
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akizindua kituo cha Kijitonyama FTTx Experience Centre Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL,) David Nchimbi amesema kituo hicho cha ubunifu wa matumizi ya teknolojia ni cha kipekee na kinachotoa uzoefu wa pamoja na elimu kuhusu matumizi ya teknolojia za kidigitali ambapo kupitia kituo hicho wananchi watapa fursa ya kuona kwa vitendo namna ambavyo intaneti ya TTCL inavyoweza kubadilisha nyumba, ofisi au biashara kwa za kidigitali na zenye ufanisi.
Amesema kituo hicho kitakuwa jukwaa la kujifunza na kubadilisha uzoefu kuhusu matumizi teknolojia za kisasa nyumbani, mifumo ya ofisi za kidigitali, na suluhisho katika biashara za mtandaoni pamoja na kuchochea na kujenga uelewa kwa jamii juu ya umuhimu wa TEHAMA katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Nchimbi amesema,ubunifu unaoendelea kufanywa na Shirika hilo ni katika kuhakikisha wateja wanapata huduma bora kwa wakati na uhakika na zenye kurahisisha shughuli mbalimbali ikiwemo mtandao, biashara mtandao, huduma za kifedha na mawasilino yenye tija.
Amesema, Serikali itaendelea kuhakikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano nchini zinapewa kipaumbele na hiyo ni pamoja na kuongeza ubunifu na wigo wa utoaji huduma wa Shirika hilo kwa wananchi, kuongeza ufanisi, mapato na kujiendesha kibiashara ili kuendelea kuwahudumia wananchi kwa ubora zaidi,
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TTCL Moremi Marwa amesema kuwa, Shirika linatekeleza Mpango Mkakati wa miaka 10 ulioanza katika mwaka wa fedha wa 2025/ 2026 kwa lengo la kuleta mageuzi katika uwajibikaji, kuongeza uzalishaji wenye tija na kufanya uendelevu katika miradi waliyoianzisha.
“Pamoja na mageuzi mengineyo mradi huu wa ´Faiba ´Fiber to The X´( FTTx) ambao umelenga kusambaza huduma ya intaneti yenye kasi , uhakika na ubora katika makazi, ofisi na maeneo ya biashara na kupitia huduma ya ´Faiba Mlangoni Kwako´shirika linaendelea kutoa huduma katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Dar es Salaam, Unguja, Arusha, Dodoma, Mwanza, Geita, Iringa na Mbeya na kwa mwaka 2026/27 Shirika limejipanga kufikisha huduma hii ya Faiba katika mikoa iliyobaki.” Amesema.
Akieleza kuhusu FTTX Experience Centre, Marwa amesema kituo hicho ni mwendelezo wa ubunifu katika utoaji huduma za intaneti nchini ambapo kwa sasa wateja wanapata huduma za inataneti zilizounganishwa, ambapo mteja anaweza kupata huduma tatu katika kifurushi kimoja yaani intaneti bila kikomo akiwa nyumbani, dakika anazoweza kuzitumia katika simu ya mkononi au mezani pamoja na GB za intaneti katika simu ya mkononi.
Amefafanua kuwa kupitia kituo hicho wateja watapata fursa ya kuona matumizi ya kidigitali kwenye smart home, uwekaji wa huduma ya intaneti ya Faiba majumbani, ofisini na maeneo ya biashara pamoja na teknolojia inayotumika katika utoaji wa huduma hizo.
Kuhusiana na faida kwa Shirika hilo Marwa amesema kwa mwaka wa fedha 2024/25 lilipata faida ya Shilingi Bilioni 22.9 kabla ya kodi na ni faida ambayo imethibitishwa na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG,) na wamejipanga zaidi katika kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja pamoja na kuliendesha Shirika hilo kibiashara na kuwashukuru wadau wao kutoka kampuni za Hisence na Huawei kwa ushirikiano wao katika ujenzi wa kituo hicho.
Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mikutano ya Baraza la Wafanyakazi ni nyenzo muhimu ya kujadili utekelezaji wa majukumu, kubaini changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.
Amesema ili kuendelea kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu, ni muhimu kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja, bidii na weledi. Tunapaswa kujipambanua kwa utendaji wa hali ya juu unaoendana na hadhi ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika nchi.
Mhe. Masauni ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais uliofanyika Dodoma, Aprili 15, 2026 akieleza kuwa Ofisi imeendelea kufanya vizuri katika kudumisha Muungano, hususan kupitia utoaji wa elimu kwa umma kwa makundi mbalimbali.
“Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, Ofisi imefanikiwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191, hususan kwa kuimarisha vifungu vinavyohusu mabadiliko ya tabianchi na kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).
Aidha, ni muhimu kuendelea kuimarisha uwezo wa kitaalam na kitaasisi, upatikanaji wa rasilimali na kuongeza jitihada za uhamasishaji wa rasilimali fedha, ikiwemo kupitia maandalizi bora ya miradi ya uhifadhi wa mazingira.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais ambaye pia Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi alisema lake kuu tangu kuanzishwa kwake baraza hilo lilikuwa kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini mipangokazi, pamoja na kuboresha uhusiano kati ya Menejimenti na watumishi.
“Madhumuni ya Mkutano huu ni kuwashirikisha wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa lengo la kupata Taarifa ya utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Ofisi.”

