ASASI ya AGENDA imesema imeridhishwa na utekelezaji wa mradi wa kuhamasisha wakulima katika Halmashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam kulima kilimo endelevu ambacho kitasaidia mazingira yawe endelevu na wenyewe wawe na afya bora.
Akizungumza na Waandishi wa habari baada ya kufanya ziara ya ufuatiliaji wa mradi huo ambao pia ulihusisha upandqji wa miche ya miti ya matunda katika mashamba ya wakulima pamoja na shule za msingi na sekondari, Katibu Mtendaji wa AGENDA Dorah Swai amesema wakulima wametekeleza mradi huo kwa kiwango kikubwa.
“Katika mradi huu tulikuwa tunahimiza wakulima kulima kilimo endelevu ambacho kitasaidia mazingira yawe endelevu kwa kulima kilimo ambacho hakitumii kemikali za viwandani zenye sumu za kuulia wadudu maarufu viuatilifu badala yake wameelekezwa jinsi ya kutengeneza viuatilifu vinatenengezwa kwa majani ya miti, miti ,mkojo wa sungura .”
Pia waliekezwa katika mashamba yao wpande miti kwasababu mbalimbali ikiwemo ya kukabiliana na tabianchi huku akieleza walikuwa wakiwahamasisha kupanda miti ya matunda ambayo inafaida nyingi kama chakula na Kivuli.
Ameongeza kwa wanafunzi shuleni AGENDA iliwafundisha kupanda miti kwa lengo la kukabiliana na tabianchi na kupendezesha mandhari ya shule zao .”Walipanda miti ya matunda.”
Aidha amesema pia utekelezaji wa mradi huo unaofanuwa na AGENDA ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali upatikanaji wa chakula mashuleni kwasababu miti itakapokuwa watoto watapata chakula pamoja na kivuli
“Katika kufuatilia tumeona kuna juhudi kubwa ya walengwa katika kutunza miche ambayo walipewa kuipanda katika kashamba kwani inaendelea vizuri.Tunawashukuru manispaa ya Kigamboni kwani mradi huu hatujautekeleza peke yetu bali na wao tulikuwa nao muda wote.
“Katika kutoa mafunzo kwa Wakulima tumeshirikiana wote na tumekuwa nao katika kila hatua ya utekelezaji wa mradi huu.Mradi huu umetekelezwa kupitia ufadhili wa fedha zilizotolewa na GGF lililopo nchini Marekani,”amesema Swai.
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi katika Halmashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam Priscila Mhina amesema wamekuwa wakiwasaidia wakulima kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kutumia watalaam waliosambazwa kila kata kwa ajili ya kutembelea wakulima kutoa ushauri na kuwaelekeza jinsi ya kulima kilimo bora
Pia amesema wanaunganisha wakulima pamoja na wadau mbalimbali wa kilimo wakiwemo AGENDA ambao wao wamekuja na ajenda muhimu kwa wakulima wetu kwa kipindi hiki.
“Kupitia mradi wa AGENDA tunawahamasisha zaidi wakulima kutumia dawa za asili kukabiliana na tabianchi, kulinda aridhi na mazao kwani kumekuwa na tabia wakulima kutumia dawa zenye kemikali ambazo zinasababisha sumu na ile sumu baadae zinakwenda kumuathiri mtumiaji.
“Sasa AGENDA wamekuja na ajenda yao nzuri ya kutumia dawa asili ambapo tulianza na shamba darasa katika kituo chetu cha rasilimali kilimo Kigamboni ambako tuliwaita wakulima kujifunza mazao mbalimbali na jinsi ya kuweka dawa asili kuanzia katika kitalu mpaka kuhamishia shambani.
“Na sasa wale wakulima baada ya kutoka pale walitakiwa waje watekeleze kwenye mashamba yao na kufundisha wakulima wengine ambao hawakuja katika darasa lile. Pia AGENDA walitusaidia kusambaza miti ya matunda katika maeneo mbalimbali ambayo ni pamoja na shule za msingi na sekondari,”amesema Mhina
Wakati huo huo wanafuika wa mradi huo akiwemo mkulima Deocretus Rwamishale pamoja na Mwalimu wa taaluma Shule ya Msingi Rupia Winfrida Mwisaka wameishukuru AGENDA kwa kuwapatia mafunzo ya kilimo endelevu pamoja na kuwapatia miche ya miti ya matunda.









































.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)