taifa staaz wakiwa ndani ya denmaki katika mchezo wao wa kwanza wa kirafiki wa mazoezi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 28 mpaka sasa

  1. kila la kheri wanangu yaani, ndio wenyewe kabisa.
    mdau morogoro

    ReplyDelete
  2. jezi hizi mbaya tutafute design nyingine

    ReplyDelete
  3. hicho kijamaa kifupi kinaonnekana hakiwezi kurudi bongo lazima kizamie.

    ReplyDelete
  4. Tupe na matokeo basi !

    ReplyDelete
  5. Vipi matokeo Braza Michu??wengine netiweki hazishiki sawasawa...hiyo timu inaitwaje??

    ReplyDelete
  6. Pigaaaaaaaaaaaaaaaaaaa! Njohole fanya fanya ujimix na masela tukawatoe manundu black mambaz.
    Babao

    ReplyDelete
  7. Salaam waungwana....Bor Michuzi una skuli ya kufunza watu kupiga snepu ndugu yangu?? Manake huyo aliyepiga snepu alinichanganya kuona wadenishi wapo wa4 na vijana wa STAAZ wapo kama nyuki.... manake kama ndio timu hapo labda iwe magoli madogo au chandimu manake tukipiga fulu timu hapo lazima tuwapige mande...ha ha ha haaaa

    all the best to STAAZ wajifunze tuanze dunculiza kwa ajili ya japo nauli Ghana 2008

    Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.....

    ReplyDelete
  8. Vipi mbona hujaweka matokeo ya mechi?

    ReplyDelete
  9. MICHUZI TUNAOMBA MATOKEO PLEASE...

    ReplyDelete
  10. Kuna mdau ametabiri matokeo ya Taifa stars na Msumbiji.Lakini kuipa uzito hiyo hoja,Naomba nitangaze dau 20,000 za kibongo kwa mdau atakaetabiri matokeo hayo sawasawa hayo.na izi pesa naomba michuzi tuwasiliane uwe nazo.
    Nawasilisha.

    ReplyDelete
  11. nadhani ilikuwa mechi ya kushtukiza, yaani hakuna mtazamaji hata mmoja!

    ReplyDelete
  12. Mbona utuwekei matokeo bwana michu sisi bado tunajifunza sasa usigope kutuwekea matokeo kila mbongo anajua kuwa timu yetu bado changa kwahiyo kufungwa kwetu sia ajabu ni moja ya kujifunza hata kama tutafungwa na timu ya daraja la5 hamna noma

    ReplyDelete
  13. STARS YACHAPWA DENMARK


    Na Elizabeth Mayemba, jijini

    TIMU ya taifa, Taifa Stars, jana ilianza vibaya ziara yake ya kimichezo baada ya kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Boldklubben Skjold ya Denmark ya daraja la pili katika mechi ya kirafiki iliyochezwa nchini humo.

    Stars wapo nchini Denmark kwa ajili ya ziara yao mafunzo kabla ya kuvaana na Msumbiji katika mechi yao ya mwisho ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Matifa Afrika mwakani nchini Ghana.

    Stars walicheza mechi hiyo jana usiku na bao la kufutia machozi lilifungwa na Amir Maftah.

    Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela, Stars wataendelea kucheza mechi za majaribio kabla ya kuondoa Jumatatu kwenda Uswisi ambako watacheza mechi tatu na kurejea nchini.

    Katika hatua nyingine, wachezaji watano wa kikosi hicho cha Stars wanatarajiwa kuondoka leo baada ya jana kushindikana kutokana na matatizo ya usafiri.

    Wachezaji hao ni Nadir Haroub 'Cannavaro', Abdulrahim Amour, Shaaban Dihile, Meshack Abel na daktari wa timu, Sheiky Mngazija.

    Kwa mujibu wa TFF, wachezaji hao wataondoka saa 10 jioni kwa ndege ya Ethiopia kwa ajili ya kujiunga na wenzao waliotangulia.

    Timu hiyo iliondoka kwa mafungu na hilo litakuwa kundi la tatu baada ya mengine mawili kuondoka kwa nyakati tofauti.

    ReplyDelete
  14. huyo annon aliyesema jezi mbaya,hii design ni poa kabisa halafu jezi huwa zinachange kutokana na msimu hivyo zitajachange baadae b4 we go to ghana kwa hio hamna shida ziendelee hizi hizi tu.

