Na Janeth Raphael, MichuziTv
Watanzania wanatarajia kupata burudani ya hali ya juu ya soka la kimataifa baada ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutangaza rasmi kuwa litarusha mubashara Michuano ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 bila malipo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 9, 2026 jijini Dodoma, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Upendo Mbelle, amesema shirika hilo limefanikiwa kupata haki rasmi za kurusha mashindano hayo makubwa ya dunia yatakayofanyika kuanzia Juni 11 hadi Julai 19, 2026 katika mataifa ya Marekani, Mexico na Canada.
Amesema Watanzania wataweza kufuatilia mashindano hayo kupitia televisheni ya TBC, redio, pamoja na majukwaa ya mtandaoni ikiwemo Facebook, YouTube, Instagram na TikTok, sambamba na tovuti rasmi ya shirika hilo.
“Tumejipanga kuhakikisha Watanzania wanapata matangazo ya ubora wa juu, yakiambatana na uchambuzi wa kina kutoka kwa wachambuzi wenye uzoefu mkubwa wa soka,” amesema Mbelle.
Ameongeza kuwa uzoefu wa muda mrefu wa TBC katika kurusha matukio makubwa ya michezo, tangu enzi za Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), umeiwezesha shirika hilo kuendelea kutoa huduma bora kwa watazamaji na wasikilizaji wake.
Kwa mujibu wa Mbelle, mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026 utapigwa Juni 11, 2026, ukiwakutanisha wenyeji Mexico dhidi ya Afrika Kusini, ambapo TBC itakuwa tayari kuurusha mubashara kuanzia dakika ya kwanza.
Aidha, amesema TBC imeweka kaulimbiu maalum ya “Pira Mtelezo”, ikilenga kuwaletea Watanzania burudani ya kipekee ya soka la kimataifa wakiwa majumbani au walipo popote.
Upendo Mbelle amesisitiza kuwa TBC imewahi kurusha pia matoleo ya Kombe la Dunia ya mwaka 2010 Afrika Kusini, 2014 Brazil, 2018 Urusi na 2022 Qatar, jambo linaloonyesha uzoefu wake mkubwa katika utangazaji wa mashindano ya kimataifa.
Pia amebainisha kuwa katika kipindi cha hivi karibuni, TBC imeendelea kuimarisha uwezo wake kupitia kurusha michuano mikubwa kama CHAN 2025 iliyofanyika Tanzania, Kenya na Uganda pamoja na AFCON 2025 iliyofanyika Morocco.
“Tunaendelea kujipanga kuhakikisha kila Mtanzania anapata nafasi ya kushuhudia soka la kiwango cha juu duniani kupitia chombo chake cha habari anachokiamini,” ameongeza.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Masoko wa TBC, Daphrosa Kimbory, amesema shirika hilo limejipanga kikamilifu kulinda haki zake za matangazo, akisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayekiuka makubaliano ya haki miliki.
Naye Mkuu wa Dawati la Michezo TBC, Evance Muhando, amesema TBC inaendelea kuwa nyumbani kwa wachambuzi na watangazaji wengi wa soka nchini, na amewakaribisha Watanzania kufurahia mashindano hayo mubashara kupitia chombo hicho cha umma.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatarajia kuandika historia mpya Julai 1, 2026 kwa kuadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, huku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitarajiwa kutoa Tuzo Maalum za Rais kwa Walipakodi Bora kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Juni 9, 2026 kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano, Richard Kayombo, amesema maadhimisho hayo yatafanyika chini ya kaulimbiu isemayo; “Miongo Mitatu ya TRA, Mlipakodi Shujaa, Tanzania Inayojitegemea.”
Kayombo ameeleza kuwa maadhimisho hayo yataambatana na shughuli mbalimbali za kitaifa na kikanda zitakazoanza kabla ya kilele chake Julai 1, 2026, kwa lengo la kuendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali, kuboresha huduma kwa walipakodi na kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari.
