Na Oscar Assenga Tanga
JUKWAA la Wanawake na Kodi limefanyika leo Jijini Tanga huku ikielezwa ni hatua muhimu inayodhihirisha dhamira ya kuendeleza usawa wa kijinsia na kukuza uchumi shirikishi nchini.

Akizungumza wakati akifungua Jukwaa hilo Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga, CPA Castro John, alisema ni dhamira ya dhati ya kujenga mfumo wa kodi unaoshirikisha makundi yote ya jamii, hususan wanawake ambao ni nguzo muhimu ya uchumi wa Taifa.


Alisema takwimu zinaonesha wanawake wanachangia kwa kiwango kikubwa katika shughuli mbalimbali za kiuchumi zikiwemo biashara ndogondogo, kilimo, huduma, viwanda vidogo pamoja na biashara za kati na kubwa.

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2024/2025, wanawake nchini, wakiwemo wa Mkoa wa Tanga, wanakadiriwa kushiriki katika nguvu kazi kwa asilimia 80, huku wakimiliki asilimia 54 ya biashara ndogo, za kati na kubwa.

“Bila ushiriki wa wanawake, juhudi za kuongeza wigo wa walipa kodi na kuongeza mapato ya ndani haziwezi kufikia malengo yaliyokusudiwa,” alisema CPA Castro John.


Alifafanua kuwa TRA imeanzisha Jukwaa hilo maalumu kwa lengo la kutoa elimu sahihi ya kodi, kusikiliza changamoto za wanawake wafanyabiashara, kujenga ushirikiano wa karibu pamoja na kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari na kwa wakati.

Aidha, alisema TRA imejikita katika kuboresha huduma kwa kuzingatia ushirikishwaji, uwazi, weledi na urahisi wa upatikanaji wa huduma. Aliongeza kuwa elimu ya kodi na mahusiano bora ni msingi muhimu wa kuongeza utii wa kodi.

Kupitia jukwaa hilo, wanawake watapata nafasi ya kupata ushauri kuhusu masuala ya kodi, kujifunza fursa mbalimbali pamoja na kuelewa wajibu wao wa kikodi.


“Tunataka mwanamke ajisikie salama, aheshimiwe na ashiriki kikamilifu katika mfumo wa kodi bila hofu wala kikwazo chochote,” alisema.

CPA Castro John alisisitiza kuwa kodi ndiyo injini ya maendeleo ya Taifa kwani mapato yake yanagharamia huduma muhimu kama elimu, afya, barabara, maji safi na miradi mingine ya kimkakati.

“Kila mwanamke anayelipa kodi anakuwa mshirika wa moja kwa moja wa Serikali katika kujenga Tanzania yenye uchumi imara na huduma bora kwa wananchi wake,” aliongeza.

Pia aliwataka wanawake kutumia jukwaa hilo kujifunza, kuuliza maswali na kuwa mabalozi wa utamaduni wa kulipa kodi katika jamii zao.


Aidha, aliwataka wadau wa sekta mbalimbali pamoja na taasisi za kifedha kuendelea kushirikiana na TRA katika kuwawezesha wanawake kukuza biashara zao kwa kuzingatia misingi ya kikodi.

Kwa upande mwingine, aliwahimiza wanawake wafanyabiashara kujisajili katika mfumo wa kodi na kutekeleza wajibu wao kwa hiari na kwa wakati.


“Kulipa kodi si wajibu wa kisheria tu, bali ni mchango wa moja kwa moja katika kujenga Taifa. Wanawake wakisimama kiuchumi, familia na jamii vinaimarika,” alisema.

Katika hatua nyingine, alisisitiza umuhimu wa kutumia mipaka rasmi ya biashara kwa wafanyabiashara wanaovuka mipaka kupitia maeneo ya Horohoro na Pangani, huku akiwataka kuachana na biashara za magendo na matumizi ya njia zisizo rasmi.


Naye Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, JW Ismail Masound, alisema jukwaa hilo lina umuhimu mkubwa kutokana na malengo ya Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ambapo sekta binafsi inatarajiwa kuwa mhimili mkubwa wa ukuaji wa uchumi.

