"KIMATAIFA"
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Balozi Mobhare Matinyi akimwonesha Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Géant Electronics, Abdelkrim Mebarkia, vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji nchini Tanzania kwenye banda la Tanzania katika Maonesho ya 57 ya Biashara ya Kimataifa ya Algiers (FIA) yanayoendelea nchini Algeria.

Balozi Mobhare Matinyi akipata maelezo ya kitaalam kuhusu uzalishaji wa nyasi bandia zinazotambuliwa na FIFA kutoka kwa Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa kampuni ya Tapidor ya Algeria, Yahia Ballalou (kulia). Kushoto ni Bounouare Adel, Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa wa Tapidor.
Balozi Mobhare Matinyi akizungumza na washiriki wa taasisi za Serikali ya Tanzania, Robert Mtendawema (kushoto) ambaye ni Meneja wa Tehama na Takwimu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Gilbert Lyimo (wa pili kulia) ambaye ni Kaimu Mhasibu Mkuu wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) na Omary Mafita (kulia), Afisa Hesabu Mkuu wa WRRB.


Kampuni za Algeria zinazojishughulisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zikiwemo za viwandani na kilimo zinatafuta wabia wa kufanya nazo biashara ya mazao na uwekezaji katika sekta ya viwanda nchini Tanzania.

Kampuni hizo zilizovutiwa kushirikiana na Tanzania zinashiriki katika Maonesho ya 57 ya Biashara ya Kimataifa ya Algiers (FIA) yaliyofunguliwa na Rais Abdelmadjid Tebboune wa Algeria mnamo tarehe 22 Juni, 2026, katika Kituo cha Maonesho cha Shirika la Maonesho na Biashara ya Nje la Algeria (SAFEX).

Maonesho haya ndiyo makubwa zaidi miongoni mwa maonesho ya kimataifa nchini Algeria yakiwa yanazishirikisha jumla ya kampuni 731 zinazojumuisha 549 za Algeria kutoka katika kila sekta na kampuni za kigeni 202 kutoka nchi 36 zikiwemo 16 za Afrika.

Akizungumza katika siku ya pili ya maonesho kwenye banda la Tanzania, Balozi Mobhare Matinyi alizitaja kampuni hizo zinazotafuta wabia nchini kuwa ni GISB inayotaka kuuza vifaa vya umeme na kutengeneza nyaya za umeme kwa kutumia shaba ya Tanzania na GETEX inayotaka kununua katani na pamba na kuwekeza katika kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi.

“Afisa Mtendaji Mkuu wa GISB, Dkt. Mohamed Khelifa, anakuja tena nchini mwezi Julai baada ya ziara yake ya kwanza mwezi Mei 2026 wakati watendaji wakuu wa kampuni tatu tanzu za GETEX wamepanga kuja nchini mwezi Oktoba 2026 kutembelea Kiwanda cha Kimataifa cha Bidhaa za Ngozi cha Kilimanjaro (KLICL) ili kuona namna ya kushirikiana”, alisema Balozi Matinyi.

Kampuni zingine ni Tapidor inayotengeneza na kuuza mazulia pamoja na nyasi bandia za viwanja vya soka, Optimaflex ya magodoro, Géant Electronics ya bidhaa za umeme, Bellat ya kusindika nyama na ujenzi wa makaazi pamoja na SARL CPC inayotaka kununua dagaa wa baharini na samaki aina ya jodari ambayo Meneja Mkuu wake, Samir Benhamada, ataitembelea Kampuni ya Uvuvi Zanzibar (ZAFICO) mwezi Julai 2026.

Balozi Matinyi aliongeza zaidi kuwa: “Kampuni zingine za Algeria zinataka kununua bidhaa za kahawa, korosho, ndizi, maharage ya soya, mchele, maziwa ya unga na nyama za ng’ombe, mbuzi na kondoo ambazo huliwa kwa wingi nchini Algeria,” akitolea mfano wa sikukuu ya Idi Al-Adha ambapo Serikali ya Algeria iliingiza kondoo milioni moja kutoka nje ya nchi.

