
ZAPOROZHYA STATE MEDICAL UNIVERSITY-UKRAINE
tel;+380612335007,fax;+380612330125,http//www.zsu.edu.ua
SERIKALI YA TANZANIA MBONA MMETUTELEKEZA?
Ni matumaini yetu kuwa waheshimiwa maofisa wa bodi ya mikopo wengi wenu mmeshawahi kusoma nje ya Tanzania na maisha ya nje ya nchi hasa huku ulaya tulipo sisi tunajua mnayafahamu vizuri sana. Sasa tunashindwa kuwaelewa kwa nini hasa tulichowafanyia kinawafanya mshindwe kututhamini? Kwa nini mnatutelekeza sisi kwenye msitu wenye wanyama wakali na kutukimbia sijui mnategemea nini hasa kututokea?
Kama ni vigezo vya kupata mikopo hiyo tuliyoomba na kuipata ni kwamba wote kati yetu tunavyo haijalishi niko Tanzania au nje ya Tanzania kama haki yetu kulingana na jinsi tulivyoomba na tunavyoendelea kuomba kila mwaka,marekebisho katika suala zima la mikopo ya nje ni suala la kufikirika kiundani zaidi na si suala la kisiasa kama ambavyo linachukulika,ni suala ambalo linahitaji uamuzi wa kitaaluma zaidi katika kuliamua kwa kuangalia tofauti ya mifumo ya maisha katika nchi za nje na ndani ya Tanzania.
Natumaini kama mliweza kufikiria uamuzi wa kuanzisha bodi ya mikopo na kututoa huko na kutuleta huku tunategemea pia suala kama hili mtakua mmelijadili kwa kina kabla ya kuamua kulitenda kwa kufuata taratibu ambazo mmeziweka wenyewe.
Kwa hiyo katika hali ya kawaida sana tunashindwa kuamini kama bado mnaendelea kutujadili na ili hali suala letu si la kuhitaji muda kama ambao mmeutumia kutufikiria wakati sisi tunaendelea kupata mateso makubwa na kusahau kama mna jukumu la kutuhudumia na sisi tuna haki ya kuhudumiwa kulingana na sheria za kimataifa kwa kutuleta huku kupitia serikali yetu hivyo katika kulifanikisha hili suala la marekebisho katika mikopo yetu ya nje ya Tanzania hasa sisi wa Ukraine ni la lazima na si ombi tena kwa sababu muda wa kufanya hivyo kwa sasa umeisha na nyinyi kama mnatujali hamna haja hata kidogo ya kuendelea kutufikiria kwa sababu ni lazima hela ije kwenye maongezo ya mikopo yetu ili tuendelee kusoma bila ya hivyo ni kwamba hela mliyotupatia ya mkopo imekaribia kuisha na kiasi kilichobaki hata tukiamua tusile sisi hakiwezi kutosheleza kiasi cha ada ya chuo ambacho kimebaki kwa hiyo mtagundua sasa si ombi tena ni suala la kuhitaji uamuzi wa haraka zaidi ili kuhakikisha usalama wetu kitaaluma na kimaisha kulingana na mazingira tuliopo sisi wanafunzi wa kitanzania tunaotokea kwenye familia ambazo umaskini bado ni kitu kikubwa kinachozisumbua,tunategemea mmetuleta huku mkiwa na lengo na nia nzuri ya kutafuta mabalozi wa kusaidia kulisukuma kwa haraka iwezekanavyo gurudumu zima la maendeleo ya nchi yetu kwa miaka ya usoni sasa ni lazima mtambue kuwa nyinyi ndio baba na mama zetu na familia zetu zipo nyuma yenu zikiendelea kuwashukuru kwa nafasi mlizotupa sisi kuja huku kujiendeleza kielimu kwa manufaa ya Tanzania nzima.
Hivyo tunaomba mtujali na kututhamini katika mawazo na hoja zetu tunazozitoa kwenu juu ya kiasi cha fedha mnachotupa sisi kama wanafunzi ambao tupo kwenye ngazi ya chuo kikuu hivyo ukomavu wa akili zetu katika kujaji na kutoa mapendekezo ni mkubwa kama wahusika tunaokutana na hali hiyo halisi hivyo hatutegemewi kupuuzwa zaidi ya hapo tutashindwa jukua zaidi kuwa mnatuweka kwenye kundi gani hasa la watu,au sisi ni wahuni?sisi si wahuni pengine kama ambavyo mnaweza kutufikiria kikawa kigezo cha kutufanyia manyanyaso haya yote katika kutufikiria kutuongezea mikopo yetu mkidhani tunahitaji hizo fedha kwa starehe binafsi, nafikiri sisi ni watu wazima ambao sasa tunajukumu la kuandaa maisha yetu wenyewe hivyo vigezo mlivyovitumia kutuleta huku nafikiri vinaweza kututoa kutoka kwenye kundi kama hili la watu,tunaimani hata wazazi wetu wangeona aina ya maisha ambayo tunaishi huku wangelia sana na wangelijua hili mapema lingelitutokea wasingelituruhusu sisi kuja huku ili hali serikali inatufanya sisi kama watoto wa kambo.
Ni aibu kubwa ambayo serikali ya Tanzania inaendelea kujizolea siku hadi siku kupitia aina ya maisha yetu kama wanafunzi wanaosomeshwa na nchi yao,hali ya kukosa fedha za kujikimu ikiwa ni pamoja na chakula,mavazi ya hali hii ngumu ya baridi kali sana,mavazi ya taaluma yetu na gharama zingine za kijamii ambazo zinapatikana hapa shuleni kama michezo,bima,usajili,utafiti wa kiafya,ulinzi,malazi ni vitu ambavyo vinapatikana nje ya ada zetu na ni miongoni mwa vitu vya kufikirika zaidi kama vigezo vyetu vya kuomba mikopo yetu kuongezwa ukizingatia gharama za maisha katika nchi hii ni kubwa.
Ucheleweshaji wa fedha zetu za ada iliyo nusu nusu kwetu zinatuzuia kuruhusiwa kuingia madarasani mara kwa mara wakati masomo yetu yanaendelea na mara kwa mara hali ya fedha za malazi na usajili zinapochelewa kwa muhula wa masomo hutufanya tuishi kwa manyanyaso na woga mwingi zaidi ya swala msituni au panya aliyemuona paka hali hii inatufanya tushindwekuwa na amani katika nafsi zetu tukijilaumu kwa nini tumekuja huku,walimu wanakiri tunauwezo mzuri kitaaluma lakini upungufu wa ufanisi wetu utaenda ukipungua kwa sababu vichwa vyetu vinasongwa na mambo mengi vikiwemo njaa na mawazo juu ya hatma yetu huku ulaya.
Hali hii inawaweka pia dada zetu ambao tumekuja nao huku kuwa katika hali ya hatari zaidi kushawishika kirahisi na wanafunzi wanaotoka nchi zingine ambazo wazazi wao wana uwezo wa kutosha au serikali zao zinawajali kifedha kulingana na gharama za maisha ya huku hivyo pia tuna wasiwasi pia na dada zetu kukosa mwelekeo wa kitu kilichowaleta na nyinyi kubeba mzigo wa lawama zote kwa kushindwa kutufikiria sisi kwa matokeo ya nyinyi kuchelewesha au kutuma fedha kidogo kulingana na mahitaji,mnaweza mkawa mlikua na lengo zuri sana juu yetu kutuleta huku ila umuhimu wenu unaweza ukakosa mwelekeo kama sio sisi kupotea kabisa kutokana na hali ngumu ya maisha ambayo tunakutana nayo huku bila nyinyi kujua au kufanya jitihada zozote kutufuatilia kwa karibu kujua tunaishi vipi.
Tunajua mnafahamu kuwa sisi ni miongoni mwa watu muhimu sana ulimwenguni pia hakuna asiyejua ya kwamba masomo tunayochukua ni miongoni mwa masomo magumu na ghali sana na yanayohitaji utulivu wa hali ya juu bila ya kuwa na mawazo au fikra zingine ambazo sio za lazima au ambazo zinazoweza zikatatulika kwa wakati husika.
Kama serikali tunajua mna uwezo mkubwa sana wa kutatua magumu ambayo tunakutana nayo huku kwa kufuata taratibu na kutekeleza utaratibu huo wa mambo mliyoyaweka na kuyajadili juu yetu kwa kuzingatia muda hasa.lakini tunashangaa kuona mambo bado yanaendelea kuwa kinyume na jinsi tulivyofikiria hii inatupa sisi wakati mgumu sana wa kwenda sambamba na masomo haya magumu,mnatakiwa mtambue kuwa mmebeba jukumu la kufanikisha lengo lenu la kutuleta huku kwa manufaa ya Tanzania ya baadae na si kutupa kwenye moto kiasi hicho kidogo cha fedha mnachotuletea.
