Na Mwandishi Wetu, Arusha

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeingia katika mpango wa ushirikiano na kampuni ya Land Africa Safaris ili kukuza utalii wa ikolojia kupitia tukio la Cape to Cairo Arusha International Marathon linalotarajiwa kufanyika Mei 28 hadi 30, 2026 mkoani Arusha.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao kilichofanyika Machi 17, 2026 katika Ofisi ya Mhifadhi Mkuu wa Ziwa Duluti, Arumeru.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Mhifadhi Mkuu wa Ziwa Duluti, Peter A. Myonga, alisema ushirikiano huo ni fursa muhimu kwa TFS kutumia michezo kutangaza vivutio vya misitu na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea maeneo hayo.

Alisema tukio hilo linatarajiwa kuvutia zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi, hatua itakayochochea ongezeko la wageni, muda wa kukaa kwa watalii jijini Arusha na mapato yatokanayo na utalii.

Kwa mujibu wa Myonga, TFS imejipanga kushiriki kikamilifu kwa kutoa ufadhili wa huduma na kifedha, pamoja na kutumia majukwaa mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kutangaza utalii wa misitu na nyuki (api-tourism).

Aidha, alisema washiriki wa mbio hizo watapata fursa ya kutembelea vivutio vya misitu ikiwemo Shamba la Miti Meru na Ziwa Duluti kabla na baada ya tukio, huku mipango ikiwekwa kuhakikisha katika msimu ujao wa 2027 njia ya mbio inapita ndani ya hifadhi hizo ili kuongeza mvuto wa utalii.

Aliongeza kuwa TFS itanufaika pia kwa kuanzisha mabanda ya maonyesho, kutengeneza vifurushi vya utalii, huduma za kambi katika eneo la Napuru na kushiriki katika hafla ya Gala Dinner itakayotoa jukwaa la kuitangaza sekta ya misitu na nyuki.

Kwa upande wake, Haffy Mohamed  kutoka Land Africa Safaris alisema wataendelea kushirikiana na TFS kuhakikisha tukio hilo linakuwa chachu ya kukuza utalii wa michezo nchini.

Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuunganisha sekta ya michezo na utalii ili kuongeza mchango wa rasilimali za asili katika uchumi wa Taifa.






 Na: Calvin Gwabara – Morogoro Tanzania.

Mradi wa Mpunga Himilivu kwa mabadiliko ya Tabianchi na Rafiki kwa Mazingira Barani Afrika (Climate-resilient and Eco-friendly Rice for Africa) (CERA) umechukua hatua muhimu katika kuboresha kilimo cha mpunga kwa kuendesha mafunzo maalum kwa wakusanyaji takwimu katika utafiti unaotarajia kufanyika kwenye Mikoa ya Morogoro, Shinyanga na Songwe nchini Tanzania.

Mtafiti Mkuu wa mradi Prof. Suzana Nchimbi Msolla akizungumza na watafiti hao kabla ya kuanza zoezi hilo.

Mafunzo hayo yamewaleta pamoja washiriki ambao watakuwa mstari wa mbele katika ukusanyaji wa taarifa kutoka kwa wakulima, hatua inayotarajiwa kusaidia kufanya maamuzi sahihi ya kisayansi kwenye utekelezaji wa mradi huo wa utafiti.

Akizungumza na watafiti hao wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mtafiti Mkuu wa mradi Prof. Suzana Nchimbi Msolla alitumia nafasi hiyo kueleza kwa kina kuhusu mradi wa CERA, akieleza malengo, muda wake pamoja na matarajio yake hasa katika  kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Prof. Msolla ameeleza kuwa mradi huo unalenga kuzalisha mbegu za mpunga zinazostahimili ukame pamoja na kuhamasisha matumizi ya mbinu rafiki kwa mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi yanayoleta athari kubwa katika uzalishaji wa mazao hasa zao la mpunga nchini Tanzania.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa wa watafiti hao kwenda kuzingatia usawa wa kijinsia kwa kueleza kuwa mradi unalenga kuwafikia zaidi wakulima wanawake katika maeneo yenye ukame ili kuhakikisha wanufaika wote wanashirikishwa.

Mtafiti huyo pia alizungumzia suala la kujenga uwezo kwa taasisi za ndani kwa kutoa mafunzo kwa watafiti na kuboresha miundombinu ya utafiti wa kilimo.

