Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amesema dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa ni fursa muhimu ya kukuza sekta ya viwanda, kuongeza thamani ya malighafi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa. 

Akizungumza katika kikao cha mawaziri kilichofanyika jijini Istanbul nchini Uturuki, Juni 5, 2026, kilichobeba mada ya Mageuzi ya Kijani ya Viwanda: Mtazamo wa taka sifuri na urejeshaji bidhaa, Kapinga amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta ya viwanda huku ikisisitiza matumizi bora ya rasilimali na uhifadhi wa mazingira.

Ameeleza kuwa dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa inatoa fursa kwa nchi zinazoendelea kupitia matumizi endelevu ya malighafi, kupunguza upotevu baada ya mavuno, kupunguza uzalishaji wa taka na kuongeza thamani ya bidhaa zinazotengenezwa viwandani. 

Kapinga amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kuunganisha masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sera na mipango ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ufanisi wa nishati na teknolojia rafiki kwa mazingira.


Aidha, amesisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi ya kijani yanategemea uwekezaji wa kutosha, upatikanaji wa teknolojia za kisasa pamoja na ushirikiano madhubuti kati ya serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo. 

Amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuendeleza viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali, kudhibiti taka na kuvutia uwekezaji huku akiwakaribisha wafanyabiashara kuwekeza nchini kwa lengo la kujenga uchumi imara na shindani.

Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Uturuki kupitia taasisi ya Zero Waste Foundation inayosimamiwa na Mwenza wa Rais wa Uturuki Bibi Emine ErdoÄŸan na umeleta pamoja washiriki zaidi ya 3,000 kutoka nchi zote duniani, pamoja na taasisi za kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Mataifa, Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu na Shirika la Maendeleo na Biashara la Umoja wa Mataifa (UNCTAD).

-Elimu bila malipo, Bima ya Afya kwa Wote ni ushindi

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa, Stephen Wasira, amesema ujamaa bado ni msingi mkuu unaoendesha sera na mipango ya maendeleo nchini.

Akizungumza na wanachama wa CCM mjini Moshi, leo Juni 6 2026, Wasira alisema alikana madai kuwa mfumo huo umepitwa na wakati.

"Wale wanaojidanganya hawaujui. Misingi inayoendesha nchi sasa ni ileile ya ujamaa. Tuanzie na elimu bila malipo, tuendelee na jitihada za kuanzisha Bima ya Afya kwa wote. Haya yote ni mafanikio ya ujamaa," alisema.

Wasira alitoa mfano wa Mkoa wa Kilimanjaro, akibainisha kuwa kama sio ujamaa, ardhi na mashamba ya kahawa yangekuwa yamenunuliwa na watu binafsi na wananchi wasingeweza kumiliki.

"Kama hapa Kilimanjaro tungekosa ujamaa, kahawa yote ingenunuliwa. Ni uongo kusema ingekuwa bado mikononi mwa wananchi," alieleza.

Pia, alizungumzia umuhimu wa uwekezaji wa sekta binafsi, akisema ni jambo la kawaida na la lazima kwa ukuaji wa uchumi wa nchi.

Akimnukuu Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere alisema: "Watu wote hawatakuwa na mapato sawa. Mkulima wa nyanya Kilimanjaro na mchimbaji wa gesi Lindi hawawezi kulingana. Hata wachimbaji madini nao hawalingani na wale wasiochimba."

Kwa mujibu wa Wasira, serikali inaleta haki kwa kuwatoza kodi wenye uwezo na kuwasaidia wasio na uwezo.

"Huwezi kujenga nchi bila mtaji. Wenye mtaji ni watu binafsi na kampuni. Kazi yetu ni kuwatoza kodi na kuwasaidia wanyonge," alisema.











 

 Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu ametoa onyo kali kwa watu wanaojihusisha na udanganyifu na uchakachuaji wa taarifa katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kusisitiza itaendelea kuchukua hatua ili kuhakikisha misingi ya uadilifu na uwazi inazingatiwa ipasavyo.

Bangu,ametoa onyo hilo baada ya kufanya kikao kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro, kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Amesema mfumo huo unaendelea kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya uadilifu na uwazi, huku WRRB ikiendelea kushirikiana na mamlaka za mikoa, wilaya na halmashauri kusimamia utekelezaji wake.

“Moja ambalo nataka kuliweka wazi kwa Watanzania ni kwamba mfumo huu unafanya kazi kwa kuzingatia uadilifu. Kuna maeneo mengi mfumo unafanya vizuri, lakini tumeanza kuona baadhi ya watu wakiingiza taarifa zisizo sahihi kwenye mfumo kwa lengo la kujipatia fedha. Nataka nitoe onyo kali kwao kwamba tunasimamia mfumo huu kwa karibu na hatua stahiki zitachukuliwa,” amesema Bangu.

