Unaweza kustaajabu lakini ukweli upo hivyo, ukitaka kuwaona simba wakiwa katika harakati za kuongeza familia fika katika  Kasoko ya Ngorongoro eneo la mti mmoja ambalo limezungukwa na vichaka, miti na nyasi za wastani.

Eneo hili ni maarufu sana kwa waongoza utalii kutokana na makundi ya simba waliopo katika hifadhi hiyo kupenda kupumzika  na hasa wanapokuwa katika msimu wao wa kujamiina ama kutafuta watoto na kuongeza familia.

Simba hupenda kujamiiana mara baada ya kushiba ambapo zoezi hilo linafanyika mda wowote mchana au usiku.

Tofauti na Binadamu ambapo Kazi Ngumu hufanywa na wanaume, kwa Simba ni tofauti, kazi ya kutafuta chakula ama Mawindo kwa ajili ya msosi wa familia huongozwa na simba jike ambapo mara baada ya kuhisi njaa na tamaa ya kujamiina huamua kutafuta chakula ili kwanza kushiba halafu kuingia kwenye harakati ya kuongeza familia.

Wakati wa mawindo simba huchagua chakula cha kushiba na hapa ina maana simba hahangaiki sana na wanyama wadogo wadogo kama swala kwani kwake ni kama kupoteza nguvu nyingi kwa mnyama mdogo ambae hatashiba,  badala yake simba huhangaika na wanyama wakubwa kama Nyati, Pofu, pundamilia au Nyumbu nyumbu.

Baada ya simba jike kuongoza mawindo na kupata chakula kinachofuata ni kwa simba dume kula chakula kwa kuanza na Nyama laini kama maini, Steki  na akishashiba ndipo huingia mzigoni kwa kumfuata simba jike na kuanza faragha yao.

Kama walivyo wanyama wengi simba dume hatumii muda mwingi kula tunda kwa mama,  raundi moja ni wastani wa Sekunde 20 hadi  40 anapumzika kusubiri raundi nyingine

Ukitaka kuona namna ambavyo simba wanashiriki katika tendo hilo pita eneo la mti mmoja na maeneo mengine ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro ili uweze kuona burudani ya aina yake kupitia simba ambayo hufanyika hadharani na wala si vichakani.



Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt Aneth Komba leo tarehe 27/3/2026 amefunga rasmi kikao kazi cha siku tatu cha kuandaa maudhui ya Kuhesabu katika “Kalimani App” kwa kutumia Mtaala ulioboreshwa wa Mwka 2023 na Kamusi ya Lugha ya Alama ya Tanzania.

App hiyo inaandaliwa kwa ajili wanafunzi viziwi wa Darasa la Awali, la Kwanza na la Pili. Kikao Kazi hicho kilichofanyika katika Hotel ya Protea iliyopo jijini ,Dar es Salaam.

Akifunga kikao kazi hicho Mkurugenzi Mkuu Dkt. Komba amesema, maboresho ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023 yemejikita katika kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa ni jumuishi na kuwa hakuna mtoto hata mmoja anayeachwe.

"Wazazi wenye watoto wenye mahitaji maaalum naomba muwapeleka shuleni kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeandaa mazingira wezeshi kwa watoto wote wakiwemo wenye mahitaji maalumu."amesema Dkt.Komba

Pia , amewashukuru Jenga Hub kwa maono na ubunifu wao katika kuandaa App hiyo ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Kisayansi wa KKK, uliozinduliwa na Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hivi karibuni.

Vilevile, ameeleza kuwa TET itashirikiana kwa ukaribu na Jenga Hub kuhakikisha kuwa lengo la kuandaa App linafikiwa na kuwa App hiyo inawanufaisha walengwa wote nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Jenga Hub iliyobuni Kalimani App, Bi Nancy Sumari, ameeleza kuwa App hiyo imelenga kutumiwa na watoto viziwi wa Darasa la Awali, Darasa la Kwanza, Pili na la Tatu.