Katika maonesho haya Tanzania inatangaza fahari yake ya utalii wa hifadhi, fukwe za bahari, milima, historia ya kale na utamaduni pamoja na fursa za uwekezaji katika sekta za madini, viwanda, kilimo, nishati na usafirishaji na vilevile mazao ya chakula na biashara.

Mbali ya Ubalozi, taasisi mbili za Serikali ya Tanzania zinazoshiriki ni Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) inayowakilishwa na Meneja wa Tehama na Takwimu, Robert Mtendawema; na Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) inayowakilishwa na Kaimu Mhasibu Mkuu Gilbert Lyimo na Afisa Hesabu Mkuu Omary Mafita.

Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania,

Algiers, Juni 24, 2026.

A nation’s place in the world is determined not only by economic strength or diplomatic presence but by the vision of its leadership at decisive moments. President Samia Suluhu Hassan’s State Visit to the Russian Federation represented such a moment for Tanzania, demonstrating a commitment to increasing international engagement, partnerships, and preparing the country to capitalize on new opportunities in a complex international order.


1. Introduction.

For fifty-seven years, the page remained unturned. The last time a Tanzanian Head of State walked the corridors of power in Moscow, the world was divided by the Cold War, ideological blocs competed for global influence, and Mwalimu Julius Kambarage Nyerere stood as one of Africa’s most respected voices of independence and non-alignment. Then, in June 2026, history returned to the Kremlin. As President Samia Suluhu Hassan arrived in the Russian Federation for a State Visit from June 3 to 5 at the invitation of President Vladimir Putin, she became only the second Tanzanian Head of State ever to undertake such a journey since Nyerere’s landmark visit to the Soviet Union on 8 October 1969.

The symbolism was impossible to ignore. In the image of President Samia and President Putin meeting beneath the grandeur of the Kremlin, many saw echoes of a relationship forged in the early years of Tanzania’s nationhood and now being reimagined for the present day. Yet the world that President Samia entered was different from the one Nyerere encountered. The ideological certainties of the Cold War have given way to a multipolar international order in which influence is dispersed across multiple centres of power and nations are compelled to navigate a more complex geopolitical landscape.

The timing of the visit was equally significant. As Tanzania extends its international outreach under President Samia’s economic diplomacy agenda, the search for investment, technology, trade opportunities, scientific cooperation, and new markets has become a feature of the country’s foreign policy. Tanzania’s engagement with Russia reflected neither memory of the past nor alignment with any single bloc but the continuation of a long-standing foreign policy tradition of an independent, pursuit of national interests wherever opportunities for partnership, development, and mutual benefit can be found. Russia, meanwhile, has been seeking to increase its partnerships across Africa, creating a convergence of interests that made the June 2026 visit particularly consequential.

Taken together, President Samia’s State Visit to Russia was more than a bilateral visit and it was a statement about Tanzania’s place in the world. It continued diplomatic ties that stretch back to the dawn of independence, celebrated nearly sixty-five years of relations between the two nations, while remaining faithful to its non-aligned heritage. By bridging the historic legacy of Nyerere’s 1969 journey with the conditions of the contemporary international order, President Samia transformed a ceremonial visit into a memorable moment of diplomacy. It was a historic return to Moscow, but more importantly, it was a declaration that Tanzania intends not simply to witness the formation of a new world order, but to participate actively in it.

1.1. Early Relations.

In the late nineteenth century, as Zanzibar flourished as a busy crossroads of Swahili civilization and Indian Ocean commerce, the foundations of contact between the territories of present-day Tanzania and the Russian Empire were already beginning to form gradually. Russian interest in East Africa grew as the region became more active in Indian Ocean trade, resulting in formal engagement with the Sultanate of Zanzibar. The 1896 trade agreement between the Russian Empire and Zanzibar established a framework for commercial interaction and official representation, showing an early recognition of the region's place in the wider Indian Ocean world.

