
Mazungumzo hayo yamefanyika leo, tarehe 03 Juni 2026, Ikulu Zanzibar, alipofika kujitambulisha pamoja na ujumbe alioambatana nao kutoka Taasisi ya Samia Foundation.
Rais Dkt. Mwinyi amesifu kazi nzuri anayofanya mwanazuoni huyo katika kutangaza na kuhamasisha Utalii Halali katika mataifa mbalimbali duniani, na kuahidi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaridhishwa na inaunga mkono juhudi zake za kukuza na kuendeleza utalii unaofuata misingi ya Kiislamu.
Aidha, amesema Zanzibar itaendelea kujifunza zaidi kupitia uhamasishaji na mafunzo anayoyatoka kwa wadau wa sekta ya utalii, na kumshauri kuendelea na jukumu hilo kutokana na manufaa makubwa yanayopatikana kwa nchi na wadau wa utalii katika kufahamu njia bora na sahihi za kutekeleza Utalii Halali (Halal Tourism).
Dkt. Mwinyi amepongeza hatua ya Bw. Ismail Bullock ya kuchapisha na kusambaza nakala za Kitabu Kitakatifu cha Qur'an kilichotafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza, akieleza kuwa ni hatua muhimu inayoweza kuwasaidia wadau wengi zaidi kuelewa dhana ya Utalii Halali, na kumhakikishia ushirikiano zaidi.
Naye mwanazuoni Bw. Ismail Bullock amesema dhamira yake kuu ni kuona dhana ya Utalii Halali inaeleweka na kutekelezwa katika mataifa mbalimbali duniani. Amesema tayari dhana hiyo imeendelea kupata umaarufu mkubwa katika nchi nyingi duniani.
Bw. Ismail Bullock kwa sasa, yupo Zanzibar ambako anaendelea kutoa mafunzo kwa wadau wa sekta ya utalii kuhusu dhana ya Utalii Halali.
Mpango huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Benki ya NBC na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), ukiwa na lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi unaowawezesha kujiajiri, kuajiriwa na hata kuwa waajiri, sambamba na kuunga mkono jitihada za Serikali za kujenga uchumi shindani unaotegemea nguvu kazi yenye ujuzi, ubunifu na tija.
Hafla ya uzinduzi wa utekelezaji wa mpango huo ilifanyika jana katika Chuo cha VETA Kihonda, ambapo wanafunzi 294 wanapatiwa mafunzo, huku idadi kama hiyo ikinufaika katika Chuo cha VETA Mwanza. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa VETA wakiongozwa na Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Mashariki, Bw. John Mwanja, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Mkuu wa Chuo cha VETA Kihonda, Dkt. Ulimwengu Salumu, walimu, wanafunzi wanufaika pamoja na maofisa wa NBC wakiongozwa na Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma, Bw. Godwin Semunyu.
Kupitia mpango huo, NBC imetoa ufadhili wa zaidi ya shilingi milioni 150 kwa ajili ya kugharamia mafunzo ya muda mfupi kwa vijana hao katika fani za Ufundi Umeme, Ufundi Bomba pamoja na Ubunifu, Ushonaji na Teknolojia ya Nguo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Semunyu alisema kuwa uwekezaji wa NBC katika elimu ya ufundi stadi unalenga kuwawezesha vijana kujenga mustakabali wao wa kiuchumi na wakati huo huo kuchangia maendeleo ya taifa.
“Mbali na uwekezaji wetu katika sekta za afya, elimu na michezo, suala la ajira kwa vijana ni eneo muhimu tunalolipa kipaumbele. Takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania wana umri wa chini ya miaka 35. Hii ni rasilimali kubwa inayohitaji kupewa maarifa na ujuzi ili iweze kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa nchi,” alisema.
Aliongeza kuwa ongezeko la wahitimu wanaoingia katika soko la ajira kila mwaka linaifanya elimu ya ufundi stadi kuwa mojawapo ya suluhisho muhimu katika kukuza ajira, ubunifu na kujitegemea kiuchumi.