“Ubora wa takwimu mtakazokusanya ndio utakaoamua mafanikio ya mradi huu na utekelezaji wake hivyo nisihi kutumia utaalamu mlionao na huu mtakaopewa kwenye mafunzo haya kuhakikisha mnapata taarifa sahihi kutoka kwa wakulima,” alisisitiza Prof. Msolla.

Kwa upande wake Mtafiti Mkuu Msaidizi wa mradi huo Dkt. Emanuel Malisa, ambaye aliwasilisha mada kuhusu wajibu, maadili na mwenendo wa wakusanyaji takwimu katika kazi za utafiti amesema wakusanyaji takwimu wanapaswa kuwa waaminifu, wasiwe na upendeleo, walinde siri za washiriki, na wahakikishe wanapata ridhaa ya washiriki kabla ya kuanza mahojiano.

Dkt. Malisa aliongeza kuwa wakusanyaji takwimu hao wanawakilisha mradi mbele ya jamii, hivyo wanapaswa kuzingatia heshima na weledi wa hali ya juu katika kazi zao kwenye kila eneo mabalo watapita kwakuwa tamaduni na mila za maeneo zinatofautiana hivyo wahakikishe wanazingatia mambo hayo ili waweze kupata ushirikiano kwa wakulima na jamii watakayoikuta.

Mafunzo hayo pia yalijumuisha mbinu za kufanya mahojiano, matumizi ya teknolojia ya ukusanyaji takwimu kama KoboToolbox, pamoja na namna ya kukabiliana na changamoto za washiriki kutokutoa taarifa.

Washiriki walipata fursa ya kufanya mazoezi kwa vitendo kupitia uigaji wa hali halisi ya kazi (simulation), hatua iliyowawezesha kujiandaa vizuri kabla ya kwenda kukusanya takwimu halisi kwa wakulima.

Matokeo ya Utafiti ya mradi wa CERA yanatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika kuongeza uzalishaji wa mpunga, kuimarisha ustahimilivu wa kilimo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, na kuboresha usalama wa chakula nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA MAFUNZO HAYO.









Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga amewataka Watumishi wa Wizara ya Nishati kuendelea kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini ili kufanikisha ajenda hiyo  ambayo kinara wake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ameeleza kuwa ajenda ya nishati safi ya kupikia tayari imeanza kuonesha mafanikio nchini na hivyo kupelekea Tanzania kutambuliwa katika maeneo mbalimbali duniani ikiwemo katika nchi zilizo katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Kamishna Luoga amesema hayo tarehe 18 Machi 2026 jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha Tatu cha Mkutano wa Pili wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Nishati kwa niaba ya Ma-Katibu Wakuu wa Wizara ya Nishati.

“Katika Mkutano wa SADC ambao Tanzania ilishiriki hivi karibuni, kupitia hotuba mbalimbali zilizotolewa katika mkutano huo ikiwemo ya mgeni rasmi ambaye ni Rais wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa aliitambua na kuipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, lakini pia katika maazimio ya mwisho yaliyoandaliwa na sekretarieti ya SADC, nchi zote za SADC zilitakiwa kuunga mkono juhudi hizo za Tanzania.” Amesema Kamishna Luoga

Kutokana na hilo, amempongeza Rais, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi anazochukua kufanikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia, pia amewapongeza Watumishi Wizara ya Nishati kwa kufanikisha juhudi hizo ambazo zinalenga kuimarisha afya za watanzania na kupunguza uharibifu wa mazingira.

Aidha, katika kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi kilicholenga kujadili, kutoa maoni, ushauri na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2026/2027, Mhandisi Luoga amewataka wajumbe wa Baraza kujiridhisha kuhusu maeneo yote muhimu ya vipaumbele vya Wizara kama yametengewa fedha ili kuwezesha Wizara kuhudumia watanzania kwa ufanisi.

Vilevile, amewataka Watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao na kujiepusha na utoro, rushwa na kutanguliza uzalendo katika kuwahudumia watanzania.

Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Nishati umehudhuriwa pia na Viongozi wa TUGHE Mkoa na Tawi la Nishati, pamoja wawakilishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara.



Na. Jordan Mbwambo, WF - Dodoma

Wizara ya Fedha kupitia Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali, inaendelea na uchambuzi wa bajeti ya sekta ya uzalishaji kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Sekta hiyo inajumuisha Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Ardhi, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Madini.