The relationship became more pronounced during the twentieth century, when the global struggle against colonialism transformed the political landscape of Africa. As African nations moved toward self-determination, the Soviet Union emerged as a vocal supporter of anti-colonial movements across the continent. This historical moment created a natural basis for engagement with the peoples of East Africa. When Tanganyika achieved independence, the Soviet Union was among the first countries to establish diplomatic relations with the newly sovereign state. Diplomatic ties were similarly established with Zanzibar in January 1964, and following the Union of Tanganyika and Zanzibar on 26 April 1964, relations entered a new phase under the name of the United Republic of Tanzania.

What followed was the construction of a partnership founded on mutual respect, sovereign equality, and a commitment to national development. The Agreement on Economic and Technological Cooperation signed in 1966 provided an institutional framework through which both countries could translate political goodwill into practical cooperation. High-level engagement soon supported this foundation. President Julius Nyerere's visit to the Soviet Union in 1969 demonstrated Tanzania's growing international profile, while the state visit of Soviet leader Nikolai Viktorovich Podgorny to Tanzania in 1977 and the bilateral air services agreement concluded in 1978 further tightened diplomatic and economic ties.

While the first phase of Tanzania–Soviet relations revolved around diplomacy and political solidarity, the decades that followed were characterized by an ambitious programme of human and institutional development. Cooperation expanded into education, science, healthcare, technology, geology, and professional training, creating connections that reached far beyond government offices. Thousands of Tanzanians pursued higher education in Soviet universities and technical institutes, returning home with skills that contributed directly to the development of a young nation.

2. Bilateral Ties.

State visits are often remembered for handshakes, motorcades, and grand receptions. Yet when President Samia Suluhu Hassan entered the Kremlin for talks with Russian President Vladimir Putin, the true purpose of the visit lay beyond ceremony. The invitation itself served as recognition of Tanzania as a trusted partner in Africa and offered an opportunity to turn diplomatic goodwill into practical outcomes.

During three days of high-level engagements, both leaders sought to move the relationship from historical friendship to a modern partnership based on economic opportunity, investment, technology, and institutional cooperation. Discussions covered collaboration in trade, investment, energy, mining, agriculture, science, education, and digital transformation, with the aim of creating a more extensive and framework for bilateral relations.

The Agreements.

Behind closed doors, diplomats and technical teams worked on what would become one of the most tangible outcomes of the visit, with the signing of eight cooperation agreements intended to expand cooperation in several sectors. These agreements stretched far beyond traditional diplomacy, covering higher education, scientific research, technological innovation, digital infrastructure, trade promotion, and investment cooperation. Together, they represented a deliberate effort to build institutions capable of sustaining long-term collaboration rather than relying solely on political goodwill.

Education and research stood out among the areas receiving attention, with new arrangements intended to support academic exchanges, skills development, innovation partnerships, and scientific cooperation between Tanzanian and Russian institutions. The agreements transformed the visit from a symbolic diplomatic event into a structured roadmap for future cooperation.

Trade Levels.

One statistic featured in nearly every discussion during the visit was bilateral trade between Tanzania and Russia standing at approximately USD 307.5 million. While the figure shows steady growth over recent years, leaders on both sides acknowledged that it remains modest compared to the scale of opportunities available. Tanzania exports products with considerable untapped potential, including coffee, spices, agricultural commodities, and other value-added goods that could gain greater access to the Russian market. Russia, meanwhile, possesses strengths in machinery, industrial equipment, wheat supplies, fertilizers, technology, and specialized expertise needed to support Tanzania’s industrialization agenda.

Discussions therefore looked not only at increasing trade volumes but also at removing obstacles that have historically limited commercial exchanges. Efforts to improve payment systems, including ongoing discussions regarding transactions in local currencies, pointed to a mutual interest in making business easier, faster, and more predictable.