Amefafanua kuwa shughuli hizo zitahusisha vipindi maalum vya elimu ya kodi kupitia redio, televisheni na majukwaa ya kidijitali, kliniki za kodi, huduma za ushauri kwa walipakodi, mikutano na wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara, wahasibu na washauri wa kodi pamoja na ziara za kuwafikia walipakodi katika maeneo mbalimbali nchini.
Aidha, maadhimisho hayo yataenda sambamba na utoaji wa Tuzo ya Rais kwa Walipakodi Bora, hatua inayolenga kutambua na kuthamini mchango wa walipakodi walioonyesha uadilifu, uwajibikaji na uzalendo katika kulipa kodi na kuchangia maendeleo ya taifa.
Kwa mujibu wa Kayombo, tuzo hizo zinalenga kuimarisha utamaduni wa ulipaji kodi na kutuma ujumbe kwamba kulipa kodi si wajibu wa kisheria pekee, bali ni kitendo cha uzalendo na ushiriki wa moja kwa moja katika kujenga Tanzania yenye uchumi imara, huduma bora za kijamii na fursa zaidi kwa wananchi.
Ikumbukwe TRA ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge mwaka 1995 na kuanza rasmi shughuli zake Julai 1, 1996, ikiwa na jukumu la kusimamia ukusanyaji wa kodi na mapato mengine ya Serikali Kuu, kuwezesha ulipaji kodi kwa hiari na kuchangia maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi nchini.
Maadhimisho ya miaka 30 ya TRA yanatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kutathmini mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miongo mitatu na kuweka mikakati mipya ya kuimarisha mchango wa kodi katika maendeleo ya Tanzania.
Akiwa katika kituo hicho, Mheshimiwa Mama Jane Ittogi Shanmugaratnam alitembelea maeneo tofauti ya uzalishaji na kushuhudia hatua mbalimbali za uchakataji wa pamba hadi kutengeneza nguo zinazozingatia ubora wa hali ya juu na utunzaji wa mazingira.
Akiwa katika kituo hicho, alielezwa namna wafanyakazi wa kiwanda hicho wanavyotumia ujuzi wa jadi pamoja na teknolojia za kisasa kuzalisha bidhaa za pamba zinazokidhi mahitaji ya masoko ya ndani na kimataifa.
Mhe. Mama Jane alionesha kufurahishwa na ubunifu, ustadi na juhudi zinazofanywa na watumishi wa kiwanda hicho kidogo na wanavyotumia malighafi za ndani na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano wa kimataifa unaolenga kukuza biashara, uwekezaji na maendeleo endelevu.
Rais wa Singapore, Mheshimiwa Tharman Shanmugaratnam na mwenza wake wako nchini kwa ziara ya siku tatu ya kitaifa ikilenga kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Singapore.
RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ina fursa kubwa za uwekezaji na iko tayari kuwa lango la Singapore kuingia katika masoko ya Afrika Mashariki, Ukanda wa Maziwa Makuu na Bara la Afrika kupitia Soko Huru la Afrika (AfCFTA).
Akizungumza katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji la Tanzania na Singapore, Rais Samia alisema Tanzania ni moja ya nchi zenye uchumi imara na unaokua kwa kasi barani Afrika, huku ikiwa na nafasi ya kimkakati inayounganisha masoko ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika.
Alisema licha ya mahusiano mazuri ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Singapore, bado kuna fursa kubwa ambazo hazijatumika kikamilifu katika biashara na uwekezaji.
Kwa mujibu wa Rais Samia, biashara kati ya nchi hizo iliongezeka kutoka dola za Marekani milioni 74 mwaka 2020 hadi dola milioni 299 mwaka 2023 kabla ya kushuka tena hadi dola milioni 74 mwaka 2024.
Alisema tangu mwaka 1997, Singapore imesajili miradi 36 nchini Tanzania yenye thamani ya dola milioni 535 na iliyozalisha ajira 3,328.
