Dar es Salaam, Juni 17, 2026 – Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), imewahimiza waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini kuendelea kuwasilisha kazi zao za kuwania Tuzo za Samia Kalamu 2026 kabla ya kufungwa kwa dirisha la maombi mwishoni mwa mwezi huu.

Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa hadi Juni 15, 2026, jumla ya kazi 624 zilikuwa zimewasilishwa kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, huku vyombo vya habari mtandaoni vikiongoza kwa idadi kubwa ya kazi zilizowasilishwa.

Takwimu zinaonyesha kuwa vyombo vya habari mtandaoni vimewasilisha kazi 276, sawa na asilimia 44 ya kazi zote zilizopokelewa. Magazeti yamewasilisha kazi 178 (asilimia 29), televisheni kazi 102 (asilimia 16), redio kazi 60 (asilimia 10), huku majarida yakichangia kazi nane pekee, sawa na asilimia moja ya jumla ya mawasilisho.

Waandaaji wa tuzo hizo wameeleza kuwa Samia Kalamu Awards zinalenga kuhamasisha ubora, weledi na uwajibikaji katika uandishi wa habari za maendeleo, kwa kutambua mchango wa wanahabari katika kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu masuala ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kazi zinazostahili kushindanishwa ni zile zilizochapishwa au kurushwa katika vyombo vya habari kati ya Julai 1, 2025 na Juni 30, 2026.

Aidha, waandishi na taasisi za habari zimekumbushwa kuwa dirisha la kuwasilisha kazi litafungwa rasmi Juni 30, 2026 saa 5:59 usiku, hivyo zinapaswa kutumia muda uliobaki kuhakikisha kazi zao zinawasilishwa kwa wakati kupitia tovuti rasmi ya tuzo hizo.

Tuzo za Samia Kalamu zilianzishwa mwaka 2025 na zimekuwa jukwaa muhimu la kutambua na kuenzi mchango wa waandishi wa habari katika kuendeleza taifa kupitia kaulimbiu ya “Kalamu kwa Maendeleo.”

Kwa mujibu wa waandaaji, waandishi na vyombo vya habari vinakaribishwa kuendelea kushiriki ili kuhamasisha uandishi wenye tija kwa maendeleo ya Tanzania.
 By Muhidin Issa Michuzi


IMAGINE a vibrant hub teeming with life, that is the essence of Mnazi Mmoja Garden, once the cornerstone of community life in Dar es Salaam, a place where gatherings flourished, nurturing camaraderie and social interaction.

Just take a stroll through the garden one day, and it will unveil to you its historical weight: monuments and statues narrating Tanzania’s struggle for independence, and the ground where national heroes held crucial political rallies. 

It will be a living history lesson, that is, if you are lucky enough to be allowed in.

Mnazi Mmoja Garden hosted the inaugural gathering of TANU, forerunner of the ruling CCM, in 1954, a meeting that helped fuel the fight for statehood. In 1961, the Uhuru Torch was first ignited here, symbolising the struggle for freedom. From 1969, the garden hosted Mashujaa Day, honouring national heroes each July 25th, until the ceremony moved to Dodoma in 2016. 


The Arusha Declaration, too, was launched from this spot in 1967, charting Tanzania’s path toward socialism and self-reliance.

But ask the people who grew up around its gates, and the garden’s story takes a more intimate turn, one of swings rusted into silence, ponds gone dry, and gates that no longer open for the public they were built to serve.

Shaaban Scotto, a Kariakoo businessman who came of age in the 1960s and 70s, remembers a Mnazi Mmoja that doubled as a child’s entire world. Afternoons spent on its swings, free to wander without a single locked gate in sight. It is a freedom, he says, that today’s children in the neighbourhood will never know.

For Omary Popat, a TAZARA train driver born and raised in Kariakoo, the puzzle is more procedural than nostalgic. He cannot understand why the entire southern section of the garden remains under lock and key year-round, sealed off from a community living within walking distance of it. A public garden the public cannot enter, he says, is a contradiction nobody in authority has bothered to explain.

Yussuf Issa, known around Kariakoo as “Jesse,” built a different relationship with the garden, one of music and light. As a younger man, he made a habit of photographing the fishpond, drawn back by its stillness, and rarely missed a concert held on its grounds. For him, Mnazi Mmoja was a living cultural venue, and its slow closure has meant the quiet disappearance of a stage that once brought the city together.