Aidha, ameeleza kuwa Kalimani App inaandaliwa kwa ushirikiano kati ya Jenga Hub na TET kuwa itawawezesha watoto viziwi kujifunza Kuhesabu kwa urahisi na hivyo kuhakikisha lengo la serikali la kuwawezesha wanafunzi kuweza kuhesabu kwa ufasaha kabla ya kufika Darasa la Tatu linafikiwa.

Hata hivyo ,Bi Nancy ameishukuru TET kwa kuwa tayari kushirikiana na taasisi ya Jenga Hub katika kuhakikisha kuwa watoto viziwi nao wanapata haki yao ya msingi ya kupata vifaa vya kufundishia na kujifunzia.













Chama Kikuu cha Ushirika Lindi Mwambao kimeendelea kuimarisha utendaji wa vyama vyake vya msingi (AMCOS) kwa kukabidhi pikipiki 32 kwa ajili ya kurahisisha huduma kwa wakulima katika Wilaya za Lindi na Kilwa.

Ugawaji huo umefanyika wakati wa mkutano mkuu wa tisa wa chama hicho kwa mwaka 2025/2026 uliofanyika katika ofisi zake zilizopo Mitwero, Manispaa ya Lindi, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza ufanisi katika shughuli za ushirika.

Akizungumza katika mkutano huo, Meneja wa chama hicho, Nurdin Said Swalla, alisema mpango huo unalenga kuhakikisha vyama vyote 61 vilivyopo chini ya chama kikuu vinapatiwa vitendea kazi hivyo, hasa vile vilivyokamilisha ulipaji wa hisa, ili kuviwezesha kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi.

Baadhi ya vyama vilivyonufaika na mgao huo wa pikipiki ni pamoja na Mnali, Ng’apa, Pachani, Mtua, Nyango, Mnolela, Matandu, Navanga, Somanga, Nachunyu na Milola.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, ameipongeza chama hicho kwa mafanikio makubwa ya kiuchumi, akieleza kuwa katika msimu wa 2025/2026, zao la korosho limeingiza zaidi ya shilingi bilioni 101, ufuta zaidi ya bilioni 33, huku mbaazi zikiingiza zaidi ya bilioni 3.

Ametumia fursa hiyo kuzihimiza AMCOS za Wilaya za Lindi na Kilwa kuzingatia misingi ya ushirika na kuimarisha uendeshaji wa vyama vyao ili viwe imara kiuchumi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mohamed Nyundo, ameishukuru chama hicho kwa uwekezaji wa ghala kuu la mazao katika eneo la Hoteli Tatu wilayani humo, akibainisha kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza gharama za usafirishaji wa mazao kwa wakulima kutoka maghala ya AMCOS hadi ghala kuu.

Aidha, Mrajis Msaidizi wa Ushirika Mkoa wa Lindi, Kenneth Shemdoe, amesema uwekezaji unaofanywa na vyama vya ushirika mkoani humo unaunga mkono jitihada za serikali za kuwahudumia wakulima, huku akihimiza matumizi ya mizani za kidijitali ili kuongeza uwazi na ufanisi.

Baadhi ya wajumbe wa bodi za vyama vya ushirika walioshiriki mkutano huo wameeleza shukrani zao kwa kupatiwa pikipiki, wakisema zitapunguza changamoto ya kuwafikia wanachama na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 11 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS), uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Sipopo kilichopo Jijini Malabo nchini Guinea ya Ikweta.

 Katika ufunguzi wa Mkutano huo, salamu za Viongozi mbalimbali zimesisitiza umuhimu wa hitaji la kufanya mageuzi ya Kitaasisi na kimfumo kuwezesha Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS) kukabiliana na changamoto zinazoikabili Dunia kwa sasa ikiwemo, migogoro ya kisiasa, vita pamoja na mabadiliko ya tabianchi.