Mnapotuathiri sisi kisaikolojia msitegemee kujenga chochote bali mtakua mnasaidia kubomoa mwanzo mzuri mliouanzisha mkiwa na nia na lengo zuri mawazoni yani kama ni mkulima ameamua kula mbegu zake zote mwenyewe atapanda nini sasa?sisi ni binadamu tutakapotumia muda mwingi kufikiria manyanyaso mnayotufanyia kwa njia moja au nyingine juu ya utoaji wenu wa fedha kwetu kama kiini cha matatizo yetu yote mnaweza kumkaribisha shetani katika mawazo yetu kwa kiasi kidogo cha fedha mlizotupa tena kwa kucheleweshwa kuamua kuacha shule na kuamua kuwa msingi wa biashara huku niliko kama njia ya kutafuta kuishi zaidi baada ya nyinyi kushindwa kutuhakikishia uhai wetu kama watu mliotuleta huku ili hali mkijua huku ni ugenini ambako ndani yake kuna watu wa aina mbalimbali ambao rangi bado ni kigezo kikubwa ambacho kimejengeka katika fikra za waliowengi kuonyesha hali fulani ya ubaguzi ambao unaweza ukaonyeshwa kwako waziwazi au kwa mficho kidogo kutegemea na akili ya mtu, pesa inaweza ikawa ni kigezo kikubwa cha kuchochea hali kama hiyo kukutokea sasa hawa ni watu wenye rangi tofauti na sisi ambao manyanyaso ya aina hii kwa nchi kama hizi tulipo sisi ni kitu ambacho unaweza kukifikiria kukutokea muda wowote kulingana na mazingira uliyopo, mnatupa wakati mgumu wa sisi kutoamini hata nyinyi mnaweza kuonyesha ubaguzi wa aina kama hiyo katika ugawaji wa mikopo ubaguzi ambao tunaweza pia tukakutana nao huku kutoka kwa wazungu ambao si wastaarabu,ni ubaguzi ambao sasa nyinyi mnauonyesha waziwazi mkwetu kwenye mtandao ili kila mtu aone ni jinsi gani mnaweza kunyanyasa wengine katika suala zima la utoaji wa mikopo, kama kuna juhudi zozote mlizifanya kama serikali kuhakikisha wengine waliopo nje wanapata mkopo sahihi kulingana na gharama za maisha ya sehemu husika basi fanyeni hivyo pia kwa wengine kama sisi ambao tupo katika mazingira kama hayo ya wenzetu wanaopata kiasi fulani cha fedha kikubwa kuliko chetu, ni kitu ambacho sisi binafsi kinatukatisha tamaa sana sana kuona nyinyi mnaweza kuchangia kuharibu tamati ya malengo ambayo tumejiwekea baadae sisi na familia zetu kama pia si na watanzania ambao wako nyuma yetu wakitegemea siku moja tuje kuwa saidia katika nyanja mbalimbali za maendeleo
Tunakutana na mambo mengi sana ambayo ni mazito kuliko uwezo wetu kuyatatua katika kila wakati mgumu wa kifedha ambao tunakutana nao.
Mwanzo wa muhula huu wa mwaka wa masomo kwa mwaka 2006-2007 ambao ulianza tarehe 01/09/2006 tumekutana na mengi ambayo katika hali ya kawaida yametusononesha kwa kiasi kikubwa sana.
Tumekuja hapa chuoni mapema mwezi wa tisa baada ya kumaliza vizuri kozi zetu za lugha ya kirusi tayari kwa kuanza mwaka wa kwanza wa chuo, tukiwa na lengo na hamu kubwa ya kuanza kusoma huku mioyo yetu ikiwa na hamasa kubwa juu ya hilo kama kitu kilichotuleta huku Ukraine na kama kitu muhimu sana katika maisha yetu huku nyuma kukiwa na serikali ya Tanzania na familia zetu ambazo wanahitaji msaada wetu mkubwa katika siku za baadae lakini cha kushangaza tumeweza kukaa zaidi ya wiki 3 bila kuingia madarasani huku wenzetu wakiendelea na masomo.
Tulikuja huku tukitegemea serikali itakuwa tayari imeshafanya mazungumzo ya karibu kati yao na serikali ya Ukraine kama sio uongozi wa chuo ili sisi tusome bila kusumbuliwa katika suala zima la malipo huku serikali ikijiandaa kuleta fedha zetu za mkopo kwetu. Tumekutana na usumbufu mkubwa sana ambao mpaka sasa hivi utatuzi wake bado ni kitendawili kizito mno huku serikali ikiendelea kushindwa kututumia pesa zetu kwa wakati unaofaa, chuo kinashindwa kutuelewa kwa kila tunachowaeleza na ukweli ni kwamba chuo kilikua hakijui chochote juu ya uwepo wetu ni mtu mmoja tu ambaye nae si muhusika ndiye alikua na taarifa zetu tena zisizo na uhakika wowote juu ya taarifa zetu kuhusu malipo tukiwa chini ya serikali ya Tanzania.
Tumekuja tukiwa hatuna fedha za kutosha baada ya serikali kutupa hela kidogo siku nyingi zilizopita kutokana na mawasiliano kutokua mazuri kati ya chuo na seriklali na maelezo yetu yasiyo na uhakika kwao juu ya malipo yetu kwa sababu hata sisi wenyewe pamoja na balozi wetu wa moscow mheshimiwa Chokala kutokuwa na taarifa sahihi kutoka bodi ya mikopo juu ya ujaji wa fedha zetu katika muda muafaka iliwapelekea wao kushindwa kutuamini na kututaka tulipe mambo mengine ambayo kwao waliyaona madogo kwa wakati huo lakini sisi kwetu yalikua makubwa kwa sababu tulikua hatuna hela ya kutosha.
Huku wao wakiendelea kuwasiliana na ubalozi wetu wa moscow ilibidi tuchangishane wenyewe kwa wenyewe kupatikana fedha za kulipia malazi,usajili pamoja na utafiti wa kiafya na bima nyingine tulilipa vitu vingi na vingine hatukuweza kuvifahamu kwa sababu vilikua kwenye orodha kulingana na taratibu zao ilikua ni lazima vilipwe kwa wakati mmoja.
Ni ukweli usiofichika hata yule aliyekua nacho kidogo ilibidi akitoe na kubaki mifuko mitupu yaani isiyokua na hela hata ya kukuhakikishia utakula nini,tulimaliza hela zote na kutuacha katika hali ngumu sana kuielezea kifedha bila kujua hatma ya kuja kwa fedha zetu kutoka bodi ya mikopo.
Tuliishi maisha magum sana kiasi ambacho siwezi kuandika hata jinsi ambavyo tulikua tukisulubika ,unaweza ukashindwa kuamini lakini ni hali ambayo haiwezi kuandikika ikafanana na uhalisia wa mateso ambayo tuliyapata kwa kipindi kile,walituruhusu kuingia darasani baada ya kama wiki 3 tangu masomo yaanze tena kwa sharti la mwishoni mwa wiki hiyo waliyoturuhusu kwenda darasani hela iwe imewafikia kama ambavyo balozi aliwataarifu.
Tukiwa hatuna chochote mifukoni mwetu tuliweza kuingia madarasani na kukutana na mambo mengine mapya ambayo yanahitaji tena fedha, kila profesa anahitaji uwe na koti jeupe la kidaktari kama sare pamoja viatu maalum kwa kila somo madarasani na maabara, ni lazima ubadilishe viatu hivyo ilikua ni lazima na wala hana haja ya kujua wewe ni mgeni au mwenyeji usipokua navyo huwezi kuruhusiwa kuingia darasani yakatukuta yaleyale tena.
Wapo maprofesa ambao walikua wanatuelewa ukijieleza vizuri lakini pia wapo ambao walikua hawataki kukusikliza unaongea nini zaidi ya kutekeleza wanacho kuagiza,.wapo wanafunzi miongoni mwetu ambao mara kwa mara waliweza kutolewa kwenye vipindi kwa aibu kubwa lakini tulikua hatuna jinsi zaidi ya kuikubali tu hali kama hiyo kutokea na hatuna jinsi ya kuikataa hali hiyo kwa kuwa sisi ndio tulioshika makali,tulitegemea kwa sababu tulichelewa kuingia darasani tungepangiwa darasa letu peke yetu lakini ilikua sivyo kama ambavyo tulikua tukidhani ,kila mmoja wetu alipangwa kwenye kundi lake na wenyeji ambao walikua na kama wiki 3 mbele yetu katika masomo.
Ukizingatia tunasoma kwa kirusi na ugumu wa masomo yetu ilitupa wakati mgumu sana kwenda nao sambamba ila kadri muda ulivyokua unaenda mambo yaliweza kutuendea vizuri kitaaluma mpaka tukawa kwenye levo moja. Ila tunajiuliza bado nani anahusika kutupa hali hii ngumu kifedha wakati ni suala ambalo linaweza likatatulika kwa wakati muafaka jibu linabaki palepale ni serikali ya Tanzania ambayo ndiyo iliyotuleta huku ikiitumia bodi yake ya mikopo
Ukweli unabaki pale pale kwa sababu sisi tupo hapa na tutaendelea kuwa hapa kwa kipindi kirefu zaidi cha miaka isiyopungua 6 ijayo ni lazima serikali ya Tanzania iache kutusomesha sisi kiubabaishaji ikiitumia bodi yake ya mikopo kwa kuwa na mkataba wa muda mrefu na wa kuaminika katika chuo hiki ili kutuhakikishia usalama wetu hapa chuoni katika suala zima la malipo yetu kwa sababu serikali ndiyo inayojukumu la kutushughulikia utatuzi au usumbufu tunaoupata juu ya suala zima la malipo kwa chuo pia kwa kurejea fax ambazo tumezituma kwa bodi ya mikopo juu ya uongezaji wa mikopo yetu ni jambo la kupewa kipaumbele sana kwa sababu bado hatujui hasa inatumia vigezo gani kugawa mikopo tofauti tofauti kwa sisi wanafunzi wa kitanzania tunaosoma huku nje ya nchi kwa sababu ukweli ni kwamba hali na gharama za maisha hapa tulipo ni kubwa sana na gharama nyingi tunazokutana nazo hapa chuoni zipo nje ya ada tunayolipa na ukichunguza kwa makini utakuta hali ya maisha ya kawaida tu ya mtu mmoja tu katika kujikimu ziko tofauti sana na gharama zingine ambazo chuo wanataka tujitegemee katika malipo kwa ajili ya masomo yetu ziko juu sana kuliko hata ada ambayo tunalipa chuoni hivyo sisi tuna kila sababu ya kuongezewa mikopo yetu na hayo yakiwa hasa mambo yanayoifanya mikopo yetu kutokua na msaada wowote kwetu ingawa kama huelewi chochote unaweza kuona ni kitu cha kubuni lakini ukweli ni kwamba mkopo hautoshi na marekebisho juu ya mikopo yetu ni ya lazima yafanyike katika kipindi kifupi sana ili sisi wenyewe kwanza tujitambue halafu tulitambua hasa suala zima la sisi kuwepo hapa chuoni, hela wanayotupa kwa kulipia ada inatosha na mambo mengine atalipa nani? swali linabaki palepale,je na sisi tutaishi vipi?
Ukijiuliza maswali kama haya jibu lake bado linawarudia wahusika wakuu wa bodi ya mikopo kama sio serikali ya Tanzania kama watu waliotuleta huku kuhakikisha jitihada za makusudi zinafanyika kuhakikisha marekebisho ya haraka yanafanyika katika maongezo ya mikopoyetu kama kweli wanajali uwepo wetu huku tulipo na si kutupa hata hicho kidogo walichotupa kwenye moto,.pia hatujua kwa nini bodi ya mikopo inaendelea kufanya bajeti zake na kutuletea fedha zetu zikiwa kwenye shillingi na ili hali wanajua malipo yote huku tunafanya kwa kutumia dola ya marekani na ndio ambayo inatumika hata katika matumizi mengine ya kawaida.
