maarifa ya jadi na kukuza uchumi wa ndani,”amesema na kusisitiza umuhimu wa kazi katika maendeleo ya taifa.Ameongeza Baba wa Taifa Mwalim Julius Kambarage Nyerere aliwahi kusema:“Kazi ni kipimo cha utu na msingi wa maendeleo ya binadamu.”Kuhusu takwimu za ajira katika sekta ya tiba asili na mbadala amesema zaidi ya asilimia 70–80 ya watu duniani hutegemea tiba asilia na mbadala kwa kiwango fulani cha huduma za afya;Amefafanua hali hiyo imezalisha mamilioni ya ajira duniani, zikiwemo za waganga wa jadi, watafiti, wazalishaji wa dawa za asili, washauri wa afya na watoa huduma za tiba jumuishi huku akieleza Shirika la Afya Dunuani inatambua rasmi kundi la wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala kama sehemu ya nguvu kazi ya sekta ya afya duniani.Amesema kwa Afrika na TanzaniaBarani Afrika, zaidi ya asilimia 80 ya wananchi hutegemea tiba asilia, hivyo kuifanya kuwa sekta muhimu ya ajira vijijini na mijini;Wakati huo huo amesema TRAMEPRO inasisitiza kuwa haki, usawa na heshima kwa wafanyakazi ni nguzo kuu ya maendeleo endelevu na mwito wao kwa Serikali ni kuendelea kuimarisha sera, sheria na usimamizi wa sekta ya afya na tiba asilia.Pia kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji, utafiti na ubunifu, kukuza ajira na kulinda haki za wafanyakazi na kwa vijana kuchangamkia fursa za ajira na ubunifu katika tiba asilia na mazingira.Mwalongo amezungumzia umuhimi wa kuzingatiwa haki, mshikamano na uwajibikaji ambapo kwa kufanya hivto litajengwa taifa lenye afya bora, uchumi imara na maendeleo endelevu yanayomgusa kila Mtanzania.
Kutoka Pemba, Unguja, Mji mkongwe, Bagamoyo, Kondoa, Magofu ya kilwa, paa la mlima kilimanjaro na maeneo mengine ya Tanzania, wadau wa urithi wa dunia wamekutana katika Makumbusho ya Urithi Geopark Karatu Mkoani Arusha yanayosimamiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa lengo la kuadhimisha Urithi wa Dunia Afrika yaliyoanza leo tarehe 04/05/2026 hadi tarehe 05/05/2026.
Wakiwa katika jengo la makumbusho ya Urithi Geopark Wadau hao wameelezwa jinsi Ngorongoro ilivyo ni utajiri wa urithi wa dunia kutokana na uumbwaji wake uliotokana na mlipuko wa volcano zaidi ya miaka milioni mbili iliyopita na kutengeneza kasoko iliyokusanya asili, uhai wa binadamu, mifumo ya ikolojia, na ustawi wa viumbe mbalimbali.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Bw. Abdul-Razaq Badru amewashukuru wadau wote hasa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kuipa fursa Ngorongoro kuandaa na kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo kwa mwaka huu.
Wadau wa urithi wa duania wakiwa katika Makumbusho ya Urithi Geopark walipata fursa ya kuelezewa kuhusu uthibitisho wa wasomi unaoeleza wazi historia ya chimbuko la binadamu wa kale aliyepatikana katika bonde la olduvai takribani milioni 2 iliyopita na ushahidi wa Nyanyo za binadamu wa kale katika eneo la Laetoli takribani miaka 3.6 iliyopiTa ambapo binadamu hao walitembea kwa miguu miwili.
Taasisi zinazoshiriki maadhimisho hayo ambazo zinasimamia maeneo ya urithi wa dunia ni pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Mamlaka ya Uzimamizi wa Wanyamapori (TAWA), Wakala wa Huduma za misitu Tanzania (TFS), pamoja na wawakilishi wa maeneo ya urithi wa dunia kutoka Zanzibar.
