Kaka Michuzi. hii ni picha niliyoipiga jioni hii, Mailimoja-Kibaha. eneo la Container Bar ambapo watoto wamekusanyika kwa kukosa pa kwenda kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Eid. Hii ni Salamu kwa Mheshimiwa Mutaki aliyeko Ushelisheli, Tunamkumbuka Kibaha.
Mdau Godfrey

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. ...huko kwenye mapaa hao watoto wanafanya nini tena?watapigwa shoti ya umeme bure!!

    ReplyDelete
  2. Godfrey vipi mbona ujumbe wako umejichanganya changanya,unasema watoto wamekusanyika eneo la konteina baada ya kukosa pa kwenda.sasa pa kwenda si ndio hapo konteina wamepakosa vipi?!aisee hiyo kibaha sisi ndio tumeianzisha,tena wewe God kama sikosei ni God S. mtaalam wa sanaa ya uchoraji.kila la heri wazawa wa Kibaha,mpe salam Chacha Matiko.

    ReplyDelete
  3. Wewe Godfrey Semwaiko?

    ReplyDelete
  4. "Washikaji hii ndio hali halisi hatupendi kutibu tatizo !! viwanja vinategwa lakini wadau wanavigeuza vyao KULALEKI UTADHANI WANAKWENDA NAVYO MBINGUNI"" haya sasa watoto wanaangaika bar baada ya kwenda kubembea bembea.

    ReplyDelete
  5. Kweli wamekosa pa kwenda mpaka wanakusanyikia baa. Hao walevi wa huko...wazuri...Ingekuea huku ....mtoto karibu na baa ...mmmmm....wameshamuiba....Laikini kweli kunatakiwa kuanzishwe sehemu ya watoto wa hang out....sio kurandaranda nje ya baa.

    ReplyDelete
  6. Chacha mshikaji upo wapi? Kina Eddo na Imma wapo wapi? Samweli Maro? Martin Massawe? Yeah wewe ni mzee wa Kibaha Mkoani. Hebu nipe details za washikaji hao.

    ReplyDelete
  7. Wewe Godfrey tumia akili yako na pia macho yako unasema watoto wanafanya nini ? yaani kwanza wapo hapo konteina lakini mpaka leo ujue kwenye makonteina kuna nini ? baa, jumba la sinema ? ok ok pili soma bango hapo kuna bendi inapinga hapo Fm academ... sasa ulikuwa unafikiria nini hapo kutizama hiyo picha utaona kuna kitu so usifanye watu wajinga na kama unatakuw watu wajue hupo kibaha au ndio wewe wakujuwe sasa muombe bwana mchuzi hakutoa kwenye blog yake sio kuleta photo na jibu lipo hapo hapo..

    ReplyDelete
  8. vipi Godfrey.
    mama hajambo na baba.
    Toka kwa jilani yako MPANGALA (DK)

    ReplyDelete
  9. Kwnai kila kitu lazima mfanyiwe na serikali? Kwanz ahata mkifanyiwa mnaharibu tu. Serikali imejenga uwanja wa taifa mechi siku moja mshapaka mavi vyooo vyote kha! Mnazi mmoja bustani ya gadeni nayo ivo ivo mkiachiliwa mnachafua chafua ovyo. hadi mtakapojirekebisha na kujiheshimu ndio mtajengawa bichi au la nendeleeni kukaaa juu ya mapawa na kwenye bichi chafu chafu, kwanza kuna bicha ngapi za pablic ambazo hakuna hata mmoja wenu alishawahi kujitolea kwenda kuokota na kuondoa uchafu????

    Acheni izo bana eti serikali haijawajengea sehemu za kustarehe wakati wa sikukuu tukufu kama idi, inabidi mstuke mjenge wanyewe au muwe wasafi ili serikali ijenge.

    ReplyDelete
  10. Kweli tumeishiwa, tuna ardhi ya kutosha lakini hatujui kupanga matumizi, hivi hapo Kibaha kweli wamekosa eneo la kuweka viwanja au kiwanja cha kucheza watoto? Sasa huko Bar au kwenye FM Academia wanaenda kucheza nini? Nakumbuka enzi zetu za ujamaa na kujitegemea sikukuu kama hii huko mitaa ya Temeke kulikuwa na maeneo kibao ya kwenda kutembea na ukiona vipi unaenda zako KIDONGO CHEKUNDU huko utabembea, utakula mbatata, ice cream, ubuyu, mihogo ya kukaanga, ya kuchoma, maembe mabichi, fasheni ya chips ilikuwa bado. Sasa sijui watoto wetu watasimulia nini kwa watoto wao. Jamani hebu tuamke, angalau Unguja bado wana viwanja vizuri vya watoto.

    ReplyDelete
  11. hahaha jamani kibaha yetu iacheni,michuzi please nipe picha za Anex bar,Container, kwa Massawe,magengeni na stand kwenye chips kaka,dah u make ma day kaka hope u will be bring more pic from down uswahilini.
    Wasalimie wote kibaha one day yes nitatia mguu hapo na mtaona kivumbi.
    Eddo ,Sammy,John,Chacha,Frank,Oscar hawa ndo vichwa vya kibaha ila vyote vishapote. One day yes vitarudi tu na mambo yote uswahilini.
    Mtakoma

    ReplyDelete
  12. Nokuhuga mkono watuache na mailimoja yetu kwani sisi wenyewe twahijua vizuri tumekuwa hapa.KONTENA JUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU.

    ReplyDelete
  13. Mtakoma, wewe ulikuwa Mkoani au Maili moja? Frank Bado yupo Kibaha?

    ReplyDelete
  14. Godfrey Naona Mailimoja haijabadilika sana,The state of that Nang'ara Bar(Kwa Lebulu)realy Brings Back Memories!!
    Naona hata vijana wa Mkoani wamefurahi kuiona hiyo Pic.
    Mzee wa Kijiwe-Hauxtable.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...