-Ampongeza Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa uchapakazi

-Asisitiza Tanzania itavuka salama Kipindi hiki kigumu cha tatizo la mafuta 


Na Mwandishi Wetu.

"KAMA ambavyo imejaaliwa kuwa na aina mbalimbali ya vivutio vya Utalii,Mali asili,  yakiwemo madini na vinginevyo, pia hivyo Taifa la Tanzania limejaaliwa kuwa na viongozi hodari tangu ilipopata uhuru wake Mwaka 1961"

"Ukiacha viongozi wengine waliotangulia na kuliongoza Taifa hili,kwa sasa tunaye Mama yetu Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye kwa hakika watanzania wengi tunajivunia uongozi wake imara tangu aliposhika madaraka kutuongoza" ameanza kwa kusema hivyo Dkt.Sajad Habib Rai

Dkt.Sajad anayehudumu kama Meneja wa nchi katika Bohari ya kuhifadhia mafuta Jamii ya Petroli 'MOIL Energies' , anasema kupitia utawala wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kila jambo ndani ya nchi linakwenda sawa likiweko suala zima la nafasi kwa wawekezaji kufanya uwekezaji nchini.

"Hakika kwa hili Rais Samia anastahili pongezi, ameifanya Tanzania kuwa kimbilio la watu kutoka Mataifa ya nje kuja na kuwekeza, fursa hiyo haipo katika kila Taifa, hapa ndipo unaona uhodari wa Kiongozi huyu" anasema Dkt.Sajad

Kimsingi mtaalamu huyu katika fani za Ununuzi na Ugavi, usafirishaji, biashara katika Tasnia ya nishati ya mafuta akiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 20, kwake ni fahari kutekeleza majukumu yake chini ya utawala wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan 

"Kiongozi bora ni yule anayejulikana kwa kujenga timu zenye mshikamano, kuendesha ufanisi wa utendaji kazi, na kukuza utamaduni wa utendakazi na uwajibikaji, hakika Dkt.Samia amejitolea kufanya kazi kwa ubora, pamoja na mambo mengine hilo ni jambo pekee linalotufanya tufurahie uongozi wake" amesisitiza Dkt Sajad.

Dkt.Sajad kama mmoja wa viongozi wanaotoa mchango mkubwa katika sekta ya mafuta nchini, kupitia nafasi yake ya usimamizi wa bohari ya mafuta, ameonyesha uwezo mkubwa wa kuunganisha maslahi ya wafanyakazi, wawekezaji na Serikali kwa ujumla.

Uongozi wake umeendelea kuonekana kuwa wa vitendo siyo tu kwa timu yake anayoiongoza katika eneo lake la kazi, bali hata maeneo mengine ikiwemo Serikalini, kwani hivi karibuni kupitia mchango wake wa mawazo umesaidia kuleta tija katika eneo la kodi na ushuhuru kipitia biashara ya mafuta.

Kupitia mawazo yake ya kudhibiti vitendo vya ukwepaji kodi kutoka kwa baadhi ya wafanyabiashara wa mafuta akitoa wazo  kuwa kila muagizaji wa mafuta anapaswa kukadiriwa  kodi kulingana na kiasi Cha mafuta alichoagiza kabla ya mafuta hayo kuingia sokoni, kwa kiasi kikubwa kumesaidi kuleta tija.

Anasema wazo hilo ambalo kabla ya kulitoa kulisababisha kuwepo kwa 'ujanja ujanja' kutoka kwa baadhi ya wafanyabiashara kukwepo kodi kumesaidia kuiongezea mwanya Mamlaka ya Mapato ( TRA) kukusanya kodi yake kwa ufasaha hali ambayo pia imesaidia kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.

Anasema siku zote katika mazingira ya biashara ya mafuta ambayo yanahitaji umakini mkubwa, nidhamu pamoja na uwajibikaji, ameendelea na ataendelea kusimamia utendaji wa kazi kwa weledi mkubwa.

Moja ya mambo yanayomtofautisha ni namna anavyoweka mbele ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za Serikali, akionesha wazi kuunga mkono mifumo mipya ya usimamizi wa mafuta, ikiwemo ulipaji wa kodi kabla ya mafuta kuingia sokoni. 