Ameeleza kuwa WRRB imeweka utaratibu wa kufanya uhakiki wa bidhaa zilizopo maghalani kabla ya kutolewa kwa katalogi za mauzo ili kuhakikisha wanunuzi wanapata taarifa sahihi kuhusu kiasi cha mazao yaliyopo.

Bangu pia amewahamasisha wakulima wa ufuta kuendelea kuuza mazao yao kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kupata masoko yenye ushindani na kuongeza kipato chao.

Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha mazingira ya biashara ya mazao kupitia mfumo huo, jambo linalowezesha wakulima kunufaika zaidi na jasho lao.

“Wilaya ya Malinyi imeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mfumo huu. Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto, lakini sasa tumeridhishwa na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wakulima wananufaika na mapato yao yanaongezeka,” amesema.

Katika hatua nyingine, WRRB imekabidhi msaada wa vifaa vya usafi na vyakula kwa Hospitali ya Wilaya ya Malinyi ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za uwajibikaji kwa jamii.

Akikabidhi msaada huo katika Wodi ya Wazazi ya hospitali hiyo, Bangu amesema WRRB itaendelea kushirikiana na jamii sambamba na kutekeleza majukumu yake ya kusimamia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala nchini.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Dk. Julius Nyasongo, aliyepokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Wakili Sebastian Waryuba, ameishukuru WRRB kwa msaada huo akisema utasaidia kuboresha ustawi wa akina mama wanaopata huduma hospitalini hapo.

“Msaada huu utakuwa na mchango mkubwa kwa akina mama wanaopata huduma katika hospitali yetu. Tunawashukuru WRRB kwa kuendelea kushirikiana na sekta ya afya na jamii kwa ujumla,” amesema Dk. Nyasongo.

     
-Ni baada ya kuahidiwa kulipwa deni la sh. milioni 181


MKAZI WA CHUNYA, Bi Agnes Obeid Ole amelia machozi ya furaha mbele ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba baada ya kusikilizwa kero yake na kutolewa uamuzi kwamba mdaiwa atafutwe na amlipe sh. milioni 181 anazozidai.

“Kamanda wa Polisi mtafute huyo bwana. Mahakama ilikwishatoa hukumu na ikampa mama ushindi. Asakwe popote alipo, arudishe vifaa na arudishe fedha za huyu mama,” amesema Waziri Mkuu na kuamsha shangwe kwa wananchi waliokuwepo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Juni 6, 2026) wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya soko la Ifunda, wilayani Iringa, mkoani Iringa.

Akielezea kero yake, Bi. Agnes alisema kuwa kabla mumewe hajafariki, walikuwa wanachimba dhahabu kwenye mgodi wao huko Chunya lakini walimuomba rafiki yao, Bw. Lelevasi Fishulo mwenye mashine za kuchenjua washirikiane naye ili baadaye wagawane naye faida.

"Tulipata sh. milioni 362 lakini akasema amepata dharura na akaomba atulipe baadaye. Tukamkubalia. Mgao wetu ulikuwa sh. milioni 181 lakini siku ya kulipwa mume wangu akafariki, kwa hiyo nikaacha kufuatilia sababu ya maombolezo."

Bi. Agnes anasema baada ya mwaka mmoja kupita akamfuata kudai hela yake lakini hakumpa. "Nikaenda Serikali ya kijiji akaitwa kwa miezi mitatu hakutokea, nikaenda polisi akaitwa lakini ikapita miezi minne hakutokea ndipo nikaenda mahakamani kwa masuala ya mirathi," amesema.

Amesema alifungua kesi ya madai ya kudhulumiwa mali baada ya mumewe kufariki na mahakama ikampa haki ya kuwa msimamizi wa mirathi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemwagiza Kaimu Meneja TANROADS Mkoa wa Iringa, Mhandisi Hosea Machaka atafute fedha sh. milioni 47 za kumlipa Bi. Subira Mdoka ambaye anadai fidia ya shamba alilotoa kupisha ujenzi wa uwanja wa ndega wa Nduli.

Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa TANROADS walifanya malipo ya fidia ya eneo lenye ekari 11 kwa Bw. Taaban ilhali eneo likiwa na mgogoro ambao ulikuwa umeshafikishwa mahakamani.

"Tafuteni akiba zenu mumlipe huyu Mama fedha yake kabla ya tarehe 30 Juni, 2026, kisha ninyi muendelee kumdai huyo bwana aliyewatapeli. Katibu Tawala wa Mkoa mtafuteni huyo bwana huko chuoni aelezwe haya maamuzi," amesema Waziri Mkuu.