Rais Samia alitaja maeneo yenye fursa kubwa za ushirikiano kuwa ni bandari na usafirishaji, kilimo na usindikaji wa mazao, nishati jadidifu, miundombinu janja, utalii, uchumi wa buluu, huduma za kifedha na utatuzi wa migogoro ya kibiashara.
Alisema Tanzania ni lango la biashara kwa nchi sita zisizo na bandari ambazo ni Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Malawi, Rwanda, Uganda na Zambia, huku Bandari ya Dar es Salaam ikihudumia sehemu kubwa ya biashara hiyo.
Kwa upande wake, Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, alisema Tanzania ni nchi yenye idadi kubwa ya vijana, rasilimali nyingi za asili, fursa zinazoongezeka za uwekezaji na nafasi ya kimkakati inayounganisha masoko ya kikanda na ya kimataifa.
Alisema ushirikiano kati ya Tanzania na Singapore unaweza kuunganisha uzoefu wa Singapore katika usimamizi wa mifumo yenye ufanisi, huduma za thamani ya juu, uchumi wa kidijitali na usimamizi wa minyororo ya ugavi na hivyo kuzalisha ajira, kuongeza ujuzi na kukuza ukuaji jumuishi wa uchumi.
Rais Samia aliwataka wafanyabiashara na taasisi za pande zote mbili kutumia jukwaa hilo kujenga ushirikiano wa kudumu utakaozalisha uwekezaji, biashara na miradi yenye manufaa kwa wananchi wa nchi hizo mbili.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula, amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Kidia, ambayo ni miongoni mwa barabara zinazoboreshwa kwa kiwango cha lami katikati ya Jiji la Dodoma.
Ujenzi wa barabara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dk. Samia Suluhu Hassan, ya kutaka halmashauri za majiji kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa barabara za mitaa.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mstahiki Meya Chaula aliwataka wananchi kushiriki katika kutunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu na kuendelea kutoa huduma kwa muda mrefu.
“Wananchi kwa pamoja tunapaswa kushirikiana katika kuzitunza barabara hizi kwa kufuata taratibu zilizowekwa,Wafanyabiashara waepuke kufanya biashara katika maeneo ya barabarani kwani hali hiyo huchangia uharibifu wa miundombinu hiyo” alisema Chaula.
Aliongeza kuwa halmashauri itaendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara kupitia viongozi mbalimbali wa maeneo husika kuhusu athari za kufanya shughuli za biashara kwenye hifadhi ya barabara.
Kwa upande wake, mfanyabiashara wa eneo hilo, Peter Moshi ameishukuru serikali kwa kutekeleza mradi huo akisema kuwa wananchi walikuwa wakisubiri kwa muda mrefu kuona barabara hiyo ikiboreshwa na kukamilika kwake kutarahisisha shughuli za biashara, kuongeza usafiri wa uhakika na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo jirani.
Barabara zinazotekelezwa katika mpango huo zina jumla ya urefu wa kilometa moja kila moja na zinagharimu takribani shilingi bilioni 1.9 kwa ujumla.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Singapore uliongozwa na Rais wa Nchi hiyo Mheshimiwa Tharman Shanmugaratnam, tarehe 09 Juni, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Ziara ya Kikazi ya Rais wa Jamhuri ya Singapore, Mheshimiwa Tharman Shanmugaratnam, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 09 Juni, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Singapore, Mheshimiwa Tharman Shanmugaratnam, ambaye amewasili nchini kwa ziara ya Kitaifa ya siku 3, kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mwenyeji wake mara baada ya kuwasili ikulu.

Mheshimiwa Rais Tharman Shanmugaratnam ameweka historia ya kuwa Rais wa kwanza kutembelea nchini tangu kuanzishwa kwa mahusiano ya kidiplomasia mwaka 1980.


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)


















.jpeg)