Hii inaifanya hata mkopo wetu kubadilika badilika kama sio kushuka kiwango chake mara tu pesa yetu inaposhuka thamani yake ukiilinganisha na hela ya kimarekani,utaona ni bora basi bajeti zetu zijadiliwe na kutumwa kwetu wakiiruhusu dola ya kimarekani itumike kama pesa yetu katika mikopo yetu na sio shilingi ya kitanzania.
Pia inakua sio jambo zuri sana kututumia pesa kidogo kidogo sana kiasi cha kutuacha muda mrefu katika hali ngumu kiasi ambacho hata zingine zinapokuja zinatukuta katika madeni mengi na hivyo yote iliyokuja kuishia kulipa madeni na kubaki katika hali ngumu kama ya mwanzo hivyo kuendeleza maisha magumu tu katika elimu hii inayohitaji utulivu wa muda mrefu,inajulikana wazi ni kiasi gani cha fedha sisi tunatakiwa tukipate kwa mwaka hivyo sisi si watoto wadogo tunajua balozi ana wasiwasi mara hela zinapotuishia yeye ndio hasa huwa anasumbuliwa lakini ukweli ni kwamba ni bora ukawa na pesa yako kwenye akaunti ukajua ni jinsi gani ya kuweza kuibajeti kuliko hela kuja na kubaki ubalozini zije kwa mafungu madogo madogo zinafanyiwa nini hela zetu ubalozini wakati bodi inajua imezituma kwetu?ni vizuri tukaletewa hela yetu kama ilivyopitishwa na bodi ya mikopo na kuwekwa kwenye mitandao ili nijue nimepokea kiasi gani kutoka bodi ya mikopo na sina tena cha kuwalaumu mara tu hela yangu inaponiishia au nitajua mimi nifanye nini tena ili niweze kumalizia maisha kabla ya msimu mwingine wa hela ya bodi kunifikia.
Pia usumbufu mkubwa ambao mwakilishi wa ubalozi Mr. Francis anapata usumbufu mkubwa sana kutuletea fedha zetu katika mafungu madogo madogo kutoka moscow kuja huku Ukraine kwa wanafunzi waliopo katika miji tofauti tofauti ingawa pia inaweza ikawa ni moja ya jukumu lake lakini pia inatupa mashaka na maswali mengi kichwani kwa sababu yeye anatumia gharama nyingi kuja kutuletea hela katika miji tofauti tofauti tena bila hata ya ulinzi wowote ni kazi ambayo inahitaji moyo sana lakini pia tunajiuliza huu moyo wa kufanya haya yote anautoa wapi?
Au kuna kafaida wanakapata kupitia mgongo wa fedha zetu kukaa ubalozini?jibu la swahi hilo sisi hatuna na bado tupo kwenye wimbi la mawazo mazito juu ya hatma yetu sisi kama wanafunzi katika maisha yetu ya kishule na maisha yetu ya baadae,ni vizuri pesa yetu ikaja kwa wakati mmoja ili kuepuka gharama zingine ambazo sio za lazima
Chuo chetu kinakosa imani na sisi kwa sababu mara kwa mara havipati taarifa sahihi kuhusiana na suala letu la malipo kwao pia inatupa wakati mgumu pia hata sisi wenyewe wanapotubana kidogo kwenye suala hili ambalo hata sisi liko nje ya uwezo wetu kama wanafunzi kuwahakikishia kiasi chao cha fedha wanazotudai kitakuja kwa wakati fulani muafaka.huwa mara kwa mara tunawasiliana na balozi wetu aliopo urusi mzee wetu balozi Chokala katika kila wakati mgumu kama huu wa kifedha ili aangalie ni jinsi gani ambavyo anaweza akawasiliana nao wakamuelewa ili sisi turuhusiwe kuingia madarasani mwetu lakini hata hivyo balozi nae suala hili sidhani kama huwa anatoa maelezo ya kutosha juu ya suala hili la fedha zetu za mikopo kwa uongozi wa chuo kwa sababu mara kwa mara huwa tunakutana na suala lilelile la kusimamishwa shule kwa vipindi tofauti tofauti wakizisubiri pesa zao ziwasili kwa muda muafaka kulingana na taratibu zao.
Hiki ni chuo cha serikali kwa nini serikali yetu bado ipo kimya kuwasiliana na serikali ya hapa ili sisi tusome bila usumbufu huuu?serikali mnatuthamini sisi kweli?kwa nini mnatusomesha kwa ubabaishaji mkubwa kiasi hiki?
Chuo mpaka sasa hawaamini kama kweli sisi tunasomeshwa na serikali kwa sababu hakuna serikali kama hii ambayo inaweza kusomesha watoto wao kwa ubabaishaji wa namna hii bila hata ya mkataba wa aina yoyote na wenye kuaminika kwa sababu fedha zetu hupewa mikononi mwetu tena kwa mafungu madogo madogo kwa hiyo mara kwa mara ni sisi ndio huenda kulipa mahitaji yoyote pale chuoni,mheshimiwa balozi mara kwa mara huandika fax kwa uongozi wa chuo kuwataarifu hali halisi ya wanafunzi wao wanaosomeshwa na bodi ya mikopo ya kwamba bodi haina experience ya muda mrefu ndio kwanza ipo kwenye mwanzo ambao una mambo mengi ambayo wanaendelea kujifunza hivyo baada ya muda si mrefu marekebisho ya lazima yatafanyika na mambo yanakuwa mazuri baada ya siku chache na kuwaomba wasiwe na wasi wasi juu ya suala letu la fedha hivyo waturuhusu tu tuweze kuingia madarasani.
Hizi ni siasa ambazo wao pia wanaweza kuzitegemea kuwepo kutoka kwa viongozi wa serikali lakini siasa kama hizi zikiwa na ukweli hata mdogo wenye uhakika unaweza ukafanikiwa kuwashawishi watu wakakukubalia kile unachowaambia lakini sio siasa kama hizi zenye maneno matupu na yasiyo na maandishi yoyote kwa sababu hata chuo kinashindwa kututetea mara tu wakaguzi wa serikali wanapokuja kufanya mapitio,mheshmiwa balozi mara kwa mara huwa anakosa jibu la moja kwa moja la kuwaambia chuo kwa sababu hata yeye mwenyewe huitegemea bodi ya mikopo impe maelezo ili yeye atoe taarifa yenye uhakika kwa chuo lakini inavyoonekana hata yeye mwenyewe hukutana na ubabaishaji huo huo wa kupata maelezo yasiyo na uhakika juu ya ujaji wa fedha zetu kwa chuo hivyo ubabaishaji kuwa wa moja kwa moja na sio wenye kuwa na suluhisho la moja kwa moja.
Siku ya tarehe12/01/2007 ambayo ilikua ni sikukuu ya mapinduzi kule Tanzania,ilikua ni siku mbaya sana kwa sisi wanafunzi tuliopo hapa baada ya chuo kuamua kutusimamisha masomo kwa kipindi kingine na wengine kwenda kutolewa madarasani na kutuambia kama suala letu la kifedha halitakuwa nasuluhisho la kudumu ni bora tuondoke tukatafute vyuo vingine huku wakitupa muda wa siku chache kuhakikisha suala hilo limetatuliwa bila ya hivyo taratibu za kufukuzwa chuoni inabidi zianze kufuatwa kwa wao kusema wameshindwa kutuvumilia, inatupa sisi wakati mgumu sisi kama sisi kujadiliana na kutumia muda mwingi kuongelea swala ambalo utatuzi wake kwetu ni bado usiku wa kiza kinene sana.
Balozi wetu mzee Chokala alikuwepo hapa chuoni mwanzoni mwa mwezi wa kumi na mbili akitokea mji mkuu wa nchi hii kiev ambako mabalozi wa nchi mbalimbali walikutana kujadili masuala mbalimbali ya kimaendeleo ndipo akaamua kutupitia kwa nia ya kuja kuangalia tunaendeleaje na masomo yetu,vichwani mwetu sisi kama wanafunzi tulijua sasa mwisho wa sisi kusumbuliwa katika suala zima la malipo umefika lakini sivyo kama ilivyokua ilikua ni siasa tu za mdomo ambazo hazikua na maandishi ya aina yoyote kwa uongozi wa chuo kuonyesha uwepo wetu hapa chuoni kama wanafunzi tunaosomeshwa na serikali ya Tanzania na wao wanatutambua kama wanafunzi wao, chuo pia kilikua na wakati mgumu kuweza kumuelewa mheshimiwa chokala ambaye alikuja na kukaa kwa muda usiopungua masaa manne na nusu yakiwepo masaa machache ya kutembezwa chuoni masaa machache ya kula na kunywa pamoja na maongezi yasiyoyamuda mrefu na uongozi wa chuo na kumalizia kwa kuongea na sisi tena kwa haraka haraka kama mtu aliye safarini kuwahi kitu cha muhimi sana na kuondoka huku tukiwa hatuamini kama aliyekuja alikuwa ndie balozi wetu na hakuna chochote alichokiongea kikawa msaada kwa maisha yetu ya hapa shuleni huku akiendelea kutupa moyo kuwa hawatoweza kutufukuza tena hapa chuoni wakati sisi wenyewe wahusika wa matatizo ambayo tunakutana nayo mara kwa mara hapa tukiwa na majonzi makubwa kwa sababu ukali wa chuo ni tofauti na ambavyo balozi alivyokua anukichukulia katika hali ya urahisi hivi.
