KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM)Wilaya ya Kilosa,Mkoani Morogoro, Janus Mfaume, anatuhumiwa kumdhalilisha na kumtishia maisha mwanachama wa Chama hicho Egon Haule, baada ya kumfukuza ofisini bila sababu za msingi huku akimtolea kauli za vitisho.
Tukio hilo limetokea Julai 17 mwaka huu katika ofisi za Wilaya za Chama hicho ambapo Haule alikwenda kuitikia wito wa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi aliyemwita kwa ajili ya kumpa majukumu.
Akizungumza kwa masikitiko makubwa Haule,alisema,hii ni mara ya tatu anafanyiwa udhalilishaji na kutishiwa maisha na Mfaume huku akitishia kumfanyia kitu kibaya ambacho hata kisahau katika maisha yake.
Haule alisema,hana ugomvi wowote na Katibu wake huyo lakini anashangazwa kuona kila siku amekua akimtishia maisha sambamba na kumfukuza kufika katika ofisi za Chama hicho Wilaya.
"Mimi ni mwanachama halali ambaye nimekua nikijitolea majukumu mbalimbali ya Chama kwa mwamvuli wa UVCCM Wilaya lakini napitia manyanyaso na udhalilishaji kwa kufukuzwa kila ninapofika ofsini na nimejaribu mara kadhaa kumuomba Katibu Mfaume anieleze kuna tatizo gani kauli zake amekua akisema hataki kuniona nikifika pale,"
"Kabla ya tukio la juzi nilishamuandikia ujumbe mfupi wa maandishi kumuomba tuonane anieleze nina tatizo gani la kuzuiwa kufika ofsini lakini hajawahi kunijibu,"alisema Haule.
"Kwa masikitiko makubwa huku moyo wangu ukiwa umeelemewa na huzuni na shinikizo kubwa la kukata tamaa katika kuendelea kujifunza uongozi, Itikadi na misingi ya Chama Cha Mapinduzi Ili baadae nami niwe kiongozi sahihi wa UVCCM na hatimaye chama Cha Mapinduzi,'
"Nawasilisha kwenu kitendo cha aibu na udhalilishaji na vitisho alivyo nitendea Ndugu Janus Mfaume Katibu wa CCM Wilaya ya Kilosa Julai 17 mwaka huu nilipofika ofisi ya CCM Wilaya kwa lengo la kumsaidia kazi Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ambaye alinihitaji nifike hapo," aliandika Haule kupitia kundi sogozi la Chama hicho.
"Nimeamua kuwashirikisha kuhusu changamoto ninayopitia. Katibu wa CCM Wilaya amenieleza nisiende ofisini, na katika mawasiliano yetu kuna kauli nilizozielewa kama vitisho. Nina rekodi ya sauti ya mawasiliano hayo, ambayo niko tayari kuiwasilisha kwa mamlaka husika endapo itahitajika.
Lengo langu si kumhukumu mtu yeyote kupitia kundi hili, bali kuomba suala hili lipatiwe ufumbuzi kwa kuzingatia haki, taratibu za Chama, na misingi ya uongozi wenye uwajibikaji.
"Naomba viongozi mlipokee jambo hili na kulifanyia kazi kwa busara na haki alieleza Haule"
Alipotafutwa Katibu wa CCM Wilaya ya Kilosa, Mfaume kuhusiana na tuhuma hizo alikiri kumfukuza Haule akifafanua kuwa ni kijana ambaye ana mienendo ya kihalifu na taarifa zake zipo ndani ya Jeshi la Polisi.
Alisema,Haule ameshafanya matukio kadhaa ya uhalifu ndani ya ofisi za CCM na ushahidi upo wazi ndiyo maana amechukua jukumu la kumpiga marufuku kufika hapo.
" Huyu kijana amekua akifanya mambo mbalimbali yanayokichafua Chama ikiwemo kujifanya mmoja ya maofisa wa CCM Wilaya kwa maslahi yake binafsi," alisema Mfaume.
"Mimi ndiye Katibu wa CCM Wilaya ninawajibu wa kulinda maslahi ya ofisi za Chama na mali zake siwezi kukubali kuona mtu anafanya vitendo visivyo na maadili nikafumbia macho, nimemfukuza Haule kwa sababu hana jukumu lolote ndani ya ofisi zetu lakini pia tabia zake za kihalifu zinajulikana kila mahali ikiwemo ndani ya vyombo vya dola,"alisema Mfaume.
Kuhusu suala la kumtishia maisha alisema,ni jukumu la mlalamikaji kwenda Polisi kufungua kesi kama ana uthibitisho wa kutosha na yuko tayari kujibu tuhuma hizo.



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)









.jpeg)




.jpeg)












.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