Alisema majukwaa hayo yanasaidia kuwawezesha wanawake na wafanyabiashara kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa kwa kuongeza ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Tanga (TWCC), Aziza Ramadhani, alisema jukwaa hilo litawasaidia wanawake kuelewa umuhimu wa kulipa kodi katika kukuza uchumi wa Mkoa wa Tanga na Taifa kwa ujumla.

“Hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha Mkoa wa Tanga unalipa kodi kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya jamii,” alisema.

Aliongeza kuwa jukumu la jukwaa hilo ni kuwaunganisha wanawake wa Mkoa wa Tanga ili kuwapa nafasi ya kujifunza, kushirikiana na kupata fursa mbalimbali za kiuchumi ndani na nje ya mkoa huo.

Aidha, alisema wamekuwa wakitoa mafunzo mbalimbali ikiwemo kuanzisha mashamba darasa kwa vijana wa kiume na wa kike, huku akiwakaribisha wanawake wajasiriamali kushiriki katika shughuli za maendeleo zinazochangia ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Tanga na Taifa kwa ujumla.

Na Mwandishi Wetu
MWENYEKI wa Chama cha mawakili wa Serikali, Addo November amesema mbio za Wakili Marathon zitakazofanyika Mei 31 mwaka huu mjini Dodoma zinalenga kuhamasisha utoaji wa msaada wa kisheria pamoja na kuwajengea Watanzania utamaduni wa kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zao.

Akizungumza na waandishi wa habari Mei 17,2026 Jijini Dar es salaam, November amesema mbio hizo zitawakutanisha viongozi wa serikali, mawakili, wanamichezo na wananchi wa kawaida katika kuunga mkono kampeni ya msaada wa kisheria inayotekelezwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Samia Legal Aid Campaign.

Amesema hadi sasa mamilioni ya Watanzania tayari wamefikiwa na huduma za msaada wa kisheria bure, huku changamoto kubwa zinazowakabili wananchi wengi zikiwa ni migogoro ya ardhi, ndoa pamoja na unyanyasaji wa aina mbalimbali, jambo lililoifanya jamii kuendelea kuhitaji msaada huo muhimu.

November ameeleza kuwa marathon hiyo itakuwa na mbio za kilomita 21 pamoja na mbio za umbali mfupi kwa washiriki wa rika tofauti, huku watoto nao wakitengewa nafasi maalumu ya kushiriki ili kukuza vipaji vya michezo tangu wakiwa wadogo.

Aidha amesema maandalizi yote muhimu yamekamilika ikiwemo uwepo wa huduma za afya kutoka Shirika la Red Cross, vituo vya maji na matunda kwa washiriki pamoja na utoaji wa medali na zawadi kwa washindi wa mashindano hayo.

Aidha November amesema washiriki watatakiwa kulipia Sh40,000 kwa ajili ya usajili ambapo watapatiwa vifaa mbalimbali vya marathon hiyo, huku akibainisha kuwa lengo la awali ni kupata washiriki zaidi ya 5,000 kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Ameongeza kuwa mbio hizo zitapambwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali pamoja na uwepo wa viongozi wa kitaifa akiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari huku majina mengine ya wageni maalumu yakiendelea kutangazwa kadri siku zinavyosogea.

Naye mwanariadha mstaafu, Juma Ikangaa amesema marathon hiyo itasaidia kuibua vipaji vipya vya riadha nchini na kuongeza hamasa ya Watanzania kushiriki michezo kwa manufaa ya afya na maendeleo ya taifa.

Amesema ushiriki wa wanasheria katika mbio hizo unaonyesha namna taaluma hiyo ilivyo tayari kushirikiana na jamii katika shughuli za maendeleo, huku akiwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hilo la kihistoria litakalofanyika katika Viwanja vya Jamhuri mkoani Dodoma.


 Na Mwandishi Wetu, Arusha

Arusha. Tarehe 15 Mei 2026: Serikali imeipongeza Benki ya CRDB Bank Plc kwa juhudi zake za kuhamasisha uwekezaji nchini kupitia elimu ya fedha, uwekezaji wa hisa na uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga kuwajenga vijana kuwa wawekezaji wa baadaye.