2.1. Diplomatic Momentum.

As discussions progressed from government chambers to business forums, a clear message became visible that Tanzania was not only seeking aid or political support but investment partnerships capable of accelerating national development. President Samia used the visit to present Tanzania as a competitive destination for international capital, presenting opportunities in mining, energy, agriculture, infrastructure, tourism, and manufacturing.

Russian companies responded with growing interest, with conversations that could lead to major investments over the coming years. Government officials later projected that the relationships established during the visit could generate investment and business opportunities worth billions of dollars, showing the scale of ambition behind the diplomatic mission.

Future Growth.

Perhaps the most consequential aspect of the visit was the attention given to a wide economic direction aimed at Tanzania’s long term development path. Energy talks covered natural gas development and wider investment prospects, while mining cooperation covered graphite, rare earths, and coal, with attention on moving beyond extraction toward local processing and industries that add value within Tanzania.

Agriculture acted as a bridge between the two sides, linking Tanzania’s need for better productivity tools and modern methods with Russia’s strengths in fertilizers, wheat, and agricultural know how, creating pathways for agricultural cooperation and trade growth. Interest also stretched into tourism, transport, manufacturing, logistics, and the digital economy, bringing together a range of sectors under a partnership aimed at industrial capacity, food security, and steady economic progress.

3. Economic Diplomacy in Action.

Diplomacy proves its value not only through agreements signed between governments but also through the opportunities it creates for investment, trade, and economic transformation. It was with this objective that President Samia Suluhu Hassan carried Tanzania’s engagement with the Russian Federation beyond traditional statecraft and onto one of the world’s most influential economic stages, the St. Petersburg International Economic Forum (SPIEF) 2026. Bringing together political leaders, investors, entrepreneurs, and policymakers from more than 140 countries, the forum offered Tanzania a rare opportunity to present itself before a global audience as a stable, reform-oriented, and investment-ready economy prepared to compete for international capital and partnerships.

Within this highly competitive environment, Tanzania's message drew strength from the newly launched National Development Vision 2050, a long-term blueprint designed to transform the country into a modern, industrialized, innovation-led, and globally competitive economy. Rather than promoting isolated investment projects, President Samia presented a larger national agenda, one that connected foreign investment, infrastructure development, and industrial growth to a clearly mapped out development journey.

The visit also provided an opportunity to present Tanzania’s economic potential to international investors. Direct meetings, investment briefings, and dialogue with international business leaders supported the country’s image as a partner in sustained growth rather than a short term destination for capital. At the Tanzania–Russia Business and Investment Forum, discussions moved into practical commercial cooperation in several areas of the economy, while SPIEF 2026 also functioned as a wider platform for Vision 2050 priorities, investor confidence, and the groundwork for partnerships projected to unlock over USD 2 billion in potential investments and sustained economic cooperation.

4. Tanzania in a Changing World.

Wars, economic competition, and shifting alliances are transforming the international system in ways not seen since the end of the Cold War. Against this setting, President Samia Suluhu Hassan's State Visit to the Russian Federation was about far more than bilateral cooperation between two friendly nations. It offered a glimpse into how Tanzania is positioning itself within a growing multipolar world where influence is distributed across multiple centers of power rather than concentrated in a single bloc. The visit demonstrated that Tanzania understands the new dynamics of international politics and is actively adapting its diplomacy to seize opportunities arising from this transformation. More importantly, it showed a nation confident enough to engage globally while remaining guided by its own national interests.

Russia seeks closer ties throughout the continent, giving African countries access to a larger range of partnerships and opportunities. Tanzania's engagement with Russia forms part of this wider continental trend. Rather than viewing international relations through the narrow lens of ideological alignment, African states approach diplomacy as a tool for development and national progress. The increasing interaction between Russia and Africa is therefore not simply about geopolitics but also about development and greater choices for African nations seeking to accelerate their economic transformation.