Siwazuri Kibwana, born and bred in Kariakoo, takes the most practical view. If littering and vandalism are the real concern, he asks, why not simply post mgambo (city militia) to guard the grounds, rather than locking the public out altogether? It is, in her telling, a problem of enforcement, not access.





Beyond its serene façade, the garden holds the secrets of a bygone era when it served as a symbolic demarcation line during colonial rule, separating Indian inhabitants to the east from Africans and Arabs to the west, and as a clandestine meeting ground for freedom-seeking forefathers. Under colonial laws banning political assemblies, those forefathers turned to traditional dances as cover for secret meetings, strategising for the future while escaping the watchful eye of the authorities. The famous drummer statue standing amid the garden’s fishpond endures as a symbol of that resilience and unity.

And yet, as Scotto, Popat, Jesse, and Kibwana all attest in their own way, the garden’s significance has been allowed to recede into the past tense.

Start with the Uhuru Torch Monument at the centre of the park, on the spot where, legend holds, a single coconut tree once stood, giving the garden its Swahili name, Mnazi Mmoja, “one coconut tree.” This monument, later the venue for National Heroes Day, is today inaccessible to the very public it was built to inspire. Even after the ceremonies moved to Dodoma, the entire middle and southern end of the garden remains off-limits, gates closed every day, leaving residents like Popat with more questions than answers.

The garden’s significance extends beyond politics. In 1952, Greek entrepreneur George Anautoglou established the Anautoglou Hall, an entertainment complex that heightened its cultural standing, the very kind of cultural life that drew a young Jesse to its concerts decades later. That hall is now the seat of the Ilala District Council. Nearby stands the Amtulabhai Clinic, commissioned by the Karimjee family, alongside the Mnazi Mmoja dispensary, now elevated to hospital status, together a quiet legacy of public service.


A stone’s throw from the dispensary’s gates sits a police post that, while helping maintain order, has inadvertently contributed to neglect of the nearby Independence Stream. The monument there, adorned with the national coat of arms, once delighted visitors with a hissing jet of water for every coin tossed into its pond, perhaps the very pond that once drew Jesse’s camera. Today, it too is a no-go area.

The disparity runs deeper still. A significant portion of the park’s northern end, once a verdant oasis, has been repurposed for celebratory gatherings, becoming a cacophony of exhibition booths and tents that trample the foliage. A VIP stand was even built facing east, leaving dignitaries to bear the full glare of the sun, a puzzling choice next to the well-placed stand on the southern side.

This speaks to Kibwana’s point: the issue may be less about whether the garden should be open, and more about how it is managed when it is.

As the garden grapples with these complexities, it stands as a microcosm of challenges facing public spaces nationwide, where history and modernity often find themselves at odds. For Scotto, Popat, Jesse, and Kibwana, that tension is not abstract; it is the swing once played on, the locked gate passed daily, the concert no longer attended, the simple question of why guards could not solve what a fence has not.

A comprehensive strategy is imperative to genuinely honour the garden’s heritage and unlock its potential, one that prioritises accessibility, sustainability, and a return to its original purpose.

Dear city fathers, are you reading this?


 

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.

Na. OWM (KAM), Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema mahusiano mema, mazungumzo ya kujenga na mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu katika kuimarisha demokrasia, amani na maendeleo endelevu nchini.

Akifungua Warsha ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Juni 17, 2026, mjini Morogoro, Waziri Sangu alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote wa kisiasa kwa kuzingatia misingi ya kuheshimiana, ushirikishwaji na kutanguliza maslahi ya Taifa.

Alisema viongozi wa vyama vya siasa wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha mazungumzo yenye kujenga, kudumisha amani na kuimarisha mshikamano wa kitaifa badala ya kuhimiza migogoro.

“Mahusiano mema ndiyo msingi wa amani, umoja na maendeleo ya Taifa. Tunaposhirikiana kwa heshima na maelewano bila kujali tofauti zetu za kiitikadi, tunajenga Taifa imara lenye mshikamano,” alisema Waziri Sangu.

Aidha, aliwataka viongozi hao kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 itakayoanza kutekelezwa Julai Mosi, 2026, akieleza kuwa mafanikio ya dira hiyo yanategemea ushirikiano wa wadau wote wa maendeleo bila kujali tofauti za kisiasa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini, Juma Ali Khatibu alisema uwepo wa vyama vya siasa unatoa mchango mkubwa katika kuimarisha mahusiano na mshikamano ndani ya jamii.