Hatujaona na hatuuthamini hata kidogo uwepo wake hapa chuoni kwa sababu bado tunaendelea kukutana na matatizo yale yale ya kuisimamishwa chuo mara kwa mara sana sana siku hizi tukiutafuta ubalozi kwa kipindi kama hiki kigumu cha kusimamishwa chuo unakua haupatikani au anapokea mtu ambaye hujitambulisha kama si muhusika kwa hiyo hawezi kutoa maelezo yoyote isipokuwa tuache tu maagizo ili akija muhusika ayashughulikie,bodi ni lazima ifanye jitihada za makusudi sana ili isije kuwapoteza mabalozi wake ambao wanasoma hapa chuoni katika suala zima la pesa za chuo hasa sisi ambao tunasoma kozi za udaktari na ufamasia ambao ndio mara kwa mara tunapata matatizo na chuo chetu bila kupata muda zaidi wa kutuliza akili zetu na mambo yetu kwa ajili ya masomo, ni ukweli usiopingika kuwa sisi tunalipa ada nyingi na yenye vitu vingi sana vya kununua nje ya ada kwa ajili ya masomo yetu suala la kuongezewa mikopo yetu si la kuomba kwa sasa na wala halihitaji vikao vyovyote kutujadili tunachoomba hizo fedha zije kwa muda ambao chuo unataka kwa sababu na wao wana taratibu zao, kwa kiasi kile cha mkopo ambao tulichopewa cha shilingi za kitanzania milioni 3 walizotupa kwenye mikopo yetu ya mwaka 2006-2007 kwa kiasi kilichobaki hata tukiamua tukilipe chote katika ada kiasi hicho ni kwamba hakitatosha bila sisi hapo kujikimu kwa suala lolote sasa wanapogawa mkopo kama huu kwetu bado linahitaji ufikiriwaji wa kina na wa haraka katika utekelezaji wake, wataongeza kiasi gani? Bado wanatufikiria wakati sisi bado tunateseka na karibu mgonjwa wao mahututi anafariki,tuliomba mkopo wa dola za kimarekani 5000 kama kiwango cha chini kulingana na mahitaji ambayo tuliyaambatanisha katika fomu zetu za mikopo lakini bado wanatupa mikopo sawa ya shilingi za kitanzania milion 3 kiasi ambacho ukiibadilisha kwenda kwenye pesa ya kimarekani utapata dola chache sanaa,wanatupa mikopo bila kufanya utofauti wa mazingira ya maisha katika sehemu mbalimbali ambazo bodi ina jukumu la kuhudumia wanafunzi wake ,hili si jambo la busara hata kidogo ni kuwaumiza tu hawa wale ambao mazingira waliopo kama sisi huku ni magumu kifedha na hatuna wa kumtegemea isipokua serikali yetu ya Tanzania ambayo ndiyo iliyotuleta huku
Sasa tumefikia tamati ya maisha yetu kielimu hapa chuoni
Baada ya uongozi wa chuo kuamua kutusimamisha tena masomo mwanzo huu wa semista ya pili ambayo imeanza tarehe 05/02/2007 wakitupa muda wa mwisho wa kusubiri hela zetu kutoka bodi ya mikopo wa siku 15 yani mpaka tarehe 15/02/2007 ni muda wa sisi kukaa hostel bila ya kwenda madarasani huku wenzetu wakiendelea na masomo na ni muda pia wa kusubiri hela zetu kutoka bodi ya mikopo ziweze kuwafikia bila kuzidi muda huo ambao wameuweka, baada ya hapo kama fedha zetu zitakuwa hazijawafikia ni kwamba maisha yetu ya kusoma chuo hiki yatakua yamefika mwisho.
Tutaenda wapi? Je serikali mko wapi? Mbona mnatutelekeza ugenini?
Tunaomba msaada wenu muweze kutunusuru sisi huku kwa jitihada zozote ambazo kama serikali zitakua ndani ya uwezo wenu kabla muda wa kufukuzwa haujafika,hili sasa ni ombi kwa ngazi zote za serikali ya mheshimiwa raisi Jakaya M. Kikwete akishirikiana na mawaziri wa wizara mbalimbali,wabunge pamoja na mashirika yote yasiyo ya kiserikali,kwa sababu hiki ni chuo cha serikali tunaomba suala hili lichukuliwe kiserikali zaidi baina ya nchi hizi mbili ili kutunusuru sisi wanafunzi wenu mliotuleta hapa kusoma huku mheshimiwa raisi Jakaya M. Kikwete ukirejea usemi wako wa kuingilia kati suala kama hili lililotufika sisi katika hatua kama hii tuliyoifikia ya kubakiza siku chache tuweze kufukuzwa hapa chuoni kwa sababu ya kushindwa kumalizia kulipa ada ya shule basi hata kwa mawasiliano ya aina yoyote tunaomba yafanyike miongoni mwenu kama serikali na chuo ili mtunusuru na zahma hii nzito
Majina ya wanafunzi wa kitanzania ambao wapo katika hali ya muda mchache waweze kufukuzwa chuoni
1. JACKSON NYABUSANI-raisi wa wanafunzi chuoni
2. DENIS KANYIKA-makamu wa raisi
3. ARLON SICHONA
4. ZAWADI BWANALI
5. GIDEON DABANA
6. ATHMAN KIHARA
7. ENEZA KITILYA
8. FILBERT MKUDE
9. BAHATI MBWILO
10. SAHIB.KATYETYE
11. PILI MBAGA
12. DIANA STEMILE
13. ZAINABU ULEDI
14. ARAFA A.KACHENJE
Kama ni vigezo vya kupata mikopo hiyo tuliyoomba na kuipata ni kwamba wote kati yetu tunavyo haijalishi niko Tanzania au nje ya Tanzania kama haki yetu kulingana na jinsi tulivyoomba na tunavyoendelea kuomba kila mwaka,marekebisho katika suala zima la mikopo ya nje ni suala la kufikirika kiundani zaidi na si suala la kisiasa kama ambavyo linachukulika,ni suala ambalo linahitaji uamuzi wa kitaaluma zaidi katika kuliamua kwa kuangalia tofauti ya mifumo ya maisha katika nchi za nje na ndani ya Tanzania.
Natumaini kama mliweza kufikiria uamuzi wa kuanzisha bodi ya mikopo na kututoa huko na kutuleta huku tunategemea pia suala kama hili mtakua mmelijadili kwa kina kabla ya kuamua kulitenda kwa kufuata taratibu ambazo mmeziweka wenyewe.
Kwa hiyo katika hali ya kawaida sana tunashindwa kuamini kama bado mnaendelea kutujadili na ili hali suala letu si la kuhitaji muda kama ambao mmeutumia kutufikiria wakati sisi tunaendelea kupata mateso makubwa na kusahau kama mna jukumu la kutuhudumia na sisi tuna haki ya kuhudumiwa kulingana na sheria za kimataifa kwa kutuleta huku kupitia serikali yetu hivyo katika kulifanikisha hili suala la marekebisho katika mikopo yetu ya nje ya Tanzania hasa sisi wa Ukraine ni la lazima na si ombi tena kwa sababu muda wa kufanya hivyo kwa sasa umeisha na nyinyi kama mnatujali hamna haja hata kidogo ya kuendelea kutufikiria kwa sababu ni lazima hela ije kwenye maongezo ya mikopo yetu ili tuendelee kusoma bila ya hivyo ni kwamba hela mliyotupatia ya mkopo imekaribia kuisha na kiasi kilichobaki hata tukiamua tusile sisi hakiwezi kutosheleza kiasi cha ada ya chuo ambacho kimebaki kwa hiyo mtagundua sasa si ombi tena ni suala la kuhitaji uamuzi wa haraka zaidi ili kuhakikisha usalama wetu kitaaluma na kimaisha kulingana na mazingira tuliopo sisi wanafunzi wa kitanzania tunaotokea kwenye familia ambazo umaskini bado ni kitu kikubwa kinachozisumbua,tunategemea mmetuleta huku mkiwa na lengo na nia nzuri ya kutafuta mabalozi wa kusaidia kulisukuma kwa haraka iwezekanavyo gurudumu zima la maendeleo ya nchi yetu kwa miaka ya usoni sasa ni lazima mtambue kuwa nyinyi ndio baba na mama zetu na familia zetu zipo nyuma yenu zikiendelea kuwashukuru kwa nafasi mlizotupa sisi kuja huku kujiendeleza kielimu kwa manufaa ya Tanzania nzima.
Hivyo tunaomba mtujali na kututhamini katika mawazo na hoja zetu tunazozitoa kwenu juu ya kiasi cha fedha mnachotupa sisi kama wanafunzi ambao tupo kwenye ngazi ya chuo kikuu hivyo ukomavu wa akili zetu katika kujaji na kutoa mapendekezo ni mkubwa kama wahusika tunaokutana na hali hiyo halisi hivyo hatutegemewi kupuuzwa zaidi ya hapo tutashindwa jukua zaidi kuwa mnatuweka kwenye kundi gani hasa la watu,au sisi ni wahuni?sisi si wahuni pengine kama ambavyo mnaweza kutufikiria kikawa kigezo cha kutufanyia manyanyaso haya yote katika kutufikiria kutuongezea mikopo yetu mkidhani tunahitaji hizo fedha kwa starehe binafsi, nafikiri sisi ni watu wazima ambao sasa tunajukumu la kuandaa maisha yetu wenyewe hivyo vigezo mlivyovitumia kutuleta huku nafikiri vinaweza kututoa kutoka kwenye kundi kama hili la watu,tunaimani hata wazazi wetu wangeona aina ya maisha ambayo tunaishi huku wangelia sana na wangelijua hili mapema lingelitutokea wasingelituruhusu sisi kuja huku ili hali serikali inatufanya sisi kama watoto wa kambo.
Ni aibu kubwa ambayo serikali ya Tanzania inaendelea kujizolea siku hadi siku kupitia aina ya maisha yetu kama wanafunzi wanaosomeshwa na nchi yao,hali ya kukosa fedha za kujikimu ikiwa ni pamoja na chakula,mavazi ya hali hii ngumu ya baridi kali sana,mavazi ya taaluma yetu na gharama zingine za kijamii ambazo zinapatikana hapa shuleni kama michezo,bima,usajili,utafiti wa kiafya,ulinzi,malazi ni vitu ambavyo vinapatikana nje ya ada zetu na ni miongoni mwa vitu vya kufikirika zaidi kama vigezo vyetu vya kuomba mikopo yetu kuongezwa ukizingatia gharama za maisha katika nchi hii ni kubwa.
Ucheleweshaji wa fedha zetu za ada iliyo nusu nusu kwetu zinatuzuia kuruhusiwa kuingia madarasani mara kwa mara wakati masomo yetu yanaendelea na mara kwa mara hali ya fedha za malazi na usajili zinapochelewa kwa muhula wa masomo hutufanya tuishi kwa manyanyaso na woga mwingi zaidi ya swala msituni au panya aliyemuona paka hali hii inatufanya tushindwekuwa na amani katika nafsi zetu tukijilaumu kwa nini tumekuja huku,walimu wanakiri tunauwezo mzuri kitaaluma lakini upungufu wa ufanisi wetu utaenda ukipungua kwa sababu vichwa vyetu vinasongwa na mambo mengi vikiwemo njaa na mawazo juu ya hatma yetu huku ulaya.
