mdau aliye ughaibuni atayesema hajayamisi haya mambo nadhani wengi hawatomuelewa...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. Michuzi,

    Hii picha inanikumbusha mbali. Nilipokuwa JKT Masange Tabora nilipata uzoefu wa kupika supu ya Makongoro. Wakati huo nafanya kazi officer's mess. Tulikuwa tuna chemsa overnight. Asubuhi kila litu laini halafu nzito!

    Yalikuwa kazi kuandaa kabla ya kupika. Kulikuwa na vijana special wa kuzichuna na kuzikata na shoka.

    Kambini kila jumapili walikuwa wanachinja ng'ombe. Lakini waliokuwa wanafaidi nyama ni maafande. Sisi kuruta/service tulikuwa tunaambulia malapulapu!

    ReplyDelete
  2. Anony wa 6:41 operation gani hiyo ulikua?Je,unamkumbuka afande Wailer?Mimi nilikua Kambarage

    ReplyDelete
  3. Michuzi makongoro yapo siku hizi yanatoka Mehico na Jamaica of course ni frozen

    Honesty tulio upande wa huku tuna miss mahindi ya kuchoma...believe it or not mahindi ya kuchoma yaliyokomaa vizuri kama ya bongo hamna yote machanga tu..

    ReplyDelete
  4. Kama makongoro hata huku north America yapo hata utumbo ukitaka utaupata lakini wenzetu huku nyama haziuzwi kienyeji namna hiyo,ninashangaa kuona huko nyumbani bado watu wanauza nyama vibandani namna hiyo,ndiyo wanajitafutia rizki lakini WHAT ABOUT MADCOW DESEASE AND ALL THAT!PROTECT YOURSELF GUYS.
    mnyalukolo Toronto.

    ReplyDelete
  5. nyumbani ni nyumbani lakini bado tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu walioendelea, huku UK nimeona hayo makongoro na hata ulimi lakini yameandaliwa vizuri sana na yapo katika mazingira ya usafi sana, picha hiyo inanikumbusha sana supu tamu za bongo lakini suala la usafi wa mazingira yanapoandaliwa makongoro hayo zinatisha, pengine ni suala la muda na sisi tutafika huko.

    ReplyDelete
  6. Afande wela, rehani lori. walishatangulia mbele ya haki. RIP!
    Kazoba? Majani?

    ReplyDelete
  7. Chemi ni mzee, hawezi kuwa operesheni Kambarage!Kambarage juzi juzi tu! Mimi nilikuwa Kambarage ila nikakatwa bogi la LUWA!

    ReplyDelete
  8. Aiseeee wacha kbs... Aisee ajabu hapa nilipo (Uholanzi) makongoro no bei nafuu kuliko maini aiseeee. Hiyo kitu balaa kbs...

    Da Chemi ww ulikua unatayarisha yaani hata usionje chumvi na pande juu hadi maafande ndo waje kula?

    ReplyDelete
  9. wapi afandes msagati,sijali,chacha,rajabu n.k.?

    ReplyDelete
  10. mnaacha kuchangia mada ya Makongoro mnaaza kufagiliana, sijui wapi afande nanihii.

    Anyway, wasiwasi wangu ni usalama wa afya wa hayo makongoro, maana hapo yalipo hakuna kizuzizi chcote cha kuyakinga na mainzi,

    Pili mitaa flani ya uswahilini Mbwa au paka wakigongwa na gari, baada ya muda eti kuna jamaa wanawaondoa kwenda kuwazika, wapi? hatujui.

    Maeneo hayo supu na makongoro bei karibu na bure,

    Chengeni sana, msijelishwa makongoro na supu ya mbwa, punda, komba, n.k

    ReplyDelete
  11. Du, nakumbuka nyumbani. Jamani tusidanganyane, makongoro ya nyumbani ni matamu sana ila tu utayarishaji wake unatishia afya kama tunavyomuona huyo bwana hapo juu.
    Makongoro ya hapa UK sio sawa na ya bongo. Kusema ukweli nyama ya huku sio tamu kabisa, hata ununue organic. Itakuwaje kongoro la UK liwe tamu?? Hiyo mikuku ndio usiseme.

    Makongoro ya nyumbani ni matamu sana na yadumu daima.

    ReplyDelete
  12. Anon number mbili hapo juu....umenirusha roho ile mbaya....Yaani hilo jina la afande Wailer limenishtua sana.....eti alinipa adhabu ya kukata mti mzima....kweli yule alikuwa ni binadamu kweli!!!......ilibidi nilale mbele...tena kwa miguu yangu miwili mpaka tabora mjini.....mwee

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...