Wahitimu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakiwa kwenye maadamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo yaliyofanyika katika hoteli ya APC Bunju, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akipokea maadamano ya kitaaluma pamoja na viongozi wa Bodi pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akizungumza kuhusu namna Bodi hiyo ilivyofanikisha kuongeza idadi ya wahitimu kwa mwaka huu wakati wa mahafali ya 48 ya NBAA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Pius A. Maneno akisoma hotuba yake kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi chake cha uongoziwake wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Baadhi ya Wahitimu pamoja na wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu  kwenye mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wa ngazi ya CPA wakisoma viapo vyao wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akiwatunuku wahitimu kwenye mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wakishangilia mara baada ya kutunukiwa CPA wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA)
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akitoa vyeti kwa wahitimu waliofanya vizuri kwenye mitihani ya Bodi wakati wa mahafali ya 48.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo.
Serikali kupitia Wizara ya Nishati imeeleza kuwa hali ya upatikanaji wa mafuta nchini bado ni shwari, huku bei zikiwa himilivu, ambapo mafuta yaliyopo yanatosheleza kwa kipindi cha miezi miwili hadi mitatu.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, wakati akitoa taarifa ya hali ya upatikanaji wa mafuta nchini pamoja na hatua zinazochukuliwa na Serikali kukabiliana na uhaba wa mafuta duniani uliotokana na vita inayoendelea katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Dkt. Mataragio amesema:

“Mafuta yaliyopo nchini kwenye matenki, Petrol tuna lita 95,256,342; mafuta ya petrol yaliyowasili nchini ni lita 1,466,337; mafuta yaliyopo njiani kwenye meli ni lita 138,737,332. Hivyo, jumla ya mafuta ya Petrol yatakayokuwepo ni lita 380,677,011, na yanatosha kwa matumizi ya siku 61.”

Ameongeza kuwa kuna mikataba ya mafuta iliyoingiwa na mzabuni yenye jumla ya lita 183,500,450 ambayo yatafika nchini mwezi wa nne, hivyo jumla ya mafuta ya Petrol yaliyopo kwenye matenki, yatakayowasili nchini kwa meli pamoja na yaliyopo kwenye mikataba ni lita 563,682,461, kiasi ambacho kinatosheleza kwa siku 91.

Kwa upande wa mafuta ya Diesel, amesema mafuta yaliyopo kwenye matenki ni lita 55,744,397; yaliyowasili nchini ni lita 122,893,285; na yaliyopo njiani kwenye meli ni lita 184,662,480. Hivyo, jumla ya mafuta ya Diesel ni lita 362,433,845, yanayotosha kwa matumizi ya siku 44.

Amefafanua kuwa mafuta ya Diesel yaliyopo kwenye mikataba na wabuni ni lita 167,321,343. Kwa ujumla, mafuta yaliyopo nchini, yanayokuja kwa meli na yaliyopo kwenye mikataba ni lita 530,621,505, kiasi kitakachotosheleza kwa siku 64.

Kwa upande wa mafuta ya ndege, Dkt. Mataragio amesema yapo ya kutosha ambapo yaliyopo kwenye matenki ni lita 35,241,028 na yaliyopo kwenye mikataba ni lita 23,779,725. Jumla yake ni lita 59,020,753, zitakazotosheleza kwa siku 97.

Ameeleza kuwa kutokana na hali ya vita kuendelea, kunatarajiwa ongezeko la bei za mafuta kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.


Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

CRDB Bank kupitia Kitengo chake cha Manunuzi (Procurement) imetembelea Makao ya Taifa ya Kulelea Watoto yaliyopo Kikombo, Ihumwa jijini Dodoma, na kutoa msaada wa mahitaji muhimu kwa watoto wanaolelewa katika kituo hicho, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kuimarisha ustawi wa jamii.

Akizungumza mara baada ya kuwasili katika kituo hicho, Mkuu wa Manunuzi – Mikataba, Udhibiti na Uzingatiaji wa CRDB Bank, Victor Mukami, amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea hali halisi ya maisha ya watoto hao, kujifunza pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili.

Ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa benki hiyo wa kuhakikisha inabaki kuwa karibu na jamii, wadau wake pamoja na makundi yenye uhitaji, kupitia utekelezaji wa sera ya kurejesha kwa jamii (Corporate Social Responsibility – CSR).

“Tumekuja hapa Kikombo kuona kwa karibu hali halisi ya kituo hiki katika ngazi ya kitaifa, kujifunza na kubadilishana mawazo. Hii si mara ya mwisho, tutaendelea kutembelea vituo mbalimbali nchini,” amesema Mukami.

Aidha, Mukami ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia vituo vya kulelea watoto, akisisitiza kuwa bado kuna mahitaji makubwa yanayohitaji ushirikiano wa pamoja kutoka kwa jamii.

Pia amewasihi wazazi na walezi kuendelea kuwaonesha watoto upendo na malezi bora, akibainisha kuwa upendo una mchango mkubwa katika ukuaji wao wa kiakili na kisaikolojia.

Kwa upande wake, Meneja wa Makao hayo, Darius Karijongo, ameishukuru CRDB Bank kwa msaada huo, akisema kuwa ujio wao umeleta faraja kubwa kwa watoto pamoja na uongozi wa kituo hicho.

“Tunawashukuru sana CRDB Bank kwa kujitokeza kutuunga mkono. Hawa watoto wanahitaji upendo ambao hawakupata kutoka kwa familia zao za karibu. Sisi sote ni familia yao sasa,” amesema Karijongo.

Ameongeza kuwa msaada uliotolewa una thamani kubwa kwa maendeleo ya kituo hicho, na kuahidi kuwa utatumika ipasavyo kwa manufaa ya watoto hao.

“Leo mmetuonesha kuwa ninyi ni ndugu zetu wa karibu. Tunawashukuru sana kwa zawadi mlizotupatia, Mungu awabariki,” ameongeza.

Ziara hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya CRDB Bank katika kuendelea kugusa maisha ya Watanzania na kuchangia maendeleo ya jamii kwa ujumla.





 


Top News