HAWA NI BANANA NA MISTA BLUU. SOMA HAPO CHINI KWA MAKINI...


habari Watanzania wote na wengineo wasio watanzania. tunapenda kuwataarifu kwamba kuna website mpya inayokwenda na jina http://www.mahusiano.com/ imekamilika. website hii itajihusisha na muziki wa kizazi kipya yaani bongo flava na hapo baadae itajiweka zaidi ktk miziki ya aina nyingine yote.

katika website hii tunajitaidi kuweza kuweka video pamoja na audio files ili muweze kuburudika.

mwisho tunakaribisha maoni, ushauri wa aina wowote kuwezesha hii website kuendelea zaidi.

tunawatakia usikilizaji mwema

MK & MICHUZI


© MAHUSIANO.COM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 32 mpaka sasa

  1. WOW WOW WOW!!! KWELI MAMBO MOTO MOTO AM SO MUCH IMPRESSED MUZIKI SWAFII CLEAR!! DU SASA NA SISI WA UGHAIBUNI TUTAKUWA HATUPITWI NA MAMBO MAPYA... KEEP UP THE GOOD WORK MAHUSIANO.COM

    ReplyDelete
  2. Tunashukuru sana Michuzi.. Keep up the good work.

    ReplyDelete
  3. Haya ndio Maendeleo. Hongera sana na kazi nzuri!!!!

    ReplyDelete
  4. wow wow music is clear hata wale tulio na computer aina ya powerbook a.k.a apple tunawapata safi maana blog zingine zilikuwa zinagoma kisa program ya windows imetulia hiyo ongezeni songs ila kaka kingwendu bado hajawekwa.

    ReplyDelete
  5. Haki miliki washkaji.

    ReplyDelete
  6. Loud and clear! Na muziki unachuja swafiiii!! Michuzi, asante kwa kutupa raha. Inshaalah Mungu akuzidishie.

    ReplyDelete
  7. Michuzi naomba uposti ile picha ya Sunday Manara ana mpira na anafuatwa na Marehemu Kajole machela kwenye mechi ya Yanga na Simba iliyofanyikia Nyamagana nadhani mwaka Sabini.

    Please nitashukuru sana najua maktaba ya Daily news wanazo hizo picha

    ReplyDelete
  8. nasikia kuna habari kuwa mbunge wa viti maalum amina chifupa amekuja juu na suala la madawa ya kulevya bungeni,kiasi kwamba usalama wake uko hatarini michuzi tunaomba picha ya amina chifupa na habari zake.

    ReplyDelete
  9. michuzi hii ni nchi huru sana tunaomba picha ya amina chifupa bungeni kuhusu swala la mazungu wa unga.

    ReplyDelete
  10. michuzi kwa nini hutaki kutupa habari kamili kuhusu amina chifupa na picha yake??tunahitaji kujua mana nasikia amesikika sana kwenye magazeti ya jana yote.kuna nini??tunaomba utujulishe michuzi.

    ReplyDelete
  11. tunasikia amina chifupa amekuwa shujaa sana huko tz,imekuwaje??alafu nasikia anataka kummaliza mumewe eti ni zungu??tunaomba habari kamili na picha ya am ina chifupa.

    ReplyDelete
  12. bro michuzi thax 4 good news keep't up bro!

    ReplyDelete
  13. hivi hiyo mkaka kingwendu ana masongi mengine hebu tuwekeeni tuyasikie aisee lile la mapepe limenikuna kweli

    ReplyDelete
  14. I love it! Thanks for remembering the fans:)

    ReplyDelete
  15. hii web ni bomba mbaya.. Hongereni sana mambo hivi ndivyo yalivyo

    ReplyDelete
  16. MICHUZI TUNAOMBA PICHA YA AMINA CHIFUPA.NASIKIA ANAPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA SANA.TUELEZE HABARI KAMILI TAFADHALI.

    ReplyDelete
  17. Amaa kweli sasa Ukhaibuni tunaona kama Bongo kwa kweli Kaka michuzi,asante sana kwa jitihada zako katika kuendeleza wesite yako kwa kutupa habari zaidi.

    Kwa kweli tunaburidika sana ila tunakuomba uwape hawamajaa ushauri jinsi siku zinavyokwenda atuwekee muzic tofauti aina zote.

    Yote nasema kazi Nzuri sana kwa kweli waendelee hivi hivi siku moja Mungu atawajalia muziki wao kujilikana kwani hii ni njia mojawapo kuuu katika Kujitangaza ulimwenguni kama sisi tulivyo mbali huko tunawafagiliana sana .

    Thankx all!!!

    ReplyDelete
  18. ANONYMOUS plse tena nakuomba ushauri na pongezi moja au mbili zinatosha unamaliza ukurasa wewe mwenyewe plse huna kazi kijana???

    Wewe ulaya gani hupo lakini muda wote huo unapata??wewe kula kulala nini maana sitie maanani maisha ulaya yalivyo na jinsi wewe ulivyo na huo muda.

    Chukua muda tafakari hili ok?!1

    ReplyDelete
  19. michuzi tunaomba picha ya amina chifupa na habari zake kamili kuhusu mazungu ya unga tafadhali sana.

    ReplyDelete
  20. pia hata mimi ningefurahi sana kupata ukweli wa mazungu tz,chifupa kaja juu,michuzi tupe habari zaidi

    ReplyDelete
  21. michuzi pole na kazi nzuri tunaomba habari za amina chifupa pls,thanks in advance

    ReplyDelete
  22. michuzi nakuaminia babake naomba sana picha ya amina chifupa na habari zake za kuaminika kuhusu madawa ya kulevya.

    ReplyDelete
  23. pls michuzi we need to know about chifiupas mission for fighting against drug dealers in tz,give us latest

    ReplyDelete
  24. r u guys siblings?? they look alike!

    ReplyDelete
  25. Huu mfumo wa kusuka nywele ni mila na desturi ya mtanzania?je watoto wetu tunawafundusha nini?

    ReplyDelete
  26. Wabongo bwana, nyie mnaomba tuuuu, habari ziko kyenye magazeti hata hizo mnashindwa kuzisoma jamani, hivi ni lini nyie wabongo mtaweza kujitegemea, hebu jishuhulisheni kidogo, vitu vodogodogo kama hivi, muwe mnatafuta wemyewe, sio mekakaa tu kwenye makomputa mumsubiri Michuzi awafanyie kazi, Kalabagaho.

    ReplyDelete
  27. As ussual good work bro. Hope this doesn't change-u ain't gonna charge us in the future r u?-. Good quality, nice tracks. It's a way to keep us in touch with home. We'll appreciate a lotta sort of academia and so!! Thanks...seriously!!!

    ReplyDelete
  28. Hiyo miziki mnaisikilizia wapi????Mbona mimi sijaona link yeyote????Ninaishia kuangalia Youtube.com tu ngoma zenyew za wakenya....tuandikieni link basi jamani....????? Tunamisi nyimbo za kwetu bawana...kwnza zilipendwa ingekua so poa

    ReplyDelete
  29. link ni www.mahusiano.com na miziki ipo zaidi ya 200 ukitaka kuipata bonyeza <- na -> na wanasema mengine yaja.

    ReplyDelete
  30. videos za bongo ingia kwenye website ya bongo radio kwani wana videos nyingi sana lakini inabidi uwe na mtandao wa high speed. link yao ni hii www.bongoradio.com/videos.htm

    ReplyDelete
  31. angalia www.defunkadelic.com kuna video nyingi tu.

    ReplyDelete
  32. Blog imetulia na miziki imeenda shule. Keep the good work

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...