Hali hii inawaweka pia dada zetu ambao tumekuja nao huku kuwa katika hali ya hatari zaidi kushawishika kirahisi na wanafunzi wanaotoka nchi zingine ambazo wazazi wao wana uwezo wa kutosha au serikali zao zinawajali kifedha kulingana na gharama za maisha ya huku hivyo pia tuna wasiwasi pia na dada zetu kukosa mwelekeo wa kitu kilichowaleta na nyinyi kubeba mzigo wa lawama zote kwa kushindwa kutufikiria sisi kwa matokeo ya nyinyi kuchelewesha au kutuma fedha kidogo kulingana na mahitaji,mnaweza mkawa mlikua na lengo zuri sana juu yetu kutuleta huku ila umuhimu wenu unaweza ukakosa mwelekeo kama sio sisi kupotea kabisa kutokana na hali ngumu ya maisha ambayo tunakutana nayo huku bila nyinyi kujua au kufanya jitihada zozote kutufuatilia kwa karibu kujua tunaishi vipi.
Tunajua mnafahamu kuwa sisi ni miongoni mwa watu muhimu sana ulimwenguni pia hakuna asiyejua ya kwamba masomo tunayochukua ni miongoni mwa masomo magumu na ghali sana na yanayohitaji utulivu wa hali ya juu bila ya kuwa na mawazo au fikra zingine ambazo sio za lazima au ambazo zinazoweza zikatatulika kwa wakati husika.
Kama serikali tunajua mna uwezo mkubwa sana wa kutatua magumu ambayo tunakutana nayo huku kwa kufuata taratibu na kutekeleza utaratibu huo wa mambo mliyoyaweka na kuyajadili juu yetu kwa kuzingatia muda hasa.lakini tunashangaa kuona mambo bado yanaendelea kuwa kinyume na jinsi tulivyofikiria hii inatupa sisi wakati mgumu sana wa kwenda sambamba na masomo haya magumu,mnatakiwa mtambue kuwa mmebeba jukumu la kufanikisha lengo lenu la kutuleta huku kwa manufaa ya Tanzania ya baadae na si kutupa kwenye moto kiasi hicho kidogo cha fedha mnachotuletea.
Mnapotuathiri sisi kisaikolojia msitegemee kujenga chochote bali mtakua mnasaidia kubomoa mwanzo mzuri mliouanzisha mkiwa na nia na lengo zuri mawazoni yani kama ni mkulima ameamua kula mbegu zake zote mwenyewe atapanda nini sasa?sisi ni binadamu tutakapotumia muda mwingi kufikiria manyanyaso mnayotufanyia kwa njia moja au nyingine juu ya utoaji wenu wa fedha kwetu kama kiini cha matatizo yetu yote mnaweza kumkaribisha shetani katika mawazo yetu kwa kiasi kidogo cha fedha mlizotupa tena kwa kucheleweshwa kuamua kuacha shule na kuamua kuwa msingi wa biashara huku niliko kama njia ya kutafuta kuishi zaidi baada ya nyinyi kushindwa kutuhakikishia uhai wetu kama watu mliotuleta huku ili hali mkijua huku ni ugenini ambako ndani yake kuna watu wa aina mbalimbali ambao rangi bado ni kigezo kikubwa ambacho kimejengeka katika fikra za waliowengi kuonyesha hali fulani ya ubaguzi ambao unaweza ukaonyeshwa kwako waziwazi au kwa mficho kidogo kutegemea na akili ya mtu, pesa inaweza ikawa ni kigezo kikubwa cha kuchochea hali kama hiyo kukutokea sasa hawa ni watu wenye rangi tofauti na sisi ambao manyanyaso ya aina hii kwa nchi kama hizi tulipo sisi ni kitu ambacho unaweza kukifikiria kukutokea muda wowote kulingana na mazingira uliyopo, mnatupa wakati mgumu wa sisi kutoamini hata nyinyi mnaweza kuonyesha ubaguzi wa aina kama hiyo katika ugawaji wa mikopo ubaguzi ambao tunaweza pia tukakutana nao huku kutoka kwa wazungu ambao si wastaarabu,ni ubaguzi ambao sasa nyinyi mnauonyesha waziwazi mkwetu kwenye mtandao ili kila mtu aone ni jinsi gani mnaweza kunyanyasa wengine katika suala zima la utoaji wa mikopo, kama kuna juhudi zozote mlizifanya kama serikali kuhakikisha wengine waliopo nje wanapata mkopo sahihi kulingana na gharama za maisha ya sehemu husika basi fanyeni hivyo pia kwa wengine kama sisi ambao tupo katika mazingira kama hayo ya wenzetu wanaopata kiasi fulani cha fedha kikubwa kuliko chetu, ni kitu ambacho sisi binafsi kinatukatisha tamaa sana sana kuona nyinyi mnaweza kuchangia kuharibu tamati ya malengo ambayo tumejiwekea baadae sisi na familia zetu kama pia si na watanzania ambao wako nyuma yetu wakitegemea siku moja tuje kuwa saidia katika nyanja mbalimbali za maendeleo
Tunakutana na mambo mengi sana ambayo ni mazito kuliko uwezo wetu kuyatatua katika kila wakati mgumu wa kifedha ambao tunakutana nao.
Mwanzo wa muhula huu wa mwaka wa masomo kwa mwaka 2006-2007 ambao ulianza tarehe 01/09/2006 tumekutana na mengi ambayo katika hali ya kawaida yametusononesha kwa kiasi kikubwa sana.
Tumekuja hapa chuoni mapema mwezi wa tisa baada ya kumaliza vizuri kozi zetu za lugha ya kirusi tayari kwa kuanza mwaka wa kwanza wa chuo, tukiwa na lengo na hamu kubwa ya kuanza kusoma huku mioyo yetu ikiwa na hamasa kubwa juu ya hilo kama kitu kilichotuleta huku Ukraine na kama kitu muhimu sana katika maisha yetu huku nyuma kukiwa na serikali ya Tanzania na familia zetu ambazo wanahitaji msaada wetu mkubwa katika siku za baadae lakini cha kushangaza tumeweza kukaa zaidi ya wiki 3 bila kuingia madarasani huku wenzetu wakiendelea na masomo.
Tulikuja huku tukitegemea serikali itakuwa tayari imeshafanya mazungumzo ya karibu kati yao na serikali ya Ukraine kama sio uongozi wa chuo ili sisi tusome bila kusumbuliwa katika suala zima la malipo huku serikali ikijiandaa kuleta fedha zetu za mkopo kwetu. Tumekutana na usumbufu mkubwa sana ambao mpaka sasa hivi utatuzi wake bado ni kitendawili kizito mno huku serikali ikiendelea kushindwa kututumia pesa zetu kwa wakati unaofaa, chuo kinashindwa kutuelewa kwa kila tunachowaeleza na ukweli ni kwamba chuo kilikua hakijui chochote juu ya uwepo wetu ni mtu mmoja tu ambaye nae si muhusika ndiye alikua na taarifa zetu tena zisizo na uhakika wowote juu ya taarifa zetu kuhusu malipo tukiwa chini ya serikali ya Tanzania.
Tumekuja tukiwa hatuna fedha za kutosha baada ya serikali kutupa hela kidogo siku nyingi zilizopita kutokana na mawasiliano kutokua mazuri kati ya chuo na seriklali na maelezo yetu yasiyo na uhakika kwao juu ya malipo yetu kwa sababu hata sisi wenyewe pamoja na balozi wetu wa moscow mheshimiwa Chokala kutokuwa na taarifa sahihi kutoka bodi ya mikopo juu ya ujaji wa fedha zetu katika muda muafaka iliwapelekea wao kushindwa kutuamini na kututaka tulipe mambo mengine ambayo kwao waliyaona madogo kwa wakati huo lakini sisi kwetu yalikua makubwa kwa sababu tulikua hatuna hela ya kutosha.
Huku wao wakiendelea kuwasiliana na ubalozi wetu wa moscow ilibidi tuchangishane wenyewe kwa wenyewe kupatikana fedha za kulipia malazi,usajili pamoja na utafiti wa kiafya na bima nyingine tulilipa vitu vingi na vingine hatukuweza kuvifahamu kwa sababu vilikua kwenye orodha kulingana na taratibu zao ilikua ni lazima vilipwe kwa wakati mmoja.
Ni ukweli usiofichika hata yule aliyekua nacho kidogo ilibidi akitoe na kubaki mifuko mitupu yaani isiyokua na hela hata ya kukuhakikishia utakula nini,tulimaliza hela zote na kutuacha katika hali ngumu sana kuielezea kifedha bila kujua hatma ya kuja kwa fedha zetu kutoka bodi ya mikopo.
Tuliishi maisha magum sana kiasi ambacho siwezi kuandika hata jinsi ambavyo tulikua tukisulubika ,unaweza ukashindwa kuamini lakini ni hali ambayo haiwezi kuandikika ikafanana na uhalisia wa mateso ambayo tuliyapata kwa kipindi kile,walituruhusu kuingia darasani baada ya kama wiki 3 tangu masomo yaanze tena kwa sharti la mwishoni mwa wiki hiyo waliyoturuhusu kwenda darasani hela iwe imewafikia kama ambavyo balozi aliwataarifu.
Tukiwa hatuna chochote mifukoni mwetu tuliweza kuingia madarasani na kukutana na mambo mengine mapya ambayo yanahitaji tena fedha, kila profesa anahitaji uwe na koti jeupe la kidaktari kama sare pamoja viatu maalum kwa kila somo madarasani na maabara, ni lazima ubadilishe viatu hivyo ilikua ni lazima na wala hana haja ya kujua wewe ni mgeni au mwenyeji usipokua navyo huwezi kuruhusiwa kuingia darasani yakatukuta yaleyale tena.
