Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kimesema kinaendelea kuimarisha huduma za utetezi kwa wanachama wake, ikiwemo kuwapatia msaada walimu wanachama wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali za kikazi na kisheria.
Hayo yameelezwa na Kaimu Katibu Mkuu wa CWT, Protas Magesa, Septemba 2, 2026, jijini Dodoma, wakati wa kikao cha viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania na walimu wanachama mahali pa kazi kutoka Ofisi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, akieleza kuwa chama hicho kinatumia fedha nyingi kuhakikisha walimu wanapata huduma ya utetezi inapohitajika.
Magesa amesema CWT pia inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuwajengea uwezo walimu, ikiwemo kutoa elimu kwa walimu wenye mahitaji maalum kuhusu matumizi ya mifumo, na mwendelezo wa utekelezaji wa miradi mingine huku akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya chama hicho na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ili kubaini maeneo ambayo wanaweza kushirikiana katika kuwahudumia na kutatua changamoto zinazowakabili walimu.
Aidha, amesema CWT kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeandaa programu ya kutoa elimu kwa walimu wa sayansi ambao ni wanachama wa chama hicho kuhusu matumizi salama ya kemikali wanazotumia katika utekelezaji wa majukumu yao, amesema utoaji wa elimu hiyo unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba mwaka huu katika Mkoa wa Mara na baadae kuendelea katika maeneo mengine nchini.
Akizungumza Afisa kutoka ofisi ya Kamishna wa Elimu Mwalimu Mbutorwe Mwakyima, amesema ushirikiano kati ya CWT na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ni muhimu katika kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili walimu, amesema wanapopata haki zao na mazingira bora ya kutekeleza majukumu yao, wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na hivyo kuchangia katika kuboresha sekta ya elimu nchini.
Kwa upande wake, Afisa udhibiti ubora wa shule kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bartolomeo Mwekila, amesema CWT imekuwa na mchango katika kuwasaidia walimu katika masuala mbalimbali, ikiwemo upandishaji wa madaraja, aidha ameshauri chama hicho kuendelea kuwawezesha walimu kupitia mafunzo ya mara kwa mara pamoja na kuwatafutia fursa za ajira ndani na nje ya nchi, andapo nafasi zitahitajika.



.jpeg)


.jpeg)























.jpeg)






.jpeg)

.jpeg)