Pongezi hizo zimetolewa jana jijini Arusha na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa 31 wa mwaka wa benki hiyo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Semina hiyo ilikuwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa” na iliwakutanisha viongozi wa serikali, wanahisa, wataalamu wa masoko ya mitaji pamoja na vijana kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza katika semina hiyo, Waziri Omar alisema vijana wanapaswa kushiriki kikamilifu katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji badala ya kutegemea ajira pekee.

“Kaulimbiu ya mwaka huu imebeba ujumbe mkubwa wa kimkakati kwa taifa letu. Vijana hawapaswi kuishia kutafuta ajira pekee, bali wanastahili kushiriki katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji,” alisema Waziri Omar.

Aidha, aliipongeza benki hiyo kwa hatua ya kufungua Ofisi ya Uwakilishi Dubai, akisema hatua hiyo imeongeza hadhi ya Tanzania katika sekta ya fedha na uwekezaji kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema benki hiyo itaendelea kuwawezesha vijana kupitia huduma za kifedha, ubunifu na programu za maendeleo ya ujasiriamali.

Alisema kupitia CRDB Bank Foundation na programu ya IMBEJU, maelfu ya vijana na wafanyabiashara wadogo wamefikiwa kwa mafunzo, mitaji na ushauri wa biashara.

“Tunaamini vijana wa leo si wateja tu wa benki yetu, bali ni wawekezaji, wabunifu na viongozi wa uchumi wa kesho,” alisema Dkt. Nsekela.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Neema Mori alisema uwekezaji katika hisa ni njia muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa muda mrefu kwa vijana na familia za Kitanzania.

Profesa Mori alisema mafanikio ya Benki ya CRDB yanaonyesha namna uwekezaji wa muda mrefu unavyoweza kuleta matokeo chanya kwa wanahisa.

Alibainisha kuwa ndani ya miaka mitatu iliyopita thamani ya hisa za benki hiyo imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 253, huku bei ya hisa ikifikia wastani wa Sh2,800 kutoka Sh460 mwaka 2023.

Aidha, alisema bodi ya wakurugenzi inapendekeza gawio la Sh90 kwa kila hisa kutokana na matokeo mazuri ya kifedha ya mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 38 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Profesa Mori aliwahamasisha wazazi kuanza kuwawekezea watoto wao hisa mapema ili kuwajengea msingi imara wa maisha ya kifedha ya baadaye.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa taasisi kubwa za kifedha Afrika Mashariki na Kati, ikiwa na zaidi ya wateja milioni sita katika nchi za Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na ofisi ya uwakilishi Dubai, Falme za Kiarabu.




 Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, semina inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ambapo alitoa wito kwa Taasisi za Fedha nchini kupunguza riba na gharama nyingine za mikopo ili kuwawezesha wananchi wakiwemo vijana kupata mitaji ya kuwekeza kwenye shughuli zao za kiuchumi.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).







































KAMA unatamani kuona bahati yako ikigeuka kuwa pesa halisi, basi Gates of Arabia kutoka Meridianbet inapaswa kuwa kwenye orodha yako leo. Huu ni mchezo wenye msisimko wa tofauti unaokupeleka moja kwa moja kwenye dunia ya hazina za jangwani zenye ushindi mkubwa na burudani isiyoisha.

Ndani ya Gates of Arabia, kila ukicheza una nafasi ya kubadilisha stori yako kabisa. Unaweza kushinda hadi mara 5,000 ya dau lako na kufanya sekunde chache tu ziwe mwanzo wa furaha mpya. Hapa kila mzunguko una msisimko wake, maana huwezi kujua ni muda gani jackpot kubwa itatua upande wako.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mizunguko ya bure pamoja na jackpot zinazotoka muda wowote zimeufanya mchezo kuwa pendwa kwa vijana wengi wanaopenda ushindi wa maana. Kadri unavyoendelea kucheza, ndivyo nafasi yako ya kushinda zaidi inavyoongezeka. Hii ndiyo sababu kila ukicheza Gates of Arabia unakua na matumaini mapya.