The surrounding circumstances help explain why Tanzania's foreign policy has consistently favored a balance between global partners and pragmatic national interests. Under President Samia's leadership, the country has maintained productive relations with traditional Western partners while at the same time increased cooperation with emerging powers throughout Asia, the Middle East, and Eurasia.

Such an approach shows a clear understanding that national development is best achieved through engagement rather than exclusion. By maintaining productive relationships with a range of partners, Tanzania maximizes access to capital, trade, and expertise while preserving the flexibility needed to respond to a complex international environment. The Russia visit therefore represents not an exception to Tanzania's foreign policy, but a continuation of its long-standing commitment to constructive engagement with all nations in the spirit of non-alignment.

4.1. Diplomacy Without Alignment.

Critics of engagement with Russia often frame it through the lens of geopolitical competition, assuming that cooperation with one power must come at the expense of another. Yet Tanzania's diplomatic tradition has long rejected this zero-sum logic. Since independence, the country has pursued a foreign policy grounded in sovereignty, non-alignment, mutual respect, and peaceful cooperation. President Samia's visit to Russia should therefore be understood within this historical continuity. The objective was not to choose sides in global rivalries but to pursue Tanzania's national interests through dialogue, partnership, and economic cooperation.

Today's most successful foreign policies are often those that convert diplomatic relationships into tangible development outcomes. Tanzania's engagement with Russia shows this reality in practice, revealing a practical understanding that development challenges require multiple partnerships and that opportunities should be pursued in line with national interests. Rather than relying heavily on a single partner, Tanzania has gradually added new international relationships in different regions, a shift that reduces exposure to external shocks and gives the country bargaining ability in negotiations, creating more available choices.

5. Conclusion.

What distinguishes this moment is the contrast between the international system of 1969 and that of 2026. Nyerere operated in a bipolar world where neutrality was precarious but possible. President Samia operates in a multipolar environment characterized by competition among major powers, shifting centres of influence, and a complex pursuit of national interests. In this environment, the luxury of isolation has disappeared, but so has the excuse of limited choice. By traveling to Moscow while maintaining warm relations with Western partners, President Samia has operationalized what scholars call “hedging without hostility”, a foreign policy posture that builds bridges without burning them elsewhere. The Tanzania–Russia relationship is thus not a realignment but an addition, another pillar in a national strategy that refuses to reduce the world to a binary choice between East and West.

Viewed through geopolitical perspective, President Samia’s visit to Moscow carries meaning beyond the future trajectory of Tanzania–Russia relations alone. It shows a vision of statecraft in which sovereignty is expressed not through distance from the world but through purposeful participation in it. As new patterns of cooperation develop in different regions and parts of the world, Tanzania is demonstrating that even countries not counted among major powers can exercise influence through participation. The visit rests not only in the agreements reached or the opportunities created but also in what it reveals about Tanzania’s place in a changing world through a nation prepared to direct its own course, engage on its own terms, and contribute to the changing architecture of twenty first century international relations.

The measure of diplomatic success is no longer the number of partnerships a country maintains but the degree of freedom those partnerships provide. From today’s international environment, where economic corridors are being redrawn, technological competition is accelerating, and institutions that once appeared permanent are facing new pressures and expectations, countries that preserve flexibility while increasing their international presence are often better positioned to turn external change into national opportunity. Tanzania’s engagement with diverse partners shows an understanding that influence in the modern era does not come from dependence, but from the ability to engage while keeping and defending national interests.

State visits are judged not by the ceremonies they produce but by the opportunities they create, and President Samia Suluhu Hassan’s June 2026 visit to the Russian Federation seems likely to leave a legacy far beyond the three days it occupied on the diplomatic calendar. The agreements concluded during the visit, together with the high-level political commitments made by both sides, have created a framework for closer cooperation in trade, investment, education, science, technology, energy, transport, and industrial development. More importantly, the visit moved Tanzania–Russia relations from a friendship with long historical ties to a partnership aimed at practical economic outcomes. In the end, this is where President Samia’s leadership legacy continues to be written into history.

