Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari amewataka Watumishi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kufanya kazi kwa Weledi na Ufanisi ili kufikia malengo ya Ofisi kwani ana Imani kubwa na utendaji kazi wa OFISI ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.

Mhe. Johari amesema hayo alipofungua kikao cha kwanza cha Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria tarehe 6 Machi, 2026 jijini Dar es Salaam.


"Niwaombe muendelee kutekeleza majukumu ya Ofisi hii kwa Weledi na Ufanisi ili kufikia malengo ya Ofisi na nina imani kubwa na utendaji kazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria” amesema Mhe. Johari


Aidha Mhe. Johari ameendelea kwa kuwataka watumishi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kuzingatia kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma ili kutoathiri utendaji kazi wa Serikali.


"Utumishi wa Umma unaongozwa na Sheria pamoja na Kanuni, hivyo natoa rai kwa watumishi wote tuzingatie Miongozo ya Utumishi wa Umma ili tusiathiri utendaji kazi wa Serikali," ameongeza Mhe. Mwanasheria Mkuu wa Serikali.


Vilevile Mhe. Johari ameitaka Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kuboresha matumizi ya mifumo ya TEHAMA ili kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

"Naomba nisisitize matumizi ya mifumo ya TEHAMA ili kurahisisha utendaji kazi na kutoa kazi zenye ufanisi kwa matumizi ya Serikali na jamii kwa ujumla,* ameeleza Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari.


Awali, akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwandishi Mkuu wa Sheria, Bw. Onorius Njole, amesema Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria imewekeza nguvu kubwa kwenye mifumo ya TEHAMA ili kuendelea kuimarisha utendaji kazi.

"Katika kuendelea kuimarisha utekelezaji wa Uandishi wa Sheria tumeamua kuweka nguvu kubwa kwenye mifumo ya Tehama kwa kuanzisha e-drafting, e-translation na e-revision na kwa usaidizi wako Mwanasheria Mkuu wa Serikali tutaweza kufanikisha hili." amesema.

Pia, Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Njole amemshukuru Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuendelea kuwa kiongozi bora na mwenye msaada mkubwa kwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria.


"Kwa niaba ya menejimenti ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na Wafanyakazi wote, tunamshukuru Sana Mhe. Johari kwa kuwa kiongozi bora kwa Ofisi yetu, na kutupa ushirikiano kila tunapohitaji” Amesema.

Miongoni mwa Wageni waalikwa katika Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria ni Mkurugenzi wa Mashtaka, Bw. Sylvester Mwakitalu

Baraza la kwanza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria, limefanyika tarehe 6 Machi, 2026 katika ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) jijini, Dar es salaam.

Kuelekea ya Siku ya Wanawake Duniani, wanawake wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Morogoro wametembelea na kutoa msaada katika kituo cha kulelea watoto yatima  RAYA, MGOLOLE  pamoja na kituo cha kulelea wazee cha Fungafunga kilichopo Manispaa ya Morogoro.

Ziara hiyo imelenga kuonyesha upendo, mshikamano na kuwafariji watoto pamoja na wazee wanaohitaji msaada katika jamii, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku hiyo muhimu kwa wanawake duniani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Maneja msaidizi Ukaguzi Beatrice Stephen amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa vitendo, kwa kushirikiana na jamii na kusaidia makundi yenye uhitaji maalum.

Katika ziara hiyo, wanawake wa TRA walitoa msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo chakula, mavazi pamoja na mahitaji mengine muhimu kwa watoto na wazee waliopo katika vituo hivyo.











Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb)(kulia) akiagana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries (SBL), Bw. Paul Makanza, baada ya kikao chake na ujumbe kutoka kampuni hiyo, katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika ya sera za kifedha na kanuni ili kuhamasisha uwekezaji wa muda mrefu wa sekta binafsi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa ndani, kuongeza matumizi ya malighafi za ndani, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta ya Viwanda ili kufungua fursa za ukuaji jumuishi na endelevu wa uchumi.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb)(kushoto) akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Serengeti Breweries, Bw. Obinna Anyalebechi, baada ya kikao chake na ujumbe kutoka kampuni hiyo, katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika ya sera za kifedha na kanuni ili kuhamasisha uwekezaji wa muda mrefu wa sekta binafsi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa ndani, kuongeza matumizi ya malighafi za ndani, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta ya Viwanda ili kufungua fursa za ukuaji jumuishi na endelevu wa uchumi.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akizungumza wakati alipokutana na ujumbe kutoka Kampuni ya Serengeti Breweries (SBL), ukiongozwa na Mwenyekiti wake wa Bodi ya Wakurugenzi Bw. Paul Makanza (hayupo pichani), katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika ya sera za kifedha na kanuni ili kuhamasisha uwekezaji wa muda mrefu wa sekta binafsi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa ndani, kuongeza matumizi ya malighafi za ndani, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta ya Viwanda ili kufungua fursa za ukuaji jumuishi na endelevu wa uchumi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Serengeti Breweries, Bw. Obinna Anyalebechi, akizungumza jambo wakati wa kikao cha ujumbe wa Kampuni hiyo na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (hayupo pichani), katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika ya sera za kifedha na kanuni ili kuhamasisha uwekezaji wa muda mrefu wa sekta binafsi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa ndani, kuongeza matumizi ya malighafi za ndani, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta ya Viwanda ili kufungua fursa za ukuaji jumuishi na endelevu wa uchumi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries (SBL), Bw. Paul Makanza, akizungumza jambo wakati wa kikao cha ujumbe wa Kampuni hiyo na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (hayupo pichani), katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika ya sera za kifedha na kanuni ili kuhamasisha uwekezaji wa muda mrefu wa sekta binafsi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa ndani, kuongeza matumizi ya malighafi za ndani, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta ya Viwanda ili kufungua fursa za ukuaji jumuishi na endelevu wa uchumi.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (Katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries (SBL), Bw. Paul Makanza (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bw. Obinna Anyalebechi, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao chao kilichofanyika katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika ya sera za kifedha na kanuni ili kuhamasisha uwekezaji wa muda mrefu wa sekta binafsi, kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa ndani, kuongeza matumizi ya malighafi za ndani, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta ya Viwanda ili kufungua fursa za ukuaji jumuishi na endelevu wa uchumi.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Makalla mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), tarehe 06 Machi, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amewasili Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaotarajiwa kufanyika tarehe 07 Machi, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) tarehe 06 Machi, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amewasili Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaotarajiwa kufanyika tarehe 07 Machi, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiangalia Kikundi cha Sanaa cha Maasarie Troupe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) tarehe 06 Machi, 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amewasili Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)unaotarajiwa kufanyika tarehe 07 Machi, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). 

 





Na: OWM (KAM) - Mwanza

Serikali imehimiza wananchi kujiunga katika na Hifadhi Skimu ili kujihakikishia usalama wa maisha yao ya sasa na baadaye ikiwemo kunufaika na mafao yanayotolewa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Akizungumza katika hafla ya uhamasishaji wa kujiunga na hifadhi hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amewasihi wananchi kutumia fursa hiyo kujiunga kwa wingi na kuchangia kikamilifu ili wanufaike na mafao mbalimbali yakiwemo ya matibabu pamoja na mafao ya uzeeni.

Aidha, amesema kuwa Serikali kupitia Mfuko wa NSSF imeanzisha Skimu ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii kwa wananchi waliojiajiri kwa ajili ya kuhudumia Wananchi waliojiajiri kwenye shughuli za kiuchumi.

Waziri Sangu amebainisha kuwa Hifadhi Skimu ni mpango wa uchangiaji wa hiari unaolenga kuwafikia wananchi waliojiajiri wakiwemo wavuvi, wafanyabiashara, machinga, bodaboda, wakulima, wachimbaji wadogo, wasanii pamoja na makundi mengine  yanayounda sehemu kubwa ya nguvu kazi ya Taifa.

Vilevile, amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuweka mazingira rafiki ya ajira na kujiajiri sambamba na kuimarisha mifumo ya hifadhi ya jamii ili kuhakikisha hakuna Mtanzania anayebaki nyuma katika kunufaika na huduma hizo muhimu.

“Hifadhi ya jamii ni haki ya msingi inayosaidia wananchi kuwa na maisha yenye heshima hasa wanapofikia umri wa uzee au wanapokumbana na changamoto zisizotarajiwa kama vile maradhi” amesema.

Awali akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewahimiza wananchi wa Mkoa wa huo kuchangamkia fursa ya kujiunga na Hifadhi Skimu, akieleza kuwa ni hatua muhimu ya kuilinda familia dhidi ya majanga ya maisha pamoja na kujihakikishia kipato cha baadaye.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Masha Mshomba amesema Hifadhi Skimu itawasaidia wananchi kuboresha maisha yao kwa kuondokana na utegemezi, hivyo kuwawezesha kujitegemea kiuchumi na kupata usalama wa maisha yao si tu kwa sasa bali pia wanapofikia umri wa uzee.









Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kusimamia na kukamilisha mradi wa kupeleka umeme wa gridi mkoani Kigoma na hivyo kuokoa takribani shilingi bilioni 58 zilizokuwa zikitumika kila mwaka kwa ajili ya ununuzi wa mafuta na matengenezo ya vipuri vya majenereta ya kuzalisha umeme.

Mhe. Salome ametoa pongezi hizo tarehe 6 Machi 2026 mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo kikubwa cha Kupoza umeme cha Kidahwe kilichopo mkoani Kigoma pamoja na kituo cha kupoza umeme cha kigoma mjini na kituo cha muda cha Kidahwe.