Hatua hiyo inalenga kuchambua na kujadili mipango na mapendekezo ya bajeti ya sekta muhimu za uzalishaji ili kuhakikisha yanazingatia vipaumbele vya Taifa, sera za maendeleo, mikakati ya kitaifa pamoja na miongozo ya upangaji na uandaaji wa bajeti.

Kikao hicho kimeongozwa na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali, Bw. Fundi Makama na kuhudhuriwa na Wakurugenzi wa Sera na Mipango pamoja na wataalamu kutoka wizara na sekta husika.

Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma ambapo, washiriki walipata nafasi ya kujadili kwa kina namna bajeti za sekta za uzalishaji zinavyoweza kuyafikia malengo yaliyowekwa kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kuimarisha uchumi wa Taifa na kuchochea maendeleo endelevu.
Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali, Bw. Fundi Makama, akiongoza kikao kazi cha wataalamu wa Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa cha kupitia, kuchambua na kujadili mipango na mapendekezo ya bajeti yaliyowasilishwa na Sekta ya Uzalishaji ikiwemo, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Ardhi, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Madini ili kuhakikisha kuwa yanazingatia vipaumbele na Mipango ya Taifa, sera na mikakati ya maendeleo, pamoja na miongozo ya upangaji na uandaaji wa bajeti, kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, (Treasury Square) jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mipango na Bajeti, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Godfrey Machabe, akiwasilisha vipaumbele vya wizara hiyo wakati wa Kikao Kazi cha wataalam wa Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa cha kupitia, kuchambua na kujadili mipango na mapendekezo ya bajeti yaliyowasilishwa na Sekta Elimu ili kuhakikisha kuwa yanazingatia vipaumbele na Mipango ya Taifa, sera na mikakati ya maendeleo, pamoja na miongozo ya upangaji na uandaaji wa bajeti, kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, (Treasury Square) jijini Dodoma.


Mkurugenzi kutoka, Idara ya Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini, Tume ya Taifa ya Umawagiliaji, Dkt. Consolatha Kapinga, akiwasilisha vipaumbele vya Tume hiyo wakati wa Kikao Kazi cha wataalam wa Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa cha kupitia, kuchambua na kujadili mipango na mapendekezo ya bajeti yaliyowasilishwa na Sekta ya Elimu ili kuhakikisha kuwa yanazingatia vipaumbele na Mipango ya Taifa, sera na mikakati ya maendeleo, pamoja na miongozo ya upangaji na uandaaji wa bajeti, kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, (Treasury Square) jijini Dodoma.
Wataalam wa Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, wakifuatilia Kikao kazi cha kupitia, kuchambua na kujadili mipango na mapendekezo ya bajeti yaliyowasilishwa na Sekta ya Uzalishaji ikiwemo, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Ardhi, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Madini ili kuhakikisha kuwa yanazingatia vipaumbele na Mipango ya Taifa, sera na mikakati ya maendeleo, pamoja na miongozo ya upangaji na uandaaji wa bajeti, kikao hicho kinafanyika katika Ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, (Treasury Square) jijini Dodoma.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF - Dodoma)

Na: Dk. Reubeni Lumbagala

Wizara ya Maji inatekeleza programu mbalimbali za kimaendeleo zenye lengo la kuboresha usambazaji wa maji kwa wananchi wake na kufanikisha miradi mingine ya umwagiliaji ambayo ni kichochea muhimu kwa ustawi wa shughuli za kiuchumi kama kilimo, viwanda na huduma nyingine za kijamii.

Miongoni mwa mipango inayosimamiwa na Wizara ya Maji yenye lengo la kuchochea kasi ya usambazaji wa maji kwa wananchi ni Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (Water Sector Development Programme - WSDP) ambayo sasa imetimiza miaka ishirini tangu ilipozinduliwa mwaka 2006. 

Machi 16 hadi Machi 22, 2026, Wizara ya Maji inaadhimisha Wiki ya Maji ambapo kilele chake ni Machi 22 ambayo ni Siku ya Maji Duniani. Katika Wiki ya Maji, Wizara ya Maji inaratibu makongamano, mijadala na maonyesho mbalimbali yenye lengo la kutoa elimu kwa wananchi juu ya masuala mbalimbali ya maji na kuonyesha mafanikio yaliyofikiwa katika usambazaji wa huduma ya maji.