Mfumo huu umechangia kupunguza mianya ya ukwepaji kodi sambamba na kuongeza mapato ya Serikali kwa kuleta ushindani wa haki kwa wafanyabiashara wanaofuata sheria.

Mchango wa Dkt Sajad kwa upande wa Serikali  unaonekana katika kuongeza mapato kupitia kodi, kudhibiti upotevu wa mafuta, kuimarisha usalama wa nishati na kusaidia uchumi wa taifa tukielewa pia kuwa Sekta ya mafuta ni mhimili mkubwa wa maendeleo ya nchi, hivyo viongozi wenye maono kama Dkt Sajad wanakuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya taifa.

Aidha akizungumzia changamoto ya mafuta inayoikumba Dunia kwa Sasa, Dkt Sajad anasema hali hiyo siyo kwa Tanzania pekee bali hata upande wa mataifa mengine Duniani ikichangiwa na mzozo unaendelea Mashariki ya Kati ingawa kwa Tanzania bado Kuna akiba ya kutosha ya mafuta.

Kwa ujumla, Dkt Sajad Habib Rai ni mfano wa kiongozi anayejali maendeleo ya wafanyakazi na Taifa kwa pamoja. Utendaji wake umeonyesha kuwa mafanikio siyo kwa taasisi yake tu, bali pia taasisi yoyote inayotegemea uongozi bora, uwajibikaji na uwezo wa kuendana na mabadiliko ya kisasa katika sekta husika, kupitia juhudi zake, sekta ya mafuta inaendelea kuwa na mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Tanzania.




Na Byera Deus ,Bukoba

MBUNGE wa Jimbo la Bukoba Mjini Mhandisi Johnston Mtasingwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Dini  wameungana na wananchi wa Kata ya Kibeta katika mtaa wa Anyama   kushiriki Ibada  ya kuaga miili ya watoto wawili kati ya Wanne wa familia mbili waliofariki kutokana na Mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia Aprili 17,2026   katika Manispaa ya Bukoba, mkoani Kagera, ambayo ilisababisha vifo vya watoto wanne

Majina ya  watoto waliofariki ni  Eliza Edmund(13), mwanafunzi wa shule ya msingi Kashabo,Darasa la sita,Edwini Edmund(10), mwanafunzi wa darasa la nne Kashabo, Munihadi Mickidadi(13) aliyekuwa anasoma darasa la nne shule ya msingi Pamoja na Jamia  Mickidad(5).

Akizungumza wakati wa kuaga miili ya watoto hao Mhandisi Mtasingwa  ambaye ni Mbunge wa Bukoba Mjini amesema  licha ya kuwa na majukumu ya vikao vya Bunge alipata taarifa saa 12 asubuhi.

Ambapo  alituma msaada wa awali na mara baada ya kuuliza swali lake Bungeni alianza safari ya kurudi jimboni na  alifika saa 6 usiku kuungana na familia hizo.

Amesema amesikitishwa na vifo vya watoto hao ambapo ametoa ombi kwa TANROAD na TARURA kuzibua mitaro hasa kipindi hiki cha mvua huku akiwataka wananchi kukagua nyumba zao mara kwa mara  katika msimu huu wa mvua  

Ametumia fursa hiyo kutoa pole kwa wananchi waliopoteza mifungo na makazi  na kuomba waendelee kuchukua tahadhari kwani mvua Bado ni nyingi na nitaendelea kunyesha na kuomba wananchi kuendelea kushirikiana pale matatizo yanapojitokeza

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Bukoba Erasto Sima watoto wengine wawili  ambao wamefariki katika tukio hilo tayari wamezikwa kata ya Maruku  Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.

“Nimesikitishwa kuwa na vifo hivyo ambavyo vimekatiza ndoto za watoto wadogo ambao walikuwa na malengo makubwa ya badae.Mvua hizo ambazo zimenyesha baadhi ya wanchi wamepoteza mifungo yao hasa kuku wengi wamesombwa.