Wapo maprofesa ambao walikua wanatuelewa ukijieleza vizuri lakini pia wapo ambao walikua hawataki kukusikliza unaongea nini zaidi ya kutekeleza wanacho kuagiza,.wapo wanafunzi miongoni mwetu ambao mara kwa mara waliweza kutolewa kwenye vipindi kwa aibu kubwa lakini tulikua hatuna jinsi zaidi ya kuikubali tu hali kama hiyo kutokea na hatuna jinsi ya kuikataa hali hiyo kwa kuwa sisi ndio tulioshika makali,tulitegemea kwa sababu tulichelewa kuingia darasani tungepangiwa darasa letu peke yetu lakini ilikua sivyo kama ambavyo tulikua tukidhani ,kila mmoja wetu alipangwa kwenye kundi lake na wenyeji ambao walikua na kama wiki 3 mbele yetu katika masomo.
Ukizingatia tunasoma kwa kirusi na ugumu wa masomo yetu ilitupa wakati mgumu sana kwenda nao sambamba ila kadri muda ulivyokua unaenda mambo yaliweza kutuendea vizuri kitaaluma mpaka tukawa kwenye levo moja. Ila tunajiuliza bado nani anahusika kutupa hali hii ngumu kifedha wakati ni suala ambalo linaweza likatatulika kwa wakati muafaka jibu linabaki palepale ni serikali ya Tanzania ambayo ndiyo iliyotuleta huku ikiitumia bodi yake ya mikopo
Ukweli unabaki pale pale kwa sababu sisi tupo hapa na tutaendelea kuwa hapa kwa kipindi kirefu zaidi cha miaka isiyopungua 6 ijayo ni lazima serikali ya Tanzania iache kutusomesha sisi kiubabaishaji ikiitumia bodi yake ya mikopo kwa kuwa na mkataba wa muda mrefu na wa kuaminika katika chuo hiki ili kutuhakikishia usalama wetu hapa chuoni katika suala zima la malipo yetu kwa sababu serikali ndiyo inayojukumu la kutushughulikia utatuzi au usumbufu tunaoupata juu ya suala zima la malipo kwa chuo pia kwa kurejea fax ambazo tumezituma kwa bodi ya mikopo juu ya uongezaji wa mikopo yetu ni jambo la kupewa kipaumbele sana kwa sababu bado hatujui hasa inatumia vigezo gani kugawa mikopo tofauti tofauti kwa sisi wanafunzi wa kitanzania tunaosoma huku nje ya nchi kwa sababu ukweli ni kwamba hali na gharama za maisha hapa tulipo ni kubwa sana na gharama nyingi tunazokutana nazo hapa chuoni zipo nje ya ada tunayolipa na ukichunguza kwa makini utakuta hali ya maisha ya kawaida tu ya mtu mmoja tu katika kujikimu ziko tofauti sana na gharama zingine ambazo chuo wanataka tujitegemee katika malipo kwa ajili ya masomo yetu ziko juu sana kuliko hata ada ambayo tunalipa chuoni hivyo sisi tuna kila sababu ya kuongezewa mikopo yetu na hayo yakiwa hasa mambo yanayoifanya mikopo yetu kutokua na msaada wowote kwetu ingawa kama huelewi chochote unaweza kuona ni kitu cha kubuni lakini ukweli ni kwamba mkopo hautoshi na marekebisho juu ya mikopo yetu ni ya lazima yafanyike katika kipindi kifupi sana ili sisi wenyewe kwanza tujitambue halafu tulitambua hasa suala zima la sisi kuwepo hapa chuoni, hela wanayotupa kwa kulipia ada inatosha na mambo mengine atalipa nani? swali linabaki palepale,je na sisi tutaishi vipi?
Ukijiuliza maswali kama haya jibu lake bado linawarudia wahusika wakuu wa bodi ya mikopo kama sio serikali ya Tanzania kama watu waliotuleta huku kuhakikisha jitihada za makusudi zinafanyika kuhakikisha marekebisho ya haraka yanafanyika katika maongezo ya mikopoyetu kama kweli wanajali uwepo wetu huku tulipo na si kutupa hata hicho kidogo walichotupa kwenye moto,.pia hatujua kwa nini bodi ya mikopo inaendelea kufanya bajeti zake na kutuletea fedha zetu zikiwa kwenye shillingi na ili hali wanajua malipo yote huku tunafanya kwa kutumia dola ya marekani na ndio ambayo inatumika hata katika matumizi mengine ya kawaida.
Hii inaifanya hata mkopo wetu kubadilika badilika kama sio kushuka kiwango chake mara tu pesa yetu inaposhuka thamani yake ukiilinganisha na hela ya kimarekani,utaona ni bora basi bajeti zetu zijadiliwe na kutumwa kwetu wakiiruhusu dola ya kimarekani itumike kama pesa yetu katika mikopo yetu na sio shilingi ya kitanzania.
Pia inakua sio jambo zuri sana kututumia pesa kidogo kidogo sana kiasi cha kutuacha muda mrefu katika hali ngumu kiasi ambacho hata zingine zinapokuja zinatukuta katika madeni mengi na hivyo yote iliyokuja kuishia kulipa madeni na kubaki katika hali ngumu kama ya mwanzo hivyo kuendeleza maisha magumu tu katika elimu hii inayohitaji utulivu wa muda mrefu,inajulikana wazi ni kiasi gani cha fedha sisi tunatakiwa tukipate kwa mwaka hivyo sisi si watoto wadogo tunajua balozi ana wasiwasi mara hela zinapotuishia yeye ndio hasa huwa anasumbuliwa lakini ukweli ni kwamba ni bora ukawa na pesa yako kwenye akaunti ukajua ni jinsi gani ya kuweza kuibajeti kuliko hela kuja na kubaki ubalozini zije kwa mafungu madogo madogo zinafanyiwa nini hela zetu ubalozini wakati bodi inajua imezituma kwetu?ni vizuri tukaletewa hela yetu kama ilivyopitishwa na bodi ya mikopo na kuwekwa kwenye mitandao ili nijue nimepokea kiasi gani kutoka bodi ya mikopo na sina tena cha kuwalaumu mara tu hela yangu inaponiishia au nitajua mimi nifanye nini tena ili niweze kumalizia maisha kabla ya msimu mwingine wa hela ya bodi kunifikia.
Pia usumbufu mkubwa ambao mwakilishi wa ubalozi Mr. Francis anapata usumbufu mkubwa sana kutuletea fedha zetu katika mafungu madogo madogo kutoka moscow kuja huku Ukraine kwa wanafunzi waliopo katika miji tofauti tofauti ingawa pia inaweza ikawa ni moja ya jukumu lake lakini pia inatupa mashaka na maswali mengi kichwani kwa sababu yeye anatumia gharama nyingi kuja kutuletea hela katika miji tofauti tofauti tena bila hata ya ulinzi wowote ni kazi ambayo inahitaji moyo sana lakini pia tunajiuliza huu moyo wa kufanya haya yote anautoa wapi?
Au kuna kafaida wanakapata kupitia mgongo wa fedha zetu kukaa ubalozini?jibu la swahi hilo sisi hatuna na bado tupo kwenye wimbi la mawazo mazito juu ya hatma yetu sisi kama wanafunzi katika maisha yetu ya kishule na maisha yetu ya baadae,ni vizuri pesa yetu ikaja kwa wakati mmoja ili kuepuka gharama zingine ambazo sio za lazima
Chuo chetu kinakosa imani na sisi kwa sababu mara kwa mara havipati taarifa sahihi kuhusiana na suala letu la malipo kwao pia inatupa wakati mgumu pia hata sisi wenyewe wanapotubana kidogo kwenye suala hili ambalo hata sisi liko nje ya uwezo wetu kama wanafunzi kuwahakikishia kiasi chao cha fedha wanazotudai kitakuja kwa wakati fulani muafaka.huwa mara kwa mara tunawasiliana na balozi wetu aliopo urusi mzee wetu balozi Chokala katika kila wakati mgumu kama huu wa kifedha ili aangalie ni jinsi gani ambavyo anaweza akawasiliana nao wakamuelewa ili sisi turuhusiwe kuingia madarasani mwetu lakini hata hivyo balozi nae suala hili sidhani kama huwa anatoa maelezo ya kutosha juu ya suala hili la fedha zetu za mikopo kwa uongozi wa chuo kwa sababu mara kwa mara huwa tunakutana na suala lilelile la kusimamishwa shule kwa vipindi tofauti tofauti wakizisubiri pesa zao ziwasili kwa muda muafaka kulingana na taratibu zao.
Hiki ni chuo cha serikali kwa nini serikali yetu bado ipo kimya kuwasiliana na serikali ya hapa ili sisi tusome bila usumbufu huuu?serikali mnatuthamini sisi kweli?kwa nini mnatusomesha kwa ubabaishaji mkubwa kiasi hiki?
Chuo mpaka sasa hawaamini kama kweli sisi tunasomeshwa na serikali kwa sababu hakuna serikali kama hii ambayo inaweza kusomesha watoto wao kwa ubabaishaji wa namna hii bila hata ya mkataba wa aina yoyote na wenye kuaminika kwa sababu fedha zetu hupewa mikononi mwetu tena kwa mafungu madogo madogo kwa hiyo mara kwa mara ni sisi ndio huenda kulipa mahitaji yoyote pale chuoni,mheshimiwa balozi mara kwa mara huandika fax kwa uongozi wa chuo kuwataarifu hali halisi ya wanafunzi wao wanaosomeshwa na bodi ya mikopo ya kwamba bodi haina experience ya muda mrefu ndio kwanza ipo kwenye mwanzo ambao una mambo mengi ambayo wanaendelea kujifunza hivyo baada ya muda si mrefu marekebisho ya lazima yatafanyika na mambo yanakuwa mazuri baada ya siku chache na kuwaomba wasiwe na wasi wasi juu ya suala letu la fedha hivyo waturuhusu tu tuweze kuingia madarasani.
