Home
Unlabelled
taa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
katika picha hii Dosa Aziz alikaa pembeni ili asiiweke kazi yake serikalini matatani(kutokana na agizo la circular no.5 kwa watumishi wa serikali).Kasela Bantu hakuwepo ila aliingizwa kwenye picha hii mwaka 1974 na kitengo cha picha cha chuo kikuu cha dar es salaam.Kasela Bantu ndiye aliyemtambulisha mwalimu kwa Abdulwaheed Sykes ambaye kwa wakati huo alikuwa rais wa TAA.Dosa Aziz alijitolea kutumia gari lake kila jpili kumuwezesha mwalimu kutoka Pugu kuja Gerezani kwa ajili ya majidiliano ya kisiasa.
ReplyDeleteSijui picha hii inaambatana na majina yafuatayo:
ReplyDeleteMwalimu J.K. Nyerere – Rais wa TAA/TANU
Geremano Pacha – Jimbo la Magharibi
Joseph Kimalando – Jimbo la Kaskazini
Japhet Kirilo – Jimbo la Kaskazini
C.O. Milinga – Jimbo la Mashariki
Abubakari llanga – Jimbo la Ziwa
L.B. Makaranga – Jimbo la Ziwa
Saadani A. Kandoro – Jimbo la Ziwa
Suleman M. Kitwara – Jimbo la Ziwa
Kisung’uta Gabara – Jimbo la Ziwa
Tewa Said Tewa – Jimbo la Mashariki
Dossa A. Aziz – Jimbo la Mashariki
Abdu Sykes – Jimbo la Mashariki
Patrick Kunambi – Jimbo la Mashariki
Joseph K. Bantu – Jimbo la Mashariki
Ally Sykes – Jimbo la Mashariki
John Rupia – Jimbo la Mashariki
Wengine masutiiiiiiiiiiiiiiii, mataiiiiiiiiiiiiiiiiiii, na masurualeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee! Lakini Kambrage, kaputura ya khaki (pengine chapa Stakpoti - ka-mji ka Uingereza ka Stockport-on-Avon) na stokingi. Lakini alikuwa akizifungaje hizo stokingi, kwa sababu hakuwa na minofu (misuli) mikubwa...(pamoja na kumkumbuka kwa kutuacha, chekeni kidogo)!
ReplyDeleteNyakati hizo, sisi tuliowahi kuziona, ma-Disii, ma-Bwana Shauri, na wakoloni wengineo - kuacha Gavana - wafanyakasi serikalini, na walimu wengi walikuwa wanapenda sana kuvaa makapturua na mastokingi yaliyojaa viko.
Wenye ujuzi wa kuandika historia ya mavazi ya Tanzania, fufueni!