Thank you.

Written by Christopher Makwaia
Tel: +255 789 242 396


— The writer, is a University of West London graduate (formerly Thames Valley University) and an expert in Management, Leadership, International Business, Foreign Affairs, Global Marketing, Diplomacy, International Relations, Conflict Resolution, Negotiations, Security, Arms Control, Political Scientist, and a self-taught Computer Programmer and Web Developer.


Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwasilisha nakala za hati za utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf, jijini Algiers, leo tarehe 26 Mei, 2026.

Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwa katika mazungumzo mafupi na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf, mara baada ya kuwasilisha nakala za hati za utambulisho jijini Algiers, leo tarehe 26 Mei, 2026. Mazungumzo hayo yalihusu uimarishaji wa ushirikiano na uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Na Mwandishi Wetu

Serikali ya Kenya imezindua rasmi kampeni ya kugombea nafasi ya Jaji wa International Criminal Court kwa kipindi cha mwaka 2027 hadi 2036 kwa Justice Njoki Ndung’u, hatua inayolenga kuiwakilisha nchi hiyo katika taasisi ya kimataifa ya utoaji haki.

Uzinduzi huo ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi, ambapo Jaji Njoki Ndung’u alisifiwa kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya sheria na haki, ndani na nje ya Kenya.

Akiwa mmoja wa majaji wanaoheshimika nchini Kenya, Jaji Njoki amewahi kuhudumu katika Bunge la Kenya, Bunge la Afrika pamoja na taasisi za United Nations, jambo lililompa uzoefu mpana katika masuala ya sheria ya kimataifa, haki za binadamu na mfumo wa haki ya jinai.

Aidha, ameelezwa kuwa ameonyesha uwezo mkubwa wa kitaaluma katika sheria, uhuru wa kiakili, ujasiri katika kufanya maamuzi na kujitolea katika kusimamia haki na uwajibikaji katika majukumu yake ya kitaifa na kimataifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa wakati wa uzinduzi huo, Jaji Njoki anatajwa kuwa na mchanganyiko wa sifa muhimu ikiwemo mamlaka ya kimahakama, uadilifu, uzoefu wa kutunga sheria pamoja na uelewa wa masuala ya kimataifa unaoendana na mahitaji ya ICC katika juhudi zake za kupambana na ukwepaji wa haki duniani.

Hatua hiyo inatajwa kuwa sehemu ya juhudi za Kenya kuendelea kushiriki katika kuimarisha taasisi za sheria na haki katika ngazi ya kimataifa.
 




















Dar es Salaam, Tanzania — Women leaders, professionals and changemakers have been urged to embrace continuous learning and digital skills development in order to remain competitive in today’s rapidly evolving workplace shaped by artificial intelligence (AI) and digital transformation.

The call was made during this year’s Mother’s Day Dinner organized by Hold a Sister’s Hand (HASH), which brought together influential women from different sectors for high-level discussions under the theme “Reskilling While Caregiving.” The event focused on empowering mothers and caregivers to balance family responsibilities while adapting to the changing demands of the modern workforce.

The HASH Mother’s Day Dinner 2026 was sponsored by CRDB Bank Plc, Schweppes, Brutal Fruit, Ctrl Creative, Asilia African Honey, Serenity Beauty Bar and More With Mau, whose support contributed to the success of the event.

Held at Hyatt Regency Dar es Salaam, the event attracted more than 100 women including corporate executives, entrepreneurs, policymakers, technology experts, bankers and young professionals committed to advancing women’s economic empowerment and leadership in the digital age. 