Mheshimiwa Ruto atapokelewa kwa gwaride la heshima na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Dar es Salaam ambapo pia watafanya mazungumzo ya uwili ili kuimarisha uhusiano wa Tanzania na Kenya.
Mapema kesho, Mei 5, 2026, Mheshimiwa Ruto atalihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma kabla ya kuhitimisha ziara yake.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uturuki zimesaini Mikataba miwili ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), hatua inayotarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.
Akizungumza katika hafla ya utiaji Saini wa Mkataba huo iliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema kuwa mkataba huo ni wa Kumi na Tatu (13) kwa Tanzania na mataifa mbalimbali na unalenga kuongeza imani kwa wawekezaji kwa kuondoa hatari ya mapato kutozwa kodi mara mbili katika nchi mbili tofauti.
Mhe. Balozi Omar alisisitiza kuwa, mikataba ya aina hiyo inapounganishwa na mikataba ya kulinda uwekezaji (BITs), huwa kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi kupitia kuimarisha mtiririko wa uwekezaji na biashara.
“Tafiti zinaonesha nchi zenye mikataba madhubuti ya kodi mara mbili huvutia uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (Foreign Direct Investment-FDI) kwa kiwango kikubwa zaidi, hali inayoiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kuvutia mitaji kutoka Uturuki na mataifa mengine” alisema Mhe. Balozi Omar.
Aidha Mhe. Balozi Omar alibainisha kuwa, licha ya Tanzania na Uturuki kuwa na mkataba wa kulinda uwekezaji tangu mwaka 2011, kukosekana kwa Mkataba wa Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili, kulikuwa pengo ambalo sasa limezibwa na hatua hiyo inatoa ujumbe wa wazi kwa wawekezaji wa Uturuki kuwa Tanzania iko tayari kupokea na kuendeleza biashara.
Aliongeza kuwa, uhusiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili umeendelea kukua hasa kufuatia ziara ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Uturuki mwaka 2024, ambapo biashara kati ya nchi hizo ilifikia dola za Marekani milioni 281.68, huku Uturuki ikisafirisha bidhaa nyingi zaidi ikilinganishwa na Tanzania.
“Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara kupitia mageuzi mbalimbali ikiwemo kurahisisha usajili wa biashara, kidijitali mifumo ya kodi na forodha, pamoja na maboresho ya sheria za ardhi, ajira na utatuzi wa migogoro ya kibiashara na juhudi hizi zimeanza kuzaa matunda, huku Tanzania ikitajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa kuvutia uwekezaji katika Ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara” alisema Mhe. Balozi Omar
Kwa Upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Said Shaib Mussa, alisema Tanzania na Uturuki zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu na wenye tija tangu kuanzishwa rasmi kwa mahusiano ya kidiplomasia mwaka 1963 na kwa miongo kadhaa, ushirikiano huo umeendelea kupanuka na kugusa sekta mbalimbali muhimu ikiwemo biashara, uwekezaji, elimu, afya, usafirishaji, ulinzi pamoja na maendeleo ya kijamii.
Mhe. Balozi Mussa alisema utiaji wa Saini wa Mikataba hiyo ni hatua muhimu ya kutekeleza kwa vitendo makubaliano ya ushirikiano wa pande mbili yaliyosainiwa mwaka 2025, kufuatia ziara ya kihistoria ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Uturuki mwaka 2024.
“Lengo kuu ni kubadilisha makubaliano ya kisiasa kuwa matokeo halisi kwa kuweka mkakati wa pamoja wa biashara na uwekezaji wenye thamani ya dola bilioni moja, na baada ya utiaji Saini utafuata mkutano wa Tume ya Pamoja ambao unatoa fursa ya kupitia utekelezaji, kubaini maeneo mapya ya kipaumbele na kuimarisha ushirikiano katika sekta za kimkakati kama viwanda, kilimo, utalii, nishati na maendeleo ya rasilimali watu” Alisema Mhe. Balozi Mussa
Kwa upande wake, Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Dkt. Bekir Gezer,amesema kuwa Mikataba hiyo itasaidia kuimarisha zaidi ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.