“Tunaamini kuwa elimu ya ufundi stadi ni daraja muhimu la kuwawezesha vijana kujenga maisha yao kupitia ujuzi unaotambulika na unaohitajika katika soko la ajira la sasa. Ndiyo maana tunaendelea kuwekeza katika mipango yenye matokeo ya moja kwa moja kwa jamii,” aliongeza.
Aidha, aliwataka wanafunzi wanaonufaika na ufadhili huo kutumia kikamilifu fursa waliyoipata kwa kujifunza kwa bidii ili waweze kuhitimu wakiwa na maarifa, ujuzi na umahiri unaohitajika katika mazingira ya kisasa ya kazi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Mashariki, Bw. John Mwanja, aliipongeza NBC kwa mchango wake katika kuendeleza elimu ya ufundi stadi nchini, akisisitiza kuwa ushiriki wa sekta binafsi ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha mafunzo yanayoandaliwa yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira.
“Ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za mafunzo ni nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa. Kupitia ushirikiano huo tunaweza kubaini mahitaji ya soko la ajira, kuboresha mazingira ya kujifunzia, kuongeza fursa za mafunzo kwa vitendo na kuimarisha uwezekano wa wahitimu kupata ajira au kujiajiri,” alisema.
Naye Mkuu wa Chuo cha VETA Kihonda, Dkt. Ulimwengu Salumu, alisema kuwa mafunzo hayo ya miezi mitano yalianza rasmi Mei 25 mwaka huu na yanajumuisha masomo ya nadharia pamoja na mafunzo kwa vitendo ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kufanya kazi katika mazingira halisi ya uzalishaji.
Alisema mbali na stadi za kitaaluma, wanafunzi hao pia wanapatiwa mafunzo ya ujasiriamali na stadi za maisha ili kuwawezesha kuanzisha na kusimamia biashara zao pamoja na kujenga mahusiano bora katika jamii.
“Tuna matarajio makubwa kuwa wahitimu wa programu hii watakuwa na uwezo wa kushindana katika soko la ajira, kujiajiri na kuchangia kikamilifu maendeleo ya uchumi wa taifa,” alisema Dkt. Ulimwengu.
Baadhi ya wanafunzi wanaonufaika na mpango huo walieleza shukrani zao kwa NBC, VETA na Serikali kwa kuwapatia fursa hiyo, wakisema mafunzo hayo yanakwenda kuwafungulia njia mpya za kutimiza ndoto zao za kujitegemea kiuchumi kupitia ujuzi wa ufundi stadi.
“Tunawasjukuru sana NBC kwa kubuni na kuona umuhimu wa program hii. Matarajio yetu baada ya kuhitimu ni kuanzisha shughuli zetu binafsi za uzalishaji mali, kujiajiri na hatimaye kuwaajiri vijana wengine katika jamii,” alisema mmoja wa wanufaika, Peter Lwana, kauli iliyoungwa mkono na wenzake Penina Nilanga, Fauzia Kassim na William Amon.
Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Mashariki, Bw. John Mwanja (wa pili kushoto), Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bw. Godwin Semunyu (wa tatu kushoto), na Mkuu wa Chuo cha VETA Kihonda, Dkt. Ulimwengu Salumu (wa tatu kulia) , walimu na wanafunzi, wakisikiliza maelezo kutoka kwa mwanafunzi wa kozi fupi ya Ufundi Bomba katika Chuo cha VETA Kihonda, William Amon (katikati), kuhusu mfumo wa kilimo cha umwagiliaji uliobuniwa na wanafunzi hao. William ni miongoni mwa vijana 588 wanaonufaika na mpango wa ufadhili wa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana unaojulikana kama NBC Wajibika Scholarship, unaotekelezwa na VETA kwa ufadhili wa NBC. Tukio hilo lilifanyika leo mkoani Morogoro wakati wa uzinduzi rasmi wa utekelezaji wa mpango huo.
Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Mashariki, Bw. John Mwanja (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa utekelezaji wa mpango wa ufadhili wa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana unaojulikana kama ‘NBC Wajibika Scholarship’, kwa tawi la VETA Kihonda Morogoro. Mradi huo unaotekelezwa na na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa ufadhili wa NBC. Wengine ni Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bw. Godwin Semunyu (kushoto), na Mkuu wa Chuo cha VETA Kihonda, Dkt. Ulimwengu Salumu (kulia).
Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Semunyu (katikati) alisema kuwa kupitia mpango huo NBC inalenga kuwawezesha vijana kupata ujuzi utakaowapa uwezo wa kujiajiri, kuajiriwa na hata kuwaajiri wengine, hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bw. Godwin Semunyu (kulia), akipimwa nguo na mwanafunzi wa kozi fupi ya Ubunifu, ushonaji na teknolojia ya nguo katika Chuo cha VETA Kihonda, Amina Rashid (kulia). Amina ni miongoni mwa vijana 588 wanaonufaika na mpango wa ufadhili wa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana unaojulikana kama NBC Wajibika Scholarship, unaotekelezwa na VETA kwa ufadhili wa NBC. Tukio hilo lilifanyika leo mkoani Morogoro wakati wa uzinduzi rasmi wa utekelezaji wa mpango huo.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa VETA akiwemo Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Mashariki, Bw. John Mwanja, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Mkuu wa Chuo cha VETA Kihonda, Dkt. Ulimwengu Salumu, walimu, wanafunzi wanufaika pamoja na maofisa wa NBC wakiongozwa na Bw. Semunyu.
Kupitia mpango huo kila mwanafunzi amefunguliwa akaunti ya “NBC Kua Nasi” ili kuwaunganisha na mfumo rasmi wa kifedha, sambamba na kuwapatia fursa za kukuza ujuzi wa kibiashara kupitia majukwaa ya NBC Business Club pindi watakapomaliza mafunzo hayo.
Watumiaji wa petroli wamepata afueni mwezi Juni 2026 baada ya bei ya mafuta hayo kushuka ikilinganishwa na mwezi uliopita. Kwa Dar es Salaam, petroli sasa itauzwa kwa bei kikomo ya shilingi 4,086 kwa lita, hatua inayotarajiwa kupunguza gharama kwa watumiaji wa kawaida na baadhi ya shughuli za usafiri.
Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo.
Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu kama usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii.
Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli na Irani. Mgogoro huo umeathiri uzalishaji, uhifadhi na usafirishaji wa mafuta duniani, huku kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz kukiongeza gharama za usafirishaji na bima za meli za mafuta.
Na Janeth Raphael - MichuziTv - Bungeni Dodoma
Serikali imesema inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kulinda biashara na mitaji ya vijana kwa kuhakikisha wakandarasi na wazabuni wanalipwa kwa wakati pamoja na kuongeza ushiriki wao katika fursa za zabuni za umma.
Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Timida Mpoki Fyandomo, ambaye alitaka kufahamu hatua zinazochukuliwa na Serikali kulinda biashara na mitaji ya vijana dhidi ya ucheleweshaji wa malipo ya madeni ya wakandarasi.
Luswetula amesema kupitia Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali wa Muda wa Kati wa mwaka 2026/27 hadi 2027/28, Maafisa Masuuli wa Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa wameelekezwa kuweka kipaumbele kwa wawekezaji wa ndani katika utoaji wa zabuni, masharti ya mikataba na ulipaji wa madai yao.
Amesema Serikali pia imeelekeza kuimarishwa kwa ushirikiano wa ubia (joint venture) katika mikataba inayohusisha kampuni za kigeni ili kuongeza ushiriki wa wazawa, hususan vijana, katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Aidha, Naibu Waziri huyo amesema Serikali imetenga shilingi bilioni 700 katika mwaka wa fedha 2025/26 kwa ajili ya kulipa madeni ya wakandarasi na wazabuni.