Mhandisi Machaka alikiri kuwa walimlipa Bw. Taaban fedha hiyo wakati hukumu ya mahakama ilimpa ushindi Bi. Subira na wakawa wanamwambia asubiri fedha itakayorejeshwa na Bw. Taaban ndipo wamrejeshee.


-Walimu 35 walioshinda tuzo za ufundishaji kupatiwa viwanja

WALIMU nchini wamehimizwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kujituma na kutumia mbinu bunifu za ufundishaji ili kuimarisha ubora wa elimu na kuchangia maendeleo ya taifa. Aidha, walimu 35 walioibuka washindi katika Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji wameelekezwa kupatiwa viwanja karibu na maeneo yao ya kazi kama sehemu ya motisha.

Akizungumza Juni 6, 2026 jijini Dar es Salaam katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano hilo kwa walimu wa elimu ya awali, msingi na sekondari, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe, amesema walimu wana mchango mkubwa katika kuwalea na kuwaandaa wanafunzi kuwa wananchi wenye maarifa, stadi na maadili mema yanayohitajika katika jamii.

Prof. Shemdoe amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango wa walimu kwa kuweka mazingira bora ya kazi pamoja na motisha mbalimbali zinazolenga kuongeza ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji.

Aidha, amewataka walimu kuendelea kutumia mbinu za kisasa na bunifu katika ufundishaji ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kufikiri kwa kina, kubuni na kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.

Amesema tuzo hizo zinalenga kuhamasisha ubora, uwajibikaji, ubunifu na kujituma katika kazi ya kufundisha, akisisitiza kuwa maendeleo ya taifa yanategemea kwa kiasi kikubwa ubora wa rasilimali watu inayozalishwa kupitia mfumo wa elimu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Husna Sekiboko, amesema mafanikio katika sekta ya elimu yanahitaji ushiriki wa wadau wote, wakiwemo wazazi, walimu, wanafunzi pamoja na viongozi wa jamii.

Amesema maboresho yanayoendelea katika mifumo ya uongozi na utawala yanalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za elimu na kuimarisha matokeo ya ujifunzaji kwa wanafunzi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba, amesema Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji la mwaka 2026 ni la nne kwa walimu wa elimu ya awali na msingi, na la pili kwa walimu wa elimu ya sekondari, likihusisha halmashauri zote 184 za Tanzania Bara.

Amesema kwa upande wa elimu ya awali, shindano hilo limejikita katika kuimarisha umahiri wa ufundishaji wa stadi za kusoma, hususan matamshi ya sauti za herufi ambazo zimekuwa changamoto kwa baadhi ya wanafunzi katika kuzitamka na kuzitumia kwa usahihi wakati wa kuunda silabi na maneno.

“Lengo la shindano hili ni kusaidia kutatua changamoto za ufundishaji na ujifunzaji wa stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) ili kuhakikisha wanafunzi wanazimudu stadi hizo muhimu wanapofikia Darasa la Tatu. Eneo hili la ushindani linaunga mkono maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha watoto wote wanasoma kwa ufasaha wanapofikia Darasa la Tatu,” amesema Dkt. Komba.

Ameeleza kuwa maandalizi ya shindano hilo yalihusisha uchambuzi wa matokeo ya wanafunzi kupitia taarifa za Baraza la Mitihani la Tanzania pamoja na maeneo mapya yaliyoingizwa katika mtaala, ili kubaini maeneo yanayohitaji kupewa kipaumbele.

Kwa mujibu wa Dkt. Komba, walimu walitakiwa kuandaa andalio la somo, kujirekodi wakifundisha kwa muda wa dakika 10 hadi 15, na kupakia video pamoja na andalio hilo katika mfumo wa kidijitali wa National Teaching Skills Competition System kwa ajili ya tathmini.

Jumla ya walimu 3,153 walijisajili katika mfumo huo, huku walimu 1,263 sawa na asilimia 40 wakifanikiwa kupakia video zao kwa ajili ya tathmini katika ngazi ya halmashauri.

Amesema tathmini ilifanyika katika ngazi tatu ambazo ni halmashauri, mkoa na taifa kwa kuzingatia vigezo mbalimbali, ikiwemo ubora wa maudhui, mtiririko wa somo, matumizi ya mbinu shirikishi, matumizi ya TEHAMA, matumizi ya zana za kufundishia, ukuzaji wa stadi za karne ya 21 pamoja na matumizi ya upimaji endelevu katika mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji.