Tukio hilo lilihudhuriwa pia na Naibu Makatibu Wakuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya na Kaimu Naibu Katibu Mkuu, Bw. Rished Bade pamoja na Wakuu wa Idara na Wataalam wengine kutoka Wizara ya Fedha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kutoka Uturuki.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, wakisaini Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, wakibadilishana Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), baada ya kusaini mikataba hiyo katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kulia) na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, wakionesha Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), baada ya kusaini mikataba hiyo katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akimkabidhi zawadi ya picha yenye vielelezo vya utalii wa Tanzania, Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, baada ya kusaini Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kulia) akimkabidhi Zawadi ya baadhi ya bidhaa za kilimo zinazozalishwa nchini, Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, baada ya kusaini Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akihutubia baada ya hafla ya kusaini Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA) Kati ya Tanzania na Uturuki, katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo amesema Mikataba hiyo inalenga kuongeza imani kwa wawekezaji kwa kuondoa hatari ya mapato kutozwa kodi mara mbili katika nchi mbili tofauti hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, akizungumza baada ya hafla ya kusaini Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA) Kati ya Tanzania na Uturuki, katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer (walioketi), wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali ya Tanzania kutoka Wizara ya Fedha, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Serikali ya Uturuki, baada ya hafla ya utiaji saini Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Mei 4, 2026, amesema CCM inaamini njia sahihi ni maridhiano na inalenga kuhakikisha Taifa linakuwa moja, pia amesisitiza umuhimu wa kuundwa kwa Tume ya upelelezi ili kubaini waliohusika na kuwawajibisha kuhusu matukio hayo.
Amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuunda tume hiyo pamoja na Mwenyekiti wa Tume, Jaji Othman Chande, kwa kufanikisha uchunguzi huo.
Akizungumzia suala la Katiba mpya, amesema ni ajenda ya CCM kupitia ilani yake ya mwaka 2025–2030 na inapaswa kupatikana, ameeleza kuwa tangu miaka ya 1980, CCM imekuwa ikifanya mageuzi ya mara kwa mara ya maboresho ya sheria ili kuendana na mahitaji ya jamii.
Amesisitiza kuwa Katiba si mali ya chama chochote cha siasa bali ni mali ya wananchi na inabeba masuala mengi sio ya ajenda ya uchaguzi pekee.
Ametoa wito kwa makundi yote ya jamii kushiriki katika maridhiano, akieleza kuwa taifa haliwezi kujengwa kwa kutumia nguvu na kwamba mageuzi ya kweli yanahitaji majadiliano yenye nia njema na kufuata misingi yake.
Amewataka Watanzania kuepuka vurugu na badala yake kujadili na kufikia mwafaka, amewakumbusha vijana, hasa wasomi, kutojihusisha na vitendo vya fujo na kuzingatia umuhimu wa elimu.
Ameongeza kuwa wanaochochea vurugu mara nyingi si vijana, na endapo uharibifu wa miundombinu kama ya elimu utatokea, waathirika wakubwa watakuwa ni vijana wenyewe, hivyo amesisitiza umuhimu wa kupima hoja kwa makini na kudumisha amani ya nchi.
▪️︎ Asema mapambano dhidi ya uhalifu yanahitaji mshikamano wa kimataifa
▪️︎ Aeleza teknolojia ni nyenzo muhimu katika kukabiliana na uhalifu wa kisasa
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema ushirikiano wa kikanda na kimataifa ni sharti la mafanikio katika mapambano dhidi ya uhalifu wa kimataifa unaozidi kubadilika na kuvuka mipaka.
Amesema kuwa katika dunia ya sasa, aina nyingi za uhalifu hupangwa, hufadhiliwa na kuratibiwa kwa njia za kidijitali, hali inayohitaji mifumo imara ya kiteknolojia pamoja na ushirikiano wa pamoja ili kuudhibiti kwa ufanisi.
Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, Mei 4, 2026, wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa 11 na Kongamano la Chama cha Waendesha Mashtaka Afrika Mashariki (EAAP), unaofanyika katika Ukumbi wa Blue Sapphire, jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 4 hadi 6 Mei, 2026, wenye kaulimbiu isemayo “Matumizi ya Teknolojia katika Kukabiliana na Uhalifu Dhidi ya Wanyamapori na Uhalifu wa Kimataifa Uliopangwa.”
“Kama ambavyo uhalifu uliopangwa hauwezi kuwepo bila kuvuka mipaka, vivyo hivyo vyombo vya dola na mifumo ya haki ya jinai haviwezi kukabiliana nao kwa ufanisi bila kuwa na mifumo madhubuti ya ushirikiano wa kimataifa, hususan katika maeneo ya msaada wa kisheria na urejeshaji wa watuhumiwa,” alisema.
Akifafanua zaidi kuhusu mwelekeo wa uhalifu wa kisasa, Waziri Mkuu alisema:
“Utafiti unaonesha kuwa katika hali nyingi, uhalifu dhidi ya wanyamapori na uhalifu wa kimataifa hupangwa kidijitali, hufadhiliwa kwa njia za kielektroniki na kuratibiwa kuvuka mipaka, na pia hufichwa kwa kutumia mbinu tata za kiteknolojia, hali inayofanya mipango na athari zake kuvuka mipaka kwa kasi kubwa ambayo wakati mwingine hupita bila kugundulika.”
Alisisitiza kuwa matumizi ya teknolojia ni sehemu muhimu ya mafanikio katika mapambano hayo.
“Katika mazingira haya, hatuwezi kufanikiwa katika mapambano dhidi ya uhalifu wa kimataifa uliopangwa bila kutumia kikamilifu teknolojia kama nyenzo muhimu katika kukabiliana na changamoto hii ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki na duniani kwa ujumla,” alisema.
Akizungumzia athari za uhalifu huo, Waziri Mkuu alisema ni tishio kwa uchumi na usalama wa mataifa.
“Ni dhahiri kwamba biashara haramu ya wanyamapori na aina nyingine za uhalifu wa kimataifa uliopangwa ni tishio kubwa kwa mataifa yetu; unachangia kupotea kwa rasilimali zetu na pia ni tishio kwa utulivu na usalama wa nchi zetu,” alisema.
Akielezea hatua zilizochukuliwa na Tanzania, Waziri Mkuu alisema Serikali imeendelea kuboresha mifumo ya kisheria ili kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.
“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikipitia na kuboresha sheria zake za msaada wa kisheria ili kupanua wigo wa ushirikiano, ikiwemo matumizi ya ushahidi wa kidijitali, ufuatiliaji wa mawasiliano na mbinu za kisasa za uchunguzi,” alisema.
Aidha, alibainisha kuwa Serikali imeondoa baadhi ya taratibu za urasimu ili kuwezesha utekelezaji wa haraka wa maombi ya msaada wa kisheria kupitia mamlaka husika.
Waziri Mkuu alizitaka nchi wanachama kutumia jukwaa la EAAP kama chombo cha kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kubadilishana taarifa.
“Katika dunia ya sasa ambapo uhalifu hauna mipaka, majibu yetu lazima yawe ya pamoja, ya kimkakati na yenye mshikamano,” alisema.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainabu Katimba, alisema uwepo wa Waziri Mkuu katika mkutano huo unaonesha dhamira ya Serikali ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika mapambano dhidi ya uhalifu.
Alisema kaulimbiu ya mkutano huo ni ya wakati muafaka na inaakisi changamoto za sasa, akiwahimiza washiriki kutumia jukwaa hilo kubadilishana uzoefu na kuimarisha mifumo ya haki katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Naye Rais wa Chama cha Waendesha Mashtaka Afrika Mashariki (EAAP), ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mashtaka wa Jamhuri ya Kenya, Renson Ingonga, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano na matumizi ya teknolojia katika kukabiliana na uhalifu unaobadilika kwa kasi.