Machi 17, 2026, Waziri wa Fedha, Balozi Khamisi Omar alishiriki ufunguzi wa Mkutano wa Mapitio ya Pamoja ya Sekta ya Maji (Joint Water Sector Review - JWSR) uliofanyika katika Ukumbi wa Mkutano wa Cate Convention Centre, mjini Morogoro ambapo aliipongeza Wizara ya Maji kwa mafanikio ya usambazaji wa maji ikiwemo programu ya WSDP. 

Kwa mujibu wa Balozi Omar, programu ya WSDP imefanikiwa kuboresha upatikanaji wa maji ambapo awali maeneo ya mjini yalikuwa yakipata maji kwa asilimia 74 lakini sasa maji yanapatikana kwa asilimia 92.5. Kwa maeneo ya vijijini, upatikanaji wa maji ulikuwa asilimia 54 lakini sasa upatikanaji wa maji umefikia asilimia 85.2.

Ni jambo la faraja kuona programu ya WSDP imeleta matokeo chanya katika miaka ishirini ya utekelezaji wake ambapo usambazaji wa maji kwa wananchi umeimarika sana. Kimsingi, usambazaji maji kwa wananchi kufikia asilimia 92.5 kwa maeneo ya mjini na asilimia 85.2 kwa vijijini ni mafanikio makubwa ya kupongezwa. Maji ni raslimali yenye mnyororo mkubwa wa thamani ikizingatia maji ni uchumi katika ulimwengu huu wa maendeleo.

Iko hivi: Maji yamefungamanishwa na sekta nyingine za kiuchumi kama kilimo, viwanda, migodi, uvuvi, ufugaji samaki, ambapo mafanikio ya maji yanagusa maendeleo ya sekta nyingine moja kwa moja. Kwa upande wa Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amesema vijiji 10,758 vimeshapata maji ya uhakika huku vijiji 1,575 kati ya 12,333 vikiwa bado havijafikiwa na maji ya uhakika huku akisisitiza kuwa mpango wa serikali ni kufikisha maji kwa asilimia mia moja maeneo yote ya mjini ma vijijini.

Ni faraja kuona serikali ikionyesha utashi mkubwa wa kisiasa kuhakikisha usambazaji wa maji kwa wananchi unafikiwa kikamilifu. Mathalani, kwa mujibu wa Balozi Omar, katika kipindi cha mwezi Januari hadi Disemba 2025, serikali imetumia shilingi bilioni 883.93 katika utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira. Ikumbukwe kuwa, bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ilikuwa shilingi trilioni 1.01, jambo ambalo halijawahi kutokea katika historia ya nchi yetu huku fedha nyingi zikielekezwa katika kugharamia miradi ya maendeleo ya huduma za maji.

Wiki ya Maji inayoendelea inachagizwa na kaulimbiu isemayo "Raslimali za Maji na Usawa wa Kijinsia." Ni muhimu sana wananchi kushiriki kutunza vyanzo vya maji kwa maendeleo endelevu. Vilevile, ni muhimu kuhakikisha miundombinu ya maji inatunzwa bila kuharibiwa au kuhujumiwa. Pia, taasisi na watu binafsi wanaodaiwa fedha na mamlaka za maji wahakikishe wanalipa madeni hayo ili kuzijengea uwezo mamlaka hizo na Wizara ya Maji kuboresha zaidi usambazaji wa maji kwa wananchi. Maji ni uhai, maji ni afya, maji ni uchumi na maji ni maendeleo. Tafakari.


Maoni: 0620 800 462









Na Mwandishi Wetu,Zanzibar

Chama Cha Mapinduzi kimesema Marehemu Rais John Joseeph Magufuli alikuwa Kiongozi shujaa na Mzalendo kwa Taifa lake wakati wote wa maisha yake kabla na baada ya kuwa Rais.

Pia kimesisitiza juhudi na ushujaa wa kiongozi huyo, uliifanya Tanzania kuingia katika orodha ya nchi zenye Uchumi wa kati.

Hayo yameelezwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar , Idara ya Itikadi , Uenezi na Mafunzo , Khamis Mbeto Khamis alipozungumza na Kituo kimoja cha Habari Kisiwani unguja

Mbeto alisema katika uongozi wake kabla ya umauti kumfikia, alimtaja Dk Magufuli ndiye aliyeanzisha Ujenzi wa Reli ya Mwendokasi, Bwawa la kufua Umeme wa Maji , Ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi ,utengenezaji wa Vivuko , Meli mpya Ziwa Victoria na kuiptia Mikataba ya Migodi ya Madini.