“Wengine wamepoteza makazi hivyo nitoe mwito kwa wananchi  wanaoishi mabondeni na kando kando ya Ziwa Victoria kuchukua tahadhari kabla ya vifo havijaongezeka.”

Ibada ya kuaga miili hiyo imeongozwa na Mchungaji Ediso Rugemeleza  Mchungaji  wa Usharika wa kanisaa kuu La Kiinjili la  Kilutheri KKKT Dayosisi Kasikazini Magaribi

Ambapo ametumia fursa hiyo kwa kuzishukuru taasisi za serikali kufanya uokozi  na wananchi Kujitolea ambao anadai kuwa hiyo ndio misingi ya utu. Vifo hivyo vimetokea baada ya ukuta wa hotel ya Perfect kuzidiwa na  maji na kuangukia nyumba za majirani na kusababisha vifo vya watoto hao.








Na Mwandishi Wetu

WAKATI Chama Cha Mapinduzi  (CCM) kikifungua dirisha  kwa makada wake kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kuwania Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki leo,Kada wa Chama

hicho ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga amechukua fomu kuwania nafasi hiyo.

Mtatiro ambaye ni miongoni mwa makada vijana na wasomi katika Taifa la Tanzania amechukua fomu hiyo ya kuwania Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki leo Aprili 18,2026  katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, zilizopo Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Amekabidhiwa na fomu hiyo  na Ofisa wa Chama Idara ya Organaizesheni, Raymond Mosi.

Akizungumza baada ya kuchukua fomu Mtatiro amesema  ameamua kujitosa katika kinyang'anyiro hicho kutumia  haki  yake ya msingi katika kuliwakilisha taifa katika Bunge la Afrika Mashariki kwa maslahi mapana ya taifa.



WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikifungua dirisha kwa makada wake kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kuwania Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki leo, mwitikio umekuwa mkubwa huku makada kujitokeza kushiriki mchakato huo.

Makada hao wamefika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam, ambako wamekabidhiwa fomu hizo na Ofisa wa Chama kutoka Idara ya Organaizesheni, Raymond Mosi.

Miongoni mwa waliojitokeza ni kada kijana, Julias Mtatiro, ambaye ujio wake katika kinyang’anyiro hicho unaakisi kuongezeka kwa ushiriki wa vijana katika nafasi za juu za uongozi wa kikanda.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu, Mtatiro amesema uamuzi wake wa kuwania nafasi hiyo unatokana na dhamira ya kutumia nguvu, maarifa na mtazamo wa kizazi kipya katika kulisukuma mbele taifa ndani ya Bunge la Afrika Mashariki.

Mtatiro ameeleza kuwa vijana wana mchango mkubwa katika kuleta mageuzi chanya, ubunifu wa sera na kuimarisha ushirikiano wa kikanda unaolenga maendeleo jumuishi.

Aidha, amesisitiza anajitosa si tu kama haki yake ya msingi, bali kama wajibu wa kizazi cha vijana kushiriki kikamilifu katika maamuzi ya kimkakati yanayogusa mustakabali wa taifa na ukanda wa Afrika Mashariki kwa ujumla.


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewapongeza wanawake nchini kutokana na mchango mkubwa wanaoutoa katika kukuza uchumi uchumi wao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Amesema kuwa zaidi ya asilimia 50 ya biashara ndogo na za kati zinamilikiwa na wanawake hivyo inaonesha wazi kuwa injini ya uchumi wa Taifa inaendeshwa kwa kiasi kikubwa na wanawake. 

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Aprili 18, 2026) katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Mkutano wa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs) na Maonesho ya Uwekezaji na Biashara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Four Season jijini Arusha.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kusisitiza kuwa uchumi jumuishi huchochea amani na mshikamano katika jamii kwa sababu kitendo cha ushirikiano wa pamoja kinawezesha kubadilisha hali ya uchumi na kufikia maendeleo jumuishi kwa wote.

“Tunapaswa kujenga uchumi jumuishi unaohusisha makundi yote ya jamii, kwa upande wetu  Serikali tutahakikisha ajenda hii inatekelezwa kwa vitendo”.

