mdau wa ukerewe katuletea hii kutoa ujumbe na pia kuwasatua wabunifu wetu wa matangazo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. hiyo picha si ukerewe,kwanza plate number, pili abiria wanaingilia upande tofauti,sweden wanatumia rangi hiyo kwenye mabasi yao ya ARRIVA lakini bendera kwa mbali ni gani?Portugo? France?

    ReplyDelete
  2. Hello Mr Michuzi
    Much greetings
    I have been visiting your blog so often and I think I'm getting to like it. You are doing wonderful more than Newspapers from Tanzania that are on the net. I might be a novice but I believe to ask does not necessarily prove me a fool. My questions are:
    Who is sponsoring you?
    Many people are visiting your blog but I hope they also know that you are investing much of your time and perhaps money. Is there a way those you or are calling themselves "wadau" contribute anything? I didint see where you are asking for contributions, something common to others. Are you pioneering or volunteering?
    I dont see adverts that could compensate your efforts either. Probably if you can improve your blog you can allow chances for that ( I dont mean your blog is not nice but you know, there is always chances for improvements".
    Otherwise I would like to congratulate you for the good job you are doing

    Somebody from US

    ReplyDelete
  3. Huu mfano mzuri sana kwa aliyekua waziri mkuu wetu LOWASSA

    ReplyDelete
  4. Sanaa ya hali ya juu lakini ujumbe unafika.Hapa bongo mibasi kibao niliyoiona imejaa mipicha ya nyati,kasuku sijui na nini.Mbaya sana haina hata maelezo.Wanaweka mipicha tu,wachache angalau wanaweka matangazo ya watu/mashirika binafsi.Anyway,kanapendeza hako ka ujumbe.

    ReplyDelete
  5. Misupu, ujumbe ni mzuri sana ila anataka kutupiga changa la macho huyo jamaa yako. Hapa UK plate number system hiyo haipo na pili watu wanaingia kwenye gari mlango upo kulia kama Bongo na sio kushoto kama Marekani. Aseme vizuri hiyo picha kaitoa wapi.

    ReplyDelete
  6. sAWA. lakini gari haivuti moshi ndani huwa inatoa nje. sisi ndio tunaovuta moshi ndani na kutoa nje kidg.

    EE lakini ni ubunifu wa haja. Badala ya kuwa tayari kutoa tuwe tayari kuacha kuvuta ndani na hivyo kutoa itakwisha automatically.

    ReplyDelete
  7. Hahaha Kaka Michuzi hii nimeipenda sana! Kweli people need to think critical like that. I love that. Mdau j.m

    ReplyDelete
  8. Mvutwaji very good thinking!! I like that!!

    ReplyDelete
  9. kweli rangi za mabasi zinatofautiana mji hadi mji na mabasi ya ARRIVA yapo ukerewe pia,lakini giveaway ya hii picha ni upande wa mlango ulipo,plate number na hiyo barafu mbona siku hizi tatu hali ya hewa ni nzuri au ndio tudanganywe ni Scotland maana ndio penye sifa ya snow.Ujumbe na ubunifu wa hiyo picha ni mzuri sana.Unaweza ukaitafsiri kwa njia nyingi
    1)it encourage to quit smoking
    2)and also quit using cars the emmision from cars is damaging the environment we therefore need to be ready to quit.

    ReplyDelete
  10. Mtoa maoni wa kwanza,naona wabongo bado tunakuwa wagumu wa kuelewa siku zote,MICHUZI hajasema hapo ni UKEREWE kasema mdau wa ukerewe ndo ameleta hiyo picha.wabongo tuwe makini jamani........

    ReplyDelete
  11. Nyie wadau hapo juu, Michu kasema picha imeletwa na mdau wa ukerewe, hajasema imepigwa ukerewe. Pia mkumbuke kuna ukerewe origino, hapo kama sikosei nadhani ni Nansio, ukerewe, mwanza.

    Cheers mate!

    ReplyDelete
  12. hapo ni ukreni

    ReplyDelete
  13. Basi huyo Mdau si wa Ukerewe manake hapa ukerewe kwa SASA ni 'Free Smoking Zone'ndani ya Europe na sidhani kama matangazo kama haya katika 'public transport system' yanakuwa 'Encouraged' tena.Its actually a criminal offence if you are caught smoking in some public places here in UK.

    ReplyDelete
  14. Traditionaly Rangi ya Mabasi yatoayo Huduma za Usafiri kwa jamii hapa Jijini London(Transport for London)ni NYEKUNDU, pili nakumbuka mara ya mwisho London ilipata ku-'snow' namna hiyo ilikuwa mwaka 2005,so definately huyo jamaa siyo mkazi wa Ukerewe.Labda mimi ndo sijui kwa utani Ukerewe ni Ukraine,au ni London??

    ReplyDelete
  15. KUMRADHI MICHU..NAOMBA NITUMIE HERUFI KUBWA MAANA NIMEKEREKA..
    HIVI NYIE WATU MMESOMEA WAPI KISWAHILI?
    AU MNAKURUPUKA TU KUWEKA MAONI? MICHU KAANDIKA PICHA IMETOKA KWA MDAU WA UKEREWE, WAPI AMESEMA KUA HILO BASI LIKO UKEREWE?KWANI MTU HAWEZI KUA UKEREWE AKAWA NA PICHA YA BASI LA DC AU NY?? ALAAA!!!

    HEBU SOMENI KWANZA MUELEWE KABLA YAKUTOA MAONI YENU.

    mkereketwa wa fulana ya michu

    ReplyDelete
  16. Hapo ni Oslo, Norwei. Mtaa huu unaitwa Karl Johan na ukiangalia jengo lile mbele baada ya theluji ndio hekalu la mfalme na malkia. Zamani, miaka ya 80's, upande wa kushoto (Spikkersuppa) jamaa walikuwa wanaita bunge la waafrika sababu wabeba boksi wa nchi zote toka Afrika walikuwa wanakutanaga hapo na kuota jua!

    ReplyDelete
  17. Michuzi, pongezi kwa picha.
    Hiyo picha ya basi imepigwa jijini Oslo, Norwei. Hizo namba za basi ni za hapa Norway. Pia mabasi ya kijani huanzia katikati ya jiji, stendi kuu na kuelekea nje ya jiji la Oslo. Ni kweli kamba hilo jengo hapo mbele ndio ikulu, unaruhusiwa kukatikaza hapo muda wowote ule.
    Tunashukuru kwa ujumbe wa tangazo.

    Mdau wa Oslo.

    ReplyDelete
  18. Kwani mtu kukaa Ukerewe ndio hawezi kusafiri sehemu nyingine za Europe, mbona siku hizi ni rahisi sana kusafiri kutoka Ukerewe kwenda popote pale na kupiga picha ni rahisi pia.

    Tatizo huwa mnakurupuka kuandika bila kusoma vizuri mada iliyowekwa, hakuna hata mahala pamoja pameandikwa hilo basi ni la Ukerewe yeye amesema aliyeleta picha hii yuko Ukerewe sasa nyie mmeassume na kuonyesha ujuaji wenu. Ndio maana huwa mnafeli mitihani kwa kukupuruka kujibu maswali bila kusoma vizuri mwishoe mnakimbilia kubeba mabox baada ya kusindwa shule!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...