Hizi ni siasa ambazo wao pia wanaweza kuzitegemea kuwepo kutoka kwa viongozi wa serikali lakini siasa kama hizi zikiwa na ukweli hata mdogo wenye uhakika unaweza ukafanikiwa kuwashawishi watu wakakukubalia kile unachowaambia lakini sio siasa kama hizi zenye maneno matupu na yasiyo na maandishi yoyote kwa sababu hata chuo kinashindwa kututetea mara tu wakaguzi wa serikali wanapokuja kufanya mapitio,mheshmiwa balozi mara kwa mara huwa anakosa jibu la moja kwa moja la kuwaambia chuo kwa sababu hata yeye mwenyewe huitegemea bodi ya mikopo impe maelezo ili yeye atoe taarifa yenye uhakika kwa chuo lakini inavyoonekana hata yeye mwenyewe hukutana na ubabaishaji huo huo wa kupata maelezo yasiyo na uhakika juu ya ujaji wa fedha zetu kwa chuo hivyo ubabaishaji kuwa wa moja kwa moja na sio wenye kuwa na suluhisho la moja kwa moja.
Siku ya tarehe12/01/2007 ambayo ilikua ni sikukuu ya mapinduzi kule Tanzania,ilikua ni siku mbaya sana kwa sisi wanafunzi tuliopo hapa baada ya chuo kuamua kutusimamisha masomo kwa kipindi kingine na wengine kwenda kutolewa madarasani na kutuambia kama suala letu la kifedha halitakuwa nasuluhisho la kudumu ni bora tuondoke tukatafute vyuo vingine huku wakitupa muda wa siku chache kuhakikisha suala hilo limetatuliwa bila ya hivyo taratibu za kufukuzwa chuoni inabidi zianze kufuatwa kwa wao kusema wameshindwa kutuvumilia, inatupa sisi wakati mgumu sisi kama sisi kujadiliana na kutumia muda mwingi kuongelea swala ambalo utatuzi wake kwetu ni bado usiku wa kiza kinene sana.
Balozi wetu mzee Chokala alikuwepo hapa chuoni mwanzoni mwa mwezi wa kumi na mbili akitokea mji mkuu wa nchi hii kiev ambako mabalozi wa nchi mbalimbali walikutana kujadili masuala mbalimbali ya kimaendeleo ndipo akaamua kutupitia kwa nia ya kuja kuangalia tunaendeleaje na masomo yetu,vichwani mwetu sisi kama wanafunzi tulijua sasa mwisho wa sisi kusumbuliwa katika suala zima la malipo umefika lakini sivyo kama ilivyokua ilikua ni siasa tu za mdomo ambazo hazikua na maandishi ya aina yoyote kwa uongozi wa chuo kuonyesha uwepo wetu hapa chuoni kama wanafunzi tunaosomeshwa na serikali ya Tanzania na wao wanatutambua kama wanafunzi wao, chuo pia kilikua na wakati mgumu kuweza kumuelewa mheshimiwa chokala ambaye alikuja na kukaa kwa muda usiopungua masaa manne na nusu yakiwepo masaa machache ya kutembezwa chuoni masaa machache ya kula na kunywa pamoja na maongezi yasiyoyamuda mrefu na uongozi wa chuo na kumalizia kwa kuongea na sisi tena kwa haraka haraka kama mtu aliye safarini kuwahi kitu cha muhimi sana na kuondoka huku tukiwa hatuamini kama aliyekuja alikuwa ndie balozi wetu na hakuna chochote alichokiongea kikawa msaada kwa maisha yetu ya hapa shuleni huku akiendelea kutupa moyo kuwa hawatoweza kutufukuza tena hapa chuoni wakati sisi wenyewe wahusika wa matatizo ambayo tunakutana nayo mara kwa mara hapa tukiwa na majonzi makubwa kwa sababu ukali wa chuo ni tofauti na ambavyo balozi alivyokua anukichukulia katika hali ya urahisi hivi.
Hatujaona na hatuuthamini hata kidogo uwepo wake hapa chuoni kwa sababu bado tunaendelea kukutana na matatizo yale yale ya kuisimamishwa chuo mara kwa mara sana sana siku hizi tukiutafuta ubalozi kwa kipindi kama hiki kigumu cha kusimamishwa chuo unakua haupatikani au anapokea mtu ambaye hujitambulisha kama si muhusika kwa hiyo hawezi kutoa maelezo yoyote isipokuwa tuache tu maagizo ili akija muhusika ayashughulikie,bodi ni lazima ifanye jitihada za makusudi sana ili isije kuwapoteza mabalozi wake ambao wanasoma hapa chuoni katika suala zima la pesa za chuo hasa sisi ambao tunasoma kozi za udaktari na ufamasia ambao ndio mara kwa mara tunapata matatizo na chuo chetu bila kupata muda zaidi wa kutuliza akili zetu na mambo yetu kwa ajili ya masomo, ni ukweli usiopingika kuwa sisi tunalipa ada nyingi na yenye vitu vingi sana vya kununua nje ya ada kwa ajili ya masomo yetu suala la kuongezewa mikopo yetu si la kuomba kwa sasa na wala halihitaji vikao vyovyote kutujadili tunachoomba hizo fedha zije kwa muda ambao chuo unataka kwa sababu na wao wana taratibu zao, kwa kiasi kile cha mkopo ambao tulichopewa cha shilingi za kitanzania milioni 3 walizotupa kwenye mikopo yetu ya mwaka 2006-2007 kwa kiasi kilichobaki hata tukiamua tukilipe chote katika ada kiasi hicho ni kwamba hakitatosha bila sisi hapo kujikimu kwa suala lolote sasa wanapogawa mkopo kama huu kwetu bado linahitaji ufikiriwaji wa kina na wa haraka katika utekelezaji wake, wataongeza kiasi gani? Bado wanatufikiria wakati sisi bado tunateseka na karibu mgonjwa wao mahututi anafariki,tuliomba mkopo wa dola za kimarekani 5000 kama kiwango cha chini kulingana na mahitaji ambayo tuliyaambatanisha katika fomu zetu za mikopo lakini bado wanatupa mikopo sawa ya shilingi za kitanzania milion 3 kiasi ambacho ukiibadilisha kwenda kwenye pesa ya kimarekani utapata dola chache sanaa,wanatupa mikopo bila kufanya utofauti wa mazingira ya maisha katika sehemu mbalimbali ambazo bodi ina jukumu la kuhudumia wanafunzi wake ,hili si jambo la busara hata kidogo ni kuwaumiza tu hawa wale ambao mazingira waliopo kama sisi huku ni magumu kifedha na hatuna wa kumtegemea isipokua serikali yetu ya Tanzania ambayo ndiyo iliyotuleta huku
Sasa tumefikia tamati ya maisha yetu kielimu hapa chuoni
Baada ya uongozi wa chuo kuamua kutusimamisha tena masomo mwanzo huu wa semista ya pili ambayo imeanza tarehe 05/02/2007 wakitupa muda wa mwisho wa kusubiri hela zetu kutoka bodi ya mikopo wa siku 15 yani mpaka tarehe 15/02/2007 ni muda wa sisi kukaa hostel bila ya kwenda madarasani huku wenzetu wakiendelea na masomo na ni muda pia wa kusubiri hela zetu kutoka bodi ya mikopo ziweze kuwafikia bila kuzidi muda huo ambao wameuweka, baada ya hapo kama fedha zetu zitakuwa hazijawafikia ni kwamba maisha yetu ya kusoma chuo hiki yatakua yamefika mwisho.
Tutaenda wapi? Je serikali mko wapi? Mbona mnatutelekeza ugenini?
Tunaomba msaada wenu muweze kutunusuru sisi huku kwa jitihada zozote ambazo kama serikali zitakua ndani ya uwezo wenu kabla muda wa kufukuzwa haujafika,hili sasa ni ombi kwa ngazi zote za serikali ya mheshimiwa raisi Jakaya M. Kikwete akishirikiana na mawaziri wa wizara mbalimbali,wabunge pamoja na mashirika yote yasiyo ya kiserikali,kwa sababu hiki ni chuo cha serikali tunaomba suala hili lichukuliwe kiserikali zaidi baina ya nchi hizi mbili ili kutunusuru sisi wanafunzi wenu mliotuleta hapa kusoma huku mheshimiwa raisi Jakaya M. Kikwete ukirejea usemi wako wa kuingilia kati suala kama hili lililotufika sisi katika hatua kama hii tuliyoifikia ya kubakiza siku chache tuweze kufukuzwa hapa chuoni kwa sababu ya kushindwa kumalizia kulipa ada ya shule basi hata kwa mawasiliano ya aina yoyote tunaomba yafanyike miongoni mwenu kama serikali na chuo ili mtunusuru na zahma hii nzito
Majina ya wanafunzi wa kitanzania ambao wapo katika hali ya muda mchache waweze kufukuzwa chuoni
1. JACKSON NYABUSANI-raisi wa wanafunzi chuoni
2. DENIS KANYIKA-makamu wa raisi
3. ARLON SICHONA
4. ZAWADI BWANALI
5. GIDEON DABANA
6. ATHMAN KIHARA
7. ENEZA KITILYA
8. FILBERT MKUDE
9. BAHATI MBWILO
10. SAHIB.KATYETYE
11. PILI MBAGA
12. DIANA STEMILE
13. ZAINABU ULEDI
14. ARAFA A.KACHENJE
damn! baruaaaa au gazeti?
ReplyDeleteSiwezi kusoma, inabidi mfupishe. Elezeeni kwa kifupi. Nafikiri huu sio mkutano na bodi ya mikopo ni sehemu ya kuiambia jamii matatizo yenu.
ReplyDeleteKuna watu bado wanasoma Urusi??
ReplyDeleteKwanza poleni na matatizo mnayoyapata. Pili jaribuni kufupisha maelezo yenu - explain briefly to the point. Haya ni maelezo marefu mno.
ReplyDelete1.hii barua ni ndefu mno.urefu wa barua sio kuonyesha msisitizo.kuna hatari huko wizarani haitasomwa.nawashauri mkiituma muambatanishe na abstract.
ReplyDelete2.ingawa sijaisoma barua naomba kurudia jambo.watanzania inabidi tuelewe maana ya kuwepo kwa bodi ya mikopo.imewekwa wazi kuwa bodi haina uwezo wa kumkopesha kila mtu.hivyo basi si sahihi kwa mtanzania kudai kuwa ana vigezo vyote vya kupewa mkopo.ndio maana ingekuwa jambo la busara iwapo watanzania wote tungejiunga na wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam waliojaribu kuendesha kampeni ya kupinga kuanzishwa kwa bodi.sisi tuliwaachia peke yao,wengine wamepoteza shule wengine wamerudia mwaka,sasa hivi tunaanza kulia.kulingana na sheria iliyopo sasa kilio pekee kinachoweza kuwa na maana ni kilio cha kuomba bodi ivunjwe na kuwe na utaratibu mwingine wa kuwawezesha watanzania kusoma elimu ya juu.