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS
NA Mwandishi Wetu
HALMASHAURI ya Jiji la Dar es salaam linaendelea kutekeleza agizo la Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Sukuhu Hassan la kuhakikisha wanafunzi wote wa darasa la 6 na 7 wanaotarajia kumaliza elimu ya msingi kwa mkupuo (Double Cohort) 2027 wanapata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2028.
Katika kuhakikisha agizo hilo linafanikiwa, Halmashuri hiyo imeendelea na ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa kujenga shule kwa mtindo wa ghorofa ambapo nyingine zimekamilika na nyingine zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.
Kwa mfano kwa mwaka wa fedha 2025/26,Halmashuri ya Jiji la Dar es salaam imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 19 katika sekta ya elimu Sekondari kuhakikisha adhima hiyo inafanikiwa.
Jumla ya shule za ghorofa 9 mpaka sasa zimejengwa zikiwemo mpya na zile zilizoboreshwa ili kuweza kukidhi mahitaji ya sasa.
Shule hizo ni pamoja na shule mpya ya Kitunda Relini iliyojengwa kwa gharama za Shilingi bilioni 4.2,Kipunguni B (bilioni 2.1),Bonyokwa(bilioni 2),Ukonga (bilioni 2.2),Minazi Mirefu (bilioni 2.3),Mnazi Mmoja (kumalizia ujenzi bilioni 1.8), Liwiti(bilioni 2.1) pamoja na kumalizia ujenzi Sekondari Kimanga(milioni 998).
Mbali na ujenzi huo, baadhi ya shule hizo zimefungiwa mfumo wa "lift" kuwawezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam inatarajia kuwa ifikapo muhula wa 2027/28 iwe imekamilisha mahitaji ya wanafunzi wote wanaotarajia kuanza kidato cha kwanza kwa muhula huo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.
Na.Mwandishi Wetu-DODOMA
WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umeanzisha utaratibu mpya wa kupima utendaji wa madiwani kwa kuzingatia uwezo wao wa kuchochea ukuaji wa biashara katika kata zao hatua hiyo inalenga kuimarisha uwajibikaji na kuinua uchumi wa wananchi katika ngazi ya chini.
Hayo yamesemwa leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma ambapo amesema mfumo huo utazingatia idadi ya biashara mpya zinazoanzishwa pamoja na uwepo wa mazingira rafiki yanayowezesha wafanyabiashara kukua.
Amesema kupitia utaratibu huo, madiwani watahamasika zaidi kusimamia maendeleo ya biashara katika maeneo yao na kuhakikisha maafisa biashara wa halmashauri wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Aidha, Nyaisa amesisitiza kuwa ni wajibu wa madiwani kusimamia utekelezaji wa sheria za biashara, huku akionya dhidi ya uwepo wa shughuli haramu kama uzalishaji wa pombe bandia katika maeneo yao.
"BRELA inalenga kukuza biashara ndogondogo ili ziweze kurasimishwa, hatua itakayowawezesha wafanyabiashara kupata mikopo, kupanua shughuli zao na kufikia masoko mapana zaidi ndani na nje ya nchi."amesema Bw.Nyaisa
Nyaisa ameongeza kuwa vijana ndio kundi kubwa la wafanyabiashara nchini, hivyo kuna umuhimu wa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutumia ujuzi na elimu yao kujiajiri kupitia biashara endelevu.
Kwa mujibu wa takwimu za BRELA, kumekuwa na ongezeko kubwa la biashara katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, hali inayoashiria kuimarika kwa uchumi wa nchi.
Hata hivyo, amewahimiza wafanyabiashara kurasimisha shughuli zao ili kuongeza uwezekano wa kupata mikopo na kuepuka changamoto zinazotokana na mitaji isiyo rasmi.
Vilevile, amewashauri wamiliki wa biashara za kifamilia kuhakikisha wanawaorodhesha wanahisa wote wakati wa usajili ili kuepusha migogoro ya baadaye.
Katika hatua nyingine, Nyaisa amesema taasisi hiyo imeanza kufuatilia na kusajili bunifu zinazotokana na taasisi za elimu kuanzia ngazi ya chini hadi vyuo vikuu, hususan zile zinazolenga kuboresha shughuli za kibiashara.
Kwa upande wake, Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira, amesema mafunzo yaliyotolewa kwa madiwani yamewajengea uwezo wa kuelewa vyema taratibu za usajili wa biashara pamoja na aina mbalimbali za leseni.
"Madiwani sasa wana nafasi nzuri ya kuwaongoza wananchi kwa usahihi wanapohitaji kusajili biashara zao, hatua itakayosaidia kupunguza changamoto zilizokuwapo awali."amesema
Aidha, amefafanua kuwa leseni za biashara kundi “B” hutumika kwa biashara zinazofanyika ndani ya halmashauri moja, wakati leseni za biashara kundi “A” humruhusu mfanyabiashara kuendesha shughuli zake hadi ngazi ya kimataifa bila kutozwa tozo ya ziada za leseni za biashara kundi B.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma




.jpg)
.jpg)
.jpg)




.jpeg)

.jpeg)











