Jana jioni, mwanafunzi wa kiume mwenye umri wa miaka 18 (pichani) aliua kwa kuwapiga risasi wanafunzi saba na mwalimu mkuu wa shule katika kitongoji cha Tuusula, kaskazini mwa Helsinki, Finland. Baada ya kuwapiga risasi wanafunzi wenzakw, kijana huyo alijipiga risasi iliyomjeruhi vibaya sana, na baadae alifia hospitali. Kabla ya kijana huyo kufanya maafa hayo alipost video yake kuelezea malengo yake kwenye You Tube. Video hiyo aliita Jokela School Massacre.


Mdau Kilimanjaro, Finland

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Binafsi na habari ya kusikitisha kuona damu za hao wasio na hatia wakitolewa kafara na huyo bw Pekka-Eric.

    Naomuomba mwenyezi mungu aziweke roho za marehemu mahala pema peponi.Amaina

    Na awape moyo wa subra wale wate walioguswa na maafa haya wawe na ujasiri katika kipindi hiki kigumu.

    Pumziko la milele uwape eeeh bwana..na mwanga wa milele uwaangazie wapumzike kwa amani.amina.

    KIITOSI

    ReplyDelete
  2. Wanakijiji wenzangu,
    hebu tembeleeni kwa kaka Majid Mjengwa siku ya jumatano november 7 kuna post ya mtu kabeba ndizi ya kupikwa.Someni hapo muelewe tunakoelekea na ajenda za siri za watu na wana si "HASA"

    ReplyDelete
  3. Kama mwalimu kakufelisha ,kuna demu kakutolea nje na wale wote manaojidai much know darasani unawatia risasi ili kuleta adabu

    ReplyDelete
  4. Hahahaha wewe rhxoqsa umenifurahisha sana. Joker

    ReplyDelete
  5. Haya ndo matokeo ya amani inapozidi,watu hawajui tena madhara ya silaha za moto,maana inafika wakati hadi serikali inawamilikisha silaha watoto.Takwimu zinaonyesha karibu watu 6 kati ya 10 wa Finland wanamiliki bunduki,sijui za nini,ujambazi hakuna,wanyama hakuna ..kumbe? yatatokea mengi baada ya hili.

    ReplyDelete
  6. Haya ni mambo ambayo yanaigwa na wanafunzi/watu mbalimbali duniani. Chanzo cha mambo haya, na kwa staili ya kuacha vielelezo ni kutoka kwa taifa kuu Marekani. Dunia sasa inafikia mwisho wake. Yaani kijana wa miaka 18 anaona ameshaishi vya kutosha??? Nafikiri dunia inazalisha vichaa wengi!!!!!

    ReplyDelete
  7. Labda kuna amani kwa sababu kil amtu ana silaha kwa hiyo hakuna wa kwenda kumuonea onea mwenzie.

    Labda hakkuna ujambazi kwa sabu majambazi wanajua kila raia sita kati ya kumi ana Binduki na kwaivo jambawazi akienda kichwa kichwa hajui nani ana silaha na nani hana kwa hio basi biashara ya ujambaza jamaa anaamua kuacha na kuenda kutengeneza Nokia simu badala yake.

    ReplyDelete
  8. Kichefuchefu!!! hawa vijana balaa kabisa.. sijui ni hizo dawa za kulevya ama ndo KIAMA.... hatuna mahala pa kuweka roho zetu kwa amani sasa na imekuwa kama desturi ulaya kwamba sasa mashuleni ndo kuna akina "RAMBO".. .. .. (dRU)

    ReplyDelete
  9. HAKUNA JEMA DUNIANI,NCHI HII KILA KITU KIPO, HAKUNA NJAA, HAKUNA UJAMBZI, HAKUNA SHIDA YA UMEME WALA MAJI WALA MIUNDOMBINU, HAKUNA SCHOOL FEES YAKO, MJOMBA, SHANGAZI,YAANI MAISHA NI TAMBARARE MPAKA WENGINE WANAKOSA PURPOSE IN LIFE, UISHI U-ACHIEVE NINI? HAKUNA CHALLENGE, KWA HIYO WANAISHIA KUCHEZA MA-VIDEO GAMES, KUANGALI PICHA ZA MAUAJI ZA KINA TARANTINO, NA KUISHIA KUFANYIZIA KWA VITENDO....THE ONLY WAY TO SATISFY THEIR CURIOSITY!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...