Amebainisha kuwa katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, jumla ya shilingi bilioni 477.6 tayari zimelipwa kwa wakandarasi mbalimbali nchini.
Luswetula amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kulipa madeni yaliyosalia kwa lengo la kulinda mitaji ya wakandarasi wa ndani, wakiwemo vijana, na kuwawezesha kuendelea kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Kihongosi ametoa wito huo leo Juni 2,2026 aliposhiriki kikao cha Shina namba Mbili Kata ya Bonga wilayani Babati mkoani Manyara.
Akizungumza mara baada ya kusikiliza ajenda ya kikao hicho Kihongosi amesema pamoja na kwamba Watanzania wana sifa ya ukarimu na upendo kwa wageni, ni muhimu kuhakikisha wageni wanaopokelewa wanajulikana na hawana nia ya kuleta matatizo katika jamii.
“Nimeelezwa kwamba mnawapokea wageni wanaofika katika maeneo yenu na kuwachukulia kama ndugu. Hilo ni jambo jema na linaonyesha ukarimu na mshikamano uliopo katika jamii yetu,” amesema Kihongosi.
Ameongeza kuwa ukarimu huo unapaswa kuambatana na tahadhari ili kulinda usalama wa wananchi na maeneo yao.
“Hata hivyo, mnapopokea wageni ni muhimu kuchukua tahadhari na kujiridhisha kuwa ni watu salama. Tusije tukawapokea watu wenye nia mbaya au wahalifu ambao wanaweza kuleta matatizo katika maeneo yetu,” amesema.
Kihongosi amesisitiza kuwa viongozi wa maeneo na wananchi wanapaswa kushirikiana kuhakikisha taarifa za wageni wanaoingia katika jamii zinajulikana ili kuimarisha ulinzi na usalama.
“Ni wajibu wa viongozi na wananchi kuhakikisha taarifa za wageni wanaoingia katika maeneo yao zinajulikana na, inapobidi, zinawasilishwa kwa vyombo husika vya usalama. Hii itasaidia kulinda amani, usalama na utulivu wa maeneo yetu,” amesema.
Ameongeza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuzuia uwezekano wa watu wenye nia ovu kujificha ndani ya jamii na kusababisha changamoto za kiusalama.
Katika hatua nyingine, Kihongosi amewataka wananchi kuendelea kulinda amani na mshikamano uliopo nchini, akisema Tanzania imeendelea kuwa mfano wa utulivu kutokana na umoja na upendo wa wananchi wake.
“Tanzania yetu haigawanyiki Mungu alivyotupa nchi hii, na kama ambavyo nyinyi watu wa Babati mmepewa ardhi hii kuwa makazi yenu, basi mna wajibu wa kuilinda. Hapa ni nyumbani kwenu, msikubali mtu yeyote aje kucheza na utulivu wa maeneo yenu,” amesema.
-Masoko ya Kaboni Kufungua Fursa Mpya za Ajira na Uwekezaji
Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) kimesema kuwa mustakabali wa ajenda ya mabadiliko ya tabianchi na uchumi wa kijani nchini unategemea nguvu, ubunifu na uongozi wa vijana, huku kikihimiza ushiriki wao katika kutumia fursa zinazotokana na sekta hiyo inayokua kwa kasi duniani.
Akizungumza katika Mkutano wa Vijana wa mwaka 2026 uliofanyika jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa NCMC, Kathryn Kigaraba, amesema mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuwa moja ya changamoto kubwa zinazoikabili dunia, lakini pia ni miongoni mwa fursa muhimu za kiuchumi zinazoweza kuleta maendeleo makubwa kwa Tanzania.
Kathryn amesema tayari Tanzania inaendelea kushuhudia athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia mabadiliko ya mifumo ya mvua, ukame, mafuriko, uharibifu wa mifumo ikolojia pamoja na changamoto mbalimbali zinazoathiri maisha ya wananchi.