Mchezo huu pia umejaa ushindani wa nguvu unaofanya kila mchezaji atake kuwa juu ya wengine. Kila ushindi unaongeza imani kubwa na kufanya hamasa ya kuendelea kucheza iwe kubwa zaidi. Ndani ya dunia hii ya jangwani, kila mtu anaamini muda wake wa kung’aa unaweza kufika wakati wowote.

Usiishie kusikia wengine wakisimulia ushindi wao wakati nafasi ipo wazi na kwako pia. Ingia sasa Meridianbet, fungua Gates of Arabia na anza safari yako ya kusaka hazina kubwa. Bahati inaweza kuwa inakusubiri.



DAR ES SALAAM
WADAU wa sekta ya ukarimu na utalii wameeleza umuhimu unaoongezeka wa vyakula, mvinyo na uzoefu wa kiutamaduni katika kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kivutio cha utalii.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wa hafla ya maonesho ya mvinyo wa Afrika Kusini iliyofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo wawakilishi wa sekta hiyo walisema uzoefu wa ukarimu na burudani unazidi kuwa sababu muhimu inayowaongoza watalii kuchagua maeneo ya kutembelea na namna wanavyotumia fedha zao wanapokuwa safarini.

Meneja wa Masoko wa Afrika wa Wines of South Africa, Matome Mbatha, alisema maboresho ya miundombinu ya utalii nchini Tanzania, ukuaji wa sekta ya ukarimu na kuongezeka kwa mtindo wa maisha ya kisasa mijini vinafungua fursa zaidi za kuvutia watalii wa kimataifa.

Alisema uzoefu unaojumuisha vyakula, mvinyo, utamaduni, muziki na burudani za usiku sasa unachangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa utalii duniani na unaweza kuisaidia Tanzania kuongeza ushindani wake katika sekta hiyo.

Mbatha alisema taasisi hiyo imekuwa ikifanya kazi nchini Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita kwa kushirikiana na hoteli, migahawa, waagizaji na wasambazaji wa bidhaa ili kukuza utamaduni wa matumizi ya mvinyo pamoja na kuboresha viwango vya huduma katika sekta ya ukarimu.

Alisema sehemu ya mpango huo ni kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa hoteli na migahawa kuhusu uelewa wa mvinyo na huduma kwa wateja ili kuboresha uzoefu wa wageni wanapotembelea maeneo mbalimbali ya huduma.

Kwa mujibu wake, Wines of South Africa pia imeanzisha programu za mafunzo maalum na kozi za bure za mtandaoni zinazolenga kuongeza ujuzi kwa wafanyakazi wa sekta ya ukarimu pamoja na kuwajengea vijana fursa za ajira katika sekta hiyo.

Alisema Afrika Mashariki inaendelea kuwa soko muhimu la matumizi ya mvinyo, huku Tanzania ikiwa miongoni mwa masoko yanayokua kwa kasi kutokana na kuongezeka kwa shughuli za utalii na upanuzi wa huduma za kisasa za ukarimu.

Kwa upande wake, Kaimu Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania, Frans van Aardt, alisema matukio ya utalii na ukarimu yanasaidia kuimarisha mahusiano ya kiutamaduni na kiuchumi kati ya nchi kupitia fursa za biashara, uwekezaji na mwingiliano wa kijamii.

Alisema ushirikiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini unaendelea kukua katika sekta mbalimbali zikiwemo utalii, madini, benki na mawasiliano ya simu, ukiungwa mkono na maono ya pamoja ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya kikanda.

Tukio hilo lililofanyika katika Delta Hotels Dar es Salaam lilikuwa sehemu ya ziara ya Wines of South Africa katika Afrika Mashariki inayolenga kuwaunganisha wazalishaji wa mvinyo, wadau wa sekta ya ukarimu na watumiaji katika ukanda huo.







Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
WATAALAMU wamewahimiza wanafunzi wa tiba na madaktari bingwa wa watoto kujikita katika fani ya Pediatric Rheumatology (Magonjwa ya Mfumo wa Kinga na maungio yanayoathiri watoto) ili kupunguza uhaba mkubwa wa wataalamu katika nchi na barani Afrika kwa ujumla.