Vilevile, Ufunguzi wa Mkutano huo, umeweka mkazo kwa nchi wanachama kutoa michango kwa wakati ili kuifanya Taasisi ya OACPS kujitegemea kifedha na kuwa sauti huru kwenye jumuiya ya kimataifa. Pia msisitizo umewekwa katika kutumia vema rasilimali watu ambao ni bilioni 1.5 waliopo katika jumuiya hiyo kwa kuwajengea uwezo, ubunifu na matumizi ya akili unde ili kuleta maendeleo.

 Halikadhalika, Mkutano huo umesisitiza umuhimu wa kukuza biashara baina ya nchi wanachama pamoja na jumuiya zingine za kikanda. Pia kuwajengea uwezo vijana na wanawake ili waweze kushiriki vema katika shughuli za maendeleo.

Ushiriki wa Tanzania katika Mkutano huo ni mwendelezo wa jitihada za kuendelea kushiriki kikamilifu katika majukwaa ya kikanda na kimataifa, na kudhihirisha mchango wa nchi katika mijadala ya maendeleo na ushirikiano wa kimataifa.

Katika Mkutano huo, Rais wa Angola, Mhe. Joao Manuel Lourenzo, amekabidhi Uenyekiti wa Jumuiya ya OACPS kwa Rais wa Guinea ya Ikweta Mhe. Teodoro Obiang Nguema Mbasogo.

 Jumuiya ya Nchi za Afrika, Karibiani na Pasifiki (OACPS) yenye jumla ya nchi wanachama 79, ilianzishwa miaka ya 1970 kwa lengo la kuzisaidia kiuchumi na kisiasa nchi zilizopo Afrika, Karibiani na Pasifiki zilizotawaliwa na nchi za Bara la Ulaya. Msingi rasmi wa kisheria wa jumuiya hii uliwekwa tarehe 6 Juni 1975 kupitia Mkataba wa Georgetown. 

Katika kipindi cha miongo minne, kundi hilo lilijulikana kama Kundi la ACP lakini mnamo Aprili 2020, kufuatia marekebisho ya Mkataba wa Georgetown, kundi hilo lilibadilishwa rasmi kuwa Jumuiya ya Kimataifa ya OACPS.

Kauli mbiu ya Mkutano huo ni "OACPS Iliyobadilika na Iliyohuishwa kwa ajili ya Ushirikiano wa Kimataifa Jumuishi, Endelevu na Wenye Kuaminika” (A transformed and renewed OACPS at the service of an inclusive, sustainable and trust-based multilateralism,)". Kauli mbiu hiyo inalenga mabadiliko makubwa ya kimkakati, ambapo OACPS inajipambanua kuwa Jumuiya imara yenye mwelekeo wa kujitegemea.

Katika Mkutano huo, Makamu wa Rais ameambatana na Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Suleiman Masoud Makame, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. James Milya, Balozi wa Tanzania Guinea ya Ikweta mwenye makazi yake Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo Mhe. Said Juma Mshana pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji na Umoja wa Ulaya Mhe. Jestas Nyamanga.











Wahitimu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakiwa kwenye maadamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo yaliyofanyika katika hoteli ya APC Bunju, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akipokea maadamano ya kitaaluma pamoja na viongozi wa Bodi pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akizungumza kuhusu namna Bodi hiyo ilivyofanikisha kuongeza idadi ya wahitimu kwa mwaka huu wakati wa mahafali ya 48 ya NBAA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Pius A. Maneno akisoma hotuba yake kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi chake cha uongoziwake wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Baadhi ya Wahitimu pamoja na wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu  kwenye mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wa ngazi ya CPA wakisoma viapo vyao wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akiwatunuku wahitimu kwenye mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wakishangilia mara baada ya kutunukiwa CPA wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA)
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akitoa vyeti kwa wahitimu waliofanya vizuri kwenye mitihani ya Bodi wakati wa mahafali ya 48.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo.

Top News