Amesema hali hiyo inahitaji hatua za haraka na ushiriki wa makundi yote ya jamii, hususan vijana.
Aidha, amesema dunia inaelekea katika uchumi wenye matumizi madogo ya kaboni na unaostahimili athari za Mabadiliko ya tabianchi, jambo ambalo tayari limeanza kuzalisha mamilioni ya ajira na kuvutia uwekezaji wa mabilioni ya dola katika sekta za nishati jadidifu, kilimo himilivu, teknolojia za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, urejeshaji wa misitu, masoko ya kaboni, fedha za Mabadiliko ya tabianchi pamoja na usimamizi wa taka.
Kathryn amesema Tanzania ina nafasi kubwa ya kunufaika kutokana na fursa hizo kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili zikiwemo misitu ya miombo, maeneo ya mikoko, maeneo ya kilimo na bioanuwai yenye uwezo mkubwa wa kuvutia uwekezaji katika miradi ya kaboni na hatua nyingine za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
“Vijana ndiyo kundi kubwa zaidi la wananchi nchini. Ni wabunifu, wajasiriamali, watafiti na viongozi wa baadaye wenye uwezo wa kuongoza mageuzi ya uchumi wa kijani. Hatupaswi kuwaona kama wanufaika pekee wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, bali wawe viongozi wa mabadiliko hayo,” amesema.
Amesema NCMC inalenga kuona vijana wa Tanzania wakijitokeza kuwa wataalamu wa masoko ya kaboni, wabunifu wa nishati jadidifu, wataalamu wa fedha za Mabadiliko ya tabianchi, wataalamu wa mifumo ya taarifa za kijiografia (GIS), wataalamu wa ufuatiliaji wa mazingira kwa kutumia teknolojia za kisasa pamoja na wabunifu wa suluhisho za kidijitali za kufuatilia na kuripoti masuala ya mabadiliko ya tabianchi.
Aidha, amewataka vijana kuzingatia maeneo matatu muhimu ambayo ni ubunifu, ujasiriamali na uongozi ili waweze kunufaika kikamilifu na fursa za uchumi wa kijani.
Amesema ubunifu katika matumizi ya teknolojia za kidijitali, akili mnemba, mifumo ya ufuatiliaji wa mazingira na nishati safi utakuwa muhimu katika kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi na kuijenga Tanzania ya baadaye yenye ustahimilivu.
Pia amesisitiza umuhimu wa vijana kuanzisha biashara katika maeneo ya upandaji miti, nishati safi za kupikia, urejelezaji wa taka, kilimo endelevu, huduma za mazingira pamoja na maendeleo ya miradi ya kaboni, akieleza kuwa uchumi wa kijani una uwezo mkubwa wa kuzalisha ajira na kuongeza kipato kwa wananchi.
Amesema kuna umuhimu kwa vijana kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha jamii, kushiriki katika utungaji wa sera na kulinda mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Amesema Serikali imeendelea kuimarisha utekelezaji wa mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kupitia Mkataba wa Paris, Michango ya Kitaifa ya Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (NDCs), mifumo ya masoko ya kaboni pamoja na mipango mingine ya maendeleo endelevu.
Ameongeza kuwa NCMC itaendelea kusaidia juhudi hizo kupitia uhamasishaji wa uanzishaji wa miradi ya kaboni, mifumo ya ufuatiliaji, taarifa na uthibitishaji wa takwimu za kaboni (MRV), uhamasishaji wa fedha za Mabadiliko ya tabianchi, tafiti, ubunifu pamoja na kujenga uwezo kwa wadau mbalimbali.
Aidha, amesema vijana wanapaswa kujifunza ujuzi mpya na kutumia fursa zinazopatikana katika masoko ya kaboni, nishati jadidifu, kilimo endelevu na uhifadhi wa mazingira ili wawe sehemu ya kujenga Tanzania yenye ustahimilivu na maendeleo endelevu.


.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)










.jpeg)







.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