Pia alimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Dkt. Eveline Munisi wa Chama cha NCCR-Mageuzi kuwa Mbunge na Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, akisema hatua hiyo ni ishara ya kuendelea kuimarika kwa ushirikiano na maridhiano ya kisiasa nchini.

Naye Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mstaafu Francis Mtungi, alisema warsha hiyo ilitokana na uamuzi wa Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika Mei 21, 2026, ambapo ilikubaliwa Ofisi ya Waziri Mkuu iandae mada kuhusu jukumu jipya la mahusiano kwa lengo la kujenga uelewa miongoni mwa wadau wa kisiasa.

Katika Warsha kuhusu Dhana ya Mahusiano na Ushirikishwaji, Mkurugenzi wa Idara ya Mahusiano, Bw. Rasheed Maftah, aliwasilisha mada kuhusu dhana ya mahusiano, wadau wake muhimu, misingi yake pamoja na nafasi na majukumu ya viongozi wa siasa katika kuimarisha mahusiano mema na mshikamano ndani ya jamii.

Aidha, Bw. Maftah alieleza majukumu ya Idara ya Mahusiano katika kutekeleza jukumu jipya la Ofisi ya Waziri Mkuu la kuratibu mahusiano kati ya Serikali na makundi mbalimbali ya kijamii, kwa lengo la kuimarisha ushirikishwaji, maelewano na ushirikiano katika maendeleo ya Taifa.

Warsha hiyo imewakutanisha viongozi wa vyama vya siasa 18 kati ya 19 vyenye usajili kamili kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kuendelea kuimarisha mahusiano, mazungumzo na ushirikiano kati ya vyama vya siasa kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na maendeleo ya Taifa.

Vyama vya Siasa vilivyoshiriki ni CCM, CUF,UMD, NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP, NRA,ADA TADEA, TLP,UDP,MAKINI, SAU,AAFP, CCK, ADC,CHAUMA na ACT Wazalendo.





 

Chuo cha Ustawi wa Jamii kimewahamasisha wananchi kutumia huduma za ushauri na msaada wa kisaikolojia zinazotolewa na taasisi hiyo, huku kikisisitiza umuhimu wa afya ya akili na malezi bora ya watoto katika kujenga jamii yenye maendeleo endelevu.

Akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma Juni 17,2026, Mratibu wa Kituo cha Elimu na Msaada wa Kisaikolojia cha Chuo cha Ustawi wa Jamii, Rufina Ume, amesema kituo hicho kinatoa elimu, ushauri na msaada wa kisaikolojia kwa wanafunzi, watumishi na wananchi kwa ujumla.

Amesema huduma zinazotolewa zinahusisha ushauri wa mahusiano na ndoa, utatuzi wa migogoro, changamoto mbalimbali za kisaikolojia, elimu ya uraibu pamoja na marekebisho ya tabia.

“Kituo hiki pia kinatoa huduma za kuwafuata wananchi majumbani na katika maeneo yao ya kazi kwa wale wenye changamoto zinazowazuia kufika kituoni. Tunawahudumia pia watumishi wa sekta binafsi na umma kulingana na mahitaji yao.”

Ume amesema kituo hicho kilianzishwa rasmi mwaka 2007 ndani ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii iliyo chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, kwa lengo la kutoa elimu na msaada wa kisaikolojia kwa wanafunzi na watumishi kabla ya kupanua huduma hizo kwa jamii nzima.

Ameeleza kuwa kwa sasa taasisi hiyo imekuwa ikiwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali ikiwemo maeneo yenye majanga kwa lengo la kuongeza uelewa wa masuala ya afya ya akili na kusaidia kujenga jamii yenye utulivu wa akili na uwezo wa kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi.

Aidha, amesema ushiriki wao katika Wiki ya Utumishi wa Umma unalenga kutoa elimu kwa wananchi na kuwawezesha kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu ustawi wa jamii, afya ya akili na huduma zinazotolewa na chuo hicho.

Kwa upande wake, Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Kampasi ya Kisangara, Desderio Wambura Fortunatus, amesema chuo hicho kimejikita katika kuandaa wataalamu watakaosaidia kujenga kizazi chenye maadili, afya bora ya akili na misingi imara ya maendeleo kuanzia utotoni.

Amesema mafanikio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 yanategemea uwekezaji kwa watu kuanzia katika hatua za awali za ukuaji wao, jambo linalohitaji wataalamu wenye uwezo wa kusaidia familia na jamii katika malezi sahihi ya watoto.







Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,akitoa taarifa kwa umma kuelekea kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake Juni 19,2026 jijini Dodoma.

