Na. Edmund Salaho - Dodoma
Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limeendelea kuimarisha safu yake ya Uongozi ili kuboresha utendaji kazi wa Shirika hilo kwa kuwaapisha na kuwavisha vyeo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi (1) Makamishna Wasaidizi wa Uhifadhi (3) pamoja na Afisa Uhifadhi Mkuu (1) zoezi ambalo limefanyika leo Aprili 25, 2026 katika Ofisi Kiunganishi za TANAPA jijini, Dodoma.
Akizungumza katika hafla hiyo ya kuwavisha vyeo Makamishna hao Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Musa Nassoro Kuji,alitoa msisitizo kwa Makamishna hao kufanya Kazi kwa bidii, weledi na kusikiliza watu wanaowaongoza ili kuleta tija zaidi pamoja na kufikia malengo ya Shirika na Taifa kwa ujumla.
"Nendeni mkachape kazi kwa bidii na weledi huku mkiishi viapo vyenu mlivyoapa leo. Kiongozi mzuri ni yule anaesikiliza mawazo ya watu wake anaowaongoza hivyo, mkasikilize watu mnaowaongoza" alisisitiza Kamishna Kuji.
Akitoa shukurani kwa niaba ya Makamishna wapya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Abdallah Omary Kiwango alishukuru Bodi ya Wadhamini TANAPA pamoja na Uongozi wa Shirika kwa imani kubwa walionayo juu yao.
"Napenda kuchukua nafasi hii kwa niaba ya Makamishna wenzangu kuishukuru Bodi ya Wadhamini na Uongozi wa Shirika kwa kutuamini na kutukabidhi majukumu haya kama tulivyotoka kuapa, tunaahidi kufanya kazi kwa bidii na weledi wa hali ya juu ili kufanikisha malengo ya Taasisi ya kuendeleza Uhifadhi endelevu na kukuza Utalii katika Hifadhi za Taifa"
"Leo sio mwisho wa safari bali ni mwanzo wa dhamira mpya. Tunachukua majukumu haya tukiwa na nia thabiti ya kufanya kazi kwa weledi, nidhamu na uadilifu wa hali ya juu. Tuko tayari kujitoa kwa nguvu zote kuhakikisha tunalinda rasilimali za Taifa letu kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho" alisema Kamishna Kiwango
Makamishna wa Uhifadhi walioapishwa leo ni Abdallah Omary Kiwango ambaye ameapishwa kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Makamishna Wasaidizi wa Uhifadhi, Philbert Michael Ngoti, Joachim Shaaban Tesha, Michael Joseph Tarimo pamoja na Afisa Uhifadhi Mkuu, Manendo Peter Maziku.







.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)

Na Augusta Njoji


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