“Niwapongeze TANESCO kwa kufikisha umeme wa gridi Kigoma hasa baada ya kukamilisha mradi kutoka Nyakanazi hadi Kigoma na kwa kuamua kutumia fedha zenu za ndani shilingi bilioni tano kukamilisha kituo cha muda cha Kidahwe ambacho kwa sasa kinapeleka umeme Kigoma wakati ujenzi wa kituo kikubwa cha umeme Kidahwe ukiendelea,” amesema Mhe. Salome

Amesema kituo kipya cha umeme cha Kidahwe kitakuwa na uwezo wa megawati 192 na hivyo kitaimarisha zaidi hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Kigoma ambao kwa sasa unapata takribani megawati 30.

Ameongeza kuwa kituo hicho kinatarajiwa kukamilika mwezi Novemba mwaka huu na kitasaidia pia kuimarisha hali ya umeme katika mikoa ya Magharibi, kuendesha Treni ya Mwendo Kasi (SGR) pamoja na kuchochea biashara ya umeme na nchi jirani za Magharibi mwa Tanzania.

Kutokana na uwepo wa umeme wa kutosha mkoani Kigoma, Mhe. Salome amewakaribisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika mkoa huo.

Aidha, amewaasa wananchi kulinda miundombinu ya umeme akieleza kuwa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya nishati nchini hivyo wananchi wanao wajibu wa kuilinda na kuithamini.

Awali, Mratibu wa Mradi wa Kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Nyakanazi hadi Kigoma, Mhandisi Ramadhan Uwessu, alisema kuwa ujenzi wa kituo kipya cha Kidahwe unaenda sambamba na upanuzi wa kituo cha Nyakanazi ili kukiwezesha kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe.

Ameongeza kuwa kituo hicho pia kitapokea umeme kutoka njia ya Tabora kwa msongo wa kV 132, kutoka Sumbawanga kwa msongo wa kV 400 pamoja na umeme utakaozalishwa kutoka mradi wa Malagarasi.

Amesema mradi huo umefikia asilimia 47 ya utekelezaji na unagharimu takribani shilingi bilioni 434 zilizotolewa na Serikali ya Tanzania, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Korea Kusini (EDCF).










 

Na Mwandishi Wetu

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kufuta leseni ya rejareja ya bidhaa za mafuta ya petroli ya kampuni ya Iyan Energy Limited na kusitisha kwa muda wa miezi sita leseni ya kampuni ya Crescent Energy Tanzania Limited, baada ya kubaini ukiukwaji wa sheria na masharti ya leseni.

Kwa mujibu wa taarifa ya EWURA, uamuzi huo umefanyika kufuatia maamuzi yaliyotolewa na Bodi ya Wakurugenzi wakati wa vikao vyake vya hivi karibuni.

EWURA imesema leseni iliyofutwa ni Petroleum Retail Licence Na. PRL-2018-269, iliyokuwa ikimilikiwa na Iyan Energy Limited kwa ajili ya kuendesha biashara ya rejareja ya mafuta katika Kiwanja Na. 26 na 27, Barabara ya Pangani, Jiji la Tanga.

Wakati huohuo, Bodi imesitisha kwa muda wa miezi sita leseni ya rejareja ya bidhaa za mafuta ya petroli Namba PRL-2022-296 ya Crescent Energy Tanzania Limited, iliyotolewa kwa ajili ya kuendesha biashara ya rejareja katika Kiwanja Na. 5, Kitalu “N”, Eneo la Chamakweza, Wilaya ya Chalinze, Mkoa wa Pwani.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa maamuzi hayo yamefanyika baada ya EWURA kujiridhisha kuwa kampuni hizo zilikuwa zikijihusisha na shughuli zinazofanana na biashara ya uuzaji wa bidhaa za mafuta kwa jumla, hali ambayo haikuruhusiwa chini ya leseni za rejareja walizokuwa nazo.

EWURA imeeleza kuwa hatua hizo zinakiuka Kifungu Na. 131 cha Sheria ya Petroli, Sura ya 392, pamoja na Kanuni ya 9 na 11 za Kanuni za Mafuta (Biashara ya Jumla, Uhifadhi, Rejareja na Matumizi Binafsi), Tangazo la Serikali Na. 150/2022.

Onyo kwa umma

Katika taarifa yake, EWURA imeutaarifu umma kuwa kujihusisha kwa namna yoyote na kampuni hizo katika biashara ya usambazaji wa bidhaa za mafuta ya petroli kutakuwa kinyume cha sheria, na kwamba hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaokiuka.

Mamlaka hiyo imeongeza kuwa itaendelea kusimamia sekta ya mafuta kwa kuhakikisha kunakuwa na mazingira ya ushindani wa haki na upatikanaji wa uhakika wa bidhaa za mafuta nchini, kwa kudumisha “uwanja ulio sawa” kwa wadau wote.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akijionea shughuli za uvuvi katika maeneo ya kazi ya wavuvi katika Soko la Kimataifa la Samaki Kirumba jijini Mwanza, ambapo pia alishiriki kuvua samaki akishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba.















Top News