...

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) linatarajia kuandika historia mpya Juni 19, 2026 kwa kuhitimisha maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitarajia kuzindua kitabu maalumu kitakachobeba historia, mafanikio na mchango wake katika maendeleo ya viwanda, biashara na ustawi wa Watanzania.

Akizungumza jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya kilele cha maadhimisho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema hafla hiyo itafanyika katika ofisi za shirika hilo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi.

Dkt. Katunzi amesema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga (Mb), ambaye ataungana na viongozi, wadau na wananchi kusherehekea mafanikio ya nusu karne ya taasisi hiyo muhimu nchini.

Amesema sambamba na sherehe hizo, TBS itazindua kitabu maalumu cha miaka 50 kitakachoelezea safari ya shirika hilo tangu kuanzishwa kwake, hatua mbalimbali za maendeleo iliyopitia pamoja na mchango wake katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotolewa nchini zinazingatia viwango vinavyotakiwa.

“Kitabu hiki kitakuwa sehemu ya kumbukumbu muhimu ya taifa. Kitaelezea historia ya TBS, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 na kitakuwa rejea kwa vizazi vya sasa na vijavyo ili kuelewa mchango wa shirika katika maendeleo ya nchi,” amesema Dkt. Katunzi.

Ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 50, TBS imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda afya na usalama wa watumiaji wa bidhaa mbalimbali, huku ikichochea ukuaji wa viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinakuwa bora na zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Dkt. Katunzi, mafanikio yaliyofikiwa na TBS katika kipindi hicho si ya shirika pekee bali ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati ya taasisi hiyo, wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

“Miaka 50 ya TBS ni mafanikio ya wadau wetu na jamii kwa ujumla. Tunawakaribisha wananchi na wadau wote kushiriki katika kilele cha maadhimisho haya ili kwa pamoja tuadhimishe safari hii ya mafanikio,” amesema.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuwa fursa ya kutafakari mchango wa TBS katika maendeleo ya taifa, huku yakitoa mwanga wa matarajio na mwelekeo wa shirika hilo katika kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa na huduma kwa manufaa ya Watanzania na uchumi wa nchi.

Na Janeth Raphael MichuziTv 

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amesema Serikali itaendelea kutoa motisha kwa watumishi wa umma kupitia upandishaji wa vyeo kwa wale wenye sifa na wanaokidhi vigezo vilivyowekwa, huku akisisitiza umuhimu wa nidhamu ya kazi, uzalendo na uwajibikaji katika kulitumikia taifa.

Kikwete ameyazungumza hayo leo jijini Dodoma wakati akifungua wiki ya utumishi wa uma mkoani humo ambapo amesema 

kuhusu maendeleo ya Utumishi wa Umma, Serikali inaamini kuwa watumishi ndiyo nguzo muhimu ya maendeleo ya nchi, hivyo kuendelea kuwawezesha kutachangia kuongeza ufanisi wa utoaji huduma na kuchochea maendeleo ya taifa kwa ujumla.

“Tunapowajengea uwezo na kuwapa motisha watumishi wa umma, tunakuwa si tu tumewawezesha wao binafsi, bali pia tumekomboa taifa kupitia huduma bora kwa wananchi,” alisema.

Aidha, amewataka watumishi kuendelea kutumia mifumo ya kisasa ya utendaji kazi iliyowekwa katika Utumishi wa Umma ili kuhakikisha kunakuwa na utendaji wenye tija, uwajibikaji na matokeo chanya kwa taasisi, sekta mbalimbali na taifa kwa ujumla.

Ameeleza kuwa kwa sasa mifumo hiyo imeunganishwa na taratibu za upandishaji vyeo pamoja na kuthibitishwa kazini, hatua inayolenga kuongeza uwazi na ufanisi katika usimamizi wa rasilimali watu serikalini.

Waziri huyo pia ametoa maelekezo kwa watumishi wote wa umma kutekeleza majukumu yao kwa uwazi, uaminifu, weledi na ufanisi ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima kutoka kwa wananchi na kuongeza imani kwa Serikali.

“Ninapenda kusisitiza kuwa wafanyakazi wetu ndiyo msingi wa maendeleo yetu. Mkitekeleza wajibu wenu kwa uadilifu na kujituma, mafanikio makubwa na maendeleo tunayoyatarajia kama Watanzania yatafikiwa,” alisema.