"Ujasiri wa Rais Magufuli utakumbukwa milele. Kimekufa kiwiliwili chake ,fikra na maono yake vitabaki. Alibuni mambo akayasimamia hadi yalipotoa matokeo chanya. Alifanya mengi akingozwa na shime ya Uzalendo' Alisema Mbeto .

Aidha Katibu huyo Mwenezi alisema katika mambo ambayo Watanzania watayakumbuka , ni kiongozi huyo kufanya uamuzi wa Serikali yake kuhamishia Makao Makuu ya nchi kuwa Jijini Dodoma .

Alisema toka Awamu ya Kwanza uamuzi wa Serikali ya Rais Mwalimu Julisu Nyerere, ulipitisha Azimio la Makao Makuu kuhamishiwa Dodoma lakini kwa miaka yote azimio hilo halikuwezekana hadi Awamu ya Tano chini ya Dk Magufuli .

Mbeto aliongeza kusema Dk Magufuli aliongozwa zaidi na Uzalendo ,uaminifu na Upendo kwa nchi yake , kwani alipiga vita hadharani uzembe ,ufisadi na ukwapuzi wa mali za Umma bila kumuonea yeyote muhali.

"Utumishi wake wa muda mfupi madarakani umeacha alama na athari nyingi za kimaendeleo. Kiongozi huyo atakumbukwa kwa ujasiri wake wa kusimamia tunu za Amani, Umoja na Mshikamano wa Taifa" Alisisisitiza

Pia Mbeto alisema muda wote katika uongozi wake alisimama kidete kuhakikisha rasilimali za Taifa zinainufaisha nchi kimaendeleo huku akipiga vita maadui Ujinga ,Umasikini na Maradhi kwa vitendo .

"Hakumuonea aibu kiongozi yeyote alipoonyesha kutosimamia vyema maslahi ya Taifa. Alimtumbua yeyote bila woga na kuteuwa wengine .Pia alihakikisha rasilimali na Vitega uchumi vya kisiasa vinakinufaisha chama chake "Alieleza Mbeto

Hata hivyo Katibu huyo Mwenezi alisema Dk Magufuli akiwa madarakani ndiye aliyefufua Shirika la Ndege la ATCL kwa Serikali yake kununua Ndege mpya, Ujenzi wa Daraja la Tanzanite, barabara nyingi za lami na madaraja ya juu.

"Dk Magufuli hakuendekeza urafiki au kujuana. Alihakisha katika Serikali kunakuwepo nidhamu, uchapakazi na utumishi wenye maslahi kwa Taifa. Aliitazama nchi kwanza kuliko kitu chochote " Alieleza Mbeto.


Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani yameendelea kupewa uzito mkubwa Mjini Songea, ambapo jamii imehamasishwa kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa rasilimali maji na mazingira.
Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Songea (SOUWASA) imefanya shughuli mbalimbali za uelimishaji kwa wananchi kuhusu uhifadhi wa vyanzo vya maji, Katika kuadhimisha wiki hiyo, jumla ya miti 500 imepandwa katika bonde la mto Luhira, ambalo ni chanzo kikuu cha maji kwa wakazi wa manispaa hiyo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo leo Machi 18, 2026, Mkurugenzi wa Usambazaji Maji wa SOUWASA, Mhandisi Jafari Yahya, amesisitiza umuhimu wa kulinda vyanzo vya maji kwa vitendo. Alieleza kuwa bonde la mto Luhira lina mchango mkubwa katika upatikanaji wa maji safi kwa wakazi wa Songea, hivyo linapaswa kuhifadhiwa kwa uangalifu mkubwa.

Amewataka wananchi kuacha vitendo vya uchomaji moto katika maeneo ya vyanzo vya maji, akibainisha kuwa moto husababisha uharibifu wa mazingira na kuhatarisha uwepo wa maji kwa muda mrefu. Pia amekemea suala la kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo hayo, akisisitiza kuwa uhifadhi wa vyanzo vya maji ni jukumu la kila mwananchi.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Mhe. Abraham Mbunda, amesema kuwa upandaji miti ni hatua muhimu katika kulinda mazingira na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji, Amesema kuwa maji ni uhai, hivyo kila mtu anapaswa kushiriki kuyahifadhi.