Poleni sana.Hakuna hata jina linalofanana na la kiongozi Mkubwa serikalini hapo.Mnategemea nini?Mungu atawalinda, .Hii ndio serikali mnayotakiwa kuitumikia, kuilinda , na kuiheshimu baada ya taabu hizo zote.
ReplyDeletePoleni.
wapenzi!
ReplyDeletetunafahamu mko kwenye matatizo, hasa ukiwa nje ya nchi hilo ni tatizo kubwa mno maana huna ndugu, huna wa kukusaidia zaidi ya kuangalia nchi yako tena kwa kesi yenu ndio iliyowapelek huko. POLENI SANA: ila nina pendekezo kidogo, najua mko ktk hali gani lkn hii barua/gazeti mliyoandika mmetumia lugha ya jazba sana. sijui kama huyo mhusika atapendezwa na hili, sababu huenda akawa nae pia anashughulikia hili swala lenu ila pengine hali ya kifedha ndio hairuhusu.
pili hapa mlipoweka hii barua nafikiri sio mahala sahihi kabisa, hili nisuala lenu na serikali iliyowapeleka huko, mkiweka hapa tutaishia kutoa comments zetu za vichekesho tu hamtapata msaada wowote, maana sidhani kama mhusika wenu anasoma hii blog au hata akisoma atawapuuza tu sababu hamjatumia njia sahihi kupeleka maoni yenu zaidi ya kujidhalilisha tu mtandaoni.
Narudia tena poleni,na tumieni right channel kufikisha maombi yenu.
Mama Ushauri...
duh poleni sana.
ReplyDeleteBahati Mbwilo ni wewe ninaekufahamu au mwingine? (wa Mby)
poleni sana wadogo zangu
huo muda walotumia kuandika hili gazeti wangepiga deiwaka kingeeleweka, acheni uvivu mijitu mizima bado mnaendekeza utegemezi. wamekuleta kiwanja bado mnalalamika, watu wangapi tumefight kuja kiwanja hizo nafasi tumekosa tena tumekuna na dola mia mfukoni hatujui mtu huku tumefight leo tuko gado.
ReplyDeleteMliona kwenda kusoma huko ndio dili. Hamkuwa mnajua yaliyowapata Watanzania waliokuwa wanasoma Urusi wakati USSR ilipovunjika wengine walijuta kuzaliwa. Tatizo watu wengi mawizarani Tz NI WABABAISHAJI, wengi wana hold position nyeti wakati ni mambumbu, huenda hata anayeidhinisha fungu lenu hajui kulinganisha maisha ya ukiwa nyumbani na ukiwa kwa ugenini maana ni hatari maana hamna wakumtegemea huku au kukopa kama tulivyozoea huko kwetu. Nafikiri imefika kipindi chakuwakataa kabisa kabisa watu wazembe kwenye wizara zetu maana wanaturudisha nyuma sana. Wizara au ofisi za serikali sio mali za watu binafsi ni za wananchi na wananchi wana haki ya kudai uongozi bora na umiliki bora wa nafasi mbali mbali za serikali. WATU WASOMI NA WENYE VIPAJI MBALI MBALI WAPO WENGI HIVYO HATUONI SABABU YA KUWA NA WATU WAZEMBE NA WANOJIFANYA MIUNGU KATIKA SEHEMU ZA UTUMISHI WA UMMA. WATU WAWAJIBISHWE TUMECHOKA. MHESHIMIWA KIKWETE NA LOWASSA ONDOENI MIOZO HII!!!
ReplyDeleteKebebeni ma box acheni kelele.
ReplyDeleteBeba boksi wewe uende shule ya jasho lako mwenyewe....wee kaa tu uisubiri serikali ikutumie fweza.
ReplyDeletePamoja na kuwa wanafunzi hao wanaweza kuwa na nguvu ya hoja ihusuyo matatizo yao wajifunze kueleza suala kwa ufupi na ufasaha. Kuandika maelezo marefu kunamkanganya hata msomaji.
ReplyDeleteKama kweli hiyo ndio hali halisia, wahusika wa maslahi yao yafaa wawajibishwe. Tunaliabisha taifa kwa wanafunzi wetu kuadhirika. Twategemeaje kuwa watafuzu masomo yao bila kuwezeshwa?
Kwani kazi za kubeba mabox huko hakuna jamani mfanye na nyie kuliko kuitegemea serikali??
ReplyDeleteChangamkee sasa mmeshakuwa wakumbwa jamani mmefikishwa mbali vijana au ndiyo hivyo tena stress za kutengewe juu ya meza na mama sasa hakipatikani??
MY DEAR TANZANIAN
ReplyDeleteKitu cha kwanza poleni sana vijana serikali ya bongo ni feki sana yaani kwanini hawana aibu ? jibu nawapa kati yenu hakuna mtu anatoka...... tunaweka kwenye mabano. watoto wao wanawapeleka marekani Uk. ada uwa zinalipwa hata kabla mtu hajaenda darasani . .living allowance zinaenda kwenye account direct.. unaona mambo hayo
Nyie wamewaleta nchi kama Ukraine ingawaje life standard iko chini lakini ujue kwamba huko hata kubeba box ndoo hakuna .. kama mgelikuwa nchi kama Urusi poa kwa sasa hivi ukichangamuka unaishi akili kichwani kama ulaya yote ilivyo.lakini kwenu huko hali ni mbaya sana hata kwa wenyeji..hivyo basi hao wanaojihita viongozi wa nje sijuhi kama hawana taarifa ya wanafunzi wanaosemesha na serikali nchi za nje kwanini ...nyumbani hakuna utaratibu wa raisi kukutana na mawaziri at least once in week kuwa na detail kila wizara instead of kuzunguka nchi zote duniani ili kujua kwamba jama sasa hivi hizi hela wapelekeeni vijani Ukraine wasitie taifa aibu hilo wazo hawana mpaka mwandike sana ndiyo mtapata msaada otherwise... mie niliwai kuzuiliwa mtihani kwa sababu ya malipo hivyo hivyo.. aibu sana asie wazungu hawaelewi kabisa kwamba nchi inakupeleka kusoma halafu inashindwa kukulipia.....Eee bwana Bongo nyumbani lakini mambo yanavyoenda inatia huruma sana...na kama sikosei hamdaiwi zaidi ya dollar laki moja(100,000) hiyo hiyo serikali inanunua rada milioni therathini na....nyie mambo yakiwazidi jiripueni mingie Poland au germany jifanyie wakimbizi... hakuna njia kama serikali yako hakujali na wewe unaikana...In advice jitahidi msome hayo mambo mengine baadaye kama sisi tulivyo fanya......
Ngugu Watanzania,
ReplyDeleteKumbuka kuwa elimu ni haki yako na ni haki yako kusomeshwa na serikali ima bure kwa wale amboa hawawezi kujilipia au kwa kupewa mikopo au serikali inatakiwa iwe na policies that prove effective.
Wakati mlipopelekwa shuleni mliahidiwa na mikatabwa ilisainiwa. Mtu au taasisi yeyote iliyovunja mkataba inaweza ikapelekwa mahakamani. Kumbuka kuwa mnadai haki zenu na madai yenu ni ya halali.
Having said that, your case is a strugle agaist the broken system. It is a continuosly never ending process. With what is happening now in TZ and to you guys as a whole, we must pretest, we must oppose, and we must try to alter it. Speak up people,NEVER GIVE UP. This is the fight against the HAVES and the HAVES NOT.
Michuzi unasubiri nini kuondoa hilo gazeti kwenye blog, tumeshalisoma tumechoka, linachukua bytes za kudonload buree hapa sioni point. Haiwezekani wasomi tena wako nje ya Tanzania, yaani majuu wanashindwa kufikisha ujumbe kwa njia iliyosahihi na kwa kwa ufupi. Hii barua hata ukimpa baba yako, ataiweka pembeni hataisoma kamwe labda awe hana kazi zingine. Ukipeleka ofisini ndo sahau kupata majibu.So foolish these wasomiz
ReplyDeleteKweli kabisa michuzi TOA HILI GAZETI HUMU linajaza tu nafasi za picha, hadithi zile zile za sungura na fisi. waache hao watoto wa mama wasubirie ugali uje mezani,hawajuni life wanatupotezea muda na hayo magazeti tulioshachoka kusoma. sie tulitafuta hizo chance tukakosa angalau wenyewe wamepata na wamekuja bure wame-save nauli. sisi tumejilipia na tumebeba less than $100 peke yake mfukoni na hatujaandika email kwa wazazi,serikali au wasamaria mtandaoni tumepiga deiwaka na sasa tuko kamili hii ndo maana ya ughaibuni, hawa pumbaf wanalilia hela ya walalahoi bongo wakanyee bia urusi. hapo juu kuna pimbi anasema marekani watu wanasomeshwa bure, mjinga hajui nini anaongelea, mambo yakusomeshwa yalikuwa zamani. kama hawawezi kula deiwaka wajiripue warudishwe home pumbafu tumechoka na kusoma upuuzi michuzi
ReplyDeleteThis comment has been removed by a blog administrator.
ReplyDeleteTena wengi wenu hapo majina tunayahifadhi mlifeli Tanzania ndo mkakimbilia huko, sasa c mjilipie? mliona tuliobaki hapa ni wajingaeeee? Kuna mmoja hapo nicha pombe balaa akirudi likizo anakaa tu na mademu mlimani city huku chupa za bia zimepamba meza.
ReplyDeleteHi mimi ni WILLIAMS SARAH
ReplyDeleteJe! Ungetesha mkopaji / mkopo? Je! Unahitaji mkopo? Je! Unahitaji msaada wa kifedha wa haraka? Unahitaji mikopo ya papo hapo ili kulipa madeni yako, au unahitaji fedha ili kuboresha biashara yako? Tunatoa kila aina ya mikopo na viwango vya riba 2% kwa watu binafsi na kampuni yenye masharti na masharti ya wazi. Ikiwa unatoa mikopo yoyote kwa marudio yoyote, tafadhali wasiliana na sisi leo ili kupata mikopo yako leo. Tutumie barua pepe: (williamssarahloanfirm@gmail.com)