Aidha, Waziri Mkuu amesema kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 kunahitaji ushirikiano wa karibu kati ya sekta binafsi na Serikali, huku akiahidi kuwa chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sekta binafsi itaendelea kuwa mhimili muhimu katika ajenda kuu ya uchumi. 

Amesema Serikali inaendelea kuangalia uwezekano wa kuanzisha mfuko maalumu wa kuwawezesha wahitimu wa vyuo vikuu kifedha ili kukuza mawazo yao ya kibiashara, pamoja na kuboresha sera zitakazoruhusu matumizi ya mali zinazohamishika kama dhamana, ikiwemo vyeti vya taaluma. 

Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wajasiriamali kutumia kikamilifu fursa za miundombinu iliyoboreshwa, hususan reli ya kisasa (SGR) na reli ya TAZARA inayofanyiwa maboresho, ili kufikia masoko ya kimataifa kupitia kanda za Northern Corridor na Central Corridor, hatua itakayorahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka Tanzania hadi maeneo kama Kapiri Mposhi nchini Zambia.

Kwa upande wake,  Naibu Waziri Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Dkt. Pius Chaya ametumia furha hiyo kumshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake mahiri na msaada mkubwa anaoutoa katika ofisi yao na hivyo kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao.

Dkt. Chaya amesema kuwa wizara yao itahakikisha inaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Wafanyabiasha Wadogo na wa Kati (SMEs) pamoja na wawekezaji ili waweze kukua na kutoa mchango wenye tija katika kufikia uchumi wa dola trilioni moja.

Naye, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo amesema Serikali imeweka mkazo katika kukuza Sekta ya Biashara Ndogo na za Kati (SMEs) ili ziweze kuchangia kikamilifu katika ukuaji wa uchumi, ajira na mapato kwa Taifa yatokanayo na kodi.  

Amesisitiza umuhimu wa urasimishaji wa biashara, uzalishaji wenye kuongeza thamani, kuzingatia viwango vya ubora pamoja na matumizi ya teknolojia za kidigitali umewezesha upatikanaji wa masoko ya ndani na nje ya nchi.

 Aidha, amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara kwa kurahisisha taratibu, kuimarisha mifumo ya usajili na kulinda ubunifu ili kuwafanya wajasiriamali waaminike na kuvutia mitaji, kutoka kwa wawekezaji wa nje.





 

 

The members of the Selection Committee of The Africa Road Builders – Trophée Babacar NDIAYE met on April 17, 2026, in Abidjan, Côte d’Ivoire, as part of the 2026 Inaugural Conference, to designate the laureate of the Super Prize Great Builder – Babacar NDIAYE Trophy 2026.

This year, the central theme of the proceedings was: “Investing in roads, investing in transport: for prosperity in Africa.”

During this annual meeting, the Selection Committee meticulously assessed the quality of investments in the road and transport sectors across the continent, drawing on the 2026 report of the Media Network for Infrastructure and Finance in Africa (MIFA), as well as publicly available reports in these fields.

Following deliberations, the Committee proceeded with the designation of the laureate of the Super Prize GreatBuilder – Babacar NDIAYE Trophy 2026.

Accordingly, His Excellency General Mamadi Doumbouya, President of the Republic of Guinea, has been designated Laureate of the Super Prize GreatBuilder – Babacar NDIAYE Trophy 2026.

He has been recognized for his personal leadership as well as for the investment efforts undertaken under the Simandou Vision 2040 program. This program indeed represents one of the “largest logistical transformations ever carried out in Africa.”

The Selection Committee particularly commended his commitment to integrated and sustainable development, as well as his vision to build outstanding infrastructure in the road and transport sectors for his country.

The Selection Committee congratulates His Excellency General Mamadi Doumbouya on this distinction and solemnly invites him to receive his trophy on May 27, 2026, in Brazzaville, Republic of Congo, during the Final Conference, which will be held on the sidelines of the Annual Meetings of the African Development Bank (AfDB).