 Speakers at the event emphasized that the rise of AI and digital technologies is transforming industries globally, creating both opportunities and challenges for women. They noted that many working mothers risk being left behind if they fail to upgrade their skills and embrace innovation-driven careers.

Founder and CEO of Bloom Wellness, Sophia Byanaku, who delivered the keynote address, encouraged women to prioritize both personal wellness and professional growth, stressing that resilience and adaptability are becoming essential skills in the future of work.

Cyber Security Expert and CEO of Serensic Africa, Esther Lugoe Mengi, challenged women to break barriers in technology and cybersecurity during her presentation on “Bridging the Digital Glass Ceiling.” She emphasized the need for greater female representation in emerging technologies and digital leadership spaces. 
 

Meanwhile, Founder and CEO of Unleashed Africa Social Enterprises, Khalila Mbowe, highlighted concerns over bias in artificial intelligence systems used in recruitment and promotions. She warned that unless ethical safeguards are introduced, AI could reinforce workplace inequalities instead of eliminating them.

The discussions explored critical issues affecting women in the digital era, including bridging the digital gender gap in AI adoption, ethical leadership, responsible use of technology, and addressing bias in AI-driven recruitment and promotions. Participants also highlighted the importance of adaptability, lifelong learning, networking and mentorship in helping women remain relevant in highly competitive environments.

Founder of HASH Tanzania, Vivian Temi, said the initiative aims to create a supportive community where women can openly discuss challenges facing mothers and caregivers in workplaces increasingly influenced by automation and digital systems.


“We want women to understand that caregiving should never limit their dreams, ambitions or leadership potential. Women deserve opportunities to grow, reskill and thrive while still taking care of their families,” she said.

A fireside discussion featuring Veronica Muumba, Head of Talent Management at CRDB Bank Plc, and moderated by Maureen Njeri, Head of Brand and Marketing at Settlo Technologies Limited, highlighted how institutions can create supportive environments for employees balancing caregiving and career advancement.

The discussion showcased how progressive workplace policies such as flexible working arrangements, mentorship programs, wellness initiatives and digital upskilling opportunities are helping women thrive professionally while maintaining family responsibilities.

Participants also took part in an interactive panel discussion moderated by Lucy Tomeka, featuring Shumbana Walwa of Equity Bank Tanzania, emotional intelligence counselor Ngianasia Marealle Minja and Kai Mollel of Stanbic Bank Tanzania. The panelists shared practical experiences on overcoming workplace barriers, adapting to technological shifts and building sustainable careers while caregiving.

Many attendees called for stronger workplace policies that support women through flexible work arrangements, access to digital training, affordable childcare services and inclusive leadership programs that promote gender equality in decision-making spaces.

The event concluded with a renewed call for governments, private sector institutions and development partners to invest more in women’s digital empowerment and skills development to ensure they fully participate in shaping the future economy.

Participants agreed that empowering women with technology, financial literacy and leadership skills is not only critical for gender equality, but also essential for sustainable social and economic development across Africa in the digital age.


  Msimamizi Mkuu wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” Balozi Lindsay Kiptiness akiwakaribisha  viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini wanaoshiriki zoezi hilo Jijini Nairobi leo Mei 11, 2026. Zoezi hilo linalenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.

Na Aron Msigwa – Nairobi, Kenya

Msimamizi Mkuu wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” Balozi Lindsay Kiptiness amesisitiza umuhimu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuendelea kuimarisha umoja, ushirikiano na utayari wa pamoja katika kukabiliana na majanga, vitisho na changamoto mbalimbali za kiusalama zinazoweza kuhatarisha amani na utulivu wa kikanda.

Balozi Kiptiness amesema hayo leo Mei 11, 2026 wakati wa mapokezi ya washiriki wa Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” lililoanza rasmi Jijini Nairobi, Kenya. 