Katika hatua nyingine, Ridhiwani amesema Serikali imekamilisha zoezi la kuhuisha miundombinu ya maendeleo ya kada mbalimbali za Utumishi wa Umma zilizo chini ya wizara na taasisi zake. Maboresho hayo yamehusisha kuingizwa kwa fani mpya zinazozalishwa na vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu ambazo awali hazikuwa zimejumuishwa katika mifumo hiyo.

Amebainisha kuwa maboresho hayo yamegusa kada zote muhimu, ikiwemo sekta za afya, elimu, sheria, uhandisi, kilimo, mifugo, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), nishati pamoja na maeneo mengine muhimu ya maendeleo.

Hatua hiyo, kwa mujibu wa Waziri, inalenga kuifanya Serikali kuwa na mfumo wa Utumishi wa Umma unaokwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia, mahitaji ya soko la ajira na vipaumbele vya maendeleo ya taifa.





TAKUKURU Mkoa wa Geita imefikisha mahakamani watumishi 9 wa umma kwa tuhuma za kutumia vibaya na kuiba fedha za umma kiasi cha shilingi milioni 89,055,107 na senti 50. 

Watumishi hao walikamatwa baada ya uchunguzi wa TAKUKURU kubaini walikuwa wakifanya vitendo vya rushwa na ubadhirifu. Kati yao watumishi 3 wa Manispaa ya Geita walikuwa wakikusanya mapato ya Serikali kupitia mfumo wa LGRCS lakini walikwepa kutoa stakabadhi na kutumia mashine za POS. Pesa zote zilizokusanywa hazikufika Serikalini na jumla ya shilingi milioni 48,067,500 ilipotea.

Wengine 4 ni watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Geita ambao walirudishia fedha za Mahakama Kuu Masjala Ndogo Geita kisha wakazitaka tena kwa njia ya rushwa kupitia simu na miamala ya benki. Kiasi kilichotumika vibaya hapo ni shilingi milioni 41,987,607 na senti 50.

Watumishi wengine 2 kutoka Idara ya Utafit iwa Madawa Mwanza na Hospitali ya Rufaa Bugando pia walishirikiana nao. Baada ya kukamilisha uchunguzi na kupata vibili kutosha, washtakiwa wote wamefunguliwa mashtaka 4 mahakamani tarehe 17 Juni 2026 na kesi zao zinasikilizwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Geita.

Mkuu wa TAKUKURU Geita Ndugu Said Lipandaje amesema hatua hiyo inaonyesha Serikali imedhamiria kupambana na rushwa bila woga.




Na Mwandishi Wetu, Morogoro

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Deus Sangu amesema mahusiano mema, mazungumzo ya kujenga na mshikamano wa kitaifa ni nguzo muhimu katika kuimarisha demokrasia, amani na maendeleo endelevu nchini.

Akifungua Warsha ya Viongozi wa Vyama vya Siasa na Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Juni 17, 2026, mjini Morogoro, Waziri Sangu alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote wa kisiasa kwa kuzingatia misingi ya kuheshimiana, ushirikishwaji na kutanguliza maslahi ya Taifa.

Alisema viongozi wa vyama vya siasa wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha mazungumzo yenye kujenga, kudumisha amani na kuimarisha mshikamano wa kitaifa badala ya kuhimiza migogoro.

“Mahusiano mema ndiyo msingi wa amani, umoja na maendeleo ya Taifa. Tunaposhirikiana kwa heshima na maelewano bila kujali tofauti zetu za kiitikadi, tunajenga Taifa imara lenye mshikamano,” alisema Waziri Sangu.

Aidha, aliwataka viongozi hao kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 itakayoanza kutekelezwa Julai Mosi, 2026, akieleza kuwa mafanikio ya dira hiyo yanategemea ushirikiano wa wadau wote wa maendeleo bila kujali tofauti za kisiasa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini, Juma Ali Khatibu alisema uwepo wa vyama vya siasa unatoa mchango mkubwa katika kuimarisha mahusiano na mshikamano ndani ya jamii.

Pia alimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Dkt. Eveline Munisi wa Chama cha NCCR-Mageuzi kuwa Mbunge na Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, akisema hatua hiyo ni ishara ya kuendelea kuimarika kwa ushirikiano na maridhiano ya kisiasa nchini.

Wakati huo huo  Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mstaafu Francis Mtungi, alisema warsha hiyo ilitokana na uamuzi wa Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika Mei 21, 2026, ambapo ilikubaliwa Ofisi ya Waziri Mkuu iandae mada kuhusu jukumu jipya la mahusiano kwa lengo la kujenga uelewa miongoni mwa wadau wa kisiasa.