Katika mchujo wa shindano hilo, video 751 zilifanikiwa kuingia ngazi ya mkoa kutoka video 1,263 zilizotathminiwa katika ngazi ya halmashauri. Kati ya hizo, video 232 zilichaguliwa kuingia ngazi ya taifa.




Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

SERIKALI kupitia Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, imetangaza rasmi orodha ya washiriki 100 waliofanikiwa kuingia hatua inayofuata ya Shindano la Vijana Uchumi Challenge 2026, baada ya kukamilika kwa mchakato wa uchambuzi wa maombi 7,852 yaliyowasilishwa kutoka mikoa mbalimbali nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Katibu wa Kamati ya Kitaifa ya Vijana Uchumi Challenge, Amina Sanga, amesema mwitikio mkubwa wa vijana katika shindano hilo unaonesha namna wanavyotambua nafasi yao katika kuchangia maendeleo ya uchumi wa Taifa kupitia ubunifu, ujasiriamali na mawazo yenye tija.

Amesema washiriki 100 waliofuzu hatua hiyo sasa wanatarajiwa kushiriki kambi maalum ya siku nne, ambapo watapatiwa mafunzo ya kitaalamu yatakayolenga kuboresha mawazo yao ya biashara na miradi ya maendeleo, pamoja na kuwajengea uwezo wa kufanya mawasilisho yenye ushawishi mbele ya majaji, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Katika hatua nyingine, Sanga ametangaza kuongezwa kwa zawadi za shindano hilo kufuatia ongezeko kubwa la washiriki na ubora wa mawazo yaliyowasilishwa na vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Kwa mujibu wa maboresho hayo, mshindi wa kwanza atajishindia shilingi milioni 50 badala ya shilingi milioni 30 zilizokuwa zimetangazwa awali. Mshindi wa pili atapata shilingi milioni 30, huku mshindi wa tatu akijinyakulia shilingi milioni 20.

Aidha, washiriki watakaoshika nafasi ya nne hadi ya kumi watazawadiwa shilingi milioni tatu kila mmoja kama sehemu ya kutambua mchango wao katika kuibua mawazo bunifu yenye uwezo wa kuchochea ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Mbali na zawadi za fedha, washiriki wote 100 bora watapatiwa vyeti vya utambuzi pamoja na fursa mbalimbali za mafunzo, ushauri wa kitaalamu na kuunganishwa na taasisi na wadau wanaoweza kusaidia utekelezaji wa mawazo yao.

Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza ushiriki wa vijana katika shughuli za uzalishaji na ubunifu, sambamba na kuimarisha mchango wao katika kukuza uchumi wa Taifa na kutengeneza ajira kupitia miradi yenye tija.




Na Janeth Raphael MichuziTv 

Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, amesema tasnia ya kahawa inaendelea kuwa nguzo muhimu ya uchumi wa taifa kutokana na mchango wake katika kuongeza kipato cha wakulima, kuingiza fedha za kigeni, kuzalisha ajira katika mnyororo mzima wa thamani na kuchochea maendeleo ya maeneo ya vijijini

Akizungumza  jijini Dodoma wakati wa kufunga Mkutano wa 16 wa Wadau wa Kahawa nchini, Chongolo amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi ya kukuza sekta ya kilimo, ikiwemo tasnia ya kahawa, ili iweze kutoa mchango mkubwa zaidi katika ukuaji wa uchumi na kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana.

Amesema mafanikio yanayoonekana katika sekta hiyo yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na wadau mbalimbali wa kahawa, jambo ambalo limewezesha utekelezaji wa mikakati yenye tija kwa maendeleo ya zao hilo.

“Mafanikio haya hayapatikani kwa bahati mbaya. Yanatokana na wadau kukaa pamoja, kujadiliana na kukubaliana mambo muhimu ya maendeleo ya tasnia hii. Tukisimamia kwa pamoja yale tunayokubaliana, tutaendelea kuongeza tija na mchango wa kahawa kwa uchumi wa nchi,” alisema Chongolo.

Waziri huyo amebainisha kuwa katika msimu uliopita wa biashara, zao la kahawa liliingiza zaidi ya dola za Marekani milioni 400, na hivyo kuwa zao la pili kwa kuingizia taifa fedha za kigeni baada ya tumbaku.

Aidha, amesema tasnia ya kahawa ni miongoni mwa sekta zenye fursa kubwa za kiuchumi kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya kahawa katika soko la dunia pamoja na soko la ndani. Hivyo, aliwataka wadau wote kuendelea kutumia kikamilifu fursa zilizopo ili kuongeza uzalishaji, ubora na ushindani wa kahawa ya Tanzania katika masoko mbalimbali.