Under the Builder Trophy

The Selection Committee thanks all speakers of the 2026 Inaugural Conference and is pleased to announce the laureates of the Builder Trophy for the year 2026:

 

- Road Maintenance Fund of the Republic of Guinea

- National Road Fund of Liberia

- AGEROUTE, Côte d’Ivoire

- PMUA Project, Côte d’Ivoire

- Road Transport Regulatory Authority (ARTI), Côte d’Ivoire

- National Bureau of Technical Studies and Development (BNETD), Côte d’Ivoire

All these laureates are also invited to receive their trophies during the Final Conference on May 27, 2026, in Brazzaville.

The Selection Committee extends its gratitude to His Excellency João Lourenço, President of the Republic of Angola, Laureate of the Super Prize Great Builder – Babacar NDIAYE Trophy 2025 and High Patron of the 2026 edition, as well as to his Special Representative at the 2026 Inaugural Conference, His Excellency Victor Hugo Guilherme, Minister of Planning.

The Selection Committee expresses its deep gratitude to Côte d’Ivoire and its highest authorities for their hospitality. It extends its sincere thanks, particularly to the Minister of Transport and Maritime Affairs and to the Minister of Planning and Development, for their distinguished contributions to the success of the 2026 Inaugural Conference.

The Selection Committee also thanks the United Arab Emirates, the regular host of the Inaugural Conference over the past three years, which, despite the relocation of the event due to the current situation in the Middle East, have remained committed to supporting this development initiative led by African journalists.


It joins the General Commission in expressing its deep gratitude to His Excellency Ali Youssef Alnuaimi, Ambassador of the United Arab Emirates to Côte d’Ivoire, for his advice, his effective presence at the Inaugural Conference, and the messages of cooperation and development he conveyed.

The Selection Committee thanks all its members across Africa, as well as all participants and partners of The Africa Road Builders – Trophée Babacar NDIAYE , 2026 edition.

The Selection Committee honors the memory of Dr. Babacar Ndiaye, inspirer of The Africa Road Builders – Trophée Babacar NDIAYE, and thanks the Babacar Ndiaye family for their remarkable contribution.

Finally, the Selection Committee thanks the African Development Bank and its President, Dr. Sidi Ould Tah, for their patronage and continued support for this organization.

For the Selection Committee
Mr. Kimwanga Bakari
Journalist, Spokesperson (Tanzania)





WADAU  wa sekta binafsi wamehimizwa kutumia kikamilifu fursa za uwekezaji kupitia miradi ya ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP) ili kuchochea kasi ya maendeleo nchini. Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam katika mafunzo maalum yaliyolenga kuongeza uelewa na uwezo wa wadau kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha PPP na Jukwaa la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), yamekuja wakati ambapo Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji kupitia maboresho ya sheria na miongozo ya ubia. Hatua hiyo inalenga kuvutia ushiriki mpana zaidi wa sekta binafsi katika miradi ya maendeleo.

Washiriki walipata fursa ya kujifunza kwa kina kuhusu mfumo wa PPP, ikiwemo taratibu za kuibua, kuandaa na kutekeleza miradi, sambamba na namna ya kutathmini hatari na faida zake. Aidha, walielekezwa jinsi ya kutumia taarifa za orodha ya miradi (pipeline) ili kubaini maeneo yenye fursa za uwekezaji.

Kupitia majadiliano ya kitaalamu na uzoefu wa wataalam, ilibainika kuwa sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kusaidia Serikali kufanikisha malengo ya muda mrefu ya maendeleo, ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Wadau walisisitizwa kuwa ubia si ubinafsishaji, bali ni ushirikiano unaolenga kuongeza ufanisi na tija.

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameibua mwamko mpya kwa wadau wa sekta binafsi kuona umuhimu wa kushiriki katika miradi ya ubia, huku yakitoa mwanga wa namna bora ya kunufaika na fursa zilizopo na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa taifa.



Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC), David Kafulila, ameeleza kwa kina dhana ya ubia (PPP) akisisitiza kuwa si ubinafsishaji, bali ni mfumo wa ushirikiano unaolenga kuongeza ufanisi na tija katika miradi ya maendeleo ya umma.