Katika wa Warsha kuhusu Dhana ya Mahusiano na Ushirikishwaji, Bw.Rasheed Maftah Mkurugenzi wa Idara ya Mahusiano amelezea kuhusu Dhana ya Mahusiano,wadau husika, Misingi yake na majukumu ya Viongozi wa Siasa katika kuimarisha Mahusiano mema katika jamii.

Aidha, alieleza pia kuhusu Majukumu ya Idara ya Mahusiano katika luteleleza jukumu jipya la Ofisi la kuratibu Mahusiano baina ya Serikali na Makundi ya Kijamii.

Warsha hiyo imewakutanisha viongozi wa vyama vya siasa 18 kati ya 19 vyenye usajili kamili kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kuendelea kuimarisha mahusiano, mazungumzo na ushirikiano kati ya vyama vya siasa kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na maendeleo ya Taifa.

Vyama vya Siasa vilivyoshiriki ni CCM, CUF,UMD, NCCR-Mageuzi, NLD, UPDP, NRA,ADA TADEA, TLP,UDP,MAKINI, SAU,AAFP, CCK, ADC,CHAUMA na ACT Wazalendo.




Na Mwandishi Wetu

HALIMASHAURI ya Wilaya ya Kisarawe,Mkoani Pwani imeendelea kung'ara kwa kupata hati safi kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serkali (CAG), kwa kipindi cha miaka minne mfurulizo.

Wilaya hiyo imepata hati safi katika mwaka wa fedha 2021/22 , mwaka wa fedha 22/23, mwaka wa fedha 23/24 na mwaka huu wa fedha wa 24/25.

Akizungumza katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani la halmahauri hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe Abubakar Kunenge, amewapongeza viongozi wa wilaya na halimashauri hiyo kwa uwajabikaji.

Kunenge amesema hati safi hizo ziwe chachu kwa wilaya na halimashauri hiyo kutekeleza mikakati ya maendeleo na kupunguza changamoto za wananchi.

Ameeleza, hati safi ni lazima iakisi maendeleo yaliyopo katika halimashauri hivyo kuwataka viongozi na watendaji kuongeza nguvu katika kubuni vyanzo vya vipya vya mapato,ukusanyaji wa mapato na uwekezaji.

"Hati safi inatokana na ukaguzi wa hesabu za fedha zilivyo tumika kwa usahihi, hivyo Kisarawe ni lazima sasa mjielekeze katika kupanga bajeti ya kutekeleza mirdi ya maendeleo,"amesema Kunenge.

Amesema, Kisarawe inatakiwa kufanya jitihada kubwa za kuinuka kiuchumi kwani ina fursa nyingi zinazo vutia uwekezaji.

"Naomba tu ni wachane, Kisarawe kuna changamoto ya migogoro ya ardhi. Unaleta wawekezaji lakini wanakimbia kwa sababu ya migogoro.Malizeni migogoro yenu," amesema

Amebainisha Kisarawe inafursa za utalii na uchmbaji madini unaoweza kuvuta ujenzi wa viwanda hivyo kuongeza mapato.

"Mjiulize kwanini watu wanachimba madini hapa lakini hawajengi viwanda.Ondoeni migogoro.Madiwani msiogope kueleza wazi kuhusu wavamizi wa ardhi katika maneno yenu,"ameeleza Kunenge.

Mwenyekiti wa Baraza la Halimashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Aidan Kitare, alimhakishia mkuu huyo wa mkoa kuwa Halmashauri hiyo inamikakati kabambe ya kujikwamua kiuchumi, ikiwemo uwekezaji katika ardhi na usimamizi wa vyanzo vya mapato.

Mkaguzi wa Nje kutoka Ofisi ya CAG Mkoa wa Pwani, Faith Mutune, ameipongeza halmashaurihiyo kwa kupata hati safi na kuitaka kufunga hoja nane za ofisi hiyo zilizo salia.

Awali Mweka Hazina wa halmashauri hiyo ,Grace Maembe, alieleza utekelezaji wa hoja za CAG kwa mwaka 2024/25 kuwa zilikuwa 29, ambapo hoja 19 zimetekelezwa sawa na asilimia 66%, hoja nane zinaendelea kutekelezwa sawa na asilimia 28%, hakuna hoja isiyo tekelezwa, hoja mbili zimejirudia hivyo kufanya halmashauri hiyo kutekeleza kwa asiliomia 100 ya hoja zote za CAG.











Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.

















Top News