Licha ya kuongezeka kwa magonjwa hayo, takwimu zinaonyesha kuwa Afrika yenye zaidi ya watu bilioni 1.4 ina wataalamu wasiozidi 20 wa magonjwa hayo ya watoto (pediatric rheumatologists) katika bara zima, huku Tanzania ikiwa na mtaalamu mmoja tu, hali ambayo wataalam wanaieleza kuwa ya kutia wasiwasi kwa watoto wanaougua magonjwa ya kinga mwilini na ya viungo.

Kimataifa, tafiti zinaonyesha kuwa magonjwa ya rheumatic, ambayo huainishwa kama magonjwa adimu, huathiri watoto kati ya mmoja hadi wanne kwa kila watoto 1,000 duniani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa sita wa magonjwa ya viungo na misuli kwa watoto wa Afrika lililofanyika leo Mei 14, 2026 kwa mfumo wa mseto jijini Dar es Salaam , Profesa Francis Furia kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) alisema uhaba wa wataalamu umesababisha watoto wengi kuchelewa kugundulika na kukosa matibabu kwa wakati, jambo linalozidi kuzorotesha hali zao za kiafya.

Profesa Furia, ambaye ni daktari wa watoto, alisema kuongeza idadi ya wataalamu wa pediatric rheumatology kutaimarisha kwa kiasi kikubwa huduma za afya kwa watoto na kusaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wengi wanaoathiriwa na magonjwa hayo.

“Kwa sababu ya changamoto hizi, tunaendelea kusisitiza umuhimu wa kuongeza idadi ya wataalamu katika fani hii. Kupitia kongamano hili la sita, tumewapatia mafunzo madaktari wanaoendelea na mafunzo na madaktari wa watoto ili waweze kutambua dalili mapema na kutoa matibabu kwa wakati,” alisema Profesa Furia.

Pia aliipongeza serikali kwa hatua inazochukua katika kuimarisha huduma hizo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

“Tanzania imeanza kupiga hatua. Uwekezaji mkubwa umefanyika Muhimbili ambapo huduma hizi zinatolewa. Maabara zimeboreshwa na vipimo vingi ambavyo awali vilikuwa vikifanyika nje ya nchi sasa vinafanyika hapa nchini,” alieleza.

Aliongeza kuwa hospitali hiyo imeanzisha kliniki maalum kwa watoto wanaougua magonjwa hayo, ambapo zaidi ya watoto 50 kutoka mikoa mbalimbali wanapata matibabu.

“Hii ni hatua muhimu kuhakikisha watoto hawa wanapata huduma wanazostahili,” alisema.

Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Dkt. Gunini Kamba alisema serikali iko tayari kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kutoa fursa za elimu, ikiwemo udhamini wa masomo hasa katika fani adimu za tiba.

“Tunahamasisha wote wenye nia na uwezo kujitokeza na kusomea fani hizi maalum ili kusaidia kuboresha huduma za afya nchini,” alisema.

Rais wa Jumuiya ya Madaktari wa Watoto wa Umoja wa Afrika dhidi ya Magonjwa ya Rheumatism (PAFLAR), Dkt. Ayodele Faleye alizitaka serikali za Afrika kusaidia udhamini wa madaktari wa watoto wenye nia ya kujikita katika pediatric rheumatology.

“Kuna uhitaji mkubwa wa kuwazalisha wataalamu zaidi katika fani hii,” alisisitiza.

“Tunahitaji kwa dharura kuimarisha uwezo wa maabara. Katika nchi nyingi za Afrika, sampuli za damu bado hutumwa nje ya bara kwa ajili ya uchunguzi. Hii husababisha kuchelewa kwa matokeo ya uchunguzi na matibabu, ambapo wakati mwingine huchukua siku 7 hadi 10.”

Aliongeza kuwa kuimarishwa kwa maabara za ndani kutasaidia utambuzi wa haraka na kuanza matibabu kwa wakati.

Pia alisema upatikanaji wa dawa muhimu bado ni changamoto kubwa, akieleza kuwa dawa nyingi huagizwa kutoka nje ya Afrika, jambo linalofanya ziwe ghali na wakati mwingine kukosekana.

“Uingiliaji wa serikali ni muhimu kuhakikisha dawa zinapatikana kwa uhakika na kwa bei nafuu,” alisisitiza.






Top News