    ReplyDelete
  15. Matokeo ni kwamba tumepigwa bao 2-1, timu ya taifa inafungwa na timu ya daraja la pili ya Denmark. Kweli wabongo tuna ndoto za mafanikio

    ReplyDelete
  16. Starz imelala 2-1.

    ReplyDelete
  17. Eti Ally Mustapha ndo golie wa stars!! Huku kuna Kaseja mwenye uzoefu chungu nzima anakula jua bongo..

    ReplyDelete
  18. ..kweli wametudharau maana hata huo uwanja ni wa high school...maskini ni maskini tuu,tujitahidi kuondoa njaa zetu labda ndio tutapata heshima kidogo

    ReplyDelete
  19. tuwatakie afya njema kwa maandalizi ili waje wote wakiwa wazima tayari kwa mechi ya mwisho

    ReplyDelete
  20. Jamani hawa Taifa Stars wasisome kabisa hizi blog wanaweza wakashindwa hata kucheza mpira. Kha! wajameni Wadau wapeni moyo ndo wanatambaa

    Michu, hivi Nico Njohole, Deo Njohole, Likembe Njohole wapo wapi??? Angalau huyo Renatus Njohole tunamsikia hao kakaze wamenda wapi?

    ReplyDelete
  21. Aminia Pius babaake, Kaseja amejaa tele watu wanaleta majungu tu. Haiwezekani kipa ambaye kwenye timu yake ni wa akiba akachukuliwa kwenye timu ya Taifa yule kipa wa kwanza akaachwa hasa kwa situation kama hii ya Tanzania ambayo wote ni watanzania. Wanaofahamu soka watakuwa wamenielewa, wasiofahamu lazima waibuke na mipumba yao!!!!!!

    ReplyDelete
  22. safi sana taifa stars wamepewa changamoto ya nguvu ,hongera barthez mwanzo mzuri kijana hofu ondoa si tuko nyuma yako.

    ReplyDelete
  23. HATUTAKI MAKIPA WAFUPI NA WASIO NA NIDHAMU KAMA KASEJA!bARTHEZ NI BETTER SANA.

    ReplyDelete
  24. hili timu letu kweli limechoka yaani litimu inacheza na kitimu cha daraja la pili lakini bado linachapwa? hii kaazi kwelikweli. ama kweli ktk soka bado tupo karne ya 18.

    ReplyDelete
  25. Kipa kama kaseja HAFAI kuichezea taifa star.Kwanza mfupi pili hana nidhamu nje na ndani ya uwanja.Mimi aliwahi kuninyang'anya demu wangu Mwile wa Morogoro.Atoe hapo ufupi wake!!!!fyuuu

    ReplyDelete
  26. Thobias P. unajishughulisha na shughuli gani? Huo mpira baba, kama rahisi wewe unachezea timu gani? Hao wenzetu wameweka investment kwenye soka kwa muda mrefu sana, na hayo ndio matokeo yake. Kwa upande wetu sisi nia ipo, na njia ipo, muhimu ni kuwapa motisha hao vijana wetu (Taifa Stars) watuwakilishe vyema sio porojo porojo tu. Vijana wetu mie nimewapenda sana kifizikia wametulia muhimu sasa ni: nidhamu, bidii ya mazoezi, na kujiamini - Tutafika
    Babao

    ReplyDelete
  27. Kama huna nidhamu, hakuna atakayejali "your looks", au umesuka msuko gani, au ulilala na nani kwenye michezo. Twende nao haohao stars wachache tu, ila waongeze kujituma! Tuko pamoja!

    ReplyDelete
  28. HATA MAXIMO ANAJUA KWA KUWA MECHI IMEBAKI MOJA HAKUNA HAJA YA KUONGEZA MCHEZAJI YEYOTE KWA SASA KWANI ANAWEZA KUWAVUNJA MOYO WACHEZAJI WALIOPO AMBAO WAMESHAFANYA KAZI NZURI SANA. ANAWAACHA WAMALIZIE NG'OMBE WAO .WANACHOHITAJI SASA NI SUPPORT YA NGUVU TOKA KWETU TOWAUE THE MAMBAZ. TAIFA STARS OYEE!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...