Zoezi hilo limewakutanisha viongozi na maafisa wa kijeshi kutoka nchi za Kenya, Tanzania, Burundi, Uganda, Rwanda, Somalia na Sudani Kusini kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kikanda pamoja na kuongeza uwezo wa pamoja wa kukabiliana na changamoto za kiusalama zinazoikabili kanda hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo kuna umuhimu mkubwa katika kuimarisha mfumo wa usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, akibainisha kuwa mabadiliko ya hali ya usalama duniani yanahitaji nchi wanachama kushirikiana kwa karibu zaidi katika kulinda amani, utulivu na ustawi wa wananchi wake.

Aidha, amesema migogoro na hali ya kutokuwa na utulivu katika maeneo mbalimbali duniani, hususani Mashariki ya Kati pamoja na maeneo mengine yenye migogoro, inaendelea kuathiri kwa namna mbalimbali uchumi, usalama na maisha ya wananchi wa nchi za EAC. Amesema hali hiyo inaonesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha mshikamano wa kikanda, kubadilishana taarifa za kiusalama na kuwa na mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto hizo.

Balozi Kiptiness ameongeza kuwa Zoezi la “Ushirikiano Imara 2026” ni jukwaa muhimu linalowezesha taasisi za ulinzi na usalama za nchi wanachama kuongeza uwezo wa uratibu wa operesheni, kuimarisha mipango ya kimkakati na kujenga uaminifu miongoni mwa mataifa shiriki. Amesema hatua hiyo inaakisi dhamira ya pamoja ya nchi za EAC katika kuhakikisha ukanda huo unaendelea kuwa wa amani, usalama na utulivu.

Aidha, amesisitiza kuwa amani na usalama ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu, ushirikiano wa kikanda, biashara na ustawi wa kiuchumi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki akitoa wito kwa nchi wanachama kuendelea kuwekeza katika mipango ya pamoja ya kuzuia migogoro, kuimarisha utayari wa kukabiliana na majanga pamoja na kuboresha mifumo ya utoaji wa misaada ya kibinadamu katika ukanda huo.

Zoezi la 14 la Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Uamrishaji vya Jumuiya ya Afrika Mashariki “Ushirikiano Imara 2026” linatarajiwa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama wa EAC na kuendeleza dira ya pamoja ya kuwa na Afrika Mashariki yenye amani, usalama na ustahimilivu mkubwa dhidi ya changamoto mbalimbali

 

Na Mwandishi Wetu, Nairobi

Rais wa Kenya, William Ruto, amempongeza Jaji Mohammed Abdullahi Warsame baada ya kuapishwa rasmi kuwa jaji wa 14 wa Mahakama ya Juu ya Kenya, akieleza kuwa uzoefu wake mkubwa utasaidia kuimarisha utoaji wa haki nchini humo.

Akizungumza katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Nairobi, Rais Ruto alisema ana imani kuwa Jaji Warsame ataleta mchango chanya katika mahakama hiyo ya juu kabisa nchini Kenya kupitia weledi na uzoefu wake wa muda mrefu katika sekta ya sheria.


 “Unaungwa mkono kikamilifu na tunakuombea mafanikio unapoanza jukumu hili muhimu la kulitumikia taifa letu,” alisema Ruto wakati wa hafla ya kuapishwa kwa jaji huyo.

Katika hafla hiyo pia, Rais Ruto aliwapongeza Evans Thiga Gaturu na Jedidah Wakonyo Waruhiu baada ya kutunukiwa hadhi ya Senior Counsel, akisema wameonyesha mchango mkubwa katika kuimarisha utawala wa sheria na demokrasia ya kikatiba nchini Kenya.

Ruto alisema Serikali ya Kenya itaendelea kushirikiana na mihimili mingine ya dola kuhakikisha haki inatendeka na mfumo wa sheria unaendelea kuimarika kwa manufaa ya wananchi wote.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Naibu Rais wa Kenya, Kithure Kindiki pamoja na Jaji Mkuu na Rais wa Mahakama ya Juu Kenya, Martha Koome.