Akizungumza na wadau wa sekta binafsi jijini Dar es Salaam, Kafulila alisema mkanganyiko uliopo miongoni mwa wananchi unatokana na kufananisha PPP na ubinafsishaji, huku akifafanua kuwa katika ubia, Serikali hubaki na umiliki wa rasilimali zake huku sekta binafsi ikishiriki katika uwekezaji na uendeshaji.

Alieleza kuwa kuanzishwa kwa sera ya PPP mwaka 2009 na sheria ya mwaka 2010 kulilenga kurekebisha changamoto za mikataba ya nyuma, na kuhakikisha kuwa pande zote Serikali na wawekezaji—zinanufaika kwa usawa na kwa uwazi.

Kwa mujibu wa Kafulila, sababu kuu tatu zinazoifanya Serikali kuingia ubia ni pamoja na kutumia mtaji wa sekta binafsi badala ya kutegemea kodi za wananchi pekee, kupata teknolojia ya kisasa, na kuongeza ufanisi wa usimamizi wa miradi.

Aidha, alitofautisha kati ya mkandarasi wa kawaida na mwekezaji wa PPP, akieleza kuwa mkandarasi hulipwa baada ya kukamilisha kazi, wakati mwekezaji wa PPP huwekeza fedha zake na kurejesha gharama kupitia uendeshaji wa mradi kwa muda maalum.

Alisisitiza kuwa Kituo cha PPP kina jukumu la kuhakikisha mikataba yote inazingatia uwazi, ushindani na maslahi ya Taifa, akihitimisha kuwa ubia ni nyenzo muhimu ya maendeleo na si njia ya kupoteza mali za umma.




Picha za Pamoja.

 

Timu ya Mpira wa miguu ya TCDC Sports Club imechukua alama tatu (3) baada cha kuifunga Timu ya Mpira wa miguu ya Wizara ya Kilimo goli mbili (2) kwa moja (1) katika mechi iliyochezwa leo Aprili 17, 2026 saa 2:30 3:45 katika viwanja vya Venite mkoani Njombe.

Timu hizo zimekutana katika mashindano ya Michezo ya Wafanyakazi (Meimosi) yanayoyafanyika kitaifa mkoani Njombe.

Hapo Kesho Aprili 18, 2026 Timu ya Mpira wa miguu TCDC Sport Club inatarajia kukutana na Timu ya Mpira wa miguu ya TAMISEMI saa10:15 jioni katika viwanja vya Kibena mkoani humo.

 Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, leo Aprili 17, 2026 ameipokea Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyofanya ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu na taasisi mbalimbali za sekta ya afya Tanzania Bara.

Ziara hiyo imehusisha kutembelea Makao Makuu ya Wizara ya Afya, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na Bohari ya Dawa (MSD).

Akiongea mara baada yakuwapokea, Dkt. Samizi amesema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya afya kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Amesema kuwa juhudi hizo zimejikita kuimarisha miundombinu ya afya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na kuboresha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi nchini.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Nasra Nassor, amesema ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa wajumbe wa kamati kwani imewapa fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu uendeshaji wa sekta ya afya.

Ameongeza kuwa maarifa waliyoyapata yatawasaidia kuboresha utoaji wa huduma za afya Zanzibar kwa kuzingatia mifumo na mbinu walizojifunza kutoka Tanzania Bara.




Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) leo tarehe 17, Aprili 2026 amefanya kikao kazi na maafisa na askari wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Makao Makuu jijini Arusha katika ukumbi wa Phase II.

Akizungumza na watumishi hao, Waziri alielekeza changamoto mbalimbali za kiutendaji zinazokabili shughuli za uhifadhi na usimamizi wa rasilimali za taasisi zitatuliwe. Vilevile, ametoa maelekezo ya namna bora ya kushughulikia na kuzitatua changamoto hizo kwa ufanisi na kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Kwenye kikao hicho Mhe. Dkt. Kijaji aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas na Mkurugenzi wa Wanyamapori Dkt. Alexander Lobora huku akipokelewa na mwenyeji wake Kamishna wa Uhifadhi TANAPA CPA Musa Nassoro Kuji.














Top News