Chongolo amesisitiza kuwa ushirikiano, ubunifu na uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa kahawa ni muhimu katika kuhakikisha sekta hiyo inakuwa chachu ya maendeleo ya uchumi na ustawi wa wananchi, hususan wakulima wa maeneo ya vijijini.

“Mahitaji ya kahawa yanaendelea kuongezeka duniani na ndani ya nchi. Hii ni fursa kubwa kwa wadau wote kuhakikisha wanaitumia ipasavyo ili kuongeza uzalishaji na kunufaika zaidi na soko linalokua kila siku,” alisisitiza.

NIANDIKIE Tena upya hii stor UPYA Kwa maboresho zaidi na MTIRIRIKO mzuri WA kihabari unaoeleweka na Kwa ajil ya Instagram ila Ibebe thima mzima ya stor husika fup 

KAHAWA YAENDELEA KUNG’ARA KIUCHUMI, YAINGIZA ZAIDI YA DOLA MILIONI 400

Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo amesema tasnia ya kahawa inaendelea kuwa nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania kwa kuongeza kipato cha wakulima, kuzalisha ajira na kuingiza fedha za kigeni.

Akifunga Mkutano wa 16 wa Wadau wa Kahawa jijini Dodoma, Chongolo alisema mafanikio ya sekta hiyo yanatokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau mbalimbali wa kahawa, hali iliyochangia kuimarika kwa uzalishaji na biashara ya zao hilo.

Amesema katika msimu uliopita wa biashara, kahawa iliingizia taifa zaidi ya dola za Marekani milioni 400 na kuwa zao la pili kwa kuingiza fedha za kigeni baada ya tumbaku.

Chongolo alibainisha kuwa ongezeko la mahitaji ya kahawa duniani na ndani ya nchi linafungua fursa kubwa zaidi kwa wadau kuongeza uzalishaji, kuboresha ubora na kuimarisha ushindani wa kahawa ya Tanzania katika masoko ya kimataifa.









Na Janeth Raphael MichuziTv

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amewataka watumishi wa Wizara ya Madini na taasisi zake kushiriki kikamilifu katika shughuli za michezo na mazoezi ya mwili, akieleza kuwa michezo ni nyenzo muhimu ya kuimarisha afya ya akili, kujenga mshikamano mahali pa kazi na kuongeza ufanisi wa utendaji.

Akizungumza katika Bonanza la Michezo lililowakutanisha watumishi wa Wizara hiyo pamoja na Tasisi zilizo chini yake, Dkt. Kiruswa amesema michezo ina mchango mkubwa katika kuboresha afya za watumishi kwa kuwasaidia kujikinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza na kuongeza ustawi wao wa kimwili na kiakili, Amesisitiza kuwa mazoezi ya mara kwa mara ni msingi wa maisha yenye afya na tija kazini.

Aidha, amesema michezo si chanzo cha burudani pekee bali pia ni fursa ya ajira na kuongeza kipato kupitia vipaji mbalimbali vinavyoweza kuibuliwa na kuendelezwa. Kwa mujibu wake, watumishi wanapaswa kuendeleza utamaduni wa kushiriki michezo ili kujenga afya bora, furaha na mahusiano mazuri katika mazingira ya kazi.

Bonanza hilo limewakutanisha watumishi wa Wizara ya Madini pamoja na taasisi zake zote katika utaratibu wa kawaida wa kukutana kila robo mwaka kwa lengo la kuimarisha ushirikiano, mshikamano na kufahamiana zaidi. Washiriki walipata nafasi ya kushiriki michezo mbalimbali ikiwemo jogging, mpira wa miguu, mpira wa pete, basketball, kuvuta kamba, riadha na michezo ya burudani iliyovutia ushiriki mkubwa wa watumishi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Yahya Samamba, amesema bonanza hilo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya viongozi wa Wizara ya kuhakikisha watumishi wanapata fursa za kufanya mazoezi na kuimarisha afya zao. Amebainisha kuwa ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza katika jamii linaifanya michezo kuwa moja ya njia muhimu za kinga na uhamasishaji wa maisha yenye afya.

Katika bonanza hilo, washindi wa michezo mbalimbali walitunukiwa medali na zawadi, huku wanamichezo waliowakilisha Wizara katika Mashindano ya Mei Mosi wakikabidhi vikombe viwili walivyovishinda katika mbio na mchezo wa pool table. Bonanza hilo limeelezwa kuwa hatua muhimu ya kuimarisha mahusiano, umoja na ari ya kazi miongoni mwa watumishi wa sekta ya madini, jambo litakalosaidia kuongeza ufanisi wa utendaji na mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya uchumi wa nchi.











Top News