Aidha, amewataka SOUWASA kuendelea kutoa elimu kwa madiwani ili waweze kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi katika maeneo yao. Amesema elimu hiyo itasaidia kuongeza uelewa na kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa vyanzo vya maji.

Naye Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja SOUWASA, Bi. Baby Bicko, ameeleza kuwa Wiki ya Maji Duniani huadhimishwa kila mwaka kuanzia Machi 16 hadi 22, ikiwa na lengo la kuhamasisha jamii kutambua thamani ya maji kama rasilimali muhimu.

Ameongeza kuwa kauli mbiu ya mwaka huu isemayo “Maji na Jinsia,” ikilenga kuhimiza ushiriki wa watu wa jinsia zote katika kulinda rasilimali maji, akibainisha kuwa miti ina mchango mkubwa katika kuhifadhi vyanzo vya maji, hivyo ni muhimu kuendelea kuipa kipaumbele.

Kwa ujumla, Wiki ya Maji Duniani imeendelea kuwa jukwaa muhimu la kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa maji na uhifadhi wa mazingira, huku matarajio yakiwa ni kuona mabadiliko chanya yanayodumu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.






Na Mwandishi Wetu, Tanga.
WANANCHI wa Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga wanatarajiwa kunufaika zaidi kiuchumi kupitia uwekezaji wa Serikali katika sekta ya kilimo cha mwani, hatua inayolenga kuongeza thamani ya mazao ya bahari na kuboresha maisha ya jamii za pwani.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kaushio jipya na mashine mbili za kisasa za kusaga mwani uliofanyika tarehe 16 Machi 2026 katika Kijiji cha Kichaka Miba, Wilaya ya Mkinga, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. Ummy H. Nderiananga, amesema mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuimarisha uchumi wa wananchi wa maeneo ya pwani.


Mradi wa Kuimarisha Usalama wa Bahari unaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), na unatekelezwa na Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP) Tawi la Mwanza kwa ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga ambapo Lengo lake ni kuimarisha ufuatiliaji na ulinzi wa bahari pamoja na kuongeza thamani ya rasilimali za baharini kwa manufaa ya jamii.


Mhe. Nderiananga amesema kupitia mradi huo, Serikali imenunua boti mbili za doria, kujenga kaushio la kisasa la mwani, kusimika mashine za kusaga mwani na kutoa mafunzo kwa vikundi vya wakulima. Ameongeza kuwa hatua hizo zitaboresha ubora wa mwani, kupanua masoko, kuongeza kipato cha wakulima na kusaidia kuzuia vitendo vya kihalifu baharini.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP), Dkt. Guvenail Mkonoko, amesema kabla ya utekelezaji wa mradi huo wataalamu walifanya tathmini iliyobaini changamoto za mbinu duni za kilimo, ukaushaji usio salama na ukosefu wa miundombinu ya kisasa ya uchakataji.




Naye mwakilishi wa wakulima wa mwani, Bi. Mwamvua Bwebwe, Ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kuongeza uzalishaji, kupunguza upotevu wa mazao na kuboresha kipato chao.






=MWISHO=
KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Juma Mwenda amesema Mamlaka hiyo itaanzisha utaratibu mpya wa kuingiza mafuta ya kupikia Tanzania Bara kutoka Zanzibar ili kuwezesha kufanyika kwa biashara halali ya mafuta na kuzuia mafuta ya magendo.

Amesema hayo Machi 17, 2026 katika Hoteli ya Madinat Al Bahr wakati wa Iftari iliyoandaliwa na TRA Zanzibar na kuhudhuriwa na watumishi wa TRA pamoja na Walipakodi huku mgeni rasmi akiwa ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema utaratibu huo unalenga kuingiza mafuta yanayowiana na upungufu uliopo ili kulinda viwanda vya ndani ambapo vitatolewa vibali maalum kwa waingizaji hao wa mafuta.

Amesema TRA inatambua mchango wa walipakodi wote wakiwemo waingizaji wa mafuta ndiyo maana imeandaa Iftari na kuwakutanisha pamoja na watumishi wa TRA.

Amesema TRA itaendelea kuwezesha biashara za walipakodi wote nchini na kuwapongeza watumishi wa TRA kwa kujituma na kuvuka malengo ya makusanyo kwa kila mwezi.





Top News