Alisema mkutano huo ni fursa ya kujenga mitandao imara ya kitaaluma, kuimarisha uaminifu na kukuza mifumo ya ushirikiano itakayowezesha kukabiliana ipasavyo na uhalifu wa kimataifa uliopangwa.
Mkutano huo wa kimataifa unawakutanisha Wakurugenzi wa Mashtaka, Mawakili Wakuu wa Serikali, viongozi wa vyombo vya sheria pamoja na wadau kutoka mashirika ya kikanda na kimataifa kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na mifumo ya haki jinai katika kukabiliana na uhalifu wa kuvuka mipaka.
Chama cha Waendesha Mashtaka Afrika Mashariki (EAAP) kinaundwa na nchi wanachama ambazo ni Tanzania, Burundi, Ethiopia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Kenya, Msumbiji, Rwanda, Seychelles, Sudan Kusini, Somalia, Malawi, Sudan, Zambia na Uganda.
Akihitimisha, Waziri Mkuu aliwataka washiriki kuhakikisha mkutano huo unazaa matokeo yenye tija kwa ukanda wa Afrika Mashariki.
“Kwa maneno hayo machache, natangaza rasmi kufunguliwa kwa Mkutano Mkuu wa 11 na Kongamano la Chama cha Waendesha Mashtaka Afrika Mashariki,” alisema.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
SERIKALI imeanza kuvuna matokeo ya mageuzi ya kidijitali katika sekta ya habari baada ya Waandishi wa Habari 3,357 kuthibitishwa na kupatiwa ithibati ndani ya kipindi cha chini ya mwaka mmoja kupitia mfumo wa kisasa wa TAI HABARI.
Mafanikio hayo ni hatua kubwa katika kuimarisha weledi, uwajibikaji na usimamizi wa taaluma ya uandishi wa habari nchini, kwa kuwa kwa mara ya kwanza sekta hiyo imeanza kuwa na mfumo rasmi, wa kidijitali na unaowezesha kuchakata maombi na kuhakiki waandishi wanaokidhi vigezo kwa mujibu wa sheria ya Huduma za Habari.
Akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa wizara hiyo, Mhe. Paul Christian Makonda, alisema kuanzia Julai 2025 hadi Aprili 2026, Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imepokea na kushughulikia jumla ya maombi 4,139 ya usajili kupitia mfumo huo wa TAI HABARI.
Kati ya maombi hayo, Waandishi wa Habari 3,357 waliokidhi vigezo vilivyoainishwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, wamepatiwa ithibati.
Katika hatua nyingine, Waziri Makonda alisema JAB imeshughulikia malalamiko 14 ya uvunjifu wa maadili ya taaluma ya habari, jambo linaloonesha kuanza kuimarika kwa mfumo wa uwajibikaji katika sekta hiyo.
Aidha, Mheshimiwa Makonda alisema Serikali kupitia JAB imeandaa mwongozo maalumu wa kisheria utakaowawezesha Waandishi wa Habari wakongwe walioathiriwa na mfumo wa ithibati kureiea katika mfumo rasmi, kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 ambayo ilitungwa kwa ajili ya kukuza taaluma ya uandishi wa habari.
Alisema kuwa sheria hiyo ilitungwa kwa ajili ya kukuza taaluma ya uandishi wa habari kwa kuweka mfumo wa kitaasis utakaosimamia sekta ya habari.
“Mwongozo huu unaweka utaratibu wa kisheria wa kutambua na kuthibitisha umahiri wao kupitia tathmini maalumu ya uzoefu, weledi na maadili ya taaluma, na kuwawezesha kupata ithibati kwa mujibu wa sheria.” Alisema Mhe. Makonda
Hatua hii inalenga kulinda taaluma ya uandishi wa habari kwa kuhakikisha hata waandishi wa habari wenye uzoefu mkubwa wanapata nafasi ya kuingia katika mfumo rasmi unaotambuliwa kisheria.






.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.png)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)